Rutunga M
JF-Expert Member
- Mar 16, 2009
- 1,769
- 1,382
Imeandikwa na mwananchi la leo
soma hapa
Raymond Kaminyoge
LUNINGA au televisheni za teknolojia ya analojia zenye `matumbo' hazitafanya kazi kuanzia Januari Mosi, 2013 hadi ziunganishwe na ving'amuzi vitakavyonunuliwa kutoka kwa kampuni ambazo ni wakala wa vituo vya televisheni.
Hatua hiyo imekuja baada ya Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa kutangaza kusitishwa kwa matangazo ya Televisheni kwa kutumia analojia kwenda digitali kuanzia Januari Mosi 2013.
Akizungumza na Mwananchi kuhusu kauli hiyo ya Waziri, mtaalam wa vifaa vya elektroniki, Damas Mligo alisema zile luninga za zamani itabidi ziunganishwe na ving'amuzi ndipo zifanye kazi. Bei ya ving'amuzi katika kampuni mbalimbali zinaanzia Sh70,000.
Alisema kuna baadhi ya luninga za digitali ambazo ving'amuzi vimejengewa ndani hizo zitatumika kama kawaida.
Waziri Mbarawa aliwataka wananchi kujiandaa mapema hasa kununua ving'amuzi kwa luninga ambazo zinatumia teknolojia ya analojia.
Alisema faida ya digitali ni kuongezeka kwa ubora wa matangazo na ongezeko la vituo vya televisheni.
Aidha Mbarawa alisema faida nyingine ya kuingia kwa teknolojia ya digitali ni matangazo ya televisheni kupatikana katika wingi zaidi vya mawasiliano kama vile simu za mkononi na kompyuta kupitia mtandao wa intaneti.
" Nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki zimekubaliana kuwa ifikapo Desemba 31, 2012 saa sita kamili usiku vituo vyote vya utangazaji vinavyotumia teknolojia ya analojia vitazima mitambo yake na kutumia digitali,"
alisema Profesa Mbarawa.
soma hapa
Raymond Kaminyoge
LUNINGA au televisheni za teknolojia ya analojia zenye `matumbo' hazitafanya kazi kuanzia Januari Mosi, 2013 hadi ziunganishwe na ving'amuzi vitakavyonunuliwa kutoka kwa kampuni ambazo ni wakala wa vituo vya televisheni.
Hatua hiyo imekuja baada ya Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa kutangaza kusitishwa kwa matangazo ya Televisheni kwa kutumia analojia kwenda digitali kuanzia Januari Mosi 2013.
Akizungumza na Mwananchi kuhusu kauli hiyo ya Waziri, mtaalam wa vifaa vya elektroniki, Damas Mligo alisema zile luninga za zamani itabidi ziunganishwe na ving'amuzi ndipo zifanye kazi. Bei ya ving'amuzi katika kampuni mbalimbali zinaanzia Sh70,000.
Alisema kuna baadhi ya luninga za digitali ambazo ving'amuzi vimejengewa ndani hizo zitatumika kama kawaida.
Waziri Mbarawa aliwataka wananchi kujiandaa mapema hasa kununua ving'amuzi kwa luninga ambazo zinatumia teknolojia ya analojia.
Alisema faida ya digitali ni kuongezeka kwa ubora wa matangazo na ongezeko la vituo vya televisheni.
Aidha Mbarawa alisema faida nyingine ya kuingia kwa teknolojia ya digitali ni matangazo ya televisheni kupatikana katika wingi zaidi vya mawasiliano kama vile simu za mkononi na kompyuta kupitia mtandao wa intaneti.
" Nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki zimekubaliana kuwa ifikapo Desemba 31, 2012 saa sita kamili usiku vituo vyote vya utangazaji vinavyotumia teknolojia ya analojia vitazima mitambo yake na kutumia digitali,"
alisema Profesa Mbarawa.