Stevemike
Senior Member
- Mar 12, 2011
- 117
- 15
Katika biashara ya nyama ni kawaida waislamu ndio wamepewa jukumu la kuchinja na bila muislamu kuchinja nyama hiyo ni kama hairuhusiwi kuuzwa. Hili limeleta mtafaruku hivi majuzi kati ya muuza nyama na muislamu mmoja baada ya muuza nyama kuchinja mwenyewe na huyo muislamu akataka hiyo nyama itupwe. Sasa nauliza swala la waislamu kuchinja ni la kisheria au ni ustaarabu tu? Kumbuka siko kidini. Msinielewe vibaya.