King Kong III
JF-Expert Member
- Oct 15, 2010
- 51,685
- 68,667
Pole mkubwa nishaona watu kama wa3 hv wenye problem kama yako!
JF DCTORS;
naomba msaada wenu, mimi nina vipele flani kisogoni, ni vile ambavyo watu wengi huwtoka wakati wakinyoa kwa wengi hupona baada ya muda mfupi, lakini kwangu haikuwa hivyo vipo mpaka sasa ni mwaka wa tisa na kila siku vinazidi kuongezeka, nmeshawahi kumuona dr. mmoja pale udsm akanambia kuwa haviponi hivyo nisijaribu kuvichezea tu havitakua, nkaona haitoshi nkaenda kairuki kuonana na specialist wa pale nae akanambia haviponi ila kuna dawa yeye anatengeneza ya ku-mix chemicals hiyo anaiuza yeye tsh. laki tano na unatumia hiyo dawa kwa mda wa miezi sita mpaka mwaka mmoja,kwa uwezo wangu nikawa nmeshindwa kuipata.
Hivi vipele haviumu ila vinanikosesha uhuru na kuniaribia pozi mida flani hivi na kila siku vinaongezeka, nmeshawahi kumuona mtu akiwa na li-nyama likubwa kisogoni ambayo ni baada ya vipele hivi kufikia stage ya mwisho ya ukuaji, naomba msaada wenu jamani hata kwa dawa ya asili
Paka medicated cream inaitwa Betacort-N,nilikuwa navyo vikapotea jumla,sasa sijui vyako viko kwenye extent gani,kwani mimi vilishanitokea kama mara mbili na nilipotumia hiyo dawa ika-work very successful.
Pole sana ndugu yangu.Mimi nilikuwa navyo nimetumia dawa moja kutoka Bk NIMEPONA KASIBA wao BK wanaita nshundo.Anyway nPM nikupedata zaidi na jinsi tunaweza kuwasiliana
Nilipata vipele hivyo kwa kinyozi. Nilichofanya niliacha kwenda salon, nikanunua vifaa vyangu vya kunyolea nyumbani.
Vipele vilidumu kwa miaka kama 3 au 4 hivi, nilichukuwa mdalasini na asali nakoroga kisha napaka kwa kusugua kwa nguvu jioni baada ya kuoga, vilianza kupungua na baadaye vilitoweka kabisa.
unataka akupm ili umpe jina la dawa, unaona ukiweka hapa peupe watu watafaidika? watu wabinafsi bwana...saidia wenzio wenye tatizo, kuna wengi hapa wanahitaji kama hilo, hapa ni jf where we dare to talk openly, sasa mambo ya sirisiri ya kupm ya nini? weka jina hapa peupe ili watu walijue wakatafute iyo dawa, kwani wewe pia si unafaidia na vingi tu vya wenzio wanaoweka mambo mazuri hapa na haulipii chochote kwao?....acha ubinafsi.Pole sana ndugu yangu.Mimi nilikuwa navyo nimetumia dawa moja kutoka Bk NIMEPONA KASIBA wao BK wanaita nshundo.Anyway nPM nikupedata zaidi na jinsi tunaweza kuwasiliana
umepanga kwenda hospital. nenda mkuu humu utaombwa picha tu. cc mzizimkavu
Mkuu ivo vipele usivitumbue la sivyo utaota linyama nyuma ya Shingo. Kwa uchunguzi wangu niligundua ugonjwa huu unaambukizwa kwa kupitia mashine za kunyolea masaluni Nina ushahid wa watu waliotoka linyama nyuma ya shingo
Chukuwa kitunguu Saumu Ukitwange mpaka kiwe laini kisha Uchukuwe maji ya moto Uoshe sehemu zenye vipele Ufanye kama Unasugua
Hivi huu ni ugonjwa kumbe? Hee mi nlijua ni kunenepa ka kitambi tu
Duuuh yaelekea wewe hata chunusi unajua ni unene!