Elections 2010 Sitta: Kutoka Uspika hadi Uwaziri; safari ya anguko inakaribia

Mwenye macho haambiwi tazama,even a lil child will know that jus a muv 2 silence him...i wish 6 angeturn dwn da offer!
 
Kutoka kiongozi wa mhimili wa pili wa dola (bunge) hadi kuongoza wizara isiyojulikana ya Afrika Mashariki naweza kusema isiyo na hadhi kwake kwa vile huwezi kuilinganisha na wizara kama ya Katiba na Sheria.

Sitta amepewa nafasi hiyo ili kumpoza kutokana na machungu aliyopata baada ya jina lake kukatwa kwa makusudi kwenye kinyang'anyiro cha uspika kwa madai kwamba safari hii ni zamu ya wanawake kuongoza mhimili huo wa dola.

Sitta amewekwa hapo kama pazia kwa nia ya kumfunga mdomo ili asitumie nafasi yake kama mbunge huru kuichachafya serikali kama alivyokuwa akiruhusu mijadala ya aina hiyo wakati alipokuwa spika katika Bunge lililopita.

SS ajifunze kwa waliomtangulia kuongoza wizara hiyo kama Dk. Ibrahim Msabaha na Deodorous Kamala kuwa hawakusikika na mwisho wa siku si kuwa walianguka kisiasa tu bali walishindwa kwenye majimbo yao pia.

Nampa miaka miwili tutakuwa tumemsahau kwenye nyanja za siasa.

Chatu kafuga mbwa?? Au mbwa kafuga chatu?
 
Kutoka kiongozi wa mhimili wa pili wa dola (bunge) hadi kuongoza wizara isiyojulikana ya Afrika Mashariki naweza kusema isiyo na hadhi kwake kwa vile huwezi kuilinganisha na wizara kama ya Katiba na Sheria.

Sitta amepewa nafasi hiyo ili kumpoza kutokana na machungu aliyopata baada ya jina lake kukatwa kwa makusudi kwenye kinyanganyiro cha uspika kwa madai kwamba safari hii ni zamu ya wanawake kuongoza mhimili huo wa dola.

Sitta amewekwa hapo kama pazia kwa nia ya kumfunga mdomo ili asitumie nafasi yake kama mbunge huru kuichachafya serikali kama alivyokuwa akiruhusu mijadala ya aina hiyo wakati alipokuwa spika katika Bunge lililopita.

SS ajifunze kwa waliomtangulia kuongoza wizara hiyo kama Dk. Ibrahim Msabaha na Deodorous Kamala kuwa hawakusikika na mwisho wa siku si kuwa walianguka kisiasa tu bali walishindwa kwenye majimbo yao pia.

Nampa miaka miwili tutakuwa tumemsahau kwenye nyanja za siasa.

Huyu mzee SIX alishatangaza rasmi kuwa hatagombea tena ubunge. Alisema hii itakuwa ndiyo ngwe yake ya mwisho kuwa mbunge. Kinachonishangaza ni kwa nini ameamua kukubali uwaziri!!! Kwa hadhi yake, angeweza kubaki tu kuwa mbunge wa kawaida akawa na uhuru kamili wa kuipigia kelele serikali inapofanya makosa badala ya sasa ambapo hawezi kuipigia kelele kwa kuwa naye atakuwa sehemu ya mkosa yatakayofanywa na serikali.

Ninachoombea ni kitu kimoja nacho ni kuwa mzee wa watu asikumbwe na kashfa. Karaha ya masuala ya utendaji ndiyo hiyo, wakati wowote ujiandae kuingia kwenye aidha kwa makusudi au bila makusudi. Mafisadi wanaisuibri siku hiyo kwa matumaini makubwa.
 
Nanukuu .....

"Hata hivyo, wiki hii Sitta alifafanua kwamba kuenguliwa kwake katika uspika kutamfanya awashe moto zaidi kwa uhuru kwa mafisadi, kwani anayo tiketi ya uwakilishi ya wananchi wa Urambo Mashariki.

Akizungumza na Mwananchi wiki hii Sitta alisema 'Sita ni yule yule' na kwamba wanaodhani kuwa mbunge wa kawaida kutampunguzia nguvu kusimamia anayoamini ni makosa makubwa.

Sitta alisema kuanzia Bunge la Februari atawasha moto pale itakapostahili na kwamba ataendeleza misingi aliyoacha Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere ya kupambana na rushwa na ubabaishaji wa aina yoyote.

Alisisitiza kuwa hataruhusu ubabaishaji wala ufisadi kwani vinaondoa thamani ya utu wa mtanzania wa kawaida na kumkosesha haki zake za kufaidi raslimali za nchi."


TUNASUBIRI TUONE KAMA SIX ATAKWENDA SAWIA NA KAULI ZAKE AU ATAGEUKA JIWE!
 
Wengi wetu tulitabiri kwamba hatua ya kwanza ya kumuua Sitta kisiasa itakuwa ni kwa kumwondoa kwenye kiti cha uspika. Hiyo haikuwa kazi rahisi lakini mafisadi kwa nguvu yao ndani ya chama tayari wamefanikisha na sasa Sitta siyo spika tena. Hivi sasa mafisadi watakuwa bado wanagonganisha glasi za vinywaji moto na baridi kwa kufanikisha kazi hiyo ngumu. Wananchi wengi walisikitika kwa kitendo cha kumwangusha Siita lakini kama kawaida yao, tayari wamesahau na umaarufu wa Sitta umeendelea kuyeyuka kama barafu juani.

Mafisadi walijua kwamba kwa kumwondoa kwenye uspika bila shaka kungemtia hasira kubwa na kusababisha awe mlopokaji ndani ya jengo na kuendelea kuiadhibu serikali kwa maswali magumu, akiwa mbunge wa kawaida. Uhuru huo angekuwa nao kwa mantiki ndogo tu. Mzee Sitta tayari ameshatangaza kwamba hatagombea tena ubunge ifikapo mwaka 2015 na hivyo kwa kuwa mlopokaji ndani ya bunge hakuwa na cha kupoteza. Mafisadi waliliona hilo na dawa yake ndiyo hiyo ya uwaziri. Waswahili wanasema 'mchawi mpe mtoto akulelee' walichofanya mafisadi ni kumfanya Sitta awe sehemu ya serikali. Kwa kufanikisha hilo mafisadi 'wamelamba dume' kwani Sitta siyo kwamba tu hataikosoa serikali lakini hatakuwa na jambo la maana la kusimamia na kupata umaarufu. Wizara ya Afrika Mashariki haina fursa hiyo (rejea Dr. Msabaha na Dr. Kamala).

Pamoja na hilo, lengo la mafisadi siyo kumfanya awe sehemu ya serikali tu. Kama wengi ndivyo wanavyodhani basi wapo nje ya mstari. Ikumbukwe kuwa pigo walilopata mafisadi chini ya uongozi wa Sitta kama spika lilikuwa ni kubwa sana na limeendelea kuwaumiza mpaka leo. Fisadi mmoja mwandamizi alitamka bayana kuwa ''najua tatizo ni uwaziri mkuu''. Tafsiri yake ni kwamba Sitta alikuwa nae anauwinda uwaziri mkuu. Hivyo, ulipizaji kisasi wa mafisadi hauwezi kuishia hapo na kuwa laini kiasi hicho. Wengi wetu tulitabiri na hili ndilo lengo mahsusi la mafisadi ni kumwingiza Sitta kwenye masuala ya utendaji (uwaziri) ili iwe rahisi kumtega. Kwa kawaida, ukiwa waziri wakati mwingine unalazimika kubeba lawama hata kwa makosa yaliyofanywa na watu walio chini yako. Mahesabu au karata zilizochangwa na mafisadi ni kuhakikisha kuwa Sitta anakumbana na kashfa itakayojadiliwa bungeni kwa nguvu zote ili hatimaye wamchafue na kufuta hadhi yake yote. Hilo angeweza kulikwepa kwa kukataa kistaarabu uwaziri. Kwa kuwa amekubali kuingia, ajiandae na pigo la pili la mafisadi litakalomfanya awe raia wa kawaida kama mimi.
 
If he was brave enough to tell Mr. President that he does not wan't to accept ministerial position, I'd agree with him.
 
Nanukuu .....

"Hata hivyo, wiki hii Sitta alifafanua kwamba kuenguliwa kwake katika uspika kutamfanya awashe moto zaidi kwa uhuru kwa mafisadi, kwani anayo tiketi ya uwakilishi ya wananchi wa Urambo Mashariki.

Akizungumza na Mwananchi wiki hii Sitta alisema 'Sita ni yule yule' na kwamba wanaodhani kuwa mbunge wa kawaida kutampunguzia nguvu kusimamia anayoamini ni makosa makubwa.

Sitta alisema kuanzia Bunge la Februari atawasha moto pale itakapostahili na kwamba ataendeleza misingi aliyoacha Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere ya kupambana na rushwa na ubabaishaji wa aina yoyote.

Alisisitiza kuwa hataruhusu ubabaishaji wala ufisadi kwani vinaondoa thamani ya utu wa mtanzania wa kawaida na kumkosesha haki zake za kufaidi raslimali za nchi."


TUNASUBIRI TUONE KAMA SIX ATAKWENDA SAWIA NA KAULI ZAKE AU ATAGEUKA JIWE!

Kwa mwenendo huo uliopo sasa hivi na Wizara aliyopewa amabayo mimi naona ni dormant tu nahesabu kuwa in less than two years SS atakuwa kwishnei unless aukatae uwaziri which i also doubt it kama anaweza kufanya hivyo
 
Bora SS angebaki kuwa mbunge huru na kuwa mshauri wa vyama kama wenzake kina SAS na Warioba.
 
Ukiwa mchapa kazi utang'ara kwenye kazi yoyote utakayopewa. Mrema, alisha prove hivyo, kwani hata walipompeleka kwenye wizara ambayo ilionekana kama wana mmaliza kisiasa, bado alipata kazi za kufanya na aka nga'ra. Hivyo hivyo Magufuli.

Huenda ni wakati muafaka kwa mheshimiwa Sitta ku prove beyond reasonable doubt kwamba yeye ni mchapa kazi kweli kweli na sio opportunist aliyetumia nafasi ya uspika kujikweza.

Huko EA kuna changamoto nyingi sana ambazo zinaenda na maslahi ya taifa. Atusaidie mikataba ya EA iwe yenye manufaa kwa Tanzania.
 
Tunachoshindwa kufahamu wengi ni kua cheo ni dhamana pamoja na kua ni neno tunalitumia kila siku. Mh Sitta alikua na bado ni muajiriwa wa serikali na serikali ina utaratibu wake wa kuongoza lakini ni lazima tukubali kua kupanda cheo au kushuka cheo ni vitu vya kawaida ktk maisha, ingawaje mimi sijkubaliani na wale wanaoona kua Sitta ameshuhwa cheo.

Kwa wale wanaohimiza Democracy basi hivyo anavyofanya Sitta ndio demecracy haswa na hao wakuu wa democracy ndivyo haswa wanavyofanya. Kwa mfano Gordon Brown Aliekua waziri mkuu wa UK, Na yule alieshindwa na Obama wote walikubali na wanaendelea na shughuli za kawaida. Sasa kama utamuhamasisha kila anaeshindwa au kushushwa cheo afanye vurugu wakati upande mwingine unadai democracy, inaweza ikatia shaka hata kama hiyo democracy yenyewe haswa tunaijua. Ni moja ktk ushujaa kukubali kushindwa na asiekubali kushindwa si mshindani.
 
Ukiwa mchapa kazi utang'ara kwenye kazi yoyote utakayopewa. Mrema, alisha prove hivyo, kwani hata walipompeleka kwenye wizara ambayo ilionekana kama wana mmaliza kisiasa, bado alipata kazi za kufanya na aka nga'ra. Hivyo hivyo Magufuli.

Huenda ni wakati muafaka kwa mheshimiwa Sitta ku prove beyond reasonable doubt kwamba yeye ni mchapa kazi kweli kweli na sio opportunist aliyetumia nafasi ya uspika kujikweza.

Huko EA kuna changamoto nyingi sana ambazo zinaenda na maslahi ya taifa. Atusaidie mikataba ya EA iwe yenye manufaa kwa Tanzania.

mkuu tupo pamoja, niwakati wake sasa kuonyesha ni jinsi gani alivyo bora bila kujalisha anaongoza wizara ipi.
Wengi tunazungumzia anguko la kisiasa,naamini kabisa sita ni mtu makini na amesoma alama za nyakati thats why amesema hataki tena ubunge ujao. Swala ni kwamba anataka sasa kupumzika siasa au analenga urais jambo ambalo ni gumu kwake ukizingatia wabaya wake wengi wako ktk maamuzi ya nani agombee urais.
Lakini ktk siasa anything can happens miaka mitano mingi, nani alitegemea jk ambaye alipendwa 2005 angekuja kuwa hivi.
kutegemea na utendaji wa serikali na mawaziri ,linaweza kujitokeza swala la hitaji la mtu makini na anayekubalika na jamii kugombea urais kupitia ccm ili kukinusuru chama, hapa ndipo 6 anapo pavizia. Na unapotaka walau watu wenye sifa hizo huwezi kumpuuzia 6.
Baada ya kuukosa uspika na kuambulia uwaziri sasa 6 ata act smart kama sumaye
 
Wana JF!

Spika ambaye ni Kiongozi mkuu wa Bunge la Tanzania (mhimili mmoja wapo wa Taifa) kupewa uwaziri wa maswala ya Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi (E.A.C) ambayo twaweza kusema ni idara ndani ya wizara ya Mambo ya Nje si ni sawa kumteua Mzee Mwinyi au Mkapa kuwa mbunge ili awe waziri wa Michezo.
Ama pengine JM-mstaafu Barnabas Samatta ateuliwe kuwa waziri wa Afya!!!!!!!
Je, aliyefanya uteuzi na aliyeteuliwa wanaona mantiki hiyo??? Lengo ni nini kama sio mwendelezo wa sanaa???
Eeee Mola tupe uzima waja wako tufike 2014 na 2015 ili watawala wajue Life is not a rehearsal
 
Kuna mdau alianzisha thread kwamba Sita kakataa hiyo post.
Sijui imefikia wapi?
 
Ile habari iliyoletwa asubuhi hapa jamvini iliishia wapi? au ilikua uzushi? sasa tumwamini yule wa asubuhi au huyu? mmh haya afadhali mmeandika
 
yaani sitta akikubali hii position ntamshangaa sana ..yaani ni dharau iliyopindukia
 
Back
Top Bottom