Swali la ugomvi: Mnataka vipi mabadiliko wakati tayari mmebadilika?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,478
39,998
Kingunge-udhamini.jpg


51Z4cxF7CAL._SX450_.jpg

Na. M. M. Mwanakijiji

Mojawapo ya vitu vinanishangaza sana wakati huu wa kampeni na hasa tangu Lowassa apewe kiti cha enzi CHADEMA ni kuwa watu waliompokea na wenye kumuuza mbele ya umma wanadai kuwa wamempokea ili aongoze harakati za mabadiliko. Utawasikia watu wanasema - bila kufikiria sana "tunataka mabadiliko" na kuwa CCM ikitoka tutapata mabadiliko. Wengi wanazungumzia "mabadiliko" kama tukio fulani ambalo litatokea baadaye.

Cha kusikitisha ni kuwa wao wenyewe hawajui au hawataki kujua, hawaamini au hawataki kuamini kuwa tayari mabadiliko yameshatokea; mabadiliko ambayo yamewabadilisha wao. Kama watu wenye akili timamu walishapata mgombea wao wa Urais, wakampitisha na kumthibitisha halafu wiki chache baadaye wakaenda kumchukua mgombea toka CCM na hivyo wakamtupa mgombea wao wenyewe, tena si mtu baki tu Katibu wao Mkuu wa chama, watu hawa hawa wanaweza vipi kuja na kusema ati wanataka "mabadiliko"? Yaani, watu waliobadilika wanataka kubadilika tena? Waweje?

Ukiangalia kwa jicho lililotulia utaona kuwa ni sisi ambao hatujabadilika au kubadilishwa na ujio wa Lowassa ndio hasa tunataka mabadiliko au tunahitaji mabadiliko. Ndio sisi ambao tunatakiwa kubadilika! Ndio maana watu wanatuona tumekuwa wagumu na hatuungi mkono harakati zao (hatujabadilika!). Kumbe kati yetu na wao ni sisi tunaweza kwa haki kabisa kuzungumzia mabadiliko kuliko wao. WAo hawana uhalali (legitimacy) wala hoja (reason) za kusema wanataka mabadiliko. Wanayataka mabadiliko yapi na ya nini?

Ndio maana mwisho wa siku jibu lao ni "kuitoa tu CCM madarakani mengine baadaye". Kumbe wakati huo huo wamechukua CCM, mgombea wa CCM na wanachama wa CCM wenye kumuunga mkono mwana CCM mwenzao ambao waliapa kuwa "alipo" na wao "wapo"!

Wenzetu mnaoimba na kushabikia "mabadiliko" yajayo, hivi hamjioni kuwa tayari mmebadilika? au mtabadilika tena ikitokea mshinde au mkishindwa tena mtabakia hivyo hivyo - naamini wengi watabadilika baada ya kushindwa na kujaribu kurudi mlikokuwa - mkitaka mabadiliko tena! Isije kuwa wenzetu ni watu wa kubadilika badilika tu na ujio wa upepo wa mabadiliko! Si kiongozi mwenyewe wa mabadiliko tayari ameshabadilika? na akija kubadilika tena sijui tutawaitaje.

Vinyonga wa kisiasa?

Fikiria.

MMM
 
Mwanakijiji wewe unasema hujabadilika wenzio wanakuona umebadilika. Siyo yule kamanda waliyekuwa naye wakati huo.

Tatizo ni nini? Tatizo kubwa kwangu mimi ni mtazamo wa mabadiliko. Wakati wewe muda wote uliangalia watu wenzio walingalia mfumo. Kwa mfano wewe unaona Lowassa ambaye alikuwa kiongozi CCM na kwa hiyo na yeye amechangia kutufikisha hapa, hawezi kuleta mabadiliko. Wenzio wanaona CCM kama mfumo ambaye imetufikisha hapa haiwezi kuleta mabadiliko. Hivyo wakati wewe unakataa mtu wa CCM asichukuliwe wenzio wanaamini yeyote atakayesaidia kubomoa mfumo CCM anafaa.

Nachoshangaa mimi ni wewe kuwaona wenzio kama hawafikirii vizuri
 
Mbowe amewaingiza mjini kwa sasa hawana jinsi zaidi ya kufuata mkumbo kama bendera.

Mbaya zaidi eti wanakuja na excuse wakisema wanawatumia tu kina Lowassa kuiondoa CCM madarakani pamoja na kwamba wanafahamu ni mafisadi. Hawafahamu kuwa Lowassa amewabadilisha na sasa wanaimba nyimbo alizozitunga akiwa CCM kabla hajakatwa.

Kwa sasa wale ambao hawajabadilika wanalazimishwa kwa hoja za nguvu ili wabadilike.

Fist priority ya Lowassa kama Rais ni tofauti naya CHADEMA iliyoko kwenye Ilani ya Uchaguzi.

Ndiyo maana ninasema, Lowassa ni mgombea binafsi lakini anaitumia CHADEMA kutimiza matakwa ya kisheria.

Lowassa mabadiliko, Mabadiliko Lowassa. My left foot.
 
Poor analysis. Kwani huyu Katibu mkuu alitoka wapi? Sio CCM? Sasa ana tofauti gani na hawa watanzania wengine waliojiunga na CHADEMA sasa? Lowasa kwa sasa ni mwanachama wa CHADEMA na kadi alipewa mbele ya macho ya watu wote. Ana haki ya kugombea urais kwa mujibu wa katiba ya CHADEMA na ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mabadiliko yanatakiwa ni kuitoa CCM na mfumo wake madarakani. Kama hujakubali hulazimishwi, wengine wamestaafu siasa. Hii ni demokrasia.
 
MM mimi siyo Pro-Lowassa wala Pro-Magufuli,lakini ni MTANZANIA ambaye nimeyakubali Mageuzi ya vyama vingi vya siasa toka 1995,nilipopata uelewa wa nini maana halisi ya vyama vingi vya siasa.

Kwa upande wangu sioni sababu kubwa sana ya kuwalaumu wenyeviti wanaounda UKAWA au waliounda UKAWA kwa sababu kuu moja au mbili.

Hali ya kisiasa hapa kwetu si rafiki kwa vyama vya upinzani.Vyama vya upinzani havina uhuru uliokamili wakunadi sera zao kwa uhuru na haki kama ilivyo kwa chama tawala.

Ugumu huu unakuja tukianzia na NCCR mageuzi ilikufa mara baada tu ya kuchomoza na kuwa chama cha upinzani chenye nguvu miaka hiyo ya tisini,kikawekewa mizengwe mingi sana ya kufananishwa na mauaji ya kimbari ya Rwanda na Burundi,NCCR ikafa kwa kukosa muelekeo.

Ikaja zamu ya CUF hii tukaaminishwa kuwa ni chama cha kigaidi,kimeleta mapanga nk nk na kwamba lengo hasa ni kufanya mauaji kutumia zaidi itikadi za kidini,na CUF nayo ikafananishwa na uislamu ikafa pia kabla hata haijafika miaka saba ya kwenda shule ya msingi.

Leo tunaona namna ambavyo CHADEMA kimepitia magumu mengi sana,ya kupigwa na polisi,kuuawa kwa wanachama wake mfano mzuri ni wale waliouawa Arusha wakati wa mikutano ya kufunga Kampeni..Na hakuan kinachoendelea kwa kumtafuta muhusika mkuu wa shambulio lile ni nani.

Tumeona mwandishi mwenzako Mwangosi akiuawa sababu tu alikuwa mwanamageuzi,sasa najiuliza kwa hili hawa wapinzani tuwasaidiaje???

Kinachotakiwa siyo lazima sana tupate rais toka huko,bali tunachohitaji zaidi sana ni wabunge ambao nadhani hata wewe umeona wakiwa 48 tu waliweza kuliweka njia panda Bunge.

MM tusiwalaumu wameshakosea wamekosea twende mbele zaidi kutafuta nini hatima ya Tanzania kwa sasa ,je bado unadhani Magufuli ataleta Mabadiliko ndani ya CCM???

Nasema kwa sauti kubwa hapana hawezi na hataweza maana hata CCM yenyewe haijui makosa yake,haitafakari kwanini na Maovu yote ya Lowassa lakini bado watanzania waliowengi wana imani naye.Tujiulize CCM kama chama Tawala kinatafakari hili???

Au yote ni yatakwisha kama upepo uvumao baharini???Siwalaumu ila nawahimiza watanzani tunahitaji wabunge wengi sana toka upinzani hatuna jinsi,ni kuwapeleka akina Mnyika wengi Bungeni hilo ndilo la kwanu kubwa.

Kwanu vyama vyote viwili vimetupa wezi wawili tuawapigie kura,Magufuli=Lowassa hawana tofauti.Tofauti yao ni uovu umefanywa katika vipindi tofauti.
 
Mwanakijiji wewe unasema hujabadilika wenzio wanakuona umebadilika. Siyo yule kamanda waliyekuwa naye wakati huo.

Tatizo ni nini? Tatizo kubwa kwangu mimi ni mtazamo wa mabadiliko. Wakati wewe muda wote uliangalia watu wenzio walingalia mfumo. Kwa mfano wewe unaona Lowassa ambaye alikuwa kiongozi CCM na kwa hiyo na yeye amechangia kutufikisha hapa, hawezi kuleta mabadiliko. Wenzio wanaona CCM kama mfumo ambaye imetufikisha hapa haiwezi kuleta mabadiliko. Hivyo wakati wewe unakataa mtu wa CCM asichukuliwe wenzio wanaamini yeyote atakayesaidia kubomoa mfumo CCM anafaa.

Nachoshangaa mimi ni wewe kuwaona wenzio kama hawafikirii vizuri

mfumo wenu ni upi mtakao, tuwekea, na nani atauweka, Mwenyekiti, au EL.....Mfumo kitu gani hii.
 
Huyu Mwanakijiji anaonekana ni mtu wa kupishana na hali halisi siku zote. Hata mwaka 2005 alikuwa kinara hapa wa kumkubali na kumnadi Kikwete na wanao ona mbali walimuambia anakosea na kuwa hakuna jipya lolote litakalo tokea zaidi ya shida. Leo miaka kumi baadae anarudia kosa lile lile.
 
Mzee Mwanakijiji

Nimefuatilia sana hoja zako unazotoa.napenda kukiri kuwa mimi ni miongoni mwa watu waliokuwa wakifuatilia sana tena kwa uzito michango yako ya kina kuhusu siasa za hapa nchini ila nimekuja kugundua kuwa wewe ni mpenzi na mfuasi wa Dr Slaa.wewe kwako mageuzi ni lazima Dr slaa awe mgombea.lakini je lengo la Dr slaa lilikuwa nini.amekuwa akihubiri change of government ili aweze kubadili system ya utawala.kwa kuwa sasa Dr slaa si mgombea tena basi kwako change haina maana tena.kaa chini na utafakari vizuri.
 
Last edited by a moderator:
" Mwanakijiji tuambie tukukute wapi tukupatie nyembe na tukukamulie malimau umeze.."
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom