Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
TUNA IMANI NA MHE. SPIKA, KATIBU WA BUNGE WATUMISHI WA BUNGE
Wafanyakazi wa Ofisi ya Bunge wameeleza kuwa wana imani na Spika wa Bunge, Samuel Sitta, ambaye wamemuelezea kuwa ni mtu makini asiyetetereka katika kutetea hadhi ya Bunge na Taifa kwa ujumla.
Akisoma risala kwa niaba ya watumishi wa ofisi hiyo katika sherehe ya wafanyakazi baada ya kumaliza Mkutano wa 16 wa Bunge, Katibu wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Bunge, Bwana Angumbwike Ngwavi alisema kuwa wamesikitishwa na baadhi ya habari zinazozagaa kuwa eti Mheshimiwa Spika anawagawa watumishi wa Bunge, tunafahamu kuna kundi la watu linalokereka na uhuru wa taasisi ya Bunge unavyokuwa na namna Bunge linavyofanya kazi zake kutokana na sasa Bunge kuwa mstari wa mbele kupambana na uovu uliopo katika jamii yetu. Mtu yeyote anayetetea haki na kupambana na uovu mtu huyo siku zote atakuwa na uadui kutoka kwa wale wanaonufaika na uovu huo alisema Bwana Ngwavi.
Aidha, Bwana Ngwavi alieleleza kuwa mtu mwema kupakwa matope kwa lengo la kumkatisha tamaa siyo kitu cha kushangaza katika ulimwengu huu kwani hata vitabu vitakatifu vinaeleza kuwa Mitume wa Mungu pamoja na mema yote waliyoyatenda bado walipigwa vita na wanadamu. Wengine waliteswa na hata kuuawa.
Wafanyakazi wa Bunge tuna imani na Mheshimiwa Spika na tunapenda kutoa wito kwa Spika kuwa aendelee na ujasiri huo katika vita dhidi ya ufisadi kwani baadaye historia itaonyesha ni nani hasa alikuwa mkweli na mtetezi wa nchi hii na wananchi wake. Kuna mwanafalsa moja aliwahi kusema, kwa lugha ya Kiingereza If want your name to continue living even after your death do something worth writing or write something worth reading Kwatafsiri isiyo rasmi mwanafalsafa huyu anasema ukitaka jina lako liendelee kuwa hai hata baada ya kifo chako fanya jambo linalostahili kuandikwa au andika kitu kinachostahiliki kusomwa ilisema sehemu ya risala hiyo.
Wakizungumzia kuhusu madai kuwa Katibu wa Bunge wa sasa, hana sifa za kushikilia nafasi hiyo, Wafanyakazi hao walisema kuwa wanashangazwa na madai hayo kwa kuwa katibu wa sasa ni mtaalam aliebobea katika masuala ya Bunge na uendeshaji wake, Bahati mbaya wanaoeneza hayo hawajafanya utafiti wa kutosha, kwani kama wangefanya utafiti wa kutosha wangegundua kuwa Dk. Thomas Kashililah ana uzoefu wa masuala ya Bunge kwa zaidi ya miaka ishirini akiwa ameshika nyadhifa mbali mbali ikiwemo Ukurugenzi wa Idara nyeti ya MipangO naTeknolojia ya Mawasiliano, Ofisa wa Bajeti, Katibu Mezani, Katibu wa Kamati za Bunge na Afisa Mfawidhi wa Ofisi Ndogo ya Bunge jijini Dar es salaam ilisema sehemu ya risala hiyo.
Wafanyakazi hao walisema kuwa Dkt. Kashililah ambae ni daktari wa falsafa ana sifa za kutosha na zimepita sifa za msingi anazopaswa kuwa nazo Katibu wa Bunge na wametoa wito kuwa asikatishwe tamaa na maneno hayo ya uzushi bali aendelee kuchapa kazi na kwa kushirikiana na Mhe. Spika aboreshe mazingira ya kazi na vitendea kazi.
Hivi karibuni kumekuwa na juhudi zinazofanywa na watu wasiopenda jitihada zinazofanywa na taasisi nyeti ya Bunge kwa kujaribu kuwachafua viongozi wa juu wa taasisi ya Bunge kupitia magazeti na mitandao ambapo Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Bunge limelaani na kusema kuwa sio sahihi hata kidogo.
Imetumwa na Said Yakubu