KOKUTONA
JF-Expert Member
- Jan 29, 2011
- 8,649
- 6,088
Aisee mimi kama bin Adam hzi tabia kwa kweli zinanikera sana...
1. Kuchungulia mtu anaoga bafuni
2. Kusoma SMS inayoandikwa na mtu asiyekuhusu wala hamjuani
3. Kujitapa kwa vitu usivyokuwa navyo kama vile kujidai umesoma au unamiliki gari wakati siyo
4. Mtu kukataa asili yake au kukana ndugu zake
5. Wapenzi wanaosimulia kwa wengine jinsi walivyofanya ngono na wenzi wao usiku uliopita
6. Mgeni kuwasha TV au kufungua friji bila ya kuruhusiwa na mwenyeji wake
7. Watu wanaoongea mambo yao binafsi ya mahusiano kwenye usafiri wa Umma
8. Watu wanopenda kuvaliana nguo za ndani au kuazimana nguo na viatu
9. Wenzi wanaopiga mayowe wakati wa ku..do ilhali wanajua wanaishi kwenye nyumba isiyo na dari
10, Watu wanaoporomosha matusi hadharani bila ya kujali hadhira iliyopo mchanganyiko wake ukoje.
Kama na wewe una tabia kama hizi tafadhali sana USINIKWAZE!!
5. Inakuwaje mtu mnajifungia chimbani mmeduu for your own interest, pleasure and sectrecy afu mkimaliza ukamtangaze mwenzio?
Hii kweli lazima ikere..ni tabia mbaya saaaaana