TCRA mmebariki huu Upuuzi wa Viongozi wa Timu za Ndondo Cup Kusifia kufanya Ushirikina Mubashara Redioni Clouds FM?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,738
109,177
"Hela tuliyopata tumeenda kununua Mayai Viza, Kuku Mweusi na Udi na kumpelekea Mganga wetu wa Kienyeji na kwa jinsi tunavyoenda Kuwaroga Watatukoma" Shabiki wa Timu Moja inayoshiriki Michuano iliyosifiwa na inayosapotiwa na Rais wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ya Ndondo Cup' kwa Mikoa ya Dar es Salaam na Dodoma.

Je, TCRA huu Uhuni, Upuuzi na kutokuheshimu Maadili ya Mwafrika na hata kwa Mwenyezi Mungu kutotaka Ushirikina kwa Wanadamu nyie kama Wadhibiti Wakuu wa Maudhui ya Utangazaji mmeubariki na labda ndiyo maana mnaachia tu lizoeleke?

Nguvu ya Kumdhibiti Msanii Ney wa Mitego ambaye Nyimbo zake zina Ujumbe Mkubwa na Afya ya Akili ( Fikra ) Kwetu wenye Akili akina GENTAMYCINE mnayo, ila ya Kuzuia na Kukemea Maudhui ya Kiushirikina ( hasa Kuusifia na Kujivunia ) nao Redioni au katika Runinga hamna na wala hamthubutu.
 
Back
Top Bottom