MaxShimba
JF-Expert Member
- Apr 11, 2008
- 35,772
- 4,054
Simba yamong'onyolewa Mwanza
@Yashindiliwa 4-1 na Toto Africans
Na Mwandishi Wetu
TIMU ya Simba jana iliwalaza mapema mamia ya mashabiki wake baada ya kukubali kipigo kitakatifu cha mabao 4-1 kutoka kwa Toto Africans katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, mjini Mwanza.
Katika mchezo huo, askari wa kutuliza ghasia waliingilia kati kuwaokoa wachezaji na viongozi waliokaa kwenye benchi la ufundi baada ya mashabiki waliojawa na hasira kuvurumisha mvua ya mawe baada ya timu hiyo kuchapwa bao la tatu.
Simba inatarajiwa kuvaana na wapinzani wao wakubwa Yanga katika mchezo wa Ligi Kuu unaotarajiwa kufanyika Jumapili ijayo kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Toto Africans ikiwa chini ya Kocha Mkuu, Mbwana Makata ilianza kuhesabu bao la kwanza dakika ya nane ya mchezo lililofungwa kwa kichwa na mchezaji, Juma Seif. Seif aliyekuwa mwiba mkali kwa mabeki wa Simba aliipatia timu yake bao la pili.
Uzembe wa mabeki wa Simba uliigharimu timu hiyo baada ya kuiruhusu Toto kupata bao la tatu lililofungwa dakika 44 na Oscar Joshua.
Saidi Dilunga alihitimisha kipigo cha mabao kutoka kwa vijana hao wa Msimbani baada ya kufunga bao la nne dakika 82.
Simba ilipata bao la kufutia machozi dakika mbili kabla ya mpira (Tusi)(Tusi)(Tusi)(Tusi)lizika kwa mkwaju wa penalti iliyofungwa na mshambuliaji kutoka Nijeria, Orji Obinna.
Baada ya mchezo huo, Kocha Mkuu wa Simba Kasmir Bezisnki alisema safu ya ulinzi ya timu hiyo ilicheza chini ya kiwango kwa kuruhusu mabao ya kizembe.
Katika mchezo mwingine wa michuano hiyo uliofanyika kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, timu ya Kagera Sugar iliichapa Azam United mabao 2-1.
Tuma kwa Rafiki Nakala inayochapika