Simuamini tena mke wangu!

naomba no yake ya simu nimshauri vizuri labda umeshindwa kuongea nae vizuri
 
Mimi na wife tumebahatika kupata watoto 2 wa kiume! Mm nafanya kazi dsm yy anafanyia mara. kijana wetu yupo grade 1 kwenye hizi academy! Takriban wiki kadhaa nilienda kumsabahi! Nije kwenye pt niligundua amekuwa akiwatumia ndg zake pesa nyingi paspo kunijulisha nahc kuna business wanafanya yy na dadake! Niligundua baada ya kumwambia kwamba mm kulingana na ujio wangu siko fresh kiuchumi hivo jitahidi ada ya mtoto make ndo wanafungua mwezi wa tisa kwa kifupi alinipa majibu ya kunikatisha tamaa akadai hana hela na isitoshe kwenye ubini wa mtoto anaandikwa yy au mm? Km sitaki kumsomesha akae nyumbani! Nikamuuliza km waweza tumia ndg zako malaki ya pesa unashimdwa nn kumlipia mwanao? Akakanusha wakati mm nilicheki kwenye mpesa ametuma pesa two times tena last month! Tukazinguana sana mm nikapanda basi nikasepa kwa ufupi hana mpango wa kusaidiana na mm ktk kusukuma gurudumu! Nimfanyaje mke wa namna hii?

Iisee for money haina noma kama ulimkuta kasomeshwa mbya kama na KIDUMU hiyo noumer.
 
Mwanamme anaependa kuteleza utamjua tuu! hahahahaaaa.....kidding!. ameeleza kweli huyo baby hapo juu

Bila kuteleza michubuko bhana!!!!!!!

Yaaani kweli pato la.mke liishie kwa braider na pedicure!!!
Familia mipango mamy sio club ya tendo la ndoa kula na kulala ni unit for production and consumption sasa kama jitu kupe hata unapoomba msaada mpaka tindo!!!!!!!

Ha ha haaaa kuna rafiki yangu anawaita kota pini yaani kuingia nyundo na kutoka nyundo!!!!
 
Najua kiasi gani anapata na anaweza kumlipia huyu mtoto isitoshe hata elimu aliyonayo nimechangia sana mpaka anafikia hapa alipofikia! Baada ya kugraduate na kukaa home huku ajira zikiwa magumashi hatiwae fursa ikapatikana huko tukashauriana kulikoni kukaa nyumban bora aende huko halafu tutafanya uhamisho mabadiliko ya kitabia yameanza ndan ya miezi miwili hii ya karibuni! Anyway sintojali sana

Dah kila nikisoma hizi posts zako naona huzuni! Inaelekea wewe mstaarabu sana. Nakushauri usikate tamaa na huyu mke, mna watoto!
 
Mkuu, mi nakushauri hivi, mwambie aache kazi na awe mama wa nyumbani, hi italeta heshima hata kwao cause hadi pichu itanunuliwa kwa cost code yako.

Mazindu huu ni unyanyasaji aisee! kuomba hela ya kufuli, saloon, pads, wanja , lipstick, perfume, we mwnyw utachemka lol! Utasema bora angekuwa na kazi ajihudumie mwnyw
 
Mimi na wife tumebahatika kupata watoto 2 wa kiume! Mm nafanya kazi dsm yy anafanyia mara. kijana wetu yupo grade 1 kwenye hizi academy! Takriban wiki kadhaa nilienda kumsabahi! Nije kwenye pt niligundua amekuwa akiwatumia ndg zake pesa nyingi paspo kunijulisha nahc kuna business wanafanya yy na dadake! Niligundua baada ya kumwambia kwamba mm kulingana na ujio wangu siko fresh kiuchumi hivo jitahidi ada ya mtoto make ndo wanafungua mwezi wa tisa kwa kifupi alinipa majibu ya kunikatisha tamaa akadai hana hela na isitoshe kwenye ubini wa mtoto anaandikwa yy au mm? Km sitaki kumsomesha akae nyumbani! Nikamuuliza km waweza tumia ndg zako malaki ya pesa unashimdwa nn kumlipia mwanao? Akakanusha wakati mm nilicheki kwenye mpesa ametuma pesa two times tena last month! Tukazinguana sana mm nikapanda basi nikasepa kwa ufupi hana mpango wa kusaidiana na mm ktk kusukuma gurudumu! Nimfanyaje mke wa namna hii?

Wachukue watoto kisiri na ukafanye DNA. Baada ya kupata majibu ndio fanya maamuzi magumu. Kama ni wa kwako mwambie aanze mbele akakae na ndugu zake anakotuma pesa kuliko kumlipia mwanae. Kama si wa kwako, yeye na watoto waanze mbele uone kama hatatoa hiyo pesa.

Hivi wewe ndugu zako unawatumia pesa? Tuma tena si lazima kila wakati ajue umetuma. Ukitaja issue ya DNA, akili yake mbona itarudi kwenye mstari!
 
Haya ni matatizo ya kufunga ndoa na kutokuishi pamoja.

Hyo jeuri ya kukujibu hivyo anaitoa wapi lolz?

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Sijawahi kuacha kutekeleza majukumu yangu km baba wife nilimwambia mapema kuhusu swala la ada na mipango ya mwezi huu hata ya mwezi ujao anaijua vema kabisa lkn leo ndo tulienda benki nikamwambia ndo ugomvi ukawa mkubwa nimekausha mpaka ss baada ya kuona msimamo wangu anadai tujadiliane na tupange sijasema lolote!
 
Mnajulikana chako chako changu cha familia sio fair.

Msinung'unike sana, ndiyo mgawanyo wa majukumu! Khaa mmezidi sasa, yaani kutuhonga mshindwe, kubeba mimba na kuzaa hamuwezi,kupika, kufua, kudeki, kuosha vyombo, kulea watoto mnategea, kuwa waaminifu hamuwezi, sasa mnaweza nini nyie? Kazi yenu ni kugegeda tuuu? Msitulazimishe kuwakosea heshima! Msiweke sheria hizo bana, vitu vingine mnamezea!
 
Chanzo cha migogoro kwenye ndoa ni Pesa na Mapenzi
  1. Wanawake wengi wanapenda wapewe uhuru wa kufanya kazi. Lakini walio wengi wakishapata kipato wanakitumia kujipendezesha na kujijenga kwenye familia walikotokea - si walikoolewa.
  2. Wanawake wengi hawapendi kuchangia matumizi ya nyumbani - hata kama mapato yao ni makubwa kuliko ya mme. Wanapenda ile model ya mme kufadhili kila kitu, lakini hawapendi matokeo ya model hiyo - mme kuwa na maamuzi ya mwisho juu ya hatima ya familia
  3. Wanawake wengi wanapenda kushiriki na kufanya maamuzi juu ya kipato cha mme. Lakini hawapendi kabisa mme ajihusishe na mapato wanaopata wao - wanasema wakati unaoa ulijua kuwa utahimili familia.
  4. Wanawake wengi mwanzoni huwa wako flexible sana. Ila wanapokuwa kwenye ndoa wanashauriana sana na wenzao na hapo wengi hubadirika sana mbele - hasa naona mwanamke akishapata watoto wawili huwa ni turning point.

Mambo hayo husababisha migogoro sana kwenye ndoa nyingi.
 
Pole mkuu. Huyu mama amezidi mtoto wake wa kuzaa ashindwe kumlipia ada..tena kwa sababu mmewe amekwama, sasa anafanya kazi ya nini. Si aache kazi basi awe mama wa nyumbani.
 
Haya ndiyo matatizo ya wanaume wa cku hizi wanaoa wanawake wenye kazi ili kupunguziwa majukumu yao! Aaaagh! Kwani kutuma pesa home ni tatizo? Labda kama hajakushriksha! Je,mlikubalianaje kuhusu matumizi yenu ya pesa?au umemkurupusha tu?afterall mwanaume ndiye mwenye jukumu la kutunza familia zakwangu nitatoa nikiamua tena penye ulazima eboo! usilalamike kakope! ndo uanaume huo!
...unaaibisha wanawake wenzako bana....
 
Wanamme ndio mnasapoti huu ujinga, sijui ili kulinda ego zenu.

Hivi kwa resourse chache zilizo ndani ya familia, unaruhusuje pesa ya mkeo iwe inachezewa? Mtaanza ku-investi lini? Mie naona mnasapoti ujinga, ujinga tena ujinga.

Ndio maana familia nyingi zinasumbuliwa na umaskini wa hiari, eti hela ya mke ni yake tu.
Wengi mkuu wameshapata shida kwa kujadili au kuulizia hela za wake zao! ni wanawake wachache wenye mioyo ya kuwashirikisha waume zao katika vipato vyao, na hiyo basi mpaka wao wapende wenyewe!! ndio hali halisi hata kama hatupendi hatuwezi kukwepa!!
 
Wala tatizo si pesa, tatizo ni hakuna mawasiliano kati yenu.

Mie siwezi samehe mwenza anayetuma pesa kwao bila kunishikisha, awe mke au mume.

Na kwa kujibu, eti kwani ubini umeandikwa wa nani, tayari keshakupanda kichwani, sioni pa kumrekebisha zaidi ya kuvumilia tu kwa hatua aliyofikia.

Hata siku moja siwezi mjibu baba nani eti kwani ubini wa nani. Mume ana heshima yake jamani, khah!
...ur brainy women...hata kwenye majibu ya mke wa jama....inaonekana kuna shida....
 
PesA aliyotumia ndugu zake ulimpa?au kaitokea jasho.hahhaha wanaume bwana.we unafanys kazi mbona hujatwambia pesa unapeleka wapi? Inaonekana hata hapo nyumbani hujui wanachokula wanatoa wapi na ndio mana kakujibu hiv yo na ndio maana kaamua kudeal na ndugu zake
...angebaki kwao basi...wanawake wa siku hizi mana matatizo gani...?
 
Back
Top Bottom