Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,712
Najua wengi mlio na familia mtakua mnapanga namna ya kuifurahia w/end yenu kwa wale mtakaopata muda wa kufanya hivyo.Wacha leo niwaulize swali hili;Hivi itakuaje pale umefika nyumbani akaja mwanao kisha akakuita kwa jina lako kisha akakusalimu bila kutamka baba au mama,mfano AshaDii au Dark City shikamoo,utachukia?Kama ni ndiyo,kwanini uchukie wakati hilo ni JINA LAKO?Si ndo utambulisho wako?Kama unadhani kutokukuheshimu,kwani heshima iko kwenye jina?Kabla hujaanza kuwaza kama akili yangu ina matatizo,hebu jiulize heshima hasa ni kitu gani na kama inahusiana na jina.Hebu leo tuache kufikiri kimazoea angalau kidogo!!Najua unaweza kushangaa sana,lakini huo mshangao wako ni kutokana na kuaminishwa na jamii kuwa heshima iko kwenye vitu au sifa kama vile,mheshimiwa,bosi,mama,baba,dada,kaka n.k.Hebu nipe mtazamo wako na usipate hasira na kutoa povu kisa mwanao leo kakuita jina lako na kukusalimu!!
Last edited by a moderator: