Sitosahau yaliyonipata kijijini Kwamsisi

MUENDELEZO SEHEMU YA 2

"Ngo ngo ngo!" Mlango wa nyumba yangu ulikuwa ukigongwa. "Ni nani mwenzangu?" niliuliza. "Ni mimi mzee Kingalu nina shida na wewe mara moja!" Nilitoka na kushangaa kwa nje kulikuwa na mwanga mkali sana wa jua, kumbe ilikuwa ni saa nne asubuhi, nimechelewa kazini isivyo kawaida yangu. Mzee Kingalu alikuwa ameongozana na mwenyekiti wa Kijiji, niliwasalimia huku nikionyesha wasiwasi mkubwa, wala hawakujibu salamu hiyo walinidakisha kwa maneno.

"Kijana wewe ni mwalimu wetu na umeletwa ili uwasaidie watoto wetu kielimu, hatuwezi kuvumilia watu wachache wasio kuwa na nia njema waweze kukukatisha tamaa na kukuharibia maisha yako ya sasa na ya baadaye, tumepata taarifa kuwa ile kinga tuliyokupa imeporwa, je kuna ukweli gani kwenye hili?"

Wamewezaje kufahamu kwamba ile kinga imeporwa ijapokuwa sikuwaambia, niliwaza moyoni. "Ndio!" Nilijibu na nikawaelezea kuhusu ile ndoto niliyoiota usiku wa jana kuamkia siku hii ya leo.

"Ndio swala hilo tunalijua, kuna wazee walikuja kwako usiku huu kwa lengo la kukudhuru sisi tulifanya juhudi kubwa kuwazuia na ndio maana tupo hapa saa hii kwa sababu hatupendi kukukosa," alimalizia mzee Kingalu kisha kuingiza mkono wake kwenye mkoba mweusi aliokuja nao na kutoa kichupa cheusi. Alinipa kichupa cheusi chenye mafuta yaliyochanganywa na mavumba fulani, mafuta hayo yalikuwa ni mafuta ya mbarika na mavumba ni majivu ya mchanganyiko wa vingira fulani vya kichawi. alinishauri niwe napaka utosini kila usiku ninapotaka kulala.

Nilijiandaa haraka na kuelekea shuleni nilipofika wala hakuna mtu yeyote aliyeniuliza kitu chochote ama kushangazwa na kuchelewa kwangu kazini kwa sababu ilikuwa ni jambo la kawaida kwa wafanyakazi kuchelewa, mimi sikutaka kujiingiza kwenye mkumbo huo ni siku hii tu nilichelewa bila hata mwenyewe kutarajia.

Mwalimu mwenzangu wa kike aliyeitwa Siti ndiye pekee aliyenihoji na nilimpa jibu moja tu la mkato kwamba aniache kidogo kwani kichwa changu hakipo sawa kwa wakati ule, nashukuru alinielewa. Alinitia moyo sana binti yule, alikuwa ndiye rafiki yangu kwa wakati ule kwani hata ki umri tulikuwa hatujapishana sana tofauti na walimu wengine waliokuwa ni watu wazima kutuzidi sisi. "Soka wewe ni mtoto wa kiume, hapa kijijini umekuja kikazi japo ninakuonea huruma lakini huna budi kujifunga mkanda."

Nilimsikiliza na kuwaza moyoni, mbona haya maswahibu mwenzangu hayampati? Baadaye nilikuja kugundua kuwa yeye mahali napoishi ni nyumba ya Mganga mkuu wa kienyeji pale kijijini, na alikabidhiwa pale na baba yake mzazi kwahiyo wachawi wengi wa pale kijijini Kwamsisi walikuwa wakiogopa kumfanya chochote.

ITAENDELEA...
Kwamsisi kijiji kina wachawi wengi kuliko wakazi
 
Angalizo, kuna watu wanaquote thread hii wakisema kwamba hadithi hii ni ya uongo na wengine wakisema kwamba ninampango wa kuuza hadithi hii kupitia mtandao wa whatsapp. Naomba puuzeni watu hao kwani hadithi hii ni ya kweli kabisa na wala sio ya kutunga. Atakaye amini niyule mtu anayeamini kwamba uchawi upo ama labda alisha wahi kukutana nao, wale msio amini siwakatazi wala siwazuii kufanya hivyo.
 
SEHEMU YA 3

Mwalimu mkuu alituita kikao kilikuwa ni kikao kizito kujadili ujumbe ulioletwa na mzazi mmoja kwenye karatasi iliyokuwa imefungwa kwenye bahasha ya khaki alionekana kuwa akitetemeka na hakuwa sawa kisaikolojia, mimi nilikuwa ndio kwanza nikisahihisha madaftari huku nikibadilishana maongezi na mwalimu huyu wa kike aliyetokea kuwa karibu sana na mimi nilishtuka kumuona mwalimu mkuu akiwa kwenye hali ile.

"Walimu habari za mchana?" Tulikuwa walimu wanne wote tulitahamaki na hakuna hata mmoja aliye jibu wote tulikaa kimya. Siti akajibu, "nzuri." Sauti yake ikasikika kwa wote nasi tukarudia tena "nzuri." "Inaweza kuwa ni nzuri kwenu au la mmejibu kwa mazowea tu lakini kuna vita kali sana inayoendelea kati yetu haswa kwa nyinyi walimu wageni, inaonekana mmeshindwa kabisa kuheshimu wazee wa kijiji hiki, mzee Sa-Masimba ameleta barua hii amemtuma mwanaye ailete barua hii imenitisha kidogo kuisoma japo sijaielewa lakini ina alama ya damu.

"Alama ya damu?!" wote tulihamaki. "Ndio ni damu ya halisi kabisa ni kidoti kimewekwa juu ya bahasha kikiwa kimechovywa kama na kidole cha mkono, inaonekana kuna mtu anawindwa hapa je ni nani anayewindwa na kwanini?" alihoji mwalimu mkuu.

Barua ilisomeka, "Ndugu mwalimu mkuu hongera kwa kupata wafanyakazi wapya lakini sidhani kama vijana hao uliwafunza juu ya mila za kwetu, kuheshimu wazee na kuto jiingiza kwa namna yoyote na mipango ya kujaribu kupambana na wazee wa kimila, kama hiyo haitoshi kutengeneza wigo na kujiona kuwa huingiliki kwetu sisi tunahesabia kwamba ni dharau. Kama wameshindwa kutuheshimu japo kwa salamu mpaka kufikia hatua ya kupambana na sisi ki chawi hakika hatuta waacha salama." ilimalizika shemu ya barua hiyo.

Nakumbuka siku hiyo tuliwaruhusu wanafunzi mapema sana ilikuwa kama mchana wa saa nane hivi. Mimi nilijua fika ndiyo mlengwa mkuu hivyo niliogopa sana tulitembea mpaka kwenye nyumba ya Mzee Samasimba tulivyo karibia tu tulipiga magoti huku tukitembea kwa magoti mpaka tulipoufikia mlango wa nyumba yake, mwalimu mkuu akiwa ametangulia mbele. Mzee mwenyewe hatuku mkuta basi wakatumwa watoto kwenda kumwita alikuja huku akiwa amevaa msuli wake kiunoni aliambatana na vijana wengine wawili mmoja alimtazama sana Siti kisha akaendelea mpaka wakaingia ndani mzee alisimama pale nje mkewe akamletea kigoda(kiti cha kukalia), akakaa kutusikiliza.

Mwalimu mkuu alikuwa ametangulia mbele aliongea naye kwa lugha ya Kizigua na mwisho aliinama sana huku akimwomba msamaha. Kwakweli nikiri wazi kwamba sikuwahi kushuhudia mchawi akiabudiwa kama siku hiyo, huyu mzee inasemekana alikuwa moja kati ya wazee wenye kauli sana pale kijijini, mambo mengi yalikwama endapo tu yeye asinge shirikishwa na kukubaliana. Ilifika zamu yangu ya kumwomba msamaha kwani tulimwendea kwa zamu, niliinama na kupiga magoti na kusema shikamoo mzee Masimba mimi ni mgeni hapa kijijini naomba unisamehe kama nilikukwaza kwa namna yoyote, sikumpa mkono kama wenzangu walivyofanya niliogopa kuchukuliwa nyota.

Tuliondoka baada ya kupakwa usembe(unga mweupe) usoni na kichwani na wale vijana wake, tulidhalilishwa sana siku hiyo hamna siku nilichukia kazi hii ya ualimu kama siku hiyo tulirudi nyumbani kila mtu akiwa kimya hamsemeshi mwenzake, nilitembea huku nikiwa na mawazo mengi macho yangu yakitazama chini huku machozi yakinilengelenga. "Kwanini binadamu anaabudiwa kama Mungu!" niliwaza moyoni ilikuwa yapata majira ya saa kumi nambili jioni ikikaribia saa moja usiku, nilishtuka kumuona Siti akiwa amenishika bega la kulia kwa nyuma niligeuka na kumtazama.

"Kwahiyo ndio unaenda nyumbani, uende salama ila uwe makini, hapa ndio Kwamsisi uache ubrazameni uheshimu watu." Kumbe ile hali yangu ya kujitengetenga na kutosalimia watu iliwaudhi wengi pia kujiweka karibu na mzee Kingalu ilikuwa ni hatari kwangu niliogopa kuiendea ile njia inayokwenda nyumbani, nilipokumbuka lile jicho alilonikata mzee Masimba nilipogoma kumpa mkono wa msamaha kwa kuwa sikutaka kushikana mkono na mchawi. Basi nikajua kuwa usiku huo lazima atanijilia nyumbani kwangu.

ITAENDELEA...

Sitosahau yaliyonipata kijijini Kwamsisi-4
 
SEHEMU YA 3

Mwalimu mkuu alituita kikao kilikuwa ni kikao kizito kujadili ujumbe ulioletwa na mzazi mmoja kwenye karatasi iliyokuwa imefungwa kwenye bahasha ya khaki alionekana kuwa akitetemeka na hakuwa sawa kisaikolojia, mimi nilikuwa ndio kwanza nikisahihisha madaftari huku nikibadilishana maongezi na mwalimu huyu wa kike aliyetokea kuwa karibu sana na mimi nilishtuka kumuona mwalimu mkuu akiwa kwenye hali ile.

"Walimu habari za mchana?" Tulikuwa walimu wanne wote tulitahamaki na hakuna hata mmoja aliye jibu wote tulikaa kimya. Siti akajibu, "nzuri." Sauti yake ikasikika kwa wote nasi tukarudia tena "nzuri." "Inaweza kuwa ni nzuri kwenu au la mmejibu kwa mazowea tu lakini kuna vita kali sana inayoendelea kati yetu haswa kwa nyinyi walimu wageni, inaonekana mmeshindwa kabisa kuheshimu wazee wa kijiji hiki, mzee Sa-Masimba ameleta barua hii amemtuma mwanaye ailete barua hii imenitisha kidogo kuisoma japo sijaielewa lakini ina alama ya damu.

"Alama ya damu?!" wote tulihamaki. "Ndio ni damu ya halisi kabisa ni kidoti kimewekwa juu ya bahasha kikiwa kimechovywa kama na kidole cha mkono, inaonekana kuna mtu anawindwa hapa je ni nani anayewindwa na kwanini?" alihoji mwalimu mkuu.

Barua ilisomeka, "Ndugu mwalimu mkuu hongera kwa kupata wafanyakazi wapya lakini sidhani kama vijana hao uliwafunza juu ya mila za kwetu, kuheshimu wazee na kuto jiingiza kwa namna yoyote na mipango ya kujaribu kupambana na wazee wa kimila, kama hiyo haitoshi kutengeneza wigo na kujiona kuwa huingiliki kwetu sisi tunahesabia kwamba ni dharau. Kama wameshindwa kutuheshimu japo kwa salamu mpaka kufikia hatua ya kupambana na sisi ki chwawi hakika hatuta waacha salama." ilimalizika shemu ya barua hiyo.

Nakumbuka siku hiyo tuliwaruhusu wanafunzi mapema sana ilikuwa kama mchana wa saa nane hivi. Mimi nilijua fika ndiyo mlengwa mkuu hivyo niliogopa sana tulitembea mpaka kwenye nyumba ya Mzee Samasimba tulivyo karibia tu tulipiga magoti huku tukitembea kwa magoti mpaka tulipoufikia mlango wa nyumba yake, mwalimu mkuu akiwa ametangulia mbele. Mzee mwenyewe hatuku mkuta basi wakatumwa watoto kwenda kumwita alikuja huku akiwa amevaa msuli wake kiunoni aliambatana na vijana wengine wawili mmoja alimtazama sana Siti kisha akaendelea mpaka wakaingia ndani mzee alisimama pale nje mkewe akamletea kigoda(kiti cha kukalia), akakaa kutusikiliza.

Mwalimu mkuu alikuwa ametangulia mbele aliongea naye kwa lugha ya Kizigua na mwisho aliinama sana huku akimwomba msamaha. Kwakweli nikiri wazi kwamba sikuwahi kushuhudia mchawi akiabudiwa kama siku hiyo, huyu mzee inasemekana alikuwa moja kati ya wazee wenye kauli sana pale kijijini, mambo mengi yalikwama endapo tu yeye asinge shirikishwa na kukubaliana. Ilifika zamu yangu ya kumwomba msamaha kwani tulimwendea kwa zamu, niliinama na kupiga magoti na kusema shikamoo mzee Masimba mimi ni mgeni hapa kijijini naomba unisamehe kama nilikukwaza kwa namna yoyote, sikumpa mkono kama wenzangu walivyofanya niliogopa kuchukuliwa nyota.

Tuliondoka baada ya kupakwa usembe(unga mweupe) usoni na kichwani na wale vijana wake, tulidhalilishwa sana siku hiyo hamna siku nilichukia kazi hii ya ualimu kama siku hiyo tulirudi nyumbani kila mtu akiwa kimya hamsemeshi mwenzake, nilitembea huku nikiwa na mawazo mengi macho yangu yakitazama chini huku machozi yakinilengelenga. "Kwanini binadamu anaabudiwa kama Mungu!" niliwaza moyoni ilikuwa yapata majira ya saa kumi nambili jioni ikikaribia saa moja usiku, nilishtuka kumuona Siti akiwa amenishika bega la kulia kwa nyuma niligeuka na kumtazama.

"Kwahiyo ndio unaenda nyumbani, uende salama ila uwe makini, hapa ndio Kwamsisi uache ubrazameni uheshimu watu." Kumbe ile hali yangu ya kujitengetenga na kutosalimia watu iliwaudhi wengi pia kujiweka karibu na mzee Kingalu ilikuwa ni hatari kwangu niliogopa kuiendea ile njia inayokwenda nyumbani, nilipokumbuka lile jicho alilonikata mzee Masimba nilipogoma kumpa mkono wa msamaha kwa kuwa sikutaka kushikana mkono na mchawi. Basi nikajua kuwa usiku huo lazima atanijilia nyumbani kwangu.

ITAENDELEA...

Pole sana mkuu,

Hakika tunayopitia ni mengi.
 
Back
Top Bottom