Johnny Sack
JF-Expert Member
- Jan 21, 2017
- 8,834
- 18,837
Nimeisikiliza hotuba ya Dk Slaa kuhusu Legacy ya Magufuli, sikatai kuwa Magufuli ana mambo mazuri na ana legacy yake inayopaswa kuenziwa, lakini alikuwa na mapungufu mengi ambayo hata wana CCM wenyewe wanakubali, na Rais Samia mabye ndiye mwenyekiti wa CCM na Rais kwa sasa anarekebisha mabaya ya Magufuli
Sasa Dk Slaa alipaswa kujikita kwenye m,azuri ya Magufuli na kuyaacha yale mabaya na sio kulazimisha kutetea mabaya
Kwanza kabisa Slaa anaanza kwa kuilamumu Serikali ni kwa nini ilikaa kimya kuhusu Magufuli kuugua, anailamu serikali ya sasa huku akijua Magufuli na serikali yake ndiyo ambayo ilikuwa ikiendesha mambo kwa usiri na propaganda, Serikali yake tunakumbuka ilivyoingiza propaganda nyingi kwenye ugonjwa wa Covid na waliokuwa wakifariki kwa ugonjwa huo walisemwa wamefariki kwa changamoto za kupumua
Slaa anaenda tena kumtetea Magufuli kuhusu mauaji ya watu, na kusema pia mbona Ulaya watu pia wanauawa, sasa Ulaya watu wakiuawa ndio inakuwa excuse ya kuua?
Slaa pia anatetea uamuzi wa Magufuli kuhusu kubambikiza watu kesi na kusema pia kipindi cha Kikwete kuna watendaji wa vijiji walikuwa wakibambikiza watu kesi, jamani baya linahalalisha baya? ameshindwa kujikita tu kuelezea mazuri badala ya kulazimisha kumsafisha?
Slaa ameonekana pia kuunga mkono uamuzi wa Magufuli kuhusu wanafunzi wanaopatga mimba kurudi shule na kusema hata Ulaya walikuwa wanafanya forced sterlization, sasa inahusiana vipi?
Slaa ambaye alikuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Upinzani anasema Magufuli anasemwa alikuwa sio mwanademokrasia lakini alipendwa na wanyonge na hilo ndio la muhimu, kweli? sasa alijiunga na upinzani ya kazi gani kama demokrasia haina umuhimu?
TBC kuweni makini, msomeni Samia kwa sasa anataka nchi yenye amani, siasa safi na maendeleo, ufashiti tulishaachana nao
Sasa Dk Slaa alipaswa kujikita kwenye m,azuri ya Magufuli na kuyaacha yale mabaya na sio kulazimisha kutetea mabaya
Kwanza kabisa Slaa anaanza kwa kuilamumu Serikali ni kwa nini ilikaa kimya kuhusu Magufuli kuugua, anailamu serikali ya sasa huku akijua Magufuli na serikali yake ndiyo ambayo ilikuwa ikiendesha mambo kwa usiri na propaganda, Serikali yake tunakumbuka ilivyoingiza propaganda nyingi kwenye ugonjwa wa Covid na waliokuwa wakifariki kwa ugonjwa huo walisemwa wamefariki kwa changamoto za kupumua
Slaa anaenda tena kumtetea Magufuli kuhusu mauaji ya watu, na kusema pia mbona Ulaya watu pia wanauawa, sasa Ulaya watu wakiuawa ndio inakuwa excuse ya kuua?
Slaa pia anatetea uamuzi wa Magufuli kuhusu kubambikiza watu kesi na kusema pia kipindi cha Kikwete kuna watendaji wa vijiji walikuwa wakibambikiza watu kesi, jamani baya linahalalisha baya? ameshindwa kujikita tu kuelezea mazuri badala ya kulazimisha kumsafisha?
Slaa ameonekana pia kuunga mkono uamuzi wa Magufuli kuhusu wanafunzi wanaopatga mimba kurudi shule na kusema hata Ulaya walikuwa wanafanya forced sterlization, sasa inahusiana vipi?
Slaa ambaye alikuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Upinzani anasema Magufuli anasemwa alikuwa sio mwanademokrasia lakini alipendwa na wanyonge na hilo ndio la muhimu, kweli? sasa alijiunga na upinzani ya kazi gani kama demokrasia haina umuhimu?
TBC kuweni makini, msomeni Samia kwa sasa anataka nchi yenye amani, siasa safi na maendeleo, ufashiti tulishaachana nao