Tanesco wamekaa kikao kuandaa waraka wa kuwalipa dowans.

Mungu saidia watz wapate akili, wajue la kufanya

Nadhani Mungu ametupa akili lakini hatujataka kuzitumia. Labda tumuombe awasaidie watanzania ktumia akili alizowapa. Kuzitumia kwa manufaa ya nchi. Waliopewa akili wamedhani ni kuzitumia kwa ajili ya kuibia wengine kwa makaratasi.
 
TANESCO ni mlango mmojawapo unaotumainiwa na mafisadi kuiangamiza nchi hii. 30% ndio ndoana kuu na wala sio 10% tena.
 
Dowans ni mfupa uliomshinda fisi!
Kwakweli inavyoonyesha ni kwamba JITIHADA HAISHINDI KUDRA..
Move zote zinaonyesha kuwa hii hela inatoka bila tatizo...
Mkubwa ameamua jamani...Fungukeni macho enyi mbayuwayu, na changanyeni na zenu!
 
Kamba kukatikia pabovu.

Kikwete akimlipa Rostam Aziz fedha zetu basi ndio kiama cha mafisadi wote Tanzania - maandamano kote nchini mpaka uwanja uwe msafi vyakutosha.
 
Kaa chini jiulize,kwa nini hukumu hii imetoka wakati huu,uchaguzi umeisha,hamna bunge,na watu wana force malipo yafanyike haraka.Watanzania kweli ni Mandondocha,sijui tuna nini.kuna haraka gani ya kukimbizana kulipa!
 
Kamba kukatikia pabovu.

Kikwete akimlipa Rostam Aziz fedha zetu basi ndio kiama cha mafisadi wote Tanzania - maandamano kote nchini mpaka uwanja uwe msafi vyakutosha.

Sema wanalipana kwasababu na yeye ni mmoja hivi uliishawahi kujiuliza kwanini Kikwete ameng'ang'ania sana Energy Sector stuka mapema all in all kuna kitu anacho ndani yake humo na maslahi yake ndiyo hayo ya Dowans unayaona more to come i tell you subiri uje usike habari ya WIND ENERGY kwenye zile WIND MILLS.
 
Sema wanalipana kwasababu na yeye ni mmoja hivi uliishawahi kujiuliza kwanini Kikwete ameng'ang'ania sana Energy Sector stuka mapema all in all kuna kitu anacho ndani yake humo na maslahi yake ndiyo hayo ya Dowans unayaona more to come i tell you subiri uje usike habari ya WIND ENERGY kwenye zile WIND MILLS.

Wind Energy kuna Sixtelecoms na pia kuna tenda imebuniwa ya kutengeneza vocha za LUKU ziwe kama za simu na ni mradi wa Riz 1
 
Kwa hiyo TANESCO ndo wanalipa? kesi imeshaandikishwa mahakama kuu?
Waraka unaandaliwa kwenye kikao?...........waraka ni nini?

Kwa hiyo TANESCO ndo wanalipa? TaANESCO ndiye mdaiwa wa DOWANS na analipa kwa hela zile ambazo Dr Rashid alikopa toka mabenki mbalimbali zikahifadhiwa pembeni kusubiri hukumu ya ICC ambayo dhahir ilikuwa TANESCO washindwa(ilipangwa)
Kesi imeshaandikishwa mahakama kuu?Jaji Werema kama Mwanasheria mkuu anapaswa kusajili kesi hii mahakama kuu...kwa kuwa amesema alazima tulipe basi ameshasajili kesi tayari na anasubiri mgao wake
Waraka unaandaliwa kwenye kikao?...........waraka ni nini?Waraka ni kwa ajili ya taarifa kwa umma(kama hii ya mwema tunayoiona sasa) katika kujaribu kujustify uhalali wa malipo...hivi kikao muhimu ku minute waraka
 
What can Nigeria do to live up the promise of its postcolonial dream? First, we will have to find a way to do away to do away with the present system of political godfatherism. This archaic practice allows a relative handful of wealthy men - many of them half-baked, poorly educated thugs - to sponsor their chosen candidates and push them right through to the desired political position, bribing, threatening and, on occasion, murdering any opposition in the process.

Source: Chinua Achebe, New York, 15 January 2011
 
Wind Energy kuna Sixtelecoms na pia kuna tenda imebuniwa ya kutengeneza vocha za LUKU ziwe kama za simu na ni mradi wa Riz 1
Du...Ama kweli enzi za mwalimu zilishapita!..(Namkataa Nyerere, Na mambo yake yote..ninayakataa!)
 
Kwanini wanaharakisha hivyo? Labda tuelezwe sababu za kuwa na haraka kiasi hicho. Hisia zangu zinaniambia kuwa wanataka mambo hayo yaende haraka kabla Bunge halijakaa ili lisilete matatizo. Pengine Bunge linaweza kupiga kelele kiasi kwamba kama watakuwa hawajalipa fedha hizo, basi hazitalipwa tena. Kwa hiyo inaonekana kuwa ni lazima zilipwe kabla Bunge halijakaa.
 
Taarifa za uhakika kutoka ndani ya mwanakikao. Zinasema uongozi wa TANESCO wako leo wamekaa kikao wanaandaa waraka wa kuwalipa DOWANS. Ni Mungu tu aingilie kati hali ya nchi hii. Saa chache zilizopita bado walikuwa ndani ya kikao hicho.
Mtaka Haki na wana jf wenzangu mnaoitakia mema nchi hii, hii issue ya malipo kwa Dowans ina pande mbili.
  1. Hoja ni ya kisheria, hapa tumefungwa kisawasawa, back, front, left and right, hakuna mahali pa kutokea, mkataba ule ni mkataba mbovu hata mwanafunzi wa mwaka wa sheria linakofundishwa omo la law of contract, ataling'amua. Kisheria Dowans wana haki asilimia 100% kulipwa. Licha ya kuwa ni kampuni feki, wamiliki feki, usajili feki na kila kitu feki, yale majenereta, ni majenereta kweli na yanafua umeme kweli, hivyo fidia ni kufidia hizo genereta, haijalishi ni za nani, lakini zipo ndio maana ICC wakatupilia mbali uhalali wa kampuni na kuzingatia tuu mkataba.
  2. Kisheria naamini wanasheria wa Tanesco na wale wa Mwanasheria Mkuu, sio vilaza ki vile, kupitisha mkataba ule kama ulivyokuwa, wamekuwa taken care vizuri ndio maana wakapitisha madudu yale.
  3. Naamini timu ya defence ya Tanesco kwenye shauri la ICC, sio butu kivile kwenda na hoja nyepesi nyepesi ili Tanesco washindwe, wamekuwa well taken care off ili mambo yaende.
  4. Watu wanantaja taja fisadi Rostam as as if ni yeye ndie atakayeyachukua hayo mabilioni ya fidia, mimi nasema no, sio Rostam, yeye Rostam ametumika tuu kama front, kama ilivyo kwa Kagoda, ni front tuu ya kuchotea pesa llakini wafaidika wakuu ni wengine, na amini nawaambieni, siku mkisikia who is behind Rostam, mtashindwa kuamini!. Kikulacho ki nguoni mwako.
  5. Sasa hao walio behind Rostam, ndio waliomtuma mwanasheria mkuu kukubali tulipe, na kumtuma Ngeleja kulitangazia taifa tutalipa, hata bili kulipitishia baraza la Mawaziri, maana kina Sitta, Mwakiembe, Magufuli etc wasingekubali upuuzi huo.
  6. Kwa vile kisheria limesimama, bodi ya Tanesco, haina njia bali kujipanga ili mahakama kuu ikisha thibitisha tuu faini ilipwe, Tanesco walipe papo hapo, tena kwa kukopa CRDB!.
  7. Lengo la Tanesco kulipa papo kwa papo ni kuepuka ongezeko la Shilingi Milioni 25, kila siku ya Mungu itakayopita, tangu siku Mahakama Kuu imeiamuru Tanesco kulipa. Hiyo inamaana deni linaongezeka kwa milioni 100 kila baada ya siku 4, na zikifika siku 40, ni bilioni moja nyingine.
  8. Ubishi wa kina Sitta na wote tunaopinga malipo hayo, hatuna hoja za kisheria bali za kisiasa, kina Sitta na Mwakiembe wanataka kuleta siasa kwenye sheria ambayo pia inawezekana.
  9. Tanzania tunaweza tukapinga kulipa hizo pesa na tukajitoa kwenye ICC, hata kama hao wawekezaji Wazungu, watakosa imani na nchi yetu na kususa kuwekeza, wafungashe na kwenda zao kwao, tuone hao Baric watachimba dhahabu gani Canada etc. Madini ni yetu, sio jukumu letu kuwabembeleza wawekezaji, kwa sababu wenye mali ni sisi, ni jukumu la wawekezaji kuja kutubembeleza sisi ndio tuwape madini yetu, waneemeke wao na kutuachia mashimo. Kwa Tanzania its the other way round, sis ndio wenye mali, ala tunawalamba miguu hawa jamaa wanaokuja kutukanyaga.
  10. Na mwisho, vunjilia mbali mikataba yote ya kimataifa isiyo na maslahi kwa taifa, wachina wapo tayari kuendesha kila kitu kwa mikataba yenye maslahi kwetu, na hata tukiwafukuzia mbali wazungu wote, watalii wa kichina pekee wanaweza kushibisha soko la utalii maradufu kuliko wazungu ambao fedha yote ya maana, huilipia huko huko, hapa hubakisha fedha ya kulipia shanga, vinyago, karanga na kuwalipa madada zetu kwa zile huduma!.
 
Huu ni wizi wa mchana peupe, kwa nini wasingoje bunge likae?????????? Wanalipa kwa budget ipi, imeidhinishwa na nani????????? Wote watakao husika wapelekwe mahakamani, bila kujali wamepewa amri na nani, watatajana huko mbele ya sheria. Sheria gani inaruhusu kutumia fungu kubwa la fedha bila kupitia bungeni au baraza la mawaziri??????????? CHADEMA nawaomba wainitiate vote of no confidence kwa huyo aliye toa amri, hata kama ni mkuu wa nchi he should be imperched. Si dhani kama CCM wote ni wezi wa aina hii, bila shaka kuna watakao suport hiyo motion. Bandugu twafa tugangamale!!!!!!!!!


Tungekuwa na mahakama zenye meno wasingekuwa na guts za kufanya hivyo,hatuna independent judicial organs nchi hii,Rais bado ana nguvu kubwa sana hakuna kitakachoeleweka huko,kwenye impeachment ndo kabisa,utakuta Mwakyembe na Sitta ndo wanaunga mkono.....Hawa ni kubanana nao kwa nguvu ya umma+media.......huku tukisubiri Katiba mpya ambayo natumai ita-address mapungufu haya...........
TANESCO wao wanafuata order kutoka kwa Ngeleja anayepokea kutoka kwa JK na Rostam,they have no option bali kutii mamlaka zilizowaweka hapo na mkurugenzi ndo yule aliyeteuliwa na Rais.......ndo maana tunasema Rais ana mamlaka kubwa na Katiba mpya ni suluhisho.:plane:
 
Mtaka Haki na wana jf wenzangu mnaoitakia mema nchi hii, hii issue ya malipo kwa Dowans ina pande mbili.
  1. Hoja ni ya kisheria, hapa tumefungwa kisawasawa, back, front, left and right, hakuna mahali pa kutokea, mkataba ule ni mkataba mbovu hata mwanafunzi wa mwaka wa sheria linakofundishwa omo la law of contract, ataling'amua. Kisheria Dowans wana haki asilimia 100% kulipwa. Licha ya kuwa ni kampuni feki, wamiliki feki, usajili feki na kila kitu feki, yale majenereta, ni majenereta kweli na yanafua umeme kweli, hivyo fidia ni kufidia hizo genereta, haijalishi ni za nani, lakini zipo ndio maana ICC wakatupilia mbali uhalali wa kampuni na kuzingatia tuu mkataba.
  2. Kisheria naamini wanasheria wa Tanesco na wale wa Mwanasheria Mkuu, sio vilaza ki vile, kupitisha mkataba ule kama ulivyokuwa, wamekuwa taken care vizuri ndio maana wakapitisha madudu yale.
  3. Naamini timu ya defence ya Tanesco kwenye shauri la ICC, sio butu kivile kwenda na hoja nyepesi nyepesi ili Tanesco washindwe, wamekuwa well taken care off ili mambo yaende.
  4. Watu wanantaja taja fisadi Rostam as as if ni yeye ndie atakayeyachukua hayo mabilioni ya fidia, mimi nasema no, sio Rostam, yeye Rostam ametumika tuu kama front, kama ilivyo kwa Kagoda, ni front tuu ya kuchotea pesa llakini wafaidika wakuu ni wengine, na amini nawaambieni, siku mkisikia who is behind Rostam, mtashindwa kuamini!. Kikulacho ki nguoni mwako.
  5. Sasa hao walio behind Rostam, ndio waliomtuma mwanasheria mkuu kukubali tulipe, na kumtuma Ngeleja kulitangazia taifa tutalipa, hata bili kulipitishia baraza la Mawaziri, maana kina Sitta, Mwakiembe, Magufuli etc wasingekubali upuuzi huo.
  6. Kwa vile kisheria limesimama, bodi ya Tanesco, haina njia bali kujipanga ili mahakama kuu ikisha thibitisha tuu faini ilipwe, Tanesco walipe papo hapo, tena kwa kukopa CRDB!.
  7. Lengo la Tanesco kulipa papo kwa papo ni kuepuka ongezeko la Shilingi Milioni 25, kila siku ya Mungu itakayopita, tangu siku Mahakama Kuu imeiamuru Tanesco kulipa. Hiyo inamaana deni linaongezeka kwa milioni 100 kila baada ya siku 4, na zikifika siku 40, ni bilioni moja nyingine.
  8. Ubishi wa kina Sitta na wote tunaopinga malipo hayo, hatuna hoja za kisheria bali za kisiasa, kina Sitta na Mwakiembe wanataka kuleta siasa kwenye sheria ambayo pia inawezekana.
  9. Tanzania tunaweza tukapinga kulipa hizo pesa na tukajitoa kwenye ICC, hata kama hao wawekezaji Wazungu, watakosa imani na nchi yetu na kususa kuwekeza, wafungashe na kwenda zao kwao, tuone hao Baric watachimba dhahabu gani Canada etc. Madini ni yetu, sio jukumu letu kuwabembeleza wawekezaji, kwa sababu wenye mali ni sisi, ni jukumu la wawekezaji kuja kutubembeleza sisi ndio tuwape madini yetu, waneemeke wao na kutuachia mashimo. Kwa Tanzania its the other way round, sis ndio wenye mali, ala tunawalamba miguu hawa jamaa wanaokuja kutukanyaga.
  10. Na mwisho, vunjilia mbali mikataba yote ya kimataifa isiyo na maslahi kwa taifa, wachina wapo tayari kuendesha kila kitu kwa mikataba yenye maslahi kwetu, na hata tukiwafukuzia mbali wazungu wote, watalii wa kichina pekee wanaweza kushibisha soko la utalii maradufu kuliko wazungu ambao fedha yote ya maana, huilipia huko huko, hapa hubakisha fedha ya kulipia shanga, vinyago, karanga na kuwalipa madada zetu kwa zile huduma!.
Nakubaliana nawe kuwa tunaweza kukataa kulipa na kuvunjilia mbali uhusiano wetu na mahakama ya usuluhishi lakini point yako namba 10 kuwa wachina wanaweza kuziba pengo la wazungu ni ndoto za mchana.

Wachina ni watu wabaya kweli ila wazuri kujipendekeza kwa watawala. Ukitaka kumkaribisha mchina jiandae kuona serikali ya kidikteta kama Mugabe. Hawana habari yoyote na haki za watu ikiwepo malipo kwa wafanyakazi wao. Wao wanachojali ni kuchuma fedha kwa migongo ya kiutawala.

Hapa Tanzania tuna miradi ya madini inayoendeshwa na wazungu kama GGM nk. Kuna watu wanalipwa hadi 10M per month na hata wafanyakazi wa chini wanalipwa ahueni kulinganisha na mashirika ya serikali, serikali yenyewe au taasisi za benki. I always imagine hali ingekuwaje kama mgodi ungekuwa wa Mhindi au Mchina.

Wachina ni wanyanyasaji wakubwa wa haki za watu. China hata Mei mosi hawasherehekei make haki za wafanyakazi kwao ni tatizo kubwa. Wakija hizi nchi zetu ndo balaa tupu. Miradi mikubwa haifai tu kuwapa wawekezaji ili mradi wana pesa bila kuangalia watakavowatendea wafanyakazi ambao kwa sehemu kubwa wanasupport sehemu jamii. Imefika wakati serikali iangalie haki za wafanyakzi kwanza na malipo yatakayokuwepo kwao kutoka kwa mwekezaji.
 
Back
Top Bottom