Tafadhali Lowassa: Achana na 'active politics'; Bakia mshauri wa Taifa; furahia 80% yako

Warioba na Salim walitulia baada ya kuona kuwa wale wenye makundi na wanaosemekana kupendelewa wametoswa.
Unajua Salim na Warioba washashughulikiwa sana na makundi ndani ya CCM.
Wanaamini kuwa Magufuli atanyoosha mambo hadi kieleweke.
Kuna ambao wangepitishwa wallahi wangelianzisha...hata mkapa na mwinyi washagoma kupiga kampeni..
Tafuta nyuzi za vikao vya wazee kabla ya utezi na updates zake alizokuwa anatoa Msekwa kwny media.

Unaposema Magufuli atanyoosha mambo hadi kieleweke unazungumzia kwa masuala ya ndani ya CCM au ndiyo ahadi anazotoa za kupambana na ufisadi, uzembe na uonevu serikalini?

Kwangu mimi, kama kweli atafanya hayo anayoahidi kwa Taifa (ambayo ndiyo yamekuwa yakipiganiwa na upinzani) basi ana kura yangu. Tatizo kubwa naloliona ahadi hizo ni kama kuipindua CCM yenyewe. Sijui wakubwa wa chama hicho watakuwa tayari kuruhusu mageuzi radical kiasi hicho? Ndio maana wengi wana mashaka kuwa hayo ni maneno ya kutafutia kura tu.
 
Unaposema Magufuli atanyoosha mambo hadi kieleweke unazungumzia kwa masuala ya ndani ya CCM au ndiyo ahadi anazotoa za kupambana na ufisadi, uzembe na uonevu serikalini?

Kwangu mimi, kama kweli atafanya hayo anayoahidi kwa Taifa (ambayo ndiyo yamekuwa yakipiganiwa na upinzani) basi ana kura yangu. Tatizo kubwa naloliona ahadi hizo ni kama kuipindua CCM yenyewe. Sijui wakubwa wa chama hicho watakuwa tayari kuruhusu mageuzi radical kiasi hicho? Ndio maana wengi wana mashaka kuwa hayo ni maneno ya kutafutia kura tu.

Ndizo kauli za hao wazee kuwa wanaamini Magufuli atanyoosha mambo.
Anyway kampeni huwa ni kupeana hopes na ahadi kibao.
Kila mgombea anakuahidi kitu flani utakachokiona cha maana.
Wasikilize, wachambue...kisha kikatio chako kiwahusu
 
Ikulu ya monduri.. au ya hewan??
Ataishia kuisikia ukulu kwenye vyombo vya habari

Kwa kichwa kigumu kilichoshindwa kuzisoma nyakati hili suala la Lowassa kuingia ikulu ni ndoto lakini ni jepesi kinyume cha ugumu wa kichwa chako.
 
Kwa kichwa kigumu kilichoshindwa kuzisoma nyakati hili suala la Lowassa kuingia ikulu ni ndoto lakini ni jepesi kinyume cha ugumu wa kichwa chako.

Na kwa kudhihirisha ni jepesi sasa wapambe wa Lumumba mmekuwa wepesi kujishitukia kuliko kufata mambo yenu na kutuacha sisi na Rais wetu wa wapumbavu na malofa.
 
Ameshasema wamepwaya, mwenye macho haabiwi tazama. Wamepoteza wiki nzima ya kampeni huku uswazi wakatiwenzao wanakata mbuga.

Umemaliza kila kitu! Na kwa sasa waliobaki kumshabikia Lowassa ni opportunistic people ndani ya Chadema. Ndiyo maana kampeni imepwaya!
 
Mzee Mwanakijiji,

Nilishawahi kulinena hili miaka mitatu nyuma nikisema Lowassa akiamua kugombea urais basi atashinda Monduli tu. Kwengineko in Tanzania Lowassa ni sumu na atachangia kwa kiwango kikubwa chama chake kushindwa katika uchaguzi. Nilishauri aachane na ulingo wa siasa ajikalie kama mbunge mpaka atakapotosheka nao anaweza kustaafu na kuwa mshauri. Narudia bado msimamo wangu ule ule kuwa active politics particularly urais is a bad move for Lowassa. Richmond haijasahaulika, Madudu ya wizara ya ardhi bado hayajasahaulika, na kwengineko. Kuna msemo mtu ukifanya mazuri ni rahisi watu kusahau but baya halisahauliki ndani ya mioyo ya watu. Nguvu ya pesa katika urais ni kugumu maana sio rahisi kuhonga watu milioni 20 wakupigie kura wewe labda uwe na utajiri kama wa Bill Gates.

Hata hivyo mie ningelifurahi akagombea ili CCM kiwe chama cha upinzani kwani wamejisahau sana na kufanya madudu mengi. Ni wakati muafaka tupate chama cha upinzani tubadilishe kidogo taswira ya nyumba yetu ya Tanzania.

Hii post, mkuu aliipost mwaka 2012, kama yupo jf, atakuwa anajua kuwa kile kilichokuwa kiwakumbe ccm sasa kinaikumba cdm..

Maana wanawagombea 2, mmoja anatoka ccm mwingine anotoka caf..

Sasa hebu fanya hyo hesabu
Ccm+cafu+cdm=??

Hii topc ilianzishwa kitambo lkn ki ukwel, edo ameenda kuuwa upinzani, ambapo kama vile angebaki ccm angeua ccm...

Polen cdm huo mchanganyiko mwisho wa novemba...

Ndyo maana watu wenye akili zao wamekaa pembeni..
Jf ni hazina kubwa mngeitumia (cdm) ingewasaida..

Ila sasa mnamasikia ila hamsikii, mnamacho hamuoni, mnaongozwa na upofu, mkistuka mpo shimoni..
 
hapo mwanzo nlikuwa nkiona watu wanajiita great thinkers but what they post and discuss vilikuwa agaist what they claim to be,,but now nmegundua kuwa kuna great thinkers kweli,na kuna kenge ambao wengi wamejoin recently,,but cio wote waliojoin recent ni kenge na wafata mkumbo,,ila wengi waoo!!!!uzi haukuwa na biaz m2 ameeleza fact then great thinkers wanachambua bila hamasa!!!god bless tanzania na kila aitakiaye heri nchi yetu.
 
Ufunguzi umeisha sema.

Pasco

Mods poleni na kazi acha watanzania wajiulize na kujadili.

Nadeclare interest kwamba mimi ni Team #hapakazitu


Tukiingia kwenye mada napenda kwa ufupi tu niseme yafuatayo kwa mustakabali wa Taifa.

Napenda nifanye tathmini hii kwa kujaribu kugusa watu waliozungumza na hoja zao na mandhari walizozileta na ikiwezekana reaction ya wasikilizija au audience.

Pia tathmini hii itajikita kwenye saikolojia ya ushindani kwenye siasa au jambo lingine lolote linalohitaji ushindani.

Nitaanza na maandalizi ya tukio lenyewe.

Hapa niseme wazi bao la mkono lilitumika kuwavuruga UKAWA,baada ya kutishiwa kuwa watanyimwa kuhutubia kwenye viwanja vya jangawani.Lakini hata hivyo baada ya swala hili kutatuliwa Ukawa waliadapt na kujipanga upya na hatimaye kufanikiwa kuandaa kwa weledi mkubwa despite challanges walizopata.Hapa namaanisha kimiundo mbinu na kimatangazo ili watu wawepo.ni kweli watu walifika wa kutosha.

Pili ni suala la burudani.Hapa pia Ukawa walifanikiwa kwa kuweza kucontrol idadi ya wasanii waliotumbuiza.wasanii hawakuuteka mkutano.lakini pia msanii wa 'singeli'au mchiriku aliweza kuleta hamasa na kuicharge crowd iliyopo kabla mgombea hajawasili au hotuba kuanza.huyo bwana anayeenda kwa jina la 'msaga sumu' kama sikosei yuko vizuri namfananisha na wale wa ccm walioimba lile singeli la 'Tinga Tinga liko uwanjani' siku ya kampeni ya ccm.

Tatu ni MC John Mrema ambaye amaweza saba kudhibiti jukwaa,crowd na muda.Huyu amewakilisha vyema Chadema asilia.ameweza kulipamba tukio na kulilinganisha na lile la ccm.Amempiku kibonde siku ile lowassa alipoanza safari ya matumaini.

Nne nimsifu msanii wa singeli au mchiriku au bongo fleva anayeenda kwa jina la msaga sumu nikikosea nisameheni.

Tano ni protokali.
Hapa kulikuwa na mikanganyiko kadhaa..uhudhuriaji wa wageni haukuwa na mpango.waliokaa meza kuu hawakujulikana na wala hakukuwa na utambulisho.Tususahau kulikuwa na makamu wa rais wa zanzibar lakini alichukuliwa kama msanii flani.

Sita utambulisho na hotuba ya naibu katibu mkuu wa chadema zanzibar.Ni kama vile alikuwa hajaandaliwa kuja kusema kitu.Ni kama vile hakubaliani na tukio linaloendelea ingawa mwishoni kabisa alikuwa charged na kuanza kutoa maelekezo.

Mnyika alikuwepo lakini hakuichukua nafasi kwa niaba ya Dr Slaa.hii inadhihirisha kizungumkuti kilichopo Chadema.

Saba ni utambulisho wa Mbowe na hotuba yake.

Mbowe hakuwa kwenye mood kabisa.Mbowe hakujua afanye nini kama Mwenyekiti.Mbowe

Hakujipanga kuclear doubts za kwa nini Chadema na pengine UKAWA walichukua uamuzi waliochukua.Mbowe hakuongea na wanachadema waliogawanyika ili warudi pamoja na kuingia kwenye kampeni kama wamoja na kuwaeleza kwamba maamuzi yake ni sahihi na sio ya kununuliwa.Mbowe hakuinadi ilani ya chadema kama ilivyotegemewa(moyoni akijua mgombea wake ni dhaifu katika hilo)
Mbowe alitarajiwa kuonesha kuwa bado chadema ni salama na Changamoto za kujitokeza kwa wagombea wawili wa Ukawa katika baadhi ya sehemu zimepata ufumbuzi.

Nane ni hotuba ya Mbatia.

Huyu hakuwa na jipya lenye kuunganisha Ukawa.Mbaya zaidi Mbatia amesimika rasmi ule wasiwasi wa watu kuhusu tatizo lilopo ni udini katika kushika hatamu za nchi.Mbatia ameonesha wazi kuwa vita vilivyopi kwenye urais ni kati ya Lutheran na RC.Mbatia ameimbisha nyimbo ya kilutheri au kiprotesrant ambayo lowassa na Sumaye waliimba kwa hisia kali.

Tisa ni Mama Regina...kiukweli huyu mama alikuwa yuko composed na amewakilisha wifw materials ndani ya Tanzania.amejaribu sana kujieleza kwa ufasaha na kujitanabaisha kuwa ni mke mwema na mwenye weledi...hana majivuno na inawezekana ndiye aliyemshawishi EL angie Chadema badala ya ACT kwa kuwa ameonesha alikuwa ni mpenzi wa Chadema.

Kumi ni Halima Mdee na utambulisho wake.

Mdee amejitahidi kubakia kama alivyo.ingawa kuna kitu kinamtatiza.pengine ana wasiwasi mkubwa sana wa kupoteza jimbo la kawe.isitoshe bado anaonekana kuvaa viatu visivyomtosha.ana kitu moyoni!

Kumi na moja ni Julius Mtatiro

Huyu anajiamini kwamba majadiliano ya ukawa yatambeba awe mgombea wa kuungwa mkono na Ukawa despite kwamba kuna mdada wa chadema aliyechukua fomu.

Kumi na mbili ni Sumaye na hotuba yake.
Kama kawaida ameendelea kutoa hotuba isiyoeleweka.Bado JK ataendelea kutomuelewa tu!
Sumaye anaonekana ni mtu aliyetendwa na ccm bila kujua kwanini ccm ilimfanya alichofanyiwa.mi mtu anayeonekana kutafuta ahueni ya maisha kwa kuikosoa ccm.Ni mtu anayeamini yeye ni muhimu na amefanya mengi mazuri ndani ya serikali kiasi cha kustahiki heshima zaidi anayoipata.Ameonesha bado anaipenda ccm na aim yake ni kuifunza ccm a lesson!inaelekea alikuwa anampenda sana Slaa na Chadema ilivyokuwa inapark umma wa watanzania kwa kuibua hoja za uchafuzi!

Lakini amechemsha kwa kutopangilia hoja kwa nini amekuja chadema au Ukawa.Bado Sumaye haamini kwamba Ukawa kuna watu wenye uwezo wa kuendesha serikali na hivyo yeye anaamini ni mtu wa kusaidia Ukawa kuendesha serikali.

Kumi na mbili ni Tambwe hizza.Huyu amajipambanua vizuri katika propaganda.
Amejaribu kujirudisha kwenye chati na alijipanga kwa yale aliyotaka kuyasema.kwa mbali ana uchungu kwa ccm kukipotezea kitengo chake cha propaganda.

Kumi na tatu ni Maalim Seif.
Itoshe kusema ameonesha ukongwe wake katika siasa na majukwaa.alijali muda na kueleza na kutenda kwa nini hataki kupoteza muda.

Kumi na nne ni babu Haji Duni.
Huyu ni mwerevu lakini anaathiriwa na utani na mzaha mwingi.Bado yuko kwenye kujitafakari kwa nini yeye ni mgombea mwenza.Bado anakumbuka na kuheshimu kwa nini kuna muungano huu wa Ukawa..ndio maana hata kama hakuwa na ilani basi aliweza kukumbuka suala la Katiba na kulisema hili litakuwa ni kipaumbele.Bado ni mwana Cuf mtiifu ingawa anajitahidi kulificha hili.

Kumi na nne ni lowassa.

huyu hajabadilika pengine kwa kukosa uwezi wa kufanya hivyo.Bado anaonekana ni mtu mwenye kupambana na afya yake.amejaribu saba kuimprove katika kuonesha physical strenth lakini hajafanya hivyo kiakili.
Ameonesha wazi kuwa bado hajarudi kwenye mental state aliyokuwanayo.

Amepotea sana katika kuuteka umma na kujieleza.anaharibu sana kuficha kilema alichonacho kwa sasa.

Ameshindwa kuwapa watu kile kilichotarajiwa pengine ni kutokana na afya aliyonayo.

Ameshindwa kutoa kipya au hata kile alichokifikia pale Shekh Amri Abeid.

kwa ufupi amewaangusha watanzania na wafuasi wake na ameshindwa kutumia the final opportunity aliyoipata.


Jiulize kwa nini Lissu,Safari,Marando,Jussa,lema,Sugu,Kafulila,Machali na Msigwa hawakuwepo kwenye Stage.
 
hapo mwanzo nlikuwa nkiona watu wanajiita great thinkers but what they post and discuss vilikuwa agaist what they claim to be,,but now nmegundua kuwa kuna great thinkers kweli,na kuna kenge ambao wengi wamejoin recently,,but cio wote waliojoin recent ni kenge na wafata mkumbo,,ila wengi waoo!!!!uzi haukuwa na biaz m2 ameeleza fact then great thinkers wanachambua bila hamasa!!!god bless tanzania na kila aitakiaye heri nchi yetu.

Mkuu gt wako wengi ttzo vifuata mkumbo me binafsi nmejoin Jf mwaka 2009 nlkuta gt wengi sana lkn saizi wanaanza kuadimika na kubaki fuata mkumbo
 
Kwenye hii mada namrudushia Mungu utukufu! Na ninaamini bado unabii utatimia tu. Hata uchelewe vipi! There is a prophecy on our country, a prophecy that WILL be fulfilled. And in that prophecy Lowassa is not in it. It doesn't matter millions bow before him.

Don't be like Sheikh Yahya. (R.I.P). You pray and probaly Lowassa and those millions bowing before him prays too what is the problem and how can you end up concluding that you are right?.

Ni heri yoyote awaye kama anaweza kutuvusha miaka mitano ya kuwa Magogoni hayaweze kutupunguzia chochote zaidi ya kutuimarisha kwenye ushindani wa kisiasa!

 
Back
Top Bottom