Tabia hii ya Ufoo Saro wa ITV ni uandishi wa habari au nini!

Status
Not open for further replies.

Jacobus

JF-Expert Member
Mar 29, 2011
4,681
1,698
Jumamosi tarehe 26/01/2013 nikiwa ofisini mida ya saa mbili usiku mie na jamaa zangu tukisubiri kusikiliza taarifa ya habari (StarTv) jamaa yetu mmoja akingia na watu watatu (mwanamke mmoja) wakiwa na laptops na video camera na kuanza kutafuta switchsockets ili kucharge.

Mwanamke akaenda moja kwa moja kwenye tv na kuizima na kuchomeka charger ya kilaptop chake na kutuacha wenyeji tukiduwaa na hatua hiyo.

Kwa kweli ilituuma mno na sikuvumilia, nikamuomba atafute pengine kwani switchsockets zipo nyingi cha ajabu mdada akasema sisi ndo tutafute pahala pengine pa kuangalia/kusikiliza taarifa hiyo ya habari. Sikuvumilia na niliamka kwenda toa charger yake na kuwasha tv. Baadae mmoja wao akaniambia yule mdada ni Ufoo Saro wa ITV, tulishangaa sana kwa tabia hiyo na kujiuliza mbona busara hana au kwa kuwa ni mwandishi wa habari (tena ITV) au katoka Mzizima (Dar) na kutudharau wa mikoani?

Sasa kama mtu ambae hana simile si angemzaba kibao?
 
Labda anadhani yeye ni celebrity na anaamini kuwa celebrity maana yake ni kufanya atakavyo...
Pamoja na hayo lakini kitendo cha kukuta wenzio wanafanya jambo fulani na kuwakatisha bila kuwaomba sidhani u-celebrity unakuwa hivyo! Na yawezekana ndio maana wanapigwa hivihivi.
 
Huo ni ushamba na ulimbukeni wa kutupa!! Wewe unakuta watu hata angekuwa mmoja halafu wewe unaleta mambo yako bila hata kuomba ridhaa? Kama kweli alifanya hivyo atakuwa amejishushia hadhi sana!!!
 
Huo ni ushamba na ulimbukeni wa kutupa!! Wewe unakuta watu hata angekuwa mmoja halafu wewe unaleta mambo yako bila hata kuomba ridhaa? Kama kweli alifanya hivyo atakuwa amejishushia hadhi sana!!!
KAFANYA na kuwa mkali kutetea KITENDO alichokifanya.
 
Jamani mbona hii imekaa ki-private private sana? haya ngoja niishie hapa hapa
Huyu ni mwandishi (reporter) wa habari tena chombo kikubwa na kinachoheshimika ITV, ni sawa na wasanii tu ambao wanajulikana mno hivo matendo yake kama hayaendani na ustaarabu INAKERAAAAAA.
 
Mkuu yawezekana yeye alikuwa sahihi zaidi kwani umetuambia mlikuwa ofisini ambapo kazi ni kipaumbele kuliko hiyo habari na inawezekana alikuwa na kazi ya haraka. Katika mazingira hayo lazima uwe mvumilivu na muelewa usikurupuke kumlaumu. Siamini journalist akaandaa taarifa na hapo hapo azuie wateja kuiona
 
Msameheni huyo dada huenda tu hakusafiri na mumewe, inasemekana wadada wakiwa na kiu tabia huwa zinabadilika, akiwa kwao huyu dada huwa hana tabia zilizosemwa kwenye uzi huu. akikata kiu atarudia tu tabia yake nzuri ya kawaida
 
Jumamosi tarehe 26/01/2013 nikiwa ofisini mida ya saa mbili usiku mie na jamaa zangu tukisubiri kusikiliza taarifa ya habari (StarTv) jamaa yetu mmoja akingia na watu watatu (mwanamke mmoja) wakiwa na laptops na video camera na kuanza kutafuta switchsockets ili kucharge.

Mwanamke akaenda moja kwa moja kwenye tv na kuizima na kuchomeka charger ya kilaptop chake na kutuacha wenyeji tukiduwaa na hatua hiyo.

Kwa kweli ilituuma mno na sikuvumilia, nikamuomba atafute pengine kwani switchsockets zipo nyingi cha ajabu mdada akasema sisi ndo tutafute pahala pengine pa kuangalia/kusikiliza taarifa hiyo ya habari. Sikuvumilia na niliamka kwenda toa charger yake na kuwasha tv. Baadae mmoja wao akaniambia yule mdada ni Ufoo Saro wa ITV, tulishangaa sana kwa tabia hiyo na kujiuliza mbona busara hana au kwa kuwa ni mwandishi wa habari (tena ITV) au katoka Mzizima (Dar) na kutudharau wa mikoani?

Sasa kama mtu ambae hana simile si angemzaba kibao?

Ilikuwa ofisini kwa nani kako au ofisi ya mtu mwingine?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom