Kumbe maamuzi hayatoki kwa wananchi, we need Bottom-up decision approach and not Top-down approach.Wadau huo ni utaratibu wa Chama, maamuzi yatatoka juu. Tuache kufanya utabiri usiokuwa na tija na kuanza kukashifu watu kwa maisha binafsi.
Mkuu Gracious umesema maneno mazito na haswa hiyo para ya mwisho!.Tatizo kubwa la CCM ni Rushwa ambayo imekita mizizi,Ufisadi ni kitu cha kawaida CCM.Usishangae hata hao wanaolalamika kwamba sioi kachaguliwa kwa rushwa nao wametoa rushwa isipokua sioi kawazidi dau.Ni vigumu kuitenganisha CCM na rushwa.Hii equation ina hold sana kwa CCM; Corruption=CCM.Tatizo kubwa pia no one is clean there.Lowassa kamsaidia mkwewe Sioi,kampa hela kutoa mlungura.Lowassa mwenyewe ndo the Master Corrupt King No 1 in Tanzania.
Hii sinema itaishia pagumu,kwa sababu katika ulingo wa kawaida i mean fair play sasa CCM wameshaishiwa nguvu.Kazi kubwa atapewa Lubuva (Mzee wa NEC) Huyu Lubuva ni shemeji wa Lowasa.So mnaweza kupata picha hapo jinsi mbinu chafu zitakavyotumika.
CDM Wanatakiwa kuwa makini.Linda kura,Piga kampeni wakiwa werevu kama NYOKA na wapole kama NJIWA lakini wakiwa na hekima kama mfalme SULEIMAN.Pamoja Tutashinda,divided we fall.
Angalau hapa umetoa a balanced statement sijui labda kwa sababu inamhusu EL au vipi, ila sikubaliani na wewe kuwa kumpitisha Sioi ni kulinusuru jimbo maana sioni safari hii CCM watatokea wapi.Mkuu Gracious umesema maneno mazito na haswa hiyo para ya mwisho!.
Rushwa ndio utaratibu rasmi wa kupata uongozi ndani ya CCM, this is order of the day!. Wagombea wote walikata kitu kidogo, ila mwenye kisu kikali, ndie aliyekula nyama!. Hata hivyo vikao vya maamuzi vitawajibika kumpitisha Sioi ili kulinusuru hilo jimbo!.
Siwajui sana Wameru kama ni watu wa msimamo, matokeo ya sanduku la kura ndio yatatupa picha halisi ya Wameru. Uchaguzi huu pia ndio kipimo cha kwa cha kupima upepo Jee EL anakubalika?. CCM ikishinda Arumeru, means 2015 ni EL Magogoni!. Chadema ikishinda Arumeru, hiyo itakuwa ndio kitchen Party ya CCM kujiandaa kwa send-off ya kuelekea kuwa Chama kikuu cha ipinzani, kwani ndio ufunguo wa Chadema kuingilia Magogoni!.
mamvi ananguvu ya pesa hvy sioi lazma awaoe wote wanaompinga sasa
Magwanda wanapotafuta pakutokea huwa ni raha sana.
Pole sana Zomba. Kama ukofit kichwani utakuwa unaujua ukweliMagwanda wanapotafuta pakutokea huwa ni raha sana.
MVUTANO mkali unadaiwa kuibuka katika kikao cha Kamati ya Siasa ya CCM mkoani Arusha baada ya baadhi ya wajumbe kupinga uongozi wa chama hicho Wilaya ya Arumeru, kumpitisha Sioi Sumari kugombea Ubunge Jimbo la Arumeru Mashariki.
Chanzo cha habari ndani ya kikao hicho kilichoanza saa 5:00 asubuhi hadi saa moja usiku juzi, zinadai kuwa kitendo cha kupitishwa kwa jina la Sumari ambaye ni mtoto wa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo marehemu Jeremiah Sumari, kimeibua malumbano makali ndani ya chama hicho.
Habari hizo zimeeleza kuwa wajumbe wawili waliokuwa katika kikao hicho ambao ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo na Katibu wa CCM mkoani Arusha Mary Chatanda, walipinga kupitishwa jina la Sumari, kwa sababu ushindi wake umelalamikiwa kila kona.
Taarifa zimedai kuwa kitendo cha Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Mahusiano na Uratibu, Stephen Wassira kuhudhuria kikao hicho kama msikilizaji, kimezua utata baada ya baadhi ya wajumbe kuhoji ugeni wake ndani ya kikao hicho cha maamuzi ya chama.
Baadhi ya wajumbe waliokuwa wakipinga kupitishwa jina la Sumari, wametaja sababu iliyowafanya kutopitisha jina hilo kwa kutoa hoja kwamba ushindi wake umegubikwa na malalamiko mengi, hususan madai ya rushwa.
Mkuu wa Mkoa pamoja na Chatanda ndio walikuwa wakipinga kupitishwa kwa jina la Sioi kulikuwa na mvutano mkali sana, lakini hadi dakika ya mwisho kikao kilipitisha majina ya watu wawili ambao ni Sioi na Sarakikya, kilisema chanzo chetu.
Hata hivyo, mvutano huo unasemekana kukiweka CCM katika wakati mgumu katika harakati za kutetea jimbo la Arumeru Mashariki ambapo kwa sasa makundi mawili, yameonekana kuvutana rasmi ambapo moja linaunga mkono jina la Sioi kupitishwa huku lingine likipinga.
Baadhi ya wanachama wa CCM mkoani Arusha wamekosoa utaratibu uliotumika kupitisha majina mawili (Sumari na William Sarakikya) ambayo yatapelekwa katika ngazi za juu kwa uamuzi wa mwisho wakisisitiza kwamba lililopaswa kupitishwa jina moja.
Wanachama hao bila kutaja majina yao, wamepinga vilevile kitendo cha Wassira kuhudhuria kikao hicho kama msikilizaji huku wakisema, kiongozi huyo hakustahili kuhudhuria kikao hicho kama msikilizaji kwa vile kilikuwa kikao cha maamuzi.