Sintosahau: Siku mwandishi wa habari alipotushawishi tulie mbele ya kamera ili habari yetu na yake ipate uzito, wanawake waliweza, wanaume tulishindwa

chiembe

JF-Expert Member
May 16, 2015
12,505
21,563
Katika taaluma ambayo ina " wasanii" wengi ni taaluma ya habari, kulikuwa na tukio moja la kubomoa nyumba katika eneo letu, jamaa mmoja mjanja mjanja akasema ana namba ya mwandishi wa habari, akampigia akaja fasta.

Baada ya kufika akadai tumpe za kwake kwanza, na pili, ili habari iwe ya kwanza au ya pili, lazima tufanye mpango mhariri wa makao makuu, aonwe, tukampa.

Baada ya hapo alitoa ushauri ulioacha kizaa zaa na fadhaa, akasema kila mtu akusanye hisia aanze kulia kwa sauti kuu kama mjita au mkerewe au mnyakyusa amefiwa.

Kwa wanaume ikawa changamoto, watu walikuwa wanakamua macho chozi litoke, wapi, sauti za kulia zinagoma, zinatoka kama za spika iliyopasuka, wengi wakaishia kudondosha kope tu kwa kukaza macho.

Kwa wanawake ilichukua sekunde, zilifyatuka sauti kama mtu kaumwa na nyoka. Habari ikaenda.

Nchi hii usanii mwingi sana, baada ya hapo mwandishi akawapongeza walioloa kwa sauti kubwa, akasema lazima kesho watapata majibu.
 
Nakumbuka tulipokuwa secondary kipindi kile kuna changamoto ya usafiri kwa wanafunzi kuna siku jioni tupo stendi akaja mwandishi wa habari ITV (jiji letu) alituambia likija gari twende wengi kugombania ili yeye achukue video
 
Katika taaluma ambayo ina " wasanii" wengi ni taaluma ya habari, kulikuwa na tukio moja la kubomoa nyumba katika eneo letu, jamaa mmoja mjanja mjanja akasema ana namba ya mwandishi wa habari, akampigia akaja fasta.

Baada ya kufika akadai tumpe za kwake kwanza, na pili, ili habari iwe ya kwanza au ya pili, lazima tufanye mpango mhariri wa makao makuu, aonwe, tukampa.

Baada ya hapo alitoa ushauri ulioacha kizaa zaa na fadhaa, akasema kila mtu akusanye hisia aanze kulia kwa sauti kuu kama mjita au mkerewe au mnyakyusa amefiwa.

Kwa wanaume ikawa changamoto, watu walikuwa wanakamua macho chozi litoke, wapi, sauti za kulia zinagoma, zinatoka kama za spika iliyopasuka, wengi wakaishia kudondosha kope tu kwa kukaza macho.

Kwa wanawake ilichukua sekunde, zilifyatuka sauti kama mtu kaumwa na nyoka. Habari ikaenda.

Nchi hii usanii mwingi sana, baada ya hapo mwandishi akawapongeza walioloa kwa sauti kubwa, akasema lazima kesho watapata majibu.
No wonder uchawa (professional unafki) unataka kuwa normalized ili mtu apate hela. Professionalism kwenye kazi ina kufa kwa speed ya ajabu
 
Sikuwepo hila ninaamini hitakuwa mhandishi halikuwa wa Manara TV maana ndo chanel pekee hiliyo kaa kiccm zaidi
 
Katika taaluma ambayo ina " wasanii" wengi ni taaluma ya habari, kulikuwa na tukio moja la kubomoa nyumba katika eneo letu, jamaa mmoja mjanja mjanja akasema ana namba ya mwandishi wa habari, akampigia akaja fasta.

Baada ya kufika akadai tumpe za kwake kwanza, na pili, ili habari iwe ya kwanza au ya pili, lazima tufanye mpango mhariri wa makao makuu, aonwe, tukampa.

Baada ya hapo alitoa ushauri ulioacha kizaa zaa na fadhaa, akasema kila mtu akusanye hisia aanze kulia kwa sauti kuu kama mjita au mkerewe au mnyakyusa amefiwa.

Kwa wanaume ikawa changamoto, watu walikuwa wanakamua macho chozi litoke, wapi, sauti za kulia zinagoma, zinatoka kama za spika iliyopasuka, wengi wakaishia kudondosha kope tu kwa kukaza macho.

Kwa wanawake ilichukua sekunde, zilifyatuka sauti kama mtu kaumwa na nyoka. Habari ikaenda.

Nchi hii usanii mwingi sana, baada ya hapo mwandishi akawapongeza walioloa kwa sauti kubwa, akasema lazima kesho watapata majibu.
Mlikosa vitunguu au pilipili?
 
Back
Top Bottom