TCU: Darasa la saba sasa kujiunga na chuo kikuu moja kwa moja

Sina uelewa mpana wa mifumo ya elimu duniani, lakini kuna ka-harufu ka hatari kananukia nchi yetu. Yaani darasa la saba hili la Tanzania ya leo ambapo mtoto anashindwa kupata alama za kujiunga na shule za kata, then akasome chuo kikuu kwa mitihani ya masomo matatu? Sasa practically, huyu darasa la saba wa miaka hii 25 atapata udhoefu wa kutoka wapi, na fani ipi/ Kwa sababu nijuavyo mie, Serikali na waajiri wengi wanachukua kuanzia form 4, hawa Darasa la 7 wengi ni ma-house boy na house girl ambao hata hivyo wengi nao hawawataki siku hizi. TCU mnataka kutupeleka wapi, hebbu tunaomba wekeni hadharani utafiti mlioufanya ili tuone ikiwa kweli mko sahihi, lakini kama mnafanya kazi kwa ki-memo; kwa kweli Taifa laelekea kubaya sana. Nadhani ingefaa kuimarisha mfumo wa QT na VETA na kuifanya iwe lazima kwa anayeshindwa kuendelea na Kidato cha kwanza, badala ya hii mnayotaka kufanya, ni msiba huu. Kama watoto wadogo wa drs la saba na kidato cha 4 wanaiba mitihani, mnadhani hawa watu wazima wenye hela zao waliokimbia shule na sasa kutaka kuwa na veti vya chuo kikuu watashindwa kuiba mitihani?

Lakini pia Kwani utalaam na kulitumikia Taifa mpaka uwe na cheti cha elimu ya chuo kikuu pekee. Mbona tunao wasio na na vyeti vya chuo kikuu lakini wako vema kwa utambulisho wao huo wa Darasa la saba n.k. Whats motives behind this move? Jibu la watanzania kimya
Mkuu usichoelewa hapa ni nini!tayari kuna wakuu huko serikalini wameshajijua wana ma vyeti ya kufoji na wameshahisi kustukiwa kwahiyo wamebuni mpango ambao utawasaidia kupata vyeti vya chuo kikuu kihalali,std seven ambaye anafanya kazi ya kuajiriwa anapatikana wapi kama si wale wa mwaka 47 wanaokaribia kustaafu!
 
Nafasi nzuri kwa Sugu na Lema wakaongeze elimu ya matusi na udini
 
kifutajasho kwa waliokosaga kuchaguliwa wakati shule zilipokuwa chache kuna wa2 kibao walikuwa na uwezo kiakili. lakini hawakufaulu.pia kwa walimu itasaidia waongeze elimu.
 
kwanini hao watu VETA haiwafai? kama iko kiufundi zaid basi itanuliwe waingie na watu wasio wa ufundi. au vyuo vya vya vipaji maalum. kutakuwa na faida gani ukimaliza darasa la 7 usiende kutafuta hela na uendelee kusoma?
 
Tume ya vyuo vikuu nchini Tanzania ( TCU) imeanza mchakato kwa watu wenye elimu ya darasa la saba kuweza kupata elimu ya shahada ya kwanza katika kozi mbalimbali hapa nchini. Ofisa Uhusiano wa TCU bwana Edward Mkaku amesema vyuo vitakavyotumika ni chuo cha Tumanini cha Dar es Salaam, UDSM na chuo kikuu cha Mzumbe! vigezo mwombaji lazima awe na umri wa miaka 25 na kuendelea, barua ya mwajiri, awe ana uwezo wa kuongea na kuandika kiingereza kwa ufasaha na utayari wa kusoma elimu ya juu.Alimalizia kwa kusema wameanzisha program hii kubaini vipaji vya watu walioshia darasa la saba.

huu pia ni ushauri wa mtaalam mwelekezi toka malaysia?duh!hii itakuwa kwenye lab gani?
 
STOP SHOUTING !

Binafsi sitaacha kupambana na wasomi wapumbavu tena baadhi yao wemeendelea kuwa victims mpaka hapa JF bila kufikiria kuwa this is the home of great thinkers.

Theres no any problem with RPL System na kwa mtu mwenye ubongo wenye afya ni muda wa kujilaumu kwanini mfumo huu haukuwepo tangia miaka 10 iliyopita.

wanao lalamikia kuwa ni kitendo cha kuhalibu mfumo wa elimu ni wale wote waliopoteza a lot o years o level & Advance Thats Stupid, hebu tizama tafsiri ya RPL according to Wikipedia

Recognition of prior learning
(RPL), prior learning assessment (PLA), or prior learning assessment and recognition (PLAR), describes a process used by colleges and universities around the world to evaluate learning acquired outside the classroom for the purpose of assigning academic credit. Common ways individuals have acquired college-level learning include: corporate or military training; work experience; civic activity; and independent study.

Methods to assess prior learning are varied and include: standardized exams such as those delivered by the College Board, the Excelsior College Examination Program or DANTES Subject Standardized Tests Program; American Council on Education (ACE) Guides to credit recommendations for civilian and military training programs; evaluations of local training programs by local colleges, campus challenge exams; and portfolio assessments of experiential learning.
Prior Learning Assessment programs should not be confused with so-called life experience degrees, which purport to offer academic recognition of work experience but do not in fact have degree status and are illegal in many jurisdictions.

mfumo huu utamuwezesha mzee ilasi mfanya biashara mkubwa Mbozi mwenye mashule na mahospitali na mabasi ya mikoani huku akiwa na elimu ya darasa la saba kwenda kusomea business admistration na kuwa mtu mwenye ujuzi zaidi, na uwezo wa kufanya makubwa zaidi.

HONGERA SANA TCU TENA SANA hii itasaidia sana pia katika kuleta development competition baina ya wasomi katika jamii, wale wenye degree magamba inabidi watumie degree zao kufanya changes au la Watajuta.
 
sipati picha fundi magari alieshia darasa la 7 mwaka 1989 aanze mwaka wa kwanza chuo kikuu kusomea mechanical engineering pamoja na vijana waliotoka ftc na form 6. watafundishwa hesabu pamoja, ds etc. teh teh. hah hah hah.
 
Tanzania kwa ngonjera mnafurahisha sana! wapo maelfu waliomaliza kidato cha sita na diploma na wamekosa nafasi za kujiunga na chuo kikuu kutokana na ufinyu wa mikopo na nafasi leo mnazungumzia darasa la saba,.Nyie viongozi wapanga sera mmeshatuona watanzania hatuna ubongo kabisa au vipi??
Mi nadhani kuna njama za makusudi zinafanywa na viongozi wa hii serikali ili kuhakiki 2015 haiingii madarakani,kama hivyo ndivyo ni safi sana endeleeni tu ku-implement sera za mtindo huo na mkihitaji nyingine niambieni niwape!
 
Kwa msaada zaidi huyu jamaa anajiita click yeye akizungumzia RPL wakati akijibu swali miaka miaka 5 iliyopita kwenye mtandao wa yahoo answers alisema
"I've been in managing a small business for the past 10 years, and when I finally went to University to get my Bachelor of Business they gave me RPL for some of the courses."

Follow the link What does rpl mean???? - Yahoo! Answers

Acheni upuuzi wa kuponda hata vitu vizuri kwakuwa wewe ulisha teseka.
 
Jamani, kwani Veta vimewakataa darasa la saba? Hizo kozi wapeleke huko.

Kuna watoto wa wakuu wameshindikana kupata credit sasa wanatafutiwa degree
 
Je watapewa boom? Je utamjuaje mtu mwenye kipaji? Au, je vyuo vitakuwa na wataalamu wa uanishaji wa vipaji vya waombaji mbalimbali? Kama ni hivyo, hata wale waalimu wa UPE wanastahili kusoma shahada kwa kuwa wanavipaji vya kufundisha. Je watapewa boom? Je huu mfumo umetoka nchi gani? Maswali yanazaliwa kila dakika nikifikiria juu ya uendeshwaji wa mpango huo. Naomba mnaofahamu vizuri mtupe majibu, kwa kuwa jamii inahitaji ufafanuzi wa kina.
 
Ona mbele zaidi huu mfumo .unatumika Marekani ,Uingereza , Ufaransa e.c.t nyingi duniani ,Nimfumo mzuri sana kwa kukuza vipaji ,mfano hapo meru Arusha kuna kijana kaunda trekta ni darasa la saba ,unaonaje huyu akichukuliwa chuo kikuu kwa elimu zaidi ?

Hii biashara ya kufanya kila ukisikia Marekani unahisi umesikia Mbinguni muache nyie vilaza, leo hii nchi imeharibika kwa ajili ya mambo yenu ya kukopi na kupaste. Wao ni developed we are just LDC yaani mlima na kichuguu alafu mnalinganisha??? Embu mkuwe kifikra jamani
 
Wakuu..

Nimesoma hii habari kuwa Watu waliofika kuanzia darasa la saba na kuendelea ambao hawakuweza kujiendeleza lakini wana uzoefu kazini watapata Nafasi ya kusoma Digree katika Vyuo hapa TZ.

Habari hii ni Nzuri lakini pia ni Mbaya.

Ubaya ni kuwa sasa Digrii Itakuwa kitu cha Kawaida sana,Kiasi kwamba Mtu mwenye Bachelor Degree atakuwa kama vile Mtu wa Form Four kwa Sababu itakuwa ni Yeboyebo.

Nachelea kusema kuwa UPATIKANAJI WA AJIRA UTAKUWA MGUMU SANA Kwa sababu karibu kila mtu sasa atakuwa na Digrii.

 
Naziona digirii za sanaa kibao sasa maana hawa wasanii wetu na viingereza vyao vya kuungaunga hii hawaishindwi
 
Back
Top Bottom