Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,813
- 11,991
Pia amemshukuru Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Utalii Tanzania (TATO) Bwana Sirili Akko kwa niaba ya bodi ya TATO kwa namna walivyo Fadhili safari yao katika hifadhi ya Taifa Tarangilie iliyopo kaskazini mwa Tanzania ambapo amebainisha kuwa hifadhi hiyo ni nzuri huku akiwaomba watanzania kutembelea hifadhi hiyo.
Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Utalii Tanzania (TATO) Bwana Sirili Akko amesema wataendelea kushikiana na Jeshi la Polisi kwa karibu huku akibainisha kuwa mtaji Mkubwa wa sekta hiyo ni usalama kwa watalii ambapo amebainisha kuwa mafunzo ya ukaguzi wa vyombo vya moto umekuja wakati sahihi kukiwa na wingi wa wageni wa ndani na nje ya Tanzania.
Bwana Sirili ametumia fursa hiyo kumshukuru Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuwa kinara wa kutoa dira katika sekta ya utalii nchini ambayo ilichagizwa na filamu ya Tanzania The Royal Tour ambayo imesaidia kuongeza watalii wengi kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika na Ulaya.
Nae Mkuu wa Mkuu wa kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha Mrakibu mwandamizi wa Polisi SSP Zauda Mohamed amesema kikosi hicho kimepata mafunzo ya viwango vyaa juu kulingana na mabadiliko ya teknolojia ya vyombo vya moto ambavyo vimekuwa vikiingia hapa nchini huku akiwaomba wadau wa utalii kutumia wataalam wa Jeshi hilo kufanya ukaguzi wa vyombo vyao ambavyo hubeba watalii.