VIP passport ndio kitu gani?Kanumba nchi nyingine huwapa VIP passport na huwa wanapewa mazishi ya Kitaifa
Mara nyingi binadamu huwa tunachagua vifo vyetu!!
Umenena...uzito wa msiba anaufeel mfiwaInategemea na watu wengi wapo kundi gani. Kwa wasomi kama mimi, kifo cha Prof kinakuwa na uzito kuliko cha msanii ambaye hana mchango wa karibu katika maisha yangu au kifo cha rais wa nchi nyingine. Kwa watu wa filamu na udaku udaku na usanii, kifo cha msanii kinakuwa na uzito kwao kuliko cha Prof, kwani kwao elimu haina maana. Kwa waMalawi waliopo Tanzania, kifo cha rais wao kina uzito kuliko msanii wa bongo na Prof wa bongo. Sasa kama utafiti wako upo sahihi na umeonyesha Kanumba kawafunika wengine, basi unatakiwa kugundua mara moja kuwa waTanzania wasomi walioshtushwa na kifo cha Prof ni wachache (na huo ndio ukweli, nchi hii ina wasomi wachache kuliko wajinga), na waMalawi waliopo nchini ni wachache kuliko waTanzania wanaopoteza muda kuangalia movies za Kanumba (na huo ndio ukweli, sitegemei kuwa na Wamalawi wengi nchini kuliko wasoma magazeti ya udaku yanayoandika wasanii kila siku). Kwa hiyo hii thread haiko valid, kwani ni kitu kinachotazamiwa kabisa. Lakini kukiwa na coincidence ya mazishi na iwapo kuna ulazima wa kuhudhuria mazishi, mimi nitahudhuria ya Prof (wengine hudhurieni ya mcheza filamu)