Janie_Kelvin
Member
- Jun 5, 2022
- 33
- 51
Ni simulizi inayohusu familia, mapenzi, kazi na safari ya maisha kwa ujumla.
Ungana na mimi katika simulizi hii…..
SEHEMU YA KWANZA
TANZANIA
1995
“Pushhhhhh!!!!!”
“Mrs Hernad jitahidi sukuma mtoto yupo karibu kutoka jitahidi yaani bado kidogo tu.. sukuma!!!”
“Nurse I can’t.. do it anymore… Siwezi nahisi nguvu zinaniishia kabisa “
“Hapana Mrs jitahidi unajua bado…..”kabla hajamalizia hali ya Mrs Hernad ilibadilika ghafla
“Nesi nashindwa…. Aaaaah siwezi..siwe…aaah msaidie mwanangu tafadhali msaid…. Mwana…….”Ghafla akakata moto.Ilikuwa ni taharuki ndani ya chumba hiko cha kina mama kinachojulikana kama labour ward.
Huku nje alionekana mwanaume akiwa amesimama huku kama amevurugwa hata kiti hakikaliki ni kama mwendawazimu alienda mbele na kurudi nyuma akikuna kichwa chake, tai yake ilining’inia shingoni haikueleweka ni staili gani aliifunga kifupi tu alikuwa rafu sana kama mtu aliyechanganyikiwa na pembeni yake aliketi mama ambaye umri wake umeenda yaani ni mtu mzima tayari naye japo alikaa lakini hakuonekana kutulia.Ghafla aliona kitanda cha wagonjwa kikitoka ndani ya labour ward na aliyekuwa akiburuzwa ni mke wake Mrs Hernad ambaye alikuwa akihema kwa mbali tena kwa shida sana, kwa haraka alimfuata daktari mmoja ili aongee nae na daktari huyo alimpa taarifa kuwa haikuwa rahisi kwa mke kujifungua kwa njia ya kawaida hivyo alitakiwa kufanyiwa upasuaji ili mtoto aokolewe kingine alimtoa wasiwasi kuwa wote wawili yaani mama na mtoto wangekuwa salama.Baada ya kusema hayo daktari alimuacha hapo Mr Hernad na kuelekea chumba cha upasuaji naye Mr Hernad alipiga magoti na kusali huku akilitaja jina la Sumaya alimgeukia mama yule ambaye ni mama yake huku naye akimtuliza ili asiwe na papara.Ni katika hospitali ya Aga Khan jijini Dar es salaam pirika pirika za kila siku katika hospitali hiyo kubwa ziliendelea kama kawaida kwani hakukuwa na muda wa kula bata ukiwa hospitalini hapo hakuna daktari wala nesi aliyoenekana kuzembea kwa muda huo.
Huku chumba cha upasuaji kilichojulikana kama thieta, madaktari walizidi kushauriana huku kila daktari akionekana kutoa mchango wake.Huku Mrs Hernad akifanyiwa matayarisho kwaajili ya operation.
“Ni sahihi lakini hii ni win to loose situation, ni lazima tukubali matokeo yatakayo tokea na pia tusikubali kupoteza vyote hapa kuna uwezekano mdogo sana wa kumuokoa mama ni kama asilimia ishirini tu za makadirio ila kuna uwezekano mkubwa wa kumuokoa mtoto ni kama asilimia tisini.So let’s do it”Wote walikubaliana na mawazo ya Dokta Luis ambaye ndiye aliyekuwa akizungumza na Mr Hernad wakati wakitoka labour ward ni daktari bingwa wa mambo yote yanayohusiana na uzazi na saikolojia hakuwa mzembe hata kidogo. Kwa haraka Mrs Hernad alifanyiwa upasuaji ili kuweza kumuokoa mtoto kwa sababu uwezekano wa mama kupona haukuwepo.
Shughuli ilikuwa pevu siku hiyo ni karibia saa nne zilitumika kwenye zoezi hilo, ndipo daktari mmoja mmoja alionekana kutoka ndani ya thieta lakini hakuna aliyethubutu kuzungumza na Mr Hernad kazi hiyo ilikuwa chini ya Dokta Luis, hivyo Dokta Luis alimfuata Mr Hernad na kuongozana mpaka ofisini kwake.Waliketi huku Dokta Luis hakuonesha wasiwasi lakini alionesha sura ya furaha hali iliyompa matumaini Mr Hernad.
“Well… Mr Hernad my super hero hongera sana Mungu amekujalia hatimaye umempata Princess wa Kasri lako, tena mrembo haswa kama mama yake”Alizidi kuonesha sura ya furaha
“Dokta Sijui niseme nini nina furaha sana hatimaye ndoto yangu ya kuitwa baba imetimia.. am… vipi kuhusu Sumaya wangu Dokta anaendeleaje? Naweza kwenda kumuona?”
“Ooh worry out Mr Hernad, unajua ni kipindi kirefu sana umehangaika juu ya jambo hili la kupata mtoto na leo ndoto zako zimetimia amini kuwa Sumaya alikuja kwako kama malaika mkombozi, kukutoa kwenye huzuni uliyokuwa nayo kwa muda mrefu sana lakini ni furaha iliyoleta huzuni pia”
“Ni kweli Dokta sijui nimpe nini kama zawadi yangu kwake Sumaya wangu, Mungu ni mkubwa sana”
“And you know Mr Hernad wanaume siku zote tumeumbiwa moyo wa ujasiri sana tofauti na wenzetu kina mama japo nao ni majasiri sana kwa upande mwingine, am… Mr Hernad I’m very very sorry ilikuwa ni vigumu mkeo kujifungua kwa njia ya kawaida licha ya hayo alipoteza damu nyingi sana lakini ni jambo ambalo hatukuweza kuforce kwani tungewapoteza wote wawili, ukweli mkeo hatupo naye tena Mr Hernad”
Lilikuwa ni pigo kubwa sana kwa Mr Hernad alikuwa kama mtu aliyemwagiwa maji ya baridi kwenye baridi kali alisimama ghafla kuanza kupiga mikono yake kwenye ukuta kama mwendawazimu naye Dokta Luis kama mtaalamu alimfuata na kuanza kumtuliza ili angalau hasira zake zishuke ili waangalie utaratibu unaofuata.Jambo hilo lilimchanganya sana kwani hakulitegemea kwa wakati huo, licha ya hayo Sumaya alikuwa ni binti mdogo kabisa wa miaka ishirini na mitano tu.
Wakati akitoka katika ofisi ya Dokta Luis ndipo alipomuona mwanadada ambaye alijitanda vizuri mtandio wake kama kujisitiri akija upande wake alimtambua vyema kabisa mwanadada huyo ndipo walisalimiana kisha yule dada alianza kuuliza maswali Mr Hernad mfululizo kutokana na wasiwasi kwa hali aliyoiona kwa Mr Hernad.
“Shemeji kuna nini? Dada ameshajifungua? Vipi mtoto na dada wanaendeleaje? Aah samahani nimechelewa kuja na chakula shemeji nilishindwa kuja mapema kwasababu ya mitihani”
“Aah Usijali Zuleya… hata hivyo chakula hakina umuhimu kwa sasa”
“Kwanini au mmeshamnunulia chakula? Shemeji ongea na mimi”
“Zuleya dada yako hatupo naye tena Zuleya ila mtoto yupo salama kabisa” Aliongea Mr Hernad kwa huzuni na kumfanya Zuleya aangushe kapu ambalo alihifadhia chakula kwaajili ya dada yake ambaye kwa sasa ni marehemu.
“Aaaahhhhhhhhhhh!!!!!!!!”Alipiga ukunga wa maumivu Zuleya kwani ni kama amechomwa na msumari wa moto kwenye moyo wake katika familia yao walibahatika kuzaliwa wawili tu yeye na dada yake ambaye waliishi maisha magumu sana baada ya kufariki wazazi wao kwa mtego kwani ajali ya gari waliyopata haikuwa ya kawaida na ndugu kuwanyang’anya mali zote za wazazi wao na kuwatenga na Sumaya ndiye alikuwa mlezi mkuu wa Zuleya angalau hata mjomba wao alikuwa upande wao kuwasomesha japo hakuwa na kipato kikubwa naye hakuchukua muda alifariki kutokana na maradhi tofauti yaliyomsumbua ndipo Sumaya aliacha chuo akiwa anakaribia kuingia Mwaka wa tatu na kuanza kumuhangaikia mdogo kwake ili asome ndipo alipoonana na Mr Hernad na kufunga ndoa ya serikali, na hapo Mr Hernad alimalizia kumsomesha Sumaya mwaka mmoja uliobaki na kumsomesha Zuleya huku akiwanunulia nyumba nzuri ya kuishi na kumuajiri msaidizi wa kazi ambayo aliishi Zuleya na ndipo maisha yao yalipobadilika na kuwa mazuri tofauti na mwanzo.
Zuleya alimtizama shemeji yake huku uso wake ukiwa umeiva na kuwa mwekundu kutokana na kilio. Machozi tayari yalishalowanisha sehemu kubwa ya mwili wake.
Kwakuwa Sumaya alikuwa ni muislamu hivyo kama ulivyo taratibu zao maandalizi ya mazishi yalianza kufanyika mapema sana na siku iliyofuata Sumaya alizikwa, ilikuwa ni huzuni kubwa sana ni kama kitoto kichanga kilikuwa kinaelewa nini kimetokea kililia mfulilizo huku kikionesha huzuni ulikuwa ni wakati mgumu sana kwa Mr Hernad na wasaidizi wa kazi kumtuliza mtoto huyo ambaye Mr Hernad aliamua kukuaita Sumaya kwani kalifanana sana na mama yake kwa kila kitu hata watu wa nyumbani hapo walishangaa sana jambo hilo.
Mr Gedione Hernad alikuwa ni mfanyabiaahara mkubwa sana ndani na nje ya nchi, masomo yake alisomea nchini Australia katika chuo cha mambo ya siasa Deakin University pia alisoma vilevile masuala ya masoko (marketing) na huko ndipo alipokutana na Dokta Luis ambaye alikuwa akisoma chuo cha udaktari La Trobe University, wawili hao walikutana katika mashindano ya vyuo vikuu nchini Australia katika mambo mbalimbali ya elimu, vipaji na michezo tofauti ndipo walipoonana na kujenga urafiki wao wa kudumu japo Mr Hernad alimzidi Dokta Luis kwa miaka na elimu kwani Dokta Luis muda huo ndio alikuwa akianza masomo yake nchini Australia.Vilevile alikuwa ni kiongozi mwenye madaraka serikalini naam alikuwa ni Waziri wa mambo ya nje lakini kabla ya kushika wadhifa huo alipitia nafasi mbalimbali za uongozi na mwisho kuwa Waziri wa mambo ya nje.Pia alimuoa mwanamke na kuishi naye.Hakuna ambaye alikuwa hamfahamu Mr Hernad kwa sifa zake upendo ustaarabu na moyo wa huruma na kutoa lakini miaka mitano ya ndoa yake mke wake alifariki bila kuwa na mtoto, aliishi maisha hayo kwa miaka karibia mitatu alipata mwanamke mwingine na kumuoa naye alikuwa na matatizo ya uzazi hivyo hawakubahatika kupata mtoto katika miaka mitatu ya ndoa yao. Suala la mtoto lilimsumbua sana akili Mr Hernad huku familia yake ikihangaika huku na huko kumuombea Mr Hernad japo apate mtoto na ndipo mke wake alipomruhusu atatute mwanamke ambaye angeweza kumpa watoto kuliko kuendelea kusononeka jambo hilo hata familia yake ililiafiki na ndipo alipokutana na Sumaya na kufunga nae ndoa ya serikali kwa wakati huo Mr Hernad alishafikia umri wa miaka arobaini huku mwaka mmoja kupita kwenye ndoa yao alipata ujauzito, ni kama neema iliingia katika familia ya Mr Hernad naye hakuruhusu mke wake huyo Kufanya chochote hata kujikuna yaani alikuwa akimlea kama yai Sumaya aliishi kama malikia huku daktari wake alikuwa alimfuata nyumbani kwa vipimo vyote na mazoezi alifanyia hapo hapo nyumbani kwani kulikuwa na kila kitu.Mapenzi ya Mr Hernad kwa Sumaya yaliongezeka mara dufu mpaka alifunga CCTV Camera chumbani kwake ili muda wote amuone mke wake kipenzi.
Hayo Ndio maisha ya Mr Hernad aliyepitia changamoto kadhaa kwenye maisha yake licha ya kuwa na pesa za kutosha na kugundua kuwa pesa haiwezi kununua furaha katika maisha bali furaha unaipata kutoka kwa watu wa karibu na kutoka kwako mwenyewe na aina ya maisha unayoishi uwe na masikini au tajiri unaweza kutengeneza furaha yako mwenyewe unaweza ukawa na kila kitu katika maisha ukawa tajiri na ukakosa furaha lakini masikini ambaye hawezi hata kupata milo mitatu kwa siku akawa na furaha kwenye maisha yake.
2000
Ilipita miaka mitano na tayari Sumaya alikua na alishaanza shule, mtoto huyo alipendwa sana na Mr Hernad Kwani halikuwa jambo rahisi kupata mtoto kwake hivyo alimlea kwa mapenzi yote Princess wake huyo mmoja na wa pekee kwenye maisha yake.Hakuwahi kumjua mama yake ila mke wa Mr Hernad Bi Rahel ndiye alikuwa akimlea kama mama yake na yeye alijua kuwa huyo Ndio mama yake mzazi licha ya kuwa hawakufanana hata chembe.
Mr Hernad aliongea na mama yake pamoja na mke wake na kuwaambia lengo lake na kutaka kumpeleka Sumaya Jamaica ili akasome huko lakini alipendelea aende na mama yake mdogo Zuleya japo walijaribu kupinga hilo lakini alishikilia msimamo wake Ila hakuna aliyetambua kuwa licha ya Mr Hernad kuamua hivyo moyoni aliumia sana kuwa mbali na Princess wake Sumaya wake wa pekee aliyebaki katika huu ulimwengu uliojaa mambo tofauti ya kila aina.
Mwezi mmoja ulitosha kwaajili ya maandalizi ya Visa ya Zuleya na Sumaya pamoja na kila kitu muhimu kilichohitajika kwenye safari hiyo na hatimaye Zuleya na Sumaya waliiacha nchi ya Tanzania na kwenda Jamaica.
Mr Hernad alibaki na huzuni kubwa sana baada ya Sumaya kuondoka kwani uwepo wake kwenye maisha yake ni kama faraja kubwa sana ambayo aliikosa kwa muda mrefu sana.
“Mwanangu hivi unaona maamuzi uliyofanya ni sahihi?”
“Mama hayo ni maamuzi niliyoamua mwenyewe kutoka moyoni”
“Hata kama Gedione ni maamuzi yako Ndio sasa kama yametoka moyoni mbona unaumia sana?”
“Hapana mama nipo sawaa”
“Gedione mimi ni mama yako na nakujua vizuri sana kuliko mtu yeyote hata marehemu baba yako hakukujua kama mimi hivi”
“Mama najua hilo Ila nimeona ndo njia pekee ambayo itamsaidia pia Sumaya maana hata wewe unafahamu magumu niliyoyapitia mama japo huko nje naonekana kuwa na furaha.Sina amani mama tokea Sumaya binti mdogo kabisa kuniacha mwenyewe”
“Najua Ged usiwaze sana najua ulimpenda sana Sumaya kuliko kitu chochote ni kama Sumaya alikuwa zawadi ya kwako lakini zawadi ambayo haikudumu”
“Ni kweli mama na mimi ndiye nilikuwa mwanaume wa kwanza kwa Sumaya lakini nimesababisha haya yo…”
“Shii!!! Gedione tema mate chini mwanangu futa kabisa hiyo kauli kichwani kwako kuwa mwanaume wa kwanza kwa Sumaya sio sababu ya hayo yote kutokea.Ila tambua mimi Nakupenda sana mwanangu hata Rahel anakupenda sana na anaumia kukuona katika hali kama hiyo na kushindwa kukuzalia”
Yalikuwa na maongezi marefu sana lakini yaliyotengeneza taswira mpya ndani ya akili ya Mr Hernad angalau alipata ahueni na kuwa mchangamfu.
Kila siku iliyoitwa leo Mr Hernad aliwasiliana na binti yake wa pekee huku mali zote alizonazo aliandika jina la binti yake Sumaya Gedione Hernad kuwa mrithi wake.
Maradhi ya uzee yalianza kumsumbua mama yake Gedione hivyo kupelekea kuwa tu kitandani huku akiwa hajiwezi na mtu pekee aliyetoa msaada wa hali na mali ni Bi Rahel kwani ndiye mkwe wake, lakini naye Mr Hernad hakuwa nyuma kumsaidia mama yake kwani ndiye mtu pekee aliyemlea sana kuliko hata baba yake aliyekuwa akuhangaika na maisha kutwa kucha na asiijali familia yake hata pale umauti ulivyomkuta.Mama Gedione hakubahatika kupata mtoto mwingine zaidi ya huyo mmoja kwani maisha yao ya zamani hayakueleweka hata mume wake hakuwa akijali hilo muda mwingi alikuwa mbali na familia yake mara chache sana alirudi na kuchungulia kisha angeondoka na kwenda kula bata alikokuwa akikujua yeye maisha yake yalikuwa ya starehe sana kuliko kutulia na familia yake hata kusoma kwa Gedione kulikuwa kwa shida sana na ndo maana Gedione alipambana kwa hali na mali ili familia yake isije kuteseka kama walivyoteseka na mama yake.
Lakini mwisho wa siku hakuna kitakachodumu milele, mama yake Gedione alifariki ni kama Mr Hernad alizidi kupoteza watu wa muhimu sana kwenye maisha yake ambao Ndio faraja kwake siku zote.Hata Sumaya na Zuleya walikuwepo pia kwenye msiba huo wa mtu muhimu sana kwenye maisha yao.
JAMAICA
2005
“Mama where you? I’m here….. Mama Zuleya niko hapa?”Ilikuwa ni sauti nzuri ya binti mrembo Sumaya Hernad
“Aah toto you are here… I’m so happy”Akimkumbatia kwa upendo, “ My only daughter Sumaya you remind me about something past, I only have Sumaya who gave me happy but now I also have only one Sumaya who give me happy.I love you “
“Binti yangu wa pekee Sumaya unanikumbusha kitu nyuma nilikuwa na Sumaya mmoja ambaye alinipa furaha lakini sasa pia nina Sumaya mmoja ambaye ananipa furaha.Nakupenda”
“Mmh Mama penda pia”
Sumaya msichana mrembo ambaye urembo wake ulijidhihirisha akiwa bado mdogo alikuwa ni mrefu wa wastani mwenye mwili wa kawaida si mwembamba sana wala mnene, macho makubwa ya wastani na mdomo uliojichora vizuri sana huku shavuni akipambwa na vishimo ambavyo viliongeza uzuri wake maradufu.
Walikuwa wakiishi wawili tu kwenye nyumba na wao hawakuacha kuzungumza kiswahili mara chache hiyo iliwafanya wazungumze Kiswahili muda mwingine japo hakikuwa kizuri sana hasa upande wa Sumaya ambaye aliondoka Tanzania akiwa bado mdogo sana lakini pia muda mwingine walizungumza lugha ya asili ya kijamaica ni kama krioli kwa wajamaica iliyojulikana kama Patois kwa namna fulani waliuzoea sana utamaduni wa Jamaica hasa Sumaya ambaye alikulia huko.
Maneno aliyoyaongea Zuleya kwa upande fulani yaliwasha taa ya njano kwa mtoto Sumaya na kuwaza Mama yake huyo alikuwa na maana gani mpaka kumwambia maneno hayo.Katika nchi ya Jamaica ndani ya jiji maarufu Kingston na ndio mji mkuu wa Jamaica ndipo Zuleya aliishi na mwanaye Sumaya na kupatiwa nyumba ya kuishi na rafiki mkubwa wa Mr Hernad ambaye walikuwa wakiishi wote Australia, Sumaya alisoma shule maarufu na iliyojulikana sana ndani na nje ya Jamaica Allman Town Primary School.Alikuwa ni mwanafunzi mwenye akili na bidii sana darasani hata walimu na wanafunzi wenzake walishangazwa sana na uwezo mkubwa alionao Sumaya mara nyingi alipokea tuzo mbalimbali kama mwanafunzi bora.Alikuwa pia na rafiki yake aliyeitwa Lukas naye ni mtanzania na huyo ndiye aliyekuwa rafiki wa pekee kwake waliambiana mambo mengi ambayo walikuwa wakiambiana kila mmoja wao akipata tatizo.Siku iloyofuata Sumaya hakutoka ndani wakati wa mapumziko lakini Lukas alijua tu kuwa rafiki yake huyo ana shida alimfuata iliongee nae.
“Lukas!!!”
“Yow!! Wadup?”Aliuliza Lukas kwa lugha ya Patois akimaanisha “Hey What’s up” yaani anaendeleaje lakini Sumaya alionekana mnyonge sana
“I know you Sumaya it’s like we shared the same blood uko vipi?”
“Lukas it’s true niko na problem.It’s about family issues”
“If possible you can let me know and look a possible solution that can be helpful you are my friend best friend”
“Unajua Lukas in my family me and my mom Zuleya are only Islamic even my dad and my mom are christians also I wonder I’m not familiar with my dad and mom but I look familiar with mom Zuleya, why?”
“Mmmmmh”Alivuta pumzi kijana Lukas akiwa amemuelewa kabisa Sumaya “But Sumaya mmh I guess there is something wrong about this issues what if mom Zuleya is your biological mother?”
“How this can be possible Lukas and if this is true why they are not make me aware about this?”
Akili yake sasa ilizidi kuchangamka kutokana na maneno aliyoambiwa na Lukas naye aliapa kutoliacha hilo lipite hivi hivi, aliona atafute muda mzuri ambao yeye na mama yake mdogo watakuwa free kuongea kwasababu muda mwingi Zuleya alikuwa busy na kazi zake hospitalini naye Sumaya busy na shule hivyo sio rahisi sana kupata muda wa kukaa pamoja labda mwisho wa wiki lakini napo sio siku zote, mtoto huyo wa miaka kumi alionekana kuwa na akili ya kuchumbua mambo zaidi na kuyafikiria sana kuliko hata umri wake jambo ambalo hata mtu mzima hawezi kutambua hilo.Lakini alijitahidi asioneshe hilo kwa Mama yake lakini damu ni nzito kuliko maji Zuleya aliitambua vema hali aliyonayo Sumaya nae alificha hilo mpaka atakapo pata nafasi ya kuzungumza nae kwa uzuri zaidi na hata hivyo tabia za Sumaya hazikuwa tofauti sana kama marehemu mama yake na hiyo ilikuwa rahisi sana Zuleya kutambua kwa haraka tatizo lolote alilonalo Sumaya.
ITAENDELEA………
Ungana na mimi katika simulizi hii…..
SEHEMU YA KWANZA
TANZANIA
1995
“Pushhhhhh!!!!!”
“Mrs Hernad jitahidi sukuma mtoto yupo karibu kutoka jitahidi yaani bado kidogo tu.. sukuma!!!”
“Nurse I can’t.. do it anymore… Siwezi nahisi nguvu zinaniishia kabisa “
“Hapana Mrs jitahidi unajua bado…..”kabla hajamalizia hali ya Mrs Hernad ilibadilika ghafla
“Nesi nashindwa…. Aaaaah siwezi..siwe…aaah msaidie mwanangu tafadhali msaid…. Mwana…….”Ghafla akakata moto.Ilikuwa ni taharuki ndani ya chumba hiko cha kina mama kinachojulikana kama labour ward.
Huku nje alionekana mwanaume akiwa amesimama huku kama amevurugwa hata kiti hakikaliki ni kama mwendawazimu alienda mbele na kurudi nyuma akikuna kichwa chake, tai yake ilining’inia shingoni haikueleweka ni staili gani aliifunga kifupi tu alikuwa rafu sana kama mtu aliyechanganyikiwa na pembeni yake aliketi mama ambaye umri wake umeenda yaani ni mtu mzima tayari naye japo alikaa lakini hakuonekana kutulia.Ghafla aliona kitanda cha wagonjwa kikitoka ndani ya labour ward na aliyekuwa akiburuzwa ni mke wake Mrs Hernad ambaye alikuwa akihema kwa mbali tena kwa shida sana, kwa haraka alimfuata daktari mmoja ili aongee nae na daktari huyo alimpa taarifa kuwa haikuwa rahisi kwa mke kujifungua kwa njia ya kawaida hivyo alitakiwa kufanyiwa upasuaji ili mtoto aokolewe kingine alimtoa wasiwasi kuwa wote wawili yaani mama na mtoto wangekuwa salama.Baada ya kusema hayo daktari alimuacha hapo Mr Hernad na kuelekea chumba cha upasuaji naye Mr Hernad alipiga magoti na kusali huku akilitaja jina la Sumaya alimgeukia mama yule ambaye ni mama yake huku naye akimtuliza ili asiwe na papara.Ni katika hospitali ya Aga Khan jijini Dar es salaam pirika pirika za kila siku katika hospitali hiyo kubwa ziliendelea kama kawaida kwani hakukuwa na muda wa kula bata ukiwa hospitalini hapo hakuna daktari wala nesi aliyoenekana kuzembea kwa muda huo.
Huku chumba cha upasuaji kilichojulikana kama thieta, madaktari walizidi kushauriana huku kila daktari akionekana kutoa mchango wake.Huku Mrs Hernad akifanyiwa matayarisho kwaajili ya operation.
“Ni sahihi lakini hii ni win to loose situation, ni lazima tukubali matokeo yatakayo tokea na pia tusikubali kupoteza vyote hapa kuna uwezekano mdogo sana wa kumuokoa mama ni kama asilimia ishirini tu za makadirio ila kuna uwezekano mkubwa wa kumuokoa mtoto ni kama asilimia tisini.So let’s do it”Wote walikubaliana na mawazo ya Dokta Luis ambaye ndiye aliyekuwa akizungumza na Mr Hernad wakati wakitoka labour ward ni daktari bingwa wa mambo yote yanayohusiana na uzazi na saikolojia hakuwa mzembe hata kidogo. Kwa haraka Mrs Hernad alifanyiwa upasuaji ili kuweza kumuokoa mtoto kwa sababu uwezekano wa mama kupona haukuwepo.
Shughuli ilikuwa pevu siku hiyo ni karibia saa nne zilitumika kwenye zoezi hilo, ndipo daktari mmoja mmoja alionekana kutoka ndani ya thieta lakini hakuna aliyethubutu kuzungumza na Mr Hernad kazi hiyo ilikuwa chini ya Dokta Luis, hivyo Dokta Luis alimfuata Mr Hernad na kuongozana mpaka ofisini kwake.Waliketi huku Dokta Luis hakuonesha wasiwasi lakini alionesha sura ya furaha hali iliyompa matumaini Mr Hernad.
“Well… Mr Hernad my super hero hongera sana Mungu amekujalia hatimaye umempata Princess wa Kasri lako, tena mrembo haswa kama mama yake”Alizidi kuonesha sura ya furaha
“Dokta Sijui niseme nini nina furaha sana hatimaye ndoto yangu ya kuitwa baba imetimia.. am… vipi kuhusu Sumaya wangu Dokta anaendeleaje? Naweza kwenda kumuona?”
“Ooh worry out Mr Hernad, unajua ni kipindi kirefu sana umehangaika juu ya jambo hili la kupata mtoto na leo ndoto zako zimetimia amini kuwa Sumaya alikuja kwako kama malaika mkombozi, kukutoa kwenye huzuni uliyokuwa nayo kwa muda mrefu sana lakini ni furaha iliyoleta huzuni pia”
“Ni kweli Dokta sijui nimpe nini kama zawadi yangu kwake Sumaya wangu, Mungu ni mkubwa sana”
“And you know Mr Hernad wanaume siku zote tumeumbiwa moyo wa ujasiri sana tofauti na wenzetu kina mama japo nao ni majasiri sana kwa upande mwingine, am… Mr Hernad I’m very very sorry ilikuwa ni vigumu mkeo kujifungua kwa njia ya kawaida licha ya hayo alipoteza damu nyingi sana lakini ni jambo ambalo hatukuweza kuforce kwani tungewapoteza wote wawili, ukweli mkeo hatupo naye tena Mr Hernad”
Lilikuwa ni pigo kubwa sana kwa Mr Hernad alikuwa kama mtu aliyemwagiwa maji ya baridi kwenye baridi kali alisimama ghafla kuanza kupiga mikono yake kwenye ukuta kama mwendawazimu naye Dokta Luis kama mtaalamu alimfuata na kuanza kumtuliza ili angalau hasira zake zishuke ili waangalie utaratibu unaofuata.Jambo hilo lilimchanganya sana kwani hakulitegemea kwa wakati huo, licha ya hayo Sumaya alikuwa ni binti mdogo kabisa wa miaka ishirini na mitano tu.
Wakati akitoka katika ofisi ya Dokta Luis ndipo alipomuona mwanadada ambaye alijitanda vizuri mtandio wake kama kujisitiri akija upande wake alimtambua vyema kabisa mwanadada huyo ndipo walisalimiana kisha yule dada alianza kuuliza maswali Mr Hernad mfululizo kutokana na wasiwasi kwa hali aliyoiona kwa Mr Hernad.
“Shemeji kuna nini? Dada ameshajifungua? Vipi mtoto na dada wanaendeleaje? Aah samahani nimechelewa kuja na chakula shemeji nilishindwa kuja mapema kwasababu ya mitihani”
“Aah Usijali Zuleya… hata hivyo chakula hakina umuhimu kwa sasa”
“Kwanini au mmeshamnunulia chakula? Shemeji ongea na mimi”
“Zuleya dada yako hatupo naye tena Zuleya ila mtoto yupo salama kabisa” Aliongea Mr Hernad kwa huzuni na kumfanya Zuleya aangushe kapu ambalo alihifadhia chakula kwaajili ya dada yake ambaye kwa sasa ni marehemu.
“Aaaahhhhhhhhhhh!!!!!!!!”Alipiga ukunga wa maumivu Zuleya kwani ni kama amechomwa na msumari wa moto kwenye moyo wake katika familia yao walibahatika kuzaliwa wawili tu yeye na dada yake ambaye waliishi maisha magumu sana baada ya kufariki wazazi wao kwa mtego kwani ajali ya gari waliyopata haikuwa ya kawaida na ndugu kuwanyang’anya mali zote za wazazi wao na kuwatenga na Sumaya ndiye alikuwa mlezi mkuu wa Zuleya angalau hata mjomba wao alikuwa upande wao kuwasomesha japo hakuwa na kipato kikubwa naye hakuchukua muda alifariki kutokana na maradhi tofauti yaliyomsumbua ndipo Sumaya aliacha chuo akiwa anakaribia kuingia Mwaka wa tatu na kuanza kumuhangaikia mdogo kwake ili asome ndipo alipoonana na Mr Hernad na kufunga ndoa ya serikali, na hapo Mr Hernad alimalizia kumsomesha Sumaya mwaka mmoja uliobaki na kumsomesha Zuleya huku akiwanunulia nyumba nzuri ya kuishi na kumuajiri msaidizi wa kazi ambayo aliishi Zuleya na ndipo maisha yao yalipobadilika na kuwa mazuri tofauti na mwanzo.
Zuleya alimtizama shemeji yake huku uso wake ukiwa umeiva na kuwa mwekundu kutokana na kilio. Machozi tayari yalishalowanisha sehemu kubwa ya mwili wake.
Kwakuwa Sumaya alikuwa ni muislamu hivyo kama ulivyo taratibu zao maandalizi ya mazishi yalianza kufanyika mapema sana na siku iliyofuata Sumaya alizikwa, ilikuwa ni huzuni kubwa sana ni kama kitoto kichanga kilikuwa kinaelewa nini kimetokea kililia mfulilizo huku kikionesha huzuni ulikuwa ni wakati mgumu sana kwa Mr Hernad na wasaidizi wa kazi kumtuliza mtoto huyo ambaye Mr Hernad aliamua kukuaita Sumaya kwani kalifanana sana na mama yake kwa kila kitu hata watu wa nyumbani hapo walishangaa sana jambo hilo.
Mr Gedione Hernad alikuwa ni mfanyabiaahara mkubwa sana ndani na nje ya nchi, masomo yake alisomea nchini Australia katika chuo cha mambo ya siasa Deakin University pia alisoma vilevile masuala ya masoko (marketing) na huko ndipo alipokutana na Dokta Luis ambaye alikuwa akisoma chuo cha udaktari La Trobe University, wawili hao walikutana katika mashindano ya vyuo vikuu nchini Australia katika mambo mbalimbali ya elimu, vipaji na michezo tofauti ndipo walipoonana na kujenga urafiki wao wa kudumu japo Mr Hernad alimzidi Dokta Luis kwa miaka na elimu kwani Dokta Luis muda huo ndio alikuwa akianza masomo yake nchini Australia.Vilevile alikuwa ni kiongozi mwenye madaraka serikalini naam alikuwa ni Waziri wa mambo ya nje lakini kabla ya kushika wadhifa huo alipitia nafasi mbalimbali za uongozi na mwisho kuwa Waziri wa mambo ya nje.Pia alimuoa mwanamke na kuishi naye.Hakuna ambaye alikuwa hamfahamu Mr Hernad kwa sifa zake upendo ustaarabu na moyo wa huruma na kutoa lakini miaka mitano ya ndoa yake mke wake alifariki bila kuwa na mtoto, aliishi maisha hayo kwa miaka karibia mitatu alipata mwanamke mwingine na kumuoa naye alikuwa na matatizo ya uzazi hivyo hawakubahatika kupata mtoto katika miaka mitatu ya ndoa yao. Suala la mtoto lilimsumbua sana akili Mr Hernad huku familia yake ikihangaika huku na huko kumuombea Mr Hernad japo apate mtoto na ndipo mke wake alipomruhusu atatute mwanamke ambaye angeweza kumpa watoto kuliko kuendelea kusononeka jambo hilo hata familia yake ililiafiki na ndipo alipokutana na Sumaya na kufunga nae ndoa ya serikali kwa wakati huo Mr Hernad alishafikia umri wa miaka arobaini huku mwaka mmoja kupita kwenye ndoa yao alipata ujauzito, ni kama neema iliingia katika familia ya Mr Hernad naye hakuruhusu mke wake huyo Kufanya chochote hata kujikuna yaani alikuwa akimlea kama yai Sumaya aliishi kama malikia huku daktari wake alikuwa alimfuata nyumbani kwa vipimo vyote na mazoezi alifanyia hapo hapo nyumbani kwani kulikuwa na kila kitu.Mapenzi ya Mr Hernad kwa Sumaya yaliongezeka mara dufu mpaka alifunga CCTV Camera chumbani kwake ili muda wote amuone mke wake kipenzi.
Hayo Ndio maisha ya Mr Hernad aliyepitia changamoto kadhaa kwenye maisha yake licha ya kuwa na pesa za kutosha na kugundua kuwa pesa haiwezi kununua furaha katika maisha bali furaha unaipata kutoka kwa watu wa karibu na kutoka kwako mwenyewe na aina ya maisha unayoishi uwe na masikini au tajiri unaweza kutengeneza furaha yako mwenyewe unaweza ukawa na kila kitu katika maisha ukawa tajiri na ukakosa furaha lakini masikini ambaye hawezi hata kupata milo mitatu kwa siku akawa na furaha kwenye maisha yake.
2000
Ilipita miaka mitano na tayari Sumaya alikua na alishaanza shule, mtoto huyo alipendwa sana na Mr Hernad Kwani halikuwa jambo rahisi kupata mtoto kwake hivyo alimlea kwa mapenzi yote Princess wake huyo mmoja na wa pekee kwenye maisha yake.Hakuwahi kumjua mama yake ila mke wa Mr Hernad Bi Rahel ndiye alikuwa akimlea kama mama yake na yeye alijua kuwa huyo Ndio mama yake mzazi licha ya kuwa hawakufanana hata chembe.
Mr Hernad aliongea na mama yake pamoja na mke wake na kuwaambia lengo lake na kutaka kumpeleka Sumaya Jamaica ili akasome huko lakini alipendelea aende na mama yake mdogo Zuleya japo walijaribu kupinga hilo lakini alishikilia msimamo wake Ila hakuna aliyetambua kuwa licha ya Mr Hernad kuamua hivyo moyoni aliumia sana kuwa mbali na Princess wake Sumaya wake wa pekee aliyebaki katika huu ulimwengu uliojaa mambo tofauti ya kila aina.
Mwezi mmoja ulitosha kwaajili ya maandalizi ya Visa ya Zuleya na Sumaya pamoja na kila kitu muhimu kilichohitajika kwenye safari hiyo na hatimaye Zuleya na Sumaya waliiacha nchi ya Tanzania na kwenda Jamaica.
Mr Hernad alibaki na huzuni kubwa sana baada ya Sumaya kuondoka kwani uwepo wake kwenye maisha yake ni kama faraja kubwa sana ambayo aliikosa kwa muda mrefu sana.
“Mwanangu hivi unaona maamuzi uliyofanya ni sahihi?”
“Mama hayo ni maamuzi niliyoamua mwenyewe kutoka moyoni”
“Hata kama Gedione ni maamuzi yako Ndio sasa kama yametoka moyoni mbona unaumia sana?”
“Hapana mama nipo sawaa”
“Gedione mimi ni mama yako na nakujua vizuri sana kuliko mtu yeyote hata marehemu baba yako hakukujua kama mimi hivi”
“Mama najua hilo Ila nimeona ndo njia pekee ambayo itamsaidia pia Sumaya maana hata wewe unafahamu magumu niliyoyapitia mama japo huko nje naonekana kuwa na furaha.Sina amani mama tokea Sumaya binti mdogo kabisa kuniacha mwenyewe”
“Najua Ged usiwaze sana najua ulimpenda sana Sumaya kuliko kitu chochote ni kama Sumaya alikuwa zawadi ya kwako lakini zawadi ambayo haikudumu”
“Ni kweli mama na mimi ndiye nilikuwa mwanaume wa kwanza kwa Sumaya lakini nimesababisha haya yo…”
“Shii!!! Gedione tema mate chini mwanangu futa kabisa hiyo kauli kichwani kwako kuwa mwanaume wa kwanza kwa Sumaya sio sababu ya hayo yote kutokea.Ila tambua mimi Nakupenda sana mwanangu hata Rahel anakupenda sana na anaumia kukuona katika hali kama hiyo na kushindwa kukuzalia”
Yalikuwa na maongezi marefu sana lakini yaliyotengeneza taswira mpya ndani ya akili ya Mr Hernad angalau alipata ahueni na kuwa mchangamfu.
Kila siku iliyoitwa leo Mr Hernad aliwasiliana na binti yake wa pekee huku mali zote alizonazo aliandika jina la binti yake Sumaya Gedione Hernad kuwa mrithi wake.
Maradhi ya uzee yalianza kumsumbua mama yake Gedione hivyo kupelekea kuwa tu kitandani huku akiwa hajiwezi na mtu pekee aliyetoa msaada wa hali na mali ni Bi Rahel kwani ndiye mkwe wake, lakini naye Mr Hernad hakuwa nyuma kumsaidia mama yake kwani ndiye mtu pekee aliyemlea sana kuliko hata baba yake aliyekuwa akuhangaika na maisha kutwa kucha na asiijali familia yake hata pale umauti ulivyomkuta.Mama Gedione hakubahatika kupata mtoto mwingine zaidi ya huyo mmoja kwani maisha yao ya zamani hayakueleweka hata mume wake hakuwa akijali hilo muda mwingi alikuwa mbali na familia yake mara chache sana alirudi na kuchungulia kisha angeondoka na kwenda kula bata alikokuwa akikujua yeye maisha yake yalikuwa ya starehe sana kuliko kutulia na familia yake hata kusoma kwa Gedione kulikuwa kwa shida sana na ndo maana Gedione alipambana kwa hali na mali ili familia yake isije kuteseka kama walivyoteseka na mama yake.
Lakini mwisho wa siku hakuna kitakachodumu milele, mama yake Gedione alifariki ni kama Mr Hernad alizidi kupoteza watu wa muhimu sana kwenye maisha yake ambao Ndio faraja kwake siku zote.Hata Sumaya na Zuleya walikuwepo pia kwenye msiba huo wa mtu muhimu sana kwenye maisha yao.
JAMAICA
2005
“Mama where you? I’m here….. Mama Zuleya niko hapa?”Ilikuwa ni sauti nzuri ya binti mrembo Sumaya Hernad
“Aah toto you are here… I’m so happy”Akimkumbatia kwa upendo, “ My only daughter Sumaya you remind me about something past, I only have Sumaya who gave me happy but now I also have only one Sumaya who give me happy.I love you “
“Binti yangu wa pekee Sumaya unanikumbusha kitu nyuma nilikuwa na Sumaya mmoja ambaye alinipa furaha lakini sasa pia nina Sumaya mmoja ambaye ananipa furaha.Nakupenda”
“Mmh Mama penda pia”
Sumaya msichana mrembo ambaye urembo wake ulijidhihirisha akiwa bado mdogo alikuwa ni mrefu wa wastani mwenye mwili wa kawaida si mwembamba sana wala mnene, macho makubwa ya wastani na mdomo uliojichora vizuri sana huku shavuni akipambwa na vishimo ambavyo viliongeza uzuri wake maradufu.
Walikuwa wakiishi wawili tu kwenye nyumba na wao hawakuacha kuzungumza kiswahili mara chache hiyo iliwafanya wazungumze Kiswahili muda mwingine japo hakikuwa kizuri sana hasa upande wa Sumaya ambaye aliondoka Tanzania akiwa bado mdogo sana lakini pia muda mwingine walizungumza lugha ya asili ya kijamaica ni kama krioli kwa wajamaica iliyojulikana kama Patois kwa namna fulani waliuzoea sana utamaduni wa Jamaica hasa Sumaya ambaye alikulia huko.
Maneno aliyoyaongea Zuleya kwa upande fulani yaliwasha taa ya njano kwa mtoto Sumaya na kuwaza Mama yake huyo alikuwa na maana gani mpaka kumwambia maneno hayo.Katika nchi ya Jamaica ndani ya jiji maarufu Kingston na ndio mji mkuu wa Jamaica ndipo Zuleya aliishi na mwanaye Sumaya na kupatiwa nyumba ya kuishi na rafiki mkubwa wa Mr Hernad ambaye walikuwa wakiishi wote Australia, Sumaya alisoma shule maarufu na iliyojulikana sana ndani na nje ya Jamaica Allman Town Primary School.Alikuwa ni mwanafunzi mwenye akili na bidii sana darasani hata walimu na wanafunzi wenzake walishangazwa sana na uwezo mkubwa alionao Sumaya mara nyingi alipokea tuzo mbalimbali kama mwanafunzi bora.Alikuwa pia na rafiki yake aliyeitwa Lukas naye ni mtanzania na huyo ndiye aliyekuwa rafiki wa pekee kwake waliambiana mambo mengi ambayo walikuwa wakiambiana kila mmoja wao akipata tatizo.Siku iloyofuata Sumaya hakutoka ndani wakati wa mapumziko lakini Lukas alijua tu kuwa rafiki yake huyo ana shida alimfuata iliongee nae.
“Lukas!!!”
“Yow!! Wadup?”Aliuliza Lukas kwa lugha ya Patois akimaanisha “Hey What’s up” yaani anaendeleaje lakini Sumaya alionekana mnyonge sana
“I know you Sumaya it’s like we shared the same blood uko vipi?”
“Lukas it’s true niko na problem.It’s about family issues”
“If possible you can let me know and look a possible solution that can be helpful you are my friend best friend”
“Unajua Lukas in my family me and my mom Zuleya are only Islamic even my dad and my mom are christians also I wonder I’m not familiar with my dad and mom but I look familiar with mom Zuleya, why?”
“Mmmmmh”Alivuta pumzi kijana Lukas akiwa amemuelewa kabisa Sumaya “But Sumaya mmh I guess there is something wrong about this issues what if mom Zuleya is your biological mother?”
“How this can be possible Lukas and if this is true why they are not make me aware about this?”
Akili yake sasa ilizidi kuchangamka kutokana na maneno aliyoambiwa na Lukas naye aliapa kutoliacha hilo lipite hivi hivi, aliona atafute muda mzuri ambao yeye na mama yake mdogo watakuwa free kuongea kwasababu muda mwingi Zuleya alikuwa busy na kazi zake hospitalini naye Sumaya busy na shule hivyo sio rahisi sana kupata muda wa kukaa pamoja labda mwisho wa wiki lakini napo sio siku zote, mtoto huyo wa miaka kumi alionekana kuwa na akili ya kuchumbua mambo zaidi na kuyafikiria sana kuliko hata umri wake jambo ambalo hata mtu mzima hawezi kutambua hilo.Lakini alijitahidi asioneshe hilo kwa Mama yake lakini damu ni nzito kuliko maji Zuleya aliitambua vema hali aliyonayo Sumaya nae alificha hilo mpaka atakapo pata nafasi ya kuzungumza nae kwa uzuri zaidi na hata hivyo tabia za Sumaya hazikuwa tofauti sana kama marehemu mama yake na hiyo ilikuwa rahisi sana Zuleya kutambua kwa haraka tatizo lolote alilonalo Sumaya.
ITAENDELEA………