hahahaha kwa TZ hii ni ndoto aisee
Mh! Mbona kwa mlolongo huo wa sheria, kuna hatua nyingi sana kufikia hatua ya vote of no confidence. By the way, this can be just the begining, there might be many more to come, let us see what will happen on this Jairo's saga.
Mkuu nchi gani hiyo unayoongelea? Kama ni Tanzania, basi hizi zitabaki tu kuwa ni day dreams. Hakuna kitu kama hicho kwa nchi na wananchi mazuzu kama watanzania.Kwa mujibu wa mtazamo wangu wa hali ya siasa na bunge katika bunge hili la kumi, nadiriki kusema kwamba sitashangaa sana kama kabla ya mwaka 2015 bunge likaomba kupiga kura ya kutokuwa na imani na serikali hii.
Serikali watch your back you are running solo and soon you will meet an hungry Lion, believe me it wont leave you
<br />TF uko kama mimi hii kitu siamini na haitotokea <br />
Ngoja niweke hapa kifungu cha katiba uone mlolongo ilivyo mrefu na ambao magamba hawatakubali hata tone <br />
<br />
<br />
46A]46A. Bunge laweza kumshtaki Rais Sheria Na. 20 ya 1992 ib. 8; 12 ya 1995 ib. 4<br />
(1) Bila ya kujali masharti ya ibara ya 46 ya Katiba hii, Bunge linaweza kupitisha azimio la kumuondoa Rais madarakani endapo itatolewa hoja ya kumshtaki Rais na ikapitishwa kwa mujibu wa masharti ya ibara hii.<br />
(2) Bila ya kuathiri masharti mengineyo ya ibara hii, hoja yoyote ya kumshtaki Rais haitatolewa isipokuwa tu kama inadaiwa kwamba Raisâ<br />
(a) ametenda vitendo ambavyo kwa jumla vinaivunja Katiba au sheria ya maadili ya Viongozi wa Umma;<br />
(b) ametenda vitendo ambavyo vinakiuka maadili yanayohusu uandikishwaji wa vyama vya siasa yaliyotajwa katika ibara ya 20(2) ya Katiba; au<br />
(c) amekuwa na mwenendo unaodhalilisha kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano, na haitatolewa hoja ya namna hiyo ndani ya miezi kumi na miwili tangu hoja kama hiyo ilipotolewa na ikakataliwa na Bunge.<br />
(3) Bunge halitapitisha hoja ya kumshtaki Rais isipokuwa tu kamaâ<br />
(a) taarifa ya maandishi, iliyotiwa sahihi na kuungwa mkono na Wabunge wasiopungua asilimia ishirini ya Wabunge wote itawasilishwa kwa Spika siku thelathini kabla ya kikao ambapo hoja hiyo inakusudiwa kutolewa Bungeni, ikifafanua makosa aliyoyatenda Rais, na ikipendekeza kuwa Kamati Maalum ya Uchunguzi iundwe ili ichunguze mashtaka yaliyowasilishwa dhidi ya Rais;<br />
(b) wakati wowote baada ya Spika kupokea taarifa iliyotiwa sahihi na Wabunge na kujiridhisha kuwa masharti ya Katiba kwa ajili ya kuleta hoja yametimizwa, Spika atamruhusu mtoa hoja kuiwasilisha hoja hiyo, na kisha Spika atalitaka Bunge, bila ya kufanya majadiliano, lipige kura juu ya hoja ya kuunda Kamati Maalum ya Uchunguzi na kama ikiungwa mkono na Wabunge wasiopungua theluthi mbili ya Wabunge wote, atatangaza majina ya wajumbe wa Kamati Maalum ya Uchunguzi.<br />
(4) Kamati Maalum ya Uchunguzi, kwa madhumuni ya ibara hii, itakuwa na wajumbe wafuatao, yaaniâ<br />
(a) Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano, ambaye atakuwa ndiye Mwenyekiti wa Kamati;<br />
(b) Jaji Mkuu wa Tanzania Zanzibar; na<br />
(c) Wabunge saba walioteuliwa na Spika kwa mujibu wa Kanuni za Bunge na kwa kuzingatia uwiano wa uwakilishi baina ya vyama vya siasa vinavyowakilishwa Bungeni.<br />
(5) Endapo Bunge litapitisha hoja ya kuunda Kamati Maalum ya Uchunguzi, Rais atahesabiwa kuwa hayupo kazini, kisha kazi na madaraka ya Rais yatatekelezwa kwa mujibu wa masharti ya ibara 37(3) ya Katiba hii hadi Spika atakapomfahamisha Rais juu ya azimio la Bunge kuhusiana na mashtaka yaliyotolewa dhidi yake.<br />
(6) Ndani ya siku saba baada ya Kamati Maalum ya Uchunguzi kuundwa, itakaa, ichunguze na kuchambua mashtaka dhidi ya Rais, pamoja na kumpatia Rais fursa ya kujieleza, kwa kufuata utaratibu uliowekwa na Kanuni za Bunge.<br />
(7) Mapema iwezekanavyo, na kwa vyovyote vile katika muda usiozidi siku tisini, Kamati Maalum ya Uchunguzi itatoa taarifa yake kwa Spika.<br />
(8) Baada ya Spika kupokea taarifa ya Kamati Maalum ya Uchunguzi, taarifa hiyo itawasilishwa Bungeni kwa kufuata utaratibu uliowekwa na Kanuni za Bunge.<br />
(9) Baada ya taarifa ya Kamati Maalum ya Uchunguzi kuwasilishwa kwa mujibu wa ibara ndogo ya (8), Bunge litaijadili taarifa hiyo na litampa Rais fursa ya kujieleza, na kisha, kwa kura za Wabunge wasiopungua theluthi mbili ya Wabunge wote, Bunge litapitisha azimio ama kuwa mashtaka dhidi ya Rais yamethibitika, na kwamba hastahili kuendelea kushika kiti cha Rais, au kuwa mashtaka hayo hayakuthibitika.<br />
(10) Endapo Bunge litapitisha azimio kuwa mashtaka dhidi ya Rais yamethibitika na kwamba hastahili kuendelea kushika kiti cha Rais, Spika atawafahamisha Rais na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi juu ya azimio la Bunge, na hapo Rais atawajibika kujiuzulu kabla ya kuisha kwa siku ya tatu tangu Bunge lilipopitisha azimio hilo.<br />
(11) Endapo Rais ataacha kushika kiti cha Rais kutokana na mashtaka dhidi yake kuthibitika, hatakuwa na haki ya kupata malipo yoyote ya pensheni wala kupata haki au nafuu nyinginezo alizo nazo kwa mujibu wa Katiba au Sheria yoyote iliyotungwa na Bunge.
<br />
<br />
Rocky imenibidi kucheka tu maana kwa katiba hii na kwa staili hii watu wataendelea kupeta kama kawa huku sisi tunapiga kelele za vijiweni
<br />Mkuu huo mlolongo waliouweka ni balaa na wanajua kabisa kule bungeni majority ni nani na je kuna mwanamagamba atakayeunga mkono hoja hata mmoja <br />
Na je akiunga mokono maisha yake na siasa si ndio itakuwa mwisho <br />
Vipi kuhusu biashara zake na mali zake na usalama wake yeye mwenyewe <br />
Kwani hajipendi
<br />Kwa maoni yangu inawezekana. Wabunge wa ccm wasipofanya hivyo, watapoteza majimbo yao kwa 90% come next election.
<br />
<br />
Mkuu hapo ni ukweli maana wao huwa wanawaza maslahi binafsi nafikiri cha msingi uchaguzi ujao ni kupunguza idadi ya wabunge wa CCM bungeni
<br />tunahitaji kama kweli tungependa tuwe na maamuzi magumu na uwajibikaji kw aviongozi na watendaji mbalimballi ni kuwa na wabunge wengi wa upinzani bungeni<br />
Viongozi wakuu kuanzia waziri mkuu na wakurugenzi wote na majaji wote wathibitishwe na bunge ambalo pia litakuwa na uwezo wa kumtimua atakapoboronga<br />
Tuache huu mtindo wa waziri ni mbunge hapo hapo hauna tija na wathibitishwe na bunge pia hata wakiteuliwa na rais <br />
na madaraka ya rais yapunguzwe sana asiwe kama mfalme kweney nchi ambako tunajiita tuna democrasia
Kwa mujibu wa mtazamo wangu wa hali ya siasa na bunge katika bunge hili la kumi, nadiriki kusema kwamba sitashangaa sana kama kabla ya mwaka 2015 bunge likaomba kupiga kura ya kutokuwa na imani na serikali hii.
Serikali watch your back you are running solo and soon you will meet an hungry Lion, believe me it wont leave you
Kwa maoni yangu inawezekana. Wabunge wa ccm wasipofanya hivyo, watapoteza majimbo yao kwa 90% come next election.
<br />
<br />
Tatizo jingine Rocky ni asilimia chache ya Watanzania wanaoijua katiba ya nchi hii nalo pia ni tatizo
<br />
<br />
Mkuu hapo ni ukweli maana wao huwa wanawaza maslahi binafsi nafikiri cha msingi uchaguzi ujao ni kupunguza idadi ya wabunge wa CCM bungeni
Mr.Rocky ebu tucheki tuone hizi sindimba za wana-ccm,yani wanatia kinyaa na wametufika kooni kwakweli
shida ingine ni wanataaluma walioshika izo nyadhifa serikali yani wamelewa pesa na wote washenzy tu