Tanzania: Kushuka kwa thamani ya shillingi, mfumuko wa bei na siasa zetu!

Mkuu,
Hii hali inayoendelea ni nchini kote,kila kipembe, mkoa, mji na kijiji.
Lililo baya ni kuwa kiwango cha wagonjwa wa kisukari itazidi sana kwa sababu watu watalazimika kula vyakula vya uwanga tu zaidi. Pia utapia mlo kwa watoto na watu wazima.
Hii itapelekea watu kufa kama kuku na kuziumiza familia nyingi kiuchumi zaidi ya huu umaskini walionao leo.

wakati watawala wetu wanataka tuamini uchumi unaboreka, uhalisia wa maisha kwa wananchi wa kawaida uko tofauti, maisha yao yanazidi kudidimia na kuwa ya shida zaidi.

Katika nchi nyengine wananchi yamewashinda na wamepeleka ujumbe kwa watawala, sisi hatujafikia kiwango cha ujasiri bado. Tunakula "amani na utulivu wetu" huku tunajifea kama kuku na hata wa kutuzika hatuna.....Lakini tutafika! Lini!!???

Serikali inavyosema inajizatiti kukabiliana na kisukari... Vituko kweli kweli!
Hii habari ipo IPPMEDIA
Serikali yajipanga kudhibiti kisukari

Na Elizabeth Zaya 27th January 2011

[FONT=ArialMT, sans-serif]Serikali imezindua programu maalum inayolenga katika kushughulika na udhibiti wa ugonjwa wa kisukari nchini ambapo jumla ya Dola za kimarekani milioni 2.3 zinatarajia kutumika.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Akizindua programu hiyo jijini Dar es Salaam jana, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Hadji Hussein Mponda, alisema programu hiyo itadumu kwa miaka minne na lengo lake ni kuhakikisha ugonjwa huo unadhibitiwa kwa asilimia kubwa.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Dk. Mponda alisema kati ya magonjwa yasiyoambukiza, kisukari ndio unaonekana kuwa wa kwanza kwa kuongeza idadi ya wagonjwa ambapo asilimia tano mpaka sita ya wagonjwa wa kisukari wanaishi mijini, na asilimia moja tu ni waishio vijijini.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Alizitaja baadhi ya sababu zinazochangia ni umaskini, matumizi mengi ya tumbaku, kutofanya mazoezi, matumizi mabovu ya chakula na matuimizi mengi ya kilevi.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Aidha alisema programu hii pia inalenga kutoa huduma kwa wagonjwa wanaougua ugonjwa huo katika Hospitali, Kliniki na katika kila Zahanati zilizoko nchi nzima.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Alisema kwa sasa Serikali imeboresha mfumo wa utoaji wa huduma kwa wagonjwa wa kisukari, kwa kuhakikisha kwamba kila mwananchi anapatiwa elimu mahsusi ya na namna ya kujijengea tabia ya kupima ugonjwa huo kila mara ili wale wanaobainika waweze kutibiwa mapema.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Aliongeza kuwa endapo wananchi watajenga tabia ya kuchunguza afya zao mara kwa mara, idadi ya vifo vinavyotokana na uzembe wa kuchunguza afya vitapungua.[/FONT]
 
Hayo ndio matokeo yakuendekeza USISIEMU badala ya kuangalia maslahi ya Taifa..Wale jamaa sio wazalendo na ndio maana wakapinga AZIMIO LA ARUSHA wakabariki AZIMIO LA RUSHWA...
bado huo ni mwanzo tu! kuna miaka minne na ushei ya kulia na kusaga meno, mfumuko haujaikia kile kiwango chake! maana yake itafikia wakati hatutajadili tena hapa siasa bali mkate wa leo tunaupataje!! huko ndiko tunakoelekezwa kama hamjui! Inabidi tufanye kazi wa bidii kwelikweli... na rushwa ndio zitaota chaza sasa! ole wetu!
 
Mfumko wa bei umeshuka toka 13% mpaka kufikia 5.6% ni tafauti na jirni zet ambapo makwao ni avarage ya 9.5%

Uchumi wetu unaenda vizuri kulinganisha na nchi nying afrika na wataalam wa uchumi wanatabiri kama Tanzania itaendelea na nguvu zake za uchumi kwa muda wa miaka kui nchi itakuwa mbali

Vyama vya upinzani hawana cha kuikejeli serikali na ukuuaji wa uchumi kwa sababau wkina Mchungaji Slaa na wenzakehawana uwezo wa kujieleza au kuuzungumzia uchumi kutokana na elimu aliokuwa nayo haisadii ktk karne hii ya sayansi na technologia


Tafadhali ni nini source ya ulichoandika hapo juu?
 
Serikali inavyosema inajizatiti kukabiliana na kisukari... Vituko kweli kweli!
Hii habari ipo IPPMEDIA
Serikali yajipanga kudhibiti kisukari

Na Elizabeth Zaya 27th January 2011

[FONT=ArialMT, sans-serif]Serikali imezindua programu maalum inayolenga katika kushughulika na udhibiti wa ugonjwa wa kisukari nchini ambapo jumla ya Dola za kimarekani milioni 2.3 zinatarajia kutumika.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Akizindua programu hiyo jijini Dar es Salaam jana, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Hadji Hussein Mponda, alisema programu hiyo itadumu kwa miaka minne na lengo lake ni kuhakikisha ugonjwa huo unadhibitiwa kwa asilimia kubwa.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Dk. Mponda alisema kati ya magonjwa yasiyoambukiza, kisukari ndio unaonekana kuwa wa kwanza kwa kuongeza idadi ya wagonjwa ambapo asilimia tano mpaka sita ya wagonjwa wa kisukari wanaishi mijini, na asilimia moja tu ni waishio vijijini.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Alizitaja baadhi ya sababu zinazochangia ni umaskini, matumizi mengi ya tumbaku, kutofanya mazoezi, matumizi mabovu ya chakula na matuimizi mengi ya kilevi.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Aidha alisema programu hii pia inalenga kutoa huduma kwa wagonjwa wanaougua ugonjwa huo katika Hospitali, Kliniki na katika kila Zahanati zilizoko nchi nzima.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Alisema kwa sasa Serikali imeboresha mfumo wa utoaji wa huduma kwa wagonjwa wa kisukari, kwa kuhakikisha kwamba kila mwananchi anapatiwa elimu mahsusi ya na namna ya kujijengea tabia ya kupima ugonjwa huo kila mara ili wale wanaobainika waweze kutibiwa mapema.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Aliongeza kuwa endapo wananchi watajenga tabia ya kuchunguza afya zao mara kwa mara, idadi ya vifo vinavyotokana na uzembe wa kuchunguza afya vitapungua.[/FONT]


Serikali wahuni watupu, wanacheza na maisha ya watu.....ahadi chungu mbovu lakini huduma za afya za Tz kwa kweli ni aibu tupu. Life expectancy ya WaTz imeshuka, na inaendelea kushuka kila mwaka. Kuna vielelezo hai vingi venye kuonyesha uduni wa huduma zote za msingi kwa wananchi katika maeneo ya afya, elimu, barabara, uchumi nk

Wameshindwa kupambana na malaria ugonjwa ambao nchi nyingi za kawaida zimefanikiwa kuupunguza na kuziokoa jamii zao. Hili la kisukari ni usanii mwingine.
 
ndugu katika jf, nilienda jana kununua bidhaa za kibandani kwangu bei nilizo zikuta zikanifanya ninunue bidhaa 2/3 ya kiwango nilichopanga kununua. je hali hii tutafika?
je tatizo lipo Arusha tu au na mikoa mingine?

Na bado! Mpaka tujiny... kwa kuendekeza shishiem.
 
Mkurugenzi wa usalama wa Taifa amebainisha viashiria vya uvunjifu wa amani kuwa ni ukosefu wa ajira kwa vijana....

Sasa kama Taifa ni lazima kufikiria namna ya kutengeneza kwa haraka ajira za dharura milioni 5...ndani ya kipindi cha miaka 5...thats is the pain truth....ukiangalia statistics za population ...asilimia 50 ya wananchi wana umri wa zaidi ya miaka 18.....umri wa nguvu kazi kati ya huoAge structure

0–14 years: 44.3% (male 7,988,898; female 7,938,979)
15–64 years: 53.1% (male 9,429,959; female 9,634,102)
65 years and over: 2.6% (male 405,803; female 524,713) (2003 est.)


0–14 years: 43% (male 8,853,529/female 8,805,810)
15–64 years: 54.1% (male 10,956,133/female 11,255,868)
65 years and over: 2.9% (male 513,959/female 663,233) (2009 est.)



Utafiti uliofanywa na ILO unaonyesha yafuatayo....


Econ. Active:17.9 millions17.9 millions


  • Employed:15.6 millions15.6 millions
  • Unemployed:2.3 millions2.3 millions

Zaidi ya hiyo taarifa za ziada zinaonyesha kuwa kila mwaka vijana 700,000 Wanaingia kwenye soko la ajira .....na kati ya hao wanaopata ajira rasmi[ie ofisini,jeshi,polisi,magereza etc] ni vijana 30,000 /mwaka.....wanaobaki hapo wanaingia mitaani bila kazi ya kueleweka ....HILI NI BOMU KWENYE TAIFA....tena wengi wanakimbilia mijini kwenye wanafikri kuna maisha bora...ni wazi kadiri watakapokosa hayo maisha bora na idadi yao ikiendelea kuongezeka kwenye miji yetu WATALIPUKA..factor ya kwanza ni FIMBO WALIYOCHAPWA CCM KWENYE MIJI YOTE MIKUBWA NI MATOKEO YA HAYA NINAYOYAANDIKA...

KIKWETE NA SERIKALI YAKE WACHUKUE HATUA GANI HARAKA??

Kwanza juhudi binafsi na za haraka zifanyike kubadili sura ya vijiji vyetu .....kupeleka maji,umeme na barabara....LENGO kuwavutia wananchi wabakie vijijini au miji midogo...

Pili kuwawezesha na kuwavutia wawekezaji kuwekeza vijijini au kwenye miji midogo haasa katika processing industries ......

UWEKEZAJI PEKEE WENYE UWEZO WA KUAJIRI WATU WENGI KWA MARA MOJA NI UKULIMA WA KIBIASHARA[COMMERCIAL FARMING].......mashamba ya chai,pamba,katani,kahawa,mpunga,mahindi etc......iwapo wawekezaji wakubwa watapatikana haraka ....wenye uwezo wa kulima hadi hekari 30,000 kwa shamba moja ........shamba moja la namna hiyo lina uwezo wa kuajiri watu 3,000 na kuwapa makazi ,huduma za jamii etc...refer mfumo wa estate za zamani........hao wataajiriwa moja kwa moja lakini kumbukeni kuna wataoajiriwa indirect kutoa huduma pembezoni mwa mashamba hayo makubwa........na walulima wadogo watakaonufaika na out growers schemes....

Tukiweza kuwa na mashamba angalau 20 ya namna hiyo kila mkoa ....ninamaanisha kuwa kila mkoa utaweza kuajiri vijana 60,000 kwenye mashamba na namaanisha ajira 1,500,000 kwa nchi nzima .......
Tukiweza kujenga viwanda vya kusindika mazao kila mkoa [vitakavyomilikiwa na wafanya biashara pia]....tutaweza kutengeneza ajira hadi 700,000.....ukijumuuisha na informal employment kwa watoa huduma .....naamini tutaweza kwa awamu ya kwanza kuwapatia vijana zaidi ya milioni 3 walio kwenye mitaa sasa.........

Hapa nimeongelea sekta moja tu ya KILIMO CHA KIBIASHARA...SIO HICHI KILIMO KWANZA CHA KISIASA...

ZAIDI YA HAYO TUJUWE KUWA FAIDA YA KIUCHUMI ITALETA MSUKUMO KWA UJUMLA KUINUA SEKTA NYINGINE......

HAPO HATUJAONGEELEA MCHANGO WA SEKTA ZA MADINI,UVUVI....VIWANDA etc KATIKA KUSAIDIA KUWAONDOA VIJANA HARAKA MITAANI!!!
 
Waungwana mfumuko wa bei za vitu duniani kote wanalalamika sasa hivi. Kilichosababisha mfumuko huo ni kutokana na bei za malighafi ya mafuta toka nchi zinazozalisha kupanda juu.
Juzi nilitembelea nchi moja kati ya mataifa yaliyoendelea nikaona leo gallon moja ya petrol ni zaidi ya $3 wakati mwaka mmoja uliopita ilikuwa ni $2. Hao hawalalamiki kama wabongo.
Jamani wabongo tunalalamika mno, tusome ishara za nyakati pia.

Hapa siyo kwamba watu wanalalamika bali wanaelezea ukweli wa mambo. Mfumko wa bei wa Tanzania hauna uhusiano na kupanda kwa bei ya mafuta Duniani. Mfumko wa bei wa hapa Tanzania unatokana na matumizi yasiyoendana na mapato kwa serikali na hivyo kuishia kukopa kutoka katika mabenki. Hakuna kitu kinachosababisha mfumko mkubwa wa bei kama kwa serikali kukopa kutoka katika mabenki.

Ikumbukwe kuwa katika kipindi chote cha miaka miwili iliyopita, bei ya mafuta katika soko la Dunia ilikuwa imeshuka sana lakini kwa Tanzania mfumko wa bei ulipanda hadi wakati mwingine kufikia 17%. Kama ingekuwa mfumko wa bei katika Tanzania unasababishwa na kupanda kwa mafuta katika soko la Dunia, basi kipindi hicho cha miaka miwili iliyopita ungekuwa chini lakini ndiyo kwanza ulipanda kuliko kipindi kingine chochote.

Ni uwongo mkubwa kueleza kuwa Tanzania ina mfumko wa bei wa chini kuliko mataifa jirani. Katika Afrika Mashariki ni Tanzania na Burundi pekee yake ndizo zenye mfumko wa bei wa zaidi ya 4%, huku Rwanda ikiwa ina mfumko wa bei 2%; Kenya na uganda 3-4%.
 
Kwa ufahamu wangu mdogo, hili nilitegemea sana kutokea miezi michache ijayo. Uchaguzi umeingiza pesa nyingi sana katika mzunguko wa pesa.Pesa zilizoingizwa hazikutokana na production ni zawadi na hongo.
Pili, inaweza changiwa na trade imbalance kati ya import and export inayopelekea kushuka kwa thamani ya shilingi.
Wachumi tusaidieni zaidi.

Mkuu Nguruvi hapo umenena! Katika kipindi cha miezi mitatu kuelekea uchaguzi kulikuwa na matumizi makubwa sana ya pesa kuliko kawaida, na tukumbuke hakuna uzalishaji uliokuwa unafanyika kulingana na mapato zaidi ya posho za kuhudhuria mikutano na 'kulinda kura'. Huu mfumuko wa bei utaendelea hadi hiyo pesa ya bure itakapotoka kwenye mzunguko.

Hii hali hutokea kila baada ya uchaguzi lakini mwaka huu makali yamechangiwa na hali ya uchumi wa dunia kipindi hiki hasa kupanda kwa bei ya mafuta.
 
Jana nilikuwa naangalia KIJAMBO CHA WIKI cha Mlimani Tv, walimtoa Makamba akiwashangaa Watanzania kulalamika vitu vidogo kama kupanda kwa gharama za maisha na bei ya mafuta kuwa ni vitu vidogo sana havipaswi kulalamikiwa kwa kuwa hapa ni duniani wala SIO PEPONI, tusubiri tuende peponi tukavipate hivyo huku tukuimba milele!

Kwa kweli nilshikwa na butwaa !na kujiuliza kama Watanzania tuna akili timamu kuendelea kumwacha mtu kama huyu anayetukana watu zaidi ya matusi ya nguoni !Inawezekana tuna kasoro kubwa ndio maana wapumbavu kama hawa wamekuwa wakifanya wanavyotaka.

Nafikiri ni nchi hii tu ambayo mtu anaweza akadhallisha watu na bado akwa ni kiongozi.

Jamani hatumtendei haki Mungu aliyetupa akili na nguvu ,kama YESU aliweza kuwachapa viboko watu hivi sisi tunashindwa nini! Akili na nguvu zetu tunazitumia wapi!

Bila ya kuja kuchanjana mapnga na visu nchi hii itaendelea kuwa shamba la bibi!

Hebu angalia mijadala inayofanywa hapa ...inaishia humu tu 1 suluhisho nini ni lazima watu tuanze kujito muhanga la sivyo ,tuache kulalamika!
 
Huyu mtu ni Juha! Bila shaka uongozi wa ngazi mbali mbali alizopitia alizipata kwa njia za kishirikina! Sielewi kwanini bado tunamchekelea akiharibu maisha yetu na zaidi sana ya kizazi kijacho. Hatumtaki aende zake!
 
Niliposikia hilo la makamba jana siyo siri nilijikuta ninatukana kwa ngùvu tusi ambalo mke wangu ajawahi kulisikia ingawa alinimind lakini walipo rudia tena maneneo ya hako kazee aliniunga mkono tena yeye akaenda mbali zaidi kwani alimfananisha makamba na muuaji na ilimpandishia wife hasira kwani asubuhi yake tulikuwa tunabishana baada ya umeme kwisha kuwa hata kama umeme umepanda haiwezi kufikia 30000 kwa mwezi toka 25000 . Kwakweli makamba kachoka na sijui waliokuwepo pale walimfanya nimi?
 
naogopa ban jamani hizi topiki zitanisababishia ban hizi,, invisible akisinzia kidogo mnistue nikandamize na mie maoni yangu
 
Huwa wakati mwingine najiuliza hivi watanzania tumelaaniwa au tuna matatizo ya akili???????:twitch:
 
unajua nini,inabidi kwenda nao sawa.
kwa mfano bili ya umeme ikipanda na mwenye saluni anapandisha bei ya huduma
muuza duka nae anapandisha bei ya unga,dreva tax nae anapandisha nauli yake.
tutajikuta tumeenda sambamba na tumezoea.
 
Huyo mzee ni fyatu! Ndiyo maana anaropoka hivyo. Ukiendelea kumsikiza, utapata BP buree. Sisi wenzio tulishampuuza tangu zamani.
 
Vizee ka Makamba ni kuvitunis tu...ajue hivyo vitu vidogo (kama anavyoviita yy) vinavyogusa maisha ya watu ndo hutoa viongozi wabovu kama wao madarakani...mi nshachoka kulalamika wanajamvi..... i need to act...
 
Tuesday, 15 February 2011

kwesigabo%20takwimu.jpg

Mkurugenzi wa idadi ya watu na takwimu za jamii, Ephraim Kwesigabo.

Elias Msuya

OFISI ya Taifa ya Takwimu imesema mfumuko wa bei ni tishio la maisha kwa Watanzania kutokana na kupanda kwa kasi isiyo ya kawaida.

Imesema kwa kipindi cha mwaka mmoja mfumuko umepanda kutoka asilimia 5.6 hadi asilimia 6.4 kutokana na sababu kadhaa za msingi zikichangiwa na kupanda kwa gharama za umeme.

Aidha ilisema thamani ya shilingi imeshuka kimatumizi kutoka Sh100 ya Septemba 2010 hadi Sh 92 na senti 10.

Mfumuko huo wa bei umekuja ikiwa ni miezi miwili tangu Shirika la Umeme (Tanesco) likiwa limepandisha bei ya umeme kwa asilimia 18.

Akitangaza taarifa ya mwaka ya mfumuko wa bei Kitaifa, jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa idadi ya watu na takwimu za jamii, Ephraim Kwesigabo, alisema mfumuko huo unatokana na kupanda kwa bei za vyakula na nishati hasa umeme.

Alisema kuwa taarifa hiyo inafuata mapendekezo ya kimataifa ya matumizi kwa mtu mmoja mmoja (COCOP) ikihusisha vyakula na vinywaji visivyo na vileo vinavyotumika majumbani na hotelini, Nishati na mafuta ya kuendeshea mitambo.

Alisema katika kipindi hicho cha mwaka kulikuwa na ongezeko la mfumuko wa bei kutoka alama (index) 97.82 Januari 2010 hadi (index) 104.10 Januari mwaka huu, huku gharama za makazi, maji, umeme, gesi na mafuta zikipanda kwa asilimia 17.7.

Akizungumzia suala la kupanda kwa bei ya vyakula, Kwesigabo alisema kuwa chakula kinachotumika ndani na nje ya nchi imepanda kutoka asilimia 6.3 Desemba 2010 hadi asilimia 6.7 mwaka huu. Bei za bidhaa zisizo za vyakula nayo imepanda kutoka asilimia 4.7 ya Desemba 2010 hadi asilimia 6.1 ya Januari mwaka huu.

Kuhusu bidhaa zisizo za vyakula na nishati, alisema kuwa mfumuko umepanda kwa asilimia 4.4 kutoka asilimia 3.7 ya Januari mwaka 2010, wakati mfumuko wa bei ya nishati umepanda kwa asilimia 19.1 kutoka asilimia 12.3 ya Desemba 2010.

Alisema mfumuko huo siyo kwa Tanzania pekee bali hata kwa nchi jirani kama vile Kenya ambako mfumuko pia umepanda kwa asilimia 5.42 kutoka asilimia 4.52 ya mwaka jana huku Uganda ukipanda kufikia asilimia 5.0 kutoka asilimia 3.1 ya mwaka jana, akitaja sababu pekee kuwa ni kupanda kwa bei ya chakula.

Ameishauri serikali kuhakikisha kuwa inatatua tatizo la umeme haraka ili kuinua uzalishaji wa umeme.

“Kwa mawazo yangu tu, ni lazima serikali ihakikishe kuwa tatizo la umeme linakwisha ili kuongeza uzalishaji wa ndani kwasababu tukitegemea bidhaa za nje zitazidisha mfumuko wa bei. Ni jukumu la Tume ya mipango kuangalia hali hii” alisema Kwesigabo.

Chanzo: Mwananchi
 
Ni vyema CCM wakatoa tamko kuwa maisha bora kwa kila mtanznia ilikuwa ni danganya toto................
 
Maisha bora kwa kila mTanzanzania kwa CCM haiwezekani kwani gharama za uzalishaji zipo juu.
 
Kwa kweli tutaipata maana mfumuko huu utaendelea sana, ukichangiwa pia na kuzagaa kwa noti za bandia mitaani!
 
Back
Top Bottom