Dah! hii kitu inaboa sana aisee, kuna siku nilikuwa ukweni, sasa katika kujifanya kuwaimpress wakwe nikajifanya nimesomea karate, kumbe bamkwe na yeye alipitia hako kakozi lakini ananichora tu. Mara akaniambia nipige side kick aone, mzembe ile kuruka nikafyetuka na suruali ikakwapuka na mbaya zaidi nikateguka shingo. Yule mamkwe ili kunipa moyo nisijiskie nishai akajidai, "Kumbe tukivamiwa na wizi tukupigie simu wewe tu bamkwe wala hatuna haja ya kuwahi polisi".
Ha ha ha aah! Kuna suruali za buku mbili?
Leo asubuhi nawahi zangu kwenye majukumu ya kila siku nimekumbwa na balaa.
Nilipokuwa napanda katika daladala ghafla suruali ikaachia(ikatatuka) kuanzia usawa wa maungio ya miguu mpaka usawa zip inapoanzia. Mbaya zaidi nilikuwa nimechomekea, sikushuka hadi kituo cha mwisho konda aliponiazima sare yake nikavaa kwa muda wakati fundi akinirekebishia hii iliyotatuka
Hata ofisini sikuenda tena.....
Ha ha ha aaah!! Mtundu Kisu sikuweka manjonjo yoyote katika kuvaa nia ajali tu ya kawaida.Una umri gani?Usije kuwa na old skuli afu unatuiga vijana kupiga model!!! Haha zina wenyewe modo ndugu yangu usizivamie zitakuumbua hahah
Pole lakini my brother..