owawajr
Member
- Jul 30, 2009
- 46
- 36
Wapendwa wana JF kuna post iliyoomba CV yangu kwa madai kuwa alikuwa katika utafiti katika wilaya yetu ya Rorya na kuzua baadhi ya maswali na majibu ya ukweli kutoka kwa watu tunaofamhamiana katika harakati,Nashukuru kwa wale walionipigia simu na wale wote waliotoa majibu ya ukweli kwa kile wananchokijua juu yangu,Bado nadhani kuna baadhi ya mambo humu yanahitaji majibu kutoka kwangu au kusema ukweli ili ukweli utuweke huru japo kuna ya kujibu hasa yale ya msingi ila siyo kujibu ya uongo.Naomba kujibu haya:
Wana JF kama kuna maswali ya msingi na ya Ukweli yanayostahili kujibiwa nitayajibu kwa maana ya ukweli wake nilionao na uhalisia wake kutoka kwangu.
Naomba kuwasilisha.
- Jina: Stephen Juma Johnson Owawa
- Nilipo: Bukoba-Kagera
- Kazi:Mkaguzi (Auditor) ofisi ya Taifa ya Ukaguzi
- Elimu: Primary-Ratia primary School-Rorya,Sekondary-Arwing secondary School-DSM,A-Level-SHYCOM shinyanga-ECA,Chuo,University of Dar es Salaam (B.COM-Accounting)
- Kuhusu kumaliza Chuo:Nimemaliza UDSM 2010 baada ya kufukuzwa mara nyingi kutokana na kupinga sera ya elimu ya juu hasa mfumo dhania ya uchangiaji
- Kushiririki uchaguzi jimbo la Rorya 2010: Nilishiriki katika uchaguzi kupitia CHADEMA kama mratibu wa kampeni wa Mgombea Ubunge Martin Ochola Ndira kuanzia kuhame kwake NCCR kuja CHADEMA na kushiriki kwa mwezi moja kwenye kampeni
- Kugombea Ubunge Rorya: Ni haki ya kikatiba kwa mtu yeyote ili mradi atimize matakwa ya sheria
Wana JF kama kuna maswali ya msingi na ya Ukweli yanayostahili kujibiwa nitayajibu kwa maana ya ukweli wake nilionao na uhalisia wake kutoka kwangu.
Naomba kuwasilisha.