DOKEZO Walinzi wa Stendi ya Daladala Mbezi Luis waangaliwe. Wanyanyasa Wafanyabiashara wadogo

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Sisi tunaokaa Stendi ya Daladala ya Mbezi Luis kila siku tumelalamika vya kutosha kuhusu changamoto ya ulinzi unaofanywa na walinzi wa Suma JKT hapa.

Changamoto zao kubwa hazijulikani kwa mamlaka za juu, tatizo lipo hivi stendi hiyo ina watu wanaolinda yaani Suma JKT ambao wamekuwa wanawafukuza Wafanyabiashara humo ndani.

Kuna muda wanazima taa makusudi ili wawakamate Wafanyabiashara waliomo ndani ya kituo na wakiwakamata huwa Wanawanyanyasa na wakati mwingine kuwapora biadhaa zao wanazoziuza kisha kuzitumia wao, mfano Samaki au sigara na vitu kama hivyo.

Ukitaka kupata uhakika tembelea kituoni hapo mida ya mchana, kuna mtu wanamwita Msambaa, huyo jamaa ni hatari kwa kuwa ndio anaongoza ‘uhalifu’ huo unaofanywa kwa mgongo wa ulinzi.

Wanachofanyiwa Wananchi tena Watanzania wenzetu hiyo stendi ina mambo jamani.
 
Tena umenikumbusha Zanzibar juzi Mgambo wa manispaa wanaibia wananchi .

Wanaenda kwa wauza mahindi ya kuchoma na kuwatishia kuwakamata kwenda kuwaweka ndani wasipowapa hela wanazotaka,

Wanachukua Hela kwa wauza mahindi shilingi 10,000/-

Mgambo wa manispaa mna laana nyie,

Unachukua rushwa kwa mnyonge?

Hiyo elfi kumi ndio Mtaji wake Mahindi’s yanatoka mbali mashambani mbali mno usafiri ni shida na gharama wewe ukija unachukua shilingi 10,000/- kirahisi tu ?



Wauza mahindi hawachafui mazingira wanaweka majani na magunzi kwenye mikokoteni yao kisha wanaenda kutupa sehemu sahihi tatizo liko wapi hapo ?

Viongozi wa Mgambo wa manispaa Unguja kana hamjui hiyo michezo washughulikieni wakomesheni waache kuonea wananchi wanaojitafutia riziki halali .

Mnataka wawe wezi na vibaka?

Kama nyie sio sehemu ya huo wisi Basi waonyeni waache mara moja.
 
Tanzania my nchi yaani mpaka mlinzi anawanyima raha .

Ngoja nianze kushona gwanda za G4S niwe natinga na buti langu nililogawiwa na afande mjuni ili nikiwa napita mtaani ni mwendo wa kaa chini simama juu

Poleni wanyonge wa Dasalam hakika wananyanyasika wakuja mtoto wa Dar humfanyii huo undezi kisa gwanda za SUMA kwanza kila mtoto wa Dar ana ndugu yake ni usalama

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
 
Tuanzie hapa,
Kwa nini hao wafanyabiashara wanafanyia biashara sehemu wasiyotakiwa kufanya biashara??
 
Juzi nilitaka nimtandike mmoja ya hao walinzi suma jkt wa hapo mbezi.
Kwanza ustaarabu hawana.

Nilichokuja kugundua hao jamaa elimu ya maadili ndogo sana wanapenda kutumia nguvu sehemu ambayo haitaji nguvu.
 
Sijasema hazitambuli, nauliza kwa nini wafanyie hizo mobile petty business zao sehemu hawaruhusiwi??



Unafahamu maana ya mobile ?

Ako na mkokoteni wake anazinguuka akiuza hakai mahala maalum kwa mrefu isipokuwa kusimama kidogo kuuza kuna tatizo gani ?
 
Unafahamu maana ya mobile ?

Ako na mkokoteni wake anazinguuka akiuza hakai mahala maalum kwa mrefu isipokuwa kusimama kidogo kuuza kuna tatizo gani ?
Wakajaribu kuuza hivyo na Lugalo, UDSM, Mlimani City au Ikulu tuone kuna shida gani.
 
hao hao wanahimizwa walipe kodi hao hao wanpigwa faini, busara itumike kutoka kwa mamlaka husika uchunguzi ufanyike wa kimya kimya kubaini kama ni kweli kuna mambo yanayoendelea, wananchi wa hali ya chini ikumbukwe hao ndio walipa
kodi za maendeleo wapo na harakati za kutafta riziki pia.
 
Back
Top Bottom