Tendwa: CCM inaporomoka na upinzani unakuwa kwa asilimia 40

Najua uko kazini,timiza wajibu, ukweli wa wazi ni kuwa CCM inaporomoka kwa kasi ya ajabu, na kwa bahati mbaya inaporomoka tokea mjini kuelekea vijijini,Strategy ya Upinzani nimeipenda ya kuwadhoofisha kuanzia mjini, believe me 2015 Dar es Salaam CCM itakuwa chama cha upinzani, zile sera zenu za kuwatisha watu kuwa ukichagua upinzani unaleta vurugu zimepruvu wrong, majiji yamekamatwa na upinzania na maisha yanakwenda bila vurugu.
Uungwa ni kukubali ukweli halafu ukajenga hoja. asilimia 80 ya urais hadi 60 ya kuchakachua wakati rais yuleyule si ya kujifanya huioni, mgombea mgeni anakomba 44.5 asilimia bado unajitutumua kuwa una nguvu
Samsoni yule wa biblia(samahani kama hujawahi kuisoma) aliponyolewe nywele nguvu zilimuishia alipoambiwa anavamiwa alikitutumua akidhani bado nguvu zipo,alichoambulia ni kutobolewa macho yote mawili
Mungu akikuweka hai 2015 utakuwa shuhuda wa kifo cha CCM, naomba tu JF idumu daima ili tuelezane ukweli humuhumu.
Sikio la kufa halisikii dawa.

Kitu kimoja kizuri sana ambacho kitaiendeleza Tanzania ni kuwa na upinzani wa kweli, hiyo ni faraja na neema kwa kila Mtanzania, lakini si upinzani kama wa CHADEMA, upinzani wa kuongelea watu badala ya sera.

Kwa kuwa Tanzania bado ni mwanjo mwanjo katika siasa za vyama vingi, kila mtu anawaona magamba kwa sasa wamaana sana kwa kuwa wanachokiona ni wao kwa mara ya kwanza ndio hicho cha kuongelea watu, Watanzania ni kama vipofu tilioona punda. Lakini, kizuri ni kuwa watu wameshaanza kujuwa siasa maji taka ni nini na siasa za maendeleo ni nini, siasa maji taka ni turufu ya ya garasa, turufu ya mali ni siasa za kuleta maendeleo kwa vitendo. Hakuna mpaka sasa chama pinzani kilichoonesha haswa namna yakutatuwa matatizo yanayomkabili Mtanzania kila siku, wapinzani kila kukicha, Rostam, Kingunge, Makamba, Januari, Februari. Ni nini hii?

Tunataka kusikia upinzani umeingia ubia na kampuni la kufuwa umeme wa bei poa, kama alivyojaribu Mrema. Tunataka kuona upinzani unajenga shule bora za kuigwa japo moja kila mkoa kwa kuanzia, tunataka kuona upizani unaanzisha viwanda vya mfano, ambavyo watasema haya ndio mnayakosa kwa kuichaguwa CCM.

Leo upinzani umekazana Rostam, Rostam, Rostam, Rostam. Huyo Rostam amekuwa mkubwa kuliko upinzani wote, anatisha kwa kutukuzwa na upinzani, kama mnajuwa ana madhambi mbona hatuwaoni mkampeleka mahakamani? au mnaogopa atawaadhiri kama alivyomwadhiri Mtikila?

Hakuna wa kusifiwa kwa kuuboresha upinzani katika Tanzania kama Kikwete, yeye ndio alioahidi kuikuza demokrasi na kweli anafanya hivyo, kwa wengine hatuoni ajabu, ila tunachostaajabu tunapoona upinzani umepewa fursa kubwa sana katika awamu hii lakini hawazitumii ipasavyo, wao wamebaki na ngonjera za Rostam.
 
nnyambwate umeniudhi sana leo,shukuru tu kuna ban vingnevyo....cjui nani aliweka hii ki2 inaitwa ban maana imeninyima uhuru wa kusema ki2 juu ya nnyambwate
 
Kitu kimoja kizuri sana ambacho kitaiendeleza Tanzania ni kuwa na upinzani wa kweli, hiyo ni faraja na neema kwa kila Mtanzania, lakini si upinzani kama wa CHADEMA, upinzani wa kuongelea watu badala ya sera.

Kwa kuwa Tanzania bado ni mwanjo mwanjo katika siasa za vyama vingi, kila mtu anawaona magamba kwa sasa wamaana sana kwa kuwa wanachokiona ni wao kwa mara ya kwanza ndio hicho cha kuongelea watu, Watanzania ni kama vipofu tilioona punda. Lakini, kizuri ni kuwa watu wameshaanza kujuwa siasa maji taka ni nini na siasa za maendeleo ni nini, siasa maji taka ni turufu ya ya garasa, turufu ya mali ni siasa za kuleta maendeleo kwa vitendo. Hakuna mpaka sasa chama pinzani kilichoonesha haswa namna yakutatuwa matatizo yanayomkabili Mtanzania kila siku, wapinzani kila kukicha, Rostam, Kingunge, Makamba, Januari, Februari. Ni nini hii?

Tunataka kusikia upinzani umeingia ubia na kampuni la kufuwa umeme wa bei poa, kama alivyojaribu Mrema. Tunataka kuona upinzani unajenga shule bora za kuigwa japo moja kila mkoa kwa kuanzia, tunataka kuona upizani unaanzisha viwanda vya mfano, ambavyo watasema haya ndio mnayakosa kwa kuichaguwa CCM.

Leo upinzani umekazana Rostam, Rostam, Rostam, Rostam. Huyo Rostam amekuwa mkubwa kuliko upinzani wote, anatisha kwa kutukuzwa na upinzani, kama mnajuwa ana madhambi mbona hatuwaoni mkampeleka mahakamani? au mnaogopa atawaadhiri kama alivyomwadhiri Mtikila?

Hakuna wa kusifiwa kwa kuuboresha upinzani katika Tanzania kama Kikwete, yeye ndio alioahidi kuikuza demokrasi na kweli anafanya hivyo, kwa wengine hatuoni ajabu, ila tunachostaajabu tunapoona upinzani umepewa fursa kubwa sana katika awamu hii lakini hawazitumii ipasavyo, wao wamebaki na ngonjera za Rostam.
kwako wewe hakuna jema kwa chadema, umejaa ushabiki tu
 
Kitu kimoja kizuri sana ambacho kitaiendeleza Tanzania ni kuwa na upinzani wa kweli, hiyo ni faraja na neema kwa kila Mtanzania, lakini si upinzani kama wa CHADEMA, upinzani wa kuongelea watu badala ya sera.

Kwa kuwa Tanzania bado ni mwanjo mwanjo katika siasa za vyama vingi, kila mtu anawaona magamba kwa sasa wamaana sana kwa kuwa wanachokiona ni wao kwa mara ya kwanza ndio hicho cha kuongelea watu, Watanzania ni kama vipofu tilioona punda. Lakini, kizuri ni kuwa watu wameshaanza kujuwa siasa maji taka ni nini na siasa za maendeleo ni nini, siasa maji taka ni turufu ya ya garasa, turufu ya mali ni siasa za kuleta maendeleo kwa vitendo. Hakuna mpaka sasa chama pinzani kilichoonesha haswa namna yakutatuwa matatizo yanayomkabili Mtanzania kila siku, wapinzani kila kukicha, Rostam, Kingunge, Makamba, Januari, Februari. Ni nini hii?

Tunataka kusikia upinzani umeingia ubia na kampuni la kufuwa umeme wa bei poa, kama alivyojaribu Mrema. Tunataka kuona upinzani unajenga shule bora za kuigwa japo moja kila mkoa kwa kuanzia, tunataka kuona upizani unaanzisha viwanda vya mfano, ambavyo watasema haya ndio mnayakosa kwa kuichaguwa CCM.

Leo upinzani umekazana Rostam, Rostam, Rostam, Rostam. Huyo Rostam amekuwa mkubwa kuliko upinzani wote, anatisha kwa kutukuzwa na upinzani, kama mnajuwa ana madhambi mbona hatuwaoni mkampeleka mahakamani? au mnaogopa atawaadhiri kama alivyomwadhiri Mtikila?

Hakuna wa kusifiwa kwa kuuboresha upinzani katika Tanzania kama Kikwete, yeye ndio alioahidi kuikuza demokrasi na kweli anafanya hivyo, kwa wengine hatuoni ajabu, ila tunachostaajabu tunapoona upinzani umepewa fursa kubwa sana katika awamu hii lakini hawazitumii ipasavyo, wao wamebaki na ngonjera za Rostam.

Rejea manifesto ya CHADEMA pamoja na hotuba mbadala za mawaziri Vivuli kwenye bajeti iliyopita. Ndugu yangu ni vizuri kufungua macho yako kidogo tu na kujiuliza baadhi ya mambo yafuatayo ambayo yanadhihirisha kupoteza kwa dira kwa Chama cha Magamba:
1) Tatizo la umeme Tanzania lina miaka mingapi mpaka?
2) Uwekezaji wa madini umeleta nini katika nchi hii? Sisi kama nchi hatuwezi kupata the best kutoka rasilimali zetu?
3) Ufisadi wa EPA, Tangold, Meremeta, Kuuzwa kwa NBC, mikataba ya uwindaji,
4) Njaa wakati nchi ina mabonde mazuri ajabu ya kuzalisha chakula kulisha yote na jirani wanaotuzunguka
5) Kuporomoka kiwango cha elimu. Rejea matokeo ya Kidato cha nne 2010.
6) Msongamano na urasimu bandari ya Dar es Salaam kiasi nchi za jirani kama Rwanda, Burundi, DRC kulazimika bandari ya Mombasa.
7) Nchi kutothamini wananchi wake. Rejea mauaji ya Arusha, Nyamongo na kuhamishwa kwa wafugaji bila utaratibu kule Ihefu na hasara walizopata.
8) Ahadi zisizotekelezeka wakati wa kampeni za uchaguzi. Rejea ahadi ya daraja la Mbutu, Meli ziwa Nyasa, Tanganyika, Reli ya kati, reli ya Tanga - Musoma, majosho ya wafugaji, malambo kwa wafugaji wa Igunga.
9) Foleni Dar es Salaam.
10) Tatizo la rushwa katika idara mbalimbali za umma linazidi kukua bila juhudi au mikakati ya kudhibiti tatizo hili. n.k

Kwa hali hii, unafikiri wananchi hawaoni? Fikiria tena kwa makini. Tuache ushabiki kwa ushabiki tu. Ngoma ikilia sana -----------.
 
Haya yamezungumzwa na mh Tendwa kuwa upinzani unakuwa kwa kasi ya 40 asilimia na magamba yanaporoka. Kuna watu humu jamvini wakiambiwa huwa wanabisha sana nadhani sasa wataelewa maana hata hao wakubwa wao wanalijua hilo. Source: Nipashe
upinzani? au chama cha upinzani CHADEMA? anapaswa awemuwazi wakati mwingine.
 
Haya yamezungumzwa na mh Tendwa kuwa upinzani unakuwa kwa kasi ya 40 asilimia na magamba yanaporoka. Kuna watu humu jamvini wakiambiwa huwa wanabisha sana nadhani sasa wataelewa maana hata hao wakubwa wao wanalijua hilo. Source: Nipashe
Jana Dr Banna alisema lake, leo Tendwa nae kanena lake. Watajitokeza wengi na watasema ukweli zaidi. Safari hii wachawi wote watatubu madhambi yao hadharani.
 
Kinachokua ni mawazo ya upinzani na sio vyama vya upinzani. Vyama vya upinzani vinaporomoka kila kukicha na hakuna chama chenye msimamo kudumu; mfano mzuri ni viongozi wa upinzani wanavyohama kutoka chama kimoja kwenda kingine kila kukicha na kusemana wao kwa wao. Mbona wasiwaelimishe wapiga kura na kuachiana majimbo ambayo wanaona mmoja wao ana nguvu? Kwa nini waende kugawa kura?

Kinachokuwa ni mawazo ya upinzani miongoni mwa Watanzania, lakini hayaratibiwi ipasavyo kama Chama tawala kinavyoratibu mambo yake. Na ieleweke kuwa mawazo ya upinzani yanakua kwa sababu ya ulegevu wa Chama tawala, kama cha tawala kikijipanga na kurekebisha hali ya maisha ya Watanzani kwa maana ya huduma za Jamii, mawazo ya upinzani yataisha na kwa maana hiyo upinzani utadorora. Kitakachofuata ni vyama vya upinzani kukosa wafuasi. Vyama vya upinzani vitambue kwamba katika hali ya Tanzania hakuna wanachama wa vyama vya upinzani bali Wapenzi wa vyama hivyo ambao hata kadi za vyama.

Hali hii inadhihirshwa na idadi ya watu wanaojitokeza kwenye mikutano ya Kampeni za uchaguzi na idadi ya kura zinazopigwa kwa vyama vya upinzani. Kuna wengine mtasema chama tawala kinaiba kura, lakini kitaibaje kama vyote viitapiga kura kwa chama cha upinzani na wakti wa kuhesabu ziakonekana kuwa Chama tawala hakikupata kura zozote katika vituo husika?

utajuaje km jimbo hili chama fulani kina nguvu? mfano mzuri ni igunga 2010 cdm hawakuwa na mgombea ,cuf wakapata kura elfu kumi na ushee.
na uchaguzi wa juzi chadema wamepata kura elfu 23 na cuf elfu 2.....je ulitaka cdm wamwachie cuf based on what?
 
Jana Dr Banna alisema lake, leo Tendwa nae kanena lake. Watajitokeza wengi na watasema ukweli zaidi. Safari hii wachawi wote watatubu madhambi yao hadharani.

Bora ya hawa wanaoona hali ya upepo unavyobadilika. Dbagbo na Gadhafi hawakutaka kupima upepo unakoelekea.
 
tendwa1(38).jpg


Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa



Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa, amesema matokeo ya uchaguzi mdogo wa Igunga ambao mgombea wa CCM alishinda kwa mara nyingine yametoa picha kuwa upinzani unazidi kukua na CCM inashuka.....

Akitoa tathimini ya uchaguzi huo, ambao ushindani mkubwa ulishuhudiwa miongoni mwa vyama vitatu wakati wa kampeni, CCM, Chadema na CUF, Tendwa, alisema alikwisha kusema tangu baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana kuwa upinzani umekua kwa asilimia 40 ikilinganisha na ushindi wa kishindo wa CCM wa mwaka 2005. "Matokeo ya uchaguzi wa Igunga yanaonyesha kuwa upinzani unazidi kukua na CCM inashuka," alisema Tendwa alipokuwa akijibu maswali ya waandishi wa habari. Alisema hali hiyo inatokana na ushindani mkubwa wa kisiasa uliopo hivi sasa nchini kati ya vyama vya upinzani na CCM.


Kadhalika alitaja sababu za watu wachache kujitokeza kupiga kura katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Igunga, mkoani Tabora, ikilinganishwa na idadi ya walioandikishwa, kuwa ni pamoja na
ujambazi wa kisiasa uliofanywa na baadhi ya wanasiasa kununua shahada za wapigakura.


Wakati Tendwa akitaja sababu hizo, Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo hilo, Protace Magayene, ameitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) kubuni mbinu mbadala ya kuhakikisha wananchi wanajitokeza kupiga kura. Wapigakura walioandikishwa katika Jimbo la Igunga ni 171,019 na waliojitokeza kupiga kura mwaka huu ni 53,672 sawa na asilimia 31.3, kukiwapo ongezeko la asilimia 2.7 ikilinganishwa na idadi ya waliopiga kura katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana, ambao walikuwa 49,013 sawa na asilimia 28.6 ya 171,077 waliokuwa wamejiandikisha.


Hata hivyo, Tendwa, alisema:"Uchaguzi ulikuwa wa amani na utulivu. Kura zilipigwa kwa amani, hakukuwa na msukosuko, ingawa kulikuwa na kasoro za kiutendaji. Kasoro hizo zimewaathiri watu wa Igunga kutokupiga kura. Aliongeza: "Athari hizo si kubwa, lakini athari ni athari. Idadi ya waliojitokeza kupiga kura Igunga inasikitisha … Nasubiri ripoti, lakini nimeambiwa kulikuwa na kununua kwa kadi za kupiga kura na baadhi ya wanasiasa. Huu ni ujambazi wa kisiasa."


Alisema sababu nyingine iliyochangia watu wachache kujitokeza kupiga kura katika uchaguzi huo, ni kauli na vitendo vya vitisho vilivyotolewa na baadhi ya wanasiasa wakati wa kampeni. Tendwa alisema vitisho hivyo viliwafanya wananchi wa Igunga, ambao wengi wao wanaishi vijijini kuogopa kwenda kupiga kura, badala yake kuamua kwenda kutafuta mahitaji yao muhimu, kama vile maji..............

........Hata hivyo, alisema kila chama cha siasa, kikiwamo chama tawala (CCM), kinawajibika kubadilika na kuzingatia utawala bora, uongozi mzuri na uvumilivu wa kisiasa kwa vile hakiko peke yake katika medani za siasa.

Source: IPPMedia
 
:bolt:Kwa Kauli hii ya Msajili wa vyama vya kisiasa nchini ni uthibitisho kuwa kuna chama cha kisiasa cha majambazi nchini, tuweni makini sana jamani. Inatisha.
 
Niliyasema haya kabla ya uchaguzi wakati mtu mmoja alikamatwa akiwa na kadi za watu na nukuu ya majina na namba zao. Mchezo ule ulikuwa kuyaondoa majina hayo katika orodha ya wapiga kura, kwa sababu ukiuza kadi ndio umeuza haki yako ya kupiga kura,huwezi kupiga kura bila kuwa na kadi ya kupigia kura - Umaskini ni adui wa haki kwani umewaponza haki yao!
 
… Nasubiri ripoti, lakini nimeambiwa kulikuwa na kununua kwa kadi za kupiga kura na baadhi ya wanasiasa. Huu ni ujambazi wa kisiasa."

Indeed this statement shows that Tendwa is continuously improving to the extent of becoming honest
 
Hayati baba wa Taifa alisema maadui wa 3 ni Ujinga, Maradhi na Umasikini.

Tunatakiwa tupambane nayo, ndo maana Mwalimu Nyerere alianza kutoa elimu bure na Elimu ya watu wazima.

Ila baada ya Nyerere kuacha madaraka serikalini, wengine wakaacha kutoa elimu bure ili wao wasomeshe watoto wao na ili wajinga waongezeke Tanzania. Mkakati wa CCM ya sasa ni kutumia ujinga wa watanzania ili waendelee kutawala.

Akina Faiza Fox, Malaria Sugu, Mwita 52 na Nnauye JR (bosi Wao anaewatuma hapa JF) ni mojawapo ya wajinga wanaotegemewa na CCM ili CCM iendelee kutawala.

Wao CCM wanafikiri watanzania wa leo bado ni wajinga sana, Operation Sangara imesaidia sana kuwaelimisha Watanzania na kuwaamsha usingizini.

CCM haijawahi kujenga chochote, zaidi ya kuiba kura tu. Kodi zetu tunazolipa direct au indirect ndo zinajenga nchi. Isitoshe serikali fisadi ya ccm inawatumia akina Rostam, Chenge na R One kuiba kodi zetu na kuchangia kampeni za CCM. CCM wanafaidi ujinga wa baadhi ya watanzania kwa kununua shahada zao za kura au kugawa mahindi ya msaada.
 
Tendwa utapona kweli au wakribia ku staafu au unatuzuga kwamba huko nao jamaa wanunua shahada ? Polisi walisema si kosa mkakaa kimya leo baada ya kila kitu kuwa wazi ndiyo mnakurupuka ? Kweli Tanzania ina maajabu .
 
Back
Top Bottom