PMNBuko
JF-Expert Member
- Dec 27, 2010
- 967
- 154
Kwa miaka mingi sana nimekuwa nikisikia namna watanzania wanavyohujumiwa na shirika lao la umma, Tanesco. Leo yamenikuta. Baada ya kulipia gharama zote za kuunganishiwa huduma ya umeme kwa zaidi ya miezi mitano bila kupewa huduma husika kwa kisingizio kuwa hakuna nyaya, hakuna mita na juzi kuambiwa kuwa mita zipo lakini hakuna box za mita, leo nimetoa kidogo ndipo nimeunganishiwa umeme tena siku ya jumapili. Nimeumia sana kutoa rushwa. Lini Tanesco wataanza kutoa huduma stahili?