Mbonea
JF-Expert Member
- Jul 14, 2009
- 640
- 20
Kumekuwa na kasumba hapa nchini kwetu ya kuwakaribisha kwa bashasha esp kwa watu walioweza kufanya mambo fulani makubwa. Hilo sikatai lakini jeh, kuna haja ya kufanya zaidi ya hapo? Kwa mfano, hivi majuzi Hashim Thabeet (kijana aliyetumia juhudi zake binafsi kufika hapo alipofika), alirudi nchini na kupokelewa na viongozi wa serikali na si kwamba hiyo ilitosha bali pia alipata fursa ya kukaribishwa ikulu. Lakini je! Na wale wasiojiweza kama vile ombaomba, wajane, watoto wa mitaani n.k walishawahi fanyiwa hivyo?. Ikumbukwe hawa Wako hapa hapa nchini
.!
Nani wakuangaliwa zaidi? Waliofanikiwa tayari, au hawa waliochini? NISAIDIENI WADAU
Nani wakuangaliwa zaidi? Waliofanikiwa tayari, au hawa waliochini? NISAIDIENI WADAU