Tanzania Imekwisharidhia Ushoga Siku Nyingi!

Omutwale

JF-Expert Member
Feb 4, 2008
1,429
1,045
Nina uhakika wa asilimia 100% kuwa hata kabla Serikali ya ccm haijaondoka madalakani, suala la ushoga lita-RASIMISHWA Tanzania. Na si kweli kwamba, kupinga kwa kauli kunakofanywa na serikali ni kutoridhia ushoga. Atakaye taka kubisha, abishe. Atakayetaka kutusi, afanye hivyo. Lakini ukweli wa mazingira ya kihistoria utasimama hivyo daima.

Ni mwaka 1994 wakati somo la UKIMWI linapigiwa chepuo kuingizwa S/M, Watanzania walikuwa wanapinga sana kwa kutoa sababu kuwa suala la kuzungumzia mambo ya ngono mbele ya watoto wao ni kinyume na maadili. Neno kondomu lilikuwa haramu. Leo tunashuhudia Watanzania walewale wanaimba hadharani "Usione soo kusubiri au tumia kondomu" Baba na bintiye sasa wanakaa sebuleni, wanaangalia wote mwanzo-mwisho matangazo ya TACAIDS yasiyokuwa na tafsida hata chembe, na lile la pedi nalo linapita .... wala hakuna wa kumwonea soo mwenziwe anymore! Zaidi utasiki Baba anamwambia mwanae; hapo Mjomba Mrisho Mpoto kakoleza!

Juzi juzi tu kina Mongella walipokwenda Beijing, Watanzania wakasema hao wanawake wanajifurahisha tu na hayo maazimio yao. Na kweli moyoni Waafrika wengi nami nikiwemo tumebaki kuamini na kuishi na wanawake kama wasaidizi na si kinyume chake. Lakini angalia jinsi waasisi wa masuala ya jinsia walivyoweza kupigania agenda yao na kuipenyeza katika mataifa yetu kupitia serikali na serikali kuizamisha kwenye ngazi ya familia. Kila uchao utasikia campaigns mara Gender-Based-Violence, Women Rights, Rights of Inheritance, Property Rights, etc na kubwa kuliko yote ni Gender Mainstreaming iliyowezesha kuifanya jinsia kuwa suala mtambuka na kusababisha mabadiliko ya sera na sheria mbalimbali. Matokeo yake kwenye ngazi ya jamii ni wanafamilia mfano wa kambare-kila moja ni mkubwa kwa mwenzie na hivyo kusababisha ndoa nyingi hasa za waliopata kozi ya Dr. Rose Shayo (Gender-Elimu ya Juu) kufungwa Jmosi na kuvunjika Jpili! Ngazi ya serikali tunaona vyeo vya sandakalawe-wabunge wasio na majimbo wala kazi, majaji wa kike wasio na sifa na nafasi zingine nyingi tu ambazo lengo ni kufikia malengo na kuwafurahia Wahisani (Kina Cameron).

Mtu yeyote mwenye akili anaamini chandarua si suluhisho la kudumu kuondoa malaria. Sasa iweje kama hayawani mtaani anajua huu ukweli kwa nini serikali badala ya kuziba vifuu na kusisitiza kufyeka machaka, wao wanahamasisha vyandurua? Ukipata ukweli wa lililowafunga viongozi wako kung’amua jambo rahisi kama hili, basi huna budi kuafikiana nami kuwa tayari nchi yetu inawatambua mashoga na haki zao na hivi punde itatamka wazi. Lakini mambo mengine si mpaka usikie; kama kusoma hujui hata picha ukutani huioni? Nani, wapi imeandikwa na lini ccm walikwambia hii ni nchi ya kibepari ; lakini ukweli ni upi?

Ni kazi rahisi sana kulifanikisha hili la ushoga na kiufupi tukubali tu kwamba tayari tuko kwenye Taifa linalowatambua mashoga. Tunaona media zinafanya endorsement campaigns kwa kuwatumia Bongo Superstars (Banana zorro, Mzee yusuph, na wengine). Wanauzunguka mbuyu kwa kuyafanya haya ni matangazo ya ya uzazi wa mpango...(walio wengi wanaona huu mfano uko kaskazini ya ukweli ulio kusini!). Hii ni science of behavioral change using marketing techniques! Shtuka! Rais wako tayari amearikwa na anakwenda kuhudhuria mkutano juu ya masuala ya uzazi wa mpango. Nakudokeza, kaa chonjo kusikia maazimio ya mkutano. Ogopa mpango unaokamilishwa taratibu bila haraka (gradually). Mara zote unajikuta umeishatumbukia na kuwa mlevi wa lile unalodai unalipinga kwa nguvu zako zote. Tukubali tu, wakati wakubwa (Obama na Cameroon) wanatamka hadharani kuweka sharti la haki za mashoga si kwamba ndo muda huo lango la ushoga lilikuwa linafunguliwa rasmi, bali ilikuwa ni kuwashtueni wale wote mnaodhani bado hamjarasimisha ushoga kuwa tayari mko kwenye ukanda wa ushoga. Jiulize, kama huna waumini, msikiti utajenga wa nini? Nyongeza ya hapo, Katiba tunayobadilisha sasa ilikuwa inaukubali ushoga! Wasiojua waulize, wanaojifanya kujua wabishe, na wale wasio na hoja kabisa-matusi ruksa!

Siku njema.
 
hapana kwa nguvu zangu zote katiba tuliyokuwa nayo haiainishi kifungu chochote kinachotambua ushoga! Labda tukumbushe ni ibara ya ngapi katika katiba inayokubali ushoga?
 
hapana kwa nguvu zangu zote katiba tuliyokuwa nayo haiainishi kifungu chochote kinachotambua ushoga! Labda tukumbushe ni ibara ya ngapi katika katiba inayokubali ushoga?

Asante....ni Kipengele kilekile kinachotoa msingi wa kuhararisha ushoga kwenye Katiba na Azimio la Uhuru wa USA...nimerejesha kazi kwako...ukitafute!
 
shindoooooo kwa jina la yesu pepo mchafu wa ushoga na ata wanaokula hizo pesa za wanaotaka kutuletea hiyo laana na ziwalaaan
 
shindwaaaaaaaa kwa jina la Yesu pepo mchafu wa ushoga na ata wanaokula hizo pesa za wanaotaka kutuletea hiyo laana na ziwalaaan

Wanaokula hiyo pesa ni wote wanaoishi kwenye nchi yenye bajeti tegemezi kwa zaidi ya 50%. Je, wewe haumo au hukujua wakati unatoa laana?

Daima, the beggar has no choise! Mkuu JK aliishasema; ukitaka kula lazima nawe uwe tayari kuliwa! Wafikiri wazungu ni wajinga kutujengea mifumo ya kutufanya daima tuwe ombaomba?

Mshahara wa walio serikalini unategemea mikopo toka benki za biashara, ujira wa sekta binafsi hasa katika NGO unategemea donations na grants. Haya ndiyo malango makuu ya wazungu kusukuma jambo lolote katika nchi yoyote. Hata sasa ukiomba hela ya donor lazima ukubaliane na matakwa yake kwanza.

Leo hii wafadhili wa TGNP, Haki Elimu, Haki Ardhi, Human Rights, TAWLA, REPOA n.k wakisema tunaondoa misaada haraka sana utawaona wanaoitwa wanaharakati wako mabarabarani na mabango wanaunga mkono ushoga kurasimishwa.

Njaa ni mbaya na umaskini hauondoki kwa kukemea tu..... Mch. Msigwa alikwishasema; hakuna theory inayosema matatizo yatonayo na uchumi dawa yake ni kuombewa...!
 
Apolonary na Young Tanzanian someni haya maneno ya "Mfadhiri" na mniambie nchi inayoongozwa na viongozi ombaomba itakwepea wapi ushoga rasmi?

Obama: Marriage benefits should cross state lines
DAKAR, Senegal (AP) - President Barack Obama says the Supreme Court's rulings on gay marriage were a victory not just for gays and lesbians, but for American democracy.

He says as president, he believes federal benefits should be granted to couples married in a state that recognizes gay marriage even if they move to a state that doesn't.
Obama says he asked his lawyers to start evaluating how to update federal statutes to grant gay couples federal benefits even before the high court ruled.
Obama spoke in Dakar, Senegal, at a joint news conference with Senegal's President Macky Sall. Obama said different customs and religious beliefs must be respected in different countries, but states and laws should treat everyone equally.
Sall says Senegal is not ready to decriminalize homosexuality.
source

cc:omujubi, Azote, KASHOROBANA, genekai
 
Jamani sijui dunia ya sasa imeingiwa na PEPO gani la kuzungumzia Ushoga kama jambo zuri vile! Yaani nikisoma habari ya USHOGA au kuisikia kwenye vyombo vya habari nawashwa Pua na Masikio. Eee Yesu Rudi Upesi Dunia imeoza watu hawana AIBU!!
 
Naomba nisiwepo kabisa duniani kuliko kushuhudia vitendo vya ushoga katika jamii yangu!!!God help us!"!!
 
Ccm+obama=cameroon
Cha muhimu nikujilinda mwenye maana ukizubaa utasikia umeolewa
 
Hayo mashoga yahalalishwe, yapewe na utambulisho kisha yatozwe kodi yaongeze pato la taifa
 
Omutwale, samahani: kwanza mimi simvumilii mtu anayekosea Kiswahili na hasa endapo anaandika Kiingereza bila makosa, kama wewe! Ni madaraka na si madalaka, amealikwa na si amearikwa na hapo chini umeandika kuhararisha lakini sawa ni kuhalalisha.Tukija kwenye maudhui yako ni nzuri sana na mimi nakubaliana na wewe. Wajua tatizo kuu la Mwafrika ni kupuuza utamaduni wake. Kwa kweli bila ya utamaduni hakuna independence. Haya yamesemwa na watu wengi wenye akili akiwemo Nkurumah, sijui kwa nini viongozi wetu hawasikii.Katika hilo hilo la kupuuza utamaduni wetu ndio ukaona hivi sasa tunashangilia kupewa misaada. Thubutu!Wazee wetu wa zamani, hata kama mafukara vipi, walikuwa hawakubali wapewe kitu bure.....kwa vile walijua fika hakuna kitu cha bure duniani. Leo mwanaume mzima na akili zake afunga safari kwenda kuomba na anaona hilo ni moja ya terms of reference za kazi yake. Kuomba na kupewa misaada ndiyo matokeo yake haya tunayoyaona, kwamba mgeni anakuja katika nchi ya watu (kwa wazee wetu: mji wa watu) na anathubutu kumwambia mwenyeji avue nguo! Leo ni ushoga kesho watatuambia turuhusu ndoa na mama zetu!Ili nisifahamike vibaya: ushoga ulikuwepo Afrika toka zamani, ukipigiwa kelele kuwa ni tabia mbaya, lakini kwa kiasi kikubwa ukivumiliwa, kama mtu atakuwa na staha na kufanya kwa siri. Hii inaonesha wazi tolerance na democracy ya mifumo ya Kiafrika. Wanachotutaka hivi sasa sio demokrasia na hakika ni ukandamizaji- kwamba haki ya watu wachache iwe juu ya utamaduni na silika za walio wengi! Wanachotaka ni kutufanya sote tuone ushoga ni kitu cha kawaida na hata tuwafundishe watoto wetu hivyo kuwa wanaweza kuchagua kuwa mashoga.Huku Ulaya kwa kweli mashoga wana satwa na sauti kubwa. Katika maashirika na taasisi nyingi wao ndio wakuu. Kwa hiyo wanataka kuufanya ushoga Afrika namna hiyo yaani uwe ni 'society'. Kama ulivyosema, naamini kuwa ni suala la wakati tu Tanzania itakubali hayo kwani Waingereza walisema: 'beggars have no choices' na wakazidisha 'you do not look a gift horse in the mouth'
 
Naomba nisiwepo kabisa duniani kuliko kushuhudia vitendo vya ushoga katika jamii yangu!!!God help us!"!!

Una maanisha nini kusema jamii yako? Kama una maanisha familia sawa. Lakini kama ni jamii ya Watanzania umekosea kwa kuwa kulikuwa na kongamano la wasagaji na mashoga 400 hapa Dar. Isitoshe kwenye mkutano wa wabunge kuhusu UKIMWI. Alikuwepo shoga mmoja akijieleza bila shida. Humu nchini mashoga ni wengi na tena wanadai haki zao. Ushauri ninaoweza kukupa ni kwamba usipeleke watoto wako wadogo shule za bweni. Huko wanajifunza haya machukizo.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Well said!!!


Mashoga tunaishi nao mtaani, wanafahamika. Wengine hata mavazi wamebadilisha.

Tunakutana nao kwenye kumbi za starehe. Wapo huru.

Zaidi siku chache zilizopita wameshirki semina na wabunge jinsi ya kupambana na Ukimwi.

Kwa kifupi kinachosubiriwa ni filimbi ya mwisho tu mchezo uanze.
 
@Omutwale, samahani: kwanza mimi simvumilii mtu anayekosea Kiswahili na hasa endapo anaandika Kiingereza bila makosa, kama wewe! Ni madaraka na si madalaka, amealikwa na si amearikwa na hapo chini umeandika kuhararisha lakini sawa ni kuhalalisha.
Nakushukuru sana kwa kunipa dalsa. Ninakiri kilema katika uandishi na matamshi ya la/ra, na ha/a. Tatizo langu naona ni la Kabila langu pia japo siyo sababu kuniruhusu kuandika au kutamka kimakosa.
..Tukija kwenye maudhui yako ni nzuri sana na mimi nakubaliana na wewe.
Kama ujumbe hauna makosa basi ni vema maana hadhira imepata na itakuwa imeelewa kusudi la mada.
 
Ni kweli hata N/WAZIRI UMMY MWALIMU alisema akiwa Dodoma kuwa watu wanaofanya mapenzi ya jinsia 1 wasibaguliwe(ukimwi).
 
Serikali ilisharuhu mashoga ndo maana mpaka sasa wapo wanaendelea na hawakamatwi japo haitaki kukiri. CCCCCCMMMMM
 
Imenisikitisha sana baada ya kusoma habari hii Katika gazeti la Raia Mwema:Yakwamba rais wetu alipokea dola 10,000 baada ya kahaba mkuu huko uswis kufanya harambee ya kusaidia mapambano dhidi ya malaria kwa nchinyetu..Inamaana serikali haikuwa na uwezo wa kupata dola 10,000? uwwwwwwwwwwwwwwwwwwwwwiiiiiiiii tumekwisha
Tuliishasema siku nyingi hapa kwamba kwa mtindo wa fikra za umatonya zikiongozwa na Rais wetu fedheha na kufuru kama hizo haziepukiki.
 
Back
Top Bottom