Kabwelavoice
New Member
- Mar 30, 2023
- 1
- 3
Habari Wadau,
Ukweli hii ni kero ambayo mwisho wa siku itakuja kuzaa magonjwa ya mlipuko. Stendi ya Mbezi mwisho ya daladala ambayo hata magari ya Mwendokasi yanapaki pale, kuna kero ya watu kukojoa hovyo ndani ya stendi huku walinzi na migambo wa jiji wakifukuzana na wamachinga tu lakini wanaokojoa wanawaangalia tu.
Kujihakikishia fika Mbezi mwisho asubuhi, simama lile eneo ambalo abiria wanapanga foleni kusubiri mwendokasi, mkojo unatiririka na unatoa harufu kali kwelikweli. Lakini Mamlaka zipo tu. Hii stendi wakati mwingine hata taa unakuta haziwaki ni giza tu, kilichobaki pale ni watu kuanza kujisaidia haja kubwa tu.
Kwa mtindo wa usimamizi huu, uongozi wa Manipaa ya Ubungo nachelea kusema ni useless kwasababu ni zaidi ya mwaka hali ni hiyohiyo tu kila siku.
Pia soma:
Ukweli hii ni kero ambayo mwisho wa siku itakuja kuzaa magonjwa ya mlipuko. Stendi ya Mbezi mwisho ya daladala ambayo hata magari ya Mwendokasi yanapaki pale, kuna kero ya watu kukojoa hovyo ndani ya stendi huku walinzi na migambo wa jiji wakifukuzana na wamachinga tu lakini wanaokojoa wanawaangalia tu.
Kujihakikishia fika Mbezi mwisho asubuhi, simama lile eneo ambalo abiria wanapanga foleni kusubiri mwendokasi, mkojo unatiririka na unatoa harufu kali kwelikweli. Lakini Mamlaka zipo tu. Hii stendi wakati mwingine hata taa unakuta haziwaki ni giza tu, kilichobaki pale ni watu kuanza kujisaidia haja kubwa tu.
Kwa mtindo wa usimamizi huu, uongozi wa Manipaa ya Ubungo nachelea kusema ni useless kwasababu ni zaidi ya mwaka hali ni hiyohiyo tu kila siku.
Pia soma: