Tamthilia: Mtu Aliyethibitishwa Kwenye Maisha Yangu/Certified Person of My Life

Apr 1, 2022
96
175
SEASON 01

TAMTHILIA: MTU ALIYETHIBITISHWA KWA MAISHA YANGU
CERTIFIED PERSON OF MY LIFE (CPL)
( 1-5 )


SEHEMU YA 01.
D ARASANI:

llikua ni muda wa kipindi cha ujasiriamali kwa wanafunzi wa kozi ya biashara. Mwalimu wa somo alikuwa mbele ya Darasa akifundisha. Kutokana na ukali wa Mwalimu huyo; darasa lilikua kimya sana. Frank akiwa kama mmoja wa wanachuo alikua makini sana kusikiliza. Ilifikia hatua alitikisa kichwa juu chini kuonyesha namna ambavyo alielewa mafunzo kutoka kwa mwalimu wake. Kabla kipindi hakijaisha Mwalimu aliuliza swali;

MWALIMU: Wanafunzi, nani anapenda kuwa mfanyabiashara? kwanini? Na mtaji utaupata wapi? (Mwanachuo wa kwanza kunyosha mkono alikuwa ni Loveness, aliambiwa ajibu swali, naye bila kupoteza muda alisimama kisha alijibu kama ifuatavyo)

LOVENESS: Mimi sipendi kuwa mfanyabiashara kwa sababu biashara zina hasara nyingi, ni ngumu kupata mtaji kwa sababu watu wengi wanaitaji fedha na fedha ni ngumu kupatikana.

(Love alimaliza kutoa jibu lake. Kabla mwalimu hajaongea chochote mara aliona mkono mwingine kutoka kwa Frank)
MWALIMU: Naona mkono mwingine pale, bila shaka uliyenyosha mkono una jibu jipya; Ebu tupe jibu lako. FRANK:

(Alisimama kisha alijibu) Mwalimu nataka nimjibu Loveness. Love unaposema kwa m ba hupendi kuwa mfanyabiashara una maana gani? Na kama hupendi tuambie kwanini unasomea kozi ya biashara?

LOVENESS: Mfanyabiashara ni sawa na mtu aliyejiajiri, sasa mimi nikijiajiri kuna faida gani za kusoma? Si nitakua nimepoteza fed ha zangu. Sasa si bora ningekaa nyumbani na hizo fedha za ada ningezitumia kama mtaji. Nasomea Biashara kwa sababu Serikali itanipa ajira zinazohusu usimamizi wa biashara za wananchi.

FRANK: Hapana, kumbe una mawazo finyu hivyo? Tena wewe mwanachuo wa elimu ya juu unawezaje kutupatia majibu kama hayo? Hata hiyo Serikali haiwezi ikakuamini kwa sababu huwezi kuongoza wafanyabiashara wakati hupendi biashara.
LOVENESS: Kwani tatizo lipo wapi? Jamani kila mtu ana ndoto zake. Humu ndani kuna watu wanawaza kujiajiri na kuna wengine akina sisi hatuna mpango huo. Mimi nachoamini ni kwamba baada ya kuhitimu chuo kinachofuata ni kuajiriwa tu, na nina imani kuwa nitaajiriwa tu. Siwezi kupoteza muda wangu na fed ha zangu bure! Eti nijiajiri, looh! hata wale wenzangu walioko mtaani si watanicheka?

FRANK: Loveness!! kwanza serikali ni nini? Unataka kusema Serikali haifanyi biashara? Hivi hujawai kusikia Serikali inanunua au kuuza vitu nje ya nchi? Tena ni juzi tu tulimaliza mada ya biashara za kimataifa (international trade), unataka kusema ile mada hukuilewa au?

SEHEMU YA 02

LOVENESS: Kwanza wewe unataka nini? Kama unaona jibu langu sio sahihi basi tupatie jibu lako. Kwa sababu naona unapinga sana mawazo yangu. (aliongea akiwa amepanick, kwa hasira aliamua kukaa chini)

FRANK: Haina haja ya kukasirika kwa sababu swali liko wazi kwa sisi wote ambao tunachukua kozi ya biashara. Mimi sijamaanisha kwamba sitaki kuajiriwa, pia sijamkataza mtu kuajiriwa, ila kutokana na swali la mwalimu; majibu ya dada yetu Love sidhani kama ni sahihi. Mwanachuo aliye kamili kifikra hawezi kutujibu majibu kama hayo, alafu....

(Frank kabla hajamaliza kuongea; Loveness alisimama akiwa amejazwa hasira na jazba)

LOVENESS: Kwahiyo mimi sina fikra? mimi sifai kuwa mwanachuo au sio? unaamua kunitu.... (Love alishindwa kuendelea kuongea, pale pale alianza kulia kwa kwikwi, ghafla alipiga hatua alitoka nje ya darasa pasipo kugeuka nyuma)
(Baada ya tukio hilo kulitokea ukimya mzito, wanachuo walikausha kimya.

Baadhi walimuonea huruma Love. Wengine waliona ni jambo la kawaida. Frank bado alisimama, alitaka kukaa lakini alisimamishwa na mwalimu, aliambiwa ajibu swali kwa faida ya wengine)
FRANK: Mimi napenda kuwa mfanyabiashara, hata kama ikitokea nikapata ajira selikalini lakini sitoacha kufanikisha ndoto zangu za kuwa mfanyabiashara. Na ndio maana niliamua kusomea kozi hii. Napenda biashara kwa sababu inapatikana kila sehemu. Biashara ipo kwenye sekta za umma hata sekta binafsi. Kuwa mfanyabiashara kuna faida nyingi kama vile uhuru wa maisha, uhuru wa maamuzi, pesa zisizo na kikomo na faida nyinginezo. Biashara inatengenezwa na bidhaa pamoja na huduma za kijamii, hivyo basi ni rahisi mtu yeyote kujikita katika sekta hiyo, na ndio maana hata serikali inatengenezwa na biashara.

Kuhusu mtaji ni rahisi tu, kuna mikopo kutoka benki na mashirika, akiba binafsi, misaada toka kwa watu wa karibu (familia na marafiki), wadhamini na kadhalika.


MWALIMU: Safi sana, nadhani hakuna
hasiyekuelewa, hii inaonyesha ni jinsi gani una upeo wa kielimu hasa katika kozi yako ya biashara.

Darasa tutaonana kipindi kijacho. (Mwalimu aliondoka darasani).
(Baada ya Mwalimu kuondoka tu; huku nyuma kulisikika minong'ono na mijadala kuhusu yaliyotokea, kuna waliosema Frank amekosea sana kwa kumdhalilisha Loveness, wengine walisema Frank ameongea sahihi. Ilikua ni kelele tu, kila mtu aliongea neno lake. Wanachuo walitawanyika walielekea hosteli. Ndani ya darasa alibaki Frank pekee. Ilikuwa ni mida ya saa sita mchana, jamaa aliona bora ajisomee akiwa anasubiri muda wa chakula cha mchana. Alitoa daftari na peni kisha alianza kupiga pindi. Hakutaka kuwaza sana kuhusu kilichotokea kwa sababu aliona ameongea vitu ambavyo mtu yeyote angeweza kuongea.

Akiwa anajisomea mara aliingia mdada flani hivi aitwaye Maria

MARIA: Frank vipi? mbona umebaki peke yako humu ndani?

FRANK: Nimeamua tu, napitia pitia vitu flani.
MARIA: Hivi una taarifa kuwa mwenzio kapelekwa hospitali?

FRANK: Mwenzangu gani?
MARIA: Loveness. Baada ya kususa kipindi alikimbilia hosteli akiwa analia. Sie tumetoka kipindi tumefika hosteli tumekuta mtu kazidiwa, ilibidi tumuwahishe hospitali ya chuo.

FRANK: (Akishangaa) Eeh! lakini si alikua poa tuü amezidiwa kwa tatizo gani?
MARIA: Hospitali wanasema alizidiwa na maumivu ya kichwa. Na inasemekana kuwa chanzo ni wewe!
(Frank alikodoa macho, alishindwa kuelewa! Balaa zitoooo!!)

ITAENDELEA

SEHEMU YA 03

FRANK: Kwahyo hata wewe Maria unaamini mimi ni chanzo?
MARIA: Sasa chanzo ni nani? Nahisi ni kutokana na yale uliyoongea Darasani.
FRANK: Kwani niliongea vibaya?
MARIA: Hapana, ulikua sahihi tena sana tu, ila ndo hivyo mtu yupo hospitali.
FRANK: Sawa, mimi naenda kula. Kwanza nishachoka, nataka nikapumzike hosteli (Aliongea akisimama kisha alipiga hatua akiondoka)

MARIA: We Frank wewe, ina maana huendi hospitali kumuona Love?...Mmh! makubwa.
Frank alipotelea nje, Maria aliganda kwa sekunde flani akiwa anashangaa kisha nae aliamua kuondoka! HOSPITALI:

Loveness akiwa hospitali alitembelewa na marafiki zake ambao ni wanachuo wenzie. Baadhi walimletea zawadi kama Juisi, Biskuti na matunda; aliwashukuru. Issa alikuwa ni mmoja wa wanachuo ambao walimtembelea Love hospitali, yeye baada ya kufika ndani ya chumba cha mgonjwa alikaa pembeni ya Godoro kisha alitoa pole zake kama ifuatavyo;

LOVENESS: Kwa sasa naendelea vizuri, dokta kasema naweza kuruhusiwa.
ISSA: Kwani tatizo lilikua nini?
LOVENESS: Ni kichwa tu ila kwa sasa niko poa.

ISSA: Kwahiyo kesho utakuja kwenye kipindi?

LOVENESS: Nitaangalia.
(Mara aliingia daktari, aliwaomba wanachuo wampishe ili aongee na mgonjwa wake. Wanachuo walitoka nje.)
DOKTA: (Akimtazama Love) Kama nilivyosema; jitahidi kupunguza mawazo. Mara nyingi mawazo ndio sababu kubwa ya maumivu ya kichwa. Pia hakikisha unakunywa maji mengi na ufanye mazoezi ili mwili upate afya bora na nguvu. Pia usipende kukaa pekeyako, njia kuu ya kuondoa fikra, stress na mawazo mabovu ni kujichanganya na watu wengine. LOVE: Sawa.

Dokta alimaliza kutoa ushauri kisha alimruhusu Love kuondoka hospitali. Love na marafiki zake waliondoka, walirudi chuoni hosteli.

HOSTELI:
Frank baada ya kula alielekea hosteli, alitulia akijisomea. Mara aliingia Rama ambaye ni mwanachuo mwenzie, wanasoma darasa moja.

RAMA: Kwa raha zote umetulia bila wasiwasi, kaka hivi hujishtukii?
FRANK: Kujishtukia kwa lipi?
RAMA: We si ndiye umempa ugonjwa wa kichwa mwenzio, au ulimpa makusudi? (Rama aliongea akiwa anacheka)
FRANK: Ah! nikaushie, sio kila mtu lazma aende akamuone, wengine tutamuombea kwa Mungu atapona.


SEHEMU YA 04

RAMA: Dah! tena unajibu utafikiri wewe sio chanzo, haya bwana.
FRANK: We kama ulienda poa. Mimi Siwezi kwenda.

Hivyo ndivyo ilivyokuwa, Frank hakwenda kabisa kumuona Loveness. Watu wengi hawakupendezwa na jambo hilo, walimlaumu wakimwambia kuwa ana roho m baya. M baya zaidi kila akiulizwa kwanini hakwenda alijibu kirahisi tu.

Kama kawaida Love baada ya kurudi hosteli alijitupa kitandani akiendelea kupona taratibu. Rafiki zake waliendelea kumtembelea, akitoka mmoja aliingia mwingine, wanaume kwa wan awake, pia wengi walimuuliza wakitaka kujua kama kes ho ataingia darasani, hata hivyo Love hakuwa na jibu kuhusu swali hilo.

SIKU ILIYOFUATA:
DARASANI: llikuwa ni siku nyingine tena, mida ya asubuhi wanachuo walikusanyika kwaajili ya kipindi oha uchumi. Darasa lilijaa kweli kweli, kila kona kulitapakaa utitiri wa watu. Walikaa katika makundi makundi wakijadili mambo mbalimbali.

Hata hivyo macho ya watu wengi yalikuwa yakiwatafuta vijana wawili ambao ni Frank na Love, vijana hao hawakuonekana ndani ya darasa.

ISSA: Naona pasua kichwa hafiki leo, au naye anaumwa?

MARIA: Achaga unafki na wewe. Mwalimu tu bado hajafika, muda bado.
ISSA: Muda bado kivipi wakati yeye kila siku huwa anakua mtu wa kwanza kuingia kwenye kipindi!! tena huwa anakaa siti za mbele.

(Wakiwa bado wanamjadili Frank hatimaye Frank aliingia. Huwa anapenda kukaa mbele lakini kwakuwa siti za mbele zilijaa alitulia akitafuta sehemu nyingine ya kukaa, nyuma ya darasa aliziona siti mbili zikiwa hazina watu, alijongea taratibu alienda kukaa kwenye siti moja. Hazikupita dakika nyingi mwalimu wa uchumi aliingia darasani.)

MWALIMU: Natumaini kila mtu ameingia, hivyo basi CR (kiongozi wa darasa) naomba ukafunge milango yote.

(CR alisimama kisha alienda kufunga milango. Alifunga mlango wa mbele kisha aliufuata mlango wa nyuma, yaani ile anataka kufunga tu; Loveness alizama ndani, watu wote macho kodoo, patamu hapo mwanawane!!. Baada ya Love kuingia CR alifunga mlango. Balaa lilikuwa kwenye siti za kukaa, Love alizungusha macho akijiuliza akakae wapi, kwa mbali aliona siti moja ikiwa haina mtu, taratibu alipiga hatua hadi kwenye siti iliyobaki, baada ya kuifikia aliganda, macho yalimtoka kama popo bawa vile, sura ilimshuka akihisi kichefuchefu, alitamani kutapika!

Hakutegemea kama angemuona mtu anayemchukia kupita maelezo. Alitulia akijiuliza ataanzaje kukaa karibu na mtu hasiyetaka kumuona? Yaani aanze tu akae na huo utopolo? Akae na huo utelembwe? Hakunaga kitu kama hicho. Alihisi kinyaa, alitamani ateme mate chini ila alipotezea, kwa makusudi alipitiliza kama sio yeye vile, aliamua kwenda kujibana na marafiki zake. Kitendo hicho kilizua gumzo na minong'ono ya chini chini, bifu ndo kwanza limechanua! Atakufa mtu mwaka huu! Minong'ono ilizua kelele, ilibidi ticha aingilie kati)

SEHEMU YA 05

MWALIMU: Darasa naomba utulivu.
(Wanachuo walitulia, mwalimu aliendelea)
MWALIMU: Nafikiri hakuna hasiyejua kushuka kwa uchumi wa nchi. Uchumi wa nchi unategemea sana biashara mbalimbali za wananchi wa nchi husika.

Mfano kupitia kodi na tozo mbalimbali. Kama wananchi wasipofanya biashara na kuichangia nchi yao kupitia kodi hivyo basi ni lazima uchumi utashuka tu. Lakini pia biashara hizi za wananchi zina changamoto nyingi, changamoto hizo ndizo zinazofanya watu kukwepa kodi. Sasa kila mtu aandae karatasi moja kisha aniandikie ni changamoto zipi zinazowakabili wafanyabiashara hadi washindwe kulipa kodi? Natoa dakika 10 tu kwa zoezi hili. Hakikisha unaandika jina lako na namba ya usajili.

(Baada ya maelezo ya mwalimu wanachuo waliandaa karatasi kisha walijibu swali. Kila mtu alikuwa bize akiandika majibu ya ke, wengine walishuka tu, baadhi walitazama juu wakihesabu kenchi, hatimaye dakika 10 zilikwisha.)

MWALIMU: Natoa dakika 2 za kukusanya, kunja karatasi yako alafu mpe wa mbele yako nae ampe wa mbele yake hadi zifike kwangu.

(Karatasi zilikusanywa kisha ziliwekwa kwenye boksi. Mwalimu alishika box kisha alitangaza tena kama ifuatavyo)
MWALIMU: Sasa nitapita na hili box, kila mtu ataingiza mkono kisha atachukua karatasi moja alafu baadae atapita mbele atatusomea majibu ya kwenye karatasi ambayo ataichukua.

(Zoezi lilifanyika kwa haraka, wanachuo walizamisha mikono kwenye box kisha walichukua karatasi moja moja. Mwalimu aliendelea kutoa maelekezo;)
MWALIMU: Kila mtu afungue karatasi yake kisha atazame ili ajue amechukua karatasi ya nani. (Frank alifungua haraka haraka, alitazama jina la mwenzie alikuta amechukua karatasi ya LOVENESS JOHN. Jamaa alipagawa, alijiuliza abadili karatasi au afanyaje?)

"Dah hili balaa, naona kama nimechukua bomu...sasa sijui nifanyaje, na mwalimu alisema akimuona mtu anabadili karatasi atapata tabu sana!! Duh! ila itafahamika mbele kwa mbele" Frank aliteseka kwa mawazo, macho yake bado yaliganda yakitazama jina la Love.

(Wanachuo waliendelea kukagua makaratasi yao, Maria alitazama alikuta kachukua karatasi ya mtu hasiyemjua, hata Issa alikuta kachukua karatasi ya mtu hasiyemtambua. Love kabla hajafungua alichungulia karatasi za marafiki zake kisha alifungua karatasi yake kwa madoido na mbwebwe zote, alitabasam akiona raha kufungua karatasi yake, tena aliringa akiwaziba wenzie wasione. Mara ghafla tabasam lote lilikwisha, manjonjo yote yalipotea, sura ilipauka kisha ilisinyaa ilitengeneza mikunjo na minuno, alikasirika kweli kweli, alichukia kuona ameshika karatasi ya FRANK KAKOLANYA. Hapo ndo penyewe sasaa!

ITAENDELEA

IMG_2314.jpg
 
SEASON 01

TAMTHILIA: MTU ALIYETHIBITISHWA KWA MAISHA YANGU
CERTIFIED PERSON OF MY LIFE (CPL)
( 6-10 )

WHATSAPP 0768315707

SEHEMU YA 06


Love alitulia akifikiria kitu cha kufanya, aliwaza aitupe karatasi au aichane? Aliona kama amepata balaa kuchukua mtihani wa Frank. Alipata wazo, aliwaza ni heri abadilishane na rafiki yake ambaye alikaa pembeni. Aligeuka alimtazama rafiki yake kipenzi;

LOVENESS: Happy, we Happy!! Tafadhari nakuomba tubadilishane karatasi (aliongea kwa sauti ya chini)

HAPPY: Hapana Love mwalimu atatuona. Kwani hiyo ina nini?

LOVENESS: Happy nakuomba mwaya nisaidie. Mwalimu hawezi kutuona.

HAPPY: Mmh ilete basi fanya haraka (aliongea akinyosha mkono kuipokea) (Kwa siri walibadilishana karatasi. Angalau moyo wa
Love ulitulia, alipata amani. Alimchukia Frank kupita maelezo, alimuona kama shetani vile. Alafu eti apite mbele akasome majibu ya mtu anayemchukia? We uliona wapi? we ulisikia wapi?. Darasani kulikuwa kimya, wanachuo walitulia wakisuburi maelekezo kutoka kwa mwalimu. Wakiwa wanasubiri maelekezo mara Mwalimu alitoka kule mbele alianza kuzunguka dawati moja hadi jingine, usoni alionekana kuchukia sana, sasa sijui alichukia nini. Wanachuo walijua kumekucha, walihisi kuna balaa linakuja. Ghafla mwalimu alisimama pembeni ya dawati ambalo alikaa Love na Happy.)

MWALIMU: Wewe binti mwenye nguo nyeupe ebu simama (alimsimamisha Happy) (Happy alianza kuogopa, alijua kimeshanuka, alisimama akiwa anatetemeka)

MWALIMU: Humu ndani nyie wote ni watu wazima, hadi mmefika hatua hii ya chuo inaonyesha ni jinsi gani mna uelewa mkubwa sana. Sasa nashangaa kuona baadhi ya watu bado hawajielewi. Na wewe dada hapo uliyevaa nguo nyekundu ebu simama! (Hapo sasa alimuambia Loveness) (Love alisimama akihisi dili limekuwa dirisha)

MWALIMU: Nyie wawili naomba mnipe jibu sahihi kwanini mlibadilishana karatasi? au mlijua mnafanya siri? Mimi nilianza kuwaona muda mrefu sana ila niliwaacha kwanza. (Love na Happy walikua kimya, walionyesha wazi wazi kuwa ni kweli walibadilishana).

MWALIMU: Sasa ebu kila mtu arudishe karatasi ya mwenzie haraka.
(Loveness akiwa anaogopa alirudisha karatasi ya Happy kisha Happy alirudisha karatasi ya Love. Hatimaye kila mtu alichukua karatasi yake)

SEHEMU YA 07

MWALIMU: Alafu kwanini mmebanana? wewe mwenye nyeupe nenda kakae kwenye ile nafasi ya wazi. (Happy alisimamishwa aliambiwa akakae pembeni ya Frank)

MWALIMU: Na wewe mwenye nyekundu utakuwa mtu wa kwanza kupita mbele ili ukatusomee majibu ya karatasi uliyoichukua.
(Love alihisi moyo wake unataka kupasuka, alitamani ardhi ichimbike ili azame chini akajifukize. Hakuwa na namna, taratibu alipita mbele. Alisimama mbele ya steji, hapo sasa kila mtu alimtazama Love, patamu hapo. Love alitulia kimya akiwa na hasira, muda wote alitazama chini tu. Ilifikia hatua alianza kumchukia hadi mwalimu, alimuona mchochezi muharibifu. Kuna muda alitamani atoke nje ya darasa lakini ndio hivyo haiwezekani)

MWALIMU: Kabla hujatusomea majibu ya mwenzio, kwanza jitambulishe wewe mwenyewe unaitwa nani.

LOVENESS: Naitwa Loveness John (alijitambulisha kwa upole kabisa).
MWALIMU: Haya tusomee umechukua karatasi ya mtihani wa nani? Soma jina lake ili naye apite mbele.

LOVENESS: (Akionyesha kuchukia) Anaitwa FRANK KAKOLANYA. (Baada ya kutaja jina hilo kila mtu alishtuka, hata Frank mwenyewe alishangaa!!! hapo sasa minong'ono ilianza ndani ya darasa, kuna watu walicheka, wengine walitabasam wakijua kwamba yajayo sio ya mchezo mchezo)

ISSA: Aah! kumbe ndio maana Love alitaka kubadili karatasi, duuh! hata ningekua mimi mbona ningelichana kabisa.

MARIA: We nae kama mwanamke mambo yako. Basi kuwa wewe si unataka uwe mwanamke.

ISSA: Kausha basi na wewe, unataka niwe demu ili wahuni wanifanyaje kwa mfano?

MARIA: We ndo ukaushe, muone lisura lake. (llikuwa ni patashika nguo kuchanika, ndani ya mjengo kelele kama zote)

MWALIMU: Naomba utulivu. Frank Kakolanya upo humu ndani?

FRANK: Nipo mwalimu.

MWALIMU: Ningependa usimame kisha upite m bele. (Frank alisimama alipita m bele, alienda kusimama pembeni ya Love)

MWALIMU: Frank nawe ebu fungua karatasi yako alafu tuambie umechukua karatasi ya mtihani wa nani? Nataka tufanye mambo kwa haraka.

FRANK: Nimechukua karatasi ya LOVENESS JOHN.

MWALIMU: Tobaa wallah wabilahii! Mbona hayo ni maajabu ya mzee Rajabu kutaka hijabu pasipo na sababu!
(Yaani hata Mwalimu mwenyewe alishangaa, Loveness pia alishangaa, darasa zima lilikodoa macho; kila mtu alishindwa kuelewa imekuaje jambo kama hilo litokee? Mbona ni balaa zito. Hawakuamini, walijua labda Frank anatania.)

MWALIMU: Frank ebu nipe karatasi yako nione, kwanza haiwezekani!
(Mwalimu alichukua karatasi ya Frank alitazama alikuta ni kweli jamaa kachukua mtihani wa Love. Ticha alijikuta anacheka bila sababu, mambo mengine yanafurahisha kwakweli, unaweza sema ni uchawi kumbe hata sio ushirikina bali ni uhalisia wa maisha tu)

MWALIMU: Basi sawa! nafikiri hii itakuwa nzuri kwa sababu tutasikia majibu kutoka kwa hawa wote, au sio wanachuo wangu?

WANACHUO: Ndiyoooo!!

MWALIMU: Mwanzoni nilitaka Loveness aanze kuongea, lakini ngoja nibadili uteuzi, Frank anza kutusomea majibu ya Love.
(Hapo ndo penyewe sasa. Frank kabla hajaanza kusoma kwanza alimtazama Love alimuona katazama pembeni, pia aligundua kuwa Love hajapenda kinachoendelea. Hata hivyo alimpotezea, alitazama karatasi kisha alianza kusoma majibu ambayo Love aliandika

kwenye mtihani wake)

FRANK: Love ameandika hivi "Changamoto kubwa kwa wananchi katika biashara ni kutokujitambua. Watu wengi wanakurupuka kufanya biashara wakidhani biashara ipo kwa ajili ya kila mtu. Matokeo yake hawapati chochote katika hizo biashara, na ndio maana wanakwepa kodi. Sababu ya pili ni umri, watu hawazingatii kabisa swala la umri. Wao wanadhani watoto, vijana hata wazee wote wanaruhusiwa kufanya biashara. Matokeo ya ke watoto wengi hawana elimu ya kulipa kodi, vijana wengi wanatumia madawa na pombe hivyo wanakwepa kodi, na wazee wengi wanashindwa kufanya kazi kwa ufasaha hivyo basi wanashindwa kulipa kodi.

SEHEMU YA 08

(Frank alimaliza kusoma majibu ya Love. Wanachuo wote walitulia kirnya wakitafakari majibu hayo. Mwalimu alikosa neno, yeye alikuwa anatabasam tu. Love alihisi baridi ya hofu, sio kwamba alikua hasikilizi, alisikia kila kitu alichokiandika, alisubiri mwalimu aongee.)

MWALIMU: Nadhani wote mmesikia vizuri majibu ya Loveness. Sasa kabla sijaruhusu maswali, naomba Loveness nae atusomee majibu ya Frank.

LOVENESS: Ameandika hivi; " Wafanyabiashara ni nguzo kuu ya uchumi wa nchi, bila wao nchi haiwezi kuendelea. Katika biashara watu wanakutana na changamoto kubwa ikiwemo 1. Kushuka kwa thamani ya fedha. Kama fedha ikiwa haina thamani katika nchi ni ngumu sana kwa mfanyabiashara kupata faida ndio maana wanashindwa kulipa kodi. 2. Ukubwa wa kodi, kodi inatakiwa isizidi mapato ya watu, hakuna mtu atakayekubali kulipa kodi kubwa inayozidi kile anachokipata. 3. Elimu kuhusu kodi, inawezekana watu hawaelewi chochote kuhusu kodi, hakuna mtu anayependa kulipia kitu pasipo kujua umuhimu au faida ya kitu hicho, wafanyabiashara ambao ndio walipa kodi wanatakiwa wapewe elimu kuhusu umuhimu wa kodi kwa nchi yetu. 4. Sera ya ulipaji kodi, ili ni tatizo kubwa kwa wananchi. Kama sera itataka kila biashara ilipe kodi lazima watu watakwepa kodi kwa sababu kuna baadhi ya biashara ni ndogo sana, zina kipato cha chini, kumlipisha kodi mfanyabiashara wa namna hiyo ni sawa na kumkandamiza. Sera inabidi iandae mfumo mzuri utakaoeleza ni biashara zipi zilipe kodi ili kila mtu ajue.

(Loveness alimaliza kusoma majibu ya Frank. Yaani ile anamaliza tu; darasa zima walipiga makofi. Hiyo ilionyesha kwamba Frank amejibu swali kwa usahihi, ukweli na uhakika. Sio wanachuo tu, hata mwalimu alianza kupiga makofi akimpongeza Frank. Aliyeteseka sio mwingine bali ni Love! alinunaje, alinuna hadi mishipa ya hasira ilisimama, nusura aote mapembe)

MWALIMU: Safi sana Frank, safi sanaa!! Hayo ndo majibu sasa.
Frank alitabasam kwa furaha. Lakini upande wa pili hali ya Love ilikua ndivyo sivyo, alichukia vibaya mno, hasira zilipanda hadi kwenye kope, alitamani atafune watu. Haiwezekani yeye hasipigiwe makofi alafu Frank apigiwe, ndo nini sasa kama sio manyanyaso na ukatili wa kijinsia. Wanachuo wakiwa wanafurahi; mara Love alitupa chini mtihani wa Frank kisha alipiga hatua alielekea nje ya darasa!! Weuweee!! Badamu batamwagika mwaka huu.

SEHEMU YA 09

Watu waliacha kupiga kelele, walitulia wakimshangaa Love ambaye alikuwa akiondoka. Hata mwalimu alishangaa, Frank nae aliwanda! Kabla Love hajatoka nje mara alisikia akiitwa na mwalimu:

MWALIMU: Loveness bado hatujamaliza, ebu rudi hapa haraka.
Ni kwa vile tu aliitwa na mwalimu, la sivyo hasingesimama. Kwa hasira Love aligeuka kisha alirudi tena stejini, safari hii hakukaa karibu na Frank, aliamua kujitenga; alikaa mbali kabisa, tena hakutaka kumtazama mtu)

MWALIMU: Wanafunzi naruhusu maswali marine tu. Mawili kwa Loveness na mawili kwa Frank.
(Baada ya mwalimu kuruhusu maswali, Issa alionekana kufurahi sana.)

MARIA: We naye vipi mbona unafurahi sana?

ISSA: Acha tu nina hasira na huyo Frank, haiwezekani kila siku anamuumiza Loveness

MARIA: Kwahyo unatakaje?

ISSA: Subiri, swali nitakalomtandika labda aje kusaidiwa na malaika (aliongea kwa şifa). (Bila kupepesa macho Issa alinyosha mkono, mwalimu alitoa ruhusa kwa Issa; alimruhusu aulize swali)

ISSA: Swali langu ni fupi tu na nataka nijibiwe na Frank, "kama kila mtu akiipenda biashara atafanikiwa, naomba unitajie biashara tano ambazo mtu akifanya hawezi kupata hasara"

WANACHUO: Mmmh! (wanachuo waliguna baaada ya kusikia swali ambalo lilikuwa nje ya mada) (Frank alilisikia swali vizuri sana, lakini alishangaa kuona swali lipo nje ya somo la siku hiyo. Hata hivyo ha kuta ka kuogopa, alifikiria kwa sekunde chache kisha alijibu kama ifuatavyo)

FRANK: Siku zote ukipenda unachofanya ni lazima kitakupa unachotaka. Hivyo basi hata biashara ukiipenda lazima itakupa mafanikio. Kuna biashara nyingi mtu anaweza akafanya na zikampa faida lakini kumbuka hata mwizi anapenda kuiba lakini sio kila anapatoka kuiba huwa anafanikiwa. Msaanii anapenda sana kazi yake lakini sio kila akitoa nyimbo itafanya vizuri., hivyo hivyo katika biashara. Siku zote biashara haina hasara ila hasara ni matokeo ya biashara. Na katika biashara ukiona unachokifanya hakikupi changamoto ujue hicho kitu sio sahihi kwako. Lazima uipende hasara ili ikukumbushe faida.

Je wewe unataka kusema tangu uanze kusoma hadi leo hujawai küfeli somo hata moja? na unadhani waliofeli wote walikua hawapendi kujisomea? Pia unadhani küfeli shule ndio kuwa maskini? Hapanaü Küfeli ni ukumbusho wa kuongeza bidi. Waliofeli masomo walikumbushwa umuhimu wa kufaulu; walitakiwa kubadilika ili wapate wanachokitaka. Alafu fikiria kidogo, kama kungekua hakuna hasara; nani angekua maskini? hata hao matajiri wenyewe wanapata hasara na ndio maana wanahangika kutafuta faida. Hivyo basi HAKUNA BIASHARA ISIYO NA HASARA İLA DHUMUNI KUU LA KUFANYA BIASHARA Nl KUPATA FAİDA, CHA MSINGI Nl KUCHEZA SALAMA.

(Baada ya Frank kumaliza kuongea; wanachuo kwa mara nyingine walipiga kelele na m a kof i kama yote, Hata Loveness mwenyewe alishangaa, alijiiuliza huyu Frank wa namna gani? kila kitu anajua tu. Issa alikasirika sana kuona swali lake limejibiwa kirahisi, alijua mipango yake imeharibika.)

MWALIMU: (akifurahi) Wanafunzi naombeni
utulivu. Sidhani kama kuna haja ya maswali tena, na kutokana na majibu mazuri ya Frank hata kipindi changu kitaishia hapa. Swali la Issa lilikua nje ya somo letu lakini nimeshangaa sana jinsi lilivyojibiwa, ebu tumpigie tena makofi...
(Watu waligonga meza kama bungeni vile, ni raha tupu yani)

MWALIMU: Frank na Loveness mnaweza kurudi kwenye viti vyenu, na tutaonana tena katika kipindi kijacho, kwaherini (mwalimu aliondoka). (Kipindi ndo kiliisha hivyo. Wanachuo walianza kusambaratika, baadhi walimpitia Frank walimpa pongezi, wengi waliinjoy sana. Licha ya wengi kufurahi lakini Issa alikasirika vibaya mno, alielekea hosteli akiwa mwenye hasira kali. Love yeye licha ya kukasirika lakini angalau aliyaelewa majibu ya Frank, bado aliyatafakari kichwani. Taratibu alipiga hatua alimfuata Happy ambaye wanakaa chumba kimoja, kabla hajamfikia alishtuka kumuona Happy akiongea na Frank) "Sasa huyu Happy ameanza lini mazoea na Frank? au nae ameanza kujishaua" Love aliwaza akiwa ameganda, bado aliwatazama Frank na Happy.

LOVENESS: We Happy fanya haraka twende! (Aliongea kwa sauti kali akiwa amechukia kwelikweli) HAPPY: Nakuja Love, nisubiri kidogo! (aliongea akiwa anasimama). Happy kabla hajaondoka; kwa siri sana alificha kikaratasi fulani ndani ya daftari la Frank kisha aliaga aliondoka, yeye na Love walielekea hosteli. Frank pasipo kutambua lolote alikusanya madaftari yake aliyaweka kwenye begi kisha nae alipiga hatua alielekea hosteli.

HOSTELI: Issa akiwa hosteli alionekana kukasirika mno, alichukua simu yake; kuna namba alionekana kuitafuta, baada ya kuipata alipiga, simu iliita kisha ilipokelewa.

ISSA: Hallo!...Oyaa huku kumeharibika tena, eeh jamaa şifa zile zile, sasa tunafanyaje au we unaona fresh tuu?... ndo hapo sasa mi mwenyewe ningekuwa na uwezo wa kumuondoa chuo mbona saizi tungekua tushamsahau.... Sasa sikiliza; week ijayo si kuna pepa? basi tufanye kitu, tuhakikishe yeye ndo anakuwa wa mwisho darasa zima. Alafu unajua mchongo tuanze vipi?.... tuanze na kile kibegi chake cha daftari maana jamaa huwa anapenda sana kuandika, anategemea sana zile daftari zake... eeh kaka huu mchezo tufanye mapema... poa poa mzee baba.

Issa alimaliza kuongea kwenye simu, alijisifia akijiona mwamba wa juu kusini, alijiona gaidi zaidi ya Idd Amin! Sie yetu macho, wacha tuone itakavyokuwa.
****
Frank alifika hosteli aliweka begi mezani kisha alijitupa kwenye godoro. Alitaka alale kidogo lakini hakulala, ni kama kuna kitu alikumbuka vile;

"Ooh wiki ijayo nina pepa la uchumi alafu eti nataka kulala, kwa raha zipi?" alijisemea akitoka kitandani, alisogea mezani. Alitoa daftari la uchumi kisha alianza kulipitia, alionekana kama kuna kitu anatafuta.

"Mbona zile notes sizioni, au sio daftari hili?" alivuta begi alichomoa daftari nyingine kisha aliendelea kukagua notes. Sasa akiwa anaendelea kukagua mara paap alikutana na kikaratasi flani kikiwa kimekunjwa, alikichukua kisha alikikunjua, alikuta kimeandikwa hivi; "Nimependa sana jinsi ulivyojibu lile swali, nilishindwa kusema lolote mule ndani, hongera sana, nakuomba nitafute kupitia namba 0123456789 ni muhimu sana, ni mimi Happy"

Frank alimaliza kusoma ujumbe wa kwenye karatasi, hata hivyo bado hakujua huyo Happy ni yupi, aliichukua ile namba aliisave kwenye simu yake akitaka kumtafuta baadae. Muda huo aliutumia kwa kusoma kwanza.
***

SEHEMU YA 10

llikua ni mida ya jioni hivi, Happy akiwa kitandani alikuwa akijigeuzageuza tu; Mara alale kifudifudi, mara chali, kuna muda alijiongelesha mwenyewe kama kichaa vile;

"Mh! mbona hanipigii au bado hajaipata ile karatasi? au kaamua kuipotezea tu, ningejua ningemuomba namba yake maana natamani kama nipae hivi jamani" Aliwaza akiwa anajilamba lips zake. Sasa akiwa anaendelea kuteseka kimawazo mara simu yake iliita, alitoa tabasam kisha aliamka haraka akijua lazima kapigiwa na Frank. Akichukua simu kisha alitazama juu ya kioo, alinyong’onyea mara baada ya kukuta kapigiwa na Love.

"Huyu nae vipi? sijui anataka nini.. Sasa sipokei" Alitupa simu pembeni kisha alilala kitandani akiwa amekasirika. Kwa mara nyingine simu yake iliita, japo hakupenda ila alipokea.

LOVENESS: We Happy mbona hupokei simu?

HAPPY: Nilitoka alafu simu niliacha chumbani! (alidanganya)

LOVENESS: Vipi hatuendi kusoma darasani?

HAPPY: Tangulia tu mi nitakuja, saizi sina mzuka!

LOVENESS: Huna mzuka? Tangu lini huna mzuka? Twende basi!

HAPPY: Kweli tenaa, yani nimechoka hatari!

LOVENESS: Mh! sawa, kama utakuja utanikuta kwenye darasa letu lilelile. (Simu ilikatwa. Happy alifurahi kwa sababu alihisi kusumbuliwa tu, yeye mawazo yake yote yalikua kwa Frank, kuna muda alishuka chini ya godoro alipiga magoti kisha alisali kama ifuatavyo)

HAPPY: Eeh Mungu wangu hata sijielewi, ni ghafla tu nimejikuta napenda, nakuomba nifanyie miujiza yoyote ilimradi anipigie hata simu tu ili nisikie sauti yake, pia nakuomba ni (Kabla hajamaliza maombi mara alisikia simu yake ikiita, huwezi amini eti aliacha kusali kwaajili ya simu; Haraka haraka alisimama alichukua simu yake; alitazama juu ya kioo alikutana na namba ngeni, moyoni alisali kimya kimya; "Eeh Mungu wangu nimepigiwa na namba ngeni, naomba maombi yangu yatimie” Baada ya maombi hayo alipokea simu kisha aliongea;)

HAPPY: Hello, nani?
FRANK: Frank hapa,
HAPPY: Frank? Frank yupi? Kakolanya au?
FRANK: Yeah!

(Moyo wa Happy nusura ukurupuke upae juu, kabinti ka watu kalivurugwa. Kutokana na plesha alishindwa kusimama, alijilaza kitandani ili ainjoy zaidi, raha ambazo alizipata hata yeye mwenyewe alishindwa kuzielezea. Kama kupatwa tu basi alipatwa)

HAPPY: Frank, nambie mzima lakini? (alilegeza sauti, upole kama wote, kulegea kama kote)

FRANK: Yah! mi niko poa tu sijui wewe, ila sijakufahamu bado.

HAPPY: Mi ni Happy, tulikaa wote kwenye kipindi cha uchumi.

FRANK: Aah! nishakukumbuka, vipi kwema?

HAPPY: Ndiyo kwema, ila... eeh! kwemaa! (aliongea
kwa kubabaika)

FRANK: Vipi mbona hivyo, kama kuna shida nambie tu!

HAPPY: Ni kweli nina shida. Naomba uje unielekeze uchumi kuna vitu sivielewi kabisa.

FRANK: Sawa haina tatizo, upo wapi?

HAPPY: Nipo hosteli, chumba namba 43. (aliongea kimitego akiwa anajaribu bahati yake).

FRANK: Mh! sitoweza kuja hosteli kwenu, labda twende darasani!

HAPPY: Hata mimi nilitamani twende darasani, ila najisikia homa kwa mbali ndio maana nimeona bora nisome chumbani! (aliongea kwa kudeka)

FRANK: Duh! kwahyo sasa tunafanyaje? Mi huko siwezi kuja, nisamehe tu.

HAPPY: Mmh! kwani wewe upo wapi?

FRANK: Nipo hosteli nasoma!

HAPPY: Upo na nani?

FRANK: Nipo mwenyewe.

HAPPY: (Akiwa anatabasam) Basi mimi nije huko kwako, unaonaje?

FRANK: (Alifikiria kwa sekunde chache kisha alijibu) Poa njoo, nipo chumba namba 108.
(Simu ilikatwa, hata hivyo Frank kuna kitu aliwaza) "Si amesema anaumwa, amekataa kwenda darasani kisa anaumwa, sasa amepata wapi nguvu za kuja huku? Na ukicheki ni rahisi kwenda darasani kuliko kuja huku. Hawa dada zetu wana shida kweli, na usikute anatania tu, hawezi kuja" Wakati Frank akiendelea kuwaza mara alisikia mlango ukigongwa, alisikilizia kidogo kisha alisimama alienda kufungua; yaani ile anafungua tu alishtuka kukutana na mrembo wa nguvu, mtoto alipendeza kuanzia kwenye ukucha hadi kwenye unywele! Patamu hapoo.

ITAENDELEA
 
SEASON 01

TAMTHILIA: MTU ALIYETHIBITISHWA KWA MAISHA YANGU
CERTIFIED PERSON OF MY LIFE (CPL)
( 11-15)

WHATSAPP 0768315707

SEHEMU YA 11

Frank na Happy walibaki wanatazamana tu, Happy alitabasam. Macho ya Frank yalikuwa yakikagua umbo na mavazi ya Happy ambaye chini alivaa sketi nyekundu alafu juu apiga kinguo kifupi cheupe, mtoto mguu wa bia, umbo namba 8, shepu ilitanuka, kiuno kilibinuka alafu kifua kilipambwa na viembe sindano! Viembe vilichomoza bwana weee!
HAPPY: Vipi? (alimuuliza Frank ambaye aliganda)
FRANK: (Alishtuka kidogo) Safi, karibu sanaa, karibu ndani.
HAPPY: Asante nishakaribia.
(Walizama ndani, licha ya kwamba kulikuwa kuna viti lakini Happy alienda kukaa juu ya godoro. Frank alivuta viti alivisogeza mezani kwaajili ya kujisomea. Baada ya kutengeneza mazingira ya kusoma alimkaribisha mgeni)
FRANK: Happy?
HAPPY: Abee!
FRANK: Karibu ukae kwenye kiti ili tuanze kusoma, au sio?
HAPPY: Sawa! hakuna tatizo.
(Happy alionekana kama hakupenda kutolewa kwenye godoro, alilaani sana uwepo wa viti. Kinyonge alikaa kwenye kiti kimoja, Frank nae alikaa kwenye kiti kingine kisha walianza kama ifuatavyo) FRANK: Ni sehemu ipi unataka nikulekeze?
HAPPY: Naomba unielekeze kuhusu tabia za wateja katika biashara.
FRANK: Sawa! vipi umekuja na daftari lolote?
HAPPY: Aah! hapana, samahani nimesahau.
FRANK: Sawa usijali, nitatumia langu alafu utaenda kukopi.
HAPPY: Sawa, asante sana!
(Frank alivuta begi lake kisha alitoa daftari mpya ambalo halikuandikwa kitu zaidi ya jina tu, aliweka daftari hilo mezani kisha alianza kushusha pindi kama ifuatavyo)
FRANK: Ukiondoa bidhaa wanafuata wateja, Wateja ndio kitu cha kwanza na chamsingi katika biashara. Hapa namaanisha ili uwe mfanyabiashara lazima ujue utafanya biashara gani, mfano kama kuuza utauza bidhaa gani, ukishafahamu bidhaa yako hatua inayofuata ni kutafuta wateja. Wahenga zamani walisema "kizuri chajiuza kibaya chajitembeza” hapa walimaanisha ukiuza bidhaa nzuri wateja watakufuata wenyewe. Na msemo huu huwa unatumika sana pale ambapo watu wengi wanauza biashara ya namna moja (inayofanana). Ikitokea bidhaa zikawa zinafanana hata kama zote ziwe bora, mt eja atachagua kule kwenye kizuri. HAPPY: Sasa uzuri huo wa bidhaa ni upi?
FRANK: Bei nzuri, uwingi, usafi, lugha nzuri na mengineyo. Watu wengi wanauza bidhaa bora ila tatizo ni kwamba unaweza ukauza bidhaa bora alafu kum be ina bei m baya, au kumbe una lugha chafu, hakuna mteja atakayekufuata. Mtu unaweza ukawa na bidhaa bora lakini usipozipa matangazo, punguzo n.k hutoweza kupata wateja. Wateja wao wanafuata kule kutakakowapa motisha, kule ambako kile wanachokilipa kitafanana na kile wanachokipata (fedha zao wanazolipa zifanane na thamani ya bidhaa wanazonunua). Mteja lazima aridhike, wateja wanapenda sana kuchagua, hivyo basi ni muhimu mfanya biashara awe na bidhaa mchanganyiko ili mteja achague anachokitaka. Tabia za wateja zinatokana na matendo yao; kuna wale waongeaji; wao wakija dukani kwako mara ashike hiki, mara akuambie hivi mara vile, yaani hapakaliki. Pia kuna wengine hawajui kabisa kuongea, wao wakifika dukani kwako watasimama tu wakicheki bidhaa pasipo kuongea neno lolote, na wakiona huwaongeleshi wanaweza wakaondoka. Kuna wateja wana hasira, wengine wana uvumilivu, wapo ambao ni rahisi kuwaridhisha lakini wengine hata ufanyaje huwa hawaridhiki; watakulaumu kuwa unapunja, una bei kubwa, mara hivi mara vile, hizo ndizo tabia zao. Na ndio maana inashauriwa kutambua tabia ya mteja kabla hujamuhudumia. Vipi unanielewa Happy?

SEHEMU YA 12


HAPPY: (Akifurahi) Yeah nakuelewa sanaa, tena sanaa.
(Walitulia kidogo wakitazamana. Ukweli ni kwamba lengo la Happy halikuwa kufundishwa, yeye kuna kitu alikuwa anakitaka. Lakini kutokana na mafunzo mazuri kutoka kwa Frank; bidada alijikuta amenogewa kabisa, ushawishi wa Frank katika kusoma ulifanya Happy atulie na asahau mambo mengine, alijiona yupo katika mikono salama, aliburudika kuanzia kwenye mapafu hadi moyoni) HAPPY: Naamini pepa haitotoka nje ya hapa?
FRANK: Ni kweli ila usisahau kusoma mada zingine! HAPPY: Sawa! Ila nimechoka kusoma, natamani kama nilale kidogo alafu tuendelee tena; au unasemaje?
(Frank alitazama saa alikuta ni saa mbili usiku, alishtuka kidogo kwa sababu muda ulikwenda sana) FRANK: Mi naona tuishie hapa kwa leo, kwakuwa pepa ni wiki ijayo nadhani kesho tutaendelea.
HAPPY: Sawa Frank, asante sana. Naomba nikuache. FRANK: Sawa tutawasiliana.
(Happy aliondoka ila moyoni alianza kuteseka, kuna kitu alikihitaji ila kuongea ndio ishu. Hata hivyo alijiapiza kuwa ni lazima akipate kitu hicho. Alipiga hatua hadi kwenye geti la nje la hosteli hiyo, akiwa anatoka nje mlangoni alipishana na Issa. Kwakuwa hawana mazoea walipishana tu. Hata hivyo Issa ni kama alihisi kitu)
"Huyu demu ni rafiki wa Love, sijawahi kumuona akiingia humu ndani kwetu, sasa leo anatokea chumba gani? alienda kwa nani? au kuna muhuni anakula mzigo? Mh!" Issa aliwaza sana ila hakupata jibu. Alipiga mwendo alielekea room kwa rafiki yake Meshack, alimkuta akicheza game kwenye laptop.
ISSA: Kaka vipi?
MESHACK: Fresh inakuaje?
ISSA: Nimekuja ili tukamilishe ule mchongo.
MESHACK: Aah! kuhusu yule mpenda sifa au sio?
ISSA: Huyo huyo, silipendi lijamaa lile!
MESHACK: Basi fresh, ni rahisi tu; itabidi tutengeneze swali la uongo alafu tunamtumia jamaa tukimsisitiza kuwa hilo ndilo swali litakalotoka kwenye mtihani, we mwenyewe unajua hakuna asiyependa nondo, akitumiwa na watu wanne ataamini tu.
ISSA: (Akiwa na wasiwasi) Mh mbona naona kama ngumu, sasa si atauliza watu wengine kama nao wamelipata?
MESHACK: Hawezi. Akishapewa swali atahangaika kulisoma hilo hilo moja alafu siku ya pepa atakutana na swali tofauti; hapo ndipo ataimba ndombolo yasoloü
ISSA: Nimekupata, ila si itabidi tunaanza na lile begi lake au vipi?
MESHACK: Lile begi ni faşta tu, tunamvizia muda akienda kuoga, tena akishaibiwa begi lazima atachanganyikiwa, atakuwa hana notes za kusoma, hapo sasa lazima atalisoma swali letu la uongo ambalo tutamtumia. Huyu dawa yake ni kumpumbaza kiakili, hasiwaze vitu vingine zaidi ya swali letu la uongo tu.
ISSA: Mwanangu ebu nipetano
(Waligonga tano kisha walichekelea wakijua dili limekamilika)
Siku zilipita na hatimaye ikaja jumamosi. Mida ya asubuhi wanachuo wengi walikuwa bize wakijisomea. Wengine vimbwetani, wengine madarasani na wengine hosteli vyumbani. Zilibaki siku mbili wanachuo wa kozi ya biashara waingie kwenye test ya uchumi. Loveness alikua chumbani kwake pamoja na Happy wakijisomea. Kila mmoja alikua bize na daftari lake. Happy alikua akisoma huku akimuwaza Frank, kuna muda alitabasam, na kuna muda alicheka kabisa.
LOVENESS: We unachekacheka nini?
HAPPY: Hakuna, basi tu.
LOVENESS: Mmh! alafu mwenzangu siku mbili hizi hata sikuelewi, umepata mume nini? (aliuliza akiwa anatabasam)
HAPPY: Yaani ningempata mbona ningefurahi sana!
LOVENESS: Ungempata nani?
HAPPY: Si huyo mume.
LOVENESS: Ni nani huyo nisiyemjua?
HAPPY: Nakutania mwaya!
LOVENESS: Mmh! sawa. Sasa kuna hiki kiswali naomba unielekeze kama unakijua.
HAPPY: Kipi hicho?
LOVE: Kinauliza hivi; Elezea tabia za wateja katika biashara.
(Happy baada ya kusikia swali hilo alitabasam sana, alicheka hadi alipaliwa, alifurahi kwa sababu swali hilo alifundishwa na Frank. Aliona huo ndio muda wa kumuonyesha Love kuwa amekwiva. Walikaa mezani, Happy alianza kushuka vitu vya ajabu, alimpeleka Love kushoto kisha alimrudisha kulia, kuna muda alimchukua alimuweka waah!)
LOVENESS: We Happy hayo mambo yote umeyajulia wapi?
HAPPY: Ni kujisomea tu (aliongea kwa maringo)
LOVENESS: We kwenda zako; muda wote tunakuaga wote, kujisomea huko kwio?
HAPPY: Ndo hivyo, au hujaelewa nirudie?
LOVENESS: Yaani sijawai kukuelewa vizuri kama leo. Mwenzio bado sikupatii picha, hayo maakili umeyatoa wapi wewee jamani!!
Happy alibaki anachekelea tu, aliinjoy hadi sio powa! licha ya kujua wapi amepata akili lakini hakutaka kumtaja Frank.
Upande wa pili Frank alichelewa kuamka, aliamka saa 3 asubuhi, kwanza alimshukuru Mungu kwa kuiona siku mpya kisha alivuta taulo alivaa, alichukua mswaki na ndoo alielekea bafuni. Alipiga mswaki, alioga kisha alirudi chumbani, alitembea pasipo wasiwasi wowote, wala hakuwa na shaka, alizama ndani ya chumba chake, alijiandaa kwaajili ya kwenda darasani kujisomea. Baada ya kujiandaa alitazama mahali ambako huwa anaweka begi lake, alishtuka kuona begi halipo! Alikodoa macho akiwa anashangaa, hapo ndo penyewe sasa!
SEHEMU YA 13

Hata hivyo alituliza kichwa kisha alianza kulitafuta begi lake, alitazama kwenye kabati la nguo, uvunguni mwa kitanda, alipita kwenye kona zote, kwenye chaga, alitandua mashuka na manguo, alivuruga chumba kizima lakini hakuliona begi;
FRANK: Lakini si nililiweka hapa ukutani? Sasa mbona kila sehemu halipo? kwamba alichukua Happy? Lakini hapana; Happy aliondoka na daftari langu tu, kwanza aondoke na begi langu la nini?... alafu mbona muda nimeenda kuoga nililiacha hapa ukutani? au kuna mtu anayenijua kalichukua, lakini mbona sina mazoea na mtu yeyote?.... Kama ni hivyo ni bora nisiende kusoma, nikasome nini sasa? si bora nilale labda begi langu litarudi.
(Kwa hasira ya kukosa begi aliamua kujitupa kitandani, alichukia kwelikweli, mara simu yake iliita, alitazama alikuta amepigiwa na Happy; alipokea kisha aliongea)
HAPPY: Hallow Frank!
FRANK: Hello, vipi mzima?
HAPPY: Mi mzima, hofu kwako!
FRANK: Mi niko fresh.
HAPPY: Ulisema leo tutaendelea kusoma, vipi nije au? (Frank alifikiria kidogo, kutokana na kuibiwa begi alikosa hamu ya kusoma; aliona bora aendelee kulala tu)
FRANK: Samahani Happy Siwezi kwenda kusoma kwa sasa, labda badae.
HAPPY: Kwanini lakini?twende bwanaa!
FRANK: Nisamehe tu! we nenda tutaonana badae.
HAPPY: Kwani tatizo nini Frank?
FRANK: Sijisikii tu!
HAPPY: Mmh! poa bwana (alikubali kishingo upande).
(Simu ilikatwa, Frank aliendelea kulala. Akiwa amejilaza mara simu yake iliingia meseji, alisoma meseji hiyo alikuta imeandikwa hivi: "HII Nl SIRI YAKO, SWALI LA JUMATATU KWENYE MTIHANI WA UCHUMI Nl HILI " Elezea faida kuu 5 za benk kuu ya Tanzania ONYO: USISAMBAZE UJUMBE HUU WALA KU MPA MWENZIO TAARIFA KUHUSU SWALI HILI, KILA MTU AMEPEWA. FANYA HIVYO KWA USALAMA WAKO NA WETU". Frank baada ya kusoma swali hilo aliinuka haraka akiwa anatabasam, hakuamini hata kidogo) "Mmh watu wana hatari hadi wamelipata swali la mtihani. Alafu kama swali lenyewe ndio hili siwezi küfeli, tena sina haja ya kwenda darsani, wacha nilipitie muda huu nilitafutie majibu kisha niendelee kulala." Aliwaza, alizungusha macho ndani ya chumba chake aliona kidaftari flani ambacho huwa hakitumii, alienda kukiokota kisha alikaa mezani, alitafuta majibu ya swali hilo kisha aliyapata, majibu yalikuwa kama ifuatavyo;
"Faida kuu 5 za benki kuu ya Tanzania, 1. Chanzo kikuu cha usambazaji wa pesa za nchi (sarafu na noti). 2. Inatunza pesa za benki zingine. Mfano benki kama NBC, crdb, nmb, zinaweka pesa zao kwenye benki kuu ya Tanzania. 3. Inatunza mapato ya nchi na Inashauri nchi kuhusu mambo ya uchumi, mfano kupitia sera za uchumi benki kuu inashauri nchi ifanyeje kuhusiana na kupanda au kushuka kwa uchumi. 4. Inatoa misaada kwa benki zingine mfano inatoa ushauri kuhusiana na umiliki wa fedha na vitendea kazi. 5. Benki kuu ni kama kiongozi, inaongoza mfumo mzima wa mzunguko wa pesa pamoja na kuongoza benki zingine zote katika nchi husika."
(Frank alimaliza kulijadili swali hilo, tayari alipata majibu ya swali, aliweka kidaftari pembeni kisha kwa mara nyingine alirudi kitandani alilala. Sasa akiwa kitandani mara alisikia mlango ukigongwa. Alisimama alienda kufungua, alikutana na Issa akiwa na Meshack, wahuni hao walizama ndani)

SEHEMU YA 14


ISSA: Kaka niaje?
FRANK: Fresh (alijibu kwa wasiwasi)
ISSA: Kaka samahani bwana kwa usumbufu...
FRANK: Haina shida, kuna nini?
ISSA: Kuna kiswali tumetumiwa japo tumeambiwa iwe siri lakini tumeona tuje kupata uhakika, ni swali la uchumi la juma tatu, vipi na wewe umelipata au ni sisi tu?
(Frank alifurahi baada ya kusikia hivyo, hapo sasa aliamini kuwa swali hilo ni la kweli na ndio maana limetumwa kwa wanachuo wengi)
FRANK: Eeh! nimelipata, kumbe hata nyie mnalo? mi nikajua mambo ya kudanganyana tena.
ISSA: Tumelipata. Hata hvyo tunaomba kama unafahamu majibu yake tupatie maana ili lazima litatoka tu, limekaa vizuri sana! (alisisitiza).
FRANK: Majibu ninayo, mimi baada ya kulipata tu sikuliacha; nilipambana nalo mapema sana (alienda mezani alichukua kidaftari chenye majibu alimkabidhi Issa)
ISSA: Kumbe haya ndiyo majibu yake?
FRANK: Eeh! si alisema point 5? hizo hapo!
ISSA: Asante sana, aisee nashukuru; sasa ni mwendo wa kulala tu, hakuna kusoma tena, au we mwenzetu utasoma?
FRANK: Weekend hii nisome nini wakati swali nishalipata, nami ni kulala tu.
ISSA: Ah ah ah! ndio hivyo, ngoja nipige picha haya majibu yako.
(Issa alichukua simu alijidai kupiga picha majibu ya
Frank. Baada ya kupata majibu waliaga kisha waliondoka, walifika room kwao kisha waligonga tano wakiwa wanachekelea)
MESHACK: Si nilikuambia, yule dawa yake ndogo tuu na pale hawezi kusoma tena maana daftari hana, pia lile swali limempa ukichaa
ISSA: Kaka nimekukubali! We nomaa!
MESHACK: Imeisha hiyoooo!
(Wao tayari waliharibu. Kule kwa Frank jamaa alirudi tena kitandani, alilala akiwa anachekelea muda wote) FRANK: Kumbe ni kweli, mi nilijua ni swali la uongo, hapa ni kulala hadi mchana muda wa kula, nikila tena nalala, nina shida gani wakati majibu ninayo.
****
Mida ya jioni Happy na Love walikua chumbani wamelala. Ghafla Happy aliamka, alimtazama Love alimuona bado kalala. Hakuwa na mpango naye, alielekea bafuni alioga kisha alijiandaa vizuri; alivaa mavazi bomba, mtoto alinoga kuanzia mbele hadi nyuma, alivaa pamba ambazo hata kipofu ni lazima ageuke nyuma. Alijipulizia unyunyu wa nguvu kisha alisimama kwenye kioo kirefu alijitazama;
"Ila Mimi ni mzuri jamani, Asante Mungu umenipa kila kitu kasoro huyu mwanaume ninayemtaka. Hata kama amekataa kwenda kusoma ni bora niende huko huko; la kuwa na liwe. Yaani leo afe Manula afe Mwamnyeto; ni lazima nikapate nikitakacho” aliwaza akiwa anajigeuzageuza mbele ya kioo. Alichukua mkoba wake kisha alipiga hatua akiondoka, alishika kitasa kisha alikinyonga; kabla hajatoka nje alishtushwa na sauti ya Love.
LOVE: We Happy unaenda wapi?
HAPPY: (Aliganda mlangoni kisha aligeuka alijibu) Nafika hapo dukani, narudi hivi punde!
LOVE: Dukani ndo ujipambe hivyo jamani? alafu mbona sikuhizi una mambo ya siri sana?
HAPPY: Jamani nisamehe sijakuaga, nilijua umelala!. Ila ndio hivyo nafika hapo dukani.
LOVE: Mh! basi sawa, we nifiche tu
Love aliendelea kulala, Happy alifikiria kwa sekunde chache kisha alisonga mbele, alielekea mahali husika akitaka kwenda kukamilisha jambo lake.
****

SEHEMU YA 15


NJEYAHOSTELI
Issa na Meshack walikaa nje ya hosteli kwenye gogo, walikuwa wakifurahi mara baada ya kukamilisha dili lao;
ISSA: Ila jamaa tumemuweza sana!
MESHACK: Na bado, yule hadi tuhakikishe zile sifa zote zinaisha.
ISSA: Kabisa kaka, haiwezekani kila swali analiweza yeye tu; wengine wakijibu wanaonekana waharibifu.
MESHACK: Oya Issa ebu mcheki yule demu...Muone anazama hosteli kwetu...Yule si ndo rafiki wa Love au siyo?
ISSA: (Atazama mlangoni) Ndo mwenyewe huyo; sasa leo ngoja tukamshuhudie tuone anaingia chumba gani, twenzetu chapu!
(Faşta walikimbia walizama ndani, walianza kumfuatilia Happy, walishtuka kuona akiingia ndani ya chumba cha Frank.)
ISSA: Hivi ni kweli au haya macho yangu yamezeeka? MESHACK: Unajua nini? yule jamaa kuna vitu anatumia.
ISSA: Inawezekana ni mshirikina. Jamani bora hata ya Mimi ni handsome kuliko yule mwehu. Imekuaje apate pisi kali kama ile? jamaa lazima kuna kitu anatumia, haiwezekani darasani yeye, hata mademu? MESHACK: Ndio hivyo, yule jamaa sio poa.
(Kule ndani Happy baada ya kuzama ndani alikaribishwa kwenye kiti, Frank bado alilala kitandani)
HAPPY: Vipi Frank mbona niligonga sana mlango?
FRANK: Dah! Samahani, nilikua nimelala. Vipi mzima lakini?
HAPPY: Ndiyo mi mzima. Wewe vipi?
FRANK: Mimi pia niko poa, vipi mbona ghafla?
HAPPY: Niliii...natakaaa,... Kuna... (aliongea kwa kubabaika)
FRANK: Au kuna swali linakusumbua?
HAPPY: Hapana Frank, nimevumilia nimechoka; ukweli ni kwamba nahitaji kampani yako.
FRANK: Kampani ya kusoma? mbona Mimi leo sijisikii kusoma, sina mzuka kabisa yani.
(Happy aliona hajaeleweka. Taratibu alisimama kutoka kwenye kiti, alimfuata Frank kitandani, alikaa pembeni ya Frank; alimtazama usoni kisha alimuambia maneno yafuatayo)
HAPPY: Frank leo sijafika hapa kusoma wala kuelekezwa swali lolote..."

ITAENDELEA
 
SEASON 01

TAMTHILIA: MTU ALIYETHIBITISHWA KWA MAISHA YANGU
CERTIFIED PERSON OF MY LIFE (CPL)
( 16-20 )

WHATSAPP 0768315707

SEHEMU YA 16

Happy alionekana kuzidiwa sana na mapenzi, ha kuta ka kuchelewa; alinyosha mkono wake alishika bega la Frank, aliusogeza mdomo wake kuelekea mdomoni kwa Frank, mtoto wa kike aliomba rojorojo la mdomo, hata hivyo Frank alikwepesha mdomo wake!
FRANK: (akimshangaa Happy) Kwan i leo una nini leo? HAPPY: Mi leo nina mapenzi tu! (aliongea akiwa amezidiwa, macho legelege)
FRANK: Imekuaje mapenzi hayo yamekuja ghafla?
HAPPY: Hata mimi sijui, lakini sote tujajua kuwa mapenzi hayana taarifa.
FRANK: Unataka kusema kuwa hujitambui?
HAPPY: Nishakuambia kuwa sijui, sasa unataka nikuambie nini tena? Naomba nipe basi (aliongea kwa macho ya huruma)
FRANK: Ingekua ni wewe ungeweza kumpa yeyote anayetaka umpe?
(Happy hakujibu swali hilo, alikaa kimya na alionekana akilia kwa uchungu na kwikwi. Hakujua afanyeje, kwa upande wake aliona kama anateswa kimapenzi na mtu ampendae.)
FRANK: Usilie basi! wewe ni binti mzuri. Naamini kwa nafasi hii mwanaume mwingine hasingekuuliza maswali mengi, kwanza hasingekuuliza chochote; angeamua kukupa tu. Wanaume wengi huwa wanahitaji nafasi kama hii ambayo mimi naichukulia kawaida. Hata hivyo usijali, ni jambo dogo tu ambalo hujalifanya Happy, na hilo ndilo umelikosea!
HAPPY: (Akijitoa mikononi kwa Frank) Ni jambo lipi hilo Frank?
FRANK: Hujafuata sheria za mapenzi.!
HAPPY: Sijafuata sheria? Kwani mapenzi yana sheria gani? ebu niambie basi ili nizifuate.
FRANK: Nimekuuliza ikitokea mwanaume yeyote akaja chumbani kwako utampa?
HAPPY: Nisamehe Frank, lakini ni kwa sababu nakupenda, nakupenda sana.
FRANK: Basi fuata sheria za mapenzi ili ujue kama ulipopenda ni sahihi au sio sahihi.
HAPPY: Unamaanisha nini? mbona sikuelewi?
FRANK: Kwakuwa hukuja kusoma basi nakuomba uwe na nguvu za kusimama kisha urudi hosteli kwako.
Happy wala hakubisha, alijitafakari kwa sekunde chache kisha alisimama na kuondoka. Ndani ya kichwa chake aliwaza kuhusu sheria za mapenzi tu. ***
VIMBWETANI:
Usiku wa siku hiyo mida ya saa 2:30; Issa, Meshack na Maria walionekana wakisoma kwenye Kimbweta. Maria ndiye alikuwa akiwaelekeza wenzie, alikuwa akiwafundisha kujibu maswali mbalimbali;
ISSA: We maria mbona siku hizi una akili sana?
MARIA: (Alicheka kisha aliuliza) kwanini Issa?
ISSA: Hili swali lilinisumbua kwa wiki nzima; sasa wewe umeliwezaje?
MARIA: Ishi na watu usife njaa.
ISSA: Una maana gani?
MARIA: Kama hujaelewa utajiju.
MESHACK: Alafu jamani kuna hili swali, nahisi kama kes ho linaweza kutoka!
MARIA: Swali gani hilo? Ebu liweke mezani tulipige!
ISSA: Mh! Maria mbona umekuwa wamoto sana? we kila swali unalipiga tu
MARIA: Aha ha ah! acha kunifurahisha!
MESHACK: Swali lenyewe linasema hivi;" Kama ajira binafsi ni muhimu sana katika kukuza uchumi, je unaweza kutuambia faida kuu za kujiajiri?"
ISSA: Mmh! Kaka hilo swali umelitolea wapi? achana nalo bwana mwalimu hawezi kutoa maswali magumu kama hayo!.
MARIA: Issa acha uvivu wa kufikiri, unataka kusema ndani ya chumba cha mtihani swali hilo lingekushinda?


SEHEMU YA 17


ISSA: Asee lingenishinda kwa sababu nachojua mimi faida kubwa ya kujiajiri ni kupata pesa zako mwenyewe pekeako.
(Maria alicheka, hata Meshack alichekelea)
MARIA: Duuh! Issa bwanaa!
ISSA: Kwahiyo mnanicheka sio?
MARIA: Sio kukucheka, tumefurahi tu. Alafu kama hiyo ndo faida kubwa ebu tupatie faida ndogondogo. ISSA: Kujiajiri hakuna faida ndogondogo!
(Maria na Meshack walicheka tena, ilikuwa ni kama wanachekeshana ila ndo walikuwa wanasoma hivyo.) MARIA: Sikilizeni niwaambie; kujiajiri ndio maisha. Hata hao watu wakubwa serikalini wanachukua mishahara yao na kuileta huku mtaani kwa ajili ya biashara zao. Ndio maana unakuta waajiriwa wengi ni wafanyabiashara binafsi. Iko hivi, kujiajiri kuna faida nyingi sana kama vile 1. Unakuwa mfanyakazi huru, hakuna wa kukusumbua, wewe mwenyewe unafanya mikataba yoyote unayoitaka kwa sababu faida au hasara ni juu yako mwenyewe. 2. Unapata mapato makubwa; kwa mfano wewe Issa ukijiajiri kila faida utakayoipata ni yako tofauti na aliyeajiriwa; yeye anapewa kitu kidogo katika mapato. 3. Kujiajiri inasaidia kujua thamani ya fedha, Kama mjuavyo hakuna mtu anayeipenda fedha yake kama yule aliyejiajiri, mkitaka kuhakikisha nyie jiajirini tu. 4. İnasaidia kudhibiti matumizi ya pesa; mtu aliyejiajiri anajua vitu muhimu ambavyo ni muhimu kwa maisha yake, huwezi kumkuta anapoteza pesa kwa matumizi yasiyo ya lazima 5. Ukijiajiri unakua bosi na mmiliki wa biashara yako; hakuna wa kukusumbua ukiwa na kitu chako unachokimiliki. 6. Unafanya kazi bila plesha, tena unachagua ufanye kipi na uache kipi, mazingira ya kufanyia kazi unayachagua wewe mwenyewe. 7. Unaonekana mtu wa thamani na mwenye kujielewa, hata wewe mwenyewe utajikubali. 8. Unajitafutia wateja wako mwenyewe. Ziko faida nyingi, hizo ni chache tu. Hata hivyo kujiajiri nako kuna changamoto zake, mfano kulipa kodi na...
ISSA: Wee acha sifa, hujaambiwa tutaje na changamoto... Lakini wewe Maria mbona sikuhizi nakuona kama sio Maria yule wa zamani?
MARIA: (Akicheka) Kwani Maria wa zamani alikuaje? ISSA: Alikua mvivu wa kusoma na kufikiria.
MARIA: Ah aah aah! Na ndio maana nimekuambia kuwa "Ishi na watu husife njaa”
ISSA: Ni mtu gani huyo anayekupa hayo maakili?
MARIA: Ni Frank, huyo ndiyeticha wangu.
(Issa alinuna mara baada ya kulisikia jina la Frank, sio Issa tu; hata Meshack hakupenda)
MARIA: Vipi mbona mmebadilika ghafla?
ISSA: Au na wewe tayari?
MARIA: Tayari nini?
MESHACK: Itakuwa tayari kapitiwa na jamaa.
MARIA: (akishangaa) Mbona siwaelewi? jamaa gani?
ISSA: Si huyo mpenda sifa!
MARIA: Frank au?
ISSA: Sasa kuna mwingine?
MARIA: Frank kafanyaje?
ISSA: Happy si unamjua?
MARIA: Happy rafiki wa Love au?
ISSA: Huyohuyo! hivi yule dem nani anapiga?
MARIA: Sidhani kama ana mpenzi, kwanza alivyo mtu wa dini yule! Hivi mnajua kuwa yule mdada ni mlokole? Ameokoka!
ISSA: Kwahiyo walokole hawafanyi?
MARIA: Mi sijui.
ISSA: Kwa taarifa yako uyo mlokole wako na Frank mambo ni moto!
MARIA: Una maana gani?
MESHACK: Maria nawe upo kama mtoto! Sasa hapo husichoelewa ni kipi?... Frank anakula Happy, na hadi muda huu usikute bado wapo chumbani kwa Frank.
MARIA: Aah hapana! kwanza hiyo haiwezekani, Happy hawezi kuwa na ukaribu na Frank kwa sababu Happy ni rafiki wa Love, na ukicheki Love na Frank haziivi.
ISSA: Ndiyo maana tulikuuliza kuwa au na wewe tayari?
MARIA: Koma! Mimi na Frank tunaheshimiana, na mara nyingi huwa ananifundisha; kama kweli Happy ana ukaribu na Frank itakua ni kuhusu masomo tu. ISSA: Masomo chumbani? tena usiku? Kuna masomo hapo?
MARIA: Mi naondoka, tutaonana kesho kwenye pepa (alisimama na kuondoka)
ISSA: Imekuuma eeeh? Kumbe hata wewe, ila pole kama tumekukera!
Issa na Meshack walitazamana kisha walicheka kinafki, walifurahia mambo hayo ya kijinga! Aisee yajayo yanatekenya sana! sie yetu ni macho,wacha tuone itakavyokuwa.
HOSTELI:

SEHEMU YA 18


Mida ya saa 4 usiku Love alirudi hosteli akitokea darasani ambako alienda kujisomea. Baada ya kufika room alimkuta Happy kalala hovyohovyo! Paja moja kusini, paja jingine kaskazini; Alimfunika vizuri.
LOVE: Yaani huyu Happy angekuwa ni mlevi ningepata tabu humu ndani, kwa ulalaji huu si bora hata mlevi analalaga vizuri.
(Baada ya kuhakikisha rafiki yake kalala vizuri alibadili nguo alivaa kanga kisha alielekea bafuni, alioga kisha alirudi chumbani aliamua kulala. Sasa akiwa kitandani mara alimsikia Happy akiota, Happy aliota akisema; "Sheria za mapenzi, sheria zipi?". Love alikodoa macho, nae alivyo mbea aliamka kisha alikaa kitandani akimtazama Happy; alimuona kalala fofofo, pia kwa mara nyingine alimsikia akiota akisema "Sijafuata sheria za mapenzi")
LOVE: Mh! au mlokole kapenda? Alafu huyu Happy sikuhizi amezidisha sana mambo ya siri tofauti na zamani. Zamani kila kitu alikua ananiambia lakini sikuhizi haniambii kitu, anajidai amekua mkubwa; sasa ona anavyoweweseka! Ah ah ah! Jamani mapenzi haya yatauwa watu!
Love alicheka kirnya kimya, hakujua kuwa mwenzie alikuwa ndotoni akiwaza wapi atapata sheria za mapenzi ili akamilishe mchongo wake! Mweh jamani hii stori ni tamu sana!


LOVE: We Happy, Happy, Happy amkaa.... We ebu amka kwanza!
(Licha ya kumuamsha lakini mwenzie ndo kwanza alinyosha miguu juu kisha aligeukia upande wa pili; chezea usingizi wewe)
"Mh! Huyu nimuache alale, alafu sitomwambia chochote kuhusu hii mindoto yake; ila nitaanza kumfuatilia nijue nyendo na siri zake ambazo ananificha” Love aliwaza mara baada ya kuona Happy haamki. Nae alivuta shuka aliamua kutafuta usingizi.
****
Upande wa pili Issa na Meshack baada ya kutoka discussion walielekea room kwa Issa. Wao wanalala vyumba tofauti. Walizungumza stori kidogo kisha Meshack aliaga akitaka kwenda kulala;
MESHACK: Oya Issa mi wacha nikalale.
ISSA: Lakini kabla hujalala hivi unakumbuka lile swali tulilomtungia jamaa?
MESHACK: Eeh! limefanyaje?
ISSA: We unalijua lile?
MESHACK: Nilijue la nini? swali lenyewe la uongo, wacha nikalale Mimi!
ISSA: Hivi kwa mfano likitoka kweli, itakuaje? maana tumemtungia jamaa swali la uongo wakati sisi wenyewe hatulijui, si ujinga huo.
MESHACK: We mi niache nikalale, alafu si ulipiga picha yale majibu ya jamaa?
ISSA: Huwezi amini kwa dharau nilifuta yale majibu.
MESHACK: Bora ulifuta tu! kwani we una wasiwasi gani? swali lenyewe hatujui hata tulilitoa wapi, tulitunga tu ili kumfelisha jamaa, kwahiyo na wewe unataka küfeli?
ISSA: Ndo hapo sasa, mi nae nina mawenge. Swali la uongo nataka kulihangaikia. Kaka eeh usiku mwema. Baada ya kuagana kila mmoja alielekea kwake, hivyo ndivyo siku yao ilimalizika.

SEHEMU YA 19


SIKU ILIYOFUATA:
CHUMBACHA MTIHANI
Ni jumatatu sasa, mida ya saa mbili (8:00) asubuhi darasa lilijaa wanafunzi kama wote. Kama kawaida Frank alikaa mbele, Love na Happy walikaa katikati, Maria alijichanganya na watu hasiowazoea, Issa na Meshack walikaa nyuma ya darasa (back benchers). Darasa lilionekana kuwa na utulivu mkubwa, kila mtu aliwaza mawazo yake. Kuna ambao walikuwa wanakumbuka yale waliyojisomea, wengine walikuwa wanaona mtihani unachelewa kuanza, wengine kazi yao ilikuwa ni kutazama madem wenye misambwanda, pia kuna wadada ambao kazi yao ilikuwa ni kutazama wanaume waliovaa suti, na wengine hata haikufahamika wanawaza nini. Frank hakuwa na wasiwasi kwa sababu tayari alipewa swali ambalo aliambiwa kuwa litatoka kwenye mtihani huo, nae alivyo mjinga hakusoma kitu kingine chochote zaidi ya swali hilo tu, hakujua kuwa huo ni mtego ambao alipewa ili afeli. Love na Happy wao walianza kutengeneza mikakati yao ya kufaulu;
LOVE: Happy swali likinishinda nitakushtua, maana mwenzangu sikuhizi unajua vitu vingi.
HAPPY: Aha ha ha! Sawa, nami likinishinda nitakushtua.
LOVE: Inategemea na swali lenyewe, akili zenyewe sina; bora hata ya wewe sikuhizi umekuwa wa moto HAPPY: (akicheka) Ebu acha kunifurahisha! (Kule nyuma Issa na Meshack nao walikuwa wanajadiliana kimya kimya)
ISSA: Oyaa jamaa yako namuonea huruma sana, pale alipo sidhani kama amesoma.
MESHACK: Alivyo bwege anajua lile swali la uongo ndo litatoka, daadeq leo atapata tabu sana!
ISSA: Nitafurahi sana aklpata sifuri, nitaweka hadi sherehe!
(Mara msimamisi wa mtihani aliingla, aligawa karatasi za maswali na majibu kisha allanza kuongea kama ifuatavyo)
MSIMAMIZI: Kuna mtu hajapata karatasi ya maswali au majibu?
WANACHUO: Hakunaa
MSIMAMIZI: Hakikisha unafuata sheria za mtihani; sitaki kuona watu wanaigiliziana majibu! Nikikuona sijui nitakufanyaje, anza mtihani.
Issa ndiye alikua mtu wa kwanza kufungua karatasi ya maswali; alisoma instructions (miongozo) alikuta imeandikwa hivi; "Mtihani ni maswali mawili, Fanya maswali yote, muda ni saa 1, andika kwa usahihi na ukweli". Baada ya kumaliza kusoma muongozo alirukia kwenye maswali, weuwee! Hakuamini hata kidogo mara baada ya kukuta lile swali la uongo limetoka kwenye pepa. Jamaa alichanganyikiwa, alimtazama Meshack alimuona kavurugwa! Wote wawili hawakuamini hata kidogo. Frank alifurahi sana mara baada ya kukuta swali alilopewa limetoka kwenye mtihani. Swali la kwanza lilikuwa hivi "Elezea faida tano za benki kuu ya Tanzania". Alafu swali la pili lilikuwa "Elezea kwa upana tabia za wateja katika biashara''.
Love baada ya kuona maswali alitabasam kwa sababu swali la pili analifahamu, ni swali ambalo juzi
kati alielekezwa na Happy ambaye alielekezwa na Frank. Happy nae baada ya kutazama maswali alifurahi kisha alijisemea" Swali la pili nalijua, alafu hizi faida za benki kuu nitazifikiria na nitazipata tu". Kila mmoja alifanya kutokana na uwezo wake, baada ya saa 1 msimamizi alikusanya mitihani yake kisha aliondoka. Baada ya kumaliza mtihani Maria alianza kumtafuta Frank, alimuona akielekea hosteli;
MARIA: Frank! Frank! Frank!
FRANK: (aligeuka alimuona Maria) Naam, nambie
MARIA: Safi tu vipi pepa? (aliuliza kwa furaha)
FRANK: Pepa la kawaida, si umeona lile swali limetoka?
MARIA: We acha tu! yani kama husingenielekeza sijui ingekuwaje, asante sana.
FRANK: Usijali, ni vitu vya kawaida.
(Wakati Frank na Maria wakijadiliana kuhusu mtihani kumbe Happy nae alikuwa akimtafuta Frank ili amshukuru. Mbio za Happy ziliishia ukingoni mara baada ya kumshuhudia Frank akiongea na binti mwingine. Happy alichukia kwa sababu alitaka amshukuru Frank wakiwa wawili tu. Hata hivyo hakuumia sana, kwakuwa chumba cha Frank anakifahamu alipanga kwenda kumshukuru chumbani kwake. Maria na Frank wao bado waliendelea kuongea wakiwa wanatembea taratibu)
MARIA: Leo umenifurahisha sana.
FRANK: Kwa sababu ya kuotea maswali au?
MARIA: Ndiyo, nimeinjoy sana mtihani wa leo, nimetiririka kama maji! Tena leo ngoja nikupe ofa,
chakula cha mchana gharama zote juu yangu!
FRANK: Wacha wee! basi sawa asante sana, namba yako ninayo; nitakupigia.
Waliagana na kila mmoja aliondoka alielekea kwake, walikubaliana kukutana muda wa msosi ili wapeane ofa zao.
-k-k-k
HOSTELI:


SEHEMU YA 20


Love ndiye alianza kufika hosteli, akiwa mwenye furaha alijitupa kitandani kisha alitulia akimsubiri Happy. Mara mlango ulifunguliwa, Happy alizama ndani;
MARIA: (Akitabasam kwa furaha) Kwanini?
LOVENESS: Kwa kuotea maswali, hivi ulioteaje lile swali? ulilipata wapi? yani leo bila wewe mbona ningeumbuka!
HAPPY: Ah ah ah! we acha tu. Lile swali kuna sehemu nililichukua, tumshukuru Mungu kwa kila kitu.
LOVENESS: Amina mlokole wangu.
(Walitulia kwa muda, wote walikosa maneno, hata hivyo Love kuna kitu alikumbuka)
LOVENESS: Happy!
HAPPY: Abeee! (alishtuka kidogo japo sio sana)
LOVENESS: Unazijua sheria za mapenzi? (aliongea kwa msisitizo akimtazama Happy usoni) (Happy alishtuka, hakutegemea kama Love angeuliza swali kama hilo. Hakujua Love amepata wapi habari za sheria za mapenzi)
LOVE: We Happy!
HAPPY: Abee! (alishtuka kutoka kwenye mawazo)
LOVE: Hunisikii au?
HAPPY: Umesemaje kwani?
LOVE: Nimekuuliza unazijua sheria za mapenzi?
HAPPY: Hapana, sizijui.
LOVE: Je unataka kuzijua?
HAPPY: Hapana sizitaki, za nini sasa?
LOVE: Sawa kama huzitaki, ukizitaka nitafute.
Love baada ya kuongea hivyo alitulia, alipotezea. Lakini Happy alivurugwa, bado hakujua kwanini Love amezungumzia vitu hivyo.
MGAHAWANI:
Ida ya mchana Issa na Meshack walifika mgahawani, waliagiza chakula kisha walitulia kwenye meza walianza kula. Hata hivyo Issa alionekana kuwa na stress nyingi;
MESHACK: We vipi mbona huli msosi?
ISSA: Kaka hivi we ule mtihani uliuonaje? Kwa maana naona mwenzangu hata huogopi küfeli!
MESHACK: Kumbe hizo stress zote unawaza kuhusu pepa? Sikiliza nikuambie; ile pepa hatukusoma sana,
Kama tukifeli mbona haina noma, kwanza ndo itakuwa ni mara yetu ya kwanza? küfeli ni kitu cha kawaida kwa mwanafunzi yeyote! Mwanachuo mzima unaogopa küfeli?
ISSA: Kinachoniuma Mimi sio küfeli, kinachoniuma ni lile swali tulilompa jamaa ili afeli kumbe tulikuwa tunampiga chura teke!
MESHACK: Dah! sema ukiwaza sana utaumwa. Potezea tu japo inauma, alafu nakumbuka jana uliniambia tutafute majibu ila ndo hivyo!
ISSA: Si unakumbuka eeh? nilikuambia. Serna nini; haina noma, maji yakimwagika...
MESHACK: Kaka usijali, kwanza mimi nimepata wazo!
ISSA: Wazo gani tena hilo?
Meshack kabla hajajibu alitikisa kichwa juu chini akicheka, alifurahia wazo lake, sasa sijui ni wazo gani, mimi na wewe hatujui, aisee kazi ipo.

MWISHO WA SEASON 01, USISAHAU SEASON TWO
IMEKAMILIKA

TSH 1000 TU FULL,
INA VIPANDE 20..
TSH 1500 VIPANDE 40..
TSH 2000 TU VIPANDE 60..
TSH 3000 VIPANDE 100

Malipo mpesa 0768315707 jina Prisca, ukishalipia nambie nikutumie chap.
 
SEASON 02

TAMTHILIA: MTU ALIYETHIBITISHWA KWA MAISHA YANGU
CERTIFIED PERSON OF MY LIFE (CPL)
( 21-25)

WHATSAPP 0768315707

SEHEMU YA 21

Mimi na wewe hatujui, aisee kazi ipo.
ISSA: Mbona huongei? Umepata wazo gani?
MESHACK: Jamaa tulimtungia swali la uongo kwa bahati mbaya lile swali lilitoka kwenye pepa, kwakuwa lilitoka ni lazima atakuwa anawaamini wale waliomtumia, hivyo basi kuanzia sasa akitumiwa kitu chochote cha uongo ni lazima ataamini tu. Wazo langu ni kwamba inabidi tumtungie vitu vingi vya uongo ili tumpoteze moja kwa moja. Tutampoteza kwa sababu atakuwa anaamini vitu hivyo ni vya kweli kumbe vua uongo. ISSA: (Akitabasam) Kaka unafaa kuwa afsa mipango.
Walicheka kwa furaha, walijiona wababe mara baada ya kupata wazo hilo. Walikuwa na hasira ya kumuharibia Frank ikiwezekana wamuondoe chuo.
***
HOSTEL
Frank alikuwa room kwake, alionekana kuwa na furaha sana; furaha hiyo ilitokana na kuotea maswali kwenye chumba cha mtihani; aliwashukuru sana watu waliomtumia swali ambalo lilitoka kwenye pepa. Mara simu yake iliita, alitazama alikuta kapigiwa na Happy; alipokea alisogeza sikioni;
HAPPY: Mambo Frank (aliongea kwa furaha)
FRANK: Safi tu nambie.
HAPPY: Poa tu! mmh! Aisee we ni nomaa, ndio maana nakupenda jamani!
FRANK: Ah ah ah! sasa mimi noma wa nini? (aliuliza akitabasam)
HAPPY: Upo vizuri kwa kuotea maswali ya mtihani, leo nimeinjoy sana kwenye pepa, nimetiririka tu.
FRANK: Mmh! haya bwana lakini ni vitu vya kawaida tu.
HAPPY: Wee! eti kawaida. Alafu kwani unafanya nini muda huu?
FRANK: Nipo tu room.
HAPPY: Ushakula?
FRANK: Bado, nitaenda kula mida ya saa 8 na dakika 40 hivii.
HAPPY: Basi naomba nikupe ofa ya chakula cha mchana, au unasemaje?
(Frank alifikiria akubali au akatae? Na akicheki alishapewa ofa na Maria, hakujua aipitishe ofa ipi kati ya ile ya Maria au ya Happy.)
"Lakini Maria sidhani kama alimaanisha, yule nishamzoea ni mtu wa utani, usikute alikuwa ananitania tu wala hakumaanisha. Kama ni hivyo ni bora nikubali ofa ya Happy” Frank aliwaza
HAPPY: Vipi mbona kimya, au hutaki ofa?
FRANK: Sawa haina shida; ukipata sehemu ya chakula utaniambia nitakuja.
HAPPY: Sawa.
(Happy alifurahi ofa yake kukubaliwa. Aliona huo ndio muda wa kuanza kutimiza sheria zake za mapenzi. Aliwaza endapo yeye na Frank wakiongozana pamoja kwenye chakula na sehemu mbalimbali ni lazima wataonekana kama wapenzi vile, hiyo itampa sifa mbele ya wanachuo wengi. Fasta alitoka kitandani alienda kuoga kisha alijiandaa kwa kuvaa vazi bomba, manukato kama yote, alipendeza haswaa)
"Hata kama sizijui hizo sheria za mapenzi; sio mbaya, nitatengeneza sheria zangu ambazo zitaniongoza hadi nimpate” Happy aliwaza akiwa anaendelea kujipamba. Muda huo Love alikuwa kitandani akitazama tu. Happy baada ya kujipamba alichukua mkoba wake kisha alipiga hatua akiondoka, kabla hajafungua mlango mara alisikia sauti.
LOVE: We Happy mbona hatuagani?
HAPPY: (alisimama aligeuka nyuma) aah sorry! nilijua umelala.
LOVE: Hivi unajua kuwa sikuhizi hata sikuelewi mambo yako? kwani mwenzangu una harakati gani? HAPPY: Yaani we acha tu, nina haraka ila nisamehe tu!
LOVE: Una haraka unaenda wapi? HAPPY: Kuna mtu naenda kuonana nae, ila usijali nitawahi kurudi.
LOVE: Lakini si tulikubaliana saa 8 hii tukale chakula pamoja, sasa mbona sikuelewi?
HAPPY: Mi sahizi sina njaa, nitakula baadae.
LOVE: Mmh! Haya sawa!
Happy hakujali wala nini, alifungua mlango alisepa zake. Love alibaki anashangaa mataa, wenzie ndo hao wanatusua tu kwenye mahaba.
Frank bado alikuwa room kwake, alitulia akisubiri simu ya Happy ili waende mgahawani. Mara simu yake iliita, alijua lazima ni Happy, alitazama kwenye kioo akitaka kuhakikisha jina la mpigaji; badala ya Happy alikuta kapigiwa na Maria! Weuwe! Mwanaume alipagawa kwa sekunde chache kisha alipokea simu.
MARIA: Wewe upo wapi? FRANK: Nipo room.
MARIA: Mi nipo nje ya hosteli yenu, nakusubiri tuelekee mgahawani.
FRANK: Mh!
MARIA: Vipi mbona unaguna? Toka nje basi (Frank alichanganyikiwa. Ofa mbili kwa wakati mmoja, na akcheki ofa zote alizikubali, alifikiria afanyaje)
"Hapa ngoja niondoke na Maria, najua Happy akipata mgahawa lazima atanipigia simu kunijulisha; nami nitamwambia kuwa nishakula. Japo atakasirika lakini nitamtuliza” Frank aliwaza. Alitoka kitandani kisha alielekea nje alimkuta Maria
FRANK: Nilijua utanidanganya.
MARIA: Wee! eti nikudanganye! mbona wewe hukunidanganya kwenye lile swali lako ambalo lilitoka kwenye pepa?
FRANK: Ah ah ah! ok tuondoke.
Waliondoke walielekea migahawani, walitafuta mgahawa wenye utulivu kisha walitulia, waliagiza chakula walianza kula wakiwa wanapiga stori mbalimbali.
-k-k-k
MIGAHAWANI:

SEHEMU YA 22


Happy nae alifika migahawani, alianza kutafuta mgahawa ambao ungefaa kwa yeye kukaa na
mgeni wake ambaye ni Frank.
"Yani hapa sitaki kufanya makosa, inabidi nitafute mgahawa tulivu na wakuvutia ili tukikaa basi
kila atakayetuona ajue sisi ni wapendanao" Aliwaza akitabasam. Alitumia muda mwingi kutafuta mgahawa, baada ya dakika nyingi atimaye aliuona mgahawa bomba ambao ulitulia.
HAPPY: Pale panatufaa (Alijiongelesha)
(Kumbe Love naye alikuwa maeneo yaleyale, aliamua kumfuatilia Happy kimya kimya. Wakati Happy akihangaika kutafuta mgahawa; Love alikuwa kajificha sehemu akitazama tu; alishangaa kumuona rafiki yake akijizungusha tu.) "Hivi huyu Happy ameanza kuwa kichaa? alisema kuna mtu anataka kuonana nae, sasa mbona hawaonani? hata simu hampigii? Ebu muone anavyojizungusha mara huku mara kule, alafu aliniambia kuwa hana njaa; sasa mbona anazunguka migahawani? Kwani anatafuta nini? Leo simuachi hadi nijue kinachompa wazimu" Love aliwaza akiwa amejibana sehemu.
(Happy baada ya kuuona mgahawa wenye vigezo anavyovitaka; alipiga hatua kuelekea kwenye mgahawa huo. Love nae wala hakuzubaa, aliendelea kunyatia nyuma nyuma mpaka kieleweke.)
"Kumbe hapa chuoni kuna mgahawa mzuri hivi? itakuwa watu wanauogopa ndio maana wengi hatuufahamu, alafu panaonekana pana watu wachache; au bei zao kubwa? Lakini bora nilipe bei kubwa kwa mtu ninaempenda" Happy aliwaza akiwa anazama ndani ya mgahawa. Alifika ndani alishtuka kukuta kila meza ikiwa na wateja wawili wawili ambao ni wa kike na kiume, moja kwa moja alijua watu hao ni wapenzi, alijisifu kuchagua sehemu hiyo kwa sababu aliamini muda si mrefu hata yeye atakaa meza moja na mwanaume ampendaye. Hakutaka kuchunguza wateja, yeye alielekea moja kwa moja kwa wahudumu; alikuta vyakula ni vingi.
“Mmh sijui nimchagulie chakula gani, au nimpigie nimuulize anapenda chakula kipi? lakini hapana, ngoja nimchagulie chakula kizurii, yani leo namfanyia sapraizi, akija anakuta chakula kimeandaliwa" Happy aliwaza akitabasam. Baada ya kukagua vyakula aliamua kuchagua rost ya ndizi nyama pamoja na tambi, pia aliagiza juisi glasi mbili.
HAPPY: (akimtazama muhudumu) Niandalie haraka hivyo vyakula.
MUHUDUMU: Usijali dada, wewe nenda kakae mezani nitakuletea vyakula vyako.
HAPPY: Hapana, sitaki uniletee; nipe nitavichukua mimi mwenyewe.
(Happy alivurugwa na mahaba, alitaka aandae chakula yeye mwenyewe. Muhudumu hakuwa na noma, aliandaa vyakula kisha alimkabidhi Happy ambaye alivipokea kisa aligeuka, alizungusha macho akitafuta meza isiyo na watu ili akakae. Alitembea taratibu akiendelea kutafuta meza, mkono mmoja alishika sahani yenye chakula chake, na mkono mwingine alishika sahani yenye chakula cha Frank. Meza nyingi zilionekana kupambwa na wapendanao ambao walikuwa bize na vyakula vyao, wengine walilishana, wengine walitaniana, ilimradi mahaba yanogetu.
Happy yeye aliendelea kuzunguka akitafuta meza, sasa akiwa katika harakati za kutafuta sehemu ya kukaa; macho yake yalitua kwenye meza flani hivi, alishtuka, kuna kitu cha kushangaza alikiona, ghafla kukasikika "Paaaaaah", zile sahani ambazo alizibeba zote zilidondoka chini; Vyakula vilimwagikana, sahani zilivunjikana, Happy bado alikodoa macho mbele akishangaa, sasa sijui aliona nini, mweeh jamani yajayo yanatetemesha!!!
SEHEMU YA 23
Happy hakuamini hata kidogo; alishangaa kumuona muhusika ambaye alikuwa anamuhangaikia eti alikuwa akilishwa chakula na mwanamke mwingine. Happy alipoteza network kichwani, mwili wote ulikosa nguvu, kabla hajazimia aliamua kukimbia mbio; alitoka nje ya mgahawa akiwa analia kwa uchungu. Aliacha watu wakishangaa mataa, wateja walishindwa kuelewa, hakuna aliyejua tatizo ni nini.
Unajua Happy aliona nini? Alimuona Maria akimlisha Frank chakula, sasa kwa akili ya haraka aliamini kwamba Maria na Frank ni wapenzi na ndio maana walilishana vyakula. Kumbe wenzie ni marafiki wa muda mrefu, na ni mara nyingi tu washazoea kulishana. Sasa Maria baada ya kushuhudia tukio hilo aliacha utani wake wa kumlisha Frank chakula, nae aliganda akiwaza kwanini Happy kakimbia.
'Ooh! Sasa nimeelewa, nakumbuka Issa na Meshack waliniambia kuwa Happy na Frank wana mahusiano, inawezekana Happy amechukia mara baada ya kuniona namlisha Frank chakula. Pia inaonekana walikubaliana waje kula pamoja, na ndio maana alinunua chakula sahani mbili. Sasa kama kweli wao ni wapenzi, na kama Frank alijua kuwa inabidi akutane na Happy hapa mgahawani; sasa kwanini alikubali ofa yangu ya chakula?” Maria alitulia akiwaza, muda huo Frank alitulia tu.
MARİA: Frank
FRANK: Vipi?
MARİA: Mimi sijaelewa kilichotokea.
FRANK: Hata Mimi sijaelewa.
MARİA: Kweli hujaelewa?
FRANK: Ndio sijaelewa, au wewe umeelewa kwanini
Happy amemwaga chakula?
MARIA: Sijaelewa hata kidogo, ila nilijua labda ameshtuka baada ya kunikuta nakulisha chakula.
FRANK: Hapana, huo ni wasiwasi wako tu. Humu ndani tupo watu wengi, wala usijihisi vibaya.
MARIA: Mh! basi sawa, ila hii michezo yetu ya kulishana kuanzia leotuiache.
FRANK: Ah ah ah! Umekoma au sio? Lakini hajamwaga chakula kwa sababu yetu, itakuwa ana sababu zake.
MARIA: Lakini Frank; wewe na Happy si

mnafahamiana?
FRANK: Sio sana, ni siku moja tu aliniomba nimuelekeze maswali; hiyo ndiyo ni siku ambayo tulifahamiana, ila hatuna mazoea.
MARIA: Sawa.
Maria aliyaamini maneno ya Frank, lakini Frank mwenyewe alitambua kuwa yeye ndiye chanzo cha Happy kumwaga chakula, pia alitambua kuwa ni lazima Happy amechukia na amekasilika sana.
Wakati hayo yote yanafanyika; mnyapiaji Loveness alikuwa maeneo yale yale, alishuhudia kila kitu, alimuona Happy akimwaga chakula kisha alitoka mgahawani akiwa analia; hata hivyo hakujua chanzo cha Happy kumwaga chakula na kuondoka kwa hasira. Love alijibana nje ya mgahawa, licha ya kuona matukio mengi lakini hakuwaona Frank na Maria. Baada ya kushuhudia matukio hayo aliondoka mgahawani alirudi hosteli akiwa anajiuliza maswali mengi yasiyo na majibu. Mara kukasikika "tiiiih", Love aligongana kibega na mtu ambaye hakumuona; baada ya kusukumana alinyanyua macho alitazama mbele alikutana na Issa, walibaki wanatazamana tu,

SEHEMU YA 24


Issa hakuamini kama amekutana na Love laivu bila chenga.
Issa anamfahamu vyema Love, alianza kumkubali tangia siku ya kwanza anabishana na Frank darasani, pia aliwahi kwenda kumuona hospitali kipindi kile Love anaumwa. Lakini Love yeye hamfahamu Issa kiviile, aliwahi kumuona mara moja tu hospitali; kwa ufupi ni kwamba wanasoma chuo kimoja, darasa moja lakini hawana mazoea. Mara nyingi Issa huwa anamtetea Love darasani pasipo hata Love mwenyewe kutambua. Ukweli ni kwamba Issa anampenda sana Love lakini kumwambia ndo ishu. Sasa muda huo baada ya kukutana jamaa aliona aanze kutengeneza mazingira;
ISSA: Mambo vipi love.
LOVE: Safi tu habari yako?
ISSA: Fresh, unanikumbuka? (aliuliza akitabasam)
LOVE: Yeah! si ulikujaga kuniona hospitali kipindi kile? ISSA: Yaah ni mimi! kumbe una kumbukumbu.
LOVE: Nakumbuka.
ISSA: Sawa, ila natamani sana tufahamiane, kama hutojali nipe namba yako.
(Loveness alifikiria kwa dakika chache; aliwaza kama atoe au hasitoe! Hakuwa tayari kutoa namba, hata hivyo aliona hasipotoa itaonekana kama anaringa)
LOVE: Sawa andika... 012345678... Kwaheri
ISSA: (Moyoni akifurahi) Asante nitakushtua badae.
LOVE: Sawa.
(Baada ya Love kuondoka Issa alijipiga ngumi kifuani alijisifia, kuipata namba ya Love aliona amepiga hatua kubwa ya mahaba, alijiona mwamba kinoma)
"Huyu Love anaweza akawa ni binti mzuri kuliko wote hapa chuo, sasa nikimpata sijui itakuaje yani!!! yule pimbi misifa atanikoma, muda wote nitakuwa na bebi wangu tukizunguka kila kona ya chuo; daadeq" Issa alijisifu akiwa anachekelea, aliendelea na safari zake.
-k-k-k
HOSTEL
Happy alifika hostel alijitupa kitandani akiwa analia, alilia akiwa anajiongelesha maneno machungu; alilalamika kimapezi;
HAPPY: Frank ameamua kunifanyia vile makusudi ili aniumize, hata kama hanipendi hawezi kunifanyia vile; yaani wanalishana hadharani ili tu nijue kuwa ana mtu ampendaye, haya bwana.
(Alilia sana, kwa hasira akaanza kupigapiga godoro, alikuwa kama amechanganyikiwa, hakujua afanyaje, sheria za mapenzi zilimtesa, mara ajigeuze kushoto, mara kulia, kuna muda alilala kifudifudi kalio likiwa juu; akiwa amechanganyikiwa kwa kilio mara alishtushwa na sauti ya Love)
LOVE: We Happy!
(Happy alinyamaza kulia, aligeuka kisha alitazama mlangoni; macho yake yalikutana na sura ya Love)
LOVE: Mbona unalia hivyo?
HAPPY: (Alifikiria kwa muda aliona bora adanganye)
Tumbo linaniuma sana!
LOVE: Linauma? tatizo nini?
HAPPY: Sijajua, ila limeanza kuuma baada ya kula mgahawani.
LOVE: Oh! pole, lakini una uhakika kuwa ni tumbo ndilo linakusumbua?
HAPPY: Ndiyo, linauma sana.
LOVE: Sawa twende hospitali.
(Love alionekana hatanii, alianza kukusanya kadi za hospitali akitaka kumpeleka rafiki yake hospitali)
HAPPY: Usijali Love litapona tu.
LOVE: Happy huumwi unanidanganya si ndiyo? (Happy alianza kupata wasiwasi, alihisi kama ameshtukiwa vile; hakutaka kabisa Love ajue mahusiano yake na Frank)
LOVE: Happy mapenzi yanakutesa alafu
unadanganya tumbo?
HAPPY: Nini? (alishtuka)
LOVE: Kuna mtu unampenda na anakutesa, je ni uongo?
HAPPY: Ndiyo ni uongo.
LOVE: Kama ni uongo kwanini ulivunja vyombo vya watu pale mgahawani?
(Happy alichanganyikiwa baada ya kusikia kauli hiyo ya Love, aliona mambo yashakuwa mambo, dili limekuwa Dirisha, siri na imekuwa ya watu wote, bidada alivurugwa)
LOVE: Nijibu, kwanini unanidanganya tumbo linauma kisa chakula cha mgahawani wakati hata chakula chenyewe hujala?
****
Frank baada ya kutoka mgahawani alirudi hosteli, alitulia nje akifua nguo zake. Licha ya kuwa bize na kufua lakini akili yake ilikuwa mbali sana, alimuwaza sana Happy. Sio kwamba alimuwaza kimapenzi, hapana, ila aliwaza namna alivyosababisha Happy amwage chakula mgahawani. Kutokana na kosa hilo ambalo alifanya aliona bora ampigie simu amuweke sawa.
"Lakini nikimpigia nitamtuliza vipi? Nitamwambia kitu gani cha kueleweka? Atanielewa kweli? au nimfuate huko huko hosteli kwao? lakini kwenda kule hapana, bora nimpigie tu nitajua nini cha kumwambia" Frank aliwaza, alichukua simu alimpigia Happy. Simu ya Happy iliita, mwanaume alisubiri m rem bo apokee simu ili amtulize kwa maneno yenye ujazo wa hali ya juu! maneno tulivuu kabisaa! Wacha tusubiri tuone.



Simu ya Happy iliita kwa muda mrefu lakini haikupokelewa, jamaa alipiga tena na tena lakini bidada hakupokea simu. Kwa mara ya mwisho, mara ya tatu Frank alipiga tena simu, namba ya Happy iliita•••••
-k-k-k
Upande wa pili Happy aliona simu yake ikiita ila kwa makusudi hakupokea, sio kwamba hakutaka ila hasira zilifanya hasipokee. Bado aliumia kitendo cha kumkuta Frank akilishwa chakula na mwanamke mwingine. Kutokana na hasira hakutaka kabisa kupokea simu yoyote wala kujibu meseji ya Frank. Love alikuwa pembeni, alishangaa kuona Happy hapokei simu;
LOVE: Mbona hupokei simu?
HAPPY: Achana nae!
LOVE: Kwani huyo ni nani?
HAPPY: Nimekwambia achana nae (aliongea kwa hasira)
LOVE: Sawa! sawa Happy; leo hii wewe ni wa kunijibu mimi hvyo kisa mwanaume? Happy ambae kila jambo uliniambia nami nilikuambia, leo umekuwa mtunza siri au sio?. Ebu fikiria ukizidiwa humu ndani nani atakuhangaikia? mapenzi ndo yakufanye uwe wa kipekee namna hiyo? hivi unajuaje kama ukinishirikisha naweza nikakusaidia uzipate hizo sheria za mapenzi? Sawa hakuna shida, endelea kuwa msiri!! Mimi naondoka tutaonana baadae.
Love alisepa nje. Huku nyuma Happy aliwaza maneno ya Love kisha taratibu alianza kulia tena, alivuta shuka alijifunika aliendelea kuporomosha machozi! Ama kweli mapenzi ni nyokoü!
***
Kule kwa Frank baada ya kupiga simu pasipo mafanikio aliona isiwe keşi, hakumpigia tena, sasa kama mtu hapokei simu ampigie mara nyingi ili iweje? Aliachana nae.
"Na ndio maana sifuatiliagi masuala ya mapenzi, mambo yenyewe ndo kama haya; unampigia mtu simu mara 10 anakuchora tu, kwa makusudi anakukatia simu, sipigi tena1' Jamaa aliwaza kwa hasira, aliendelea kufua nguo zake, alizichukua alienda kuanika.
****
SIKU ILIYOFUATA
DARASANI:
llikuwa ni jumanne, wanachuo walijaa darasani kwaajili ya kipindi cha ujasiriamali. Hata hivyo darasa lilimkosa mwanafunzi mmoja ambaye alikuwa anaumwa ugonjwa wa mawazo ya mapenzi, mwanafunzi huyo sio mwingine bali ni Happy. Mwalimu alikua mbele ya darasa akifundisha, kama kawaida Maria alikaa siti za nyuma akiwa na Issa na Meshack, Frank alikaa viti vya mbele pamoja na wanachuo wengine, Love yeye alikaa katikati na marafiki zake. Macho ya Frank yaliangaza kila kona akimtafuta Happy lakini hakumuona, alihisi mambo yashakuwa mambo, hata hivyo mwanaume alitulia alisikiliza kipindi kama ifuatavyo;
MWALIMU: Karibuni kat ika kipindi chetu kizuri cha ujasiriamali, tukiwa hapa kila mtu ni mjasiriamali kwa sababu kuchukua kozi ya biashara ni ninii?
WANACHUO: Ni ujasiriamalii! (walijibu kwa pamoja)
MWALIMU: Safi!. Hivi mnajua kuwa kila kitu katika hii dunia ni ujasiriamali? ukigundua bidhaa ni ujasiriamali, ukiwa mchoraji ni ujasiriamali, siku hizi hadi ndoa ni ujasiriamali.
(Wanachuo waliguna "mmh" na wengine walicheka, walimuona mwalimu ni muongo)
MWALIMU: Eeeh! kila kitu ni ujasiriamali. Mnabisha, kwani ujasiriamali ni nini? UJASILIAMALI ni kile kitendo au shughuli ya kutengeneza biashara ukichukulia hatari yoyote ya fedha iwe kama kitu cha kawaida ili tu upate faida. Ujasiriamali unatengenezwa kwa fedha, wazo, mipango ya kibiashara, soko na matangazo. Katika uchumi wanasema kwamba; ujasiriamali, mtaji, wafanyakazi na ardhi ni vitu vinavopelekea uzalishaji. Na mjasiriamali ni yule mtu anayetengeneza biashara pasipo kuogopa hatari yoyote ili tu aipate faida. Lakini sio kila mtu anaweza akawa na sifa za kuwa mjasiriamali bora, kuna sifa kuu ambazo mtu lazima awe nazo ili awe mjasiriamali bora. Sasa ili swali naomba lijibiwe na mabinti katika darasa ili. Wadada mtuambie "Ni zipi sifa kuu 5 za kuwa mjasiriamali bora?''
(Baada ya mwalimu kuuliza swali hilo kukaanza vijikelele vya chini chini, miguno ilisikika, hakuna binti aliyenyosha mkono, wote walikaa kimya)
MWALIMU: Humu ndani hakuna wanawake au wasichana au mabinti, hawapo au sio?
WANACHUO: Wapoo
MWALIMU: Sasa kwanini hamnijibu? Au sijasikika? Nauliza tena, ni zipi şifa kuu tano za kuwa mjasiriamali bora?
(Bado wadada walileta mgomo, hakuna aliyenyosha mkono, Maria alitamani kujibu ila aliogopa; sasa sijui aliogopa nini)
"İli swali naweza kujaribu kulijibu lakini ili darasa ukijibu swali ni kama unajitafutia ugomvi, bora tu nikae kimya 11 Maria aliwaza (Mabinti walikua wengi darasani lakini wote walikaa kimya. Love nae alitamani kujibu swali lakini kila akikumbuka yanayomkutaga aliamua kuuchuna tu, ha kuta ka matatizo na mtu, kwanza aliogopa hasije akakosea akaaibika. Hata hivyo kuna karoho kalimwambia hasiogope)
"Kukaa kimya wakati swali nalijua hizi ni dalili za ujinga, alafu nikae kimya nimuogope nani? kwani namsomea mtu? si nasoma kwa manufaa yangu, wacha nijibu swali” Love aliwaza, aliona bora awakomboe wanawake wenzie, bila kupoteza muda alinyosha mkono juu.
MWALIMU: Nilitaka kushangaa mabinti wote nyie alafu hasitokee mtu wa kuwakomboa? Hakuna vita isiyo na mkombozi, dada karibu uwakomboe wenzio, simama kisha tujibie swali.
(Hapo sasa waliokaa mbele waligeuza shingo wakitaka kumuona mkombozi wa mabinti, wale wa nyuma nao walitazama mbele wakitaka kumuona aliyenyosha mkono, kila mtu alitabasam baada ya kumuona Love, walijua kumekucha na makucha yakee, sijui kama vita hiyo itaisha salama. Love alisimama kisha alijiseti vizuri, alijibu swali kama ifuatavyo)
LOVENESS: Sifa kuu tano za mjasiriamali bora ni zifuatazo; Kwanza Ubahiri, mjasiriamali ni lazima awe anaijua sana pesa sio kutoatoa hovyo. 2. Pesa nyingi, lazima awe ana fed ha za kutosha ili hasipate shida. 3. Afya bora, Afya nzuri itamfanya afanye kazi katika ubora. 4. Bidhaa nyingi, lazima awe ana bidhaa zitakazowatosha wateja. 5. Upendo, ni lazima awe mtu wa watu sio kila muda kukasirika.
(Love alimaliza kutaja sifa kuu tano za mjasiriamali bora, baada ya kuzitaja alikaa chini, darasa lilitulia kimya, kila mmoja alisikia pointi za Love; walisubiri maksi kutoka kwa mwalimu, ticha alitafakari kwa sekunde chache kisha aliongea)


SEHEMU YA 25

MWALIMU: Safi sana binti, maelezo yako ni mazuri; lakini je humu ndani wote tunakubaliana na majibu ya huyu dada?
(Hapo sasa ndo patamu! mambo ni moto, kila kitu ni balaa. Issa alimgeukia Maria kisha walianza kunong’ona)
ISSA: Love yupo sahihi, kila mwanachuo kamuelewa vizuri na ndio maana tupo kimya. Ila nina wasiwasi na lijitu limoja hivi, sidhani kama litaweza kuvumilia kukaa kimya...sidhani kabisaa!!!
MARIA: Linani hilo ambalo una wasiwasi nalo?
ISSa: We subiri, lisipotokea jitu lolote basi dunia itakuwa imebadilika sana!!
(Ni kweli kuna mtu hakuridhishwa na majibu yaliyotolewa, eti ubahiri ni sifa kuu ya mjasiriamali bora, Sifa ya wapi hiyo? Labda sifa ya kichaga. Kwa asilimia 1100 jamaa hakukubaliana na majibu ya Love, jamaa huyo sio mwingine bali ni Frank. Licha ya kugundua majibu sio sahihi lakini hakutaka kusimama, alihofia hasije akaonekana mkorofi, aliona bora akojoe alale ili siku ipite. Hata hivyo alikumbuka kuwa wapo darasani, tena darasa lenyewe lina wanafunzi wengi kinoma, sasa akisema akae kimya alafu watu wachukue pointi za uongo, wakifeli je? Hapana kwakweli, sio vizuri kuwaacha wenzio wafeli wakati swali unalijua. Pasipo kutarajia Frank alinyosha mkono juu, weuwee! darasa lote lilisheki!!)
ISSA: Si umeona Maria, unaona ule umama? Nilikuambia kuwa kuna jitu la kutisha haliwezi kutulia bila kunyonya damu za watu. Swali limeulizwa kwa wan awake alafu kuna mwanaume anataka kulijibu, jamani sio ushoga huo kweli? (Issa alipaniki)
MARIA: Kwahiyo kama mtu kajibu uongo aachwe tu? hivi we Issa unakuaga na matatizo kichwani?
ISSA: Wewe acha kulitetea shoga lile!!
(Kule mbele mwalimu aliuona mkono wa Frank)
MWALIMU: Safi nimeona mkono hapa mbele, sasa wacha tuone majibu au marekebisho kutoka kwa huyu kijana, alafu tutaangalia majibu sahihi kati ya yule dada na huyu kaka...Haya mjomba tujibie swali.
FRANK: (Akasimama kisha alijibu) Nadhani majibu ya dada yetu pale sio mabaya sana, ila tu kuna vitu kavichanganya kidogo, yeye amejaribu kuelezea vitu ambavyo inabidi viwepo katika maisha ya mjasiriamali lakini swali linataka şifa za kuwa mjasiriamali bora, kiukweli sina uhakika na pointi alizozisema.
MWALIMU: Huna uhakika? Ebu tupatie zako zenye uhakika tuzione.
FRANK: Şifa kuu za kuwa mjasiriamali bora ni hizi zifuatazo; 1. Ubunifu, lazima uwe mbunifu wa bidhaa na mambo mengine ili uvutie wateja. 2. Kutoogopa hatari yoyote, lazima awe mjasiri haşiye mwoga wa hasara. 3. Maarifa ya soko na bidhaa, hapa lazima alijue soko vizuri na ajue ni bidhaa gani zinapendwa na wateja. 4. Kujikubali na kujiamini, kufanya kazi kwa nguvu na nidhamu, hivyo vitu ni muhimu sana kwa mjasiriamali anayetaka kufanikiwa. 5. Umiliki mzuri wa fedha, huku sasa ndo kwenyewe, lazma awe anajua thamani ya fedha yake, na hata ile pointi ya dada yetu ya ubahiri inaweza ikaingia hapo, alafu hata...
(Kabla Frank hajamaliza kuongea Love aliingilia kati) LOVE: Sasa kama pointi zangu ni za uongo, kwanini unazitumia kat ika maelezo yako?
FRANK: Ni kwa sababu nilikua nakurekebisha.
LOVE: Unanirekebisha kwani nahitaji marekebisho? Hivi unataka kusema pointi zako ndio sahihi?
FRANK: Mwalimu ndiye atathibitisha, alafu nimejibu hizo pointi kwa faida ya darasa wala sio kwa faida yako wewe.
LOVE: Faida ya darasa? Ina maana pointi zangu hazina faida kwa darasa?
FRANK: Hivi kwanini hupendagi kurekebishwa?
LOVE: Kwa sababu hata wewe hujawahi kufunga bakuli lako endapo ukiona nimejibu swali.
FRANK: Oh! kumbe ni wewe yule ambaye hauna sifa za kijasiriamali?
LOVE: Mbona wewe hauna sifa za kuwa mwanaume bora lakini hatusemi, swali la wan awake lijibiwe na mwanaume, inahusu?
FRANK: Sikiliza nikuambie; sisi wasomi katika maisha huwa tunasema "maendeleo ya binadamu yasipotengenezwa na jinsia mbili tofauti; yapo kwenye hatari" ulikua kwenye hatari nimeona nikusaidie!
LOVE: Unisaidie we kama nani? alafu katika wasomi wewe ni msomi?
FRANK: Sasa kama nasoma elimu ya juu na nina uelewa wa kozi ninayosoma kwanini nisiwe msomi? Hivi kum be bado hujielewi tu?
(Wakati mambo hayo yanaendelea wanachuo walichekelea tu wakihisi raha, Mwalimu alibaki anashangaa; alishindwa kuingilia kwa sababu alijua watu hao wanajadili mada, hakujua kuwa wawili hao wana bifu moja kali sanaa! Hata hivyo ticha alishtuka, aliona majibizano yanaelekea kwenye kuchambana, taratibu alimfuata mwanachuo mmoja aitwaye chande)
MWALIMU: Chande.
CHANDE: Naam
MWALIMU: Kwani wale wawili wana ugomvi?
CHANDE: Ticha wale watu ni maadui waliokomaa, uhasama wao ni zaidi ya Simba na Yanga.
MWALIMU: (alishtuka, alikodoa macho akishangaa)
Weeeh!! Kwani walishawahi kugombana huko nyuma? CHANDE: Hii ni mara ya tatu, huyo jamaa Frank wanamuita pasua kichwa!
MWALIMU: "Pasua kichwa" kivipi sasa?
CHANDE: Kila mtu humu ndani alishangaa kwanini ulimruhusu pasua kichwa amrekebishe Love.
MWALIMU: Una maana gani?
CHANDE: Wale wawili walishawai kubishana hadi yule binti alilazwa hospital!
MWALIMU: Tobaaa! Umesemaje?
Ticha alishtuka kuanzia kwenye moyo, mapafu hadi makagale! Hakuamini alichokisikia, ilibidi ageuze macho kisha aliwatazama mahasimu wa jadi; patamu hapooo!!!

ITAENDELEA , BAADAE KIDOGO
 
SEASON 02

TAMTHILIA: MTU ALIYETHIBITISHWA KWA MAISHA YANGU
CERTIFIED PERSON OF MY LIFE (CPL)
( 26-30 )


WHATSAPP 0768315707
SEHEMU YA 26

MWALIMU: Una maana gani?
CHANDE: Wale wawili walishawai kubishana hadi yule binti alilazwa hospital!
MWALIMU: Niniiii!
(Alishtuka kwa mshangao hata sura yake ilibadilika.)
CHANDE: Eeh! ndio hivyo mwalimu.... MWALIMU: Mmh! kazi kweli kweli ( aliongea akicheka)
Mwalimu alionekana kufurahishwa sana na yale mabishano ya Frank na Love, alipenda sana japo ilikua ni kama ugomvi lakini kwa upande wa mwalimu ilikua ni kama somo limenoga.
Ilibidi mwalimu apite mbele atoe hitimisho. Kati ya Frank na Love upande upi ni sahihi. Alivyofika mbele, kwanza alikohoa kikoozi kikavu alafu akaongea;
MWALIMU: Kabla sijasema pointi zipi ni sahihi, kuna mtu anaweza kutuambia nani yupo sahihi kati ya wale wawili?
(Kulikua na ukirnya kwa muda mpaka pale Issa alipoamua kunyosha mkono ili aongee upande upi ulikua sahihi. Mwalimu akamruhusu ajibu)
ISSA: Nimesikiliza maelezo ya wote wawili, lakini nathubutu kusema dada Loveness poiti zake ni sahihi kabisa. Kwanza kila mtu humu ndani amezielewa, asante.. (akakaa kwenye kiti)
Baada ya Issa kuongea kuliibuka miguno ya chini chini, mara kukasikika "mmmmh", Mara "mh mh mh". Pia kuna walio onyesha kukubaliana na Issa, na kuna walio onyesha kuğuna wakiashiria kutokubaliana na Issa. Miguno iliendelea hadi pale mwalimu alivoongea;
MWALIMU: Naomba ukirnya kidogo, ukirnya tafadhali... Sasa kabla sijongea chochote wale vijana wawili waliotupatia sifa za kuwa mjasiriamali bora wasimame...
(Love na Frank wakasimama)
MWALIMU: Ebu tupige makofi kwa ajili yao.
(Makofi yakapigwa)
MWALIMU: Nilichokiona leo kupitla hawa wawili kimenionyesha ni jinsi gani wamekua kifikra na kujielewa. Hata kimaarifa pia haijalishi nani alikua sawa na nani alikosea.... wakati wanabishana nilidhani kwamba wana ugomvi lakini ule sio ugomvi, Yale ni majibizano ya hoja....vizuri sanaa, ebu tuwapigietena makofi.
(Wanachuo wakapiga makofi)
MWALIMU: Kaeni chini vijana na kuweni na amani. Nimesikiliza vizuri pointi za wote wawili, wote walikua sawa, mfano dada pale alisema Hi uwe na sifa ya kijasiriamali inabidi uwe bahili, ni kweli ubahili upo katika ujasiliamali... Nilichogundua ni kwamba dada alijaribu sana kutuambia mambo ambayo wajasiliamali wengi inabidi wawe nayo. Naomba tumpigie makofi dada yetu..


SEHEMU YA 27


(Love akapigiwa makofi)
MWALIMU: Nikiirudi upande wa pili kwa kijana wetu wa kiume, sijajua anaitwa nani, anatokea wapi, ila nathubutu kusema yule kijana... ebu asimame kwanza.
(Frank akasimama)
MWALIMU: Unaitwa nani?
FRANK: Frank kakolanya!
MWALIMU: Frank kakolanya!! au una undugu na yule kipa "beno kakolanya1'?
FRANK: (Akiwa anacheka) hapana mwalimu!
MWALIMU: (Akitabasam) makofi kwa frank kakolanya.... Natumaini huyu kijana anajua nini maana ya kujifunza, wakati yule dada kamaliza kuongea pointi zake ambazo azikuwa sahihi sana, niliruhusu mtoe marekebisho. Lakini wanachuo mnaojielewa mlikaa kimya mkikubaliana na pointi ambazo hazikuwa sahihi. Kijana huyu alijitokeza kwa lengo la kuja kumrekebisha dada pale, na nafikiri kwa pointi alizozitaja hata dada mwenyewe amefurahi... Ongera kwa frank kwa kutupatia point sahihi, ongera pia kwa dada yetu kwa kujaribu, niwatakie asubuhi njema.
Kabla hawajaanza kutoka mule ndani, CR akapita mbele ili atoe matangazo mafupi. Walikaa kimya kumsikiliza nini ataongea
CR: Jamani poleni na masomo, ningependa muda huu tuutumie katika kugawa karatasi za mitihani ya uchumi, mwalimu amesema kuna baadhi wamefanya vizuri na kuna baadhi pia wameharibu, amenitaka pia nitoe maksi za mtu wa kwanza na wa mwisho, mtu wa kwanza amepata 15/15 na mtu wa mwisho amepata 1/15,...
(Kabla CR hajamalizia kuongea, kukasikika vicheko manung'uniko na maneno watu wakiuliza nani aliyepata 15 na nani aliyepata 1)
CR: Mwalimu amesema tu nitoe maksi,
hajaniruhusu kumtaja mtu jina, ila amesema ukitaka kufanya usahihi wa ulipokosa mtafute mwenye 15.
(CR akamaliza kuongea na kuanza kugawa mitihaniIssa alionekana kuchukia, muda wote alihisi haja ndogo imebana, ni baada ya kusikia wa mwisho ana 1, Uvumilivu wa kusubiri mitihani ukamshinda, akamtazama Meshack na kumwambia,.)
ISSA: Oya Meshy mi naondoka...
MESHACK: Subiri basi tuchukue pepa tusepe wote.

SEHEMU YA 28


ISSA: Aah! naona tumbo limenikazia kinoma, bora nirudi hosteli.
MESHACK: Poa basi, tangulia. Pepa yako nitakuchukulia. (Issa akaondoka)
CR alimaliza kugawa mitihani. Baada ya kuchukua pepa zao kila mmoja akaelekea njia yake, wengine wakawa wanahakikisha maksi zao, wengine wakawa wanamtafuta huyo mwenye 15 ni yupi, na wengine baada ya kupokea tu pepa, wakatia kwenye begi bila hata kuangalia wamepata ngapi.
Frank alionekana akiongea na CR kwasababu pepa yake hakuiona..
FRANK: Samahani CR, mtihani wangu sijauona. CR: Duuh! labda kuna mtu kakuchukulia, mitihani yote nimeigawa.
(Frank akabaki akishangaa)
Sasa meshack baada ya kuipata mitihani, wake na wa issa akasogea pembeni ya watu akajitenga ili aangalie wamepiga ngapi. Akaanza na wa issa aka kuta 1/15, akaja na wa kwake akakuta 2/15... Akatabasam na kukasilika muda huo huo.
Loveness yeye alionekana akifurahi sana. Baada tu ya kupokea mtihani wake akarudi hosteli, akamkuta Happy kalala;
LOVE: Happy, Happy, Happy...
HAPPY: (Akashtuka kidogo) vipi kwani?
LOVE: Wamegawa mitihani, yaani pepa tumelinyoshaa! (akifurahi)
Love akatoa mitihani, akampa Happy... Happy baada ya kuchungulia akakuta pepa yake amepiga 13.5/15 alafu Love alipata 13/15 akafurahi sana.
Frank baada ya kurudi hostel alikua bado haelewi nani aliyechukua mtihani wake, na kwanini achukue mtihani usio wake. Yeye wala hakuogopa kwamba anaweza akawa amefeli, aliamini hawezi kukosa 10 na kuendelea, ila sasa nani kachukua pepa ? aliwaza sana. Lakini akiwa katika mawazo, simu yake ikaita, .akaangalia jina akakuta ni Maria, akapokea na kuongea;
FRANK:Maria vipi?
MARIA: Poa mzima?
FRANK: Yeah! nambie!
MARIA: Pepa yako ninayo, nilikuchukulia!
FRANK:(akitabasam) Daah! nimeutafuta sana huo mtihani, vipi si nimeharibu sana?
MARIA: Eeh! 15/15 umeharibu kweli! (akicheka)
FRANK:(Akifurahi) na wewe umepiga ngapi?
MARIA: Yani sikuhizi nafuata nyayo zako... Nimepiga 13.5/15 nimefurahi acha tu yani!
FRANK: Ongera, niletee basi pepa yangu!
MARIA: Ungejua nipo hosteli kwako nje, nakuja hivo! ******
Meshack akarudi hostel kichovu na kumkuta issa hata habari hana. Akafikiria ampe pepa yake au asimpe adanganye hajaiona. Maana kwa anavomjua Issa akawiagi kukasilika;
"lakini kama küfeli tumefeli wote, pepa ni yake wacha nimpe11 aliwaza meshack
MESHACK: Oya Issa
ISSA: Vipi babu?
MESHACK: Pepa yako hii mwanangu...
(akampa, Issa akaipokea na kuangalia alichopata)
ISSA: Dah nilijua tu, mi nilijua tu, sema fresh haina noma.
MESHACK: Usijali! mi mwenyewe nimepata 2, Hakuna tofauti. Ila tujipangetu pepa nyinngine...
ISSA: Yule chizi kapata ngapi?
MESHACK: Nani mpenda sifa?
ISSA: Kuna chizi mwingine?
MESHACK: Sijajua kapata ngapi, Ila tumuulize Maria, Maria lazma anajua.
Wakampigia Maria, simu iliita na ikakata, wakapiga tena namba haipatikani.
Sasa upande wa pili kwa Happy na Love stori zilinoga sana. Happy homa ilimuisha kwa muda kutokana na utamu wa stori. Love alikua akimliwaza rafiki yake ambaye hadi muda huo hakutaka kusema mwanaume anayemsumbua.
LOVE: Yani Happy wewe ni kiboko...
HAPPY: Kwanini sasa? (akiwa anacheka)
LOVE: Ulivyootea lile swali, tangia nije chuo sijawai kupewa swali na likatoka!
HAPPY : Kawaida tu, kuna mtu alinifundisha, yeye ndie anahitaji pongezi.
LOVE: Mmh! huyo mtu sio wa mchezo, natamani nimjue huyo kichwa.
HAPPY: Aah! hiyo 13 inakuchanganya kichwa, je ukipata 15?


SEHEMU YA 29

LOVE: Itanichanganya mwili wote!
(Wakacheka kwa pamoja)
LOVE: Alafu nimekumbuka, hivi unajua kuna limtu limepata 15/15?
HAPPY: Nani huyo? (akishangaa na kuwaza labda anaweza akawa ni frank)
LOVE: Hata sijui ni nani, yani nikimjua huyo mtu aliepata 15 nitabanana nae...
HAPPY: Kubanana nae kivipi? (alishtuka kidogo)
LOVE: Si nitambana tusome wote kila siku.
HAPPY: Mmh! ulivyo mvivu, vipi kipindi leo kilikuaje uko darasani?
(Love baada ya kuulizwa mambo ya darasani uso ukabadilika, alikasilika ghafla)
LOVE: Achana na mambo ya vipindi, tuongelee mtihani.
HAPPY: Au teyali yule muumiza kichwa wako kafanya yake?
LOVE: Yani yule simpendi yule mtu, kila nikiongeaga darasani lazma ataleta şifa zake, silipendi kama nini! HAPPY: Lakini anaongeaga vitu vikubwa yule!
LOVE: (Akifyonya).. Vitu vikubwa wapi, hana lolote!
HAPPY: Mmh! haya ugomvi wenu siuwezi!
LOVE: Ila Happy, nambie basi ni mwanaume gani anakuchanganya?
(Swali hilo Happy alilifikiria, akacheka moyoni kwasababu ukwel aliujua yeye mwenyewe)
HAPPY: Unataka kumjua anayenichanganya sio?
LOVE: Ndio. Alafu huwezi jua naweza kukufundisha hizo sheria za mapenzi unazozitaka.
HAPPY: Mh! ungejua!
LOVE: Ninii?
HAPPY: Huyo aliyefanya upate 13 ndiye
anayenichanganya kimapenzi!
Love macho yakamtoka!
Sehemu ya 13
LOVE: Ndio. Alafu huwezi jua naweza kukufundisha hizo sheria za mapenzi unazozitaka.
HAPPY: Mh! ungejua!
LOVE: Ninii?
HAPPY: Huyo aliyefanya upate 13 ndiye
anayenichanganya kimapenzi!
(Love macho yakamtoka!)
LOVE: Kwani nani kanisaidia kupata 13 zaidi yako?
HAPPY: Wewe Love mbona mgumu kuelewa? nimekwambia lile swali kuna mtu alinifundisha, huyo aliyenifundisha ndiye aliyetusaidia sisi wote tufaulu mtihani, na uyo ndiye anayeniumiza kimapenzi.
LOVE: Mmh! nani huyo sasa Happy, si umtaje tu jina? HAPPY: Kumtaja jina siwezi.
LOVE : Happy mbona hivyo! (analalamika)
HAPPY: Nisamehe mwaya, siwezi kumtaja, kamtafute mwenyewe.
LOVE: Eh! sasa nikamtafutie wapi?
HAPPY: Sikiliza, naona umepania kweli kumjua, sijui atakusaidia nini hata ukimjua., sasa kwa kukusaidia tu, wangapi wamepata 15 kwenye mtihani?
LOVE: Mmoja tu!
HAPPY: Unamjua?
LOVE: Nimjulie wapi?
HAPPY: Nenda kamtafute huyo mwenye 15, ukimuona huyo ndiye nimpendae.
LOVE: Happy mbona unanichanganya?
HAPPY: Hujaelewa nikuelekeze?
LOVE: Nimekuelewa, lakini wewe unajuaje kama nni yeye?
HAPPY: Nina uhakika ni yeye, ukimpata aliyepata 15 huyo ndiye anichanganyaye, nitafurahi sana kama utanisaidia kumpata mtu huyo.
Mida ya usiku Issa na Meshack walikua wakicheza gemu la mpira hosteli kwao, Issa akaona anafungwa sana akaamua kuacha.
ISSA: Mwanangu mimi basi, leo Sina akili ya gemu.
MESHACK: Aah! umeona nimekupiga unaamua kuacha sio (akicheka)
ISSA: Umeniotea tu (nae akicheka)
MESHACK: Haya bwana! vipi tunaenda wapi sahizi? ISSA: Oya, hivi unajua nilichukua namba ya yule mrembo, Love!
MESHACK: Wee! (anashangaa akitabasamu) acha masihala! Ilikuaje?
ISSA: (Akicheka) Mi mtoto wa mjini, yule manzi nilikua namtamani kitambo sana!
MESHACK: Fanya vitu sasa! sio unaongea tuu.
ISSA: Mmh! sasa nikimtongoza leo si ataona kama nimekurupuka hivi?
MESHACK: Kwahiyo wewe unataka hadi awe rafiki yako ndo umtongoze? fungua mdomo huo acha kuchelewa!
ISSA: Duh hasi sawa! (Issa akachukua simu yake na kutafuta namba ya Love baada ya kuipata akatabasam).
Love akiwa kwenye godoro lake alikua akiwaza sana. Aliwaza wapi atampata mtu aliyepata 15 kwenye mtihani. Hakujua aanzie wapi, afanyeje ili am pate, alikosa majibu. Akiwa bado anawaza mara simu yake ikaingia meseji kutoka kwa Issa, lakini yeye hakujua kama ni Issa.
ISSA: Mambo mrembo!
LOVE: Powa nani (akaijibu meseji)
ISSA: Issa hapa
LOVE: Issa yupi? (aliuliza lakini alishamkumbuka, akaona azuge kama hamjui vile)
ISSA: Yule uliyempa namba jana, aliyekutembelea hospital.
LOVE: Oh! nimekukumbuka!
ISSA: Vipi mzima lakini?
LOVE: Yah! sijui wewe!
ISSA: Niko fresh tu.
LOVE: Sawa niambie sasa!
Baada ya Love kutuma ujumbe huo Issa aliwaza kidogo, alichelewa kuujibu, alifikiria atongoze au asubiri:
"Sasa nitasubiri hadi lini? bwana wee! la kuwa na liwe" alijisemea issa kisha akaamua kurusha voko zake kwa Love, akamtumia meseji...
ISSA: Sikiliza Love, tangia siku ya kwanza nimekuona kwenye kipindi, siku nimekuja hospitali kukuona hadi juzi tumekuta pale mgahawani huwezi amini, nimetumia muda mwingi sana kukuwaza, hakika wewe ni binti mzuri nathubutu kusema hivyo. Mh! Love siwezi kupinga ukweli, nakuelewa sana, kwa kifupi nakupenda.
Loveness baada ya kupokea ujumbe huo alishtuka kidogo, akatabasam, na akacheka pia. Alishangaa hakutegemea, ilifikia hatua akajisemea;
"Mmh! kuna wanaume wako faşta, yani jana nimempa namba, leo kashapenda1' akacheka na kumjibu Issa..
LOVE: Mh! Issa!
ISSA: Ndio hivyo bibie, naomba tuwe wapenzi.
LOVE: (Akafikiria akaona atumie akili tu) Sawa wacha nifikirie!
ISSA: (Moyon alifurahi akajua kazi rahisi tu) Sawa nakutegemea Love.
LOVE: Usijali. Lakini wakati nakufikiria naomba na wewe unisaidie jambo moja!
ISSA: Jambo gani? sema chochote nitakusaidia.. (alijibu kwa uchangamfu)
LOVE: Nataka nimjue aliyepata 15 mtihani wa uchumi.
ISSA: Eeh! wa nini sasa?
LOVE: Unanisaidia au Hunisaidii?
ISSA: Powa nipe masaa!
Maria alikua katulia hostel kwake akijisomea. Alionekana kuwa bize na masomo kuliko kitu kingine chochote. Mara simu yake ikawa inaita, akaichukua na kutazama aka kuta mpigaji ni Issa, akapokea na kuongea;
MARIA:Hallo Issa vipi?
ISSA: Freah tu, upo wap?
MARIA: Nipo chumbani kwangu!
ISSA: Dah! aise nina shida moja hivi!
MARIA: Shida gani?
ISSA: Nimepata mtihani wangu, nimekuta kuna sehemu nimekoseshwa, sasa si unakumbuka mwalimu alisema usahihi tukafanye kwa aliyepata 15?
MARIA: Ndio, kwahiyo unatakaje?
ISSA: Nataka nimjue aliyepata 15 ili nikafanye usahihi.
MARIA: Mh!
ISSA: Vipi?
MARIA: Frank ndiye mwenye hiyo 15.
ISSA: Frank yupi, yule pasua kichwa?
MARIA: Habari ndo hiyo!
Issa baada ya kuambiwa hivyo aka kata simu, Maria akawa anacheka tu, Alijua Issa hawezi kukaa meza moja na Frank, haitowezekana.
****

SEHEMU YA 30



Frank mida ya saa 2 usiku akaamua kwenda kupata msosi mgahawani, akatafuta mgahawa uliojitenga akaingia, cha kushangaza akakuta wateja ni wengi ambao 100% walikua ni wanachuo, akajiuliza
"Mh itakua wana chakula kizuri, mbona watu wengi sana hadi m bele sioni ”
Akaelekea sehemu ya kuagizia vyakula, akaagiza ugali samaki kisha akatafuta meza akakaa akisubiri chakula alichoagiza.
Issa na Meshack nao wakawa wanaelekea kwenye mgahawa ule ule, hawakujua kama Frank yupo huko. wakiwa njiani Meshack akauliza;
MESHACK: Oya ulimcheki Maria akupe jina la aliyepata 15?
ISSA: Yah! ila achana nae.
MESHACK: Niachane nae kivipi?
ISSA: Eti aliyepata 15 ni yule chizi tuliyempa swali! MESHACK: Nani! yule paka?
ISSA: Huyo huyo, alafu yule dem Love kaniambia ili anipe jibu basi nami nimpe jina la aliyepata 15.
MESHACK: Mh! sasa Love na yule jamaa wapi na wapi?
ISSA: Yani hapo ndo hata Mimi sielewi.
MESHACK: Mpigie Love!
ISSA: Wa nini sasa?
MESHACK: Mpe ofa ya chakula, aje mgahawani mdanganganye aje umpe jina la aliyepata 15.
ISSA: Alafu akija?
MESHACK: Akija unamwambia akupe kwanza jibu lako nawe umtajie jina la aliyepata 15.
ISSA: Ah! we jamaa mbona una akili sana alafu pepa umepata 2....(wakacheka wakigongeshana mikono)
Basi Issa bila kuchelewa, akampigia Love wakutane mgahawani, kwakuwa aliambiwa atapewa jina la aliyepata 15 love akakubali, akaenda mgahawani.
*******
MGAHAWANI:
Ndani ya mgahawa kulikua na wanachuo wengi , Frank alikua amekaa kwa pembeni akila ugali wake. Bila kutambua kumbe pembeni ya Frank kulikua na watu watatu ambao ni Love, Issa na Meshack. Wao walikua wanasubiri chakula walichoagiza, wakawa wanapiga stori mbili tatu;
LOVE: Issa nitajie basi aliyepata 15!
ISSA: Subiri mbona una haraka, tule msosi kwanza. MARIA: Mmh! jamanl, jina tu hadi chakula?
ISSA: Kwani wewe huyo aliyepata 15 unamtaka wa nini?
MARIA: Nina shida nae binafsi.
ISSA: (akacheka) ah ah aah!
MARIA: Unacheka nini?
ISSA: Hamna kawaida tu!
Sasa Love baada ya kuangaza angaza macho si akamuona Frank kwa pembeni, akashtuka na kusimama, sura ilishambadilika, alichukia, hakuweza kukaa tena na mpinzani, mtu hasiyempenda hata kumuona, yaani ni bora asile chakula alale na njaa kuliko kula mgahawa mmoja na Frank Mgahawa ulishakuwa mchungu, akaona ni bora aondoke;
ISSA: Vipi wewe mbona ghafla umebadilika! unataka kwenda wapi?
LOVE: Humu ndani siwezi kukaa, samahan naondoka.
ISSA: Sawa, lakini mbona ghafla?
LOVE: Siwezi kula sehemu moja na yule mtu...
(Issa na Meshack wakageuza macho kufuata kidole cha Love, si wakamuona Frank yupo bize na msosi, wakashtuka)
ISSA: Kwahiyo unaondoka kisa yule jamaa?
LOVE: Ndio, yani sitaki hata kumuona?
ISSA: Kama hutaki mbona unamtaka aliyepata 15?
LOVE: Una maana gani?
ISSA: Uyo jamaa ndiye aliyepata 15 ya uchumi!
Love macho yakamtoka!

ITAENDELEA
Whatsapp napatikana kwa 0768315707
 
SEASON 02

TAMTHILIA: MTU ALIYETHIBITISHWA KWA MAISHA YANGU
CERTIFIED PERSON OF MY LIFE (CPL)
(31-35 )

WHATSAPP
0768315707

SEHEMU YA 31

ISSA: Kama hutaki mbona unamtaka aliyepata 15? LOVE: Una maana gani?
ISSA: Uyo jamaa ndiye aliyepata 15 ya uchumi!
LOVE: Nini!? (macho yalimtoka)
ISSA: We si ulimtaka mwenye 15, ndo huyo sasa!
LOVE: Yani 15 ya uchumi ndo kapata huyo?
ISSA: Sasa kumbe ulijua nani?
LOVE:Hapana siamini, na kama ni huyo, kwaheri, siwezi kukaa humu..
ISSA: Kisa huyu jamaa hata chakula hutaki?
LOVE: Sio chakula tu, hata mgahawa nauchukia... (Love akaanza kuondoka kweli, lakini huku nyuma Issa akawa anamfuata hadi nje)
ISSA: Love! Love...
(Love akasimama na kugeuka)
LOVE: Nini?
ISSA: Love basi nipe hata jibu langu!
LOVE: Jibu la nini?
ISSA: Kama umenikubalia.
LOVE: Sikiliza Issa, chagua moja nikujibu sahizi Jibu ambalo hutolielewa au uniache nikaendelee kufikiria? (Issa akafikilia akaona akileta ubishi atatoswa)
ISSA: Basi mama nenda tu kanifikirie! (aliongea kwa huzuni).
Love akaondoka akamuacha Issa akirudi ndani mgahawani, Issa alionyesha kuchukia Sana.
MESHACK: Usimlaumu dem, mlaumu huyo chizi.
ISSA: Alafu ili jamaa kila siku linaniharibia mishe zangu, yani ili dawa yake ipo jikoni!
Frank alikula na kumaliza akaondoka. Yeye hakujua kama kuna Issa na Meshack mule ndani, hakuwaona.
********
Huku nyuma, Happy hata njaa ilikua haiumi, baada ya kuona njia zote zimefeli akaona aamie mtandaoni. "Siwezi kushindwa kitu kwenye ulimwengu huu wa mitandao1' alijisemea happy
"Yani kutwa naumiza kichwa kuzitafuta sheria za mapenzi, sasa leo nazitafutia mtandaoni" aliendelea kujisemea huku akionekana kuwa bize na simu.
Akaingia google, akaandika "Sheria za mapenzi" alafu akabonyeza neno "tafuta", zikatokea makala nyingi ambazo zilizungumzia mapenzi, Happy alitabasam. Akaona moja imeandikwa hivi "ZIJUE SHERIA KUU TANO ZA MAPENZI" haraka haraka Happy akabonyeza kitufe na sheria zikafunguka, akaanza kuzisoma;
"Katika maisha mapenzi ni moja ya sehemu ambayo mwanadamu aliumbiwa ili ayaishi. Kila binadamu anaishi katika mapenzi. Mapenzi ndio nguzo kuu iliyowekwa ili watu wazae na kuifurahia dunia.
Mapenzi yana raha sana asa ukimpata mtu mnaye endana.
Lakini pia mtu mmoja anaweza akamtengeneza mwenzie katika mapenzi. Hivyo basi ni vizuri watu wakapendana, lakini sio lazma umpate anaekupenda ili awe mpenzi wako, kwa sababu kuna sheria zimewekwa na zipo ambazo unaweza kuzitumia kumbadilisha asiekupenda na akakupenda daima.
Wataalamu walisema "Maendeleo ya watu yasipotengenezwa na jinsia mbili tofauti, yapo kwenye h atari" hivyo basi mapenzi ni muhimu sana katika kujenga mafanikio ya maisha. Watu wengi wanapenda, lakini hawajui jinsi ya kupenda, unaweza kumpenda anayekupenda na akakukataa, pia unaweza kumpenda asiyekupenda na akakukubali, hii ni kutokana na sheria au mbinu za kimapenzi. Zifutazo ni sheria za mapenzi ambazo ukizitumia utapata unachokitaka;

SEHEMU YA 32


1. Mchunguze. Mchunguze kama ni sahihi kwako, sio kila unayempenda anafaa kuwa na wewe, kuwa makini usije penda pabaya.
2. Kuwa nae karibu. Hapa jifanye kama humpendi, mchukulie kama rafiki tu, shirikiana nae katika mambo mbalimbali.
3. Mpe furaha na muonyeshe furaha yako. Hakikisha anaona umuhimu wako, yani muonyeshe kuwa wewe ni sehemu ya furaha yake, pia onyesha ni jinsi gani uwepo wake unakupa sana furaha... atajihisi mtu m bele yako, atajiona bora.
4. Muonyeshe hisia kwa vitendo tu. Hakikisha humwambii kitu, wewe Fanya vitendo, lakini fanya vitendo vile ambavyo havitakuharibia heshima mbele yake, mfano unaweza kumtumia meseji nzuri za mahusiano n.k
5. Mwambie ukweli. Baada ya kumuonyeshea vitendo lazima utaona na kugundua kama ana hisia na wewe au la, na ukigundua ana hisia usicheleweshe, ongea pale pale. Mwambie ukweli kwamba unampenda sana, hakika kama ni wako utampata, kumbuka: unaweza kumpata hata kama hakuwai kukufikiria, hiyo ni kwasababu ya kufuata sheria za mapenzi. Usikurupuke, fuata sheria.
Happy akamaliza kuzisoma, akatabasam na kujisemea, "kumbe nilikua na haraka haraka, haya mambo ya hatua bwana, Mimi nae aah!. Akavuta shuka na kulala, akaona kazi ishaisha.
DARASANI:
Ikawa ni siku nyingine asubuhi wanafunzi walikua wengi darasani, lakini kelele pia zilikua ni nyngi, hiyo ni baada ya cr kutangaza kwamba kipindi hakipo. Loveness, Maria, Issa, Happy, Meshack, bila kusahau Frank walikuwemo mule ndani pamoja na wanafunzi wengine.
Ni kawaida kwa wanachuo kufurahi na kuondoka mara tu kipindi kinapoahirishwa. Lakini siku hiyo wanafunzi wengi walibaki darasani, hii ni kutokana na CR kutangaza kwamba muda ule wautumie kujadili maswali yanayowasumbua katika somo la biashara, somo ambalo kila mtu alikua akilipenda lakini lilikua gumu sana kupita masomo yote. Mwanafunzi mmoja akasimama na kuongea;
MWANAFUZI: Jamani tulieni nina ombi, nafikiri maswali ya biashara yanayosumbua yapo mawili. Watu wengi humu ndani tumejaribu kuyafanya tumeshindwa, tukisema tuyajadili kwa pamoja ni vizuri lakini mimi naona kama kuna mtu anayafahamu ni bora angepita mbele akatuelekeze.
(Alimaliza kuongea yule mwanafunzi, hoja ambayo kila mtu alikubaliana nayo, lakini ugumu ulikuwa ni nani apite mbele akaelekeze wenzie, na je maswali hayo anayajua?. Kila mtu alikaa kimya, waliokaaa mbele waligeuza shingo nyuma kuangalia kama kuna mtu atajitolea, lakini wapi.... Kila mtu hajui)
CR: Jamani wakati tunamsubiri mtu wa kutuelekeza, naomba niyasome maswali yanayosumbua;
1. Kwanini mtu anafeli katika biashara?
2. Elezea umuhimu wa vikundi vya kibiashara.
(CR akamaliza kusoma maswali na kuwauliza wenzie kama kuna mtu anayafaham basi apite mbele akaelekeze).
Loveness alikua amekaa karibu na Happy, akamuuliza;
LOVE: Vipi Happy unayafaham hayo maswali?
HAPPY: Ah! wapi yani pale sijaelewa kitu! vipi wewe unayajua?
LOVE: Kama wewe ninaye kuaminia unashindwa, mi nitawezea wapi?
(wakacheka).


SEHEMU YA 33

Issa nae kule nyuma alikokaa baada ya kusomewa maswali akaona giza tu, ilibidi awaulize wenzie;
ISSA: Maria wewe sikuhizi ulivyo na akili, hayo maswali yanakushinda?
MARIA: Wee! ningekua na akili si ningeringa.
ISSA: Meshy na wewe huelewi kitu?
MESHACK: Kaka pale chenga tuu!
ISSA: Du!
Frank baada ya kusomewa yale maswali aliyaelewa, aliona ni yakawaida tu, ila hakutaka kwenda mbele akihofia matatizo ambayo kila akiongea uwa yanatokea. Akaamua kukaa kimya.
Lakini ghafla kuna mtu akasimama, alionekana kuwa smati sana, na kwa haraka haraka alioneka mtu wa kupenda sana sifa. Kwanza baada ya kusimama tu akatengeneza tai yake vizuri alafu akajidai akifunga mkanda wake, baada ya kujiona yupo poa akaongea;
"Wanachuo wenzangu, Mimi kwa jina naitwa yumason, ukipenda unaweza kuniita "YUMA"
(Wanachuo wakacheka, Yuma akaendelea kuongea)
YUMA: Ah! kwa sisi wafanyabiashara hayo maswali ni marahisi sana, baba yangu ni mfanya biashara mkubwa, baadhi ya biashara zake Mimi ndo nazisimamia. Sasa basi kila mtu awe makini nikiwa nawaelekeza haya maswali.... (aliongea kwa kujitapa, alafu akapita mbele..)
YUMA: Kabla sijaanza kuongea naomba kila mtu ashike peni na daftari kwasababu majibu yangu yanaweza yakakufanya ufahulu mitihani yote ya dunia.
(Aliendelea kujitapa, baadhi ya wanachuo akiwemo Issa na Meshack walionyesha kumkubali sana jamaa., nao wakatoa peni na daftari. Happy na Love walikua wakitabasam huku wakitaman sana kumsikia pointi za Yuma. Frank pia alionekana kutulia akisubiri kuona na kusikia maelezo kutoka kwa Yumason)
YUMA: Nadhani kila mtu amejiandaa kuandika. Sasa naanza na swali la kwanza. Mtu anafeli katika biashara kwa sababu zifuatazo 1. Ujinga. Watu wengi ni wajinga katika biashara, wapo wapo tu. 2.
Umaskini, sasa kama mtu huna fed ha za kutosha utashindwaje küfeli?. 3. Woga, watu wanaogopa plesha za biashara. 4. Biashara ndogo, mfano biashara ya baba yangu ni kubwa, haiwezi kufa kamwe. 5. Kuwa smati, mfano kama Mimi hapa, Mimi siwezi küfeli katika biashara kwasababu nipo smati. Lazma mfanyabiashara upige suti kali, ndio maana wengi wanafeli kwasababu hawajipendi.
(Yuma alimaliza swali la kwanza, maelezo ambayo kuna kelele za baadhi ya watu zilisikika akiwemo Issa, alionekana kumpigia makofi jamaa)
YUMA: Nadhani mmenipata swali la kwanza, sasa najibu lile la pili..
(Wanachuo kimya, sasa sijui walielewa sana au la)
YUMA: Jamani kuna mtu hajui umuimu wa vikundi kweli? mbona rahisi tuuu, "vikundi vina faida zifuatazo I.Ushirikiano, watu wanafanya kazi pamoja. 2. Mawasiliano, watu wanatengeneza undugu. 3. Kazi zinaisha h a raka, faşta tu yani. 4. Pesa nyingi, kwa sababu mnachangishana. 5. Faida kubwa, mkiwa wengi lazma mpate faida kubwa." Mimi nimemaliza asiyeelewa anyoshe mkono (aliongea akiwa anarudi kwenye kiti chake).
Wanachuo walikua kimya sana. Ukirnya huo ulimaanisha kila mtu amekubaliana na maelezo ya Yuma, baada ya ukirnya wa muda CR akaongea;
CR: Jaman tunakubaliana na pointi za Yuma? kama tunakubaliana basi hakuna cha zaidi mnaruhusiwa kuondoka...
(Watu walikubali na wakaanza kusimama ili waondoke)
FRANK: Jamani subirini kabla hamjaondoka!
(Kila mmoja macho kwa Frank)


CR: Jaman tunakubaliana na pointi za Yuma? kama tunakubaliana basi hakuna cha zaidi mnaruhusiwa kuondoka...
(Watu walikubali na wakaanza kusimama ili waondoke)
FRANK: Jamani subirini kabla hamjaondoka!
(Kila mmoja macho kwa Frank)
llibidi watu wote wasimame na wawe kimya kusikiliza Frank alitaka kusema nini, kila mtu macho kwa Frank, macho ambayo kwa tafsiri yalikua yakiuliza "vipi wewe unataka kusemaje?"
Issa baada ya kuona Frank amesimamisha watu, akawa anaongea kitu na Meshack;
ISSA: Nilitaka kushangaa, yani tutoke hivi hivi tukiwa na furaha?
MESHACK: Si ndo hapo, alafu hivi yule jamaa we unamuelewa?
ISSA: Tangu lini uwa nawaelewa watu wenye mambo ya kimama, mfano kama pale kashaona wivu kwa Yuma... Ameona watu wamezipenda point za Yuma, anataka kuharibu.
Frank baada ya kuona macho yote yanamuangalia, akafikiria akajua kuna watu lazma wamekasirika, aliwaza kuwa makini kwenye maelezo kwasababu watu walishakubaliana na point za mwanzo za Yuma. Kuna jamaa mmoja aitwae tarick akaona wanacheleweshwa, kwa hasira akaongea;
TARICK: Oya jamaa tunakusubiri wewe, watu tuna mishe zetu.
ISSA: Alafu kama vipi usiongee tu, sio lazma kila siku uongee....
Frank akafikiria tena;
"Au nisiongee tu, maana watu wenyewe hawana hata mpango na Mimi. Lakini hapana ni muhimu kumrekebisha aliyekosea" baada ya mawazo hayo akaanza kuongea;
FRANK: Jaman samahanini, najua kila mtu alishaanza kuondoka mara baada ya maelezo ya Yuma. Mimi binafsi nimependa sana pointi ambazo Yuma ameziongea, pongezi kwake. Lakini kumbukeni, tulichokua tunatakiwa kukifanya hapa ni majadiliano, lazma tukubaliane kwamba vitu alivyoongea Yuma ni majibu sahahi!. Ebu fikirieni, je likitoka swali kwenye mtihani tujibu kama alivosema Yuma?. Nilichogundua humu ndani watu ni wazembe kufikiria, pia hawapendi kuchangia mada, na wanakata tamaa mapema.
(Maneno hayo ya utangulizi ya Frank yalitosha kabisa kumfanya kila mtu mule ndani akae tena kwenye kiti chake na kuwa msikivu, wenye masikio walitulia na kuanza kusikiliza. Frank akaendelea)
FRANK: Kwa kifupi sikutaka kuongea, lakini humu ni darasani, hiki ni kipindi, na ili tulifanyalo ni somo. Sasa Kama mtu unafahamu kitu na hutaki kuongea kwa faida ya wenzio nadhani hata mungu hapendi. Mimi binafsi nina point zangu ambazo naziona kuwa ni sahihi kat ika yale maswali mawili. Sijapenda sana muondoke na maelezo hayo hayo ya Yuma, ila kama unaona nakupotezea muda wako unaweza kuondoka!
(Baada ya Frank kusema haşiye teyari aondoke, Issa na Meshack bila kuchelewa wakaondoka. Kila mtu akawa anashangaa yaliyokuwa yanaendelea. Frank hakusita wala kuogopa, akaendelea kuongea)
FRANK: Nikianza na swali la kwanza, "kwanini mtu anafeli katika biashara", ili ni swali ambalo kila mtu akivuta picha kichwani, picha ya namna biashara ilivyo anaweza akalijibu. Mimi kwa uelewa wangu, nilisoma makala ya mtandao wa "forbes" na wao wakaelezea sababu za mtu küfeli kibiashara kama ifuatavyo;
1. Kutoshikamana na mahitaji ya wateja (not in touch with customers needs). Lazima ujue wateja wanataka nini, huwezi kufanikiwa kibiashara kama tu bidhaa unazouza sio sahihi kwa mteja
2. Kushindwa kuongoza biashara. (leadership failure). Kama hauna uwezo wa kumiliki biashara hakika hutofika popote, lazima ujue kutoa maamuzi na kuwaza mafanikio.
3. Mfumo wa kibiashara usio na faida (unprofitable business model). Lazima kuwe na faida ili biashara iendelee, huwezi kwenda mbele kibiashara kama biashara haina mapato, tengeneza njia nzuri zitakazokupa pato la biashara yako. Unaweza ukawa na biashara nzuri, lakini usipokuwa na mipango mizuri ya kukupa faida, utaanguka.
4. Mfumo mbovu wa kumiliki fedha (poor financial management). Ni muhimu ujue pesa yako umeitoa wapi na unaipeleka wapi, itunze pesa yako na uwe na njia sahihi za kuwekeza pesa ili zikusaidie mbeleni
5. Kukua kwa haraka sana na kujitanua zaidi ya uwezo wako (rapid growth and over expansion), biashara ni mdogo mdogo, usianze kuwaza mbali sana wakati karibu panakushinda, lazima ujue kukimiliki kidogo ili kikubwa kisikupe shida., watu wengi wanatumia fedha nyingi kukuza biashara ambazo hawajui wateja sahihi wa hizo biashara,
ukifanya hivyo utafeli.
Jamani hizo sababu kuu tano ambazo ni lazima uzifahamu wewe kama mfanyabiashara, lakini pia kuna sababu zingine Kama vile
6. Kuto kujitangaza 7. Eneo mbaya la kibiashara (poor location) 8. Kutokuwa na malengo au mipango, n.k.


SEHEMU YA 34


(Wakati Frank anaendelea kuongea, watu wengi walionekana kuelewa sana na kumkubali, walikua bize wakiandika huku kila mmoja akimuona Frank Kama mkombozi. Jambo lile lilimkera sana Love, hakupenda kabisa watu wamsikilize Frank, japo hata yeye maelezo ya Frank yalimuingia lakini bado alikua na hasira. Pasipo kutegemea Love akasimama, akachukua mkoba wake akitaka kuondoka)
HAPPY: (Akimshangaa Love)) We Love unaenda wapi?
LOVE: Ah naondoka zangu, naenda hostel!
HAPPY: Si usubiri kwanza tusikilize point za swali la pili?
LOVE: Yani nikae kutwa nimsikilize huyo mjinga?
HAPPY: Mmh!
Love akaondoka, akaacha watu wakimshangaa. Lakini kwasababu walimfahamu waliona ni kawaida.
Akatoka hadi nje ya mlango, sura ilishambadilika, lakini alipofika nje akajiuliza kidogo;
"Hivi yule Frank mbona ana akili sana, inafikia hatua sielewi ni kwanini namchukia. Alafu kumbe kama yeye ndiye aliyepata 15, inamaana yeye ndiye anayemtesa Happy? Mmh hapana bwana"
Akiwa anaendelea kujiuliza pale mlangoni mara akasikia ndani watu wakipiga makofi na kelele za shangwe.
"Eh vipi uko ndani" Alijiuliza Love na kuanza kurudi tena ndani, akashika kitasa kutaka kuingia lakini mawazo yakamjia ghafla;
"Niliondoka kwa jazba, nikirudi tena si watanishangaa, nitaonekana sijielewi, mh sijui wanafurahi nini ila lazma atakuwa ni huyo Frank, bwana wee nikiingia nitapata aibu bure"" alijiongelesha love kisha akaamua kuondoka kuelekea hostel.
Kule ndani makofi yalipigwa muda wote, watu walichangamka tena, hata Yuma akaona sio Mahala sahihi kukaa nae akaondoka kwa hasira.
Lakini kuondoka kwa watu wale hakukuwa mwisho wa Frank kujiamini na kushusha vitu, aliongea mambo ambayo kila mtu mle ndani alibaki anashangaa uwezo wa kiakili ya Frank. Uso wa Happy ulipambwa na tabasam pana, Happy aliachwa hoi, alimuona Frank ni kama mwanaume sahihi wa maisha yake, akajisemea;
"Sheria nimeshazipata, umebaki wewe tu "
FRANK: Nadhani kila mtu amenipata kwenye swali la kwanza, tuje swali la pili, ili nitaelezea kwa ufupi tu. "umuhimu wa vikundi vya kibiashara"
(Wanachuo walikua makini sana kumsikiliza, kila mtu aliandika. Frank akaendelea)
FRANK Vikundi vya kibiashara ni vikundi vinavyotokea baada ya watu kadhaa wenye kufahamiana na wenye malengo sawa, kuungana pamoja kibiashara ili waweze kutengeneza faida pamoja au kutoa huduma pamoja. Hii utokea pale ambapo labda watu katika jamii wanawaza kufanya biashara lakini hawajui jinsi ya kuanza, au watu wanaamua kufanikiwa pamoja, au watu wanaamua kutatua changamoto za jamii kwa pamoja.


SEHEMU YA 35


Sikuhizi vikundi vingi vinaanzishwa katika jamii, mfano vikundi vya kina mama, vya wazee, vya vijana n.K ambavyo vinasajiliwa na kutambulika na kata, halmashauri au manispaa. Umuhimu wa hivyo vikundi ni kama ifuatavyo;
1. Ni rahisi kupata mikopo. Serikali inatenga fedha maalumu kwa ajili ya vikundi hivvyo.
2. Rahisi kupata mtaji, watu Wanachangishana pesa kwa kiasi kidogo alafu wanapata pesa nyingi, tofauti na ukiwa pekeako.
3. Mnabadilishana mawazo ya kibiashara, mfano kama wewe una moja, mwenzio ana mbili mkiunganisha pamoja inakuwa tatu.
4. Ni rahisi kufanikiwa. Katika maisha ukishindwa kutoka pekeako basi toka na wenzio.
5. Mgawanyo wa majukumu, mnaweza kufanya biashara nyingi kwa kipindi kimoja, kwasababu mtagawana majukumu. Zipo faida nyingi za vikundi, hizo ni baadhi tu... Asanteni kwa kunisikiliza.
Frank alimaliza kuongea, bila kutegemea wanafunzi wenzie wakasimama na kumpigia makofi. Wakati wanafunzi wanafurahia maelezo ya Frank, Tarick alionyesha kuchukia, nae akatoka nje huku akijisemea;
"Huyu jamaa akiachwa atatusumbua, lazma akomeshwe"
Wanachuo baada ya kumpigia makofi Frank, wakakaa chini na mmoja akauliza swali;
MWANAFUNZI WA 1: Je kipi kitatokea kama watu katika vikundi watagombana?
FRANK: Inaweza kutokea watu wakagombana, lakini siku zote biashara iko mbali na mmiliki, ugomvi wao hautoweza kuiathiri biashara, na kwa kulitambua hilo, Kikundi kinaposajiliwa lazma kiwe na katiba zake za uongozi ili kuweza kutatua changamoto kama hizo.
MWANAFUNZI WA 2: Na je, nani ataongoza Kikundi? FRANK: Uongozi upo katika vikundi. Lakini uongozi hauna mahusiano na mgawanyo wa fedha. Kama nilivyosema kila kitu kinaendeshwa na katiba na mikakati mtakayojiwekea. Mfano mnaweza kumchagua muhasibu, Mwenyekiti, n.k.
MWANAFUNZI WA 3: Nifanye nini ili nisifeli kibiashara?
FRANK : Ni rahisi tu, bidhaa bora kwa wateja, ongoza vema biashara yako, miliki fedha vizuri, jitangaze kibiashara, akikisha biashara yako ipo mahala sahihi, fanya mambo pole pole na kwa mipango, hakikisha biashara inakupa faida, n.k.
Maswali yaliisha, watu wakasimama tena na kumpigia makofi Frank, huwezi amini, Happy uzalendo ulimshinda, alitoka na kwenda kumkumbatia Frank, alafu kisha

ITAENDELEA WHATSAPP
0768315707
 
SEASON 02

TAMTHILIA: MTU ALIYETHIBITISHWA KWA MAISHA YANGU
CERTIFIED PERSON OF MY LIFE (CPL)
(36-40 )


SEHEMU YA 36

Akamwambia...
Maswali yaliisha, watu wakasimama tena na kumpigia makofi Frank, huwezi amini, Happy uzalendo ulimshinda, alitoka na kwenda kumkumbatia Frank, alafu kisha akamwambia...
HAPPY: Frank nimeshindwa kuvumilia, niache tu nikukumbatie1' (alizungumza pole pole III watu wasisikie)
Frank alishangaa sana, hakutegemea tukio lile, maana yeye alijua Happy atakua amechukia tokea lie siku amedondosha sahani za chakula baada ya kumkuta na Maria pale mgahawani. Kumbe hakujua Happy alishasahau kila kitu, ye ye aliwaza kutimiza sheria tu mambo yaishe.
FRANK: Kwahiyo hizi ndizo sheria ulizojifunza? au hujui kuwa tuko darasani watu wanatuchora tu? 11 (aliongea Frank huku akitumia ujanja wa kujitoa kifuani kwa Happy)
(Alifanya hivyo ili wanachuo wengine wasielewe kitu, na kwakuwa ni mambo ya chuo watu walichukulia kawaida tu)
HAPPY: Nisamehe sana, sitorudia (alijibu akijiona mkosaji, nae akajitoa na akarudi kukaa kwenye kiti)
Bahati nzuri wakati Happy anamkumbatia Frank, Maria alikua amejiziuka kuongea na mwanafunzi mwenzake, hakubahatika kuona ule mkumbato, alipitwa.
Ilibidi CR apite mbele ya darasa na kuwashukuru wanafunzi kwa ushirikiano, alimshukuru sana Frank, hata wanafunzi wengine walipenda kilichofanyika, baada ya hapo kila mtu alichukua njia yake.
HOSTEL:
Issa mkono shavuni, kichwa kilijaa hasira, akili ilijazwa na chuki, alikasilika mno. Akamtazama Meshack na kumuuliza;
ISSA: Kaka ina maana jamaa ndo tumemshindwa? MESHACK: Labda wewe, ila Mimi siwezi kumshindwa.
ISSA: Sasa tunafanyaje?
MESHACK: Test nyingine lini kwani?
ISSA: Test ya biashara juma 4 wiki ijayo!
MESHACK: Tufanye kitu....(aiongea Meshack huku uso wake ukionekana kuchukia, na alionekana akiwaza jambo))
ISSA: Sikiliza Meshy, yule jamaa kimasomo tutamshindwa, tutafute mbinu nyingine.
MESHACK: Sawa! unajua nini Issa, yule dawa ni ndogotu.
ISSA: Dawa ipi?
MESHACK: Kwani hapa chuo hakuna wahuni wanaopiga ngumi, wanaokula vyuma, wenye miili jumba?
ISSA: Wapo wengi sana, kuna lile jamaa linaitwa Anord, wenyewe wanaliitaga "Şamata", jamaa nasikia ni mcheza kareti na kabla hajafika chuo alitaka kuwa bondia,.... Alafu kuna mwingine anaitwa "Kisura", jamaa flani hivi white, usimuone shombe shombe vile, anapiga ngumi Yule!
MESHACK: Mmh! labda huyo Anord, ila kisura sidhani!
ISSA: Hivi unaonaje tukaongee na Yuma, maana Yuma anaonekana ana pesa, lazma dili za mjini anazijua.
MESHACK: Hapo sasa umeongea, inabidi tuwe kundi, yani jamaa ale vitasa hadi ashindwe kufanya mtihani.
Happy baada ya kutoka darasani alionekana kuwa na furaha sana, akaamua kurudi hostel ili akapumzike, alipofika akamkuta Love yupo kitandani anachati.
LOVE: Naona somo lilinoga uko, furaha kama zote! HAPPY : Yani acha tu! kuna watu wanajua bwana!
LOVE: Mmh! alafu yale makofi mlipiga ya nini?
HAPPY: We si uliamua kususa kipindi, hupaswi kujuaa (aliongea Happy kama masihara akiwa anacheka))
LOVE: Niambie basi, kwanini mlipiga makofi? (aliongea kiupole kwa huruma)
HAPPY: Bibi wee umekosa sana mambo, yani yule mtu hafai (alimsifia Frank, hali iliyomuacha Love macho kodo)
LOVE: Alafu we Happy, kumbe alopata 15 ndo Yule Frank?
HAPPY: (akacheka) Ah ah ah! mi sijuii! (Sasa hapo Happy aliongea kwa Maringo kweli, utafikiri huyo Frank kashampata)
LOVE: Kuwa siriazi basi Happy!
HAPPY: Jamani misijuii!
LOVE: Mmh! kwahiyo yule ndo anakusumbua kimapenzi?
HAPPY: Love nimesema Mimi sijui...alafu sio yule anayenisumbua! (alikataa uso ukiwa siriazi)
LOVE: Kama ndo yule, hivi umempendea nini shoga angu?
HAPPY: Bibi wee usinisumbue.
(Happy kwa hasira akasimama na kutoka nje, akaamua kurudi tena alikotoka, maswali maswali ya Love hakuyapenda. Huku nyuma akamuacha Love akishangaa tu)
LOVE: Eeh yamekuwa hayo!
Issa baada ya kupanga mipango namna ya kumthibiti Frank, akaamua kumpigia Loveness simu ili ajue hatma ya ombi lake kama limekubaliwa au lah!. Moyoni akajisemea
"Ila Loveness ni mzuri sana, yani hapa chuo hakuna binti mzuri kama Love, mtoto ana kila kitu, sura, shepu, mwili 8, huko nyuma japo sio sana lakini kajaliwa kitu cha haja" aliwaza akiwa anatabasam Akaendelea kuwaza;
"Ndio maana ana maringo, ujue awa mabinti wazuri ni haki yao kuringa kwa sababu sio kila mwanaume ana nafasi kwenye moyo wa binti mzuri kama yule. Ila Mimi ni handsome hawezi kunikataa, kwanza nipo smati, vipesa vidogo vidogo havinishindi, sasa namkosaje kwa mfano" Issa alijiona bora.
Simu iliita Mara ya kwanza hadi ilikata, ikaita tena tena ikakata.
"Mmh huyu demu nae maringo yamezidi, hata kama ni mzuri lakini anajishaua kinoma1' aliwaza Issa..


SEHEMU YA 37

"Sasa napiga mara ya mwisho, kama hapokei napotezea hadi jioni " alijisemea na kupiga tena. Simu iliita na mara ikapokelewa;
LOVE: Hello Issa....
(Issa alichanganyikiwa kwa sauti tu)
ISSA: Hello Love, mambo vipi?
(Hapo Issa alilala kabisa kitandani na kuiseti sauti yake yenye bezi kidogo)
LOVE: Poa tu, eeh nambie!
(Sasa Issa akawaza, "wakuniambia ni wewe mwenye majibu yote, Mimi mbona nilishakuambia") ISSA: Loveness!
LOVE:Abeeü!
ISSA: Jibu langu mama, nakuomba basi.
LOVE: Mmh Issa mbona una haraka hivyo!
ISSA: Sio haraka Love, nataka kujua hatma yangu.
LOVE : Hatma ya nini?
ISSA: Kama wewe ndiye au la!!, hivi unajua kama nakupenda sana?
LOVE: Mi sijui eti! (aliongea kwa mapozi)
LOVE: Ndio ujue sasa!, yani hapa sijisomi kabisa, nijibu basi love!
(Sasa Love akafikiria akaona kumjibu ni ngumu sana, akaona ni kutumia maarifa na ujanja tu)
LOVE:Alafu Issa nikuulize swali?
ISSA: Niulize tu hata usijali (alijibu Issa huku akitaman sana kulisikia hilo swali)
LOVE: Eti, hivi kwa nini wateja uwa wanamkimbia mfanyabiashara mmoja na kwenda kwa mwingine? (Issa akafikiria akaona huko sasa kwingine)
ISSA: Dah sasa Love ili swali limeingiaje huku?
LOVE: Nijibu basi kama unalijua!
ISSA: Kwani ni la muhimu sana?
LOVE: Ndio, yani muhimu kweli.
ISSA: (akaona asije kupata aibu) Sawa nipe dakika 5 nakutumia majibu...
(Issa aka kata simu, bila Shaka alielekea mtandaoni kutafuta majibu ya swali).
Love alifurahi maana hicho ndicho alichokitaka, akajisemea;
"Kumbe dawa yako rahisi tu, we unadhani unaweza kukubaliwa kirahisi na haraka haraka hivyo " Love akajiona mshindi.
DARASANI:
Happy baada ya kutoka hostel akarudi chuo , akatafuta darasa ambalo halina mtu, aliangaika sana lakini kila darasa aliloingia akakuta watu au mtu akisoma, alichoka.
HAPPY: Mmh sasa nifanyaje, maana sheria ya kwanza inanitaka nimchunguze.
(alijisemea Happy)
HAPPY: Lakini sijamaliza madarasa yote, wacha nikague yote.
(Akaendelea kutafuta hadi akakuta darasa halina atu, akajisemea)
HAPPY: Sasa wacha nimpigie nidanganye kuwa kuna swali limenishinda, akija na uchunguzi ndo utakua umeanza.
(Akachukua simu na kumpigia Frank, simu ikaita na kupokelewa)
FRANK: Hallo.
HAPPY : Hallo mpe.... Hallo Frank., (nusura aseme hallo mpenzi, alijishtukia, akaona asije kuharibu misingi ya sheria)
FRANK: Nambie.
HAPPY: Safi tu, upo wapi?
FRANK: Nipo hostel.
HAPPY: Una kazi?
FRANK: Hapana, nipo tu. Vipi kwani?
HAPPY: Samahani, kuna swali limenishinda hapa, naomba uje unielekeze. (aliongea kwa utulivu mkubwa) (Frank akafikiria akakumbuka amemwambia hana kazi, na akikataa ataonekana kama anaringa flani),
FRANK: Sawa upo wapi?
HAPPY: Nipo chuo hapa, fundikira darasa namba
108.
FRANK: Sawa!
HAPPY: Unakuja?
FRANK: Tufanye hivi, nipe dakika 10. Ukiona kimya ujue siji, hadi baadae.
HAPPY: Mmh sawa
Happy sasa akawa anaomba moyoni hizo dakika kumi zilete anachokitaka, akaanza kuhesabu dakika... Ikapita dakika ya kwanza, yapili, ya 3,4 hadi ya 9. Happy akashusha pumzi, macho yote mlangoni, sheria namba moja ndo ilikua kichwani mwake.
Hatimaye ikafika dakika ya 10. Hakuna mtu mlangoni. Happy akalalia meza, uso ukaleta huzuni. Lakini sekunde zilikua bado, ile anainuka na kutupia macho mlangoni, mwanaume huyo akatokea....

SEHEMU YA 38

Hatimaye ikafika dakika ya 10. Hakuna mtu mlangoni. Happy akalalia meza, uso ukaleta huzuni. Lakini sekunde zilikua bado, ile anainuka na kutupia macho mlangoni, mwanaume huyo akatokea...
Happy akaachia tabasam murua. Frank akaenda moja kwa moja na kukaa kiti cha mbele ya Happy, wakawa wanatazamana. Happy akaona aibu, akashusha macho chini.
FRANK: Happy..
HAPPY: abee!
FRANK: Vipi?
HAPPY: Poa, nilijua hutokuja!
FRANK: Ah! si nilikuambia dakika 10?
HAPPY: Ndio, unajali sana muda!
FRANK: Sana! mbona darasa zima pekeako?
HAPPY: Lakini hapa niko na wewe! {alijibu akiwa anacheka}
FRANK: Sawa lakini kwanini umechagua darasa lisilo na watu wengi?
HAPPY: Sitaki tu usumbufu.
FRANK: Kumbe! basi sawa. Liko wapi hilo swali lenyewe?
Lakini Happy badala ya kutoa swali, akawa tu anamwangalia Frank, macho yake ni kama yalisema " swali la nini sasa, mimi nakutaka wewe". Nae Frank baada ya kuchunguza akagundua kulikua hakuna dalili za kusoma maana Happy hata daftari hakuwanalo.
FRANK: Happy..
HAPPY: Abee!
FRANK: Mbona huna daftari lolote, au swali lipo kichwani?
HAPPY: Frank..
FRANK: Nakusikilizaa!
"HAPPY: Nisamehe.
FRANK: Kwanini?
HAPPY: Nimekudanganya.
FRANK: Una maana gani?
HAPPY: Sina swali lolote, nimekuita tu uje tupige stori!
Frank akabaki akitabasam. Happy alishangaa, alijua baada ya kuongea hivyo labda Frank atakasilika na kuondoka, lakini mwanaume hata hakuonyesha dalili za kuondoka wala kuchukia. Happy alifurahi baada ya kumshuhudia Frank akikaa vizuri, tena akionyesha furaha.
FRANK: Sasa Happy... (aliita akiwa anakaa vizuri. macho yakiukagua mwili wa Happy)
HAPPY: Abee!
FRANK: Si ungeniambia tu nije tupige stori kuliko kudanganya, kwasababu mi mwenyewe nilikua mpweke kule hostel!
HAPPY: Wewe mpweke kivipi?
FRANK: Sina mtu wa kukaa nae pamoja tukapiga stori!
HAPPY: Mmh! muongo wewe, si ungemuita hata mpenzi wako mu we pamoja!
FRANK: Huyo mpenzi nimtoe wapi?
HAPPY: Kwamba huna?
FRANK: Ndio sina!
HAPPY: Mmh! na yule wa mgahawani? (aliuliza kimitego)
FRANK: Aah yule ni rafiki yangu mkubwa kama ilivyo kwako tu!
Sasa hapo aliposema kama ilivyo kwako tu, Happy hakupenda, basi akawa mpole, alinyong’onyea, akanywea kabisa. Hapendi aitwe rafiki, yeye urafiki hautaki. ghafla akajikuta anawaza kuitwa rafiki...
FRANK: Happy"""HappyWe happy?
(Happy akashtuka kutoka kwenye mawazo)
FRANK: Unawaza nini?
HAPPY: Sio kitu... Alafu Frank nikuombe kitu? "FRANK: Ktu gani?
HAPPY: Naomba niwe nasoma na wewe kila siku! FRANK: llotu hata usijali, ni wewetuu!
HAPPY: Kweli?
FRANK: Eeh! kwani tatizo liko wapi?
HAPPY: Hata hostel kwako nije?
FRANK: Popote panapofaa tutasoma!
HAPPY: Ila mi hostel kwako naogopa!
FRANK: Unaogopa nini?
HAPPY: Nikikutwa na mpenzi wako je?
FRANK: Mh! Happy, si nishakuambia sina mpenzi zaidi nina marafiki tu!
HAPPY: Aah samahani, nilisahau (alijibu kwa upole) {Maswali yote hayo Happy aliyauliza ikiwa ni kukamilisha sheria namba moja. Akajisemea "kumbe hana mpenzi, basi sawa. Sheria namba mbili nitaanza nayo siku nyingine).
Waliongea mambo mengi siku hiyo, walicheka na kufurahi pamoja. Happy alijiona kuwa mtiifu katika sheria, alifanya mambo kwa umakini pasipo Frank kujua. Frank bado alimchukulia Happy kama ni rafiki wa kawaida tu, akakumbuka hata lile tukio la hostel akaona labda inawezekana Happy alipitiwa tu siku hiyo.
*******
MGAHAWANI:
Jioni ya siku hiyo wanaume watatu ambao walikuwa na hasira na chuki kali, walikusanyika katika meza moja. Ni baada ya kukubaliana kwamba hawataki kuonekana chini ya mtu mwenye sifa darasani. Nao si wengine bali ni Meshack, Issa na mtu mwenye pesa zake, ambaye alisifika kwa kuonga pesa, nae si mwingine bali ni Yumason. Waliamua kujiwekea kikao katika moja ya mgahawa mzuri pale chuoni, ili tu mipango yao iende sawa na kwa siri.

SEHEMU YA 39


YUMA: Kilichoniuma Mimi ni kitendo cha kuaibishwa mbele ya darasa, watu walishazikubali point zangu, lakini jamaa akazikana na kuleta zake, alafu akawashawishi watu wazipende zake.... Nimeumia sanaa. (aliongea Yuma huku akigonga meza ya chakula)
ISSA: Hasira nilizonazo kwa jamaa, ningekua na uwezo ningemuondoa chuo.
YUMA: Hivi haiwezekani tukamuonge ticha jamaa adisco? (aliongea Yuma akimaanisha wakamshawishi mwalimu kwa kumpa pesa amfelishe Frank)
MESHACK: Wazee sikilizeni, haya mambo tufanye kwa siri sanaa, asijue mtu hata mmoja hapa chuoni... Sasa mkianza kuwausisha walimu itakua sio. Jambo la msingi ni kuhakikisha jamaa jumanne hafanyi pepa la biashara. Sasa hapa tupange mipango tufanyaje kama ni kumuwasha ngumi au kumfungia hata mlango.... Yani sijui tumfanyaje.
YUMA: Kwani pepa itakuwa saa ngapi?
ISSA: Saa 2 asubuhi.
MESHACK: Na kama mnavyojua sheria za chuo, mwanafunzi asipofanya pepa mbili mfululizo anafukuzwa chuo.
YUMA: Kwahiyo unataka kusema pepa la juma 4 asipofanya na likija pepa lingine nalo asipofanya, chuo basi?
MESHACK: Ndo hivyoo!
YUMA: Ebu nipe tano!!
(wakagongeshana mikono wakiamini dili limetiki).
ISSA: Sasa wazee, tunafurahi tu bila kujua tutamfanya nini ili asifanye pepa?
YUMA: Usijali hiyo kazi niachie Mimi.... Ameisha huyoo, jumatatu tuonane niwape plani!
DARASANI:
Usiku wa siku hiyo Frank na Maria walikua wakisoma pamoja, ni baada ya kula wakaona waingie darasani wapige pindi... Lakini Frank alionekana hana hamu sana ya kusoma, hali iliyomfanya Maria kumuuliza swali;
MARIA: We leo vipi mbona sio kawaida yako?
FRANK: Aah basi tuu nipo kawaida!
MARIA: Upo kawaida kivipi wakati unaonekana na mawazo kabisa?
FRANK: Usijali tuendelee kusoma!
MARIA: Haya we usiniambie tu ila kumbuka huna rafiki mwingine zaidi yangu (aliongea Maria kwa manung'uniko ya kutaka kuambiwa)
FRANK: Ni kweli, unajua Maria mi sikujuaga kama chuo kunaweza kukawa na watu wenye chuki namna hii, ebu fikiria niliibiwa begi... (kabla hajamaliza Maria akadakia..)
MARIA: Lile begi lako la daftari? kumbe ndio maana sikuoni nalo sikuhizi....


SEHEMU YA 40

FRANK: Hiyo haitoshi... Si uliona mwenyewe yaliyotokea kwenye majadiliano darasani?
MARIA: Niliona! ujue watu sijui wakoje, hawapendi kuambiwa ukweli, lakini Mungu yu pamoja nawe kwasababu wao walitoka darasani kwa chuki na hasira zisizo na faida, lakini hawatambui kuwa chuki zao zinaweza kuwaathiri wao wengewe. Ebu fikiria kama yale uliyoyaongea yakitoka katika mtihani wa mwisho?
FRANK: Mimi siwaombei mabaya, lakini yale mambo muda mwingine uwa nayawaza sana, na kwasasa naona ni afadhali nisiwe naongea darasani. Hata kama kitu nakijua ni bora nikae kimya, kwasababu hata Mimi, sio kwamba uwa naongea ili nipate şifa, hapana, uwa nafanya vile kwa faida ya watu wote na faida yangu Mimi mwenyewe, kwasabu sipendi kuona mtu anafeli wakati kitu nakifahamu. Pia sio kwamba nafahamu kila kitu, lakini angalau nilichonacho niwape na wengine. Lakini kwa sasa basi, inatosha.
(aliongea Frank kwa uchungu hata Maria alishangaa, hakuamini kama Frank angeongea maneno yale, maana anamjua Frank ni mtu wa kupotezea vitu, hakujua kwamba kuna vitu vinauma... Na vitu hivyo ndo Kama hivyo)
MARİA: Mmh! Frank najua una hasira , ila nakufahamu huwezi kukaa na chuki na kumbuka wewe ni mtu wa dini, tena sisi ni wanakwaya wa kwaya ya chuo, naamini huwezi kukaa na chuki, hasira zitaisha na nategemea atakayeongea uongo utamrekebisha.
(aliongea Maria akiamini Frank hawezagi kukaa na hasira, ikitokea mtu anadanganya wenzie alafu Frank yupo, hawezi kukaa kimya.)
Kutokana na Frank kuchukia ilibidi hata kusoma wahairishe, wakaagana hadi siku nyingine.


MWISHO WA SEASON 02, USISAHAU SEASON 03
IMEKAMILIKA

TSH 1000 TU FULL,
INA VIPANDE 20..
TSH 1500 VIPANDE 40..
TSH 2000 TU VIPANDE 60..
TSH 3000 VIPANDE 100

Malipo mpesa 0768315707 jina Prisca, ukishalipia nambie nikutumie chap.
 
SEASON 03

TAMTHILIA: MTU ALIYETHIBITISHWA KWA MAISHA YANGU
CERTIFIED PERSON OF MY LIFE (CPL)
(51-55)

Whatsapp 0768315707

SEHEMU YA 51
HAPPY: Na kama nimerudi muda huu, yule mwanaume wako mliyekuwa mnashikana hapo mlangoni nilimuonaje?
(Love alishtuka, akatoa macho yote kwa Happy)
LOVE: Ninii?
HAPPY:Ujaniskia au?
LOVE: Sijakuelewa?
HAPPY: Yule aliyekuwa anakushika shika ni nani?
LOVE: Hakuna aliyenishika ( Love aliongea akielekea kitandani kulala)
HAPPY:Mbona unaenda kulala bila kunijibu? Au ndo mlikua mnafanya yenu kwa siri?
LOVE: Happy, sijashikana na mtu na wala sina mahusiano na mtu, usiku mwema!
HAPPY: Sawa, unajidai msiri eeh!
(Licha ya Happy kumtuhumu Love lakini lengo lake kubwa ni kumpumbaza Love hasiendelee kumuuliza kuhusu wapi alienda, na alifanikiwa kwa hilo)
Love akalala, akaachana na mawazo ya kutaka kujua Happy alikwenda wapi. Ila alikuwa anawaza namna Happy alivyojicha akimshuhudia alivyokua anajibizana na issa. Lakini moyoni akajipa imani kwamba inawezekana Happy hakumtambua Issa ndio maana alitaka kumjua jina. akatabasam akijiona Mshindi.
******
Saa 06:45 asubuhi ya siku ya pili, Love baada ya kuamka na kumshukuru Mungu kwa siku mpya, ndipo akatupia macho kwenye kitanda cha Happy ili amuamshe wajiandae kwenda kwenye kipindi cha 08:00 asubuhi. Alishtuka baada ya kuona godoro limetandikwa vyema lakini Happy hayupo.
"Mmmh1' aliguna Love
Hakuwa na wasiwasi sana akiamini labda yupo bafuni. Akasimama na kwenda kuangalia mlango akaukuta haujafungwa, akajua Happy yupo bafuni au katoka nje.
Lakini cha kushangaza zilipita dakika kama kumi bila Happy kurudi. Na kibaya zaidi mazingira ya chumba hayakuonyesha kama kuna mtu ameenda kuoga. Love akashangaa na kujiuliza;
"Au alishatangulia darasani, lakini mapema yote hiyo mmh".
Alichokifanya ni kujiandaa, na hadi inafika saa 07:40 hakumuona Happy. Akafunga mlango na kwenda darasani kwa ajili ya kipindi.
******
Issa, Meshack na Yuma wao pia walikua wapo fiti kwa ajili ya kipindi cha asubuhi hiyo. Walikua ni watu wenye furaha baada ya kumuondoa mpinzani wao kwenye chati. Kabla hawajenda kwenye kipindi wakapanga mipango ya kuliongoza darasa.
YUMA: Oya wazee!
WENZIE: Oyaa!
YUMA: Sasa leo ndio siku ya kulithibitishia darasa kwamba tunajua.
ISSA: Una maana gani?
YUMA: Sikilizeni! Yule chizi si anajiuguza uko hospitali?
ISSA: Eeh!
YUMA: Sasa sisi tuna kazi moja tu. Leo kipindi cha uchumi hakuna, nimesikia tunafanya majadiliano ya darasa kama siku ile. Sasa Mimi leo naenda kujitolea kupigisha pindi, hakikisheni kila point n ita kayo ongea mnapiga m a kof i mengi sana, au vipi? MESHACK: Hilo limekwisha, au kuna lingine?
YUMA: Yani tuhakikishe kila mtu anatuamini kwamba tunajua. Si unajua mambo ya chuo, mtu akiwa anajua lazima wataanza kujileta leta, na wakifanya hivyo sisi sasa tutakua ndo wababe wa chuo, kila mtu atatufahamu na vipaumbele vyote vya darasa tutapewa sisi.
ISSA: Mkuu, umeongea bonge la point, tena kwakuwa yule pasua kichwa hayupo, kwa ninavolijua lile darasa hakuna tena mtu wa kutupinga, kila ukiongea wao ni kuandika tu.
"Ah ah ahhh1' (walicheka sana na kujiona bora, kisha wakaondoka kuelekea darasani.
******
HOSPITAL:
Wakati mishe mishe za kipindi cha uchumi zikipamba moto asubuhi ile, Maria na Happy wao walikua hospital wakisubiri muda wa kumuona mgonjwa wao. Walimlpeleka chai na vitafunwa vyake. Wakiwa wanasubiri muda ndipo Maria akaona ni muda wa kumuuliza Happy kuhusu zile nguo;
MARIA: Eeeh! ulisema leo utaniambia kuhusu zile nguo. Kwanini ulizichukua?
HAPPY: We acha tu, kuna rafiki yangu nakaa nae, ana maswali huyo, acha tu yani.
MARIA: Maswali ya nini?


SEHEMU YA 52

HAPPY: Jana kwenye lile pepa si tulikaa pamoja, sasa baada ya Frank kuzidiwa mi nilimtoroka nikimdanganya naenda toilet, kama unavyojua sikwenda toilet zaidi ya kuja hospital, na ukizingatia tulirudi usiku, we unadhani kama angeniuliza nilikua wapi ningejibu nini?
MARIA: (akashangaa) Sasa ulimjibuje, na nguo zilihusiana nini?
HAPPY: Zile nguo nilikuazima ili akiniuliza ulikua wapi nimjibu nilienda mjini mitumbani.
(Maria akacheka)
MARIA: Hakukuuliza kwanini uliacha kufanya mtihani?
HAPPY:Aliniuliza sana!
MARIA: Ulimjibuje sasa?
HAPPY: Nilimwambia sikusoma hivyo niliogopa kufeli.
(baada ya Happy kujibu hivyo Maria alicheka sana)
Punde, wakaruhusiwa kuingia kumuona mgonjwa. Wakaelekea ndani na kumkuta Frank amelala lakini macho wazi. Frank baada ya kuwaona Happy na Maria alifurahi, akatabasam na kuinuka pale kitandani, kisha akakaa sawa ili aongee na wauguzi wake ambao nao walifurahi kwa kumkumbatia na kumpa pole.
MARIA: Naona mgonjwa leo una afadhari! (aliongea akitabasam)
FRANK:Yaah! namshukuru Mungu, pia nawashukuru na nyie.
HAPPY: Usijali tupo kwa ajili yako! (Happy aliongea kwa kudeka)
FRANK: Hata mimi naona mpo kwa ajili yangu, maana nilijua saizi mtakuwa mpo kwenye kipindi cha uchumi lakini baada ya kuwaona nikakumbuka hata jana mliacha mtihani kwa ajili yangu, asanteni sana, nyie ni zaidi ya ndugu. MARIA: Usijali, kipindi hakina faida yoyote kukuzidi wewe.
(Frank akatabasam na kucheka)
HAPPY: Vipi dokta kasemaje?
FRANK: Amesema asubuhi hii nitaruhusiwa kuondoka, wacha tumsubiri.
Basi wakawa na furaha, wakatoa chai na vitafunwa wakala pamoja wakiendelea kumsubiri daktari ili aje atoe ruhusa.
D ARAŞAN I:
Japo Frank, Maria na Happy hawakuepo lakini darasa lilijaa sana. Macho ya Loveness yalikua yakiangaza darasa zima kumtafuta Happy lakini hakumuona. Kuna muda akauliza wanafunzi wenzie kama walimuona rafiki yake, lakini nao walimjibu kwamba hawakumuona. Love alishangaa mabadiliko hayo ya Happy.
Mbele ya darasa alisimama kiongozi wa darasa ili aongee machache;
CR: Jamani, kama ilivyo desturi yetu ikitokea kipindi hakipo. Nadhani wote tunafahamu kipindi kimeahirishwa, sasa kutokana na muda wa mtihani wa mwisho (FİNAL EXAMINATION) kukaribia tulikubaliana tutumie nafasi kama hizi kujadili maswali yanayotushinda. Kama kawaida yetu, yeyote anayeona yupo fiti kwenye uchumi basi tunamuomba sana apite hapa mbele ili aje kutuelekeza maswali ambayo sisi kama darasa yanatusumbua. Nadhani kila Mtu anayafahamu yale maswali mawili ambayo ni;
1. Ni maswali gani makuu ya kujiuliza katika uchumi?
2. Serikali inatumia fedha zake kwa ajili ya vitu gani? "Ndugu zangu maswali ndio hayo nadhani mmeyasikia, mwenye uelewa na hayo maswali anyoshe mkonotafadhali ili aje atusaidie'
Kulipita kama dakika moja ya ukimya mpaka pale Yuma aliponyosha mkono ili akayajibu maswali hayo. Kiongozi baada ya kuona mkono wa Yumason, akamruhusu apite mbele alafu yeye akarudi kukaa kwenye kiti chake pamoja na wenzie ili nae apate cha kuandika. Yumason alipanda stejini mbele ya darasa, kila mtu alikua kimya kumsikiliza.
YUMA: Nadhani sina haja ya kujitambulisha, kila mtu humu ndani ananifahamu. Aah! kwanza ningependa kabla ya kuanza kujibu swali la kwanza, kila mtu aandae peni na daftari lake ili aweze kuandika.
(Wanachuo wakaandaa peni na karatasi)
YUMA: Nikianza na swali la kwanza, maswali makuu ya kujiuliza katika uchumi. Kwanza tujiulize uchumi ni nini? uchumi ni ile hali ya uzalishaji na usambazaji wa bidhaa au huduma katika nchi. Ukitaka kuufaham uchumi, ni lazma ujiulize maswali makuu 6 ambayo ni;
1. Bidhaa zinapatikana wapi?
2. Nani anafaha kuwa mtoa huduma?
3. pesa zinatengenezwaje?
4. wateja wanataka nini?
5. Nifanye biashara gani?
6. Nitapata wapi mtaji?
(Wanachuo walionekana bize wakiandika point za Yuma ambazo kwa asilimia mia waliziamini na kuziona za kweli kabisa)
YUMA: H ayo ndiyo maswali makuu ambayo mtu yeyote ambaye anatamani kujiusisha na maswala ya uchumi inabidi ajiulize.
(Baada ya Yuma kumaliza tu, Issa na Meshack wakaanzisha fujo za kupiga makofi na kugonga meza hali iliyowafanya na baadhi ya wanachuo kumkubali Yuma kwa kupiga makofi)
YUMA: Vipi kuna mtu nimemuacha? Au kuna mtu ana swali lolote?
(Darasa zima kirnya, hali iliyompa matumaini Yuma kwamba kila mtu alimuelewa na kumkubali. Yuma akaendelea na swali la pili)
YUMA: Jamani, hakuna swali rahisi duniani kama hilo la pili. Ndugu zangu siku zote serikali inatumia fedha zake kwa ajili ya vitu kama,1. kutengeneza viwanja vya mpira mfano vile vya ligi kuu, 2. kulipa wachezaji wa timu ya taifa mishahara, 3. Kununua mafuta na kusimamia gharama za m safa ra wa raisi, 4. Kutengeneza mabomba ya maji na matanki kila mkoa, 5. Kutoa misaada kwa wasiojiweza na mengineyo mengi.
(Baada ya Yuma kumaliza tu, Issa na Meshack kama kawaida, wakapiga tena kelele za makofi, darasa likaunga mkono, watu wakampigia makofi na kumshangilia Yuma, walimkubali kwa kuwajibia maswali wasiyoyajua. Yuma alijiona zaidi ya bora)
Baada ya Yuma kuongea na kumaliza kuzitaja zile Point, alirudi kukaa kwenye kiti chake, alafu CR akapita m bele kuongea machache.
CR. Jamani kila mtu amesikia maelezo ya Yuma, vipi kuna mtu ana swali?
(Kila mtu kimya, Love alikuwa anashangaa tu)
CR: Kwahiyo tunakubaliana na point za Yuma? (Darasa kimya, ila kuna sauti kwa mbali zilisikika zikisema ''Tunakubaliii!")
CR: Basi kama tunakubaliana, Mimi ningependa kumshukuru Yuma kwa maelezo mazuri, pia napenda kusema asanteni sanaa!
(Kelele zilizagaa darasani, kila mtu Yuma, Yuma, Yuma. Hakika Yuma alishinda siku hiyo, hakuwa na mpinzani).
*******
Ni baada ya kuruhusiwa kutoka hospital, Frank sasa alijisikia afadhali japo hakupona vizuri. Wakiwa njiani kurudi, Frank aliwashukuru sana wale wawili ambao walionyesha upendo kwake. Walifika hadi nje ya hostel ya kina Happy na Maria, wakasimama kidogo; FRANK: Kama nilivyosema ninawashukuru sana, nadhani hata usingizi hamkupata kwa ajili yangu, nawaomba muda huu mkautumie katika kupumzika. Mungu akinipa afya zaidi basi kesho wote tutakua kwenye kipindi, Lakini ali ikiwa bado basi sitoweza kuja kwenye kipindi.. Natumaini mtakuja kunitembelea hostel..(aliongea Frank na kuanza kuondoka kuelekea hostel kwake)
MARIA: Lakini ebu subiri Frank. Hatuwezi kukutoa hospital alafu tukakuacha njiani. Happy najua kuwa una majukumu ila nakuomba mpeleke mgonjwa hadi hostel kwake itakuwa vizuri zaidi.
HAPPY: Sawa haina shida.
(Happy alifurahi, akaona amepewa nafasi kubwa duniani, yani moyo wake ndo unapenda nafasi kama hizo... Alimshukuru sana Maria)
llibidi ampeleke mgonjwa hadi hostel, alifanya hivyo. Walivyofika hostel wala hakuishia nje, wakazama wote ndani. Na baada ya kuhakikisha amemfikisha ndani wala hakuwa na papara, asije kuharibu sheria. alichokifanya akaamua kuaga.
HAPPY: Frank natumaini nimekufikisha mahali sahihi, basi wacha nikuage na nikutakie afya njema. (Happy akageuka na kuanza kuondoka)
Lakini ile anagusa kitasa tu akasikia sauti ikimuita;
Happy...
Happy mwili ulisisimka, alihisi kama amepigwa shoti, binti wa watu akagandishwa pale pale, alishindwa hata kunyanyua mguu. Akakumbuka sheria namba mbili "KUWA NAE KARIBU". Na sasa akaona huo ndio muda wa kuimalizia sheria namba mbili ili aingie sheria namba tatu ....akiwa bado anawaza, akasikia tena sauti ile ile ikimuita; "Happy.."

SEHEMU YA 53

Happy mwili ulisisimka, alihisi kama amepigwa shoti, binti wa watu akagandishwa pale pale, alishindwa hata kunyanyua mguu. Akakumbuka sheria namba mbili "KUWA NAE KARIBU". Na sasa akaona huo ndio muda wa kuimalizia sheria namba mbili ili aingie sheria namba tatu ....akiwa bado anawaza, akasikia tena sauti ile ile ikimuita; "Happy.."
Happy akageuka na kumtazama Frank kwa upole na ukarimu. Hakutaka kufanya makosa kabisa, akapiga hatua kadhaa na kumfikia Frank, na sasa ikawa macho kwa macho, kila mmoja akimkagua mwenzie. Zilipitaka kama sekunde 15 za kukaguana. Happy moyo ukienda kasi, alitamani kufanya kitu kwa muda ule lakini akajipa subra. Ukirnya ulidumu kwa muda hadi pale Frank alipofunguka na kuita;
FRANK: Happy!
HAPPY: Abee (aliitika kwa upole, heshima na nidhamu ya mapenzi)
FRANK: Umefanya kazi kubwa sana, hakika najivunia ukaribu wako. Kuacha mtihani, kushinda siku nzima bila kula, kuacha vipindi, na kutolala kwa ajili yangu, ninakushukuru sana. Sina zawadi ya kukupa, ila Mungu atakulipa. Kwa hayo uliyoyafanya yamenionyesha umuhimu wako kwangu.
(Happy alitulia kimya akisikilizia mwanaume anavyoikubali sheria namba mbili)
FRANK: Happy... .(aliita tena)
HAPPY: Abee!
FRANK: Asante sana. Moyo ulionao, huo ndio utu wema. Nina vingi vya kukuambia ila kwa sasa sina kikubwa zaidi ya asante, najisikia fahari yako.
HAPPY: Usijali Frank, tuko pamoja.
FRANK: Sawa. Najua umechoka, nakuomba sasa ukapumzike, sawa Sappy?
HAPPY: Sawa! nawewe pia pumzika sawa eeeh!. (aliongea Happy kwa tabasam huku moyoni akiwaza sheria inayofuata ni namba tatu ambayo ni "MPE FURAHA NA MUONYESHE FURAHAYAKO")
Frank akamshuhudia Happy akiondoka hadi mlangoni, akashika kitasa na kukifungua, lakini Happy kabla hajatoka akageuka nyuma kwa tabasam na kumuaga Frank kwa kutumia mikono yake huku akitoa sauti ndogo ambayo ilisikika akisema "Byee" alafu akafunga mlango na kuondoka. Frank japo alikua mgonjwa lakini alishaelewa nini Happy anataka kutoka kwake. Lakini alijiapiza kutokua na haraka kwasababu haya mambo bhana sio ya kukurupuka. Na ukikurupuka ndo zile ndoa unazosikia baada ya siku mbili waliachana, mara oh wameshikana ugoni, mara leo hajalala nyumbani kwake, mara oh dem mwenyewe wa kila mtu ("maharage ya mbeya"), mara huyo sio dem, hainaga ushemeji n. k.... Hivyo ni bora utulie na kuwa makini.
Happy akiwa njiani kuelekea hostel kwake, akawa anamuwaza Frank tu, akajisemea;
"Sheria mbili nimeshazimaliza, naingia hii ya tatu ambayo ni kumpa furaha, sasa inabidi nifanye lolote lile Frank afurahi hadi ahisi hakuwa mgonjwa.." aliwaza akitabasam
HOSTEL:
Yuma, Meshack, na Issa walikua hostel kwao wakisifiana kutokana na kazi nzuri waliyoifanya darasani. Kila mmoja alionekana kufurahi sana siku hiyo.
ISSA: Hivi mwanangu unataka kusema zile point zote ulizotoa class leo ni za kweli?
YUMA: Wee! za kweli zitoke wapi?. Mzee baba mi pale nilizitoa tu kichwani ninazozijua.
(Walianza kucheka, wakacheka kwa dharau)
MESHACK: Mi nilitaka kushangaa, nikajiuliza ina maana huyu yuma ana akili kiasi hiki, kumbe ulikua ukitupatia heshima wahuni wako.
(wakacheka tena)

SEHEMU YA 54



YUMA: Unajua nini, lile darasa ni kama lina wanachuo hewa vile. Hawataki hata kufikiria, hawataki kuumiza kichwa, wao wanataka kupewa tu ili wameze, sasa kwa jinsi ninavyopenda sifa, nafasi kama zile sitoweza kuziacha.
ISSA: Wale si walishazoea kutetewa na pasua kichwa, sasa pasua kichwa yupo huko hospital anajiuguza, watapata tabu sanaa!
MESHACK: Alafu ukitaka kujua wanachuo wale ni vilaza, we ona tukipiga makofi nao wanaunga telaa... (wakacheka tena na kugongeshana mikono)
YUMA: Ila pale kuna point zingine ni za kweli, zingine mi niliweka tu sasa ningefanyaje, lakini kuna wanachuo wengine mule ndani niliona Kama wapo makini vile.
ISSA: Mfano nani uliona ana wasiwasi?
YUMA: Kuna yule dem ambaye uwa anabishana na pasua kichwa, anaitwa nani vilee ?
MESHACK: Love au?
YUMA: Eeh! huyo huyo. Yule dem anaonekana kujitambua sana, hata akili anazo ila tu ndo vile. Alafu wazee, yule dem mnamuonaje, mzuri kichizi yani!!!
(Wakati Yuma anaongea hivyo, Issa alitulia na alishabadilika, alionekana kuchukia)
MESHACK: Oya Yuma, usiongee sana kuhusu yule dem, muhuni hapo kashapenda.
YUMA: Aah mwanangu Issa, sasa mbona usemi Mzee baba? tutambulishane ili tujuee!
ISSA: Ila mnajua nini, yule dem anazingua!
MESHACK: Kivipi?
ISSA: Aah! dem simwelewi. Jana usiku nilimfwata kule hostel kwake, tia voko, tia voko, dem kachomoa. Dem hata simsomi, yupo kama staki nataka vile!
YUMA: Kwani alikuambiaje?
ISSA: Kasema hanitaki!
YUMA: Ah tulia, hiyo kazi niachie Mimi. Jihesabie kama wako.
(Aliongea Yuma kwa sifa na kumfanya Issa afurahi sana)
MESHACK: Sasa wazee, mchana huu tuna mishe gani?
YUMA: Mishe tushamaliza, tusiyempenda yupo uko hospital anaugua. Hapa jambo la kufanya ni kujipanga, kesho tena mwendo ule ule hadi watakubali.
(walifurahi sana siku hiyo, Issa akapata matumaini ya kumpata mtoto Loveness)
******
Happy baada ya kutoka kwa Frank, kabla hajaingia chumbani kwake akapitia chumba cha Maria na kumuazima daftari la biashara ambalo alidai ana kazi nalo. baada ya kutoka kwa Maria akaingia chumbani kwake ambako alipitiliza moja kwa moja hadi kwenye kioo, akaanza kujitazama huku akijisifia. Akawa anajigeuza geuza pale kwenye kioo, alionekana na furaha sana.
Lakini, kumbe Loveness alikua akimwangalia tu
Happy, ile Happy anatupa macho kitandani akakutana na macho ya Love ambayo yalionekana kushuhudia kila kitu;
LOVE: Happy huyo mwanaume wako kumbe
ulishampataga? (aliuliza akiwa siriazi)
HAPPY: (Akashangaa) Mwanume wangu?
mwanaume gani?
LOVE: Mi simjui, lakini inaonyesha unampenda sana! HAPPY: Una maana gani?
LOVE: We huoni anakufanya uwe kama kichaa wa mapenzi, umeingia tu ukaanza kuparamia vioo, bila hata salam au hukuniona?
HAPPY: Nisamehe basi jamani! (aliongea Happy kwa upole)
LOVE: Mmh! Happy nakusikitikia, umebadilika sana.
Happy wewe ni wakutoingia vipindi? test hujafanya, na bado darasani huingii, hivi kwa mfano hayo unayoyafanya ukiharibikiwa si kila mtu ataniuliza Mimi kwanini rafiki yako anapotea na wewe unamwangalia tu!
HAPPY: Nisamehe basi!
LOVE: Sio kukusamehe, hata wewe mwenyewe fikiria ulikotoka, shule ya msingi, sekondari na sasa chuo, uko kote umepita kwanini uharibu huku Happy? HAPPY: Jamani Love nimekusikia, kesho naingia kwenye kipindi.
LOVE: Na vipi kuhusu test usiyoifanya itakuaje?
HAPPY: Nitafanya jaribio Mwalimu..
(Kwa kawaida kama mwanachuo hajafanya test kutokana na sababu maalumu, basi uwa anapewa test maalumu aifanye, kwahiyo Happy, Maria na Frank bado walikua na nafasi ya kufanya jaribio maalumu)
LOVE: Sawa. Ila ebu niambie leo saa 12 asubuhi uliondoka kwenda wapi?

SEHEMU YA 55


HAPPY: Baada ya kutofanya ile test niliamua kuamka mapema asubuhi bila kukuambia. Nilipanga kutoingia kipindi ili nikasome kujiandaa na hilo jaribio Maalumu. Na hata furaha ulizoziona baada ya kuingia ni kwasababu nimesoma mambo mengi ambayo hata wewe huyajui... Yani leo nimesoma kweli, si unaona hivi vitu ...(aliongea Happy kwa msisitizo huku akimuonyesha Love vitu vilivyoandikwa kwenye lile daftari alilochukua kwa Maria)
LOVE: Happy, Happy, Happy!. Happy uongo huo, shauri yako!
Jioni ya siku hiyo mida ya saa 1 usiku Maria na Happy walikua washanunua vyakula na kwenda navyo moja kwa moja hadi hostel kwa Frank, ambako bila kutarajia wakamkuta Frank akisoma, walifurahi sana.
HAPPY: Mgonjwa hutaki hata kupumzika kidogo, yani ushaanza na kusoma... (aliongea Happy kwa furaha)
MARIA: Mmh! mgonjwa sio kwa hasira hizo, unasoma nini kwani?
FRANK: (Akicheka) Sio kitu, hata sisomi, nilikua naangalia kama nina nguvu za kuingia kwenye kipindi kesho.
MARIA: Eh! kwahiyo baada ya kuchunguza umegundua nini? kesho utaingia au?
FRANK: Mh! sidhani. Naweza kusema nimepona kwa kiasi flani, lakini sio sanaa!
HAPPY: Kwahiyo hauna uhakika na kipindi cha kesho?
FRANK: Yeah! naweza kusema hivyo. Sina uhakika!
MARIA: Sawa! lakini utapona tu leo.
(wakacheka)
Wakatoa vyakula na kuviweka kwenye meza iliyopo mule ndani ambayo uwa inatumika kwa kusoma, meza ilizagaa vyakula vya kila namna hadi Frank akashangaa.
FRANK: Mmh! nyie mavyakula yote haya ya nini sasa? HAPPY: Tunataka ule hadi uvimbiwe!
(wakacheka tena kisha wakaanza kula huku wakipiga stori)
MARIA: Unaambiwa katika biashara, ni bora afe mfanya biashara lakini biashara isife, hivi ni kweli? FRANK: Yaah, na hiyo ndio sheria kuu ya biashara. Biashara lazma iwe endelevu!
HAPPY: Ni kweli, kwasababu wanasema mfanyabiashara hana uhusiano wowote na biashara yake.. si eti Frank?
FRANK: Upo sahihi, lazima kuwe na mipaka ya mtu na biashara yake.
MARIA: Sasa inawezekanaje kutokua na uhusiano na biashara yangu?
HAPPY: Wenyewe wanakuambia, Mali bila daftari uisha bila habari, wafanyabiashara wengi uwa wanachukua Mali zao bila kuziandikia kama ni deni. Mfanyabiashara huruhusiwi kutumia Mali za biashara yako kwa manufaa yako binafsi, ukifanya hivyo biashara itakufa.
FRANK: Na pia siku zote mfanyabiashara ni mteja wa biashara yake.
MARIA: Kivipi sasa?
FRANK: Ni hivi, mfanyabiashara anatakiwa kununua bidhaa na sio kuchukua bila kuzilipia, na watu wengi wameua biashara zao kwa kula mitaji yao.
MARIA: Aah! sasa nimekumbuka ule wimbo wa "Mkulima kala mbegu, anataka kutumaliza ooh" (wakacheka sana kwa furaha)
Waliongea mambo mengi wakiwa wanaendelea kula, baada ya kumaliza kula wakaagana Frank akiwaahidi kama akiwa fresh kesho atalngla kipindi.
*******
MGAHAWANI:
Meshack Issa na Yuma nao walikua mgahawani wakipata misosi huku wakipiga stori zao;
YUMA: Hivi mmepata habari zozote kuhusu pasua kichwa kule hospital?
MESHACK: Aah! hatujapata, kwani wanini yule?
YUMA: Lazma tujue kama bado yupo hospital III kesho kwenye kipindi tusiwe na wasiwasi!
ISSA: Ila kweli tusije tukawa tunaseti mipango kumbe jamaa alishapona muda tu.
MESHACK: Sasa tutapataje habari zake?
ISSA: Subiri, Maria lazma ana taarifa za yule mtu!
Issa alichokifanya ni kuchukua simu yake na kumpigia Maria, simu ikaita na baadae ikapokelewa. Maongezi yalikua hivi;
MARIA: We limtu niambie, umepoteaa!
ISSA: Wewe ndo umepotea, upo wapi sahizi?
MARIA: Nipo hostel hapa!
ISSA: Sawa! sasa naomba kukuliza kitu?
MARIA: Uliza tu!
ISSA: Hivi Frank ameshapona au bado yupo hospitali? (aliongea Issa kwa upole huku akisubiri majibu)

ITAENDELEA
WHATSAPP 0768315707
 
SEASON 03

TAMTHILIA: MTU ALIYETHIBITISHWA KWA MAISHA YANGU
CERTIFIED PERSON OF MY LIFE (CPL)
(56-60 )

( SEHEMU YA 56 )
WHATSAPP 0768315707

ISSA: Sawa! sasa naomba kukuliza kitu?
MARIA: Uliza tu!
ISSA: Hivi Frank ameshapona au bado yupo hospitali? (aliongea Issa kwa upole huku akisubiri majibu) (Maria akashtuka kidogo, hakutegemea swali hilo. Anajua fika Frank na Issa haziivi sasa kwanini Issa amuulizie Frank?. Akaona Issa ni mnafki tu)
MARIA: We unamuulizia Frank wa nini?
ISSA: Si mgonjwa, nataka nikamuoneü
MARIA: Wewe huyo ukamuone Frank, tangu lini?
ISSA: Unajua nini Maria, Mimi na Frank hatujawai kugombana. Kama unavyojua mtu alizidiwa mbele ya darasa, kila mtu aliona, tena mbele ya mwalimu, nimeona niweke mambo mengine pembeni nikamjulie hali yake.
(Maria alizidi kushangaa, alishangaa ustaarabu wa Issa, akaona ameongea maneno mazuri tena ambayo yanapaswa kuongelewa. Hadi hapo akafikiria na kumuona Issa ni mtu tu wa kawaida, Hana tatizo na Frank)
MARİA: Kwani unataka ukamuone usiku huu?
ISSA: Ndio. Ikiwezekana hata usiku huu kama wanaruhusu mi naenda.
(Maria akawaza itakuaje akisema Frank amepona.
Mmh! ha kuta ka aseme hivyo, alitaka ibaki tu siri. Lakini pia aliwaza endapo akisema hajapona, je issa akienda kweli itakuaje?)
MARIA: We issa nae usiku wote huu hospital!
ISSA: Sasa Maria si useme kama jamaa kapona au bado mgonjwa? (aliongea Issa kama kwa kupaniki hivi)
MARIA: Mmh! usinikoromee. (alijibu Maria huku akiwaza kama kweli Issa atataka kwenda hospital usiku huo lazima ataulizia Frank kalazwa wodi gani, na kama akiuliza hapo ndo ataamini Issa ameamua) ISSA: Nijibu basi.
MARIA: Bado amelazwa!!
ISSA: Poa.
Issa alikata simu na kumuacha Maria akiwa na mawazo ya kuongea uongo. Baada ya Issa kugundua ukweli wa kwamba Frank bado yupo hospital, akawageukia wenzake ili waendelee na mipango yao;
ISSA: Oyaa! jamaa bado hospital.
MESHACK: Acha wee! (aliongea kwa furaha)
YUMA: Basi kazi imeisha, twendeni hostel, mida ya usingizi hii.
(wakaondoka pale mgahawani na kurudi hostel kwao)
DARASANI:
Kulikucha asubuhi ya siku ya pili. Ni katika kipindi cha biashara, wanachuo walijaa kila sehem. Ndani ya darasa akiwemo Maria aliekaa katikati darasa, nyuma kabisa walikaa wahuni, Issa, Meshack, Yuma na kulikua na kijana mwingine ambaye alionekana kuwa siriazi sana. Kijana huyo ukimwangalia Alikua sio mtu wa utani, na alionekana kuwa na kiburi cha pesa, alijiamini kupitiliza, yeye hapendagi kupelekeshwa akiona kipindi kinazingua anaondoka. Si mwingine bali ni Tarick.
Lakini licha ya darasa kujaa, Happy na Loveness hawakuonekana hadi mida hiyo.
Kelele zilikua nyingi ndani ya darasa, kila mtu aliongea yake;
ISSA: Hivi mmemuona jamaa leo?
MESHACK: Nadhani hajafika, itakua kweli bado yupo hospital.
YUMA: Kama hajafika basi mambo yameiva.
(wakacheka kushangilia ushindi).
******

SEHEMU YA 57


HOSTEL:
Wakati wenzao wakiwa darasani kwenye kipindi, Loveness alikua bado kalala jambo lililompa Happy maswali. Love alionekana kutokuwa na mipango ya kwenda kwenye kipindi asubuhi hiyo, llibidi Happy aulize;
HAPPY: We love?
LOVE: Vipi?
HAPPY: Huendi kwenye kipindi? muda si ndo huu? LOVE: Mi siendi leo!!
HAPPY: Kwanini?
LOVE: Sidhani kama kuna kipindi huko, walimu wenyewe wamechoka, wanataka tufanye majadilianotu!
HAPPY: Kwahiyo we majadiliano huyataki?
LOVE: Sio sitaki, we hujui tu. Yani mtu anasimama na kwenda mbele kutuelekeza, lakini point anazoongea sijui alizitoa wapi!
HAPPY: Lini hiyo?
LOVE: Si jana. Eti nikuulize wewe shoga, ni maswali gani makuu ya kujiuliza katika uchumi?
HAPPY: Mh! maswali muhimu ya kujiuliza katika uchumi"...! Si ndo yale, inabidi ujiulize nini cha kuzalisha, jinsi ya kuzalisha na umzalishie nani?
LOVE: E-eeh! hayo hayo. Sasa alivyotujibu, eti akasemaje; Nani anafaha kuwa mtoa huduma? pesa zinatengenezwaje? wateja wanataka nini? nifanye biashara gani? nitapata wapi mtaji?. Kweli ndo majadiliano hayo? mwenzangu bora nisiende!!
HAPPY: Sasa kama uliona anadanganya kwanini haukumrekebisha?
LOVE: We hujui tu, yani akimaliza tu kuongea darasa zima wanapiga makofi... Sasa utapata wapi muda wa kumrekebisha?
HAPPY: Tatizo darasa lenu limejaa woga. Kwani ni nani alieongoza majadiliano ya jana?
LOVE: Si yule mwenye sifa sifa, yule anayependa kuvaa vizuri, anapenda sana suti, Yuma.
HAPPY: Aah! kumbe yule. Haya amka basi jiandae fasta twende, kwanza leo ni kipindi cha biashara hadanganywi mtu!
LOVE: Kivipi?
HAPPY: We jiandae fasta basi.
Ilibidi Love aamke na kuingia kuoga haraka. Wakajiandaa na kwenda darasani.
DARASANI:
Happy na Love baada ya kufika darasani, walikuta CR yupo mbele akimtaka mtu wa kupita mbele ili aongoze majadiliano. Lakini kama ilivyo kawaida ya darasa hilo, watu walianza kutegeana kupita mbele, ilifika hatua CR akaona ni bora wahairishe kama hawataki kujadiliana.
Ndipo Happy akataka kupita mbele jambo ambalo Love alimtahadharisha kuwa bora asikilize kwanza swali linasemaje kabla hajapita mbele
CR: Jamani nasoma swali, tena leo swali liko moja tu ambalo linasumbua vichwa vya watu;
"Je utatumia njia gani ili upate wateja wapya katika biashara yako? " swali ndo hilo aliye teyari aje mbele. Maria baada ya kulisikia lile swali akalielewa na aliona anaweza akalijibu japo kwa kujaribu, lakini akafikiria ni nani atamrekebisha pale atapokosea, maana darasa linapenda kumezeshwa tu kuliko kuchangia, alipata wasiwasi wa kupita mbele.
Wakati Maria akiendelea kujiuliza aende au asiende, Mara mtu na pamba zake, Yumason, kama kawaida yake alisimama na kuanza kusogea mbele, jambo lililofanya Issa, Meshack na Tarick kumpigia makofi Yuma ili kumpa nguvu na kumchochea. Kitendo kile kilimfanya Love ageuke na kumkonyeza Happy, jambo lililo maanisha KUMEKUCHA.
******

SEHEMU YA 58


HOSTEL:
Frank alikua bado kalala, lakini sio usingizi tunaoujua ule wa kweli kweli, bali ni usingizi wa mawazo ya asubuhi. Alikua akiwaza tu mambo yake, lakini ghafla akajiona kuboreka mule ndani. Akasimama na kuingia bafuni, akaoga na kujiandaa fresh kisha akatulia na kujisemea;
"Hizi homa ukiziendekeza nazo ndo zinapenda, unaweza kujikuta unafeli bure wakati una uwezo wa kutembea na kwenda darasani. Nishachoka humu ndani, hata kama nimechelewa lakini bora niende kwenye kipindi, sijisikii kabisa kubaki humu."
Baada ya kutafakari kwa muda akachukua kidaftari chake kimoja na peni moja akatoka nje. Akiwa njiani alijisemea;
"Nitaenda kuponea darasani".
Hakuchukua muda sana alikua ameshafika kwenye jengo kubwa ambalo kwa nje lilikua na maandishi makubwa yaliyosomeka "NAH" ambayo kirefu chake ni "NEW ASSEMBLY HALL". Lilikua ni jengo kubwa zuri ambalo kwa ndani lilipendezeshwa na viti vya kisasa vilivyoungana na meza. Na humo ndimo majadiliano yalifanyika.
Jengo hilo lilikua na milango minne, wa mbele kabisa ambao ulikua ukitumika na watu wa ufundi, mlango wa katikati ambao ulikua ukitumika sana na wale wanaowahi vipindi, alafu nyuma ya jengo kulikua na milango miwili ambayo ilikua ikitumika na wachelewaji ili wasionwe mwalimu.
Sasa Frank akapiga mahesabu akidhani labda ndani kuna mwalimu, alichokifanya akaamua kupita mlango wa nyuma kabisa, akaingia kimya kimya bila mtu kujua. Bahati nzuri hakuna aliyemshtukia, na aliamua kukaa mwishoni kabisa nyuma ya kina Issa. Baada ya kuingia akatazama kwa makini akagundua kulikua hakuna mwalimu zaidi ya majadiliano. Kwakuwa aliona watu wametulia akaona naye atulie asikilize. Ni Yuma ndiye alishika usukani;
YUMA: Kama nilivyosema, kuna njia nyingi sana ambazo mjasiriamali yeyote anaweza kuzitumia kupata wateja wapya. Wateja siku zote hawana shida sana, wanapatikana tu, ni rahisi sana kuwapata hasa kama ukizitumia hizi njia vizuri, njia zenyewe ni hizi hapa;
1. Kuwapa zawadi. Hakikisha unawapa vizawadi vingi vingi ili wajisikie fahari, mteja mmoja ukimpa zawadi ni lazma akamwambie mwenzie, hapo lazma watakuja wateja wengine wapya.
2. Wakopeshe. Wateja wanapenda sana kufurahishwa na kuridhishwa, mteja akikukopa mpe, kwasababu ukifanya hivyo atawatangazia wengine na utapata wateja wapya.
3. Tengeneza nao urafiki. Hakikisha unawaalika chakula cha jioni, unapiga nao stori za maisha, akikuomba kitu katika biashara yako mpe wala usimnyime hasije akakasilika. Ukifanya hivyo nae atakuletea wateja wengine.
4. Jipendekeze kwao kwa kila kitu. Kila anachotaka
mfanyie, hakikisha yeye awe kama mfalme, wateja wengi wanapenda rah a, akikisha unampa
anachotaka.
Yuma baada ya kumaliza kuzitaja hizo point kama kawaida wazee wa makofi na baadhi ya wanachuo wakapiga makofi, Yuma akajiona mfalme wa darasa. Baada ya makofi akatulia na kuliangalia darasa, akaona watu kimya, wengine wakiwa wanaandika na wengine wakiwa wanamsikiliza.
YUMA: Jamani Mimi nimemaliza kama kuna mtu hajazielewa point zangu anyoshe mkono au asimame ili atupe za kwake.
Darasani watu kimya. Hakuna mtu aliyenyosha mkono wala kusimama, kila mtu alitulia. Love baada ya kuzisikia point za Yuma akamgeukia Happy na kumuuliza;
LOVE: Mwenzangu umezielewa hizo point?
HAPPY: Mmh! zinakuja na kutoka, sidhani kama ndo hizo..
LOVE: Nilikuambia na ulisema leo hatudanganywi, haya sasa kazi kwako.
(Ilibidi Happy acheke tu)
CR akapita m bele ili akafanye hitimisho watu waondoke, maana hakuna mtu aliyeonyesha kutozielewa point za Yuma;
CR: Jamani kila mtu amesikia jinsi Yuma alivyozielezea njia za kupata wateja wapya, je wote tunakubaliana na maelezo ya Yuma?
"HAPANA"
Yuma akashtuka, Issa akatetemeka, Meshack akameza mate ya woga, darasa lilipagawa ghafla. lilikua ni jibu kutoka nyuma ya darasa, jibu ambalo kila mtu alilisikia, ilibidi kila mmoja ageuke nyuma amuone huyo mtu aliyesema ''hapana1' ni nanii?

SEHEMU YA 59

CR: Jamani kila mtu amesikia jinsi Yuma alivyozielezea njia za kupata wateja wapya, je wote tunakubaliana na maelezo ya Yuma?
"HAPANA"
Yuma akashtuka, Issa akatetemeka, Meshack akameza mate ya woga, darasa lilipagawa ghafla. Illlkua ni jlbu kutoka nyuma ya darasa, jlbu ambalo klla mtu allllsikia, Illbldi kila mmoja ageuke nyuma amuone huyo mtu aliyesema "hapana" ni nanii?
Kila mtu alishangaa, hata Yuma kule mbele akabaki mdomo wazi, uso ulijikunja kutokana na taharuki.
Hakuna aliyeamini, sio Love, Maria, Happy, Yuma, Meshack au Tarick. Wote walijua mtu huyo hakufika kwenye kipindi sababu alikua mgonjwa. Darasa lote lilifahamu kuwa mtu huyo aliyesema hapana alilazwa hospitali baada ya kuzidiwa darasani wakiwa wanafanya test. Na mtu huyo hakuwa mwingine bali ni Frank.
Ghafla ndani ya darasa kukazuka minong'ono kila Mmoja akiongea lake;
LOVE: Hivi yule si alikuaga mgonjwa?
HAPPY: Hata mimi nashangaa!
(Kilichomshangaza Happy ni kumuona Frank darasani. Yeye alifahamu kuwa Frank yupo hostel kwake akijiuguza, sasa haikufahamika aliingia darasani kupitia mlango gani hadi watu wasimuone)
LOVE: Mmh! na humu ndani kaingia muda gani, mbona maajabu ya dunia.
HAPPY: Hata sijui mwaya!
Sio Happy na Love tu, kila mtu aliwaza yake. Tena kwa upande wa kina Issa, wao walichanganyikiwa kabisa;
ISSA: Oya Meshy, tumekwisha baba!
MESHACK: Sasa tufanyeje?. Au mtumie meseji Yuma pale mbele mwambie atoke, tusepe tu.
ISSA: Asee! bora tufanye hivyo, maana naziona aibu zilee!
TARICK: Oya sikilizeni, usimtumie meseji wala nini, mwache kule kule. Kwasababu akiondoka atapata aibu zaidi, Watu watamuona hajielewi. Alafu mbona mnamuogopa sana huyo jamaa? hapa tupo kwenye majadiliano, hawezi kututishia kitu. Hata kama anapenda şifa lakini sio kumkimbia, huyu ni kupambana nae.
ISSA: Kaka, hivi unamfahamu vizuri huyo mtu? huyo jamaa anajua, utapambana nae kwa ngumi lakini sio darasani.
MESHACK: Kwanza ebu fikiria, mtu hadi anazikataa point za mwenzake unajua amejipangaje mtu huyo?. Darasa zima walishakubali kasoro yeye tu, we unamchukuliaje mtu wa hivyo?
TARICK: Tulieni, jambo la msingi ni kumpachika maswali hadi akome, lazma tumkomoe leo. Tumuulize hata vitu asivyowai kuvisikia, tuhakikishe kila mtu humu ndani anampiga swali la nguvu, au vipi wanangu?
ISSA: Mmh! labda, wacha tuone (anaonyesha kukata tamaa)
Maria japo hakutarajia kama Frank angekuwepo mule ndani lakini uwepo wa Frank ulimpa tabasam kwa sababu uwa anamuelewa sana hasa akiwa anaongelea masuala ya biashara. Anamjua Frank ni mtu wa kusoma vitabu mbalimbali vya biashara na mtu anayependa kujifunza. Aliona huo ndio muda muafaka wa darasa kupata majibu ya kibiashara.
Frank alionyesha upole, utulivu na ujasiri pale alipo, hakuwa na chembe la woga. Moyoni aliamini ile ni sehemu ya kujifunza, wala hakuwa anafanya vile ili apate sifa. Hakuwa na sababu ya kuacha watu wapotee kwa kukubali uongo wakati ukweli anaufahamu.
CR: Eeh! kaka kule nyuma, umesema" hapana", basi tunaomba usogee m bele ili maneno utakayoongea kila mtu ayasikie, au kama ni marekebisho basi kila mtu na arekebishwe, karibu sana.
Frank baada ya kuruhusiwa kuongea na kupita mbele, akafanya kama alivyoambiwa. Akapita hadi mbele, lakini hakutaka kupanda juu kwenye steji aliko Yuma, yeye alisimama kwa chini Mahali ambapo kila mtu sasa akawa anamuona na angeweza kumsikia vizuri. Baada ya kuona kila mtu katulia, Pasua kichwa akaanza kuongea;
FRANK: Jamani habari zenuü?
WANACHUO: Poaa, safiii, nzurii, freshiii (Ni baadhi tu ya majibu ya watu wakiitikia salam ya Frank)
FRANK: Kwanza, napenda kumpongeza ndugu yangu pale juukwa kutujibia swali letu la leo.
(alimaanisha kumpongeaza Yuma)
FRANK: Aah! kwa kifupi nadhani kila mtu ameyasikia maelezo yake, lakini sijajua kama kila mtu ameyakubali au ulikua ni uoga wa mtu kukubali au kukataa. Mimi kwa upande wangu sijafika hapa mbele hili kuyakataa maelezo ya mwenzangu, ila naweza kusema nimekuja ili nilijibu swali kwa jinsi nilivyolielewa, na kama ikiwezekana kumrekebisha kwasababu sidhani kama alikua sahihi sana
(Kabla Frank hajamaliza kuongea, Yuma akadakia)
YUMA: Samahani ndugu, sijajua umekuja hapa
kuuza sura au vipi..
(Baadhi ya wanachuo walicheka, wengine kwa dharau akiwemo Issa, Meshack na Tarick)
YUMA: Kwasababu sijajua hapa mbele umekuja kuongea point zako au umekuja kuzikataa point zangu.
FRANK: Kaka! sizikatai point zako, ila kwa faida ya darasa zima ni lazma zirekebishwe, hazijakaa sawa! YUMA: Eti uzirekebishe, uzirekebishe kwani wewe ni nani? umekua mwalimu?
FRANK: Sikiliza kaka! hapa tuko sisi, wanafunzi tu, ni bora hata angekuepo mwalimu ili aone ni namna gani ulikua ukijaribu kutudanganya. Point ulizoziongea zinaweza zikaendana na ukweli lakini
sio za kweli hata kidogo.
YUMA: Ebu ongea hizo zako unazoziona za kweli tuzisikie!
(Yuma aliongea kwa jeuri, nae Frank hakusita bali akaanza kuelezea;)
FRANK: Nadhani tunafahamu, biashara ni faida, na faida inatengenezwa na wateja, bila mteja hakuna biashara. Sasa ebu tuambie, kama mteja huyo tunayemtegemea tunamualika katika chakula cha jioni, tunajipendekeza kwake kwa kumkopesha, tunawapa zawadi ili tu tuwafurahishe wao, hiyo faida tutaipata wapi?
YUMA: Kwa n i hapa tunazungumzia mambo ya faida au mbinu za ku pata wateja wapya?
FRANK: Kaka, kumbuka lengo kubwa la biashara sio kumnufaisha mteja bali kumridhisha. Lengo kuu la biashara ni kutengeneza faida. Lakini kupitia mbinu za kibiashara, mbinu ambazo hazitakupa hasara pia hazitamnyonya mfanyabiashara. Kuna vitu inabidi uvifanye ili vikuletee wateja wapya ambao watakuja pale kutokana na ubora wa biashara yako ikiwemo bidhaa bora, na huduma bora. Kumbuka hata punguzo katika biashara utolewa ikiwa tu itatoa faida kwenye biashara, na inategemea na ukubwa wa biashara yenyewe, usije kudhani punguzo lipo ili kujipendekeza kwa mteja, la hasha! , Ndio maana unaona sio kila biashara inatoa punguzo.
(Wakati Frank akiendelea kuongea, kila mtu aliachwa mdomo wazi, alishangaa uwezo wa Frank katika biashara, hata Loveness alipagawa na maelezo ya mwanzo ya mwanaume.
Issa alianza kuona wanaelemewa na mzigo, Yuma ameanza kuzidiwa, alishindwa kuvumilia aibu ile, akaamua kuingilia Mada;
ISSA: Sasa mbona unaongea mambo mengi bila kututajia point zako? Lete hizo mbinu kama kweli unajua!
FRANK: Ondoa shaka, mbinu hizi nitakazokupa ndizo mbinu kuu za kijasiriamali na kibiashara ambazo hutumika na waletu wanaohitaji kufanikiwa. MESHACK: (Anacheka) Ah aah aah, kwahiyo unataka kusema kuna watu hawataki kufanikiwa? we jamaa mbona muongo hivi?
FRANK: Sawa nakubali Mimi ni muongo, lakini naomba unijibu; Je mtu anayejipendekeza kwa wateja, anayewakopesha wateja wakati biashara yake sio ya kukopesha, anayewapa wateja zawadi Hi tu awafurahishe , JE MTU HUYO ANATAKA KUFANIKIWA KIBIASHARA?
(Kila mtu alikaa kimya, Meshack maneno yalimkauka, Frank ni kama aliwasha moto vile)
FRANK: Kwa wale wanaopenda kufanikiwa, point hizi nitakazo ongea nilishawai pia kuzisoma katika mtandao wa kijasiriamali, ni mbinu ambazo ukizitumia lazima upate wateja wapya katika biashara yako, mbinu hizo ni zifuatazo;

SEHEMU YA 60


1. Mitandao (networking). Mtandao ni njia kubwa sana ya kukuletea wateja wapya. Mitandao asa ile ya kijamii mfano facebook, instagram, what's app, twitter, n.k, ni njia nzuri ambazo zinampa mfanyabiashara nafasi ya kuonyesha biashara yake au bidhaa ambazo zitamletea wateja wapya.
2. Matangazo (advertisement) , sasa matangazo yanaweza kufanywa kupitia radio, TV, magazeti, n.k. na matangazo ndio njia rahisi sana kuwapata wateja wapya. Na tofauti ya mitandao na matangazo ni moja, mitandao inajitegemea, alafu biashara katika mtandao unaweza kuifanya wewe mwenyewe, lakini matangazo ni tegemezi, yanalipiwa kwenye vyombo vya watu ili yafanyike, pia yanaweza kufanyika katika mitandao.
3. Tengeneza ushirika. (build partnership) (team up) ,kwa mfano wewe ni muuzaji wa nyanya, hakikisha unakua na ushirika, unakua na ushirikiano na muuzaji wa vitunguu ili ikitokea yule wa vitunguu amepata mteja, alafu yule mteja akahitaji nyanya basi atamleta kwako, kwa namna hiyo utapata wateja wapya.
4. Ijue biashara yako ndani na nje. Hakikisha unatambua bidhaa au huduma unayoitoa ndani ya biashara yako inawaridhisha wateja ambao wao watakua chanzo cha kukuletea wateja walio nje ya biashara yako... Lazma uelewe na ujue kuwa bidhaa zako nje ya biashara wateja wanazichukuliaje.
5. Tambua tabia za wateja wako. Ndugu zangu, kuwa karibu na wateja haimanishi kwa kuwaalika chakula au kuwapa zawadi. Wateja wakiwa eneo la biashara yako, jinsi unavyowahudumia, jinsi wanavyokupenda na jinsi wanavyokuamini wewe na kuziamini bidhaa au huduma zako, uko ndiko kuwa karibu na wateja. Na mteja akigundua unatoa huduma safi basi lazma atamwambia mwenzie.
(Wakati Frank akiongea kuhusu njia za kupata wateja wapya, hakika alikonga nyoyo za watu wengi mule ndani, nao ilifika hatua walijiona ni wajinga sana kutokana na urahisi wao wa kuziamini mapema point za Yuma ambazo zilikua sizo. Ilifikia hatua Loveness akaachia tabasam ambalo lilionwa vyema na Jappy, Happy sura ilibadilika)
FRANK: Hizo ni baadhi tu ya point zangu, ambazo zinapatikana katika vitabu na mitandao ya kibiashara, na kama kuna mtu hajanielewa au ana swali naomba aulizetu.
TARICK: Asee sijajua kwa wengine, lakini Mimi sijakuelewa, kwanza umenichanganya, sasa kwahiyo unataka kusema hakuna uhusiano wa mteja na mfanyabiashara?
FRANK: Ipo tena mkubwa sana! TARICK: Na kwahiyo, mteja haruhusiwi kuifurahia biashara?
FRANK: Anaruhusiwa! kwanini asiruhusiwe?
TARICK: Sasa mbona kule mwanzo umesema lengo la biashara sio kumfurahisha mteja?
FRANK: Lakini naona jibu unalo mwenyewe!. Hivi kati ya wewe na chuo, nani amfurahishe mwenzie?
ISSA: Tunafurahishana (alijibu kwa jeuri)
FRANK: Basi ni hivyo hivyo kwenye biashara, mteja atatoa pesa ili aifurahishe biashara lakini biashara itatoa bidhaa bora ili imfurahishe mteja. Wewe utatoa ada na chuo kitakupa mafunzo, lakini nachotaka kusema dhamira ya chuo sio kukufurahisha wewe, ila kukupa elimu itakayokuridhisha , kukuelimisha, kukufunza na kukunufahisha ndio maana ukirudi mtaana utaanza kutangaza wewe mwenyewe; "Oh chuo flani ni kizuri, kinatoa elimu bora n.k"
Majibu hayo ya Frank yaliwaacha watu midomo wazi, watu hawakuwa na budi zaidi ya kusimama na kupiga makofi kwa Frank, jambo lile lilileta hasira sana kwa Yuma, Tarick, Issa na Meshack. Walichukia na mara Yuma akauliza swali lililomshangaza kila mtu;
YUMA: Je kwa unavyojiona, mavazi yako, mwonekano wako, unafaha kweli kuwa mfanya biashara wewe?
Swali lile lilimshangaza kila mtu. Hata Frank mwenyewe akabaki mdomo wazi, hakulielewa limeingiaje. Baada ya kufikiria kwa muda akaona alijibu, lakini wakati akitaka kujibu ilisikika sauti ya kike;
Mimi nitakusaidia kulijibu swali hilo'
Watu wote wakageuza macho kumtazama binti huyo aliyetaka kumsaidia Frank. Hakuwa mwingine bali ni Loveness. Wanachuo hawakuamini, Happy akameza mate ya woga, Issa alivuta pumzi za uchungu, Frank macho yakamtoka!


MWISHO WA SEASON 03, USISAHAU SEASON 04
IMEKAMILIKA

TSH 1000 TU FULL,
INA VIPANDE 20..
TSH 1500 VIPANDE 40..
TSH 2000 TU VIPANDE 60..
TSH 3000 VIPANDE 100

Malipo mpesa 0768315707 jina Prisca, ukishalipia nambie nikutumie chap.
 
SEASON 04

TAMTHILIA: MTU ALIYETHIBITISHWA KWA MAISHA YANGU
CERTIFIED PERSON OF MY LIFE (CPL)
( 61-65 )

( SEHEMU YA 61 )

WHATSAPP 0768315707

YUMA: Je kwa unavyojiona, mavazi yako,
mwonekano wako, unafaha kweli kuwa mfanya
biashara wewe?

Swali lile lilimshangaza kila mtu.
mwenyewe akabaki mdomo wazi, hakulielewa limeingiaje. Baada ya kufikiria kwa muda akaona alijibu, lakini wakati akitaka kujibu ilisikika sauti ya kike;
"Mimi nitakusaidia kulijibu swali hilo"
Watu wote wakageuza macho kumtazama binti huyo aliyetaka kumsaidia Frank. Hakuwa mwingine bali ni Loveness. Wanachuo hawakuamini, Happy akameza mate ya woga, Issa alivuta pumzi za uchungu, Frank macho yakamtoka!
kila mtu alishangaa, Loveness kumsaidia Frank, tangu lini?. Issa sura ilibadilika, alikua kama haelewi kinachoendelea. Alifikiri labda Love kashtuka kutoka usingizini. Yaani Love badala ya kuwa upande wao anakuwa upande wa Frank?, Maajabu. Kwanza hata haikuingia akilini, ilikua ni ndoto.
Kasheshe pia lilikua moyoni kwa Happy. Happy alihisi moyo unapasuka. Kati ya vitu hataki ni ukaribu wa Love na Frank. Yeye alipenda bifu la Frank na Love liendelee ili mapenzi yake kwa Frank yawe siri. Kitendo cha Love kutaka kumsaidia Frank, japo kilikua katika mazingira ya kusoma, lakini kilimuumiza.
Maria nae aliachwa mdomo wazi. Alijua kabisa Frank na Love haziivi hata kidogo, sasa huyo Love huo msaada aliutoa wapi?.
Yuma kule mbele alitumbua macho. Alikodoa macho akitazama vizuri kuhakikisha kama ni Love ndiye anataka kumsaidia Frank. Baada ya kujihakikishia, akabaki mdomo wazi.
Kila mtu macho kwa Love. Hata Loveness mwenyewe alijishtukia lakini alijipa ujasiri. Akaanza kuongea;
LOVE: Yuma nikuulize swali dogo! hivi
mfanyabiashara ni mtu gani?
YUMA: Ni mtu anayefanya biashara (alijibu kwa jeuri) LOVE: Unaweza kunipa uhusiano wowote kati ya mfanyabiashara na mavazi?
YUMA: Ndio. Mfanyabiashara lazma uwe smart, lazma upendeze ili uvutie wateja!
LOVE: Ni kweli, lazma uwe smart. Naweza kusema Frank yupo smart sana! au u smart unaozungumzia wewe ni upi?
YUMA: We vipi! sasa huyo ana u smart gani?. Mfanyabiashara lazma upigilie suti kama Mimi hivi, lazma uhakikishe mteja akikuona anakufuata mwenyewe.
LOVE: Je suti ndio vazi pekee la kumfanya mtu awe smart?
YUMA: Ni vazi lipi sasa lenye hadhi ya kibiashara? (Love akacheka)
LOVE: Nadhani sasa nimegundua ni namna gani humu darasani tunahitaji kubadilika. Inawezekana baadhi yetu bado tuna akili finyu, wewe Yuma ni mmojawapo. Hivi wewe unataka kusema 98% ya tuliopo humu hatufai kuwa wafanya biashara?
Kwasababu nikijaribu kuangalia sidhani kama waliovaa suti wamefika hata wa 5.Na kitu kingine, hivi kinachomvutia mteja ni vazi lako au bidhaa zako? YUMA: Sitaki kujua, kwanza hili swali hukuulizwa wewe, ni kimbele mbele chako tu.
LOVE: Hakika unahitaji maombi, Na vipi unaweza kutuambia uhusiano wa mfanyabiashara na mwonekano?
(Love alionekana kubadilika sana siku hiyo, hata wanachuo walishangaa mno)
YUMA: Sasa wewe, hivi unadhani kila mtu anafaha kuwa mfanyabiashara? watu wengine hata sura za kuvutia wateja hawana. Bora Mimi handsome, nikikaa ofisini, dukani, au sokoni wateja wote hasa mabinti wanakuja wenyewe!
(Kauli hiyo ya Yuma ilifanya darasa liangue kicheko, watu walihisi wapo kwenye mdahalo wa kibiashara. Love alijua kumfanya Yuma apagawe)
LOVE: Naweza kusema kila mtu anafaha kuwa mfanyabiashara, labda tofauti itakuwa ni uwezo wa kibiashara baina ya mtu na mtu. Ndio maana katika biashara kuna vitu kama ubunifu na uwezo wa kutoa maamuzi, hivo ni vitu vitakavyomfanya mfanyabiashara mmoja awe tofauti na mwenzie. Lakini kila mtu anaweza akawa mfanyabiashara, hilo linawezekana.
YUMA: Sasa kama kutakua na tofauti inamaana mmoja atakuwa chini na mwingine juu, wewe huoni kuwa aliechini hafai kuwa mfanya biashara?
(Swali hilo lilimfanya Love afikirie kidogo, jambo lililompa matumaini Yuma ya kujiona kama ni mshindi. Lakini wakati Yuma akitaka kutoa tabasam la ushindi, Frank akaingilia kati)
FRANK: Loveness yuko sahihi kabisa.
(Moyo wa Happy ulipiga "tiii, tii, tii")
FRANK: Kati ya siku Love ameongea point ni leo. Yuma badilika, tena badilika sana!
YUMA: Nibadilike niwe wa njano?
(Anafanya wenzie wacheke na kugonga meza)
YUMA: Nibadilike vipi wakati kila kitu ninacho?
FRANK: Hauna kitu. Kwanza, Nani aliyekuambia katika biashara inabidi wafanyabiashara wote wawe sawa ili tujue kuwa wanafaha kuwa wafanyabiashara? je unataka kumfananisha muuzaji wa nyanya gengeni na mwenye kampuni?. Lakini nataka nikuambie jambo moja, inawezekana mfanyabiashara wa nyanya akaifurahia sana faida yake kuliko yule mwenye kampuni. Sio kwamba kila mwenye biashara kubwa na faida uwa kubwa, hapana. Faida ya biashara haitokani na suti yako wala sura yako, faida inatokana na ubora wa bidhaa zako ambazo zinamvutia mteja. Au nikuulize swali dogo, ukivaa suti, mteja atakuja kununua suti yako au kununua bidhaa yako?
(Yuma alikaa kimya, alikosa la kuongea, ilibidi
Tarick aingilie kati)
TARICK: Yuma yuko sahihi! sio kila mtu anafaha kuwa mfanyabiashara, na pia kuwa smat kunavutia wateja, habari ndio hiyo.
FRANK: Sikatai, Lazma uwe smart. Lakini u smart hautoki kwenye suti pekee. Mfanyabiashara bora hawezi kuwaza ni vazi lipi la gharama anunue ili limpe heshima kwa wateja, ila anawaza ni bidhaa gani yenye ubora itakayo pendwa na wateja. Pia, kumbuka hata mtu anayepata hasara katika biashara, anafaha sana kuwa mfanya biashara. Kwasababu hasara ndio matokeo ya mzunguko wa biashara yako.
(Wakati Frank akiongea, Love alikua bado amesimama, muda wote alitoa tabasam, hata yeye mwenyewe alijishangaa. Lakini upande wa pili Happy alitamani kwenda kumshika Frank aondoke nae lakini sheria zilikua hazijakamilika, ilibidi awe mvumilivu.
Issa alimuona Love kama mnafki flani, ni kama yuda vile, amewageuka, akampiga swali Loveness;) ISSA: Hivi Love, unakumbuka siku ile ulivyoongea mbele ya darasa kwamba sio kila mtu anafaha kuwa mfanyabiashara?
LOVE: Nakumbuka sana. Na naweza kusema ile siku ilinifunza mengi, huwezi kujifunza bila kufunzwa na kutaka kujifunza. Mimi niko tayari kujifunza.Hata wewe Issa nakushauri kuwa tayari.
ISSA: Nitajifunza mwenyewe lakini sio kufunzwa na huyo mtu.
LOVE: Hayo mengine utajua wewe, nadhani siku utakayojielewa ndio utatambua kuwa ukitaka kufanikiwa, fanikiwa kupitia wenzio.
ISSA: Kwahiyo Love, Mimi sahizi sijielewi?
LOVE: Wewe wasema. Lakini yaliyomo yamo! Kama hutaki kusikia la mkuu, kuwa makini na guu lako.
Loveness alikaa chini akiacha watu midomo wazi, hakika alibadilika bila kutegemea, hata Frank akatoa tabasam kutokana na majibu ya Love.
Majibu waliyoyapata yalitosha kabisa kuwafanya Yuma, Issa, Tarick na Meshack kuondoka mule ndani wakiwa wamejawa aibu na hasira.
Huku nyuma waliopenda kujifunza walitulia wakisikiliza Frank akiongea maneno yaliowatia nguvu.
FRANK: Jamani, hili darasa tunapaswa kubadilika, la sivyo tutafeli vibaya sana. Maneno aliyoongea Love lazima utajiuliza huyu ni yule Love wa zamani au Love yupi? Lakini kilichopo nyuma ya Love ni kujifunza, kubadilika na kujiamini. Humu ndani naamini kila mtu anajielewa, ana akili na anajua kuchanganua mambo. Lakini uoga na mazoea ndiyo yanayotufanya kila siku tuwe watu wa kusikiliza na kuondoka. Hapa tupo katika majadiliano, basi lazima tufanye majadiliano hasa kwa jambo linalotusumbua. Lazma kila mtu aongee anachokiwaza kichwani. Sina mengi asanteni sana.



SEHEMU YA 62


Baada ya Frank kuongea, kila mtu alimpigia makofi, watu walionyesha ni jinsi gani maneno yale yaliwaingia vema, kila mtu alijiambia moyoni kuwa anapaswa kubadilika.
Cr akawaaga wanachuo wenzie na kuwashukuru kwa majadiliano yale ambayo japo yalizua ugomvi lakini yalikuwa na manufaa kwa waliohitaji kubadilika na kujifunza. Baada ya hapo kila mtu aliondoka kuelekea kwake, Happy alikuwa wa kwanza kuondoka.
KILIMAHEWA
Wale watu wanne baada ya kutoka kwenye kipindi walikubaliana watafute sehemu ya siri wakae ili wapange mipango yao.
Baada ya kufikiria sana wakapanga watoke nje ya eneo la chuo. Walielekea kat ika msitu wenye asili ya bustani paitwapo kilimahewa. Ni eneo flani nje ya chuo, ambalo lina mazingira yenye miti mingi, nyasi za kuvutia, mabonde na milima. Ni eneo lililopendwa na wanachuo waliochoka kusoma, waliolizwa na wapenzi wao, waliofeli mitihani, wenye hasira, chuki na wengine walienda kufurahi na kupiga picha.
Basi nao bila kuchelewa wakaelekea kilimahewa. Walipofika huko wakatafuta eneo lenye miti mingi, wakakaa. Zilipita dakika kadhaa pasipo yeyote kuongea neno, kila mtu sura ilimuiva kwa hasira;
ISSA: Tumfanye nini mtu yule?
YUMA: Hadi sasa sijapata jibuü
MESHACK: Kwani tunashindwa kumpiga?
TARICK: Nadhani kumpiga sio suluhisho kwa mazingira ya hapa chuo.
MESHACK: kwasababu kuna yule jamaa mpiga chuma, yule anord mla bata, mnaonaje swala hill tukimkabidhi yule jamaa, na ule mwili wake dakika mbili mtu anakimbizwa hospital ya mkoa.
TARICK: Hapana! Mi nina wazo, ujue mambo ya kupiga haya unaweza kuua ikawa kesi nyingine.
ISSA: Sasa tumfanye nini?
TARICK: Kwani jamaa si tunataka kumkomoa kwenye masomo?
YUMA: Eeh! ikiwezekana afeli kabisa hadi watu washangae.
TARICK: Basi jambo ni moja tu, kuhonga pesa kwa mwalimu wa somo husika.
MESHACK: Mmh! si itakua balaa hiyo?
TARICK: Sikilizeni, hivi mnadhani kuna ticha ukimpa laki tano amfelishe mwanafunzi atakataa? Laki tano kwa maisha haya ya sahizi?
YUMA: Lakini kaka kumbuka wale wana mishahara zaidi ya laki tano.
TARICK: Wewe pesa ni pesa! hakunaga mtu anayekataa pesa. Ndio maana unaona hata hao akina bakhresa wana pesa chafu lakini bado wanauza juisi za jero.
YUMA: Mmh! lakini kweli! kuikataa laki tano?. Hawezi. Tena hawa maticha wanavyopenda pesa! kwahiyo sasa?
TARICK: Ndio hivyo, hapa tujipange, mfano tunamtafuta ticha wa uchumi tunampiga pesa, kwenye pepa anaua mtu na habari ya ke inaishia.
Wakakubaliana kufanya hivyo, wakaona Tarick katoa bonge la wazo, wakaondoka.
*******
HOSTEL:
Happy baada ya kutoka darasani hakuwa na muda wa kupoteza, alijiona kuwa na mawenge kichwani. Kichwa kilipata moto, alihisi maumivu ya kichwa yasiyo na sababu. Alivyofika chumbani kwake akajitupa kitandani, akaanza kuvuta kumbukumbu za kilichotokea darasani.
"Huyu Love isije ikawa ameanza kumpenda Frank. Maana leo hata sijamuelewa kabisa. Hapana, leo ni lazima nikakamilishe sheria ya tatu , nikizubaa mtu mwenyewe naona anamvutia kila mtu. sitaki kumkosa." aliwaza Happy, uso ukiwa na huruma, alionekana kuwa na mawazo sana..
Akiwa bado anajiwazia, Mara akaingia Loveness.
Love baada ya kuingia, moja kwa moja macho yake yakakutana na macho ya Happy ambayo yalijaa maswali. Wakati mwenzie akiteseka, Love akawa anatabasam tu, hakuwa na wasiwasi. Lakini alishangaa baada kumuona Happy akimuangalia sana tofauti na siku zote;
LOVE: Wewe vipi kwani?
(Happy hakujibu ila aliendelea kumkodolea macho Love. Baada ya muda akageukia upande wa pili akimgeuzia Love mgongo. Love akabaki akishangaa)
LOVE: Happy mbona hivyo?
Swali hilo nalo liliachwa likielea, jambo lililompa majibu Love labda Happy kuna kitu kina msumbua. Love akakumbuka kuwa, Happy anateswa sana na mapenzi kwa kipindi hicho. Ukimya ule wa Happy ulimkumbusha inawezekana mwanaume huyo anayemsumbua Happy ndiye chanzo.
LOVE: Au yule mwanaume wako kakuchanganya tena?
HAPPY: Hivi Love, ni kitu gani kimekusukuma leo hadi ukamsaidia kujibu swali adui yako?
(Happy aliuliza huku akigeuka tena na kumtazama Love, uso ukiwa mbwii!)

SEHEMU YA 63

Love akashtuka, akakumbuka ni kweli Frank ni adui yake wa muda mrefu. Tena kati ya watu alikua akiwachukia pale chuoni wa kwanza ni Frank, sasa ilikuaje akamsaidia kujibu swali lisilomuhusu?, kiukweli hata yeye mwenyewe alijishangaa. Akavuta kumbukumbu ya kilichotokea, akatikisa kichwa chake kikae sawa;
"Hivi ni Mimi kweli ndiye nimesaidia Frank? sasa watu watanichukuliaje" aliwaza loveness.
"Mmh! hapana, itakuwa nilipitiwa, kwa jinsi alivyonichukiza yule mtu uko nyuma, leo kitu gani kilinisukuma kumsaidia" aliendelea kuwaza love.
HAPPY: Love... We love!
LOVE: Abee! (alishtuka kutoka mawazoni)
HAPPY: Si nimekuuliza, Leo kitu gani kilikusukuma kumsaidia adui yako ambaye ulisema hutaki hata kumuona?
LOVE: Mmh! Happy nahisi nilipitiwa, nilijisahau!
HAPPY: Ulijisahau? kivipi?
LOVE: Unajua nini, ilifikia hatua niliona kabisa wale akina Yuma ni waongo, halafu kama unavyojua Mimi mwenyewe kushuhudia mambo ya uongo sipendi.
HAPPY: Kwanini sasa ulimsaidia adui? (Happy aliuliza hivyo ili apate uhakika kama Love alishaanza kuvutiwa na Frank au lah!)
LOVE: Nilijikuta tu nimeongea, sikutarajia.
HAPPY: Kila mtu ameshangaa, darasa zima wanajua ugomvi wenu, kwanini ukurupuke tu na kumsaidia mtu aliyekulaza hospital kwa maumivu ya kichwa?
Maneno hayo ya Happy yalianza kumfanya Love ajisikie kama amechanganyikiwa. Akaanza kujiona mjinga, hajielewi.
LOVE: Nisamehe Happy, kweli tena nilipitiwa na majadiliano. (aliongea akiwa na sura ya kujilaumu) HAPPY: Mmh! haya mwaya ( Happy aliongea huku moyoni akifurahi maana hadi hapo akagundua hakuna dalili za mapenzi kati ya Love na Frank.)
Lakini ghafla Love alikosa raha. Moja kwa moja alijua watu watamdharau na kumuona hana msimamo. Hata chumba alikiona kichungu. Japo alitaka kujipumzisha kitandani lakini kwa hasira akaamua kutoka jambo lililomfanya Happy atabasam. Happy akaamini kuwa ni kweli Love alipitiwa.
Baada ya kutoka hostel, Love alionekana akizunguka zunguka maeneo ya chuo pasipo muelekeo. Uso wake ulionyesha kuwa na mawazo ya kutosha. Njiani alipishana na baadhi ya wanachuo, wengine walimsalimia lakini hakuitikia. wengine wahuni wa chuo, walikuwa wakimsifia kwa kusema "Dada we mzuri1', lakini Love hakuelewa kitu, alishachanganywa.
Alitembea pole pole akiwa anafikiria vitu vingi. Kilichomuuma zaldi sio kuongea darasani ball kumsaidia kujibu swali mtu aliyewahi kumpa ugonjwa wa kichwa. Na kibaya zaldi hakujua kwanini aliongea, kwamba alikua hajielewi? Kama alikua hajielewi Ina maana aliongea maneno yasiyofaa? Aliongea vitu vya uongo? Love alishindwa kuelewa.
Lakini kitu cha kushangaza, akiwa njiani alikutana na baadhi ya wanachuo ambao anasoma nao darasa moja, ambao nao walikuwemo katika majadiliano, walimpa hongera. Mmoja wa wanachuo hao ni kijana Godlove. God love kama jina lake lilivyo alifahamika kutokana na upole wake na upendo kwa wenzie, pia alifahamika sana kwa kusema ukweli, yeye alikua ni mtu wa watu. Hajawai kuwa na roho mbaya.
Godlove akiwa katika mishe zake akamuona Loveness, akamkumbuka vizuri kwamba aliongea kwenye majadiliano;
GODLOVE: Hey mdada....hello, vipi mbona mawazo mengi?
LOVE: (Akiwa anamtazama God love) Eeh vipi?
GODLOVE: Poa, aah! usinishangae, sisi wote ni wafanyabiashara.
LOVE: (akicheka) naona, vipi lakini?
GODLOVE: Mbona unatembea kinyonge hivyo?
LOVE: Kawaida tu!
GODLOVE: Me! sawa, nilitaka tu nikupe hongera!
LOVE: Hongera ya nini?
GODLOVE: Unajua nini, Mimi nakufaham vizuri sana, tokea siku ya kwanza unabishana na Frank kuhusu biashara hadi leo hii umemsaidia kujibu swali. Nimeshangaa ni jinsi gani umebadilika. Nakumbuka ile siku jamaa alikuambia wewe hujielewi lakini ulikasilika, Ila leo hii baada ya wewe kujielewa nawe pia umemuambia Yuma hajielewi, natumaini ipo siku Yuma nae atabadilika. Nilichogundua ni kwamba, mtu ubadilishwa na mtu kupitia makosa. Sikuwahi kudhani kama ungeongea maneno mazuri kama uliyoongea leo, hongera sana na kwaheri.
Love alishangaa, wakati watu wengine wakimwambia amekosea, wengine wanamwambia amepatia, sasa akina nani wakweli?
Sio Godlove tu, siku hiyo alikutana na wanachuo wengi waliompa hongera zake, na wengine wakimsifia kwa kubadilika;
MWANAISHA: Loveness!
LOVE: Abee mwana!!
MWANAISHA: Ebu nipe siri ya mafanikio yako!
LOVE: Jamani! mafanikio gani ? (alafu akacheka)
MWANAISHA: Kwani Love aliyeongea leo kwenye majadiliano ndiye yule Wa kuumwa kichwa?
Love alicheka sana baada ya kusikia kauli hiyo ya rafiki ake mwanaisha. Mwanaisha na Love walisoma kidato cha sita katika shule moja uko nyuma kabla ya kukutana tena kwenye chuo kimoja, japo walikua hawakutani mara kwa mara lakini wakikutana walikua wakitaniana sana.

SEHEMU YA 64

MWANAISHA: Love!
LOVE: Nambie shoga angu..
MWANAISHA: Asee umebadilika, hivi ni nani kakubadilisha?
LOVE: Mwenyewe tu nimeamua. (aliongea huku akicheka)
MWANAISHA: Nyoo! eti mwenyewe. Bila shaka adui yako ndiye kakubadilisha. Najua unamchukia sana kutokana na kipindi kile kukusababishia homa, lakini ukweli ni kwamba yule mtu amekuwa chachu ya mabadiliko kwa kila mtu darasani, hata wasiompenda ni chuki zao tu.
LOVE: Sawa mwaya, lakini bado namchukia sana.
MWANAISHA: Kwenda zako, hizo sasa ndo chuki (aliongea mwana akiondoka zake)
Wakati Happy, Issa na baadhi wakimuona kama hajielewi wengine walipendezwa na mabadiliko yake, angalau alifarijika.
******
OFISINI:
llikuwa ni siku nyingine. Issa, Meshack, Yuma na Tarick hawakutaka kulaza damu mpango wao. Siku hiyo waliamua kweli, hawakutaka kuogopa. Wakajikusanya pamoja na kwenda moja kwa moja kwa mwalimu wa somo la uchumi.
Mwalimu alijulikana kwa jina la Sir Kukula. alifahamika sana kutokana na uzoefu wake katika kazi, ufundishaji wake mzuri, na upendo wake kwa wanafunzi. Alipenda sana kuwasaidia wanafunzi wanaosoma kwa bidii na katika somo lake alipenda kila mtu afaulu.
Basi wale wanne walipofika nje ya mlango wa ofisi, wakagonga mlango na kukaribishwa ndani. Wakaingia na kukaa kwenye viti. Baada ya kumsalimia mwalimu, ukapita muda bila wao kuuongea shida zao.
SIR KUKULA: Vipi mbona kimya, niwasaidie nini? (Lakini hakuna aliyeongea, kila mtu alimtegea mwenzie, jambo lililofanya mwalimu kukasilika)
SIR KUKULA: Kama hamna tatizo, ebu ondokeni.
YUMA: Ticha, tuna shida kidogo.
SIR KU KU LA: Shida gani?
YUMA: Dah! shida yenyewe ya siri sana (aliongea Yuma akiwa anaogopa ogopa)
SIR KU KU LA: Sasa kama ni siri kwanini mpo wanne? YUMA: Sisi wote ni wahusika wa hiyo siri.
SIR KU KU LA: Sawa! tatizo nini?
YUMA: Ticha, kuna mwanafunzi tunasoma nae. Kuna ishu zimetokea kati yetu na huyo mwanafunzi. Mambo aliyotufanyia hayavumiliki. Tulitaka kumpiga lakini tukamuhurumia, tulichokifanya ni kukubaliana kumfundisha adabu. Ticha Sisi tunachotaka afeli tu somo lako basii (aliongea Yuma huku akiwa na wasiwasi)
(Mwalimu akawasikiliza, akafikiria kwa muda alafu akacheka)
SIR KUKULA: Kwani huyo mwanafunzi kawafanyia nini?
YUMA: Katuibia laptop , na aliyeuziwa katuambia yeye ndiye alyiemuuzia..
SIR KUKULA: Kumbe hamna uhakika kama yeye ndiye aliwaibia?
YUMA: Uhakika tunao!
SIR KUKULA: Sasa kwanini hamjaenda kuripoti katika uongozi wa chuo pale kwa walinzi? Mi sihusiki na hayo mambo..
YUMA: Ticha sisi tunalijua hilo, ila tumeona huko tutaangaika sana bila mafanikio, ndio maana tunataka msaada wako..
SIR KUKULA: Hivi mnafikiri ninaweza kutoa Msaada gani kirahisi hivo?
(Kutokana na kauli hiyo ya Mwalimu, Yuma kajua mambo ya pesa sasa)
YUMA: Ticha kama pesa tutakupa, pesa tunayo... Ukitusaidia sisi tumeandaa kama laki tano hivi kwa ajili yako.
SIR KUKULA: Sijamaanisha nataka pesa.., namaanisha mnataka niwasaidie nini?
YUMA: Fanya vyovyote, jamaa kwenye mtihani wa mwisho, somo lako afeli.
SIR KUKULA: Huyo mtu mwenyewe anaitwa nani? YUMA: Anaitwa Frank, Frank nani? Eti Frank nani? (aliwauliza wenzie)
ISSA: Frank Kakolanya.
(Mwalimu alishtuka baada ya kusikia jina hilo. Ni kama alilifahamu)
SIR KUKULA; FRank Kakolanya! si şule kijana anayejua kujibu vema maswali, kuna siku katika kipindi changu alibishana sana na dada flani hivi? Si ndo huyo?
(Swali hilo lilifanya vijana wanne watazamane kwanza, kila mtu alimshangaa mwenzake, wote walikaa kimya kwa muda hadi Tarick alipojibu..)
TARICK: Ndio Mwalimu. Mtu mwenyewe ndo huyo!
SIR KUKULA: Yule kijana ni mwizi?
MESHACK: Mwizi sana! tena sanaai. Mwalimu hukumbuki kuna kipindi dada mmoja aliibiwaga nguo chumbani kwake?
SIR KU KU LA: Nakumbuka, si yule aliyekua akilia na kugalagala pale kwa walinzi?
MESHACK: Eeh! huyo huyo!
SIR KU KU LA: Unataka kusema kwamba?
MESHACK: Sasa allyelba zile nguo ni yule Frank!
SIR KU KU LA: Achaa! Yule kijana na kujielewa kote kule, mbona simdhanii kabisa, kumbe ni mwizi? TARICK: Mwizi mkubwa sana.
SIR KU KU LA: Sasa kwanini msimpeleke uongozi wa chuo au polisi?. Maana keşi kama hizo adhabu yake ni kufukuzwa chuo.
Wale wanne baada ya kusikia kuwa, kumbe mtu akiwa ameiba adhabu ni kufukuzwa chuo wakatazamana na kukonyezana bila mwalimu kujua.
Mwalimu akaanza kumkumbuka Frank vizuri kabisa, akaumbuka ile siku alivyoongea darasani hata akamsifia, akakumbuka jinsi anavyojua kuelezea maswali kiundani kabisa hata mgumu kuelewa akamwelewa, akatikisa kichwa kutoamini.
SIR KUKULA: Kwahiyo ni mwizi mkubwa hapa chuo?
TARICK: Mwizi sanaa!
SIR KUKULA: Ameshawaibia na nyinyi?
YUMA: Tena juzi tu!
SIR KUKULA: Na hamtaki kumfukuzisha chuo mnataka kumkomoa?
MESHACK: Ndio mwalimu!
SIR KUKULA: Alafu mmeandaa laki tano kwa zoezi hilo?
ISSA: Ndio na tunazo hapa pesa hizo!
(alijibu Issa kwa kujiamini, huku akitoa kibahasha kilichojaa noti)
Sehemu ya 29
Issa kwa ushawishi zaidi akakichukua kile kibahasha, akanyosha mkono kumkabidhi Sir Kukula. Sasa wale wanne wakawa wanamwangalia mwalimu usoni kwa macho ya "Pesa ndio hizo unataka nini tena zaidi ya kuzichukua".
Nae mwalimu akawa anawatazama kila mmoja usoni alafu macho akayaamishia kwenye ile bahasha, akaiangalia, ni kama alikua akijiuliza "Nizichukue au niziache1'.
Baada ya ukirnya wa muda, Sir Kukula akapokea kile kibahasha na kukiweka mezani, jambo hilo lilitoa tabasam kwa wale wanne.
Baada ya kupokea fedha zile bado alionekana kuwa na mashaka. Akawaza;
"Yule kijana ni mwizi, hapana, au itakuwa wamegombana kwa mambo yao alafu wanataka kulipa kisasi?. Lakini ikitokea nikamfelisha dhambi hii haitaniacha, mimi sio mwalimu wa aina hiyo. Tangu nimeajiliwa chuo hiki siijui rushwa wala aina za rushwa, kwanini iwe leo?. Alafu sifa niliyonayo chuoni hapa ni kutokana na bahadhi ya wanafunzi wangu kufaulu vizuri somo la uchumi. Na Mimi ni miongoni mwa walimu bora Tanzania waliotoa wachumi wengi, sasa kama yule kijana n d iye niliyemuona bora, ambaye anaweza kuwa mkombozi wa somo langu kwanini nataka kumuharibia, tena kwa jambo nisilolijua? " aliwaza Sir Kukula.
Wale wanne baada ya kuona mwalimu kapokea mzigo, wakaona wameshamaliza kazi, wakaaga haraka na kuanza kutoka, lakini kabla hata hawajafikia mlango wakaitwa;
SIR KUKULA: Ebu rudini.
(walishtuka. Wakarudi wakiwa na wasiwasi)
SIR KUKULA: Ebu shikeni bahasha yenu na poteeni haraka kabla sijakasirika.
.(baada ya kuambiwa hivo wale wanne walishangaa, wakataka kuoji lakini hawakuruhusiwa)
SIR KU KU LA: Nimesema tokeni, sitaki maneno.
(Wakatoka haraka. Walitoka hadi nje ya ofisi wakiwa na hasira, wakasimama na kuanza kujadiliana.)
ISSA: Wazee tunafanyaje? ticha ndo huyo kazingua!
MESHACK: Yule anataka tumbembeleze kama mtoto, ela anaitaka sema basi tu.
TARICK: Hii ndo shida ya walimu waoga.
YUMA: Au anataka tumuongeze pesa?
TARICK: Sasa kama pesa si angesema kuliko kukaa kimya. Yule ni kuachana nae tu, kama vipi twendeni kwa ticha wa biashara, nasikia jamaa bia kreti 2 tu anafanya kila kitu.
YUMA: Acha bhana! Bia kreti mbili mbona rahisi tu, inamaana huyo hata tukimpa laki tatu fresh?
TARICK: Laki tatu mbona atakuwa tayari hata kumuondoa chuo, nyingi sana hiyo.
(Wakacheka sana na kukubaliana kwenda kwa mwalimu wa biashara ili wampe laki tatu)
TARICK: Alafu hivi mnajua yule jamaa test ya biashara hakufanyaga ile siku?
ISSA: Eeh! si alikua anaumwa, inabidi afanye test maalumu. Yeye, Maria, na wengine wasiofanya test. TARICK: Kwahiyo ni lini wanafanya hiyo test?
ISSA: Nadhani ni jumatatu ijayo.
TARICK: Sasa baadae tukutane hata chumbani kwa Issa usiku niwape mpango kazi. Nataka hiyo test apate zero.
(Wakakubaliana kukutana usiku ili wapange mipango ya kumuharibia Frank, baada ya hapo wakaondoka maeneo ya zile ofisi)
HOSTEL:
Mida ya jioni Issa akaona akumbushie kwa Loveness. Akampigia simu, iliita muda mrefu mwishowe ikapokelewa;
LOVE: Vipi Issa?
ISSA: Fresh, mzima?
LOVE: Mzima, sijui wewe!
ISSA: Niko poa. Samahani Love, naomba nisamehe kuhusu ule usiku, mi bado nakupenda.
LOVE: Nishakusamehe.. Nipe mpya!
ISSA: Bado nakupenda Love, naomba nielewe basi!
LOVE: Mmh!
ISSA: Kweli tena, alafu nina zawadi yako njoo uichukue!
LOVE: muongo wewe!
ISSA: Kweli! Njoo uichukue!
LOVE: Nije wapi?
ISSA: Njoo nipo hostel. Chumba namba 121.
LOVE: Mh! kuja hosteli kwako ni ngumu. Lakini nitaangalia, nikiweza nitakuja muda wowote.
ISSA: (akifurahi) Sawa Love!
*******
Siku hiyo mida ya saa lusiku, Happy baada ya kushinda chumbani tu, akajaribu kujisomea lakini kichwa kilikataa. Alitamani kumpigia Frank lakini aliogopa asije kuharibu sheria. Uvumilivu ukamshinda akaamua kuchukua kimkoba chake cha pesa na kuelekea mgahawani. Akanunua baadhi ya vyakula akaweka kwenye kontena mbili, kisha akatoka na kuelekea wanakouza matunda.

SEHEMU YA 65


Akanunua baadhi ya matunda alafu akaondoka kuelekea mahali alipopafahamu yeye mwenyewe!
Usiku huo Frank alitoka hosteli kwake na kuelekea benki kwaajili ya kutoa pesa za matumizi. Lakini kwa bahati mbaya kadi yake ikamezwa na mashine ya
ATM, ni baada ya kukosea kuweka namba yake ya siri. Na kwa kawaida tatizo hilo umuhitaji mteja aende tawi lolote la benki ili ajaze fomu maalumu ya kupata kadi yake.
Pale chuo wao walikua wakitumia ATM tu, jambo lililomchanganya Frank kwasababu ilishakuwa usiku, benk zote zilifungwa, mfukoni hakuwa na pesa na njaa ilimsumbua.
Aliamua kurudi hosteli ili akaumize kichwa ajue ni jinsi gani atapata japo pesa ya kununulia chakula usiku huo. Alipofika akajitupa kitandani kutuliza mawazo maana kichwa kilikuwa kizito. Kichwa kiliwaza wapi apate pesa na ukicheki hakuzoeana sana na watu zaidi ya Maria ambaye ndie rafiki ake mkubwa.
"Oh! naumiza kichwa bure wakati Maria yupo" aliwaza na kuvuta simu yake ili amtafute Maria.
Akiwa katika harakati za kumpigia Maria ili amuazime pesa, mara akasikia mlango ukigongwa. Akaachana na simu kisha akaenda kufungua mlango, macho yakakutana na binti murembo, Happiness ambaye mkononi alibeba mfuko mkubwa ambao Frank hakujua kilichopo ndani.
Akamkaribisha ndani kwenye kiti.
FRANK: Mambo Happy!
HAPPY: Poa tu za toka Jana!
FRANK: Jana wapi?
HAPPY: Si jana kwenye majadiliano. Hukumbuki ulivyoumiza watu vichwa.
(Wakacheka baada ya kauli ile ya Happy)
FRANK: Aah! si unajua mambo ya majadiliano.
HAPPY: Nimekuja kuendelea kukuuguza, najua bado hujapona vizuri.
FRANK: (Akiwa anacheka) Mmh! muuguzi uko vizuri, hutaki kukaa mbali na mgonjwa wako.
HAPPY: (akiwa anafungua mfuko wa vyakula) Wee! nimuache mgonjwa wangu alafu akizidiwa na homa, hasara kwa nani?
(Wakacheka tena. Punde Frank akashangaa Happy akitoa makontena ya chakula na matunda, akaona ni kama Mungu alitenda miujiza kwasababu hakuwa na pesa usiku huo na njaa ilimtafuna vya kutosha)
HAPPY: Haya sasa mgonjwa wangu chakula hiki naomba tule.
FRANK: Mmh! Happy mbona mavyakula mengi?
HAPPY: Usijali, nataka ufidie siku ulizolala hospital. (Wakacheka tena na kufurahi pamoja, Happy alionekana kuwa na furaha sana na alionekana kumfurahisha sana Frank kwa maneno yake.... Wakiwa wanaendelea kula kuna muda Frank alicheka hadi akapaliwa, hiyo ni kutokana na utani na maneno mazuri ya Happy.)
FRANK: Happy utaniua kwa furaha! (aliongea kwa sauti ya kupaliwa)
HAPPY: Pole jamani! pole mgonjwa wangu (nae akiwa anacheka)
FRANK: Yani wewe! sikutegemea kama
ungenifurahisha hivi.
HAPPY: Kidogo tu jamani, lakini si kweli?
FRANK: kwambaa?
HAPPY: Lile darasa letu limejaa vilaza?
Frank akacheka tena na tena. Basi walifurahi sana wakiwa pamoja. Ulifika muda kama saa tatu usiku hivi, Happy aliamua kuaga ili aondoke lakini Frank hakutaka. Alimtaka Happy akae kae kidogo.
HAPPY: Frank mi nimekaa sana leo, wacha nikuache.
FRANK: Aah! Happy si ukae kidogo jamani, yani unanipa furaha sana.
Maneno hayo yaliingia moyoni kwa Happy na kutulia tuli, Happy sasa moyo ulikua mbali, aliwaza sheria zake akaona zimebaki mbili tu ya 4 na 5.
HAPPY: Mmh! jaman muda umeenda, nitakuja tena kesho, sawa?
FRANK: Utaondoka, kaa kidogo hata dakika tano tuu. Happy nae kujithibitishia umuhimu wake, akakaa. Wakapiga stori, wakacheka pamoja, ulifika muda wakabaki wanatazamana tu. Frank macho yaliiva kwa usingizi wa matamanio, Happy nae jicho liliiva kwa uchungu wa sheria zake.
Hakuna aliyemsemesha mwenzie, walitazamana hadi wakajikuta midomo ipo karibu, kila mmoja alitaka kwasababu alihisi joto la mahaba. Happy macho alifumba, akawa anasubiri mdomo wa Frank utue mdomoni kwake, lakini ghafla Frank akawa kama ameshtuka, akaishia kumkumbatia Happy kisha akamuaga;
"Happy, usiku mwema" alafu akamwachia kutoka mwilini mwake.
Happy akashusha pumzi na kutoka kitandani kuelekea kwake, akafungua mlango na kuondoka. Akiwa njiani aliwaza;
"Angalau sasa anaelekea, ilibakia kidogo anibusu. Hiyo tu ni sheria ya 3. Je ya 4 na 5 si ndo tutalala kabisa" Aliwaza kisha akatabasam mwenyewe.
Usiku huo Issa alikua na washkaji zake ambao walikuja kwa ajili ya mipango ya kumuharibia Frank. Lakini kitu cha kushangaza ni kwamba Issa alipanga chumba, alitandlka godoro vizuri, tofauti na siku zote. Hadi jamaa zake wakashangaa;
YUMA: Oya mbona leo chumba fresh sana?
ISSA: Eeh! kuna mgeni wangu asee! lazima akute chumba safi, (alafu akacheka)
TARICK: Una mtoto nini leo? basi kama vipi si tuondoke.
ISSA: Kwani si mmekuja kwa ajili ya ule mpango kuhusu yule bwege?
TARICK: Eh! ndo hivyo, sasa we si unazingua.
ISSA: Daah! lakini dem mwenyewe sidhani kama atakuja, tusubiri kidogo kama hatokei, tuanze.
Wakasubiri sana lakini Loveness hakutokea, ilifika hatua wakaona bora waanze kikao chao. Wakafunga mlango na kuanza mikakati ya kummaliza Frank.
Usiku ule Loveness alikaa sana pekeake chumbani. Hakujua Happy yuko wapi hadi muda ule, akawaza sana akahisi labda aliondoka kwenda kusoma.
Hakuwa na usingizi, bora hata angekuwa Happy wangepiga stori.
Mara akakumbuka ana zawadi yake kwa Issa.
Akaona bora nae aondoke tu akachukue zawadi yake.
Akajitazama kwenye kioo akaona yupo safi. Akafunga mlango na safari kuelekea kwa Issa ikaanza. Alivyofika hostel ya kiume, akatafuta chumba namba 121 ambacho anakaa Issa, akaiona.
Akakifuata chumba hadi mlangoni. Wakati anataka kubisha hodi, akaacha ghafla mara baada ya kusikia mazungumzo yaliyomshtua!

ITAENDELEA

WHATSAPP 0768315707
 
SEASON 04

TAMTHILIA: MTU ALIYETHIBITISHWA KWA MAISHA YANGU
CERTIFIED PERSON OF MY LIFE (CPL)
( 66-70 )
WHATSAPP 0768315707

( SEHEMU YA 66)

Akajitazama kwenye kioo akaona yupo safi. Akafunga mlango na safari kuelekea kwa Issa ikaanza. Al ivy of ika hostel ya kiume, akatafuta chumba namba 121 ambacho anakaa Issa, akaiona. Akakifuata chumba hadi mlangoni. Wakati anataka kubisha hodi, akaacha ghafla mara baada ya kusikia mazungumzo yaliyomshtua!
Akatega sikio ili asikie vizuri. Akabaki mdomo wazi, akasikia wakipanga mipango;
"Eeh! sasa kabla hajaingia kwenye test maalumu inabidi tumlaze tena hospital"
"Vipi tutatumia dawa ile ile au nyingine?"
"Tutatumia nyingine, hii nilipewaga kwa rushwa na rafiki yangu ambaye ni dokta. Aliniambia kama mtu akiiweka mdomoni basi kuna mambo mawili yanaweza kumtokea"
"Mambo gani hayo?"
"Alisema kwanza Atazimia kwa masaa 24, alafu pili wenda akapoteza kumbukumbu zote au akapatwa na ugonjwa wa akili"
"Mmh! Kaka hiyo dawa noma"
"Ndo hivyo, mi mwenyewe uwa nakaa nayo mbali, kwasababu niliambiwa hata harufu yake tu ni sumu " "Kaka tusije tukaua mtu, mi naogopa" "Msijali. Dokta alinambia kuua haiui, ila chamoto ndo atakipata1'
Sasa Love hadi muda huo hakujua mule ndani ya chumba cha Issa kulikuwa na watu wangapi, na hakujua ni akina nani.
Ki baya zaidi hakujua wan aye mpangia njama ni nani, na kwa ajili gani. Kuna muda alisikia kama sauti za viatu vya mtu akisogea mlangoni, ilibidi atoke akajifiche ili amuone.
Akiwa amejificha alimuona Issa ambaye baada ya kufungua mlango akachungulia kushoto na kulia akikagua kama kuna watu eneo hilo. Issa baada ya kujihakikishia hakuna watu akarudisha kichwa ndani na kufunga mlango.
Nae Love hakuwa nyuma, ile Issa anafunga mlango tu, akawahi tena mlangoni na kusikiliza. Moyoni alijisemea;
"Hapa leo sitoki hadi nijue ni nani wanampangia njama"
Love kitendo cha kumuona Issa akiwa ni mmoja wa watu waliopanga njama, kilikua ni jibu tosha la kuamini Issa ana roho mbaya. Akawaza;
"Kumbe Issa ni mkatili hivi? alafu ndo anataka tuwe wapenzi? Looh! haya mapenzi sio ya kujiingiza kichwa kichwa, watu wengine majambazi"
Akiwa anaendelea kuwaza pale mlangoni, Mara akaslkla maneno mengine yaliyomshangaza na kumshtua zaidi;


SEHEMU YA 67

"Wazee mimi yule Frank kukosa woga na hofu ningempa hata sumu ya panya afe"
"We kama Mimi tu, mi inafikia hatua simpendi hata kidogo"
"Kinachoniuma Mimi ni kitendo chake cha kuingilia maswali yasiyomuhusu, yani jamaa hawezagi kukaa kirnya"
"Jamaa si anatafutaga sifa kwa mademu, sasa subiri tumtoe ufahamu"
Love aliogopa, akajikuta anatetemeka, akawaza;
"Ni Frank yule mgomvi wangu au Frank gani? mbona sielewi kinachoendelea. Hawa wanamaanisha Frank yupi? au kuna Frank mwingine? lakini kwa maelezo yao wanamaanisha Frank yule yule ninayemjua. Kumbe vile anavyoongeaga darasani kuna watu wanamchukia kiasi hiki? " Aliwaza Love, alafu akatega tena sikio kusikiliza;
"Mi nadhani juzi tulivyomlaza hospital bado hajatosheka" (wakacheka))
"Sasa hata hiyo test yenyewe hafanyi"
"Alafu hivi mnajua kama mtu asipofanya test ya kwanza na test maalumu anakuwa amefeli moja kwa moja?"
"We sema kweli?"
"Ndio hivyo, sheria ya chuo inasema hivyo"
"Sasa, kwahiyo dawa hii tutamtilia kwenye maji?"
"Eeh kwenye maji ya kunywa, nyingine tutapulizia ili avute hewa yake. Serna dawa hii inaanza kufanya kazi baada ya saa moja, hivyo basi kama mtihani ni jumatatu, inabidi jumatatu tuwai kuamka kabla yake alafu tumtegee muda atakaoenda kuoga. Pia ikiwezekana hata jumapili tukiweza kumuwahi usiku atakavorudi kusoma, maana jamaa uwa anapenda kuoga akitoka kusoma, itabidi tuwe faşta sana"
Loveness akasikiliza kila kitu, na sasa akaamini mtu anayezungumziwa ni Frank yule yule adui yake. Huruma ikamuingia na hasira juu.
Akiwa bado anaslklllza mara akasikla ndani watu wakigongeshana mikono, na punde kukasikika vishindo vya viatu, Love akasahau habari za zawadi, akatimua mbio na kuondoka eneo hilo.
Love baada ya kurudi room kwake akamkuta Happy kalala laklnl macho wazi.
LOVE: Mwenzetu leo ulljua kupotea, yani saa 12 jion hadi saa nne hujaonekana, ulikua wapi?
HAPPY: [akicheka] nikuulize wewe, saa tano hii unatoka wapi na hili giza?
Love akaona asiendelee kuuliza maana hakuwa na jibu sahihi. Alichokifanya ni kuingia bafuni akanawa miguu na kurudi. Akajifuta vizuri na kujitupa kitandani baada ya kubadili nguo na kuvaa za kulalia. HAPPY: Mbona hunijibu ulikua wapi?
LOVE: We ndo uanze kunijibu masaa manne ulikua wapi?
HAPPY: Mi nilikua najisomea.
LOVE: Hata mimi nilikua najisomea.
Wakacheka kwa pamoja baada ya wote kugundua kwamba wanadanganyana, hakuna a I iy etaka kusema ukweli.
HAPPY: Kwahiyo sahizi tunaamua kutopeana siri au sio?

SEHEMU YA 68


LOVE: Nikuulize wewe mwenye siri za mapenzi.
HAPPY: Vipi kuhusu wewe na siri ya yule mwanaume wako usiku ule?
LOVE: Wee! koma, sina mwanaume.
HAPPY: Kwani yule alikua wa kike?
Love: Alafu nimekumbuka, vipi kuhusu zile sheria zako za mapenzi?
HAPPY: Kwani na wewe unazitaka?
LOVE: Akhaaa!
HAPPY: Usivunge, kama umekwama sema nikupe sheria.
Wakacheka kwa pamoja. Walizoeana sana. Utani kwao ilikua ni moja ya upendo wao. Waliongea mambo mengi na punde wote wakajikuta wamepitiwa na usingizi.
******
BENKI:
Siku nyingine. majira ya saa moja na nusu asubuhi Frank alikua ameshafika benki kwa ajili ya kufuatilia kadi yake. Akafuata taratibu zote za kibenki na baada ya kumaliza akapewa kadi yake. Alionekana kuwa na haraka ili awahi kipindi ambacho kilikua kinafanyika asubuhi hiyo.
DARASANI:
Baada ya kutoka benki, moja kwa moja akaelekea darasani ambako alikuta hakuna wanafunzi wengi. Akapata wasiwasi akijua hakuna kipindi. Akaanza kumtafuta Maria mule ndani lakini hakumuona. Akatoa simu yake akampigia, lakini kabla hata haijapokelewa akashangaa ameshikwa shati kwa nyuma, akageuka, alikua ni Maria.
MARIA: Ulienda wapi?
FRANK: Nilienda benki kuchukua kadi yangu.
MARIA: Kadi? Kadi ipi?
FRANK: Kadi yangu ya benki ilimezwa jana usiku, leo ndo niliifuata.
MARIA: Sawa. Sasa tunafanyaje kuhusu test maalumu ya jumatatu? Maana leo ni ijumaa, bado siku 2 tu.
FRANK: Alafu mbona watu wametawanyika au hakuna kipindi?
MARIA: Ndiyo hakuna. Mwalimu hayupo, pia CR katangaza kasema leo kutakuwa hamna vipindi.
FRANK: Na majadiliano vipi?
MARIA: Kuna watu walikataa kufanya majadiliano. Kulitokea mabishano kidogo hivyo CR akaona bora isiwepotu.
FRANK: Sawa. Basi tutumie huu muda kujiandaa na test. Tutafute darasa, au twende darasa la siku zote. MARIA: Poa, kama una namba ya Happy mwambie aje.
Ilibidi Frank ampigie Happy na kumpa taarifa. Walifika kwenye hilo darasa na haukupita muda Happy nae akatokea, akawasalimia wenzie na somo likaanza.
FRANK: Kwan i wao walitolewa swali gani?
HAPPY: Lile tulilojadili siku ile, umuhimu wa matangazo.
FRANK: Mmh! mbona walipata raha sana.
MARIA: Ndio hivyo, na sisi tupambane na hali yetu. {wakacheka}
HAPPY: Kwahiyo tunajadili maswali au notes za walimu?
MARIA: Bora tufanye maswali, notes tutazisoma tu. HAPPY: Sawa. Kuna haya maswali yapo mawili.
FRANK: Ebu yasome!
HAPPY:Maswali yako hivi;
1. Ni kwa namna gani utawashinda washindani wako wa biashara?,
2. Je kuna umuhimu wa kusajili biashara?
Happy alimaliza kusoma maswali akamtazama Maria usoni, akamuona akitafakari kitu. Pia akamtazama Frank usoni na kwa bahati mbaya au nzuri macho yao yakagongana, Happy akawahi haraka kushusha macho chini, aliona aibu, hasa akikumbuka jana yake.
MARIA: Mimi angalau hilo swali la kwanza naweza kujaribu.

SEHEMU YA 69


FRANK: Usijali, hapa tunajadiliana, ebu jaribu.
MARIA: Kwa ninavyojua, ili uwashinde washindani wako kwanza ni lazma uwajue, lazma uwafahamu vizuri ili wasikupe shida. Hakikisha unatambua namna wanavyoziendesha biashara zao. Pili, jifunze. kuwa mtu wa kutazama mambo na kuyafanyia kazi, hakikisha unakuwa mchunguzi. Jifunze kutoka kwao ili ubadilike na kuwazidi. Tatu, wajue wateja wako hasa wale wakubwa, hakikisha unawamiliki wateja wako ili usiruhusu waende kwa washindani wako.
(Maria akaishia pointi tatu, Frank akaja kujazia)
FRANK: Pia unaambiwa ili uwashinde ni lazma uchukulie nguvu zako, mipango yako au malengo yako kama mapungufu yako (position your strength to weakness). Ukifanya hivyo utapata akili ya kuwa mbunifu. Na ikitokea ukawazidi ubunifu washindani wako basi wateja wote watakua wako. Alafu pia tengeneza taswira ya biashara yako (brand), hakikisha biashara yako inajulikana kuwazidi wao. HAPPY: Hapo sasa nimepata picha, ina maana unaweza kuongeza point kama; kutengeneza soko lako, pia inatakiwa uwe tofauti na wao.
FRANK: Ndio Happy, lazma ulijue soko lako, pia mfumo wa biashara yako kuanzia bidhaa na shughuli zingine zinatakiwa ziwe tofauti na za wenzio.
HAPPY: Sasa nimeelewa, na vipi kuhusu swali la pili? MARIA: Mmh! swali la pili mi hata silijui mwaya, labda pasua kichwa!
(wakacheka kwa pamoja)
FRANK: (akiwa anacheka) Pasua kichwa ndio nani? MARIA: Si wewe, kila mtu darasani anakuita pasua kichwa..
(Frank akacheka tena)
HAPPY: Haya pasua kichwa tujibie basi swali la pili!
FRANK: Iko hivi, watu wengi uwa wanapenda sana kuzificha biashara zao. Wengine ni kwasababu ya woga; mfano woga wa kodi na wengine hawana uelewa kuhusu umuhimu wa kusajili biashara zao. Kwa kawaida biashara ikifikia hatua fulani, ni muhimu na itakua vizuri kama utaisajili kupitia taratibu zote za kiusajili. Mfano kupitia article of associations na memorandum of associations. Kuisajili biashara kuna faida zifuatazo;
1. Unatambulika kibiashara. Serikali, wateja na mamlaka zingine zitakujua.
2. Ni rahisi kupata mikopo. Mikopo ni chanzo chako cha kifedha, ukisajili biashara itakua rahisi kupata.
3. Heshima mbele ya wateja. Wateja wanapenda biashara inayotambulika kisheria.
4. Rahisi kupata wasambazaji wa bidhaa zako (suppliers). Inakuwa rahisi watu kukuletea bidhaa za kuuza.
5. Unajiamini katika biashara. Ukisajili biashara utaifanya bila plesha.
6. Na zinginezo nyingi... Ebu umizeni vichwa na nyie...
(wakacheka)
Baada ya kujadili maswali yale, walikaa mule ndani wakipiga stori mbili tatu wakipanga ni kwa namna gani watafaulu test hiyo, wakakubaliana kusoma kwa bidii zaidi.
FRANK: Jamani sahizi saa 7 na dakika 22 mchana twendeni tukale msosi.
MARIA: Aah! mi nitaenda badae badae sahizi sina njaa labda happy.
Sasa Happy akafikiria, aliitamani sana hiyo nafasi lakini akaona akikubali mbele ya Maria itakua sio vizuri.
HAPPY: Mi mwenyewe nitakula baadae.
FRANK: Kwahiyo hamtaki kula? basi sawa, tutakutana tena baadae.
Waliagana, Frank akaelekea mgahawani, Happy na Maria wakaelekea hostel japo moyo wa Happy uliwaza mgahawani tu.
******
HOSTEL:
Loveness baada ya kutoka kwenye kipindi ambacho akikufanyika ile asubuhi, akarudi hostel. Alilala na kuamka lakini Happy hakutokea, akatazama muda ilikuwa ni saa saba na nusu, akaamua kuingia kuoga ili atoe uchovu. Baada ya kuoga akaona bora aende kula kabla ya kuingia darasani kujisomea, ndipo akaelekea mgahawani.
MGAHAWANI:
Loveness baada ya kufika mgahawani, akaagiza chakula na kukisubiria. Baada ya muda akapewa chakula chake ambacho alikipokea na kugeuka akitazama wapi akakae.
Akaona kila meza ilikuwa na watu. Lakini kuna meza moja ilionekana ikiwa na chakula juu lakini mwenye chakula hakuwepo. Loveness bila kujiuliza akaenda kukaa kwenye ile meza. Nae Akaweka chakula mezani na kwenda kunawa mikono ili aje kula.
Baada ya kunawa akarudi kwenye meza ya ke, akaona kuna mtu aliyempa mgongo amekaa kwenye meza ile. Hakuwa na wasiwasi, akapita upande wa pili na kukaa.
Sasa ikawa upande mmoja ni Loveness na upande wa pili ni yule kijana. Loveness anakuja kuinua uso, macho kwa macho na Frank, moyo ukapiga paah! Sehemu ya 31
Akaanza kutetemeka, alitamani kuchukua sahani yake na kuondoka, lakini alishindwa. Akaangaza macho pembeni akaona kila mtu yuko bize na mambo yake.
Frank alishagundua kwamba Love pale alipo hakuwa na amani, na alijua kwanini Love hana amani, alichokifanya ni kumsalimia;
FRANK: Mambo Love!
Love plesha ilizidi, hakutamani hata chakula chake, ile salamu ndo ilimchanganya kabisa, alishindwa hata kujibu;
FRANK: Love nakusalimia...
LOVE: Eeh! mmh! safi. Mambo na wewe!
FRANK: Poa tu. Karibu.
LOVE: Asante!
Japo Frank alionekana kuwa mtulivu lakini Love bado hakuwa na amani. Alikua akila kidogo na kuangalia pembeni kama mkimbizi. Frank aliligundua hilo;
FRANK: Loveness!
LOVE: (alishtuka na kumtazama Frank) abee!
FRANK: Kuwa na amani, jisikie huru. Najua unawaza kama ungeondoka eneo hili. Lakini wewe kama mwanachuo unayejiamini na kujielewa huna haja ya kuwa hivyo.
LOVE: Mmh! hakuna shida.
FRANK: Labda niseme tusameheane!
LOVE: Kwanini?
FRANK: Usiulize kwanini, kwani unataka kusema hauna tatizo na Mimi?
LOVE:(kwa wasiwasi na aibu) Ndio sina tatizo na wewe!
FRANK: Kama hauna tatizo sawa.
Wakaendelea kula, kila mtu alikuwa kimya. Lakini Love akakumbuka kuhusu ule mpango wa kina Issa, na muhusika alikuwa mbele yake. Basi, akainua macho kwa wizi na kumtazama Frank, hakupata picha jinsi ya kuanza kumwambia.
Frank alikua bize na chakula chake. Alionekana kuwa kawaida sana jambo lililomshangaza Love.
Love alijua Frank ni mtu wa kuongea ongea na sifa mbele za watu. Akakumbuka tangia siku ya kwanza wanabishana akajua huyo mtu ni muongeaji.
Kutokana na mawazo, Love akajikuta anainua uso wote na kumtazama Frank jinsi anavyokula, akamtazama kwa makini huku akikumbuka matukio yote kuhusu mtu huyo na yeye, akamalizia kukumbuka tukio la kumsaidia kujibu swali, Love
a kaji kuta anatabasam.
LOVE: Umesema tusameheane sio?
FRANK: Lakini sisi hatuna tatizo!! (aliongea frank kwa kujiamini)
LOVE: Ni kweli, ila tulishawai kugombana!
FRANK: Wapi tuligombana?
LOVE: Darasani kwenye kipindi.
FRANK: Mbona sikumbuki tuligombana kuhusu nini? LOVE: Kwahiyo unataka kusema hukumbuki?
FRANK: Ndio, ebu nikumbushe!
LOVE: Na mbona mara ya kwanza ulinambia tusameheane, Ulimaanisha tusameheane kwa lipi?
FRANK: Nilikosea.
FRANK: Nikoje?
LOVE: Mbabaishaji hivyo!
FRANK: Hamna bhana, ebu kula.
LOVE: Lakini wewe ndie ulikua mgomvi ile siku, ulinifanya nilazwe hospital.
FRANK: Uliamua tu kwenda kulazwa, sasa kilichokupeleka hospital ni kipi?
LOVE: Ndo majibu gani hayo, yani niliumwa kwa ajili yako, tena hata hospital hukuja kuniona, alafu leo unaniruka?
FRANK: Mbona hata Mimi juzi nililazwa hospitali, vipi ulikuja kuniona?
LOVE: Kwani mi ndo nilisababisha uumwe?
FRANK: Hata Mimi sikusababisha wewe uumwe!
LOVE: Majibu yako yalikuwa mabaya, alafu huna huruma.
FRANK: Kwan i juzi ulivyomuambia Yuma hajielewi, Yuma alilazwa hospital ?
Swali hilo lilimfanya Love amshangae sana Frank, alimuona ni mtu mwenye majibu aliyoyajua mwenyewe, alimtolea macho hadi Frank akacheka na kuuliza;
FRANK: Mbona unanitolea macho hivyo?
LOVE: Yani kumbe una majibu ya hovyo hovyo hivyo? FRANK: Nadhani ni kwasababu una maswali ya hovyo hovyo!
LOVE: Ninii? (akasimama)

SEHEMU YA 70


FRANK: Eeh, hivi Love unataka kusema hadi leo huiamini biashara?
Love alikuwa kimya, akamtazama Frank kwa macho makali. Hata ile ishu ya mipango alokuwa anapangiwa na kina Yuma hakutaka kumwambia kutokana na hasira. Akamuona Frank kama sio mtu sahihi wa kuwa hata rafiki ake. Damu zao ziligoma kuendana.
LOVE: Sawa kwaheri!
FRANK: Na hiki chakula chako?
LOVE: Kula wewe ufahidi..
(aliondoka zake kwa hasira akimuacha Frank akitabasam kwa mshangao)
******
HOSTELI:
Mida ya saa nane na nusu mchana, Happy baada ya kukaa sana Hostel akakumbuka waliachana na Frank ambaye aliondoka kwenda kula.
Akafunga mlango haraka na kutoka mule chumbani. Nae akaamua kwenda mgahawani labda atabahatika kukutana na Frank. Lakini akiwa anawahi kuelekea nje, mara akakutana na Love uso ukiwa umepambwa na hasira. Ilibldl Happy asimame kwanza;
HAPPY: We Love vipi? mbona uso upo hivyo?
Lakini Love hakujibu. Alimpita Happy kama hamjui vile, akaelekea chumbani. Happy mipango ya kwenda mgahawani ilikufa, akaamua kurudi tena chumbani ili ajue rafiki yake alipatwa na nini.
Akamkuta Love kitandani kajifunika na shuka. Happy akajikuta anacheka;
HAPPY: Bibi wee! do nini sasa?
Lakini Love hakujibu, aliendelea kujifanya amelala. Happy akaona ujinga, akamfunua lile shuka, akakuta Love katokwa na jicho la hasira!
HAPPY: We tatizo nini?
LOVE: Aah! kuna limtu limeniboa.
HAPPY: Wanaume hao, nilikuambia nikupe sheria h utaki.
LOVE: Yani we mawazo yako ni mapenzi tu, huwezi kuwaza vitu vingine?
HAPPY: Sasa nitawaza vipi wakati sijui umekasirika kwa lipi?
LOVE: Kwahiyo mtu akikasirika ni mapenzi?
HAPPY: Sawa, haya nambie kipi kimekukasirisha?
LOVE: Ebu niache uko, we si ulikua unatoka, safari njema.
Happy akacheka. Akajua hakuna kitu kingine kilichomchukiza Love zaidi ya mapenzi. Aliwaza lazma Love anasumbuliwa na mwanaume ila hataki kusema.
HAPPY: Sawa mama kwaheri. Ila mambo yakikufika shingoni nijulishe nikupe hatua za kufanya. (aliongea happy huku akicheka na kutoka nje kuelekea mgahawani).
Huku nyuma Love akaamka, Akakaa kitandani vizuri, akajiuliza;
"Ina maana huyu Happy ameshampata huyo mwanaume wake alokua akimsumbua? maana kila siku sheria, eti sheria zinasaidia, sasa kama zimemsaidia mbona hatulii?. Kwanza inabidi nifanye uchunguzi nimjue huyo mwanaume aliyempata kupitia sheria. Maana kila siku ananizungusha mara hivi mara vile, sasa nitaanza tena kumfuatilia."
Happy nae akiwa njiani akawaza;
"Hivi huyu Love aanasumbuliwa na mwanaume gani? maana sikuhizi ameanza mambo ya siri siri! mara arudi kanuna, mara nimkute na mwanaume, na usikute leo kaumizwa na huyo mwanaume wake. Inabidi nianze uchunguzi. Nitaanza kumfuatilia nimjue huyo mwanaume wake"
******
Frank baada ya kutoka mgahawani, moja kwa moja akarudi hostel kwake. Akajiona mpweke kukaa mwenyewe chumbani. Alianza kukumbuka jana yake, yaliyotokea kati yake na Happy, akakumbuka utani wa Happy, akakumbuka jinsi alivyopaliwa kutokana na raha za kufurahishwa na Happy, mwisho akakumbuka jinsi walivyotaka kukiss, akatabasam. Akaona kuna umuhimu wa Happy kuwepo maeneo yale. Akavuta simu yake na kuamua kumpigia Happy;
HAPPY: Hallo Frank!
FRANK: Hallo Happy, upo wapi?
HAPPY: Niko huku mgahawani nimekuja kula (aliongea kwa utulivu na mahaba yote)
FRANK: Nimekumiss!
HAPPY: Ninii ? (alishtuka, nusura adondoshe sahani ya chakula, hakuamini alichosikia)
FRANK: Au hutaki kumisiwa?
HAPPY:Nataka bwanaa! (alideka)
FRANK: Basi kula uje rum kwangu, nimemiss sana utani wako!
HAPPY: Mh! Sawa nakuja!
(simu ikakatwa)
Lakini Happy akaona kuchelewa, akanunua kontena la chakula, akaweka haraka kile chakula. Akatoka mgahawani. Nje akanunua baadhi ya matunda ikiwemo matunda mawili ya apple, akatia kwenye mfuko na kuondoka.
Sasa Frank akiwa kavaa suruali ya track, kifua kikiwa wazi alikuwa anapanga chumba chake vizuri maana alijua Happy atawasili pale baada ya kula.
Bila kujua kwamba Happy hakula chakula zaidi ya kuweka kwenye kontena. Frank akiwa hana hili wala lile akasikia mlango ukigongwa. Hakuwa na plesha, alijua labda mwanachuo mwenzie wa kiume wa pale hostel. Kama ujuavyo hostel kuna kuazimana vitu n.k.
Akiwa na mawazo hayo alikwenda kufungua mlango vile vile akiwa kifua wazi, hakuamini ile anafungua mlango kumbe alikua ni Happy. Happy nusura adondoshe zile mfuko wa vyakula!

ITAENDELEA
WHATSAPP 0768315707
 
SEASON 04

TAMTHILIA: MTU ALIYETHIBITISHWA KWA MAISHA YANGU
CERTIFIED PERSON OF MY LIFE (CPL)
(71-75 )

( SEHEMU YA 71 )

WHATSAPP 0768315707

Akiwa na mawazo hayo alikwenda kufungua mlango vile vile akiwa kifua wazi, hakuamini ile anafungua mlango kumbe alikua ni Happy. Happy nusura adondoshe zile mfuko wa vyakula!
(CHUMBANI).
SHERIA NA. 4 MUONYESHE HISIAZAKO.
Frank akajikaza kiume. Ha kuta ka kuweweseka, akamkaribisha Happy ndani. Happy nae kwa aibu alipita mlangoni kwa haraka ili asione kifua. Alikaa kwenye kiti macho akitazama pembeni kwenye kabati la nguo. Frank akafunga mlango na kurudi, nae akakaa kwenye kiti, akatabasam baada ya kuona Happy anaangalia pembeni.
HAPPY: Frank!
FRANK: Naam!
HAPPY: Naogopa, nakuomba vaa shati.
FRANK: Sawa! basi nipe shati la kuvaa.
Happy akaona kama anamfanyiwa kusudi vile. Akasimama na kufungua kabati, akachukua shati moja na kumrushia Frank akiwa anaendelea kutazama pembeni.
HAPPY: Ukimaliza kulivaa niambie!
FRANK: Sawa.
(Lakini Frank hakulivaa lile shati, alitaka tu kutaniana na Happy. Alipenda jinsi Happy anavyo ogopa)
FRANK: Tayari nimeshalivaa!
Happy akageuza macho, ile kutazama akakutana na kifua, akashtuka na kugeuka tena haraka alafu akatoa sauti ya kama kudeka hivi "Aaahh!"
Frank alicheka sana, akajisikia raha, na vile ndivyo alivyokua anataka. Ndio maana alikua anataka Happy awe karibu yake kwasababu walifurahishana.
Kumbe, Happy licha ya kumlazimisha Frank avae shati, moyoni alitamani sana hali ile iendelee, maana hicho ndicho alichokua akikiomba siku zote. Hakika aliona hakuna kama sheria za mapenzi, akajikuta anatabasam pekeake.
HAPPY: Frank acha utani buana, vaa basi!
FRANK: Kwani nikiwa hivi kuna shida gani?
HAPPY: Mi naogopa mwenzio!
FRANK: Unaogopa nini?
HAPPY: Naogopa tuu!! (akideka)
Frank akaamua kuvaa shati, na Happy sasa akageuka wakatazama.
FRANK: Hapo umefurahi?
HAPPY: Hapo sasa siogopi! (aliongea Happy na kutoa tabasam pana lililopendwa na Frank)
Hisia zilikua kali Kati yao. kila mmoja alimtazama mwenzie kwa macho ya matamanio. Walikaziana macho hadi Happy uvumilivu ukamshinda, akaona ni bora afungue ram bo zake, akatoa chakula na matunda akaweka mezani, lakini yale matunda mawili ya apple wala hakuyatoa. Akayaficha, moyoni akajisemea;
"Hizi apple ndizo zitakazonikamilishia sheria ya nne leo"
Baada ya kuwaza kwa muda akamkaribisha Frank kwa ajili ya chakula lakini Frank alikataa akidai ameshakula. Happy hakushindwa, alimlazimisha Frank ale japo matunda. Ushawishi wa mwanamke ni mkubwa, ilibidi Frank achukue tikiti na kuanza kula. Happy nae akaendelea kula chakula chake ambacho alikatiza kule mgahawani.
Happy moyoni alikuwa na mawazo ya namna gani akamilishe sheria namba nne, akaikumbuka vizuri "Muonyeshe hisia zako". Akawaza;
"Mmh! hisia ni kama mitego tu. Hapa leo ni mitego hadi nipate busu, ikiwezekana sheria zote nimalizane nazo leo, nishachoka kusubiri"
Sasa wakiwa wanakula, kila mmoja aliikua kimya. Happy akaona akizubaa atakuja kujilaumu, akaanza kuchezesha miguu chini ya meza, kitendo kile kiliifanya gauni zuri na fupi alilolivaa kupanda juu na kuyaacha mapaja meupe ambayo yalijazwa na hips za wastani.
Baada ya kufanya hivyo akaona haitoshi, akajitikisa kidogo eneo la kifua. Mtikiso huo ulifanya kifua chake kilichopambwa na viembe vidogo vidogo vyenye ncha kali zilizosimama kuwa wazi na kuwa tayari kumvutia mwanaume yeyote atakayeviona.
Happy alikua makini, alifanya hiyo michezo yote pasipo Frank kuona wala kugundua chochote. Nae Frank alifanya makosa, ilikua ni wakati akipeleka mkono chini ili aiweke vizuri suruali yake ndipo kwa bahati mbaya mkono ulijikuta upo kwenye paja laini kabisa, paja lenye nuru, lisilo na doa.
*******

SEHEMU YA 72


Mida hiyo ya kama saa 10 jioni, Maria akiwa hostel kwake akakumbuka kuwa walikubaliana; Yeye, Frank na Happy wakutane kwa ajili ya kujisomea kujiandaa na jaribio maalumu (special test).
Kibaya zaidi sio Frank wala Happy ambaye alimtafuta ili wakasome. Kila mtu alikua bize. Maria akaona isiwe kesi, akatoka chumbani kwake na kwenda chumbani kwa Happy lakini alimkuta loveness tu.
MARIA: Mambo!
LOVE: Poa, vipi?
MARIA: Safi. Samahani, kuna mdada flani anakaa humu anaitwa Happy?
LOVE: Ndio vipi?
MARIA: Kaenda wap?
LOVE: Katoka sijajua kaenda wapi, wa nini kwani?
MARIA: Ni rafiki yangu, uwa tunasoma pamoja!
LOVE: Kwahyo mlitaka mkasome?
MARIA: Ndio. Tulipanga tukasome muda huu.
LOVE: Umejaribu kumtafuta kwenye simu?
MARIA: Mmh! hapana, alafu ngoja nijaribu kumtafuta.
Maria akatafuta namba ya Happy na kujaribu kumpigia, lakini namba haikupatikana, alijaribu tena na tena lakini bado haikupatikana, akaacha.
MARIA: Hapatikani.
LOVE: Sawa! akija niseme alikuja nani?
MARIA: Mwambie Maria.
LOVE: Poa.
Maria akaamua kuondoka na kurudi chumbani kwake, akajisemea;
"Sasa kama Happy hapatikani si bora nimpigie Frank nijue nae inakuaje"
Akatafuta namba ya Frank akitaka kumpigia, lakini akuipiga akaamua kuacha, akajisemea;
Huyu Frank haina haja ya kumpigia, wacha nimfuate huko huko hosteli kwake'
Maria akachukua kibegi chake kidogo, akafunga mlango wa chumba na kuondoka zake.
Upande wa pili mitego ilikua ishategwa kila sehemu, mwindaji alisubiria marejesho, na ndivyo ilivyokuwa. Frank baada ya kugusa paja la Happy kwa bahati mbaya, alishtuka na kutoa mkono haraka. Akamtazama Happy usoni, akamuona hana wasiwasi, ndo kwanza alijidai yuko bize na chakula. Nae Frank hakuondoa macho mwilini kwa Happy, zaidi akayaamisha kutoka usoni hadi kifuani, hapo ndipo mwili wake uliposisimka, akajikuta anameza funda la mate, mate ya uchu, uchu wa hisia za mapenzi.
Happy kupitia jicho la pembeni alishamuona Frank akitamani, hilo ndilo alilolitaka. Akabadili mwelekeo wa macho yake, kutoka pembeni hadi usoni kwa Frank, macho yakatazamana, hayakuwa macho yakawaida, yalikua ni yale macho ya mahaba, ni sheria namba nne.
Walitazamana kwa muda, Happy alitamani kutoka pale alipo na asogee mahali alipokuwa Frank, akajiuliza atasogeaje sasa, aanze vipi Happy wa watu, akaita;
HAPPY: Frank.
FRANK: Naam! (huku bado wakitazamana)
HAPPY: Nina zawadi yako, nataka nikulishe.
FRANK: Mmh! unilishe? ni zawadi gani hiyo?
HAPPY: Je utaniruhusu nikulishe?
FRANK: Ndio, lakini ni zawadi gani?
HAPPY: Usijali.
Happy akauchukua ule mfuko na kutoa apple, akalificha kwa nyuma. Akaizunguka ile meza ndogo na kumfuata Frank pale alipokaa, akasimama, wakatazamana.
Kwa mapenzi mazito, Happy akamshika na kumvuta Frank juu ishara ya kumtaka nae asimame. Frank akasimama, na sasa wakawa sawa, japo Happy alizidiwa urefu kidogo lakini hakikuharibika kitu, maana kimapenzi hiyo ilikaa poa.
Mawazo ya Happy yalimpeleka mbali, alihisi ni kama ulimi wake upo ndani ya mdomo wa mtu aliyekua mbele yake. Mawazo hayo yalimfanya atabasam. Tabasam pana, hata frank akashangaa.
Happy akapeleka apple mdomoni kwa Frank. Nae Frank hakuwa na hiyana, akalipokea. Akalimega na kuanza kulila. Kosa kubwa lilikua ni kutazamana kwao. Kwasababu Happy aliona kama tatizo ni sheria, ameshazifuata zote. Alichokifanya ni kufumba macho na kupeleka mdomo wake kwa Frank, alikua ni kama anabashiri, aliomba mdomo wake upokelewe ili aishinde bashiri yake. Frank bila kujiuliza akaupokea na sheria namba tano ilianza kufanya kazi.
Wakajikuta wapo kitandani wakibadilishana maji maji yenye kemikali za kulainisha chakula, hakika ilikua raha. Mchezo ule uliwanogea mara baada ya Happy kuzidiwa na kutoa ishara ya kwamba; ulikua ni muda sahihi wa Frank kumchuna mbuzi na kumuandaa kwa ajili ya sherehe.

SEHEMU YA 73

WHATSAPP 0768315707

Wakati Frank akitaka kuitii ishara ya Happy, ni pale ambapo alishika zipu iliyopo mgongoni kwenye gauni la Happy, ndipo kukasika; "Ngo ngo ngo, Frank" kuna mtu aligonga mlango.
BAR:
Mida hiyo hiyo ya jioni, Issa, Meshack, Yuma na
Tarick walionekana kat ika Baa moja kubwa ambayo ilikua nje kidogo ya chuo chao. Vinywaji vikiwa katikati, walionekana wakiongea mambo yao ya siri.
Wakiwa wanaendelea kupata vinywaji mara aliingia mwalimu anayewafundisha somo la biashara afahamikaye kama DR KIPOZI. Hapo ndipo waliacha kila kitu na kuanza kumwangalia mwalimu huyo alichokua akikifanya.
Dr kipozi ukiachilia mbali aina ya ufundishaji wake ambao ulipendwa na wanachuo wengi kutokana na uchekeshaji wake kwenye kipindi, urafiki wake na wanachuo, upendo wake kwa kila mtu na unadhifu wake katika mavazi jambo ambalo liliwafanya wanachuo kumuita mwalimu wa mavazi, lakini pia alikua maarufu wa chinichini kwa kuwasaidia wanachuo wanaosaidika kufaulu mitihani ya chuo.
Alikua ni mzee madili. ili akusaidie lazma na wewe umsaidie. Wanachuo wengi wengi wa kike walipitia mikononi mwake muda tu walipokuwa tayari kutoa msaada. Wale wa kiume walikua wakiweka chenji mezani nae aliwaonyesha njia, huyo ndiye Dr kipozi. Basi Dr kipozi baada ya kuingia kwenye ile baa yenye watu wengi walioingia na kutoka, moja kwa moja alienda kukaa kaunta. Akaagiza bia.
Wale wanne baada ya kuona Dr kaagiza bia, wakageukiana;
YUMA: Wazee si mlisema huyu ticha kreti mbili tu chali?
TARICK: Yani huyo ticha kuna vitu vitatu ukimfanyia lazma uende nae sawa.
YUMA: Vitu gani?
TARICK: Kitu cha kwanza pesa, weka mezani dau mtaenda sawa. Kitu cha pili bia, weka kreti mezani hapo mtakuwa marafiki. Kitu cha tatu ni madem, ticha anapenda chini huyoo!
YUMA: Sasa kama ni hivyo tuhakikishe leo bia anazitapika.
MESHACK: Pia, tunampiga na helaa!
ISSA: Alafu niwape habari kubwa?
WENZAKE: Eeeh tupe! (waliitikia kwa pamoja)
ISSA: Mnamjua yule manzi mweupee, yule mwenye mzigo flani nyuma, anayependa kuongea ongea?
TARICK: Yupi! au yule mcharuko wa darasa, jasmine au?
ISSA: Eeh! huyo huyoo! basi niwaambie tu, huyo ticha na ujanja wake wote, yule manzi kamfukuzia wee lakini kamshindwa.
YUMA: Duh! kwahiyo unataka kusemaje?
ISSA: Yani tukitaka tumteke akili Dr kipozi, tufanye mpango yule manzi ampate, basi.
MESHACK: Basi hilo limepitaa, hapa tuanze na bia, tunaweka pesa mezani, alafu tunampelekea jasmine, shughuli kwisha!
Bila kuchelewa wakasimama. Wakaenda moja kwa moja kwenye meza ya Dr kipozi, wakamsalimia kwa kumchangamkia hadi Mwalimu akachanganyikiwa.
YUMA: Wewe dada, muhudumu! mpe mwalimu wangu bia anazozitaka... Ikiwezekana mtolee kreti hata tatu.
Dr kipozi meno yote yakawa nje..

SEHEMU YA 74

WHATSAPP 0768315707

Bila kuchelewa wakasimama. Wakaenda moja kwa moja kwenye meza ya Dr kipozi, wakamsalimia kwa kumchangamkia hadi Mwalimu akachanganyikiwa.
YUMA: Wewe dada, muhudumu! mpe mwalimu wangu bia anazozitaka... Ikiwezekana mtolee kreti hata tatu.
Dr kipozi meno yote yakawa nje.
HOSTEL KWA FRANK:
Kitendo cha mlango kugongwa kulifanya Frank na Happy washtuke na kuganda kwa muda. Ilibidi Frank aache zoezi lake la kuitoa gauni mwilini kwa Happy. "Ngo ngo ngo, Frank ?" Ilisikika tena sauti kutoka nje. Hadi hapo walishafahamu sauti ya mtu aliyekuwa akibisha hodi. Ilibidi Happy atumie akili ya haraka; HAPPY: Frank!
FRANK: Naam!
(wote walikua wakihema utadhani walishakamilisha sheria, kumbe mchezo ulikwama, ni hofu tu iliwajaa)
HAPPY: Zima simu yako.
FRANK: Kwanini? (akishangaa)
HAPPY: Fanya haraka, zima simu yako.
(waliongea kwa kunong'ona)
Frank akachukua simu yake na kuizima alafu akamtazama Happy ambaye alitulia kusikiliza kinachoendelea nje ya mlango.
Sasa pale mlangoni Maria baada ya kugonga sana mlango bila mafanikio akaona isiwe kesi, akashika simu yake na kumpigia Frank, namba ikawa haipatikani, alichoka.
"Yani Happy hapatikani, Frank nae hapatikani, na tulipanga vizuri kwamba muda huu tukasome kujiandaa na mtihani, au wenzangu wametangulia kusoma?, sasa mbona hawajaniambia? na kwanini wazime simu? " Maria aliwaza kwa kujiuliza maswali yasiyo na majibu.
"Au niende nikawatafute uko uko darasani" Maria alijisemea na kisha akaanza kuondoka eneo hilo.
Kule ndani angalau sasa Frank aliweza kupumua, maana alihisi mkojo ulibana. Hakujua ingekuaje kama angekutwa na Happy. Japo Maria ni rafiki yake lakini asingewaelewa.
Lakini kwa upande wa Happy alichukia mno. Yani alikua akikamilisha sheria bila matatizo, alafu anatokea mtu anamuharibia.Moyoni alimlaumu sana Maria.
"Huyu Maria nae! anawaza kusoma soma tu, yani alishindwa kuvumilia huko hostel kwake hata kidogo? au alishindwa hata kupiga simu, anakujaje bila taarifa, aah" Happy aliwaza akionyesha kukasilika. FRANK: Happy...
HAPPY: Abee!
FRANK: Nakuomba tuondoke tuwahi maeneo ya madarasa, tukajifanye tunatafuta darasa la kujisomea.
HAPPY: Kwanini?
FRANK: Tufanye hivyo ili Maria asije akatufikiria vibaya. Ikiwezekana tumuwahi kabla hajafika darasani, alafu tumpigie simu kwamba aje.
HAPPY: Sawa haina shida. (aliongea Happy na kutoa tabasam hafifu lakini moyoni alichukia, tena sana) Frank akabadili nguo haraka, Happy nae akajiweka sawa, wakachukua baadhi ya madaftari na simu wakatoka.
BAR:
Dr kipozi alikua anabadili vyupa vya bia. Bia za bure. Na alikua akikaribia kumaliza creti. Lakini hakuwa pekeake, alikua na vijana wanne, watatu wakiwa wanakunywa bia alafu mmoja (Issa) akiwa na soda.
Sasa awa wengine tayari akili na sauti vilianza kuchanganywa na ulevi, ndipo wakaanza kuropoka dili zao;
TARICK: Ticha eeh, asee sisi tuna mchongoo!
DR KIPOZI: Mchongo gani?
TARICK: Tunataka tukupe pesaa kama upo tayari!
DR KIPOZI: Aah nipo tayari, siwezi kataa pesa. (huku akicheka, alafu akachukua bia akapiga funda moja) (Vijana wakakonyezana, ishara ya kwamba yeyote kati yao aanze kuongea)
ISSA: Ticha sahau kuhusu hizi bia ambazotumekupa ofa wewe kama mwalimu wetu. Hapa tulipo tuna pesa ambazo kuna jambo tunataka utusaidie.
DR KIPOZI: Jambo gani? (aliongea kilevi)
ISSA: Aah! ni ishu ya siri kidogo.
DR KIPOZI: Acha utoto, weka siri mezani, weka pesa mezani, maisha yenyewe ni mafupii (aliongea na kuwafanya wale wanne wapate nguvu ya kuongea) YUMA: Kuna jamaa tunasomanae katuibia nguo na laptop. Sasa tulifikiria kumpeleka kwenye uongozi wa chuo hili afukuzwe chuo lakini tunamuonea huruma. Tumewaza na kuwazua tumeona huyo jamaa dawa ni kumuharibia kidogo angalau na yeye apate maumivu. Sasa sisi ombi letu ni moja tu, jamaa ana kiburi sana darasani, anapenda sifa za kijinga, yani akifahulu test darasa zima litajua kutokana na sifa zake. Imekua kama kero, kila mtu hampendi. Tunakuomba sana, kwenye mtihani wako wa mwisho wa biashara, jamaa afeli.
(Dr kipozi alikuwa akisikiliza kwa makini)
DR KİPOZİ: Aah! nimewasikiliza sanaa, Mimi sitaki kumjua mtu huyo. Lakini nataka kujua mnataka afeli, namfelishaje? wekeni mambo mezani, mbona mnajificha ficha.
TARICK: Ticha kama tulivyosema, hapa tuna pesa. Sisi ukikubali kutusaidia hiyo ishu tunaweka mzigo mezani.
DR KİPOZİ: Mna bei gani?

SEHEMU YA 75

WHATSAPP 0768315707

(Baada ya ticha kuulizia bei, ilibidi vijana watazamane na kujiuliza wampe bei gani)
MESHACK: Sisi tumekuandalia laki tatu (alafu akatulia kumsikiliza Dr kipozi atasemaje) (Dr kipozi akaifikiria ile bei, akafikiria jambo lenyewe ni kufelisha tu, tena somo lake, yeye ndo atasahisha mitihani, na yeye ndo atapanga matokeo.)
DR KIPOZI: Kwanza mnataka kumfelisha masomo mangapi?
YUMA: Ni moja tu. Wala hatutaki kumuumiza sana!
DR KIPOZI: Sawa, lakini ongezeni pesa.
YUMA: Ticha sisi tuna hiyo tu, tusaidie. Pia, tupo tayari kufanya jambo jingine utakalotaka. (walimtega kwa jasmine)
DR KIPOZI: Hapana, kumfelisha mtu asiyekukosea kwa ajili ya ugomvi wa watu wengine Mimi ndiye nitapata dhambi. Sasa siwezi kupata dhambi bila kufanya dhambi. Na ill niifanye dhambi hii nataka muongeze laki mbili.
ISSA: Duuh! akini ticha sisi hapa kwasasa Tuna laki tatu tu.
DR KIPOZI: Hilo halina shida. Nipeni hiyo laki tatu alafu laki mbili mtanipa baada ya matokeo kutoka na kazi kufanyika.Tena nadhani nyinyi wenyewe mtaniongezea pesa nyingine.
(Wale wanne baada ya kusikia hivyo wakakubali. Issa akatoa bahasha ya pesa akamkabidhi Dr kipozi ambaye bila kuzihesabu akaziweka kwenye koti lake la suti alafu akatulia.)
DR KIPOZI: Alafu mmesema mtanisaidia jambo lolote nitakalotaka?
YUMA: Ndio mwalimu.
DR KIPOZI: Kuna binti ambae nae anasoma biashara. Nadhani mnasoma nae, anaitwa Jasmine, vipi mnamjua?
(Wale wanne wakatazamana, wakatabasam)
ISSA: Eeh! tunamfahamu vizuri sana.
DR KIPOZI: Sasa ili niwasaidie haraka jambo lenu, naomba kabla ya mtihani wa mwisho binti huyo nimpate.
ISSA: Limekwisha hilo mwalimu. (Dr kipozi alifurahi sana, wakapiga kelele na kugonga meza)
DR KIPOZI: (akiwa anacheka) Sasa kesho asubuhi nitakuwa pale ofisini kwangu, mje mniletee namba ya usajili na jina kamili la huy o mlengwa.
*******
DARASANI:
Frank na Happy walishamuwahi Maria, wakatafuta darasa na kutulia.
FRANK: Wewe ondoka, niache Mimi.
HAPPY: Kwanini niondoke?
FRANK: Tujifanye hatukuwa pamoja. Nenda kakae darasa lolote. Mimi nitampigia Maria aje, akija nitajidai nakupigia na wewe ili aamini kwamba hatukuwa pamoja. Hakikisha simu inakuwa hewani..
HAPPY: Nimekuelewa (akaondoka)
(Frank bila kuchelewa akawasha simu na kumpigia Maria.... simu ikaita, na ikapokelewa)
MARIA: Kwahiyo nyie mmeamua kwenda kusoma kwa siri bila kuniambia, na simu mkazima, sawa tu.
FRANK: Aah! tumeamua na nani?
MARIA: Si wewe na Happy!
FRANK: Mimi mbona sipo na Happy!
MARIA: Mmh! wewe upo wapi ?
FRANK: Jjoo darasa namba 309 utanikuta.
(Maria bila kuchelewa aliwasili darasani. Akamkuta Frank pekee)
MARIA: Eeh! kumbe kweli uko pekeako. Umekuja hapa mda gani, na kwanini hukuniambia, na mbona simu ulizima?
FRANK: Nimekuja sio mda sana.Nilikua nikitafuta darasa, nilipanga nikilipata ndio niwapigie. Alafu simu nimeiwasha baada ya kulipata darasa.
MARIA: Kwaahiyo hata Happy ujamwambia?
FRANK: Ndio. Wacha nimpigie nimwambie aje.
Frank akajifanya kumpigia Happy simu, akamwambia aende darasa namba 309. Nee Happy akajidai kujichelewesha kwa dakika tano alafu ndo akaenda. Wakaaanza kusoma.
SIKU IKAPITA, IKAJA JUMAMOSI.
Majira ya asubuhi, Meshack, Yuma, Tarick na Issa walimpelekea Dr kipozi jina na namba ya usajili ya Frank, wakamalizana nae.
Frank, mida ya saa tatu akiwa amevalia prova jeusi na kofia yake akalngla darasani pekeake kujisomea. Alipenda sana muda wa kujisomea akae kwenye darasa la pekeake, kusiwe na watu au mtu mwingine. Alitaka darasa lisilo na kelele, hakupenda fujo mda wa kusoma. Akafunua kidaftari chake cha biashara na kuanza kupitia notes.
Lovenes, baada ya jana yake kushinda sana chumbani kwake pekeake pasipo Happy, akajiona kama anakaa bu re wakati mwenzie anatumia muda mwingi kusoma.
Akakumbuka jinsi Maria alivyomuulizia Happy ili wakasome, akagundua kumbe Happy uwa anaondoka mara kwa mara kwenda kusoma.
Akamtazama Happy ambae alikua amelala, ha kuta ka kumsumbua, akamuacha. Akaelekea bafuni na kuoga fasta kisha akachukua mkoba wake wa daftari akatoka na kuelekea darasani.
Kwakua ilikua jumamosi akakuta madarasa mengi yamejaa watu wakisoma, akaanza kutafuta darasa angalau lenye watu wachache ili akae asome.
Katika pitapita zake akakuta darasa ambalo lina mtu mmoja tu ambae alivaa koti aina ya prova, alafu kichwani alivaa kofia ya ile prova, hakumtambua. Kutokana na madarasa mengi kujaa, akaona angalau lile lenye mtu mmoja anaweza akakaa na kusoma kwa utulivu. Alichokifanya ni kulngla na kufunga mlango kisha akaenda kwenye kona ya upande wa pili ili awe mbali na mtu aliyemkuta darasani.
Yule mwenye prova alishamtambua dada aliyeingia muda huo, akatabasam alafu akavua ile kofia kichwani, kisha akatulia aone itakuaje.
Love akatoa daftari na kuanza kusoma. Baada ya kusoma kidogo, akageuka ilii amuone vizuri jirani yake, Alishtuka, HAKUAMINI.

ITAENDELEA
WHATSAPP 0768315707
 
SEASON 04

TAMTHILIA: MTU ALIYETHIBITISHWA KWA MAISHA YANGU
CERTIFIED PERSON OF MY LIFE (CPL)
( 76-80 )

( SEHEMU YA 76 )

WHATSAPP 0768315707

Sasa baada .
Love akatoa daftari na kuanza kusoma. Baada ya kusoma kidogo, akageuka ilii amuone vizuri jirani yake, Alishtuka, HAKUAMINI.
Alimtazama kwa kumkagua juu hadi chini alafu moyoni akajisemea "Mmh ni yeye".
Sasa akiwa anaendelea kumuangalia, Frank akainua uso ili nae amuangalie Love, ilibidi Love awai kushusha uso wake na kujidai yuko bize na masomo. Na sasa ikawa ni zamu ya Frank kumtazama Love. Alimkagua vizuri, kuna muda alitabasam alafu moyoni akajisemea;
"Inawezekana hajanifahamu maana navyomjua sidhani kama angeendelea kukaa humu ndani1'
Ikawa, pale Love alipoinua uso na kumtazama Frank,
Frank akashusha uso haraka akijidai yuko bize kusoma. Nae Frank alipoinua uso kumtazama Love, Love akajidai yuko bize na kusoma. Ilikua ni kama kamchezo flani hivi.
Hakuna marefu yasiyo na ncha, ilikua ni pale Frank alipoinua uso na kumtazama Love kwa mara nyingine alafu Love alichelewa kushusha macho chini, macho yakagongana, wakabaki wanatazamana. Kila mmoja kimya. Hakuna a I iy etaka kuanza kuongea. Love uso uliiva kwa vijihasira, nae Frank uso ulionyesha hana shida na mtu.
Walitazamana hadi Love aliposhusha macho na kujidai kusoma, Frank nae akaona poa, akaweka sawa daftari, akaendelea kusoma.
HOSTEL:
Maria kule hostel kwake akaona muda wa kujisomea umefika, akajiandaa na kwenda chumbani kwa Happy ambaye alimkuta anajiandaa.
HAPPY: Uko fasta kwenye suala la kusoma.
MARIA: Hicho ndicho kilichotuleta chuo.
HAPPY: Hata mimi naona. Vipi Frank ushampa taarifa?
MARIA: Bado! Mi sina dakika, kama unazo mpigie. (Ilibidi Happy ajaribu kumpigia Frank lakini namba haikupatikana.)
HAPPY: Hapatikani.
MARIA: Sawa! twende hostel kwake usikute bado kalala.
(Wakatoka na kwenda hadi hostel kwa Frank, lakini baada ya kugonga mlango wakagundua chumba hakina mtu.)
MARIA: Humu ndani hayupo, kwanza mlango umefungwa huu.
HAPPY: Atakua kaenda wapi?
MARIA: Yule usikute kashaenda kusoma. Ndo zake hizo. Ndio maana kazima simu. Hapo hadi apate darasa ndio atatuambia.
HAPPY: Basi twende huko huko labda tutamuona.
Wakaondoka.
DARASANI:
Viburi bado vilitawala. Hakuna aliyetaka kumsemesha mwenzie. Kila mmoja alijikubali mwenyewe.
Sasa Love katika kusoma soma kwake akakutana na swali ambalo lilimshinda. Akajaribu kulitafutia majibu mtandaoni lakini hakupata kitu. Alichambua notes zote lakini wapi. Akafikiria afanyaje, lilikua ni swali la biashara, na alijua fika Frank ni mtaaramu wa biashara, lakini akakausha.
Akaendelea na swali lililofuta ambalo nalo
lilimshinda. Sasa akaanza kuruka maswali na kutafuta yale marahisi tu, lakini kwa bahati mbaya maswali karibia yote yalimshinda. Akafunika daftari, hata hamu na nguvu za kusoma ziliisha, alichoka. baadae akakumbuka kitu, akashika simu yake na kumpigia Happy, simu ikaita na kupokelewa;
LOVE: Hallow Happy...
HAPPY: We upo wapi? mbona huonekani tangu asubuhi?
Sasa Love akafikiria akaona akisema yupo darasani, Happy atataka kumfuata huko huko darasani. Na akimfuata akamkuta Frank itakua sio.

WHATSAPP 0768315707

SEHEMU YA 77


HAPPY: Sawa! kwani ulikua unasemaje?
LOVE: Kuna vimaswali hapa vya biashara vinanisumbua, sasa nilitaka unisaidie...
HAPPY: Mmh! viswali gani, ebu visome kwanza nivisikie.
LOVE: Yapo mengi lakini naomba unisaidie haya mawili.
HAPPY: Yaseme sasa.
LOVE: La kwanza, je ni zipi njia za kufanya ili kukuza mauzo katika biashara yangu?. Alafu la pili, nifanye nini baada ya biashara yangu kufeli?
(Happy baada ya kusikia maswali, akafikiria akaona ni magumu, tena kaulizwa ghafla)
HAPPY: Shoga maswali yamenishinda hayo. Vipi umejaribu kuyatafuta mtandaoni?
LOVE: Yani nimecheki kila sehemu, mtandaoni kote, sijapata majibu.
HAPPY: Mmh kwakweli nisije kudanganya, siyajui.
LOVE: Basi sawa.
HAPPY: Sawa, lakini hujaniambia upo wapi!
LOVE: Usijal nitakuambia badae
(Simu ikakatwa, Love akageuka kumcheki Frank akamuona yupo bize na masomo, akaguna, akajua leo kazi ipo)
Sasa Frank nae sio kwamba alikua bize, hata!. Alikua makini kusikiliza jinsi Love alivyokua anaangaika kumuuliza Happy maswali ambayo yeye aliyaona kama maji tu. Alijiuliza kwanini Love anapata shida?. İli kumchanganya Love, akajikoholesha kidogo, koh koh koh! Love akageuka tena kumtazama Frank, akamkuta yuko bize, hana m pango.
Love akafikiria, akaona mule ndani kama hasomi si bora aondoke. Lakini akawaza ni muda mfupi tu amekuja, alafu hakuna alichosoma cha maana, sasa akitoka si Frank atamshangaa, atamuona kama hayuko siriazi na masomo, binti wa watu akaona bora akaushe.
Frank nae alifikiria kumwambia Love kwamba hayo maswali yanayomsumbua anayafahamu. Lakini kutokana na kaugomvi kao akaona bora tu anyamaze, akajisemea;
"Mwenye shida na amfwate mganga" alafu akaendelea kusoma.
Love kila akigeuka kumuangalia Frank alimuona yuko bize kusoma;
"Huyu nae hata aniangalii, yani yeye na daftari to, aah!" alijisemea Love.
Uzalendo ulimshinda, akaona la kuwa na liwe, kama kukaushiana wamekaushiana sana na imetosha sasa. Ukizingatia hakuna la maana analolifanya mule ndani, akaita;
LOVE: Frank...
(Nae Frank ni kama alikua akisubiri muito huo, aliisikia vizuri sauti nzuri ya Love. Akageuka na kuitika)
FRANK: Naam!
LOVE: Kuna swali naomba uje unisaidie.
Frank akafikiria, atoke pale amfwate mpizani, wakati hayo yote kataka mwenyewe, akaona ili kudhiirisha umuhimu wake, ni Love kumfuata yeye. FRANK: Ebu njoo nayo hapa nikuelekeze.
Love akaona hakuna haja ya kubisha. Akachukua daftari na begi lake akaama makao.
Sasa wakawa wamekaa pamoja, Love akatoa maswali, akamuonyesha yale maswali mawili ambayo ndio yanamsumbua sana. Frank bila kuchelewa akaanza kushusha vitu vilivyomchanganya binti wa watu;
FRANK: Tukianza na hilo la kwanza, njia za kukuza mauzo katika biashara yako. Hapa ni kama mtu ambaye kwa mara ya kwanza anaingia chuo akaanza kwa küfeli mitihani, ambapo badae akaongeza juhudi akafaulu. Kwenye biashara kuna vitu inabidi uvifanye ili mauzo yako ya leo yawe tofauti na mauzo ya kesho, au mauzo ya kesho yawe tofauti na keshokutwa. Njia hizo ni kama;
1. Kuwa karibu na wateja wako. Zungumza nao kuhusu biashara yako. Waulize wanavyoiona biashara yako, wapeleleze wan ata ka nini ili uboreshe bidhaa zako na kufanya kama wanavyohitaji.
2. Toa huduma bora kwa wateja. Hapa ndipo pale wanaposema mteja ni mfalme. Ongea nae vizuri, hakikisha ukimuhudumia lazma atarudi tena na atawaambia wateja wengine.
3. Tangaza biashara yako hasa kupitia soko la mitandao. Wateja wengi wanapatikana mitandaoni. Huko ndiko utakakoongeza wateja ambao watakuja kukuza mauzo yako.
4. Fahamu ni vitu gani vinawashawishi wateja kununua. Wateja wanavutiwa sana na vitu vinavyonunuliwa sana na wateja wengine. Lakini wateja wengine wanapenda vitu vipya ili wao wawe wa kwanza kuvitumia. Kwahiyo inabidi uendane na muda na mahitaji ya kila mteja.
5. Fikiria mauzo ya juu (assume sales). Hapa jitengenezee mipaka ya mauzo yako, mfano kama leo unauza 100 hakikisha tokea moyoni mwako unapanga kesho lazma uuze 200.
6. Zipo njia nyingi ikiwemo, kufanya promotions ambazo zitakuletea wateja wengi na mauzo mengi, kuwaamini wateja wako, na kuendeleza umuhimu wa ushindani. Kumbuka ushindani utakufanya utake kuonekana kuwa juu, na hapo ndipo utakapokuza mauzo yako.
FRANK: Vipi upo hapo?
LOVE: Nipoo! mh Frank?
FRANK: Naam!
LOVE: Haya mambo yote unayajuliaga wapi?
FRANK: Mitandaoni (akicheka)
LOVE: Muongo, mi mbona nimetafuta nimekosa.
FRANK: Hujui kutafuta.
LOVE: Mmh! haya bhana. Yani sijawai kuelewa kama leo.
FRANK: Sawa! vipi tuingie swali la pili?
LOVE: Ndio, tuingie la pili.
Sasa wakati wanataka kuanza swali la pili, Love baada ya kutupia macho dirishani akawaona Happy na Maria, ni kama walikua wanakuja darasa hilo.
LOVE: We ndo umewaambia wale waje hapa?
FRANK: Hapana, kwanza hawajui kama niko hapa.
LOVE: Sasa mbona kama wanakuja kwenye hili darasa?
FRANK: Mh! subiri tuone.
Love kwa wasiwasi akaenda kufunga mlango wa darasa, asije akakutwa. Alafu akaenda dirishani kuwachungulia Maria na Happy, kwa bahati nzuri hawakua wanaenda kwenye darasa hilo, Love akashusha pumzi.
LOVE: Duuh nilishaanza kuogopa.
FRANK: Pole, mi naona humu ndani kumeshakuwa kuchungu. Tuondoke, nitakuelekeza siku nyingine.
LOVE: Hapana, mi nataka leo! Na utanielekeza maswali yote nisiyoyajua...
(Love aliongea akiwa anamaanisha)

WHATSAPP 0768315707

SEHEMU YA 78

LOVE: Duuh nilishaanza kuogopa.
FRANK: Pole, mi naona humu ndani kumeshakuwa kuchungu. Tuondoke, nitakuelekeza siku nyingine.
LOVE: Hapana, mi nataka leo! Na utanielekeza maswali yote nisiyoyajua...
(Love aliongea akiwa anamaanisha)
Frank akashangaa, Loveness wa wa muda huo hakuwa yule wa jana.
FRANK: Hapana, mazingira hayaruhusu, niruhusu niondoke.
LOVE: Hayaruhusu kivipi we mbona mwoga hivyo?
FRANK: Sio woga , tuliposoma panatosha, nishachoka.
LOVE: Basi nakuomba tufanye swali moja tu la mwisho.
Frank akafikiria akaona kama swali moja fresh, ila zaidi ya hapo haiwezekani. Wakarudi na kukaa tena kwenye dawati.
FRANK: Eeh! swali lipi unataka nikuelekeze?
LOVE: Lile la "Nini cha kufanya ikitokea biashara yako inafeli?"
FRANK: Kwani wewe ukifeli mtihani wa kwanza uwa unafanya nini?
LOVE: Najisomea zaidi.
FRANK: Kwahiyo unataka kusema wanaofeli wote huwa hawasomi zaidi?
LOVE: Mmh! hapana, wengine uwa wanasoma sana lakini wanafeli.
FRANK: Sasa kwanini wanafeli wakati uwa wanasoma sana?
LOVE: Ushaanza maswali yako. Yani wewe una maswali mengil!
FRANK: Nijibu basi.
LOVE: Jamani kufahulu inategemea. Wengine wanabahatisha, wengine walichosoma ukikuta hicho hicho, na wengine wanakuwa na uelewa wa mambo mengi.
FRANK: Hivi unajua kwanini mtu anakua anaelewa mambo mengi?
LOVE: Ni kwasababu anapenda kusoma au kujifunza mara kwa mara.
FRANK: Safi. Na hicho ndicho kinachotokea katika biashara nyingi za watu, duniani. Watu wanaofanikiwa katika biashara sio kwamba wao pekee ndo wanafaa kuwa wafanyabiashara. wengine wanabahatisha (wana bahati na biashara), wengine wanajua kuchagua bidhaa zinazopendwa na wateja, na wengine kila siku wanajifunza kuhusu biashara, wanajua mambo mengi kuhusu biashara, wana uelewa kuhusu biashara, ndio maana wanafanikiwa. Upo hapo?
LOVE: Nipoo!
FRANK: Nataka nikuambie jambo moja, ni muhimu ukazijua mbinu za kufanikiwa katika biashara, na ni muhimu pia ukajua sababu za mtu kufeli kibiashara. Vitu hivyo nitakuelekeza siku nikipata muda, lakini kwa sasa nataka nikujibu swali lako. Kwanza nikuulize; je wewe unafaha na unatamani kuwa mfanyabiashara?
LOVE: Ndio nafaha, na natamani sana kuwa mfanyabiashara.
(Baada ya Love kujibu hivyo, Frank akacheka)
LOVE: Sasa unacheka nini?
FRANK: Nakumbuka kipindi kile ulisemaga hufai na hutaki kuwa mfanyabiashara.
LOVE: Ushaanza (uso ulibadilika, alikasirika)
FRANK: Haya basi pole! hata usinunee (akicheka)
LOVE: We nianzetu (alafu akaangalia pembeni)
FRANK: Kwani vipi, utalazwa tena hospitali? (alitania) LOVE: Alafu Frank mi staki!!
FRANK: Pole! haya tuendelee sasa. Ukishaona au kugundua biashara yako imekufa, imefeli, au imeshindwa kuendelea ni vitu vifuatavyo unatakiwa kuvifanya, sawa Love?
LOVE: Sawa
FRANK: Kwanza; changanua kufeli (analyze failure). Tafuta chanzo kikuu au sababu za wewe kufeli, mfano labda pesa ndo shida, au maamuzi ya biashara huna, au hujui kuwahudumia wateja wako na kuwaongoza n.k. Jiulize, nini mzizi wa wewe kufeli?. Unaweza ukarudi nyuma, ebu angalia historia ya biashara yako alafu jiulize wapi unakosea? Ukishagundua chanzo cha tatizo, utapata pakuanzia. Pili, hakikisha unapata au unajua chanzo cha mapato au fed ha zako zitakazokusaidia katika biashara (get your finance in order). Wengi uwa wanafeli kibiashara kwasababu ya pesa, hawajui kutunza pesa zao. Ukiachilia mbali mikopo, lazma uwe una vyanzo vingine vya haraka vya mapato kutoka katika hifadhi yako ya pesa. Kumbuka kutunza fedha katika biashara ili zikusaidie baadae.
Tatu, fanya kazi na wajasiriamali wengine. (work with other entrepreneurs). Jichanganye na wenzio, kwenye mitandao, kwenye vikao, kwenye semina, alafu jitambulishe kwao kuwa na wewe ni mjasiriamali. Waonyeshe uzoefu wako na uliza kuhusu uzoefu wao, ukifanya hivyo utapata mawazo mapya yatakayokujenga upya. Kutoka kwao jifunze jisi wao wanavyotatua changamoto zao, nawe utapata mwanga. WHATSAPP 0768315707

SEHEMU YA 79


Nne, jipe muda. (take time for yourself).Usikurupuke, amini kuanguka katika biashara ni jambo la kawaida. Ndio maana wanasemaga "business is all about taking risks”. Kazi ya kibiashara inatumia muda mwingi katika kufanya kazi. Ni karibia masaa 60 kila wiki, hivyo ni rahisi kupoteza biashara. Sasa ikitokea umefeli, tumia muda ule ule kujifunza upya na kuangalia makosa., tengeneza fikra zako upya katika kutafuta mawazo mapya.
Tano, anza kufikiria kuhusu mpango mpya wa biashara yako.( start thinking about new business plan). Hapo sasa unganisha mawazo yako mapya, akili mpya, na uanze upya kuitengeneza biashara yako. Ni hivyo tuu!
Baada ya Frank kumaliza kuelezea akamtazama Love, Love nae akamtazama Frank usoni, wakatazamana. Love alishindwa kuvumilia;
LOVE: Frank!
FRANK: Naam!
LOVE: Unajua baba, yani unajua Sanaa.
Siku zikapita, ikaja jumapili. Ilikua mida ya saa tano baada kutoka kanisani, wanachuo wengi walikua vyumbani kwao huko hostel kwao. Lakini baadhi walionekana mitaani, wengine wakiingia na kutoka darasani, ilimradi kukamilisha pilika pilika za pale chuo.
DARASANI:
Frank, Maria na Happy walikutana kupanga namna gani wasome kwa mara ya mwisho kabla ya kuingia kwenye mtihani kesho yake asubuhi.
FRANK: Mimi nashauri kwa sasa kila mtu akajisomee mwenyewe. Alafu baadae tukutane jioni saa 12 ili tunayajadili maswali kwa pamoja hadi mida ya saa nne usiku au vipi?
MARIA: Mh! kwanini tusisome pamoja sahizi?
HAPPY: Ndio. Ni bora sahizi tujadili maswali kwa pamoja alafu baadae kila mtu asome kivyake..
FRANK: Mnajua kwa nini nimesema hivyo?
WENZIE: Kwa nini?
FRANK: Naamini kama kila mtu akisoma mwenyewe sahizi, akipitia na yale maswali, baadae tukikutana pamoja kila mtu atapata cha kuongea na maswali mengi tutayajibu.
MARIA: Ila ni kweli, huwezi kwenda kwenye majadiliano bila hoja.
HAPPY: Mmh! kwahiyo tutakutana baadae?
FRANK: Ndio au bado hujaridhika?
HAPPY: Hapana, kama ni hivyo hakuna shida. wakaagana.
HOSTELI:
Wakati Frank na wenzie wakipanga mipango ya kusoma na kufahulu, upande wa pili vijana wanne walikua kwenye kikao cha maangamizi.
YUMA: Tuhakikishe tunashinda maeneo ya chumba chake muda wote Hi tujue atatoka muda gani na atarudi muda gani.
TARICK: Na tuwe makini. Kuna dawa ya kupuliza na ile ya maji, tufanye tufanyavyo ile ya kupuliza tukaipulize leo ili aanze kuivuta hewa kuanzia leo. YUMA: Sasa si nguvu ya dawa itaisha?
TARICK: Hapana, ndio maana inaitwa dawa ya hewa kwasababu hewa ataivuta mdogo mdogo. Akilala na akiamka asubuhi lazma atakua amelegea kwa uchovu.
ISSA: Sawa na ile ya maji tutamtilia muda gani?
TARICK: İle sasa ni usiku huo huo au asubuhi kabla hajaenda kwenye mtihani.
MESHACK: Naona maelezo tumeyaelewa, hapa tukaanze kuzunguka zunguka maeneo ya chumba chake.
Basi kama walivyopanga. Wakatoka hadi maeneo ya chumba cha Frank. Walikua wanapishana pishana maeneo ya chumba hicho.
Frank yeye alikua ndani kwake akijisomea pekeake. Baada ya kusoma sana, mida ya saa 12 jioni akaona ni bora aondoke kwenda kwenye majadiliano.
Wale jamaa pale nje wakamuona Frank akitoka, wakapeana ishara za kuondoka. Wakaondoka eneo hilo na kuelekea hadi chumba cha issa.
YUMA: Nadhani wote tumemuona akitoka. Sasa kilichobaki ni kumsubiri muda wa kurudi.
TARICK: Kwani jamaa uwa anarudi muda gani ?
ISSA: Yule mida yake ya kurudi saa tatu au nne usiku, na akirudi kitu cha kwanza uwa anaenda kuoga.
WHATSAPP 0768315707
SEHEMU YA 80


YUMA: Basi kuanzia saa mbili tuwe pale nje tukimsubiri.
Loveness akiwa chumbani kwake akakumbuka kesho yake Frank alikua na mtihani. Na kibaya zaidi kuna watu ambao anawajua wanamchezea michezo mibaya . Akajilaumu kwanini amechelewa kumpa taarifa Frank. Haraka katoka kitandani, pasipo kufanya lolote akachukua simu yake, akatoka nje na kufunga mlango. Hata yeye mwenyewe hakujua anaelekea wapi.
Love akatoka hadi nje ya hostel, alafu akasimama akajiuliza.
"Sasa nitampata wapi huyu mtu! Nimefanya makosa, ilibidi nimuambie siku ile ile. Ona sasa ona, sina hata namba yake, sijui anakaa chumba gani, na sijui sahizi yuko wapi" Alijisemea Love huku akipiga piga miguu chini ishara ya kuchanganyikiwa.
"Au niende hostel kwao nikamuulizie uko uko? Lakini hapana Sasa nisipoenda nitampata wapi? Haina jinsi wacha niende"
Bila kupoteza muda akaelekea hostel kwa kina Frank. Alivyofika mlangoni aka kuta baadhi ya wanachuo wengi, akawauliza lakini kila mmoja akajibu hajui chumba anachokaa. Kwa bahati nzuri Love akamuona Godlove, akamuita;
LOVE: Wewee! we mkaka..
(Godlove akageuka na kumuona Love)
GODLOVE: Usiniite wewe, niite God love (aliongea akiwa anatabasam)
LOVE: Samahani, eti Frank anakaa chumba gani? (Godlove akashangaa kidogo lakinl akaona ni jambo la kawaida kwa wanachuo)
GODLOVE: Twende nikupeleke.
(Akampeleka hadl chumba cha Frank lakinl wakakuta mlango umefungwa. Love alikariri namba ya chumba alafu akaagana na Godlove)
Love baada ya kumkosa Frank, akatoka hadi nje, akajiuliza;
"Sasa itakuwa kaenda wapi, mbona hadi naanza kuogopa, au kaenda kusoma kujiandaa na mtihani wa kesho?, ndio itakuwa kweli. Acha niende uko uko nikamtafute"
Akapiga mwendo hadi madarasani, akaanza kuingia kila darasa akimtafuta Frank lakini hakumuona.
***********
DARASANI:
Katika darasa flani hivi, Frank, Maria na Happy walikuwa bize wakijisomea. hakika waliamua kusoma, hawakutaka mchezo.
Na giza lilikua lishaingia. Frank hakujua kwamba huko nje anatafutwa na Loveness tena kwa jambo lenye umuhimu kwake na maisha yake, yeye alikomaa na ya kusoma kwa muda mrefu, akaaga kwenda toilet;
FRANK: Jamani narudi, naenda toilet mara moja. HAPPY: We! isije ikawa ni mpango wako wa kutukimbia!
MARİA: Na kweli.
FRANK: Hapana, narudi sio muda.
MARIA: Sawa, si tunaendelea.
Frank akatoka nje, akaenda hadi toilet ambako hakukaa sana, alitoka. Wakati akiwa njiani kuelekea tena darasani alikowaacha wenzie, akasikia sauti nzuri ya kike ikimuita;
"Frank, Frank! afadhali nimekuonaa"

MWISHO WA SEASON 04, USISAHAU SEASON 05
IMEKAMILIKA

TSH 1000 TU FULL,
INA VIPANDE 20..
TSH 1500 VIPANDE 40..
TSH 2000 TU VIPANDE 60..
TSH 3000 VIPANDE 100

Malipo mpesa 0768315707 jina Prisca, ukishalipia nambie nikutumie chap.
 
SEASON 05

TAMTHILIA: MTU ALIYETHIBITISHWA KWA MAISHA YANGU
CERTIFIED PERSON OF MY LIFE (CPL)
(81-85 )

( SEHEMU YA 81 )

WHATSAPP 0768315707 UKIITAKA YOTE CHAP



Frank akatoka nje, akaenda hadi toilet ambako hakukaa sana, alitoka. Wakati akiwa njiani kuelekea tena darasani alikowaacha wenzie, akasikia sauti nzuri ya kike ikimuita;


"Frank, Frank! afadhali nimekuonaa"


Frank aliisikia sauti ikimuita, akageuka nyuma akamuona Love akija kwa kasi;


FRANK: Vipi kuna shida gani?

LOVE: Kuna kitu nataka nikuambie (huku akihema)
FRANK: Kitu gani mbona unanitisha.

LOVE: Nakuomba kama kuna jambo unafanya acha alafu nifuate.
FRANK: Niache kivipi na nikufuate wapi? LOVE: Usiwe mbishi Frank, nisikilize Mimi! FRANK: Ujue sikuelewi!
LOVE: Utanielewa tu.


FRANK: Acha masihara basi. Mi niko bize nasoma, tutaongea baadae.


(Frank alianza kuondoka jambo lililomfanya Love akimbie na kumshika shati. Frank akageuka kwa hasira, akamuona Love kama anamsumbua vile)


FRANK: Hivi una shida gani wewe Love? (alichukia)


Hata Love akashangaa, hakuamini kama Frank angechukia wakati jambo lenyewe ni


kwa faida yake. Hakutaka kumwambia pale pale akiamini hatoeleweka vizuri. Yeye alitaka wakakae sehemu ndio ampe kisa kizima. Sasa Love kuona Frank anamkaripia nae akapata hasira.


LOVE: Hivi unadhani ningejisumbua kutoka hostel kuja kwako pasipo umuhimu?. Nimekutafuta kila sehemu, nimeenda hostel kwenu haupo, nimekutafuta kila darasa haupo, alafu sahizi nimekupata unashindwa kunisikiliza unanikasilikia, sasa ukikasilika hasara kwa nani?
FRANK: Hasara itakua kwako.






(Love akamshangaa Frank, akamuona kama mtu wa ajabu vile)


LOVE: Hasara kwangu! kwahiyo mimi nitapata hasara gani?
FRANK: sasa kama una jambo la kuniambia na hutaki kuniambia, usiponiambia hasara kwa nani?
LOVE: Yani we unaongea tu, ndio maana wanasema; Jambo usilolijua, sawa na usiku wa giza. Sasa kama Mimi nitapata hasara naondoka, alafu tuone.


SEHEMU YA 82
WHATSAPP 0768315707 UKIITAKA YOTE CHAP


(Love akaondoka kwa hasira).


Frank nae akapotezea. Akapiga mwendo kuelekea darasani, lakini kabla hajaingia akafikiria Sana maneno ya Love. Akaona kama Love alikua akimaanisha vile.


"Lakini mbona kama alikua siriazi, lazma kuna kitu" aliwaza


****** HOSTELI:


Kule hostel tayari mambo yalishakuwa mambo. Issa na wenzie walikua wamevaa mavazi meusi ili wasijulikane. Walikua wakimsubiria Frank arudi ili wakamilishe mipango yao.


ISSA: Oya Tarick itabidi uongoze hili dili kwasababu wewe hufahamiki na maelekezo ya dawa unayo.
MESHACK: Sikilizeni, hapa wabaki wawili, tukikaa wote tutashtukiwa au mnaonaje?
ISSA: Alafu kweli, sasa abaki nani na nani?

YUMA: Meshack na Tarick wabaki. Alafu sisi tunaenda kukaa nje kuangalia usalama.






Wakagawana majukumu, Meshack na Tarick wakabaki ndani alafu Yuma na Issa wakaenda kukaa nje, wakimsubiri muhusika.


*******

DARASANI - NJIANI.

Frank baada ya kuona Love amekasilika, na ukizingatia alionekana kuwa na jambo la maana, akafikiria akaona ni bora amuwahi Love. Basi kabla hata hajaingia darasani, akageuka na kuanza kumkimbilia Kwa bahati nzuri alimuona alikoelekea,


akamfuata na kumkuta njiani;


FRANK: Love, Love..


Love akageuka, uso ukiwa umemuiva kwa hasira. Hakutaka hata kumuangalia Frank usoni.


FRANK: Nisamehe, nimekosa.

LOVE: Hivi unadhani kila kitu ni masihara?. Yani wewe sijui ukoje! Unapenda sana kujikubali wewe kama wewe pasipokujua ni vitu gani vimekuzunguka.


SEHEMU YA 83

WHATSAPP 0768315707 UKIITAKA YOTE CHAP


FRANK: Basi nisamehe!

LOVE: Mi nimechukia sana, yani sikuamini kama ungekua vile, ni bora hata ungejua ninachotaka kukuambia, lakini hujui na unakuwa mbishi.
FRANK: Nimekosa, nisamehe basi!


Ukapita muda wakawa wanatazamana tu. Frank akionyesha sura ya kutubu kosa huku Love akiwa na sura ya "nimekusamehe, lakini unaboa sana".


LOVE: Kuna jambo la muhimu nataka


nikuambie, na tukae sehemu nikuambie.

FRANK: Sawa lakini kuna watu wananisubiri darasani tulikua tukisoma, na nadhani wanapata wasiwasi kwanini nachelewa maana niliwaaga naenda toilet na kurudi.
LOVE: Kwahiyo unatakaje?

FRANK: Naomba nikawaage tu alafu narudi, nikukute hapa hapa.
LOVE: Sawa nakusubiri, fanya haraka.


Ilibidi Frank awahi hadi darasani ambako aliwakuta wenzie wakiendelea kusoma,


moyoni alijawa na shauku ya kutaka kujua Love alikua na jambo gani.


FRANK: Jamani vipi...

MARIA: We mbona umechelewa hivyo, ulikua wapi?
FRANK: Kuna mtu aliniita, nikawa naongea nae.
HAPPY: Nani?

FRANK: Ni rafiki yangu ambaye nae kesho anafanya test. Ameniomba nikamuelekeze kwasababu haelewi chochote na hajui atafanyaje test ya kesho.



SEHEMU YA 84

WHATSAPP 0768315707 UKIITAKA YOTE CHAP

MARIA: Mh! kwani alikua na shida gani hadi hakufanya test ya mwanzo?
FRANK: Anasema alikua akiumwa, na kwa maelezo yake anasema angalau kwa sasa ana nafuu, ila ndo hivyo hajasoma hadi sasa.
MARIA: Oh! jamani pole yake!!!

HAPPY: Huyo mtu ni wa kike au wa kiume (aliuliza kwa wasiwasi)
FRANK: Ni wa kiume.

MARIA: Mh! basi hakuna shida, we nenda hata sie tunamalizia alafu tunaondoka.


Ilibidi Frank awadanganye wenzake ili apewe nafasi ya kuondoka. Lakini Happy bado alikua na wasiwasi sana, alikosa na nguvu za kuendelea kusoma.


********** VIMBWETANI:
Frank baada ya kurudi kwa Love wakatafuta kimbweta kilichojitenga wakakaa na kutulia. Kabla ya kuongea wakatazamana;


FRANK: Nakusikiliza!


LOVE: Mmh! sijui nianzaje. FRANK: Anza vyovyote vile.
LOVE: Sawa. Ni hivi, unakumbuka ile siku umezidiwa darasani na ukalazwa hospitali?
FRANK: Ndio nakumbuka!

LOVE: Hospital walisema unaumwa nini?

FRANK: Hospital walisema nilizimia kwa masaa kadhaa, alafu tumbo ndilo liliniuma sana.
LOVE: We unadhani kwanini ulizimia na kwanini tumbo liliuma ghafla?
FRANK: Si homa tu kama homa zingine.. LOVE: Homa ndo uzimie? alafu hujiulizi


homa gani ya ghafla vile darasani?

FRANK: Love mbona sikuelewi, kwani we unataka kusema ilikua ni nini? kwasababu homa ni sawa na kifo tu, vyenyewe muda wote vinakutokea.
LOVE: Wewe achaga ujinga, ile sio homa ya kawaida.
FRANK: Sasa ilikua ni homa ya nini? LOVE: Uliwekewa dawa yenye sumu. FRANK: Ninii? (alishangaa Frank)
LOVE: Ndio hivyo. Ile ni sumu uliwekewa.

FRANK: Aah! acha masiala basi Love (aliongea akiwa anacheka)


LOVE:(alimshangaa Frank), Yani unanicheka?
FRANK: Sikucheki wewe, nafurahi tu jinsi unavyoniambia mambo nisiyoyaelewa.
LOVE: Sasa kama huyaelewi si ndo uyaelewe?
FRANK: Aah Love nawe! (akacheka tena)

LOVE: Shauri yako. Kama huniamini utajijua mwenyewe. Ila nataka nikuambie, hata leo ukirudi hostel kwako, ukizubaa tu kesho hutoamka salama.
FRANK: Una maana gani?

LOVE: Hao watu waliokufanyia mchezo


mara ya kwanza wanataka wakufanyie tena, na wanakusubiri tu urudi ili wakamilishe mipango yao.
FRANK: We Love mbona sikuelewi?


******* DARASANI:
Kule darasani Happy alipata wasiwasi. Hakuamini kama Frank ameitwa na mwanaume mwenzie. Moyoni aliamini kutokana na Frank kujielewa kiakili asa awapo darasani kunawavutia wasichana wengi, hivyo basi wasichana hao ni lazma watamsumbua Frank awafundishe.



SEHEMU YA 85
WHATSAPP 0768315707 UKIITAKA YOTE CHAP

Mawazo hayo yalimpa uhakika kwamba, hata aliyemuomba Frank yawezekana akawa ni mwanamke mwenzake, akaona hapana;


HAPPY: Maria mi nguvu za kusoma zishaniisha, naomba nikuache.
MARIA: Eeh! jamani na wewe unataka kuniacha?
HAPPY: Nisamehe. Nina usingizi sana leo!

MARIA: Sawa. Kwahiyo si tutaonana kesho muda wa kwenda kwenye test?


HAPPY: Ndio, kesho asubuhi nitakupitia.


Happy akaondoka akimuacha Maria akisoma. Lakini Happy wala hakuwa na usingizi, aliteswa na mapenzi ya Frank. Alikua na wasiwasi sana kuhusu kuibiwa Frank wake. Akawaza ampigie simu... Akapiga, simu ikaita...


******** VIMBWETANI:
Frank akiwa bado na Love, simu yake ikaita. Akaangalia mpigaji alikua ni Happy.


Akawaza apokee au asipokee, akapokea;


HAPPY: Uko wapi Frank?

FRANK: Nipo huku hostel kwangu, vipi? HAPPY: Nataka nije..

(Frank ni kama alishtuka vile. Akawaza na kugundua huo ulikuwa mtego wa kipelelezi)


FRANK: Sawa njoo, lakini nipo na yule mtu namuelekeza maswali.


Happy baada ya kusikia hivyo akaona kumbe hakuna jambo lolote baya, akaamini ni kweli Frank aliombwa kumfundisha mtu, tena mtu wa kiume. Akapata amani ya moyo.


HAPPY: Kumbe, basi nilikua tu nakutania tu. Usiku mwema! kesho wahi kuamka twende kwenye mtihani.
FRANK: sawa.


Baada ya simu kukatwa, Frank akamtazama Loveness ambaye alimsikia Frank akidanganya lakini hakutaka


kumuuliza kuhusu udanganyifu huo.


LOVE: Frrank hivi umenielewa nilichokuambia ?
FRANK: Ah! mi siamini vitu kama hivyo!


Love macho yakamtoka, akabaki kushangaa!


ITAENDELEA

WHATSAPP 0768315707 UKIITAKA YOTE CHAP
 
SEASON 05

TAMTHILIA: MTU ALIYETHIBITISHWA KWA MAISHA YANGU
CERTIFIED PERSON OF MY LIFE (CPL)
(86-90)

( SEHEMU YA 86 )



LOVE: Frrank hivi umenielewa nilichokuambia ?
FRANK: Ah! mi siamini vitu kama hivyo!


Love macho yakamtoka, akabaki kushangaa!


Akajiuliza;


"Hivi huyu mtu wa namna gani, mbona nilizani ana uelewa mkubwa kumbe ndo yuko hivi! Ina maana haniamini kabisa? sasa nimuache au nifanyeje ili aamini? " aliwaza Love


LOVE: Frank nina utani na wewe? FRANK: Hapana.
LOVE: Sasa kwanini hunielewi?

FRANK: Kukuelewa nini Love?, tatizo unaongea mambo ambayo hayapo. Kama nililazwa hospitalI, ile ni homa kama homa


zingine. Hata ungekua wewe ungeamini nini kwa kitu usichowai kukiona?
LOVE: Kwahiyo shida yako ni kuona? FRANK: Sasa nitaamini vipi?
LOVE: Sawa! Lakini nimekufikishia ujumbe kwamba leo ukirudi hosteli kwako kuwa makini. Tena ikiwezekana usirudi kabisa. Tafuta rafiki yako yeyote ukalale hadi mtihani wa kesho upite. Kuna watu wana nia mbaya na wewe. Kuna watu hawakupendi Frank. Kuna watu wanataka kukuharibia, wanafanya kila njama pasipo wewe kujua. Ndio maana nakuambia, wewe kuzidiwa ghafla, kuumwa tumbo na


kuzimia haikuwa homa ya kawaida. Uliwekewa dawa yenye sumu kwenye maji. Na mipango yao ni kwamba hata mtihani wa kesho usifanye ili ufeli moja kwa moja uondolewe chuo. Mbaya zaidi wanaokufanyia michezo hiyo wapo wengi, sio mmoja, na unasoma nao darasa moja. Kuwa makini usije kuishia pabaya, usijisahau. Ugomvi wangu Mimi na wewe ulitaka kunizuia nisikuambie ili jambo, lakini baadae nikagundua wewe ni mtu safi sana, nafsi yangu ikanisuta, nimeamua kuja kukuambia. Frank nakuomba, usiende kule hostel, nakuomba Frank (aliongea Love kwa hisia kali hata Frank mwenyewe


alishangaa)


Frank aliona kama ni mambo ya ajabu. Ilikua ngumu kuamini jambo asilowahi kuliona. Akajiuliza;


"Watu wananifanyia njama Mimi, kisa nini? " Hakupata jibu lakini uso wake ni kama ulibadilika, ni kama ulianza kumuamini Love.


FRANK: Sasa Love, mi hata sielewi nifanyeje, na ni akina nani hao?

kupata full story nichek whatsapp 0768315707


SEHEMU YA 87



Lakini Love hakutaka kuwataja akina Issa, aliona bora awastahi kwanza, kwasababu akiwataja mapema kutatokea ugomvi mkubwa sana.


FRANK: Eti Love ni hakina nani?

LOVE: Sikuwafahamu japo naamini wanatoka darasa letu. Ilikua ni usiku, nilipita maeneo ya pale hostel kwenu, kwa bahati nzuri nikaanza kusikia wakikuzungumzia. Nilijibana sehemu ili nisikilize. Wakasema watahakikisha unafeli chuo, unafukuzwa chuo na ikiwezekana


haufanyi mitihani yako.

FRANK: Kwahiyo nifanye nini sasa?

LOVE: Hakikisha leo usilale chumbani kwako, tafuta sehemu ya kulala!
FRANK: Lakini kila kitu changu nimeacha kule. Vitambulisho, peni, rula, hata nguo za kubadili, itakuaje sasa?
LOVE: Sikiliza, sahizi ni saa mbili, mipango yao ni kwamba wewe unarudi saa nne kama kawaida yako. Inawezekana sahizi bado hawajafika wanasubiri saa nne, kwahiyo tumia huu muda nenda kachukue vitu muhimu vyote alafu urudi mi nakusubiri, sawa?


FRANK: Sawa! (akaanza kuondoka)

LOVE: Ebu subiri, nipe namba yako alafu chukua yangu. Ukirudi nitaarifu


(wakabadilishana namba)


LOVE: Alafu hakikisha usinywe wala kula kitu chochote kilichopo chumbani kwako..
FRANK: Sawa.


Frank akaondoka akiwa na mawazo ambayo hata yeye mwenyewe hakuyaelewa. Kuna muda aliona kama mambo ya


masihara, lakini akifikiria hana utani na Love akaamini.


Akiwa njiani akahisi kiu ya maji. Akakumbuka aliambiwa na Love kuwa asitumie kinywaji chochote kilichopo hostel kwake, akaona bora apitie dukani kabisa .


DUKANI:

FRANK: Aisee una maji kopo kubwa?

MUUZAJI: Samahani sana maji nimeishiwa!!
FRANK: Dah! mbona tabu. Hiyo juisi bei


gani?

MUUZAJI: Kuna kopo la 2500 na 2000....Nikupe lipi kaka?
FRANK: Nipe hilo la 2000.

kupata full story nichek whatsapp 0768315707

SEHEMU YA 88

Akapewa juisi ya 2000 ambayo akaifungua na kuanza kunywa kuzimua koo huku akielekea hostel kwake.


****** HOSTELI:
Wakati Love na Frank wakiamini wahuni bado hawajafika eneo la kazi, eti


wakisubiria saa nne kumbe upande wa pili walikua wameshajipanga tangia saa 12 jioni. Walikua wakimsubiri Frank arudi ili wamalize kazi yao.


Na punde si punde wale walioko nje ya hostel (Yuma na Issa) wakamuona Frank akirudi, mkononi akiwa na juisi ambayo alikunywa nusu tu. Basi bila kuchelewa, Yuma akasogea pembeni haraka alafu akapiga simu.


YUMA: Oya Tarick... TARICK: Vipi baba!


YUMA: Mpo wapi?

TARICK: Sisi tupo hapa eneo la kazi!

YUMA: Sasa jamaa anakuja, amebeba juisi mkononi, naona kama ameturahisishia kazi, hakikisheni hiyo juisi na vimiminika vingine mtakavovikuta ndani tieni dawa!
TARICK: Limekwisha hilo (na simu ikakatwa haraka).


Ni kweli, Tarick na Meshack wakiwa wamejificha sehemu wakamuona Frank akija kisha akafungua mlango wa chumba chake na kuingia ndani. Wao walikuwa makini kusubiri atoke ili waingie.






Frank baada ya kuingia ndani akaweka juisi yake mezani alafu akasimama kwa muda akiwaza kwamba hakuona mtu yeyote pale nje, akajiuliza;


"Hivi huyu Love au ananidanganya, ananipima imani? Mbona hostel iko kimya, hakuna watu. Watu wako madarasani wanajisomea"


Kuna muda aliwaza kupuuzia maagizo ya Love, lakini akaona fresh tu. Basi akaanza kukusanya vitu muhimu vya kuondoka


navyo. Baada ya kukusanya akaviweka mezani. Hakutaka kuchukua vitu vingi zaidi ya vile vitakavyotumika kwenye mtihani.


Baada ya kukusanya vilivyohitajika akawaza kuondoka. Lakini akakumbuka nguo, akafikiria achukue nguo akabadilishie uko atakakokwenda.


" Lakini kwani nahama hadi nibebe nguo, si bora nioge kabisa alafu nibadili hapa hapa" aliwaza.

kupata full story nichek whatsapp 0768315707

SEHEMU YA 89


Bila kuchelewa akachukua vitu vya kuogea, akatoka na kuelekea bafuni akiacha mlango wa chumba chake kwa kuuegesha pasipo kuufunga na kufuli.


Wazee wa kazi bila kuchelewa wakazama ndani, Meshack akaanza kupulizia ile dawa ya hewa, alafu Tarick akawa anakagua kama kuna kopo lolote la maji. Mara akaliona lile kopo la juisi akatabasam. Tena aliamini juisi ndo nzuri kwasababu akitoka kuoga atakunywa tu.

akafunga na kutikisa alafu akaiweka pale pale alipolikuta. Akakagua tena kwenye kona ya chumba akaliona kopo kubwa la maji, bila kuchelewa akafungua na kutia dawa alafu akalifunga, akalitikisa kisha akaliweka pale pale.


Baada ya kujihakikishia kila kitu kimeenda sawa wakatoka. Na ilibakia kidogo wakutwe na Frank kwasabau ile wanatoka tu hazikupita dakika Frank nae akarudi.


na kuvaa nguo ambazo aliona ataingia nazo kwenye mtihani. Akachukua vitu vyake ikiwemo kitambulisho na peni akaviweka mfukoni. Alafu akaenda konani na kuchukua kopo lake la maji ili atulize kiu maana aliona juisi haitoshi.


Basi akachukua kikombe kidogo kwenye kabati, akamimina maji ili anywe, lakini kabla hajafanya hivyo kwa mbali ni kama aliisikia sauti ya Love ikisema;
"Nilikuambia usinywe kitu kilichopo chumbani kwako" Akaacha kunywa.


Lakini aliona kama anajitesa tu kwasababu Love alisema watu hao wangekuja saa nne, hivyo basi maji yake yapo salama. Aliwaza sana anywe au asinywe? akaamua kuacha, akachukua juisi yake pale mezani kisha akatoka na kufunga mlango.


******

Meshack na Yuma baada ya kumaliza kazi wakatoka nje na kuwapa taarifa Yuma na Issa kwamba kazi imeisha. Basi wakaamua kuondoka eneo hilo.


YUMA: Mna uhakika mmefanya kweli?

TARICK: We subiri matokeo, kesho asubuhi na mapema utasikia mtu anakimbizwa muhimbili.


(wakacheka)

MESHACK: Lile kopo la dawa ya hewa nimelimaliza lote, yani nimepulizia hadi uvunguni mwa kitanda, hiyo yote ni kuhakikisha kesho mtihani haufanyiki.

ISSA: Lile kopo la juisi mmelifanyia kazi?

TARICK: Unauliza jibu, yani lile kopo kwa sasa haliitwi kopo la juisi, bali kopo la kulazwa hospitali...Bila kusahau nilikuta na kopo kubwa la maji nalo nikaweka vituu..
YUMA: Basi kaisha huyoo!

ISSA: Kuna ule wimbo unaimbwa "kifo kifooo, kifo hakina hurumaaa"....


(Walicheka sanaa, walifurahia kazi yao)

ISSA: Oya leo mkilewa nawaacha uko uko baa.
MESHACK: Acha hizooo, alafu hata wewe unakua kama mrembo, yani mwanaume kamili hunywi bia? Issa leo twende ukajaribu bia hata moja.
ISSA: Wee! nisije kuzimia bure..


(wakaondoka na kuelekea baa iliyopo karibu na chuo)


*******

Frank akiwa na juisi yake mkononi, alienda hadi eneo alilomuacha Love lakini hakumkuta. Aliangaza macho huku na kule lakini hakumuona. Akafikiria aende wapi sasa, lakini akakumbuka walipeana namba, akatoa simu yake na kumpigia;


FRANK: Hallo Love? LOVE: Eeh! vipi upo wapi?
FRANK: Nipo hapa nilipokuacha.

LOVE: Aah! sawa, nisubiri nakuja muda huu.


Zilipita kama dakika tano hadi Love alipotokea, alimkuta Frank kasimama tu akimsubiri.


LOVE: Vipi umenisubiri sana? FRANK: Sio sana!
LOVE: Umechukua kila kitu muhimu? FRANK: Ndio nimechukua.
LOVE: Alafu mbona umechelewa sana, ulikua unafanya nini?
FRANK: Niliamua kuoga kabisa! LOVE: Na hiyo juisi vipi?
FRANK: Hii nilinunua muda ule nakwenda


hosteli.

LOVE: Ina maana ulienda nayo hadi hostel kwako?
FRANK: Ndio.

LOVE: Muda ulivyoenda kuoga juisi uliiweka wapi?
FRANK: Niliiacha mezani.

LOVE: Ulivyoenda kuoga mlango uliufunga? FRANK: Niliuegesha tu.
LOVE: Na baada ya kutoka kuoga hii juisi umeikunywa tena?
FRANK: Hapana, vipi na wewe unaitaka? basi ebu ninywe kidogo alafu nikuachie..






(Frank aliongea huku akitaka kuipeleka ile juisi mdomoni) kupata full story nichek whatsapp 0768315707


SEHEMU YA 90


***** BAR:
Upande wa pili wanaume walikua wameshaanza kulewa. Bia zilipangwa mezani, ilikua ni kuchukua na kunywa tu.
Lakini Issa yeye alikua akinywa soda kama kawaida yake, jambo hilo halikuwapendeza wenzie ambao walikua wakinywa bia. Walimuona Issa kama


mwanaume muoga. Wao waliamini ili uwe mwanaume kamili ni lazma usiogope kitu.


YUMA: Hivi mnajua kati yetu hapa, Issa mwanetu anatutia aibu?
MESHACK: Sanaa! tena sanaaa!

YUMA: Hivi Issa utabadilika lini? We kila siku na soda, sasa watu wakipita maeneo haya na kutuona si watakuona kama mtoto?
TARICK: Alafu mbaya zaidi yeye ni mwanachuo. Sasa Issa ukirudi nyumbani likizo, watu watajuaje kama umebadilika? hivi hujui kunywa bia kunakufanya uwe na akili ya kiutu uzima? Utajua kutafuta pesa,


kutafuta madem, na mambo mengine, badilika aisee.


Waliongea maneno mengi hata Issa mwenyewe akaanza kujidharau, akajiona kweli ni muoga. Akafikiria akaona kila siku yeye amekuwa mtu wa kubeba wenzie wakilewa, atawabeba hadi lini? lakini moyoni aliogopa sana kunywa bia, hasa akikumbuka vituko wanavyofanyaga rafiki zake wakilewa hadi wanashindwa kutembea, yeye ndo uwa anawasaidia, sasa wote wakilewa nani atatoa msaada?


YUMA: Wewe dada muhudumu, nipatie glass


(Muhudumu akaleta glass)


Yuma akachukua bia akamiminia kwenye glass ikafika nusu akaacha, akaisogeza hadi alipo Issa..


YUMA: Oya Issa leo hatutaki unywe, tunataka uonje tuu, au sio wanangu..
ISSA: Aah! hapana, mi bia hapana... (huku akicheka)


TARICK: Acha utoto basi, we onja kwani tumekuambia unywe?
ISSA: Ah! wazee acheni kuniona kama mtoto. Kama mnaonaje mi naondoka zangu.
MESHACK: Issa acha hizo. We onja kidogo tuu alafu ukionaje unaicha, we onja!


Sasa Issa akafikiria akaona ili kuondoa mzizi wa fitina, akachukua ile glass yenye bia akajikaza akainywa yote alafu kutokana na uchachu akakunja mdomo, sura ikabadilika.


MESHACK: Vipi umeionaje hapo mwanangu?
ISSA: Asee siiwezi hii kitu, hapana!

MESHACK: Ona umeanza kuogopa, acha woga mtoto wa kiume, ebu piga na hii kidogo kuna kitu utahisi mwilini..
ISSA: Kitu gani?

MESHACK: Ndo unywe sasa ujionee!


Issa taratibu akashika tena glass na kuipeleka kinywani....


ITAENDELEA
kupata full story nichek whatsapp 0768315707
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom