Swali Jamani Laniumiza Akili

kamanzi

Senior Member
Oct 28, 2007
100
23
Hivi ndugu zangu wanaoshabikia au waliowanachama wa CCM, wanafanya hivyo kwa kigezo kipi? Naamanisha ukitoa wale vigogo mafisadi, hawa wenzangu na mie wanachokipata ni kipi?

Maana kama njaa na ukosefu wa ajira hawa wanachama wa CCM wako mastari wa mbele maana wengi wao hata darasa la 3 hawajafika. Kama ni kutafuta uongozi, kila mtu anajua uongozi CCM ni wa kifamilia nikimaanisha Dr Dr Dr anamuandaa Ridhiwani na mkewe Salma, Makamba anae Januari, Mwinyi anae Husein, Marehemu Kawawa anae Vita, Sitta anae mkewe, Malecela anae mkewe, Marehemu Kighoma Malima anae mwane pia, sasa wewe chokoraa utapita wapi? Maana waliobaki na vimada wa Dr Dr Dr wewe sura unayo?

Ukisema madili, CCM wanafanya kupitia wahindi. Namaanisha Rostam, Manji Patel na wengineo. sasa wewe Andumbwisye dili atakupa nani?

Najiuliza wanaoipigia kura CCM au wanachama kama Kibonde wanamtindio wa ubongo au? Labda wengine hatujui jamani, tujuvyeni tuelewe ninini wanakipata vibaraka wa CCM.
 
Back
Top Bottom