TBC1 yasitisha kuonesha baadhi ya Mikutano ya Bunge moja kwa moja (Bunge LIVE)

Ni maafa, tena makubwa sana. Waziri Nape kaleta kauli ya serikali Bungeni kuwa maonyesho ya moja kwa moja Bungeni hayatakuwepo tena eti ni gharama na TBC1 hawana uwezo wa kugharamia shilingi Bil 4 kwa mwaka.

Dalili za kutoruhusu mijadala hiyo hasa kwa sasa wanapoijadili hotuba ya Rais ni kuwa hawataki wananchi waone wabunge wanavyo ichambua na kuiagiza serikali ifanye nini. Jee zuio hili lina baraka za Rais Magufuli?

Mbona yeye anapotumbua majipu anapenda kupata coverage ya TV na Radio na awe hataki serikali yake kuwa kikaangoni watu waone? Hii ni dalili mbaya sana ya utawala wake na ni dhahiri anayoyafanya yana ashiria kuwa ni maigizo tuu na hana nia ya dhati ya uwajibikaji kwa mawaziri ambao tayari kaonyesha kutokuwa na imani nao kuweza kuwakabili wabunge.

Namsifu sana Mhe Zitto Kabwe kwa kuonyesha ujasiri wa kulipigania hilo ingawa amekumbana na vikwazo toka kwa Mwenyekiti wa Bunge Chenge. Chenge pamoja na kutajwa kuwa ni mweledi katika mambo ya sheria lakini leo kaonyesha ni mtupu kabisa na kawekwa pale kwa malengo maalum.Sisi wananchi kama wamiliki wa TBC1 tupinge kwa nguvu chombo hicho kuzuiwa kutuonyesha Bunge live.
 
ni vema tu maana kuna baadh ya vituko vinavyofanywa na waheshimiwa ni msukumo wa kuonwa na wananchi live. i agreed with
 
Aaah! Kweli RAIA wa Tz hatuna thamani Mbele ya serikali yetu, yaani pamoja na kodi zote tunazolipa lakini bado tunanyimwa kujua nini wanafanya watu tuliowatuma kutuwakilisha bungeni, Daaah! Mama Tanzania watoto wako baadhi hatuna tena thamani na mambo yakuhusuyo na yatuhusuyo.
 
Tunapoelekea, tutakuja kuambiwa hata kuendesha magari mwisho saa kumi jioni... kwa sababu ya gharama kubwa za kukarabati barabara...
 
Safi sana hiki kilikuwa ni kilio changu siku zote, Watu wafanye kazi na waache kuangalia Bunge, mkirudi nyumbani jioni baada yakazi mtaangalia Bunge tani yenu au kama mmechoka hata wkend!

Safi sana W. Nape!
Sina hakika kama unajua unachopongeza hapo...
 
Wananchi wale tu hata wanaofanya kazi na kulipa PAYE tunaweza kutolewa hata shilling Mmoja kulipia matangazo ya Bunge Hivi nape huwaga anamka toka usingizini ati wananchi tumeafiii mlitupa tupige kura ya maoni katika uamuzi huuu kwani Nape unaleta mzaha kwenya mambo ya msingi Rais JPM huyu ndio umeona anafaaaa kwenye wizara ya Habari au ndio mbinu mbadala wa kuuwa vyombo vya habari mbona mnakinzana saaana na hali ahalisi ya ulimwengu wenzenu Media ndio kitu muhimu kuwaelimisha wananchi nyie mnakifungia na kukipa mashariti ya ajabu saaana
 
Katika kauli za Mawaziri, Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye, ametangaza kwamba, Kuanzia tarehe 26 Januari mwaka 2016, TBC1 haitaonesha tena Mikutano ya bunge live kutokana na gharama za kuonesha live kufikia bilioni nne kwa mwaka.

Badala yake TBC1 watarekodi na kuonesha katika kipindi maalum usiku kuanzia saa nne hadi saa tano.

Hii itanyima wanchi fursa ya kuona kinachoendelea Bungeni.
Huu ni uhuni. Kama TBC hawawezi kuonyesha LIVE basi wawapishe channels zingine zenye uwezo zionyeshe.
 
yelewiiiiiiiiiiiiiiiii sasa tutarajie kuona harusi live kwa wingi


hivi itv star na wengine ambao wanajitegemea wanafanyaje aisee hii wizara ni jipu.. badala kufanya ubunifu wapate jinsi ya kutuonyesha jambo hili muhimu kwa taifa wanaleta longolongo piga chini muhusika

Cc: Nape Nauye
Cc: Jonh P Magufuli
 
Sina hakika kama unajua unachopongeza hapo...

Ninakijua sana kwamba watu wafanye kazi na waache uvivu kwa kuanglia luninga muda ambao walipaswa wafanye uzalishaji na kuongeza kipato chao na cha nchi kwa ujumla!

SAFI SANA W. NAPE!
 
Sasa gharama hizi zinawahusu mpaka Star Tv?
Hii ni sehemu ndogo sana ya madhaifu tunayo enda kuyashuhudia ndani ya serikali hii ya awamu ya tano.
Walianza kwa kuleta sheria ya mitandao kabla ya uchaguzi mkuu lengo lao ikiwa kuwatisha na kuwadhibiti watu. Wakataka kuleta mswada wa vyombo vya habari ambao sehemu ya muswada huo ungelazimisha Tv stations zote kujiunga na Tbc 1 wakati wa taarifa ya habari lakini MUNGU si mwalubadu.
Juzi tu hapa wamelifungia gazeti la mawio kisa linaandika habari za ukweli.
Eti leo wanaidhibiti Tbc kuonyesha live shughuli za bunge sababu gharama za uendeshaji ni kubwa, sawa. Vipi kuhusu Star Tv? Wao pia wanarusha matangazo ya bunge Live bila kujiunga na Tbc, iweje nao waondoke hewani muda ambao Tbc wanakata matangazo? Nao wamegundua kwamba gharama za uendeshaji ni kubwa?
 
Hii itasababisha kujenga chuki kati ya serikali na wapiga kura wa nafikiri kuna vitu wanaficha kumbe wanaharibu.
 
Katika kauli za Mawaziri, Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye, ametangaza kwamba, Kuanzia tarehe 26 Januari mwaka 2016, TBC1 haitaonesha tena Mikutano ya bunge live kutokana na gharama za kuonesha live kufikia bilioni nne kwa mwaka.

Asante waziri Nape kupunguza mzigo kwa mlipa kodi kwa hayo mabilioni.Maana yangetumika ina maana mlipa kodi angekamuliwa yapatikane.Yaani mabilioni yote hayo yalikuwa yakitumika kuangalia tu sura za wabunge kwenye TV?

Tunachotaka ni maamuzi yaliyofikiwa hizo porojo,marumbano ,vijembe si vitu vya muhimu kwa mtanzania.Naunga mkono kusitisha

Ondoeni na sitting allowance za wabunge mpunguze mzigo kwa mlipa kodi
 
Kama ni garama kwa serikali, kwa nini wasitoe ruksa kwa TV binafsi kurusha hayo matangazo kama ilivyo kwenye mpira? Uhuru wa vyombo vya habari uko wapi nchi hii?
 
Back
Top Bottom