Mogambi
JF-Expert Member
- May 25, 2012
- 209
- 351
KIKOKOTOO
David Ngocho Samson
UTANGULIZI
Hakuna aliyejua sababu ya madhila yaliyomkumba mstaafu, tena ambaye enzi za ujana na maisha yake ya Kazi, alikuwa mtu aliyekuwa na nafasi nzuri, na maisha yaliyotosha sifa za kuitwa maisha bora. Lakini fununu mitaani zilienea kuwa, mstaafu huyo, afisa wa serikali, ilisemekana kwamba aliingia mkataba na kampuni moja ya ukopeshaji fedha miaka michache kabla ya kustaafu kwake.
***
SEHEMU YA KWANZA
Alipozinduka, mzee Muganyizi alijikuta hospitalini, maji ya drip yakitiririka taratibu na kuingia mwilini mwake kupitia sindano iliyochomwa mkononi mwake. Alijitutumua na kujaribu kunyanyua kichwa chake lakini alihisi uzito usiomithilika sambamba na maumivu makali kiasi cha kuhisi kichwa kinauacha mwili. Nesi aliyekuwa anamhudumia alipomuona mgonjwa wake akihangaika, alimshauri alale na asifanye jambo lolote ambalo lingemzidishia maumivu.
Hakuwa mkaidi, alimsikiliza nesi na kutuliza kichwa chake kwenye godoro huku maumivu yale makali yakimpa wazimu. Maana hakujua kama alipatwa na kizunguzungu au yalikuwa maruweruwe. Kwake, yote yalikuwa sawa tu. Alijituliza taratibu, huku kuwa kwake macho wazi, kukimpa nafasi ya kufunguka fahamu zake.
Taratibu fahamu zake ziilianza kumrejea moja baada ya nyingine. Na kwa kweli, hazikumpa nafuu yoyote aliyotarajia. Maisha yake siku za karibuni yalikuwa hayasomeki kabisa. Alishindwa kujua ni wapi alipokosea kiasi cha kuyapa mwelekeo hovyo kabisa maisha yake, tena wakati ambao alidhani angepata fursa ya kufurahia maisha baada ya kulitumikia taifa kwa uaminifu kabisa.
Kijana wake wa mwisho, kitinda mimba, Mutahaba, au mwite tu Muta, alikuwa ndani ya gereza kwa tuhuma za ujambazi na mauaji. Kijana mdogo tu wa miaka thelathini kasoro mmoja. Alikuwa kijana wake wa pekee kwa sasa, baada ya kaka zake kusemekana kwamba walikwishatangulia mbele za haki kwa kifo katili cha kunyongwa hadi kufa. Sasa, huyu aliyebaki kama tegemeo pekee na yeye alikuwa anasota gerezani, na kwa ugumu wa maisha na ukata aliokuwa nao, hata dhamana ilikuwa imeshindikana kwa ajili ya kumweka huru.
Muganyizi hakuwa na mke kwa takribani miongo miwili sasa. Ingawa alimpenda sana mkewe, ajali iliyomuacha na kilema cha mguu, haikumbakiza mke wake kipenzi mama Rutashobya. Hata hivyo alijitahidi na aliamini kwamba alikuwa baba na mlezi makini kwa wanawe wanne na hasa yule kitinda mimba, Muta.
Hakutaka kabisa wanae wapitie masahibu aliyopitia yeye enzi za utoto wake. Alipokumbuka umande na umbali aliotumia kila siku kwenda na kurudi shule bila viatu hata kufikia hatua ya kupasuka miguu, Muganyizi alijibidiisha kwenye kazi wanae wasiyapitie hayo.
Mungu alimjaalia, kwani yeye alisoma enzi za uongozi wa mwalimu J.K Nyerere, elimu bila malipo kwa ufadhili wa serikali, ambapo alitia bidii na hatimaye kubarikiwa kazi katika wizara ya elimu na kupata cheo cha afisa elimu wilayani Sumbawanga kama ajira yake ya kwanza. Bidii yake ya kazi na kujihusisha na miradi binafsi mbalimbali hasa kilimo katika bonde la ziwa Rukwa ikamwezesha kusomesha wanae shule za kisasa. Shule za malazi nchi jirani ya Kenya. Vijana hao walipofuzu elimu zao za awali, msingi na sekondari, wakapata nafasi ya kusoma elimu ya juu katika vyuo vikuu mbalimbali.
Familia yake ilikuwa ni mfano wa kuigwa. Kijana wake wa kwanza Rutashobya, alifanikiwa kupata shahada yake ya biashara chuo kikuu Cha Dar es salaam na baadaye akaendelea na shahada ya uzamivu chuo Kikuu Cha Oxford nchini Uingereza. Alipotokea hapo Oxford na kurejea nyumbani, serikali haikukawia kumpa kazi, hasa kwa kuzingatia kuwa Enzi hizo wasomi wa kiwango chake walikuwa wachache mno. Serikali ikamwajiri kuitumikia katika taasisi nyeti kabisa kwa uchumi wa nchi, Benki kuu ya Tanzania (BOT).
Kijana wa pili, Byarugaba yeye pia alifuzu mafunzo ya uhasibu pale IFM na baadaye akaendea shahada yake ya uzamivu katika chuo Kikuu cha Witwatersrand nchini Africa ya kusini, na baada ya hapo alirejea nyumbani na kuajiriwa na shirika la umeme TANESCO makao makuu kama mhasibu.
Binti yake wa pekee Kokushubira, yeye aliamua kuwa mwalimu, hivyo mara baada ya kuhitimu shahada yake ya kwanza pale chuo Kikuu Cha Dar es salaam, hakusita kwenda kufundisha huko manispaa ya Morogoro.
Mutahaba alikuwa kijana wake wa mwisho. Kipenzi cha familia. Huyu alizaliwa na kujikuta katika familia iliyosheheni ukwasi na furaha. Kila alichohitaji alikipata bila shida wala kuwaza. Alijikuta akiishi maisha ya kifalme, asiijue shida wala rangi yake.
Miaka ikasonga, maisha yalizidi kuchanua na kunawiri. Familia ya Muganyizi ilibarikiwa. Lakini nani kaiona kesho?
***
Ilikuja taarifa, haikuwa nzuri. Rutashobya kijana wake mkubwa, alituhumiwa kwa ubadhirifu na upotevu wa kiasi kikubwa cha fedha za umma katika benki kuu ya taifa (BOT). Hali ikawa tete. Kesi ikatinga mahakamani, ushahidi ukakusanywa, ikathibitishwa na mahakama kwamba ni kweli kulitokea ubadhirifu mkubwa wa fedha.
Ilikuwa kweli kwamba ubadhirifu ulifanyika, lakini haikuwa kweli kwamba Rutashobya alihusika.
Hata hivyo, Ruta ndiye aliyekuwa na dhamana ya ofisi, waliofanya ubadhirifu walikusudia kumwangushia jumba bovu, hivyo ndivyo iliyokuwa. Ruta akaona kuliko jela bora awe mkimbizi ughaibuni. Bila kuacha unyayo Ruta akafutika nchini. Mahakama ikaamuru mali zake kufilisiwa. Kwa mara ya kwanza familia ya Muganyizi ikapata doa.
Kwa kiasi fulani hali hiyo iliitikisa sana familia ya Muganyizi, kila kona ya nchi na hata nje ya mipaka ya nchi, habari hizo zilivuma kama upepo wa kisulisuli, juu ya familia hiyo kuitia serikali hasara kubwa ya kifedha. Mitaani nako, raia hawakuacha kutwa kucha kuinyoshea vidole familia hiyo na kuwabatiza majina hovyo na dhalili kama wezi, mafisadi na hata kuwaombea balaa.
Kutokana na hali hiyo, Byarugaba kijana wake wa pili, aliacha kazi na kuamua kufanya biashara binafsi. Fununu zikaeleza kuwa, hakuacha kazi bali naye kama kaka yake alifukuzwa kazi kwa sababu ambazo hazikuwa na mashiko, wengi wakihusisha tukio hilo na ile kashfa iliyomkumba kaka yake, Rutashobya, ubadhirifu wa fedha za umma.
Baada ya kufanya maamuzi ya kuacha kazi na kuamua kufanya biashara, Mungu hakumtupa mkono Byarugaba, biashara yake ya electronics ilishika kasi, hata akawa ni msambazaji mkubwa wa vifaa vya electronics jijini Dar es salam. Alikuwa na duka kubwa kabisa katika moja ya mitaa maarufu ya Kariakoo. Hakuishia kusambaza Dar es salaam pekee. Byarugaba alikuwa na mawakala kila mkoa nchini kwa kipindi cha muda mfupi sana.
Katika harakati zake za kibiashara, safari moja, Byarugaba alisafiri kufuata mzigo huko ng'ambo, nchini China. Haikujulikana nini hasa kilitokea, lakini Byarugaba hakurejea tena nchini. Hali iliyoipa familia yake wasiwasi mkubwa. Wakati, familia ya Muganyizi inaanza kukubaliana na sintofahamu ya kijana wao kupotelea ng'ambo, taarifa zilizothibitishwa na ubalozi nchini China, baadaye zilidai Byarugaba na kaka yake Rutashobya walikamatwa kwa kujihusisha na biashara haramu ya madawa ya kulevya na kuhukumiwa kunyongwa hadi kufa. Habari hizo zilimfika mzee Muganyizi kama mshituko, zilimfadhaisha mno mzee huyo kiasi cha kumfanya apoteze kabisa ufanisi katika kazi huku afya yake ikiporomoka kila kulipokucha! Kama isingekuwa Muta, Muganyizi ingekuwa habari za jana. Asingemudu kuukabili msiba huo mkubwa wa vijana wake wawili. Si kwa sababu Muta alimsaidia kuukabili msiba ule bali Muta sasa alibaki tumaini pekee la mzee huyu.
Kutokana na sonona, Muganyizi aliamua kutumia muda wake mwingi kumuomba Mungu na kufanya kila liwezekanalo ili kumsimamisha Muta.
Muta, tofauti na wanawe ambao sasa ilisemekana ni marehemu, hakuwa na kazi wala hakujua namna ya kujisimamia. Maisha yake yote hata kufikia miaka ishirini na kenda, maisha kwake ilikuwa ni matumizi tu, hakujali namna na wapi zilitoka, pesa zilitumika tu huku zikiingia. Alizoeshwa hivyo.
Vifo vya Ruta na Byarugaba vilikuwa pigo kubwa sana kwake Muganyizi lakini hofu yake kubwa sasa ilikuwa juu ya mwanae ambaye sasa alijutia malezi aliyompa na kujilaumu.
Alifanikiwa kumtafutia kazi, lakini Muta hakutaka kabisa habari za kazi. Hakuzoea kufanya kazi, alichojua ni kufanyiwa kazi. Vipi aanze kumuita mtu mwingine bosi ilhali yeye alikuwa kazoea kuitwa bosi? Ilikuwa changamoto ambayo hakuwa tayari kuikubali. Nyota iliyong’ara sasa ilianza kufifia na kupotea. Muta alipoteza dira.
Muganyizi, hofu juu ya mwanae ikamtafuna na kumdhoofisha. Kila alichojaribu kufanya ili kuyapa dira maisha ya mwanae kilimuonesha ni kwa namna gani alikuwa amechelewa.
Jioni moja, aliamua hana namna nyingine zaidi ya kumhoji Muta anataka nini. Bila kusita, akajibiwa 'pesa', pesa nyingi za kutosha kuanzisha biashara kubwa au kampuni. Muganyizi akajipata njia panda. Pesa hakuwa nayo. Tangu walipopata msiba ule mkubwa, ni kama dunia iliwatenga na kuwapuuza, hata maswahiba wake wa karibu, nao walipotea. Jambo hilo la mtaji kwa Muta likauchoma moyo wake na kumtia sonona zaidi, lakini hakutaka kulipuuza. Alijikuta akilizingatia mno na kuliwazia sana.
Usiku wa siku hiyo hakupata usingizi mapema. Muganyizi alihisi mawazo yake yanamzomea kwa kila mbinu aliyotafakari kutumia kukabili hali ya mwanae. Nyumba yake kubwa sasa ilionekana kujawa na majitu ya kutisha, kila kona ya nyumba ile ilikuwa ni kana kwamba inamzomea. Kichwa chake kilimpwaya kabisa.
Usiku wa saa tisa, Muganyizi alijikuta akijicheka kwa dharau. Umri nao ulikuwa unamtupa mkono, ilikuwa imebaki miaka mitatu kustaafu! Alinyanyuka kitandani akawasha taa kisha akajitazama kwenye kioo kikubwa cha chumbani! Hakuliona lile tabasamu lililozoeleka. Ngozi yake sasa ilikuwa na makunyanzi kibao na hata kipara chake kilichong’ara zamani sasa kilifubaa na kutengeneza taswira ya bonge moja la kovu.
Wazo hilo la uzee likaamsha wazo jipya. Sasa alirejea kitandani na kupata usingizi. Alipoamka asubuhi alijinyoosha na kujitazama tena kwenye kioo. Alijaribu kutabasamu, kwa mbali akaona nuru. Aliingia bafuni na kuoga huku akiimba wimbo wa Bob Marley, 'no woman no cry!' Alitoka na kuingia kwenye gari lake na kuelekea kazini.
****
Ilikuwa ajabu kidogo. Siku za hivi karibuni hakuonekana kabisa kutabasamu, lakini leo, ah! leo alijawa na matumaini yaliyompa fursa ya kutoa tabasamu mwanana lililowashangaza watumishi wenzake ofisini kwake. Aliingia ofisini akiwa mwingi wa furaha. Alikuwa keshafanya maamuzi yake tangu jana usiku. Hapa alikuwa amekuja kwa kusudi moja tu la utekelezaji. Aliketi kitini, akapaisha macho yake dirishani, akatazama nje kwa muda, akawa anayaona magari yakipita barabarani kutokea kwenye ofisi hiyo ambayo ipo kwenye gorofa ya pili katika jengo hilo la serikali pasipo kuyatilia maanani. Alitazama kwa namna ambayo ilionesha huenda ingelikuwa mara ya mwisho kuitumia meza hiyo kwa kazi zake za kila siku. Uamuzi wake ulikuwa kustaafu kazi. Alipojiridhisha na alichokuwa anakitazama, mzee Muganyizi alirejesha akili yake ofisini hapo. Akavuta keyboard ya komputa yake ya ofisini, akatuliza mawazo na kuruhusu vidole kudurusu kifaa hicho. Aliandika barua, barua ya kuomba kustaafu mapema. Ulikuwa uamuzi mgumu kufanya, lakini aliamini ulikuwa uamuzi sahihi. Lengo lake likiwa kwamba wakishachakata taarifa zake, atapokea pensheni yake na hiyo iwe mtaji kwa mwanae Muta kutimiza ndoto yake ya kumiliki biashara aliyokusudia.
Alianza mchakato huo rasmi Ili kustaafu mapema.
Baada ya kumalizika taratibu zitakiwazo, sasa ilibaki hatua moja ya mwisho. Kupata pesa zake benki, pesa ambazo zingemfaa kijana wake Mutahaba. Huko ndiko alikodondoka na kuzimia na kujikuta akiwa hospitalini, akiwa ana drip mkononi, iliyoruhusu maji kuingia mwilini mwake.
Itaendelea kesho...
David Ngocho Samson
UTANGULIZI
Hakuna aliyejua sababu ya madhila yaliyomkumba mstaafu, tena ambaye enzi za ujana na maisha yake ya Kazi, alikuwa mtu aliyekuwa na nafasi nzuri, na maisha yaliyotosha sifa za kuitwa maisha bora. Lakini fununu mitaani zilienea kuwa, mstaafu huyo, afisa wa serikali, ilisemekana kwamba aliingia mkataba na kampuni moja ya ukopeshaji fedha miaka michache kabla ya kustaafu kwake.
***
SEHEMU YA KWANZA
Alipozinduka, mzee Muganyizi alijikuta hospitalini, maji ya drip yakitiririka taratibu na kuingia mwilini mwake kupitia sindano iliyochomwa mkononi mwake. Alijitutumua na kujaribu kunyanyua kichwa chake lakini alihisi uzito usiomithilika sambamba na maumivu makali kiasi cha kuhisi kichwa kinauacha mwili. Nesi aliyekuwa anamhudumia alipomuona mgonjwa wake akihangaika, alimshauri alale na asifanye jambo lolote ambalo lingemzidishia maumivu.
Hakuwa mkaidi, alimsikiliza nesi na kutuliza kichwa chake kwenye godoro huku maumivu yale makali yakimpa wazimu. Maana hakujua kama alipatwa na kizunguzungu au yalikuwa maruweruwe. Kwake, yote yalikuwa sawa tu. Alijituliza taratibu, huku kuwa kwake macho wazi, kukimpa nafasi ya kufunguka fahamu zake.
Taratibu fahamu zake ziilianza kumrejea moja baada ya nyingine. Na kwa kweli, hazikumpa nafuu yoyote aliyotarajia. Maisha yake siku za karibuni yalikuwa hayasomeki kabisa. Alishindwa kujua ni wapi alipokosea kiasi cha kuyapa mwelekeo hovyo kabisa maisha yake, tena wakati ambao alidhani angepata fursa ya kufurahia maisha baada ya kulitumikia taifa kwa uaminifu kabisa.
Kijana wake wa mwisho, kitinda mimba, Mutahaba, au mwite tu Muta, alikuwa ndani ya gereza kwa tuhuma za ujambazi na mauaji. Kijana mdogo tu wa miaka thelathini kasoro mmoja. Alikuwa kijana wake wa pekee kwa sasa, baada ya kaka zake kusemekana kwamba walikwishatangulia mbele za haki kwa kifo katili cha kunyongwa hadi kufa. Sasa, huyu aliyebaki kama tegemeo pekee na yeye alikuwa anasota gerezani, na kwa ugumu wa maisha na ukata aliokuwa nao, hata dhamana ilikuwa imeshindikana kwa ajili ya kumweka huru.
Muganyizi hakuwa na mke kwa takribani miongo miwili sasa. Ingawa alimpenda sana mkewe, ajali iliyomuacha na kilema cha mguu, haikumbakiza mke wake kipenzi mama Rutashobya. Hata hivyo alijitahidi na aliamini kwamba alikuwa baba na mlezi makini kwa wanawe wanne na hasa yule kitinda mimba, Muta.
Hakutaka kabisa wanae wapitie masahibu aliyopitia yeye enzi za utoto wake. Alipokumbuka umande na umbali aliotumia kila siku kwenda na kurudi shule bila viatu hata kufikia hatua ya kupasuka miguu, Muganyizi alijibidiisha kwenye kazi wanae wasiyapitie hayo.
Mungu alimjaalia, kwani yeye alisoma enzi za uongozi wa mwalimu J.K Nyerere, elimu bila malipo kwa ufadhili wa serikali, ambapo alitia bidii na hatimaye kubarikiwa kazi katika wizara ya elimu na kupata cheo cha afisa elimu wilayani Sumbawanga kama ajira yake ya kwanza. Bidii yake ya kazi na kujihusisha na miradi binafsi mbalimbali hasa kilimo katika bonde la ziwa Rukwa ikamwezesha kusomesha wanae shule za kisasa. Shule za malazi nchi jirani ya Kenya. Vijana hao walipofuzu elimu zao za awali, msingi na sekondari, wakapata nafasi ya kusoma elimu ya juu katika vyuo vikuu mbalimbali.
Familia yake ilikuwa ni mfano wa kuigwa. Kijana wake wa kwanza Rutashobya, alifanikiwa kupata shahada yake ya biashara chuo kikuu Cha Dar es salaam na baadaye akaendelea na shahada ya uzamivu chuo Kikuu Cha Oxford nchini Uingereza. Alipotokea hapo Oxford na kurejea nyumbani, serikali haikukawia kumpa kazi, hasa kwa kuzingatia kuwa Enzi hizo wasomi wa kiwango chake walikuwa wachache mno. Serikali ikamwajiri kuitumikia katika taasisi nyeti kabisa kwa uchumi wa nchi, Benki kuu ya Tanzania (BOT).
Kijana wa pili, Byarugaba yeye pia alifuzu mafunzo ya uhasibu pale IFM na baadaye akaendea shahada yake ya uzamivu katika chuo Kikuu cha Witwatersrand nchini Africa ya kusini, na baada ya hapo alirejea nyumbani na kuajiriwa na shirika la umeme TANESCO makao makuu kama mhasibu.
Binti yake wa pekee Kokushubira, yeye aliamua kuwa mwalimu, hivyo mara baada ya kuhitimu shahada yake ya kwanza pale chuo Kikuu Cha Dar es salaam, hakusita kwenda kufundisha huko manispaa ya Morogoro.
Mutahaba alikuwa kijana wake wa mwisho. Kipenzi cha familia. Huyu alizaliwa na kujikuta katika familia iliyosheheni ukwasi na furaha. Kila alichohitaji alikipata bila shida wala kuwaza. Alijikuta akiishi maisha ya kifalme, asiijue shida wala rangi yake.
Miaka ikasonga, maisha yalizidi kuchanua na kunawiri. Familia ya Muganyizi ilibarikiwa. Lakini nani kaiona kesho?
***
Ilikuja taarifa, haikuwa nzuri. Rutashobya kijana wake mkubwa, alituhumiwa kwa ubadhirifu na upotevu wa kiasi kikubwa cha fedha za umma katika benki kuu ya taifa (BOT). Hali ikawa tete. Kesi ikatinga mahakamani, ushahidi ukakusanywa, ikathibitishwa na mahakama kwamba ni kweli kulitokea ubadhirifu mkubwa wa fedha.
Ilikuwa kweli kwamba ubadhirifu ulifanyika, lakini haikuwa kweli kwamba Rutashobya alihusika.
Hata hivyo, Ruta ndiye aliyekuwa na dhamana ya ofisi, waliofanya ubadhirifu walikusudia kumwangushia jumba bovu, hivyo ndivyo iliyokuwa. Ruta akaona kuliko jela bora awe mkimbizi ughaibuni. Bila kuacha unyayo Ruta akafutika nchini. Mahakama ikaamuru mali zake kufilisiwa. Kwa mara ya kwanza familia ya Muganyizi ikapata doa.
Kwa kiasi fulani hali hiyo iliitikisa sana familia ya Muganyizi, kila kona ya nchi na hata nje ya mipaka ya nchi, habari hizo zilivuma kama upepo wa kisulisuli, juu ya familia hiyo kuitia serikali hasara kubwa ya kifedha. Mitaani nako, raia hawakuacha kutwa kucha kuinyoshea vidole familia hiyo na kuwabatiza majina hovyo na dhalili kama wezi, mafisadi na hata kuwaombea balaa.
Kutokana na hali hiyo, Byarugaba kijana wake wa pili, aliacha kazi na kuamua kufanya biashara binafsi. Fununu zikaeleza kuwa, hakuacha kazi bali naye kama kaka yake alifukuzwa kazi kwa sababu ambazo hazikuwa na mashiko, wengi wakihusisha tukio hilo na ile kashfa iliyomkumba kaka yake, Rutashobya, ubadhirifu wa fedha za umma.
Baada ya kufanya maamuzi ya kuacha kazi na kuamua kufanya biashara, Mungu hakumtupa mkono Byarugaba, biashara yake ya electronics ilishika kasi, hata akawa ni msambazaji mkubwa wa vifaa vya electronics jijini Dar es salam. Alikuwa na duka kubwa kabisa katika moja ya mitaa maarufu ya Kariakoo. Hakuishia kusambaza Dar es salaam pekee. Byarugaba alikuwa na mawakala kila mkoa nchini kwa kipindi cha muda mfupi sana.
Katika harakati zake za kibiashara, safari moja, Byarugaba alisafiri kufuata mzigo huko ng'ambo, nchini China. Haikujulikana nini hasa kilitokea, lakini Byarugaba hakurejea tena nchini. Hali iliyoipa familia yake wasiwasi mkubwa. Wakati, familia ya Muganyizi inaanza kukubaliana na sintofahamu ya kijana wao kupotelea ng'ambo, taarifa zilizothibitishwa na ubalozi nchini China, baadaye zilidai Byarugaba na kaka yake Rutashobya walikamatwa kwa kujihusisha na biashara haramu ya madawa ya kulevya na kuhukumiwa kunyongwa hadi kufa. Habari hizo zilimfika mzee Muganyizi kama mshituko, zilimfadhaisha mno mzee huyo kiasi cha kumfanya apoteze kabisa ufanisi katika kazi huku afya yake ikiporomoka kila kulipokucha! Kama isingekuwa Muta, Muganyizi ingekuwa habari za jana. Asingemudu kuukabili msiba huo mkubwa wa vijana wake wawili. Si kwa sababu Muta alimsaidia kuukabili msiba ule bali Muta sasa alibaki tumaini pekee la mzee huyu.
Kutokana na sonona, Muganyizi aliamua kutumia muda wake mwingi kumuomba Mungu na kufanya kila liwezekanalo ili kumsimamisha Muta.
Muta, tofauti na wanawe ambao sasa ilisemekana ni marehemu, hakuwa na kazi wala hakujua namna ya kujisimamia. Maisha yake yote hata kufikia miaka ishirini na kenda, maisha kwake ilikuwa ni matumizi tu, hakujali namna na wapi zilitoka, pesa zilitumika tu huku zikiingia. Alizoeshwa hivyo.
Vifo vya Ruta na Byarugaba vilikuwa pigo kubwa sana kwake Muganyizi lakini hofu yake kubwa sasa ilikuwa juu ya mwanae ambaye sasa alijutia malezi aliyompa na kujilaumu.
Alifanikiwa kumtafutia kazi, lakini Muta hakutaka kabisa habari za kazi. Hakuzoea kufanya kazi, alichojua ni kufanyiwa kazi. Vipi aanze kumuita mtu mwingine bosi ilhali yeye alikuwa kazoea kuitwa bosi? Ilikuwa changamoto ambayo hakuwa tayari kuikubali. Nyota iliyong’ara sasa ilianza kufifia na kupotea. Muta alipoteza dira.
Muganyizi, hofu juu ya mwanae ikamtafuna na kumdhoofisha. Kila alichojaribu kufanya ili kuyapa dira maisha ya mwanae kilimuonesha ni kwa namna gani alikuwa amechelewa.
Jioni moja, aliamua hana namna nyingine zaidi ya kumhoji Muta anataka nini. Bila kusita, akajibiwa 'pesa', pesa nyingi za kutosha kuanzisha biashara kubwa au kampuni. Muganyizi akajipata njia panda. Pesa hakuwa nayo. Tangu walipopata msiba ule mkubwa, ni kama dunia iliwatenga na kuwapuuza, hata maswahiba wake wa karibu, nao walipotea. Jambo hilo la mtaji kwa Muta likauchoma moyo wake na kumtia sonona zaidi, lakini hakutaka kulipuuza. Alijikuta akilizingatia mno na kuliwazia sana.
Usiku wa siku hiyo hakupata usingizi mapema. Muganyizi alihisi mawazo yake yanamzomea kwa kila mbinu aliyotafakari kutumia kukabili hali ya mwanae. Nyumba yake kubwa sasa ilionekana kujawa na majitu ya kutisha, kila kona ya nyumba ile ilikuwa ni kana kwamba inamzomea. Kichwa chake kilimpwaya kabisa.
Usiku wa saa tisa, Muganyizi alijikuta akijicheka kwa dharau. Umri nao ulikuwa unamtupa mkono, ilikuwa imebaki miaka mitatu kustaafu! Alinyanyuka kitandani akawasha taa kisha akajitazama kwenye kioo kikubwa cha chumbani! Hakuliona lile tabasamu lililozoeleka. Ngozi yake sasa ilikuwa na makunyanzi kibao na hata kipara chake kilichong’ara zamani sasa kilifubaa na kutengeneza taswira ya bonge moja la kovu.
Wazo hilo la uzee likaamsha wazo jipya. Sasa alirejea kitandani na kupata usingizi. Alipoamka asubuhi alijinyoosha na kujitazama tena kwenye kioo. Alijaribu kutabasamu, kwa mbali akaona nuru. Aliingia bafuni na kuoga huku akiimba wimbo wa Bob Marley, 'no woman no cry!' Alitoka na kuingia kwenye gari lake na kuelekea kazini.
****
Ilikuwa ajabu kidogo. Siku za hivi karibuni hakuonekana kabisa kutabasamu, lakini leo, ah! leo alijawa na matumaini yaliyompa fursa ya kutoa tabasamu mwanana lililowashangaza watumishi wenzake ofisini kwake. Aliingia ofisini akiwa mwingi wa furaha. Alikuwa keshafanya maamuzi yake tangu jana usiku. Hapa alikuwa amekuja kwa kusudi moja tu la utekelezaji. Aliketi kitini, akapaisha macho yake dirishani, akatazama nje kwa muda, akawa anayaona magari yakipita barabarani kutokea kwenye ofisi hiyo ambayo ipo kwenye gorofa ya pili katika jengo hilo la serikali pasipo kuyatilia maanani. Alitazama kwa namna ambayo ilionesha huenda ingelikuwa mara ya mwisho kuitumia meza hiyo kwa kazi zake za kila siku. Uamuzi wake ulikuwa kustaafu kazi. Alipojiridhisha na alichokuwa anakitazama, mzee Muganyizi alirejesha akili yake ofisini hapo. Akavuta keyboard ya komputa yake ya ofisini, akatuliza mawazo na kuruhusu vidole kudurusu kifaa hicho. Aliandika barua, barua ya kuomba kustaafu mapema. Ulikuwa uamuzi mgumu kufanya, lakini aliamini ulikuwa uamuzi sahihi. Lengo lake likiwa kwamba wakishachakata taarifa zake, atapokea pensheni yake na hiyo iwe mtaji kwa mwanae Muta kutimiza ndoto yake ya kumiliki biashara aliyokusudia.
Alianza mchakato huo rasmi Ili kustaafu mapema.
Baada ya kumalizika taratibu zitakiwazo, sasa ilibaki hatua moja ya mwisho. Kupata pesa zake benki, pesa ambazo zingemfaa kijana wake Mutahaba. Huko ndiko alikodondoka na kuzimia na kujikuta akiwa hospitalini, akiwa ana drip mkononi, iliyoruhusu maji kuingia mwilini mwake.
Itaendelea kesho...