USTAADHI
JF-Expert Member
- May 10, 2011
- 1,516
- 136
Kikao cha kamati tendaji cha Bavicha kilicho fanyika tarehe 13 na 14 Nov 2011 chini ya mwenyekiti wake John Heche kiliazimia yafuatayo kama jana ilivyotolewa kwenye press CDM makao makuu.
Baada ya kufanya uchaguzi wa sekretariati yake tarehe 13/11/2011, kamati tendaji ya BAVICHA iliendelea na kikao chake tarehe 14/11/2011 kwa kujadili ajenda kuu mbili ambazo ni hali ya BAVICHA kitaifa na hali ya siasa nchini.Katika ajenda yake ya hali ya siasa nchini, mambo makuu matatu yalijadiliwa kwa kina ambayo ni mchakato wa katiba mpya nchini, hali ya mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu na suala la wamachinga Tanzania.BARAZA LA VIJANA LA CHADEMA (BAVICHA
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
.
Kamati tendaji ya BAVICHA imejadili kwa kina mchakato wa uundwaji wa katiba mpya hususani katika hatua hii ya awali ambayo ni muswada wa mapitio ya katiba hiyo na kuona yafuatayo;Muswada uliosomwa bungeni jana ni batili kwa kua ulipaswa kusomwa kwa mara ya kwanza ili kutoa fursa pana kwa wananchi kuujadili kwani ule wa awali ulikataliwa na hivyo serikali kuamriwa na wananchi kwenda kuandaa muswada mpya na kuingiza pia baadhi ya maoni yaliotolewa.Muswada huo uliosomwa kwa mara ya pili ulikua ni mbovu kupindukia kuliko hata ule wa kwanza kwani baadhi ya mambo hasi yameongezwa na yale kandamizi yaliyokuwamo katika muswada wa kwanza hayakuondolewa.Aidha, kamati tendaji imeona kuwa, kulazimisha kusomwa kwa muswada huo kwa mara ya pili ni ujanja ujanja wa serikali ya CCM na maswahiba wao wa kubaka mchakato na kuzalisha katiba itakayolinda zaidi maslai yao wao na chama chao na siyo matakwa ya wananchi kwa kua wananchi wenyewe hawasikilizwi zaidi ya kuburuzwa katika mchakato huu wa kuandaa katiba mpya.
- Mchakato wa katiba mpya.
Azimio la kamati tendaji ni kupinga mchakato huu kwa kuongoza wananchi kupaza sauti zao za kuupinga muswada kwa nguvu zote ikiwamo maandamano yasio na kikokomo kwa nchi nzima. Baraza linaungana na wanaharakati wote ndani ya nchi wanaolitakia taifa hili mema katika kupinga muswada huo.
2. Mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu.
Kamati tendaji imejadili kwa kina mfumo wa mikopo unao ongozwa na serikali ya CCM unaopigania na kuendeleza juhudi kubwa za kuwanyanyapaa watoto wa masikini. Kitendo cha wanafunzi zaidi ya 12,000 kunyimwa mikopo kwa kigezo kuwa wanafunzi hao hawana vigezo vya kupata mikopo hiyo, jambo hilo ni uhuni kwa kua mpaka sasa bodi ya mikopo haijaweza kuwa na uwezo wa kubaini ni nani masikini wa kweli na ni nani tajiri wa kweli kwani matajiri wamegeuzwa kuwa masikini ilhali watoto hao wa masikini wakigeuzwa kuwa watoto wa matajiri.Pia kamati ilibaini kuwa wale walioonekana kukidhi vigezo vya kupata mikopo hiyo hawapati mikopo hiyo kwa wakati na hivyo kusababisha wanafunzi hao kukosa masomo na wengine hasa wasichana kujitumbukiza katika biashara ya UKAHABA.Mazimio, BAVICHA inalaani vitendo vya serikali kupitia jeshi la polisi kuwapiga wanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es salaam kwa kutumia mabomu na virungu pale walipojaribu kuonyesha msimamo wao na matatizo yanayowakabili kwa njia ya maandamano ya amani. Kamati Tendaji ya BAVICHA inaitaka bodi ya mikopo kuacha ubabaishaji katika kuwapatia wanafunzi mikopo hiyo na pia ieleze ni kwenye biashara gani wanapo wekeza fedha hizi kiasi kwamba zinapohitajika kwa wanafunzi hazipatikani kwa wakati.Rais Kikwete aache usanii na atakeleze ahadi yake kwa vitendo aliyoitoa kwa wanafunzi wa elimu ya juu wa CCM alipokutana nao kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee kuwa hakuna mwanafunzi wa masikini atakayeshindwa kusoma na aangalie kundi hili la wanafunzi zaidi ya 12000 waliokwama kusomaTunaitaka serikali iache kuihusisha Chadema na migogoro ya wanafunzi inayotokea vyuoni kwani ni uzembe wao serikali wakutokujali kwake wanafunzi wa vyuo vikuu. Chadema haina serikali na haitoi mikopo ambayo ndio chanzo cha migogoro hiyo. BAVICHA inamkumbusha Raisi Kikwete kutimiza ahadi yake aliyoitoa katika ukumbi wa Diamond Jubilee mwaka 2006 ya kwamba hakuna mtoto wa masikini ambaye atakaekosa elimu ya juu kwa hoja ya kukosa mkopo.
3. Hali ya wamachinga
BAVICHA inasikitishwa na unyanyasaji wanaofanyiwa wamachinga nchini kwa kukimbizwa na viongozi wa serikali kwenye maeneo yao ya kazi kwa kigezo cha kuweka miji katika hali ya usafi. Usafi wa miji kwa serikali ya CCM ni bora kuliko ubinadamu na ajira za vijana wa watanzania ambao wameamua kujiajiri wao wenyewe.
Aidha BAVICHA inasikitishwa na matumizi ya nguvu zisizo na kifani dhidi ya wamachinga wa jiji la Mbeya.Maazimio ya KamatiTunapinga unyanyasaji wa wafanya biashara wadogo wadogo nchini kote na pia kinalaani kwa nguvu matumizi ya nguvu kwa wamachinga wa jiji la MbeyaBAVICHA inaitaka serikali kuwatengea maeneo maalumu wamachinga ambayo ni rafiki kwa biashara zao.BAVICHA inalitaka jeshi la polisi kuacha mara moja kuwakamata vijana na raia wengine wa Mbeya kwa kigezo kuwa walihusika katika kufanya vurugu ndani ya jiji hilo. Pia, kwa kua jeshi la polisi ndio chanzo cha vurugu za Mbeya ambazo polisi wenyewe walishindwa kupambana na nguvu ya wananchi, BAVICHA inalitaka jeshi la polisi kuwaachia huru raia 300. Tufauti na hapo baraza litachukua hatua nyingine za kuwahamasisha wananchi kudai haki zao za msingi.Wananchi waelewe, tatizo la wamachinga nchini ni uzembe na ubovu wa serikali ya chama cha mapinduzi katika kubuni mipango na mikakati ya kubuni fursa za ajira kwa vijana nchini. Jonh HecheMwenyekiti BAVICHA Taifa