Tanzania Imekwisharidhia Ushoga Siku Nyingi!

shindoooooo kwa jina la yesu pepo mchafu wa ushoga na ata wanaokula hizo pesa za wanaotaka kutuletea hiyo laana na ziwalaaan

Hivi kwenye bunge letu tukufu hatuna wake kwa waume ambao ni mashoga na wasagaji wanaojulikana na watanzania wamewachagua au wameteuliwa? Kama wamo basi ndipo patakapo anzisha sakata la kuuhalalisha ushenzi Tanzania. Jamani tusichague wabunge Kama hao. Kata mti kwenye shinsshins
 
Haha...nimecheka kweli.Yaani nisikie Lipumba ana dai benefit kwa maalim au JK? Kweli hii dini mpya ya ushoga inajiingiza kwa nguvu hata kwa watu....

Bora tuu wasijiingize kuhubiria wanangu huu upuuzi nitawachapa moto kuanzia mikuuni hadi kichwani..hapo ndipo tunahitaji kufuatilia hata walimu wetu wanafundisha nini watoto..nimewahi sikia walimu matukio ya walimu kiume kuwagawaia wanafunzi wa kiume mgongo, kujenga urafiki na wanafunzi laini laini ili kuwapa ujasiri na moyo wa kuwa waliberali....of course ni mbaya kuwashmabulia ila nikiwadaka wanajidai ni haki yao ktk familia yangu hakuna mjadala.


Sasa hivi hata wagonjwa wa ukimwi wanalindwa kwa nguvu bila kufundishwa kuwajibika.
 
Mawazo yako tu haya, halafu siyo ya msingi sana kwa sasa tunatamani kuzungumzia mambo ya maendeleo siyo ya ushoga. Waache mashoga wazungumze yao na sisi tuendelee na yetu!.
Inamaana wewe serikali ikikubali kuhalalisha swala la ushoga nawewe utakuwa shoga?
 
deonova na Bujibuji rejea hii post...Tanzania tulikwisha ridhia mambo hayo siku nyingi.

Naomba @invisible au deonova weka hii taarifa ya nyongeza kwenye uzi wako. Mnakumbuka kulikuwa na NGO ya Sisi kwa Sisi ambayo ndiyo ilikuwa mahususi kwa ajili ya mashoga. Serikali iliwahi kuwalaghai Watanzania kwamba imeifuta. Sasa nawapa taarifa za uhakika kwamba Sisi kwa Sisi ilirejeshewa usajili kimyakimya na inafanya kazi kihalali. Amini musiamini hata TGNP wanafaprogramme maalumu kwa ajili ya mashoga na wanawatambua! Ukiishakuwa tegemezi, huwezi kuwa na chaguo katika maisha.

...Nilipodadisi zaidi kwamba Serikali ama Wizara ya Afya inatambua kazi za hawa jamaa nikaambiwa huu ni mradi ambao Wizara ilishasaini tangia mwaka jana, nikastuka loooh ina maana tulikuwa tunawanyooshea vidole Uganda kwa ule muswada wa mashoga, kumbe Serikali yetu wao wameridhia kimya kimya? nikaona labda niko nje ya ulimwengu wa 'updates' may be kuna ambaye amewahi kukutana na hii kitu atujuze zaidi wadau?..

 
hapana kwa nguvu zangu zote katiba tuliyokuwa nayo haiainishi kifungu chochote kinachotambua ushoga! Labda tukumbushe ni ibara ya ngapi katika katiba inayokubali ushoga?
1541776960086.png
 
Nina uhakika wa asilimia 100% kuwa hata kabla Serikali ya ccm haijaondoka madalakani, suala la ushoga lita-RASIMISHWA Tanzania. Na si kweli kwamba, kupinga kwa kauli kunakofanywa na serikali ni kutoridhia ushoga. Atakaye taka kubisha, abishe. Atakayetaka kutusi, afanye hivyo. Lakini ukweli wa mazingira ya kihistoria utasimama hivyo daima.

Ni mwaka 1994 wakati somo la UKIMWI linapigiwa chepuo kuingizwa S/M, Watanzania walikuwa wanapinga sana kwa kutoa sababu kuwa suala la kuzungumzia mambo ya ngono mbele ya watoto wao ni kinyume na maadili. Neno kondomu lilikuwa haramu. Leo tunashuhudia Watanzania walewale wanaimba hadharani "Usione soo kusubiri au tumia kondomu" Baba na bintiye sasa wanakaa sebuleni, wanaangalia wote mwanzo-mwisho matangazo ya TACAIDS yasiyokuwa na tafsida hata chembe, na lile la pedi nalo linapita .... wala hakuna wa kumwonea soo mwenziwe anymore! Zaidi utasiki Baba anamwambia mwanae; hapo Mjomba Mrisho Mpoto kakoleza!

Juzi juzi tu kina Mongella walipokwenda Beijing, Watanzania wakasema hao wanawake wanajifurahisha tu na hayo maazimio yao. Na kweli moyoni Waafrika wengi nami nikiwemo tumebaki kuamini na kuishi na wanawake kama wasaidizi na si kinyume chake. Lakini angalia jinsi waasisi wa masuala ya jinsia walivyoweza kupigania agenda yao na kuipenyeza katika mataifa yetu kupitia serikali na serikali kuizamisha kwenye ngazi ya familia. Kila uchao utasikia campaigns mara Gender-Based-Violence, Women Rights, Rights of Inheritance, Property Rights, etc na kubwa kuliko yote ni Gender Mainstreaming iliyowezesha kuifanya jinsia kuwa suala mtambuka na kusababisha mabadiliko ya sera na sheria mbalimbali. Matokeo yake kwenye ngazi ya jamii ni wanafamilia mfano wa kambare-kila moja ni mkubwa kwa mwenzie na hivyo kusababisha ndoa nyingi hasa za waliopata kozi ya Dr. Rose Shayo (Gender-Elimu ya Juu) kufungwa Jmosi na kuvunjika Jpili! Ngazi ya serikali tunaona vyeo vya sandakalawe-wabunge wasio na majimbo wala kazi, majaji wa kike wasio na sifa na nafasi zingine nyingi tu ambazo lengo ni kufikia malengo na kuwafurahia Wahisani (Kina Cameron).

Mtu yeyote mwenye akili anaamini chandarua si suluhisho la kudumu kuondoa malaria. Sasa iweje kama hayawani mtaani anajua huu ukweli kwa nini serikali badala ya kuziba vifuu na kusisitiza kufyeka machaka, wao wanahamasisha vyandurua? Ukipata ukweli wa lililowafunga viongozi wako kungamua jambo rahisi kama hili, basi huna budi kuafikiana nami kuwa tayari nchi yetu inawatambua mashoga na haki zao na hivi punde itatamka wazi. Lakini mambo mengine si mpaka usikie; kama kusoma hujui hata picha ukutani huioni? Nani, wapi imeandikwa na lini ccm walikwambia hii ni nchi ya kibepari ; lakini ukweli ni upi?

Ni kazi rahisi sana kulifanikisha hili la ushoga na kiufupi tukubali tu kwamba tayari tuko kwenye Taifa linalowatambua mashoga. Tunaona media zinafanya endorsement campaigns kwa kuwatumia Bongo Superstars (Banana zorro, Mzee yusuph, na wengine). Wanauzunguka mbuyu kwa kuyafanya haya ni matangazo ya ya uzazi wa mpango...(walio wengi wanaona huu mfano uko kaskazini ya ukweli ulio kusini!). Hii ni science of behavioral change using marketing techniques! Shtuka! Rais wako tayari amearikwa na anakwenda kuhudhuria mkutano juu ya masuala ya uzazi wa mpango. Nakudokeza, kaa chonjo kusikia maazimio ya mkutano. Ogopa mpango unaokamilishwa taratibu bila haraka (gradually). Mara zote unajikuta umeishatumbukia na kuwa mlevi wa lile unalodai unalipinga kwa nguvu zako zote. Tukubali tu, wakati wakubwa (Obama na Cameroon) wanatamka hadharani kuweka sharti la haki za mashoga si kwamba ndo muda huo lango la ushoga lilikuwa linafunguliwa rasmi, bali ilikuwa ni kuwashtueni wale wote mnaodhani bado hamjarasimisha ushoga kuwa tayari mko kwenye ukanda wa ushoga. Jiulize, kama huna waumini, msikiti utajenga wa nini? Nyongeza ya hapo, Katiba tunayobadilisha sasa ilikuwa inaukubali ushoga! Wasiojua waulize, wanaojifanya kujua wabishe, na wale wasio na hoja kabisa-matusi ruksa!

Siku njema.
Makala hii niliiandika mwaka 2012. Nilichokisema kimetimilika na kuhitimishwa kwa kauli za Serikali. Kauli ya kwanza ilitolewa na Balozi Mahiga-Vita dhidi ya ushoga Dar es Salaam si msimamo wa serikali na ya pili imetolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani- Wapenzi wa jinsia moja wapo salama Tanzania
 
Tungekuwa tunaweka nguvu hivi ku kemea
Rushwa, njaa na umasikini tulionao tungefika mbali sana.
 
JF Ina watu wanavichwa hasa.
JF ina wafukua makaburi hasa.

Yaani ni taaabu tabuni

Bazazi
 
This is bull shit MTU unaiongelea nchi as if wewe ndo msemaji wa taifa. Ndomaana inabidi tuwe na sheria Kali za mitandao maana MTU analazimisha upuuzi usiokuwepo. Katiba mpya imeruhusu wapi huo upuuzi?? Waiii ustupotezee muda
 
Back
Top Bottom