Siwezi kuisahau siku ya jana-mwanamke ajifungua kwenye foleni

njija

Senior Member
Jun 30, 2011
110
62
Wadau maisha ya mtanzania siku hadi siku yanazidi kuwa magumu,kwa upande wa Dar miongoni mwa mambo ambayo yanaendelea kututesa na kutupotezea muda mwingi barabarani ni foleni za magari, katika siku ambazo zimeniumiza mimi ni jana, nilikuwa nikitokea posta mpya kuelekea tandika nikiwa kwenye daladala, tulipofika kituo cha baharini mama mjamzito alipanda katika gari ambalo nilikuwepo,tulipovuka usawa wa mnazimoja basi likiwa limejaa sana mama yule ghafla alilia kwa uchungu, mwanamke mmoja aliyekuwa karibu naye alimuliza vipi akajibu naumwa dereva akaelezwa asimamishe gari, wakati anajaribu kupaki ili watafute taxi na watu wampishe ashuke yule mama akashindwa hata kusogeza mguu kilichofuata akakaa ktk ngazi ya mlangoni mara mtoto akalia wanawake walio kuwa karibu yake wakamsaidia kupokea mtoto watu wote wakiona ikawa shida watu kushuka, ikabidi dereva kuendesha gari mpaka hosp iliyokuwa jirani abiria tukiwepo, kweli sipendi kuendelea kwani inaumiza sana MUNGU ATUSAIDIE WATANZANIA, sasa kwa tukio la jana nikajiuliza vipi kuhusu zile bajaji zilizonunuliwa maalumu kwa wajawazito kuna sehemu ya nurse kukaa ikitokea dharura aweze kumsaidia mama? au zina ukubwa gani kumwezesha mama mjamzito kulala vizuri wakielekea hosp? nawasilisha
 
Kweli ni habari ya uchungu sana.
nadhani na mama hakua makini lakini. ukianza kusogea karibu ya tarehe ya kuzaa kwa nini utembee peke yako tena kwenye daladala? Machungu yanaanza mapema kidogo hivo angeweza kujipanga mapema kidogo.
Bahati yake mlimsaidia na akajifungua salama.
 
Wadau maisha ya mtanzania siku hadi siku yanazidi kuwa magumu,kwa upande wa Dar miongoni mwa mambo ambayo yanaendelea kututesa na kutupotezea muda mwingi barabarani ni foleni za magari, katika siku ambazo zimeniumiza mimi ni jana, nilikuwa nikitokea posta mpya kuelekea tandika nikiwa kwenye daladala, tulipofika kituo cha baharini mama mjamzito alipanda katika gari ambalo nilikuwepo,tulipovuka usawa wa mnazimoja basi likiwa limejaa sana mama yule ghafla alilia kwa uchungu, mwanamke mmoja aliyekuwa karibu naye alimuliza vipi akajibu naumwa dereva akaelezwa asimamishe gari, wakati anajaribu kupaki ili watafute taxi na watu wampishe ashuke yule mama akashindwa hata kusogeza mguu kilichofuata akakaa ktk ngazi ya mlangoni mara mtoto akalia wanawake walio kuwa karibu yake wakamsaidia kupokea mtoto watu wote wakiona ikawa shida watu kushuka, ikabidi dereva kuendesha gari mpaka hosp iliyokuwa jirani abiria tukiwepo, kweli sipendi kuendelea kwani inaumiza sana MUNGU ATUSAIDIE WATANZANIA, sasa kwa tukio la jana nikajiuliza vipi kuhusu zile bajaji zilizonunuliwa maalumu kwa wajawazito kuna sehemu ya nurse kukaa ikitokea dharura aweze kumsaidia mama? au zina ukubwa gani kumwezesha mama mjamzito kulala vizuri wakielekea hosp? nawasilisha

Inaumiza sana mkuu.

Labda siku wake zao wakijifungulia kwenye foleni au mitaro watazinduka....Na hapo inabidi kumshukuru Mungu kwamba amejifungua salama. What if kungetokea complications?

Hii nchi inakera sana kwani watu wengine tumechukuliwa kama viumbe tusiopumua. Tunaonekaa kama mjitu ya ajabu ajabu kiasi kwamba hata mijusi ni bora zidi yetu!!
 
Hata mimi niliwaza hivyo, lakini muda tulio kaa ktk foleni lazima ingekuwa hivyo hata kama angekuwa kwenye taxi angejifungua njiani hakuwa peke yake alikuwa na binti yake ila hakuwa na la kufanya kwasababu ilikuwa kama kitendo cha dakika kumi tu mtoto tayari akazaliwa.
 
Hii inaleta uchungu sana, yaani mtu anajifungua akiwa kwenye daladala iliyojaa abiria!! our country will soon become evil land.
 
... baya zaidi ni kweli kwamba pamoja na udhalimu huu, habari ya kusikitisha, ya kutia huzuni kama hii inasahaulika na kuyeyuka mithili ya petroli kesho yake. Inawezekana mama huyo mjamzito hakuwa na choice ya kubaki nyumbani au kwenda kliniki akijua siku imesogea kutokana na makali ya maisha. Mbaya zaidi ni future inayomsubiri huyo aliyezaliwa ikiwa mabadiliko ya haraka hayafanyiki nchini.
 
Haya mambo yanatokeaga na yanaweza kutokea kwa masikini hata tajiri kwa sababu kutokana na hizi foleni mwanamke anaweza kuwa katika gari yoyote daladala au gari ndogo,ni mambo yanatokeaga hata wanawake wengine wanajifunguliaga mpaka kwenye ndege
 
Kweli ni habari ya uchungu sana.
nadhani na mama hakua makini lakini. ukianza kusogea karibu ya tarehe ya kuzaa kwa nini utembee peke yako tena kwenye daladala? Machungu yanaanza mapema kidogo hivo angeweza kujipanga mapema kidogo.
Bahati yake mlimsaidia na akajifungua salama.
Nadhani unakufuru kama wewe umejaliwa uwezo wa kutembea na teksi shukuru mungu wanawake wengi tuuuuuuuu wanapanda daladala kabla na hata baada ya kujifungua mambo ambayo zamani hayakuweko pale ocean road walikuwa wanarudisha majumbani mwao na ambulance,hata wakipiga simu ambulance ziliwafuata ndio Tanzania baada ya miaka 50
 
Habari ya kuhuzunisha, polen mama. Folen ni janga .Hapa tusiangalie indicators za kwenye makaratasi. Tunafundishwa early self referral lakin access ya kuzifikia hakuna. Then wabunge wanapongezana kwa kupunguza vifo vya wajawazito. Ujinga mtupu.
 
pole mamy,ila kinamama nasi tupende kwenda kliniki huwa mara nyingi wanakadiriaga muda utakaojifungua na ni vyema kuuzingatia ili mambo kama haya yastokee!
 
pole mamy,ila kinamama nasi tupende kwenda kliniki huwa mara nyingi wanakadiriaga muda utakaojifungua na ni vyema kuuzingatia ili mambo kama haya yastokee!

Flora mleta mada hapa ameweka vitu viwili. Kuna hili la foleni sasa hata kama angekuwa anakwenda huko hospitali na hizi foleni zetu zisizo tabirika jibu sitakuwa hilo hilo!
 
Pole kwa tukio hili na wanaojaribu kulaumu kwa kusema akuwamakini kuangalia tar za makadirio fikirieni Mara 2 Akuna anaependa hadha Kama hii
msiba usikiege kwa mwenzako tu
 
pole mamy,ila kinamama nasi tupende kwenda kliniki huwa mara nyingi wanakadiriaga muda utakaojifungua na ni vyema kuuzingatia ili mambo kama haya yastokee!
unafikiri kuna mama wa mjini asiyeenda clinic kwa sasa?sio mara nying wanakadiriaga NI LAZIMA WAKADIRIE , Imagine imetokea 2weeks before?? Na kama alikuwa anaenda hospital? Unazijua hospital zetu zilivyo na msongamano? Watu wanarudishwa majumban kisa uchungu haujakuwa mkubwa kupisha nafasi. Jaribun kwenda kwenye hospital za government mjionee hali halisi.
 
huyu mama hastahili lawama wamama wengine uchungu mara moja wala hauchukui muda mrefu. Clinic nyingi hazina ultrasound hivyo ni ngumu kukadiria na hata wakikadiria wakati mwingine haiwi sawa mfano shemeji yangu walikadiria 13 februari lakini alijifungua tarehe 24 januari na kadiria yenyewe ni ya ultrasound
 
Kuna jitu naona anasema mama hakuwa makini..... Hivi wewe ukiwa na uwezo wa kuchukua tax unadhani wote wanaweza
 
Uchungu hauna taarifa mpendwa,unaweza kuanza popote tena ghafla hasa mimba ikiwa ni ya pili na kuendelea. Af kingine kutokana na ugum wa maisha mtu huwez kukaa kisa et unakaribia kujifungua,lazma kutafuta. Dala dala ndio usafir wa walio wengi hapa jijin so hiv vitu ni vya kuomba Mungu tu visikukute
 
Kweli ni habari ya uchungu sana. nadhani na mama hakua makini lakini. ukianza kusogea karibu ya tarehe ya kuzaa kwa nini utembee peke yako tena kwenye daladala? Machungu yanaanza mapema kidogo hivo angeweza kujipanga mapema kidogo.Bahati yake mlimsaidia na akajifungua salama.
ndugu yangu uzazi hauna kujipanga. Unaweza kuzaa wakati wowote. Kwa wanawake waliozaa wanaelewa zaidi. Unaweza kushikwa uchungu hata mimba ya miezi 7! Nampa pole sana huyo dada.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom