SKONGA: Kipindi 'kinachovua nguo' wanafunzi

You have the right to your thinking. Try me.

ulishaone lile tangazo la Twaweza? Lile ambalo wanafunzi wanakimbia mchakamchaka, wanajifunza stadi za maisha na mengine. Hiyo ilikuwa enzi za Mwalimu. Baada ya hapo mambo yakabadilika. Sasa wanafunzi wanaenda shule wanakaa chini, madarasa yamebomoka, n.k. Twaweza walikosea?
 
ulishaone lile tangazo la Twaweza? Lile ambalo wanafunzi wanakimbia mchakamchaka, wanajifunza stadi za maisha na mengine. Hiyo ilikuwa enzi za Mwalimu. Baada ya hapo mambo yakabadilika. Sasa wanafunzi wanaenda shule wanakaa chini, madarasa yamebomoka, n.k. Twaweza walikosea?

Baadhi ya wanafunzi wa moja ya Sekondari za kata, Rombo wakiwa darasani


Baadhi ya wanafunzi wa Sekondari ya Urauri, Wilaya ya Rombo.
8d6u1855.jpg

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua mojawapo ya darasa katika shule mpya ya sekondari ya Masengwa wilayani Shinyanga muda mfupi baada ya kuifungua rasmi jana mchana.25-01-2010
 
Mwingine akaulizwa mdahalo ni nini??
akiwa hajui maana ya mdahalo alijibu hivi.
1. unachukua mdahalo wako unauosha vizuri.
2.hakikisha mdahalo wako haujakomaa.
3. bandika sufuria yako jikoni.
4. wekamdahalo wako kisha uache uchemke kwa dakika kumi na tano.
5. mdahalo wako ukiwa tayari uepue.
6.mdahalo huu unaweza kuula na kinywaji chochote.
 
Baadhi ya wanafunzi wa moja ya Sekondari za kata, Rombo wakiwa darasani


Baadhi ya wanafunzi wa Sekondari ya Urauri, Wilaya ya Rombo.
8d6u1855.jpg

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua mojawapo ya darasa katika shule mpya ya sekondari ya Masengwa wilayani Shinyanga muda mfupi baada ya kuifungua rasmi jana mchana.25-01-2010

This is not random selection. Ulitegemea Rais akafungue kimeo? Hata kati ya vipofu mwenye chongo mfalme. Elimu yetu dada Faiza imedidimia hasa miaka ya karibuni
 
Kuna mwanafunzi wa kidato cha tatu,aliulizwa binadamu ana figo ngapi??
Akasita kwanza (akionyesha hajui figo ni nini)......kisha akajibu MOJA...
Ilivyofika Wakati wa kuimba sasa...nilichoka...
 
Umesaema atlas nimekumbuka, tulikuwa tunapenda kucheza michezo wa kutafuta miji kwente atlas.
Anayeona, anachagua yeye mji mtafute.

Ilikuwa inasaidia sana kujua ramani, it was fun.
Hivi tuna ramani ya mikoa mipya kweli? Uoto wa asili sijui na ma nini nini?

Mimi nimeacha kutizama kabisa, naona kama naweza kuzimia. Hawa watoto wanamjua 50 cent lakini hawamjui hata rais wa awamu ya pili wa Nchi hii.

Leo hakuna hata Atlas yenye kuonyesha miji, mikoa, mataifa mbalimbali na hata hali ya hewa. Hawa mabepari mamboleo wameviondoa kabisa, inatia hasira.

Hata somo la sanaa wamefuta!

Na ushahidi wa wazi hata hapa JF, graduate mzima anaandika "dhambi" - zambi, "uongo" - uhongo...nk nk. Si hilo tu hata suala dogo la kuweka 'paragraph' linawashinda. Huu ni msiba.
 
Nami niliisha mshauri waziri wa elimu wakati wa kuunda tume ya kuchunguza matokeo ya kidatio cha nne , nilisema kuwa sample ya EATV kupitia kipindi cha skonga ni jibu tosha kabisa ya kidudu mtu kilichopo kwa madenti wetu wa xaxa.
 
This is not random selection. Ulitegemea Rais akafungue kimeo? Hata kati ya vipofu mwenye chongo mfalme. Elimu yetu dada Faiza imedidimia hasa miaka ya karibuni

Elimu iliyokufa imekuja kufufuliwa na Kikwete na imeanza kupanda kuliko wakati wowote ule. Kwa mtu mwenye macho lakini asiye na muono kama wewe, huwezi kuyaona hayo.
 
Dogo kila swali hajui mwisho akaulizwa habari za diamond anamjua kuliko wazazi wake,alipopewa chance wacha aimbe karibia nyimbo zote za diamond,

Ukweli tatizo linaanzia mashuleni mpaka ndani ya family zetu,tusitegemee maajabu sana kama walimu wenyewe ndio hawa waliopata dv 4 na wazazi wenyewe hawa wakisasa wakirudi home mkononi wana magazeti ya udaku na na DVD za bongo movie,tuna kazi ndefu sana

Umemaliza mkuu maana haya mambo ya madogo kuna factors nyingi sana kwani utasikia watu kila kitu "WATOTO WA SIKU HIZI" tunasahau kwamba hata "WAZAZI WA SIKU HIZI" nao wanachangia hivyo kuna haja ya ku-trace hata historia ya wazazi wa wanafunzi wanao-fail tunaweza tukagundua kitu aisee
 
Umesaema atlas nimekumbuka, tulikuwa tunapenda kucheza michezo wa kutafuta miji kwente atlas.
Anayeona, anachagua yeye mji mtafute.

Ilikuwa inasaidia sana kujua ramani, it was fun.
Hivi tuna ramani ya mikoa mipya kweli? Uoto wa asili sijui na ma nini nini?

Hii issue ilikuwa very interesting, unakuta unachagua mto umeandikwa kwa herufi ndogo alafu unamwambia mwenzako autafute, siku hizi hata mtu umuulize mto Malagalasi hajui ulipo, niliwahi kukutana na swali toka kwa dogo yupo form 3 ananiuiza kama Dodoma kuna ziwa
 
Mwingine akaulizwa mdahalo ni nini??
akiwa hajui maana ya mdahalo alijibu hivi.
1. unachukua mdahalo wako unauosha vizuri.
2.hakikisha mdahalo wako haujakomaa.
3. bandika sufuria yako jikoni.
4. wekamdahalo wako kisha uache uchemke kwa dakika kumi na tano.
5. mdahalo wako ukiwa tayari uepue.
6.mdahalo huu unaweza kuula na kinywaji chochote.

Nimeipenda hii mdau, kweli hii au mazungumzo baada ya habari ya enzi zile za "Tenge mkwapua nyama"
 
Ha ha ha, ungemwambia kuna ziwa Mtera.

Ilikuwa raha sana kutafuta miji, mito

Ila kuna mmoja aliwahi tusumbua, tulitafuta kwa saa nzima hatuoni, tena ilikuwa ramani ya asia
Kasema tutafute 'mate', tumetafuta hadi tumechoka tunaomba atuoneshe
Kumbe katema pembeni kwenye ramani, afu akatuonyesha mate si haya hapa. Kidogo tumuue

Sitakaa nimshahau yule binti

Hii issue ilikuwa very interesting, unakuta unachagua mto umeandikwa kwa herufi ndogo alafu unamwambia mwenzako autafute, siku hizi hata mtu umuulize mto Malagalasi hajui ulipo, niliwahi kukutana na swali toka kwa dogo yupo form 3 ananiuiza kama Dodoma kuna ziwa
 
Hahahah....but before you do that remember;

No matter how hot your anger is, it can not cook yams-Nigeria

back to Topic:

Nakumbuka nikiwa sekondari ya Mawezi, Moshi.
Likizo tulikuwa tunakutana na washikaji tuliosoma wote primary halafu wakapangiwa special schools Kibaha, Mzumbe, na Ilboru.
Na wale wa seminary ambapo wanapewa notes na test kila wiki…jamani kuna watu wana raha.
Basi hawa woote tunakutana mtaani tunafundishana weee na kubadilishana knowledge mpaka likizo inaisha…hiyo ndo ilikuwa tuition yetu. Ndiyo si tulisoma wote primary kwahiyo bado ni marafiki.
Na likizo wanakuja nyumbani. Wana interact na sie wa shule za kata tunabadilishana mawazo.
Matokeo form four: Division one (leo hii ningekuwa top ten ya watahiniwa wa CSEE 2012)

A level nikapangiwa Same sekondari. Huko tukawa tunatoroka na kuja kupiga kitabu Moshi sekondari (Old Moshi Sec) wenyewe waliamua kujiita Gold Moshi…dem dayz!
Likizo tena tunakutana na washkaji waliopangiwa Special schools hizo tunabadilishana utirial ma test pepa manini.
Matokeo form six: Division one nzuri tu ya kunipa grades za kusoma Electronic Science & Communication chuo.

Mtazamo wangu:
Ile dhana ya special schools ilisaidia sana kuboresha elimu na kuongeza morali wa wanafunzi kusoma.

  1. Sasa hivi unakuta mwanafunzi anasoma hapo hapo na wale wale aliosoma nao primary hawapati challenges za nje hata kidogo.
  2. Waliofuta special schools hawakukumbuka ule usemi wa, "the world is a book and those who don't travel read only a book" otherwise walidhani kina Nyerere pamoja na umaskini tuliokuwa nao bado walifanya hivyo. Walipeleka hadi watu kusoma nje kwanini???
My call:
Kawambwa & Co. rudisheni special schools kwa maana ile ile ya special schools….

Pia sisi kama taifa hatujaamua kuchagua mfumo wa elimu inayotufaa nakupata elimu endelevu,kwamfano unayoizungumzia ni elimu tuliorithi kutoka kwa mkoloni tukaiboresha ikaenda nasi kwa wakati huo,kumbuka pia baada yahapo tukaona kama elimu hiyo ilipitwa na wakati tukaja na maboresho mengine ambayo yalizidi kututumbukiza shimoni ikiwa ni kuongeza idadi ya watoto wanao anza elimu ya awali na darasa la kwanza,baada yahapo tukaja namfumo waelimu ya kata nayo ilkuja kwa nia njema kwamba idiadi ya vijana wanasoma sekondari na kuhitim iongezeka lakini tukasahau nyuma mambo muhimu katika uwasilishwaji wa elimu hii,ikiwamo uhaba wa waalimu na vitendea kazi,ubadirishwaji wa mitaala bila ya kuwapa waalimu miongozo nk.
Naona sasa niwakati wakuchagua kilicho bora na chenye manufaa katika elimu yetu ilikutuwezesha kuzalisha wataalam wenye ufanisi na watakao weza kukabiliana na changamoto zandani na nje ya nchi
 
Ha ha ha, ungemwambia kuna ziwa Mtera.

Ilikuwa raha sana kutafuta miji, mito

Ila kuna mmoja aliwahi tusumbua, tulitafuta kwa saa nzima hatuoni, tena ilikuwa ramani ya asia
Kasema tutafute 'mate', tumetafuta hadi tumechoka tunaomba atuoneshe
Kumbe katema pembeni kwenye ramani, afu akatuonyesha mate si haya hapa. Kidogo tumuue

Sitakaa nimshahau yule binti

Au ningemwambia ziwa Hombolo, ila huyo wa mate ni noma
 
Pia sisi kama taifa hatujaamua kuchagua mfumo wa elimu inayotufaa nakupata elimu endelevu,kwamfano unayoizungumzia ni elimu tuliorithi kutoka kwa mkoloni tukaiboresha ikaenda nasi kwa wakati huo,kumbuka pia baada yahapo tukaona kama elimu hiyo ilipitwa na wakati tukaja na maboresho mengine ambayo yalizidi kututumbukiza shimoni ikiwa ni kuongeza idadi ya watoto wanao anza elimu ya awali na darasa la kwanza,baada yahapo tukaja namfumo waelimu ya kata nayo ilkuja kwa nia njema kwamba idiadi ya vijana wanasoma sekondari na kuhitim iongezeka lakini tukasahau nyuma mambo muhimu katika uwasilishwaji wa elimu hii,ikiwamo uhaba wa waalimu na vitendea kazi,ubadirishwaji wa mitaala bila ya kuwapa waalimu miongozo nk.
Naona sasa niwakati wakuchagua kilicho bora na chenye manufaa katika elimu yetu ilikutuwezesha kuzalisha wataalam wenye ufanisi na watakao weza kukabiliana na changamoto zandani na nje ya nchi

Kwa mtazamo huo huo ni heri turudi kule kwa wakoloni...then tuendelee from there!!!
 
Kwa mtazamo huo huo ni heri turudi kule kwa wakoloni...then tuendelee from there!!!

kwa elimu kama ile bado tutakuwa palepale kama hatutaboresha mazingira ya utoaji waelimu yenyewe,kipindi hicho wanafunzi wachache walipata nafasi ya kwenda sekondari na pia shule zilikuwa chache,tukbali hii ni changamoto kwetu sote wazazi,wadau waelimu,wanasiasa,serikali..nilichogundua wengi tunaopiga kelele na kuilaumu mojamoja serikali,kwanza kabisa watoto au wadogo zetu hawasomi hizi shule za watoto wa makabwela,naona kelele za lawama nikama kuwacheka waliokasa nafasi ya kuwapeleka watoto wao shule za gharama juu..Elimu yetu ndio msingi imara wa ukombozi wa Tanzania
 
Mimi lawama zangu naanza kuzitupia media, toka saa sita usiku mpaka saa sita usiku wa siku nyingine vipindi vinavyowekwa ni miziki na filamu za kifilipino. Yanayooneshwa humo sidhani kama yana mchango mzuri kwenye ukuaji na elimu ya vijana wetu.

Tujiulize kwanza ni vipindi vingapi vyenye kumjenga kijana kielimu na kimaadili vinaoneshwa na media zetu. Matokeo yake wanakufa wahadhiri, madaktari bingwa, wanasayansi wenye kuletea taifa hili sifa, wanasheria na wanasiasa mahiri kama Kawawa hakuna vipindi maalumu vya maombolezo yao.

Lakini tumeona wamekufa wasanii(Kanumba, na huyu aliyekuwa anasifia mikasi, majani na mitungi sijui naitwa Ngwea) vinawekwa vipindi maalumu kwenye media kuomboleza. Ina maana Ngwea alikuwa anaitangaza nchi yetu vizuri nje kuliko Marehemu Kawawa, Dokta F. MASSAU,Wahadhiri wetu vyuo vikuu, Majaji, Wabunge na Mawaziri wetu.

Juzi kati wanajeshi wetu wamefariki huko Sudani wakitekeleza majukumu ya kitaifa, wanaojua wanieleze hapa ni TV, radio ilirusha live shughuli nzima toka miili ilipotua uwanja wa ndege mpaka ilipoagwa pale upanga na je kulikuwa na kipindi gani maalumu cha kueleza michango na japo historia zao tu kwa kifupi kama mashujaa wetu, hakuna!!!!!!!!!
 
Lakini na maswali mengine jamani,... hivi gracier erosion ina maana gani kuifundisha kwenye nchi zetu hizi?. Tunabaki kukariri vitu vya kufikirika tu. Kuna physical features nyingi tu za kujifunza kwenye mazingira yetu tubadilike, huo ndio ukoloni wa fikra au uvivu wa kutafiti tu
 
Back
Top Bottom