Simulizi: Biashara haramu ilivyosababisha mauaji

gstar

JF-Expert Member
Jun 19, 2011
759
1,250
Bado sijapata Title maalum ya hii Simulizi twende nayo hivyo hivyo.

UTANGULIZI

Kuna jamii ya watu iliyozuka na kuleta sintofahamu miongoni mwa jamii nyinginezo, watu wanaozisaka pesa kwa namna yeyote ile hata ikibidi kumkufuru mwenyezi Mungu, amini nakwambia si kila ukionacho kwa macho kuwa kipo sahihi basi ukakitafsiri hivyo bila kukifanyia uchunguzi. Ungana nami katika mkasa huu wa kusisimua uweze kujifunza mengi, usisite kunitumia ujumbe mfupi kwa maoni na ushauri.

SEHEMU YA 01

Alfajiri na mapema vishindo vilisikika, ni kama vile kuna mtu aliyekuwa akikimbizwa kisha sauti ya kuomba msaada ilisikika. "Nisaidiee nisaidiee nakufaa!" Sauti ilikuwa kubwa na ilisambaa kwenye maeneo mengi ya kitongoji cha Iptus katika jiji la Greenville hakukuwa na mtu yeyote aliyethubutu kuufungua mlango wake kutoa msaada. Si kwamba walikuwa hawasikii la hasha, walijua fika jambo ambalo linampata mtu huyo anayepiga kelele kwa hivyo waliogopa kujitokeza kupambana na watu hao hatari.

Sauti ya kuomba msaada iliendelea kusikika na mwisho ikapotea na ukimya ukatawala. Damu nyingi zilitapakaa, tukio la kinyama la mauwaji ya kikatili lilikuwa limekwisha kutendeka. Kijana aliyeuwawa na kuchomolewa moyo wake alibaki akiwa amelala huku damu zikiwa zimesambaa, alikuwa amelala juu ya dimbwi la damu!

"Kijana huyu ameonyesha msimamo mkali kwa Mungu wake na kugoma kujiunga na kikundi chetu cha dini mpya na hivyo imempasa kuuwawa, na hili ni onyo kwa yeyote ambaye atakiuka agizo la kujiunga na dini mpya ya Wateule itampasa kuteketea kabisa." sauti ya mtu ilisikika kupitia kwenye kipaza sauti. Wafuasi wa dhebu hili la wateule (The chosen one) waliokuwa mstari wa mbele katika kusambaza dini hiyo mpya wakiongozwa na kiongozi wao Mchungaji Masambula walijizatiti kuisambaza dini hii mpya.

Askari walizungushia utepe kwenye eneo ambalo tukio hili lilitokea, picha zilipigwa na kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii, hii iliongeza woga kwani watu wengi walikuwa wakiogopa kujitenga na dini hiyo mpya, vituo vya kujiunga na dini hiyo vilikuwa busy kupokewa waumini waliokuwa wamefurika kujiandikisha.

"Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa, ni kwanini watu hawapendi kusoma maandiko, upotoshaji huu mpaka lini, siwezi kukubaliana na jambo hili lazima nitafanya kitu." Kijana Marcus alikuwa amekaa mgahawani akipata kahawa huku akisoma matangazo ya dini hiyo kupitia mitandao ya kijamii.

Marcus alikuwa kijana mahiri na msomi alisomea theolojia na mambo ya sheria huko Roma Italia, hakupenda kuona yale mauwaji yaliyoshamiri katika kitongoji kile, watu waliokuwa na malengo binafsi wakifanya mambo ambayo kwake aliona kwamba hayampendezi Mwenyezi Mungu. Alitoka kuelekea kwenye maegesho ya magari akaingia kwenye gari yake ya kifahari aina ya Marcedez Benz na kutembea taratibu kuelekea kwenye makazi yake. Huko njiani hali ilikuwa inatisha alipishana na mizoga ya watu iliyokuwa wametapakaa kila kona ya mji ule. "Kwanini serikali imekaa kimya kanakwamba hawafahamu lolote linaloendelea juu ya mauwaji haya?" aliwaza moyoni mwake.

****

Mlipuko wa makanisa ya 'wateule' ulishangaza wengi siku hii ya Jumapili matawi mbalimbali ya makanisa yakiwa yamefurika waumini, watu wakisifu na kuabudu. Kwenye kanisa kuu lililokuwepo kwenye kitongoji cha Iptus mchungaji alikuwa amesimama mbele akihubiri.

"Sikilizeni enyi waumini, hakuna jiwe litakalo salimika juu ya jiwe hii ni amri kutoka kwangu ya kwamba kila mtu lazima ajiunge nasi atakayegoma kujiunga nasi huyo sio mwenzetu, naamuru kuanzia sasa watu hao waangamizwe popote mtakapo waona." Waumini walishangilia kwa nguvu, "ndioo hao wasiokuwa nasi ni lazima waangamizwe." Baada ya ibada mchungaji aliondoka huku akisindikizwa na walinzi wake.

Marcus aliingia kwenye viunga vya kanisa la Wateule akiwa na lengo la kuonana na mchungaji Masambula. Aliegesha gari yake na moja kwa moja akaelekea eneo la mapokezi, waumini wengi walikuwa wakitoka kuelekea majumbani mwao. Marcus, akiwa amevaa suti yake nyeusi na miwani nyeusi, alificha bastola yake ndogo iliyofanana na kalamu kwenye mfuko wa koti lake hakuna aliyeweza kumshtukia akafika mpaka pale mapokezi. "Naitwa Marcus Desmond ni mwana utume wa Jesuits kutoka kanisa la magharibi nimekuja kuonana na mchungaji Masambula." alijitambulisha.

"Mchungaji, kuna mgeni yupo hapa anahitaji kuonana na wewe," alisema dada wa mapokezi kupitia kwenye simu ya mezani. "Mwambie apite," ilisikika sauti kutoka upande wa pili. Marcus aliingia pale ndani, michoro ya kushangaza ilikuwa kwenye chumba kile msalaba uliogeuka juu chini ukiwa ndio alama kuu ya dini ile, kwa mbele kabisa kulikuwa na picha kubwa ya moyo uliotobolewa kwa kisu ukivuja damu. "Hizi ndizo alama kuu za dini hii, kwanini wanatumia alama hizi? Msalaba uliogeuka juu chini na moyo uliotobolewa na kuvuja damu?" alijaribu kuhusianisha michoro ile na matukio ya kinyama yaliyokuwa yakiendelea mitaani.

"Kila mtu aliyeuwawa akihusishwa na mauwaji yale basi alitobolewa kifuani na kuchomolewa moyo wake, na vipi kuhusu msalaba uliogeuka juu chini, hii haiwezi kuwa alama ya ukristo labda wapinga kristo...?" Aliwaza huku akiingia kwenye chumba kikubwa kilichokuwa ndani ya jengo hilo la kifahari lililokuwa ndio makao makuu ya kanisa la Wateule. Kila kona kulikuwa na nakshi za dhahabu, sanamu ya fuvu la kichwa ilikuwa mezani na mchungaji alikuwa ameketi kwenye kiti chake wakati Marcus akiingia.

Alifika wakapeana kupeana mikono na kisha kuketi kwenye kiti mbele ya mchungaji aliyekuwa ameketi kwenye kiti cha kifahari chenye kuzunguka. Mara tu baada ya kusalimiana kwa ujasiri mkubwa Marcus anamweleza sababu zilizomfanya afike hapo. "Naitwa Marcus ni mwana theolojia na mwandishi wa habari nimesoma na kuhitimu huko Roma Italia nimekuja kukusanya habari juu ya uendeshaji wa kanisa hili na dini hii mpya, nashangazwa na namna yako ya kuhubiri injili, ni dini gani unayo isambaza kwa namna hii?" alihoji Marcus na kuendelea.

"Angalia ni watu wangapi ulio wauwa kwa kuwa tu wamegoma kufuata matakwa yako ya kidini, unadhani jambo unalolifanya lina baraka za kweli kutoka kwa Mwenyezi Mungu?" Mchungaji Masambula alionyesha uso wa kukasirika, hakupenda kabisa kukosolewa naye akajibu. "Sikiliza kijana nchi hii nimeiweka mikononi nakuhakikishia kuwa hakuna kiongozi yeyote atakayenizuia kwasababu ninagawana nao maslahi kila inapoitwa leo, na kuhusu dini kusambazwa kwa upanga mbona hilo sio jambo jipya?"

"Waulize wakatoliki na vita ya msalaba, watu wangapi walikufa wakiutetea ukristo, waislamu nao vivyo hivyo walipigana jihad kuutangaza uislamu, dini yoyote lazima isambazwe kwa vita kwasababu haya ni maelekezo ya mwenyezi Mungu na kwa ninavyojua sio kila mtu atakayekubaliana na maelekezo haya wapo watakao kubaliana na pia wapo watakao pinga, watakao pinga ni lazima tuwateketeze hatuwezi kumuacha mchawi aishi imeandikwa kwenye biblia," alisisitiza mchungaji Masambula.

"Kwahiyo unataka kuniambia kwamba dini yenu ni ya kweli na ya haki kuliko vikundi vingine vyovyote vya kidini na kiimani?" alihoji Marcus.

"Kila mtu huona dini yake kuwa ndio yenye haki kwahiyo kwangu mimi ninaamini kwamba dini yetu ndio yenye haki na hivyo nitatumia mbinu zozote zile kuhakikisha kwamba dini hii inasambaa kwa kila raia wa nchi hii," alizidi kusisitiza mchungaji Masambula.

"Vipi kuhusu hizi alama zenu mnazo zitumia msalaba uliogeuka juu chini pamoja na moyo uliotobolewa na unaovuja damu?"

"Sitoweza kukujibu kwa sasa juu ya haya maswali yako yote labda unipe muda ndio nitaweza kukujibu maswali haya.

Kufumba na kufumbua, Marcus alichomoa bastola yake iliyokuwa kama kalamu ya kuandika ni bastola ndogo sana ambayo ilikuwa na kiwambo cha sailensa na kisha kumuelekezea mchungaji na hapo akamsihi asali sala zake za mwisho. "Haiwezekani haya mateso yote yawe yanatokea kwa ajili yako kwahiyo nitakupoteza kwa manufaa ya wengine!" Mchungaji alishangaa, alinyoosha mikono yake juu kuomba msamaha Marcus hakufanya makosa alimlenga moja kwamoja kifuani kwa risasi moja tu ilitosha kabisa kumfanya mchungaji Masambula kuanguka chini.

Haraka haraka alichomoa kisu alichokificha kwenye mfuko wa koti akamtoboa kifuani na kutoa moyo, akaufunga kwenye mfuko wa nailoni na kisha kuuweka kwenye kibegi chake cha mgongoni. Akatoka pale mapokezi bila hata kugundulika na kuingia kwenye gari yake kisha kuondoka kwa kasi na kutokomea. Kilikuwa ni kitendo cha haraka kilichotokea ndani ya nusu saa tu. Mchungaji aliyeonekana kuwa ni kinara wa mauwaji ya kidini leo hii yamemtokea yaleyale aliyokuwa akiyafanya kwa watu waliokataa kujiunga na dini yake.

ITAENDELEA...
 
Bado sijapata Title maalum ya hii Simulizi twende nayo hivyo hivyo.

UTANGULIZI

Kuna jamii ya watu iliyozuka na kuleta sintofahamu miongoni mwa jamii nyinginezo, watu wanaozisaka pesa kwa namna yeyote ile hata ikibidi kumkufuru mwenyezi Mungu, amini nakwambia si kila ukionacho kwa macho kuwa kipo sahihi basi ukakitafsiri hivyo bila kukifanyia uchunguzi. Ungana nami katika mkasa huu wa kusisimua uweze kujifunza mengi, usisite kunitumia ujumbe mfupi kwa maoni na ushauri.

SEHEMU YA 01

Alfajiri na mapema vishindo vilisikika, ni kama vile kuna mtu aliyekuwa akikimbizwa kisha sauti ya kuomba msaada ilisikika. "Nisaidiee nisaidiee nakufaa!" Sauti ilikuwa kubwa na ilisambaa kwenye maeneo mengi ya kitongoji cha Iptus katika jiji la Greenville hakukuwa na mtu yeyote aliyethubutu kuufungua mlango wake kutoa msaada. Si kwamba walikuwa hawasikii la hasha, walijua fika jambo ambalo linampata mtu huyo anayepiga..
Lini??
 
Bado sijapata Title maalum ya hii Simulizi twende nayo hivyo hivyo.

UTANGULIZI

Kuna jamii ya watu iliyozuka na kuleta sintofahamu miongoni mwa jamii nyinginezo, watu wanaozisaka pesa kwa namna yeyote ile hata ikibidi kumkufuru mwenyezi Mungu, amini nakwambia si kila ukionacho kwa macho kuwa kipo sahihi basi ukakitafsiri hivyo bila kukifanyia uchunguzi. Ungana nami katika mkasa huu wa kusisimua uweze kujifunza mengi, usisite kunitumia ujumbe mfupi kwa maoni na ushauri.

SEHEMU YA 01

Alfajiri na mapema vishindo vilisikika, ni kama vile kuna mtu aliyekuwa akikimbizwa kisha sauti ya kuomba msaada ilisikika. "Nisaidiee nisaidiee nakufaa!" Sauti ilikuwa kubwa na ilisambaa kwenye maeneo mengi ya kitongoji cha Iptus katika jiji la Greenville hakukuwa na mtu yeyote aliyethubutu kuufungua mlango wake kutoa msaada. Si kwamba walikuwa hawasikii la hasha, walijua fika jambo ambalo linampata mtu huyo anayepiga..
Lini??
 
SEHEMU YA 02

Gari ya ambulance iliyokuwa imeubeba mwili wa mchungaji Masambula lilizidi kukatiza mitaa ya jiji la Greenville ili kumwahisha hospitali kujaribu kuokoa maisha yake, mchungaji Masambula aliyekuwa amechomolewa moyo wake ilikuwa kanakwamba amesha fariki na hakukuwa na matumaini yoyote kwamba mtumishi huyo wa Mungu angeweza kuyaponya maisha yake kwa namna yeyote ile, hii ni baada ya kushambuliwa na kijana Marcus ambaye aliingia kama mgeni na kumpiga risasi kisha kuuchomoa moyo wake.

Gari iliingia mpaka kwenye hospitali kuu ya rufaa mwili wa mchungaji Masambula ukiwa ndani ya gari hilo alifika mpaka kwenye kitengo cha wagonjwa mahututi na haraka haraka madaktari na wauguzi walimpokea na kisha kumuwahisha kupata huduma stahiki. "Mgonjwa amepoteza damu nyingi na kuna uwezekano mdogo sana wa kuyaokoa maisha yake, inabidi afanyiwe upasuaji haraka iwezekanavyo kuweza kuwekewa moyo wa bandia" alisema daktari wa zamu katika kitengo cha moyo kwenye hospitali ile ya rufaa ya jiji la Greenville.

Walimuwahisha na moja kwenye chumba cha upasuaji. Waumini wa kanisa la wateule walikuwa wamejazana nje ya hospitali wakisubiria kufahamu hatma ya maisha ya mchungaji wao mpendwa. Madaktari walikuwa busy wakipambana kuyaokoa maisha ya mchungaji huyo. Operation iliyochukua zaidi ya masaa matatu iliyohusu kupachika moyo wa bandia kwenye mwili wa Mchungaji Masambula ilitekelezwa kikamilifu.

Ni moyo wa bandia walioupachika kifuani kwa mchungaji huyo na kufanikiwa kuunganisha mishipa yote iliyokuwa ikivuja damu. "Kitu cha msingi kilichobaki ni kujitahidi kudhibiti uvujaji wa damu kwani ndio haswa unaweza kusababisha kifo pia inabidi tumuongezee damu chupa nne kwa sababu amepoteza damu nyingi sana." Baada ya operation iliyochukua zaidi ya masaa matatu muujiza ulitendeka, mapigo ya moyo yalirudi upya na damu ikaanza kuzunguka kwenye mwili wa mchungaji Masambula.

Mapigo ya moyo yalikuwa yakiendelea kukaa sawa, Mr Masambula alikuwa amelala kwenye chumba cha wagonjwa mahututi huku akiendelea kupata matibabu watu wachache walikuwa wamemzunguka huku wakiendelea kufuatilia afya yake, alikuwa bado hajazinduka ingawa kila kitu kilionekana kuwa sawa kwa wakati huo. "Mgonjwa anahitaji kupewa nafasi ya kutulia na muda si mrefu ataweza kuzinduka, tumemuwekea moyo wa bandia." alisema dokta mtaalamu wa upasuaji wa moyo.

Ilikuwa ni muujiza ulioje baada ya kuchomolewa moyo wake mchungaji Masambula alikuwa amewekewa moyo wa bandia na uliweza kuanza kufanya kazi. Watu wachache tu ndio walio ruhusiwa kuwa karibu na mgonjwa huyo, watu wengine hawakuruhusiwa kabisa kuwa karibu na mgonjwa huyo kwani ilipaswa kuachwa kwa muda ili aweze kupumzika, alibaki mkewe na madaktari pamoja na watu wengine kadhaa wakaribu. Ulinzi uliimarishwa sana lengo lilikuwa ni kuzuia watu wenye nia mbaya na kupata nafasi ya kumdhuru mgonjwa huyo. Mgonjwa alikuwa akiendelea kupumua kwenye mashine ya oksijeni lakini dalili njema zilionekana kwake.

Muujiza ulitokea! kweli kabisa mgonjwa aliyekuwa akipumua kwa mashine alifungua macho yake akatazama hakuna aliyeweza kuamini, kuanzia nesi wa zamu mpaka madaktari waliokuwa wakimhudumia mgonjwa huyo, wote walikuwa wakishangaa jambo hilo, ulikuwa ni moja kati ya muujiza mkubwa sana kutokea. watu walirukaruka kwa shangwe. "Ashukuriwe Mungu wa mbinguni tunaye muabudu, leo hii amemkumbuka mja wake na kumponya na maumivu makali yaliyokuwa yakimsumbua," alisikika mke wa mchungaji Masambula.

****

Marcus alitoroka na kuingia kwenye gari yake ya kifahari mara baada ya kufanya tukio la hatari la kumuangamiza mchungaji Masambula, aliendesha gari yake mpaka katika mitaa ya Brookside ni mitaa iliyokuwa ikikaliwa na watu matajiri katika jiji la Greenville. Aliingia mpaka kwenye Hoteli fulani iliyokuwa na paking ya chini ya ardhi, mlango ulifunguka na moja kwa moja aliendesha gari yake mpaka chini ya ardhi akaingia ndani na kupaki. Akafungua mlango wa mbele wa ile gari na kupokewa na mzee mmoja wa makamo aliyekuwa amejazia kwa mwili na muonekano wake ingawa pia alivaa msalaba mkubwa kifuani kwake. Alikuwa na walinzi wawili waliokuwa wamejihami kwa silaha za moto.

"Karibu sana Marcus, ni matumaini yangu kuwa kazi niliyokutuma umeifanikisha kikamilifu!" Yule mzee alikuwa amevaa singlendi iliyoacha sehemu kubwa ya kifua chake wazi, mkufu wenye msalaba ulikuwa ukining'inia shingoni pake. "Kazi nimeikamilisha baba askofu, nimefanikiwa kummaliza kabisa mchungaji Masambula," alisema kisha kukabidhi kifurushi kilichokuwa na moyo wa mchungaji yule. Aliupokea na haraka haraka akauingiza kwenye chumba maalum cha kuhifadhi viungo vya binadamu, chumba kilifunguliwa majokofu yaliyosheheni viungo vya binadamu yalikuwa yamepangwa kwenye shelfu za chumba kile, ni biashara kubwa iliyoshika kasi hasa kwa kipindi hicho.

"Inamaana hata mchungaji Masambula alijihusisha biashara hii?" alihoji Marcus. "Ndio, yeye hutumia kivuli cha kupigania dini ili tu aweze kuua watu na kisha kuwachomoa viungo mbalimbali vya miili yao, lengo kuu likiwa ni kufanya biashara hii haramu," alijibu yule mzee. Marcus alikabidhi ule mzigo na kisha kutoka nje haraka akapanda juu na kuingia kwenye hoteli na kubook chumba na kulala kwa usiku huo, hakutaka kabisa kujulikana kwamba yupo kwenye hotel ile ya kifahari.

Mchoaji mahiri wa picha aliingia kwenye chumba cha wagonjwa mahututi (ICU), mchungaji Masambula alikuwa ameshapata fahamu, lengo lilikuwa ni kumhoji ili kuweza kupata sura na muonekano wa yule mtu aliyemfanyia ukatili ule. "Habari naitwa Fortunatus Ndilla, ni mchoraji mashuhuri, nahitaji kufahamu juu ya muonekano wa yule kijana aliye kupiga risasi ili tuweze kutengeneza picha yake," alikuwa amesha toa karatasi yake nyeupe pamoja na penseli tayari kwa kuanza kumchora Marcus.

Kwa taabu sana huku akihema kwa shida, mchungaji Masambula alijibu. "Ndio ninaweza kukuelezea," akaendelea. "Ni kijana aliyekuja ofisini kwangu kwa ajili ya kunifanyia mahojiano na alijitambulisha kama mwandishi wa habari, alikuwa na urefu wa wastani kadirio kama futi tano na nusu hivi." "Ndio sura yake ilikuwaje?" alihoji yule mchoraji. "Alikuwa na sura ndefu na nyembamba kiasi." "Endelea." aliendelea kumhoji huku akianza kumchora yule mtu. "Alikuwa na pua ndefu kiasi, macho yake ni ya kusinzia na alikuwa na nyusi nyembamba, midomo mipana na ndevu kiasi." "Nywele zake zilikuwaje?" "Kipilipili, zilikuwa zimejikunja, rangi ya ngozi yake ilikuwa ni ya maji ya kunde," alimaliza mchungaji Masambula.

Mchoraji alimaliza kazi yake na kwa kipaji alichokuwa nacho, aliweza kuipatia sura ya Marcus kwa zaidi ya asilimia tisini na tano, ilikuwa ni kama amepigwa picha ya passport size. Ndani ya muda mfupi matangazo yenye sura ya Marcus yalikuwa yamesha sambazwa kwenye mbao za matangazo katika jiji lote la Greenville. Wafuasi ya dini ya Wateule walisambaa kila kona ya jiji kumsaka Marcus, kijana aliyesemekana kuwa ni adui yao namba moja kwakuwa aliyahatarisha maisha ya mchungaji wao mpendwa.

****

"Marcus huna namna ya kutoroka hawa vijana wamesambaa kila kona ya mji huu!" Mzee wa makamo aliyekuwa amevaa msalaba mkubwa kifuani mwake alikuwa amesimama kwenye mlango wa chumba alichokuwamo Marcus, huyu mzee alikuwa ni askofu mkuu wa Kanisa la magharibi. Lakini sasa kwa historia Marcus ni nani? hilo swala utalifahamu baadaye. Kwa ufupi tu Marcus alikuwa ni kijana aliyekuwa na mahusiano ya karibu sana na huyu mzee. Mzee aliyekuwa moja ya mawakala wakubwa wa kupokea viungo vya binaadamu, alimiliki ghala kubwa la kisasa la kuhifadhia viungo hivyo, ilikuwa kwenye handaki chini ya ardhi katika hoteli ya Holly Cross, hoteli ya kifahari iliyomilikiwa na kanisa la magharibi.

Alimwonyesha ishara kwa mkono wake na kisha kufungua pazia la dirisha. Wakiwa kwenye ghorofa ya sita walitazama chini, vijana waliokuwa wameshikilia picha ya Marcus walijazana kuizunguka hoteli hiyo. Waliamini kwamba Marcus ni lazima angekuwepo kwenye hoteli ile. Nifuate alisema yule mzee, alimfuata wakaingia kwenye lifti na moja kwa moja walishuka mpaka kwenye floo ya chini ya ardhi, hapo kulikuwa na njia za siri za chini cha chini, walifuata njia hizo wakatembea ili kuwatoroka wale watu.

Walitokea kwenye eneo la mashamba na hapo walikuta gari iliyokuwa ikiwasubiri, ni gari iliyokuwa na namba za usajili wa kibinafsi lakini ilimilikiwa na kanisa la magharibi. Picha ya bikira maria ilionekana kwenye gari hiyo kwa mbele pamoja na rozali iliyokuwa ikining'inia kwa mbele kwenye kioo cha dereva. Waliingia na kukaa siti ya nyuma dereva aliendesha gari. Huko njiani miili ya watu waliokufa ilikuwa imesambaa waliipita na kwakweli hali ilikuwa ikitisha sana.

"Mkuu hali ya usalama ni ndogo sana sidhani kama tutaweza kutoboa kukwepa hawa vijana, ni lazima itumike mbinu fulani." alisema yule dereva. Walitembea na hapo walikutana na kizuizi cha askari wa polisi. "Habari mnaelekea wapi?" alisikika yule askari wa barabarani akimuuliza yule dereva ambapo kwa pembeni aliketi yule mzee aliyekuwa amevaa msalaba mkubwa kifuani kwake, alikuwa ni mhashamu Desmond Matumbo, askofu aliyekuwa na ushawishi mkubwa sana katika eneo hilo.

"Salama kabisa, mimi ni askofu Desmond, tunaelekea kwenye parokia ya Moyo wa Yesu." "Tumsifu Yesu Kristo baba Askofu." Yule askari hakuwa na jinsi zaidi ya kupiga magoti kwa unyenyekevu mkubwa. "Tutembee hakuna haja ya kusimama hapa." aliamrisha yule mzee, dereva alikanyaga mafuta wakatembea mpaka eneo waliloona kuwa ni salama kwao. Ilikuwa ni kwenye eneo la parokia ya moyo wa Yesu, geti kuu la kuingia ndani ya eneo la parokia lilifunguka gari ilitembea mpaka eneo la maegesho ya magari.

Alishuka kijana Marcus akiwa amejifunika kofia huku akiwa amevaa kanzu ndefu yenye rangi ya damu ya mzee. Alitembea mpaka walipoingia kwenye jengo kubwa lililokuwa na nakshi za masanamu na picha mbalimbali za watakatifu, walifika mpaka ndani. Ilionekana kabisa kwamba kijana huyu anafahamiana vyema na watawa wale, kitu kimoja tu kilichomtofautisha nao ni kwamba yeye hakuwa mtawa lakini walimfahamu vyema na waliishi naye kama mwanautume mwenzao. Hawa ndio waliokuwa wakifahamika kama wana utume wa Yesu (Jesuits) waliokuwa wakiendesha shughui zao chini ya mgongo wa kanisa la Kimagharibi.

Padri Leonardo Fernandez alikuwa ni moja kati ya wanautume wa Yesu mwenye asili ya uhispania, huyu aliishi kwenye nyumba ya watawa kama mmisionari. Kitu kimoja tu ambacho watu wachache hawakuweza kutambua juu ya utaalamu wake ni kwamba, padri huyu alikuwa na utaalamu mkubwa katika kutengeneza sura bandia. Alikutana na askofu Desmond na kupewa maelekezo ya siri. "Padri tumsifu yesu kristu." "Milele amina askofu," alimwendea na kisha kubusu pete ya kiaskofu hii ilikuwa ni ishara ya heshima kubwa kwa askofu yule.

"Nimekuja hapa na huyu kijana kwa lengo moja tu, nahitaji, umtengenezee sura ya bandia, na kazi hiyo uifanye mara moja kuanzia sasa," alisema askofu Desmond. "Nakubaliana na maelekezo yako baba Askofu, nitafanya kadiri itakavyo wezekana kukamilisha kazi hii, kutengeneza sura bandia atakayoitumia Marcus ili kujiepusha na mikono ya wale maharamia."

Kazi ya kutengeneza sura ya bandia ilianza mara moja, padri Leonardo Fernandez alikuwa na kazi kubwa kwa siku hiyo, kutengeneza sura itakayomtofautisha kabisa Marcus ili aweze kuwa salama. Alichagua sura iliyokuwa tofauti kabisa kwa kutumia madini ya silikoni aliweza kuumba sura nyingine iliyokuwa tofauti kabisa na sura ya Marcus, zoezi lililochukua takriban siku tatu.

"Hapa sasa utakuwa salama mwanangu," ilikuwa ni sauti yenye lafudhi ya kihispania, alisema hivyo kisha kumkabidhi Marcus ile sura aliyoichonga ili aijaribishe alivaa sura ile na kwakweli ilimkaa vyema na kumfanya kuwa na muonekano wa tofauti kabisa. Hakuna mtu ambaye angeamini kwamba sura ile haikuwa ya kwake Marcus kwani rangi ya sura haikutofautiana hata chembe na rangi yake halisi ya mwili. Aliivaa sura ile na kisha kusimama mbele ya kioo kujitazama. "Yes umepatia Father Leonard, hii itanifaa kabisa!"

Huyu kijana hakuwa mtawa lakini maisha yake mengi aliishi na watawa, hawa walikuwa kama wazazi wake na walizoeana sana, halikuwa jambo rahisi kwa mtu wa kawaida kuishi na watawa wa Kijesuits lakini kwa Marcus hali ilikuwa ni tofauti. Alilelewa katika nyumba ya watoto yatima, akapata elimu katika shule za kanisa na kupelekwa mpaka Roma nchini Italia kusomea theolojia. Kitu kimoja tu alikikataa Marcus, kupokea daraja la upadri kwani hakutaka kuwa mtawa kama baba yake mzazi askofu Desmond Matumbo.

ITAENDELEA...
 
Sijaisoma, wewe si ndio ulikuwa na hadithi ile ya "yaliyokukuta Katika Kijiji cha Kwamsisi" then unataka tukufuate inbox ili utulipishe pesa na ututumie ile hadithi yako iliyobuma? Umepoteza followers humu JF, Hata hii hatutaisimoma. Usiendelee kuiandika tu kwani unapoteza muda wako.
 
Sijaisoma, wewe si ndio ulikuwa na hadithi ile ya "yaliyokukuta Katika Kijiji cha Kwamsisi" then unataka tukufuate inbox ili utulipishe pesa na ututumie ile hadithi yako iliyobuma? Umepoteza followers humu JF, Hata hii hatutaisimoma. Usiendelee kuiandika tu kwani unapoteza muda wako.
mkuu kama una shusha shushaaa
 
SEHEMU YA 02

Gari ya ambulance iliyokuwa imeubeba mwili wa mchungaji Masambula lilizidi kukatiza mitaa ya jiji la Greenville ili kumwahisha hospitali kujaribu kuokoa maisha yake, mchungaji Masambula aliyekuwa amechomolewa moyo wake ilikuwa kanakwamba amesha fariki na hakukuwa na matumaini yoyote kwamba mtumishi huyo wa Mungu angeweza kuyaponya maisha yake kwa namna yeyote ile, hii ni baada ya kushambuliwa na kijana Marcus ambaye aliingia kama mgeni na kumpiga risasi kisha kuuchomoa moyo wake.

Gari iliingia mpaka kwenye hospitali kuu ya rufaa mwili wa mchungaji Masambula ukiwa ndani ya gari hilo alifika mpaka kwenye kitengo cha wagonjwa mahututi na haraka haraka madaktari na wauguzi walimpokea na kisha kumuwahisha kupata huduma stahiki. "Mgonjwa amepoteza damu nyingi na kuna uwezekano mdogo sana wa kuyaokoa maisha yake, inabidi afanyiwe upasuaji haraka iwezekanavyo kuweza kuwekewa moyo wa bandia" alisema daktari wa zamu katika kitengo cha moyo kwenye hospitali ile ya rufaa ya jiji la Greenville.

Walimuwahisha na moja kwenye chumba cha upasuaji. Waumini wa kanisa la wateule walikuwa wamejazana nje ya hospitali wakisubiria kufahamu hatma ya maisha ya mchungaji wao mpendwa. Madaktari walikuwa busy wakipambana kuyaokoa maisha ya mchungaji huyo. Operation iliyochukua zaidi ya masaa matatu iliyohusu kupachika moyo wa bandia kwenye mwili wa Mchungaji Masambula ilitekelezwa kikamilifu.

Ni moyo wa bandia walioupachika kifuani kwa mchungaji huyo na kufanikiwa kuunganisha mishipa yote iliyokuwa ikivuja damu. "Kitu cha msingi kilichobaki ni kujitahidi kudhibiti uvujaji wa damu kwani ndio haswa unaweza kusababisha kifo pia inabidi tumuongezee damu chupa nne kwa sababu amepoteza damu nyingi sana." Baada ya operation iliyochukua zaidi ya masaa matatu muujiza ulitendeka, mapigo ya moyo yalirudi upya na damu ikaanza kuzunguka kwenye mwili wa mchungaji Masambula.

Mapigo ya moyo yalikuwa yakiendelea kukaa sawa, Mr Masambula alikuwa amelala kwenye chumba cha wagonjwa mahututi huku akiendelea kupata matibabu watu wachache walikuwa wamemzunguka huku wakiendelea kufuatilia afya yake, alikuwa bado hajazinduka ingawa kila kitu kilionekana kuwa sawa kwa wakati huo. "Mgonjwa anahitaji kupewa nafasi ya kutulia na muda si mrefu ataweza kuzinduka, tumemuwekea moyo wa bandia." alisema dokta mtaalamu wa upasuaji wa moyo.

Ilikuwa ni muujiza ulioje baada ya kuchomolewa moyo wake mchungaji Masambula alikuwa amewekewa moyo wa bandia na uliweza kuanza kufanya kazi. Watu wachache tu ndio walio ruhusiwa kuwa karibu na mgonjwa huyo, watu wengine hawakuruhusiwa kabisa kuwa karibu na mgonjwa huyo kwani ilipaswa kuachwa kwa muda ili aweze kupumzika, alibaki mkewe na madaktari pamoja na watu wengine kadhaa wakaribu. Ulinzi uliimarishwa sana lengo lilikuwa ni kuzuia watu wenye nia mbaya na kupata nafasi ya kumdhuru mgonjwa huyo. Mgonjwa alikuwa akiendelea kupumua kwenye mashine ya oksijeni lakini dalili njema zilionekana kwake.

Muujiza ulitokea! kweli kabisa mgonjwa aliyekuwa akipumua kwa mashine alifungua macho yake akatazama hakuna aliyeweza kuamini, kuanzia nesi wa zamu mpaka madaktari waliokuwa wakimhudumia mgonjwa huyo, wote walikuwa wakishangaa jambo hilo, ulikuwa ni moja kati ya muujiza mkubwa sana kutokea. watu walirukaruka kwa shangwe. "Ashukuriwe Mungu wa mbinguni tunaye muabudu, leo hii amemkumbuka mja wake na kumponya na maumivu makali yaliyokuwa yakimsumbua," alisikika mke wa mchungaji Masambula.

****

Marcus alitoroka na kuingia kwenye gari yake ya kifahari mara baada ya kufanya tukio la hatari la kumuangamiza mchungaji Masambula, aliendesha gari yake mpaka katika mitaa ya Brookside ni mitaa iliyokuwa ikikaliwa na watu matajiri katika jiji la Greenville. Aliingia mpaka kwenye Hoteli fulani iliyokuwa na paking ya chini ya ardhi, mlango ulifunguka na moja kwa moja aliendesha gari yake mpaka chini ya ardhi akaingia ndani na kupaki. Akafungua mlango wa mbele wa ile gari na kupokewa na mzee mmoja wa makamo aliyekuwa amejazia kwa mwili na muonekano wake ingawa pia alivaa msalaba mkubwa kifuani kwake. Alikuwa na walinzi wawili waliokuwa wamejihami kwa silaha za moto.

"Karibu sana Marcus, ni matumaini yangu kuwa kazi niliyokutuma umeifanikisha kikamilifu!" Yule mzee alikuwa amevaa singlendi iliyoacha sehemu kubwa ya kifua chake wazi, mkufu wenye msalaba ulikuwa ukining'inia shingoni pake. "Kazi nimeikamilisha baba askofu, nimefanikiwa kummaliza kabisa mchungaji Masambula," alisema kisha kukabidhi kifurushi kilichokuwa na moyo wa mchungaji yule. Aliupokea na haraka haraka akauingiza kwenye chumba maalum cha kuhifadhi viungo vya binadamu, chumba kilifunguliwa majokofu yaliyosheheni viungo vya binadamu yalikuwa yamepangwa kwenye shelfu za chumba kile, ni biashara kubwa iliyoshika kasi hasa kwa kipindi hicho.

"Inamaana hata mchungaji Masambula alijihusisha biashara hii?" alihoji Marcus. "Ndio, yeye hutumia kivuli cha kupigania dini ili tu aweze kuua watu na kisha kuwachomoa viungo mbalimbali vya miili yao, lengo kuu likiwa ni kufanya biashara hii haramu," alijibu yule mzee. Marcus alikabidhi ule mzigo na kisha kutoka nje haraka akapanda juu na kuingia kwenye hoteli na kubook chumba na kulala kwa usiku huo, hakutaka kabisa kujulikana kwamba yupo kwenye hotel ile ya kifahari.

Mchoaji mahiri wa picha aliingia kwenye chumba cha wagonjwa mahututi (ICU), mchungaji Masambula alikuwa ameshapata fahamu, lengo lilikuwa ni kumhoji ili kuweza kupata sura na muonekano wa yule mtu aliyemfanyia ukatili ule. "Habari naitwa Fortunatus Ndilla, ni mchoraji mashuhuri, nahitaji kufahamu juu ya muonekano wa yule kijana aliye kupiga risasi ili tuweze kutengeneza picha yake," alikuwa amesha toa karatasi yake nyeupe pamoja na penseli tayari kwa kuanza kumchora Marcus.

Kwa taabu sana huku akihema kwa shida, mchungaji Masambula alijibu. "Ndio ninaweza kukuelezea," akaendelea. "Ni kijana aliyekuja ofisini kwangu kwa ajili ya kunifanyia mahojiano na alijitambulisha kama mwandishi wa habari, alikuwa na urefu wa wastani kadirio kama futi tano na nusu hivi." "Ndio sura yake ilikuwaje?" alihoji yule mchoraji. "Alikuwa na sura ndefu na nyembamba kiasi." "Endelea." aliendelea kumhoji huku akianza kumchora yule mtu. "Alikuwa na pua ndefu kiasi, macho yake ni ya kusinzia na alikuwa na nyusi nyembamba, midomo mipana na ndevu kiasi." "Nywele zake zilikuwaje?" "Kipilipili, zilikuwa zimejikunja, rangi ya ngozi yake ilikuwa ni ya maji ya kunde," alimaliza mchungaji Masambula.

Mchoraji alimaliza kazi yake na kwa kipaji alichokuwa nacho, aliweza kuipatia sura ya Marcus kwa zaidi ya asilimia tisini na tano, ilikuwa ni kama amepigwa picha ya passport size. Ndani ya muda mfupi matangazo yenye sura ya Marcus yalikuwa yamesha sambazwa kwenye mbao za matangazo katika jiji lote la Greenville. Wafuasi ya dini ya Wateule walisambaa kila kona ya jiji kumsaka Marcus, kijana aliyesemekana kuwa ni adui yao namba moja kwakuwa aliyahatarisha maisha ya mchungaji wao mpendwa.

****

"Marcus huna namna ya kutoroka hawa vijana wamesambaa kila kona ya mji huu!" Mzee wa makamo aliyekuwa amevaa msalaba mkubwa kifuani mwake alikuwa amesimama kwenye mlango wa chumba alichokuwamo Marcus, huyu mzee alikuwa ni askofu mkuu wa Kanisa la magharibi. Lakini sasa kwa historia Marcus ni nani? hilo swala utalifahamu baadaye. Kwa ufupi tu Marcus alikuwa ni kijana aliyekuwa na mahusiano ya karibu sana na huyu mzee. Mzee aliyekuwa moja ya mawakala wakubwa wa kupokea viungo vya binaadamu, alimiliki ghala kubwa la kisasa la kuhifadhia viungo hivyo, ilikuwa kwenye handaki chini ya ardhi katika hoteli ya Holly Cross, hoteli ya kifahari iliyomilikiwa na kanisa la magharibi.

Alimwonyesha ishara kwa mkono wake na kisha kufungua pazia la dirisha. Wakiwa kwenye ghorofa ya sita walitazama chini, vijana waliokuwa wameshikilia picha ya Marcus walijazana kuizunguka hoteli hiyo. Waliamini kwamba Marcus ni lazima angekuwepo kwenye hoteli ile. Nifuate alisema yule mzee, alimfuata wakaingia kwenye lifti na moja kwa moja walishuka mpaka kwenye floo ya chini ya ardhi, hapo kulikuwa na njia za siri za chini cha chini, walifuata njia hizo wakatembea ili kuwatoroka wale watu.

Walitokea kwenye eneo la mashamba na hapo walikuta gari iliyokuwa ikiwasubiri, ni gari iliyokuwa na namba za usajili wa kibinafsi lakini ilimilikiwa na kanisa la magharibi. Picha ya bikira maria ilionekana kwenye gari hiyo kwa mbele pamoja na rozali iliyokuwa ikining'inia kwa mbele kwenye kioo cha dereva. Waliingia na kukaa siti ya nyuma dereva aliendesha gari. Huko njiani miili ya watu waliokufa ilikuwa imesambaa waliipita na kwakweli hali ilikuwa ikitisha sana.

"Mkuu hali ya usalama ni ndogo sana sidhani kama tutaweza kutoboa kukwepa hawa vijana, ni lazima itumike mbinu fulani." alisema yule dereva. Walitembea na hapo walikutana na kizuizi cha askari wa polisi. "Habari mnaelekea wapi?" alisikika yule askari wa barabarani akimuuliza yule dereva ambapo kwa pembeni aliketi yule mzee aliyekuwa amevaa msalaba mkubwa kifuani kwake, alikuwa ni mhashamu Desmond Matumbo, askofu aliyekuwa na ushawishi mkubwa sana katika eneo hilo.

"Salama kabisa, mimi ni askofu Desmond, tunaelekea kwenye parokia ya Moyo wa Yesu." "Tumsifu Yesu Kristo baba Askofu." Yule askari hakuwa na jinsi zaidi ya kupiga magoti kwa unyenyekevu mkubwa. "Tutembee hakuna haja ya kusimama hapa." aliamrisha yule mzee, dereva alikanyaga mafuta wakatembea mpaka eneo waliloona kuwa ni salama kwao. Ilikuwa ni kwenye eneo la parokia ya moyo wa Yesu, geti kuu la kuingia ndani ya eneo la parokia lilifunguka gari ilitembea mpaka eneo la maegesho ya magari.

Alishuka kijana Marcus akiwa amejifunika kofia huku akiwa amevaa kanzu ndefu yenye rangi ya damu ya mzee. Alitembea mpaka walipoingia kwenye jengo kubwa lililokuwa na nakshi za masanamu na picha mbalimbali za watakatifu, walifika mpaka ndani. Ilionekana kabisa kwamba kijana huyu anafahamiana vyema na watawa wale, kitu kimoja tu kilichomtofautisha nao ni kwamba yeye hakuwa mtawa lakini walimfahamu vyema na waliishi naye kama mwanautume mwenzao. Hawa ndio waliokuwa wakifahamika kama wana utume wa Yesu (Jesuits) waliokuwa wakiendesha shughui zao chini ya mgongo wa kanisa la Kimagharibi.

Padri Leonardo Fernandez alikuwa ni moja kati ya wanautume wa Yesu mwenye asili ya uhispania, huyu aliishi kwenye nyumba ya watawa kama mmisionari. Kitu kimoja tu ambacho watu wachache hawakuweza kutambua juu ya utaalamu wake ni kwamba, padri huyu alikuwa na utaalamu mkubwa katika kutengeneza sura bandia. Alikutana na askofu Desmond na kupewa maelekezo ya siri. "Padri tumsifu yesu kristu." "Milele amina askofu," alimwendea na kisha kubusu pete ya kiaskofu hii ilikuwa ni ishara ya heshima kubwa kwa askofu yule.

"Nimekuja hapa na huyu kijana kwa lengo moja tu, nahitaji, umtengenezee sura ya bandia, na kazi hiyo uifanye mara moja kuanzia sasa," alisema askofu Desmond. "Nakubaliana na maelekezo yako baba Askofu, nitafanya kadiri itakavyo wezekana kukamilisha kazi hii, kutengeneza sura bandia atakayoitumia Marcus ili kujiepusha na mikono ya wale maharamia."

Kazi ya kutengeneza sura ya bandia ilianza mara moja, padri Leonardo Fernandez alikuwa na kazi kubwa kwa siku hiyo, kutengeneza sura itakayomtofautisha kabisa Marcus ili aweze kuwa salama. Alichagua sura iliyokuwa tofauti kabisa kwa kutumia madini ya silikoni aliweza kuumba sura nyingine iliyokuwa tofauti kabisa na sura ya Marcus, zoezi lililochukua takriban siku tatu.

"Hapa sasa utakuwa salama mwanangu," ilikuwa ni sauti yenye lafudhi ya kihispania, alisema hivyo kisha kumkabidhi Marcus ile sura aliyoichonga ili aijaribishe alivaa sura ile na kwakweli ilimkaa vyema na kumfanya kuwa na muonekano wa tofauti kabisa. Hakuna mtu ambaye angeamini kwamba sura ile haikuwa ya kwake Marcus kwani rangi ya sura haikutofautiana hata chembe na rangi yake halisi ya mwili. Aliivaa sura ile na kisha kusimama mbele ya kioo kujitazama. "Yes umepatia Father Leonard, hii itanifaa kabisa!"

Huyu kijana hakuwa mtawa lakini maisha yake mengi aliishi na watawa, hawa walikuwa kama wazazi wake na walizoeana sana, halikuwa jambo rahisi kwa mtu wa kawaida kuishi na watawa wa Kijesuits lakini kwa Marcus hali ilikuwa ni tofauti. Alilelewa katika nyumba ya watoto yatima, akapata elimu katika shule za kanisa na kupelekwa mpaka Roma nchini Italia kusomea theolojia. Kitu kimoja tu alikikataa Marcus, kupokea daraja la upadri kwani hakutaka kuwa mtawa kama baba yake mzazi askofu Desmond Matumbo.

ITAENDELEA...
Leta habari
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom