Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,230
Aisee mimi kama bin Adam hzi tabia kwa kweli zinanikera sana...
1. Kuchungulia mtu anaoga bafuni
2. Kusoma SMS inayoandikwa na mtu asiyekuhusu wala hamjuani
3. Kujitapa kwa vitu usivyokuwa navyo kama vile kujidai umesoma au unamiliki gari wakati siyo
4. Mtu kukataa asili yake au kukana ndugu zake
5. Wapenzi wanaosimulia kwa wengine jinsi walivyofanya ngono na wenzi wao usiku uliopita
6. Mgeni kuwasha TV au kufungua friji bila ya kuruhusiwa na mwenyeji wake
7. Watu wanaoongea mambo yao binafsi ya mahusiano kwenye usafiri wa Umma
8. Watu wanopenda kuvaliana nguo za ndani au kuazimana nguo na viatu
9. Wenzi wanaopiga mayowe wakati wa ku..do ilhali wanajua wanaishi kwenye nyumba isiyo na dari
10, Watu wanaoporomosha matusi hadharani bila ya kujali hadhira iliyopo mchanganyiko wake ukoje.
Kama na wewe una tabia kama hizi tafadhali sana USINIKWAZE!!
1. Kuchungulia mtu anaoga bafuni
2. Kusoma SMS inayoandikwa na mtu asiyekuhusu wala hamjuani
3. Kujitapa kwa vitu usivyokuwa navyo kama vile kujidai umesoma au unamiliki gari wakati siyo
4. Mtu kukataa asili yake au kukana ndugu zake
5. Wapenzi wanaosimulia kwa wengine jinsi walivyofanya ngono na wenzi wao usiku uliopita
6. Mgeni kuwasha TV au kufungua friji bila ya kuruhusiwa na mwenyeji wake
7. Watu wanaoongea mambo yao binafsi ya mahusiano kwenye usafiri wa Umma
8. Watu wanopenda kuvaliana nguo za ndani au kuazimana nguo na viatu
9. Wenzi wanaopiga mayowe wakati wa ku..do ilhali wanajua wanaishi kwenye nyumba isiyo na dari
10, Watu wanaoporomosha matusi hadharani bila ya kujali hadhira iliyopo mchanganyiko wake ukoje.
Kama na wewe una tabia kama hizi tafadhali sana USINIKWAZE!!
1.Kukojoa halafu ukimaliza unamsalimia mtu kwa mkono.
2. Kuingiza kidole puani halafu unampa mtu mkono.
3. Kutoa makohozi wakati wa kula.
4. Kusimulia movie wakati wenzako wanaitazama mara ya kwanza.
5. kubeep beep kila mara.
6. Kudanganya kwenye simu, niko hapo nakuja kumbe ndio unatoka home.
7. Kukaa siti ya nyuma na kuanza kuweka mikono mbele kwa mtu aliyekaa siti ya mbele.
8. Kuuliza uliza nyakati kila mara, " sasa hivi ni saa ngapi??, sasa hivi ni saa ngapi?? bado dakika ngapi?? "
9. Kutembelea wenzako nyakati za msosi. Ikifika saa sita tu tayari ushafika, halafu stori nyingi, huondoki tu tule.
10. Kukojoa bara barani.
asilimia kubwa ya wabongo tuna hizi tabia zinakera