Balantanda
JF-Expert Member
- Jul 13, 2008
- 12,476
- 4,755
Katika pitapita yangu kwenye mtandao wa gazeti la Tanzania Daima nimekutana na habari ambazo zimenifanya niamini kwamba hawa jamaa (wa Tanzania Daima) hawapo makini kabisa....Hivi wahariri wanafanya kazi gani???....Soma hbari hizi hapa chini utaona ni kitu gani namaanisha
Mtangazaji ITV kuwania ubunge Ulanga Magharibi
na Marietha Mkoka na Benidect Kiwia
MTANGAZAJI mwandamizi wa kituo cha runinga cha ITV, Reinfred Masako, ametangaza nia ya kuwania ubunge katika jimbo la Ulanga Magharibi kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) linaloshikiliwa na Juma Kapuya ambaye ni Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Masako alisema ameamua kwa dhati kuwania ubunge katika uchaguzi mkuu mwaka huu kutokana na haki yake ya msingi aliyonayo ya kuchagua na kuchaguliwa katika ngazi yoyote ya uongozi.
Masako alisema nia hiyo ya kuwania ubunge kwenye jimbo hilo zaidi ni kusambaza elimu kuhusu hifadhi ya jamii, lishe bora kwa makundi maalamu ya kina mama wajawazito na wazee, siasa, uchumi na maendeleo ya jamii pamoja na usalama wa raia na mali zao katika michezo.
Mkongwe huyo wa habari aliyefanya kazi takriban miaka 32 toka mwaka 1978 hadi hivi sasa na katika vipindi vitatu tofauti visivyopungua miaka 10 alitumia muda huo kutoa elimu ya jamii zaidi kitu ambacho kinampa fursa ya kuwania jimbo hilo.
Nimedhamiria kuhamisha uzoefu wangu niliopata katika utendaji wangu kwa miaka yote isiyopungua 32 kwa wananchi wenzangu katika kulenga maeneo makuu matatu ikiwa ni pamoja na shughuli za kilimo, uvuvi na ufugaji, alisema Masako.
Aidha, Masako alisema fursa zilizopo katika jimbo ambalo ameweka nia ya kugombea ni pamoja na mito yenye maji yanayotiririka mwaka mzima, miradi ya skimu za maji akielezea kuwa hizo ni rasilimali tosha zinazohitaji maelekezo sahihi ya jinsi ya kutumia na kubadilisha maisha ya wakazi wa jimbo hilo.
Pia alisema amedhamiria kuutumia uzoefu wake ambao kwa ujumla ni sawa na mgodi unaotembea ili wananchi wa jimbo lake waweze kunufaika nao na utekelezaji wake upo ndani ya matumizi sahihi ya fursa ya mapinduzi ya kijani.
na hii
CCM wakorogana kampeni za JK
na Hellen Ngoromera
KAMATI za kampeni za mgombea urais za Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa ajili ya Rais Jakaya Kikwete zimeanza kukorogana.
Mkorogano huo umeanza kujitokeza katika Kamati ya Fedha na Vifaa vya Kampeni iliyotangazwa awali kuwa inaongozwa na Mhazini wa CCM, Amos Makala.
Wakati wa uzinduzi wa uchangishaji fedha kwa njia ya simu za mkononi katika Ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam, Makala aliwatangazia wanachama kwamba ndiye mwenyekiti wa kamati hiyo na makamu wake ni Zakhia Meghji.
Lakini katika mkutano wa chama hicho na waandishi wa habari uliofanyika jana katika ofisi ndogo ya CCM, chama hicho kilitangaza kuwa Meghji ndiye mwenyekiti wa kamati hiyo.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Propaganda, Ibrahim Msabaha, alisema kuwa Meghji ameteuliwa na NEC iliyomaliza kikao chake hivi karibuni jijini Dar es Salaam kuongoza kamati hiyo.
Msabaha aliitaja pia kamati nyingine ya Utekelezaji ambayo itasimamia shughuli zote za kukiletea ushindi chama hicho katika uchaguzi mkuu ujao ambayo itaongozwa na Katibu Mkuu wa chama hicho, Yusuf Makamba.
Kamati nyingine ni ya Mkakati na Uenezi itakayokuwa chini ya Abdulrahman Kinana.
Alisema katika maandalizi ya uchaguzi, pamoja na kununua magari 150 ambayo yamesambazwa katika halmashauri zote za wilaya kurahisisha usafiri kwa viongozi, CCM inatarajia kununua magari mengine hivi karibuni kwa ajili ya wagombea urais na wagombea wenza, pia mengine 26 kwa ajili ya mikoa yote.
Katika hatua nyingine, Msabaha alisema kuwa pamoja na kutenga sh bilioni 40 kwa ajili ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba, mwaka huu, bado kiasi hicho hakitoshelezi mahitaji yao.
Msabaha alisema fedha hizo hazitoshi kutokana na mahitaji mbalimbali wakati wa uchaguzi, hasa ikizingatiwa kuwa chama chao ni kikubwa.
Ukinyumbulisha matumuzi ya fedha hiyo hayatoshelezi kabisa. Hapa tulipo tuko vichwa vinatuuma tuko hoi bin taaban kwani ukipiga hesabu kuna suala la kuzunguka huku na huko, kwa hiyo tutahitaji kuweka mafuta na mambo mengine. Sisi ni chama kikubwa, alisema Msabaha baada ya kuulizwa swali kuhusu malalamiko ya wapinzani kuhusu CCM kutenga kiasi hicho na kwamba haioni kwa kufanya hivyo inakiuka sheria ya gharama za uchaguzi.
Akizungumzia kuhusu msimamo wa chama hicho kuhusu kura za maoni Zanzibar, kuhusu kuwa na serikali ya umoja wa kitaifa, Msabaha alisema CCM inakubali kuingia katika ushirikiano kuunda serikali ya pamoja.
Kwa mujibu wa Msabaha, suluhu ya suala hilo ni kumaliza migogoro Zanzibar ambayo imekuwepo kwa muda mrefu kwa amani na maelewano.
Ukiisoma habari ya kwanza utaona kwamba ni ya upotoshaji maana Mbunge wa Ulanga Magaharibi si Profesa Juma kapuya,ni Dk. Juma Ngasomgwa....Na habari ya pili nayo jina la Ibrahim Msabaha limeandikwa sivyo...Yule bwana wa Propaganda CCM anaitwa Salum Msabah ....Kuweni makini Tanzania Daima,wahariri fanyeni kazi mnayotakiwa kuifanya...Ni hayo tu
Mtangazaji ITV kuwania ubunge Ulanga Magharibi
na Marietha Mkoka na Benidect Kiwia
MTANGAZAJI mwandamizi wa kituo cha runinga cha ITV, Reinfred Masako, ametangaza nia ya kuwania ubunge katika jimbo la Ulanga Magharibi kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) linaloshikiliwa na Juma Kapuya ambaye ni Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Masako alisema ameamua kwa dhati kuwania ubunge katika uchaguzi mkuu mwaka huu kutokana na haki yake ya msingi aliyonayo ya kuchagua na kuchaguliwa katika ngazi yoyote ya uongozi.
Masako alisema nia hiyo ya kuwania ubunge kwenye jimbo hilo zaidi ni kusambaza elimu kuhusu hifadhi ya jamii, lishe bora kwa makundi maalamu ya kina mama wajawazito na wazee, siasa, uchumi na maendeleo ya jamii pamoja na usalama wa raia na mali zao katika michezo.
Mkongwe huyo wa habari aliyefanya kazi takriban miaka 32 toka mwaka 1978 hadi hivi sasa na katika vipindi vitatu tofauti visivyopungua miaka 10 alitumia muda huo kutoa elimu ya jamii zaidi kitu ambacho kinampa fursa ya kuwania jimbo hilo.
Nimedhamiria kuhamisha uzoefu wangu niliopata katika utendaji wangu kwa miaka yote isiyopungua 32 kwa wananchi wenzangu katika kulenga maeneo makuu matatu ikiwa ni pamoja na shughuli za kilimo, uvuvi na ufugaji, alisema Masako.
Aidha, Masako alisema fursa zilizopo katika jimbo ambalo ameweka nia ya kugombea ni pamoja na mito yenye maji yanayotiririka mwaka mzima, miradi ya skimu za maji akielezea kuwa hizo ni rasilimali tosha zinazohitaji maelekezo sahihi ya jinsi ya kutumia na kubadilisha maisha ya wakazi wa jimbo hilo.
Pia alisema amedhamiria kuutumia uzoefu wake ambao kwa ujumla ni sawa na mgodi unaotembea ili wananchi wa jimbo lake waweze kunufaika nao na utekelezaji wake upo ndani ya matumizi sahihi ya fursa ya mapinduzi ya kijani.
na hii
CCM wakorogana kampeni za JK
na Hellen Ngoromera
KAMATI za kampeni za mgombea urais za Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa ajili ya Rais Jakaya Kikwete zimeanza kukorogana.
Mkorogano huo umeanza kujitokeza katika Kamati ya Fedha na Vifaa vya Kampeni iliyotangazwa awali kuwa inaongozwa na Mhazini wa CCM, Amos Makala.
Wakati wa uzinduzi wa uchangishaji fedha kwa njia ya simu za mkononi katika Ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam, Makala aliwatangazia wanachama kwamba ndiye mwenyekiti wa kamati hiyo na makamu wake ni Zakhia Meghji.
Lakini katika mkutano wa chama hicho na waandishi wa habari uliofanyika jana katika ofisi ndogo ya CCM, chama hicho kilitangaza kuwa Meghji ndiye mwenyekiti wa kamati hiyo.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Propaganda, Ibrahim Msabaha, alisema kuwa Meghji ameteuliwa na NEC iliyomaliza kikao chake hivi karibuni jijini Dar es Salaam kuongoza kamati hiyo.
Msabaha aliitaja pia kamati nyingine ya Utekelezaji ambayo itasimamia shughuli zote za kukiletea ushindi chama hicho katika uchaguzi mkuu ujao ambayo itaongozwa na Katibu Mkuu wa chama hicho, Yusuf Makamba.
Kamati nyingine ni ya Mkakati na Uenezi itakayokuwa chini ya Abdulrahman Kinana.
Alisema katika maandalizi ya uchaguzi, pamoja na kununua magari 150 ambayo yamesambazwa katika halmashauri zote za wilaya kurahisisha usafiri kwa viongozi, CCM inatarajia kununua magari mengine hivi karibuni kwa ajili ya wagombea urais na wagombea wenza, pia mengine 26 kwa ajili ya mikoa yote.
Katika hatua nyingine, Msabaha alisema kuwa pamoja na kutenga sh bilioni 40 kwa ajili ya kufanikisha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba, mwaka huu, bado kiasi hicho hakitoshelezi mahitaji yao.
Msabaha alisema fedha hizo hazitoshi kutokana na mahitaji mbalimbali wakati wa uchaguzi, hasa ikizingatiwa kuwa chama chao ni kikubwa.
Ukinyumbulisha matumuzi ya fedha hiyo hayatoshelezi kabisa. Hapa tulipo tuko vichwa vinatuuma tuko hoi bin taaban kwani ukipiga hesabu kuna suala la kuzunguka huku na huko, kwa hiyo tutahitaji kuweka mafuta na mambo mengine. Sisi ni chama kikubwa, alisema Msabaha baada ya kuulizwa swali kuhusu malalamiko ya wapinzani kuhusu CCM kutenga kiasi hicho na kwamba haioni kwa kufanya hivyo inakiuka sheria ya gharama za uchaguzi.
Akizungumzia kuhusu msimamo wa chama hicho kuhusu kura za maoni Zanzibar, kuhusu kuwa na serikali ya umoja wa kitaifa, Msabaha alisema CCM inakubali kuingia katika ushirikiano kuunda serikali ya pamoja.
Kwa mujibu wa Msabaha, suluhu ya suala hilo ni kumaliza migogoro Zanzibar ambayo imekuwepo kwa muda mrefu kwa amani na maelewano.
Ukiisoma habari ya kwanza utaona kwamba ni ya upotoshaji maana Mbunge wa Ulanga Magaharibi si Profesa Juma kapuya,ni Dk. Juma Ngasomgwa....Na habari ya pili nayo jina la Ibrahim Msabaha limeandikwa sivyo...Yule bwana wa Propaganda CCM anaitwa Salum Msabah ....Kuweni makini Tanzania Daima,wahariri fanyeni kazi mnayotakiwa kuifanya...Ni hayo tu