Spika, jinsi wabunge wanavyoiba/kufisadi pesa za walipa kodi wanazopewa kama mishahara ya makatibu, wahudumu na dereva wa mbunge

Deo Meck Mbagi

JF-Expert Member
Apr 19, 2015
360
525
Mh. Spika simamia ajira za wasaidizi wa Mbunge kuondoa ubinafsi, uchoyo na ufisadi.
  • Wabunge wengi hawalipi mishahara kamili kama inavyotoka bungeni.
  • Watumishi hao ambao ni watatu, Katibu, Dereva na Mhudumu wa ofisi hawapewi mikataba ya kazi na wabunge kinyume na agizo la Bunge.
  • Wasaidizi hao wakidai haki zao wanafukuzwa kazi sababu hawana mikataba
  • Ajira zao zirasimishwe ili waweze kulipa kodi na kuchangia maendeleo ya Taifa.
  • Kuna wabunge toka wachaguliwe/kuteuliwa hawana wasaidizi hao na wanalipwa pesa za kodi za Watanzania kinyume cha utaratibu.
Kwa Mujibu wa Sheria/Kanuni za Bunge letu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wabunge wanapaswa kuwa na wasaidizi watatu; ambao ni Katibu wa Mbunge, Dereva na Mhudumu wa Ofisi. Watumishi hawa wote wanatambuliwa na ofisi ya Bunge na kila mwezi Mbunge anapolipwa mshahara basi mishahara/posho zao pia zinalipwa katika akaunti ya mbunge ili mbunge azitoe na kuwalipa hao wasaidizi wake.

Bunge la Jamhuri lina idadi ya wabunge 369 wakiwa wametimia wote. Kwa idadi hiyo kila mtu akiwa na wasaidizi watatu ina maana jumla ya watu 1107 watakuwa wamepata ajira kila kipindi cha bunge. Na ajira hizi zikirasimishwa ili wasaidizi hao wawe wanalipwa mshahara moja kwa moja na bunge, litachangia kuongeza idadi ya ajira rasmi za bunge na pia kuongeza idadi ya walipa kodi.

Hivi sasa ajira za watumishi hao wa mbunge imekuwa kama hisani, wabunge wengi hawaajiri na kutoa mikataba ya kazi kama wanavyoagizwa na bunge. Na watu hao sababu wanakuwa hawana mikataba wanakuwa wanyonge na wananyonywa na wabunge hao. Na kibaya zaidi watumishi hao hawajui ni kiasi gani kinachotoka bungeni na kuingizwa kwenye akaunti ya mbunge kama mishahara yao.

Kwa dunia ya sasa lazima tubadilike, wabunge wengi wamekuwa hawawalipi stahiki za hao watumishi. Badala yake wamekuwa wanawalipa kiwango kidogo sana na wakati mwingine hawawalipi. Na baadhi ya watumishi hao pindi wanapodai mishahara ambazo ni haki zao basi wabunge huwafukuza kazi. Huu ni ubinafsi, uchoyo na ufisadi ulio wazi unaofanywa na wabunge wako Mh. Spika.

Wakati kukiwa na kilio kikubwa cha vijana kukosa ajira, huku ajira zaidi ya 1000 zikiwekwa mifukoni mwa wabunge bila utaratibu maalum ni jambo ambalo linapaswa kukomeshwa.

Nashukuru nimepiga simu bungeni na kupewa ushirikiano, kwa maelezo ya aliyepokea simu ni kuwa waajiriwa wote wa ofisi ya mbunge wanapaswa kuwa na sifa ambazo bunge limeanisha na wanapaswa kupewa mikataba. Lakini akakiri ni kweli idadi kubwa ya wabunge hawapeleki mikataba. Wanawapa ajira kwa midomo jambo ambalo linakuwa gumu wakati wanadai mishahara/haki zao. Na ameniomba nisistize kuhusu mikataba. Ni jukumu la wanaoajiriwa na mbunge katika ofisi yake pia kuomba mikataba, na sio kukubali kufanya kazi kiholela, unakuja kufukuzwa kazi huna pa kudai maana hauna mkataba wa maandishi, na wakati serikali inafanya kazi kwa maandishi na kwa nyaraka.

Hivyo ni muhimu bunge kama chombo kinachopaswa kuisimamia serikali kionyeshe mfano wa kujisimamia wenyewe na kusimamia wabunge wake. Kila mbunge lazima awe na jukumu la kuhakikisha anapeleka mikataba ya ajira za watu hao ndani ya muda utakaowekwa toka achaguliwe au ateuliwe kushika wadhifa huo wa mbunge. Na apeleke na akaunti namba za watumishi hao ili bunge badala ya kumuingizia Mbunge mishahara ya watu hao, basi kila mtu aingiziwe mshahara wake yeye mwenyewe.

Wakilipwa watawezwa kukatwa kodi na kuchangia maendeleo ya Taifa. Hapa tunaongelea walipa kodi wapya zaidi ya 1100 hapa ambao hivi sasa hawalipi kodi sababu mfumo sio mzuri na ambao pia hawalipwi wanachostahili.

Na ni aibu kubwa kwa Mbunge ambaye anaitwa Mheshimiwa kuwa mwizi wa posho ambazo zinastahili kwenda kwa wasaidizi wake, ambao pia wengine ni wapiga kura wake.

Hivyo nihitimishe kwa kumuomba na kumsihi Mh. Job Ndugai, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Tanzania walau katika bunge lako hili tukufu uweze kuliangalia jambo hili na kutumia busara yako kuweza kusimamia haki hizi na ajira hizi za watanzania wanaoonewa na kudhurumiwa haki zao na wabunge wako. Ili ajira hizi zirasimishwe na kuweza kuchangia katika ujenzi wa Taifa.

Mungu libariki Bunge, Mungu Ibariki Tanzania.

Deo Meck
 
Wabongo tulivyo wabinafsi hadi kero, jitu linapata 12M bado michongo ya miradi huko nako kuna kubunya hela nyingi tu. Still mtu anapambana na shillingi million 1 ya dereva 😂 anataka ampe nusu!

Wabunge tubadilike jamani 😂
Hivi kwenye hiyo 12 kuna dereva wa 1M tena?
Mbona hubak na kitu bobo
 
Hii ni hoja nzito sana na ya maana sana. Hawa watu ndiyo wanatakiwa wawe ngazi ya kwanza kabisa katika kuonyesha kutenda haki kwa sababu hata Hakimu au Jaji aliyeko Mahakamani, anatoa haki kwa kutumia mawazo yao waliyowahi kuyaidhinisha wao na hatimaye yakaweka kwenye makaratasi na kuanza kutumika kwa ajili ya kutoa haki.

Mtengeneza haki inabidi awe wa kwanza kuhakikisha kuwa haki hiyo haivunjwi.
 
Wabongo tulivyo wabinafsi hadi kero, jitu linapata 12M bado michongo ya miradi huko nako kuna kubunya hela nyingi tu. Still mtu anapambana na shillingi million 1 ya dereva 😂 anataka ampe nusu!

Wabunge tubadilike jamani 😂
Mimi naomba waruhusiwe hata kuajiri ndugu zao, kama labda wanaona ni vigumu kufanya kazi na watu wengine wasiowajua, provided ndugu zao hao wawe na sifa zinazostahiki.

Hii itapanua ajira kwa watanzania na pia Serikali itapata kodi. Hili tatizo ni dogo sana. Wanachotakiwa kufanya Spika na Naibu wake ni kuwaagiza Wabunge wote wa JMT, wapeleke watu hao Bungeni wenye sifa stahiki, halafu waajiriwe na Bunge moja kwa moja na mishahara yao iwe inalipwa moja kwa moja kutokea Bungeni, na si kupitia kwa Mbunge.

Waajiriwa hao wawe chini ya Mbunge husika lakini kama kuna maswala ya kinidhamu hayaendi sawa, basi Mbunge husika atatoa recommendations kwenye ofisi ya Spika na hiyo ndiyo itachukua jukumu la kutoa adhabu stahiki.

"Tusiache kila mtu na lwake, inavuruga, na inaweza ikaleta matatizo makubwa kabisa"
 
Hii ni hoja nzito sana na ya maana sana. Hawa watu ndiyo wanatakiwa wawe ngazi ya kwanza kabisa katika kuonyesha kutenda haki kwa sababu hata Hakimu au Jaji aliyeko Mahakamani, anatoa haki kwa kutumia mawazo yao waliyowahi kuyaidhinisha wao na hatimaye yakaweka kwenye makaratasi na kuanza kutumika kwa ajili ya kutoa haki. Mtengeneza haki inabidi awe wa kwanza kuhakikisha kuwa haki hiyo haivunjwi.
Wabunge gani mnaowazungumzia hawa hawa wa Bunge la Ndugai?

Hawana tofauti na wale kina dada wanaofanya promotion ya condoms mchana halafu usiku ndiyo wakwanza kufanya ngono zembe.
 
Deo!

Umenena vyema japo nawe huna tofauti sana na hao wabunge? Kwanini kwa kuwa mishahara hiyo ni kwa mujibu wa sheria kwanini usiweke figure hapa nani anatakiwa kulipwa nini?

Yamkini ukiacha Katibu ambaye anaweza kuwa na Elimu juu ya haki zake. Dereva na Mtumishi wa ofisi wanaweza kutokua na taarifa hizo.

"Kumbuka kinachoshinda vita si ujasiri bali mbinu"
 
Yani ulipwe 12M halafu usibaki na kitu? Kaka kuna kitu umetumia asubuhi hii au ni swala la hesabu mgogoro?
Sasa 1M dare
Karibu labda 500k
Sijui Msaidizi labda 300k
Personality 3M
Madeni weka 1M
Wananchi (wanyonge) weka 600k
Hamna kitu hapo mzee wa kaz...
 
Mh. Spika simamia ajira za wasaidizi wa Mbunge kuondoa ubinafsi, uchoyo na ufisadi.
  • Wabunge wengi hawalipi mishahara kamili kama inavyotoka bungeni.
  • Watumishi hao ambao ni watatu, Katibu, Dereva na Mhudumu wa ofisi hawapewi mikataba ya kazi na wabunge kinyume na agizo la Bunge.
  • Wasaidizi hao wakidai haki zao wanafukuzwa kazi sababu hawana mikataba
  • Ajira zao zirasimishwe ili waweze kulipa kodi na kuchangia maendeleo ya Taifa.
  • Kuna wabunge toka wachaguliwe/kuteuliwa hawana wasaidizi hao na wanalipwa pesa za kodi za Watanzania kinyume cha utaratibu.
Kwa Mujibu wa Sheria/Kanuni za Bunge letu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wabunge wanapaswa kuwa na wasaidizi watatu; ambao ni Katibu wa Mbunge, Dereva na Mhudumu wa Ofisi. Watumishi hawa wote wanatambuliwa na ofisi ya Bunge na kila mwezi Mbunge anapolipwa mshahara basi mishahara/posho zao pia zinalipwa katika akaunti ya mbunge ili mbunge azitoe na kuwalipa hao wasaidizi wake.

Bunge la Jamhuri lina idadi ya wabunge 369 wakiwa wametimia wote. Kwa idadi hiyo kila mtu akiwa na wasaidizi watatu ina maana jumla ya watu 1107 watakuwa wamepata ajira kila kipindi cha bunge. Na ajira hizi zikirasimishwa ili wasaidizi hao wawe wanalipwa mshahara moja kwa moja na bunge, litachangia kuongeza idadi ya ajira rasmi za bunge na pia kuongeza idadi ya walipa kodi.

Hivi sasa ajira za watumishi hao wa mbunge imekuwa kama hisani, wabunge wengi hawaajiri na kutoa mikataba ya kazi kama wanavyoagizwa na bunge. Na watu hao sababu wanakuwa hawana mikataba wanakuwa wanyonge na wananyonywa na wabunge hao. Na kibaya zaidi watumishi hao hawajui ni kiasi gani kinachotoka bungeni na kuingizwa kwenye akaunti ya mbunge kama mishahara yao.

Kwa dunia ya sasa lazima tubadilike, wabunge wengi wamekuwa hawawalipi stahiki za hao watumishi. Badala yake wamekuwa wanawalipa kiwango kidogo sana na wakati mwingine hawawalipi. Na baadhi ya watumishi hao pindi wanapodai mishahara ambazo ni haki zao basi wabunge huwafukuza kazi. Huu ni ubinafsi, uchoyo na ufisadi ulio wazi unaofanywa na wabunge wako Mh. Spika.

Wakati kukiwa na kilio kikubwa cha vijana kukosa ajira, huku ajira zaidi ya 1000 zikiwekwa mifukoni mwa wabunge bila utaratibu maalum ni jambo ambalo linapaswa kukomeshwa.

Nashukuru nimepiga simu bungeni na kupewa ushirikiano, kwa maelezo ya aliyepokea simu ni kuwa waajiriwa wote wa ofisi ya mbunge wanapaswa kuwa na sifa ambazo bunge limeanisha na wanapaswa kupewa mikataba. Lakini akakiri ni kweli idadi kubwa ya wabunge hawapeleki mikataba. Wanawapa ajira kwa midomo jambo ambalo linakuwa gumu wakati wanadai mishahara/haki zao. Na ameniomba nisistize kuhusu mikataba. Ni jukumu la wanaoajiriwa na mbunge katika ofisi yake pia kuomba mikataba, na sio kukubali kufanya kazi kiholela, unakuja kufukuzwa kazi huna pa kudai maana hauna mkataba wa maandishi, na wakati serikali inafanya kazi kwa maandishi na kwa nyaraka.

Hivyo ni muhimu bunge kama chombo kinachopaswa kuisimamia serikali kionyeshe mfano wa kujisimamia wenyewe na kusimamia wabunge wake. Kila mbunge lazima awe na jukumu la kuhakikisha anapeleka mikataba ya ajira za watu hao ndani ya muda utakaowekwa toka achaguliwe au ateuliwe kushika wadhifa huo wa mbunge. Na apeleke na akaunti namba za watumishi hao ili bunge badala ya kumuingizia Mbunge mishahara ya watu hao, basi kila mtu aingiziwe mshahara wake yeye mwenyewe.

Wakilipwa watawezwa kukatwa kodi na kuchangia maendeleo ya Taifa. Hapa tunaongelea walipa kodi wapya zaidi ya 1100 hapa ambao hivi sasa hawalipi kodi sababu mfumo sio mzuri na ambao pia hawalipwi wanachostahili.

Na ni aibu kubwa kwa Mbunge ambaye anaitwa Mheshimiwa kuwa mwizi wa posho ambazo zinastahili kwenda kwa wasaidizi wake, ambao pia wengine ni wapiga kura wake.

Hivyo nihitimishe kwa kumuomba na kumsihi Mh. Job Ndugai, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Tanzania walau katika bunge lako hili tukufu uweze kuliangalia jambo hili na kutumia busara yako kuweza kusimamia haki hizi na ajira hizi za watanzania wanaoonewa na kudhurumiwa haki zao na wabunge wako. Ili ajira hizi zirasimishwe na kuweza kuchangia katika ujenzi wa Taifa.

Mungu libariki Bunge, Mungu Ibariki Tanzania.

Deo Meck
Vipi sasa ikatokea kesi ya nyani ukampelekea ngedere!! Yaani ukakuta hata Spika mwenyewe hatoi hiyo mikataba kwa wasaidizi wake?

Dawa hapo ni Bunge/Serikali tu kubadilisha kanuni/sheria zake. Yaani ije na tamko la kuwahakiki hao wafanyakazi wote wa Wabunge mara baada tu ya kuajiriwa kwa hizo sifa zilizo ainishwa, wasaini mikataba ya ajira kama zilivyo ajira nyingine, na malipo yao yatokee Hazina kama ilivyo pia kwa Watumishi wengine wa Serikali.

Kwa njia hii hao wabunge wote janja janja watakosa pa kupigia.
 
Ni kweli kabisa. Ajira za wasaidizi wa mbunge zirasimishwe. Nakumbuka kuna mbunge mmoja hivi na bado yuko bungeni, upande wa viti maalumu DSM.

Alimfanyia unyama sana msaidizi wake mmoja hivi mpaka akaishia kumwachisha kazi kwa fedheha kabisa na bila huruma.

Kisa ni kwamba msaidizi huyo bada ya kugundua kuwa mshahara anapewa mdogo wa mbunge ambae hafanyi kazi yoyote na msaidizi kulalamikia hilo, ndipo mbunge akaamua kumwachisha kazi bila hata senti moja, na huyo msaidizi akaenda kujifia mbali kutokana na stress.

Spika Ndugai tunaomba ulitatue hilo naamini wengi wanapata maswaibu kama hayo lakini wako kimya.
 
Mh. Spika simamia ajira za wasaidizi wa Mbunge kuondoa ubinafsi, uchoyo na ufisadi.
  • Wabunge wengi hawalipi mishahara kamili kama inavyotoka bungeni.
  • Watumishi hao ambao ni watatu, Katibu, Dereva na Mhudumu wa ofisi hawapewi mikataba ya kazi na wabunge kinyume na agizo la Bunge.
  • Wasaidizi hao wakidai haki zao wanafukuzwa kazi sababu hawana mikataba
  • Ajira zao zirasimishwe ili waweze kulipa kodi na kuchangia maendeleo ya Taifa.
  • Kuna wabunge toka wachaguliwe/kuteuliwa hawana wasaidizi hao na wanalipwa pesa za kodi za Watanzania kinyume cha utaratibu.
Kwa Mujibu wa Sheria/Kanuni za Bunge letu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wabunge wanapaswa kuwa na wasaidizi watatu; ambao ni Katibu wa Mbunge, Dereva na Mhudumu wa Ofisi. Watumishi hawa wote wanatambuliwa na ofisi ya Bunge na kila mwezi Mbunge anapolipwa mshahara basi mishahara/posho zao pia zinalipwa katika akaunti ya mbunge ili mbunge azitoe na kuwalipa hao wasaidizi wake.

Bunge la Jamhuri lina idadi ya wabunge 369 wakiwa wametimia wote. Kwa idadi hiyo kila mtu akiwa na wasaidizi watatu ina maana jumla ya watu 1107 watakuwa wamepata ajira kila kipindi cha bunge. Na ajira hizi zikirasimishwa ili wasaidizi hao wawe wanalipwa mshahara moja kwa moja na bunge, litachangia kuongeza idadi ya ajira rasmi za bunge na pia kuongeza idadi ya walipa kodi.

Hivi sasa ajira za watumishi hao wa mbunge imekuwa kama hisani, wabunge wengi hawaajiri na kutoa mikataba ya kazi kama wanavyoagizwa na bunge. Na watu hao sababu wanakuwa hawana mikataba wanakuwa wanyonge na wananyonywa na wabunge hao. Na kibaya zaidi watumishi hao hawajui ni kiasi gani kinachotoka bungeni na kuingizwa kwenye akaunti ya mbunge kama mishahara yao.

Kwa dunia ya sasa lazima tubadilike, wabunge wengi wamekuwa hawawalipi stahiki za hao watumishi. Badala yake wamekuwa wanawalipa kiwango kidogo sana na wakati mwingine hawawalipi. Na baadhi ya watumishi hao pindi wanapodai mishahara ambazo ni haki zao basi wabunge huwafukuza kazi. Huu ni ubinafsi, uchoyo na ufisadi ulio wazi unaofanywa na wabunge wako Mh. Spika.

Wakati kukiwa na kilio kikubwa cha vijana kukosa ajira, huku ajira zaidi ya 1000 zikiwekwa mifukoni mwa wabunge bila utaratibu maalum ni jambo ambalo linapaswa kukomeshwa.

Nashukuru nimepiga simu bungeni na kupewa ushirikiano, kwa maelezo ya aliyepokea simu ni kuwa waajiriwa wote wa ofisi ya mbunge wanapaswa kuwa na sifa ambazo bunge limeanisha na wanapaswa kupewa mikataba. Lakini akakiri ni kweli idadi kubwa ya wabunge hawapeleki mikataba. Wanawapa ajira kwa midomo jambo ambalo linakuwa gumu wakati wanadai mishahara/haki zao. Na ameniomba nisistize kuhusu mikataba. Ni jukumu la wanaoajiriwa na mbunge katika ofisi yake pia kuomba mikataba, na sio kukubali kufanya kazi kiholela, unakuja kufukuzwa kazi huna pa kudai maana hauna mkataba wa maandishi, na wakati serikali inafanya kazi kwa maandishi na kwa nyaraka.

Hivyo ni muhimu bunge kama chombo kinachopaswa kuisimamia serikali kionyeshe mfano wa kujisimamia wenyewe na kusimamia wabunge wake. Kila mbunge lazima awe na jukumu la kuhakikisha anapeleka mikataba ya ajira za watu hao ndani ya muda utakaowekwa toka achaguliwe au ateuliwe kushika wadhifa huo wa mbunge. Na apeleke na akaunti namba za watumishi hao ili bunge badala ya kumuingizia Mbunge mishahara ya watu hao, basi kila mtu aingiziwe mshahara wake yeye mwenyewe.

Wakilipwa watawezwa kukatwa kodi na kuchangia maendeleo ya Taifa. Hapa tunaongelea walipa kodi wapya zaidi ya 1100 hapa ambao hivi sasa hawalipi kodi sababu mfumo sio mzuri na ambao pia hawalipwi wanachostahili.

Na ni aibu kubwa kwa Mbunge ambaye anaitwa Mheshimiwa kuwa mwizi wa posho ambazo zinastahili kwenda kwa wasaidizi wake, ambao pia wengine ni wapiga kura wake.

Hivyo nihitimishe kwa kumuomba na kumsihi Mh. Job Ndugai, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Tanzania walau katika bunge lako hili tukufu uweze kuliangalia jambo hili na kutumia busara yako kuweza kusimamia haki hizi na ajira hizi za watanzania wanaoonewa na kudhurumiwa haki zao na wabunge wako. Ili ajira hizi zirasimishwe na kuweza kuchangia katika ujenzi wa Taifa.

Mungu libariki Bunge, Mungu Ibariki Tanzania.

Deo Meck
Kwani kuna bunge mkuu?
 
Back
Top Bottom