TCU hopeless kabisa!

KIDUNDULIMA

JF-Expert Member
Aug 18, 2010
966
538
Kwa kweli nasema TCU hopeless kabisa maana wamedandia kazi ambayo hawaiwezi. Vyuo vimeshatangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa lakini ukilog in kwenye website ya TCU sehemu ya selection status unakuta wameandika "pending" reason "selection not done". Kinachotokea ni kuwa ili uweze kujua kama umechagulia unalazimika kupitia website zote za vyuo ulivyoomba na bahati mbaya baadhi ya vyuo havijaweka taarifa zozote za selection kwenye website zao, vingine website hazifunguki na vingine ndo wana kulink TCU ambako majina hayapo (kama yapo ni yale machache ambayo wao wameita first batch). Option nyingine ni kununua magazeti ya kila siku na kuangalia ni chuo gani kimetoa majina. Ni Vyuo vichache kama UD,UDOM, RUCO, SEKUCO, SJ, SAUTI, SUA, ndio vimeweka majina ya waliochaguliwa kujiunga.

Kwa kweli TCU wamekula Sh 30,000 za applicants kwa kazi ambayo hawana uwezo nayo.
 
Kwa kweli nasema TCU hopeless kabisa maana wamedandia kazi ambayo hawaiwezi. Vyuo vimeshatangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa lakini ukilog in kwenye website ya TCU sehemu ya selection status unakuta wameandika "pending" reason "selection not done". Kinachotokea ni kuwa ili uweze kujua kama umechagulia unalazimika kupitia website zote za vyuo ulivyoomba na bahati mbaya baadhi ya vyuo havijaweka taarifa zozote za selection kwenye website zao, vingine website hazifunguki na vingine ndo wana kulink TCU ambako majina hayapo (kama yapo ni yale machache ambayo wao wameita first batch). Option nyingine ni kununua magazeti ya kila siku na kuangalia ni chuo gani kimetoa majina. Ni Vyuo vichache kama UD,UDOM, RUCO, SEKUCO, SJ, SAUTI, SUA, ndio vimeweka majina ya waliochaguliwa kujiunga.

Kwa kweli TCU wamekula Sh 30,000 za applicants kwa kazi ambayo hawana uwezo nayo.
Hata haijawatendea haki waombaji wengine. Mtu anatoa orodha ya kozi 8 sijui 12 halafu anapangwa ya mwisho badala ya zile za mwanzo ambazo bila shaka ndilo lilikuwa chaguo lake la kwanza. Hii itwasababishia wanafunzi matatizo mbele ya safari kwa kukutwa wamepangwa kozi wasizozipenda au kuzimudu.
 
Hata haijawatendea haki waombaji wengine. Mtu anatoa orodha ya kozi 8 sijui 12 halafu anapangwa ya mwisho badala ya zile za mwanzo ambazo bila shaka ndilo lilikuwa chaguo lake la kwanza. Hii itwasababishia wanafunzi matatizo mbele ya safari kwa kukutwa wamepangwa kozi wasizozipenda au kuzimudu.
TCU Wameleta Mradi wa KIFISADI ambao Mwisho wake ni 31 Oct. 2011 lazima Mahakama zijae.:mad2:
 
TCU wajiweke sawa katika masuala ya tecknologia ya mawasiliano (ICT) ili kufanikisha mambo yao. Matokeo yanatoka kwao lakini wao wenyewe hawawezi kuyaweka. Mtu inabidi apekue chuo kimoja baada ya kiingine ili ajue kapata wapi. Inaelekea hata server yao haina uwezo kabisa. Nahisi kitengo chao chao ICT ni dhaifu kabisa.
Njia nyingine ni kuweka hayo majina tena kwa wakati mmoja katika tovuti ya Serikali na ile ya wizara ya elimu. Wanaweza pia kuweka katika tovuti za baraza la mitihani na bodi ya mikopo. Zote hizo ni taasisi ambazo wanapaswa kuwa na uhusiano wa karibu.
Tunajua mwanzo una matatizo yake lakini mwakani waboreshe kutokana na walioyaona mwaka huu.
 
Back
Top Bottom