Katika Press yake na waandishi wa habari aliyoifanya leo, Katibu Mkuu wa Chadema, Babu Slaa amerudia utaratibu wake wa kusema uongo mtakatifu kuwa Chama Cha Mapinduzi kwa kumtumia Mwenyekiti wake ambaye pia ni Rais wa nchi Mhe Dr Jakaya Mrisho kikwete wamepanga kununua mashine ya kuiba kura kwa ajili ya kuwadhibiti wasiweze kushinda katika uchaguzi mkuu wa mwakani 2015.
Jambo hili ni uongo wa wazi kabisa, hivi kwa hali waliyonayo chadema, haiingii akilini kwa Chama makini cha CCM ambacho kimedumu katika ziara chini ya Katibu Mkuu wake mkali wa siasa Ndugu Abdulrahaman kinana, kiwe na hofu dhidi ya chama choka mbaya kilichopoteza mwelekeo na chenye viongozi waliokosa uadilifu mbele ya macho ya familia zao na jamii. Ni UONGO wa MCHANA kweupe.
Ama jambo lingine lenye uongo usiomithilika ni kuwa Babu Slaa amemtuhumu Mheshimiwa Rais kuwa anatarajia kwenda nchini china kufanya manunuzi ya helkopta ambayo imetengenezwa ujerumani na kwamba yeye Mheshimiwa Rais ameagiza kuwa Helkopta hiyo ipelekwe china ili aweze kuiona.
haiingii akilini kuwa Rais aagize helkopta itoke Ujerumani ipelekwe China ili aweze kuiona tu, ni jambo ambalo Rais Makini kama Jakaya hawezi kulifanya.
Chama Cha CHADEMA, ambacho kimeendelea kupoteza umaarufu wake kwa kasi ya ajabu kimeendelea kuwatumia viongozi wake matabola-rasa kutunga na kueneza uongo ambao watanzania siku zote wamekuwa wakiustukia.
Siasa za aina hii zitaendelea kuimaliza Chadema, na kukifanya kisahaulike haraka zaidi katika vichwa vya watanzania.
Daaaaaaaaaaaaaah! jamani ama nimeamini njaa ni mbaya sana, Mwampamba wakati unagombea ubunge mbozi kwa tiketi ya chadema ulimsifu sana Slaa akiwa kama mgombea wa uraisi.. Uliiponda sana ccm kwa kukidhiri kwa ufisadi, ulimponda sana Kikwete na godfrey Zambi. Na tulikuamini sana na ndio maana wengine tukajitolea kusindikiza msafara wako kuanzia Isangu hadi Manyara takribani km 7 kwa miguu na baiskel huku wewe ukiwa umepanda gari. Kwenye kampeni zako ulikuwa unasema ukiishabikia ccm ujanani ukizeeka utakuwa mchawi,. Je ndiko wewe unakoelekea? Hueleweki kabisa wewe maana siku wakikufurusha huko ukaenda ACT bila shaka utawaponda tena wafadhili wako CCM, hizo ni tabia za kibinti.