Kuelekea Derby ya Simba na Young Africans, hebu tuangalie hii tofauti kati Kocha Robertinho na Gamondi

Kurunzi

JF-Expert Member
Jul 31, 2009
9,287
9,923
Kuelekea Mchezo wa Derby ya Kariakoo inayotegemewa kuchezwa jumapili Movembe 5, 2023

Hebu tuangalie Staili ya kucheza ya makocha hawa Miguel Gamondi wa Young Africans na Roberhno wa Simba

Tukianza na Kocha Gamondi Staili yake ya kucheza inamvutia shabiki yeyote ambaye anataka kutazama soka safi, amekuwa akiitengeneza timu yake kucheza mchezo wa kuvutia kwenye kila mechi, pasi nyingi, kosa kosa nyingi na zaidi mpira wa burudani, Hii ni staili bora ambayo mashabiki wanaipenda na amekuwa na uwezo wa kubadilika kwenye kila mchezo kwenye eneo la ushambuliaji, kiungo na hata mabeki kutokana na kikosi chake kuwa na watu wengi.

Siyo jambo la ajabu kucheza bila mshambuliaji kwenye mechi zake, siyo ajabu kumuona Mzize akianza na siyo ajabu kumuona akiwatumia mabeki watatu badala ya wanne kama ilivyokuwa kwenye mchezo dhidi ya Azam.

Kwa upande wa Kocha wa Simba Robertinho, amekuwa tofauti na Gamondi msimu huu timu yake haijacheza mechi hata moja ikivutia, lakini ni timu ambayo ni ngumu kupoteza mchezo kwenye dakika tisini pamoja na kwamba imekuwa ikiruhusu mabao mengi kwenye timu yake.

Robertinho amekuwa akibadili kikosi chake kila kila kinachopata bao au kinaporuhusu bao kwenye mchezo wowote, ni kocha ambaye analinda alichonacho, huku Gamondi akiendelea kutafuta kitu kipya hata baada ya kupata, akifunga bao moja anatafuta la pili, Robertinho akifunga moja analilinda hilohilo.
 
Madunduka msimu huu baada ya kugundua wamebolonga kwenye usajili..nguvu zoote wameelekeza kwenye ushirikina.

Hivyo kinachombeba kocha mburazil ni ushirikina na hawana kubeza timu yoyote wanayokutana nayo, hata wakikutana na timu ya jiji wapo sambamba na mganga wao.

Otopolo wasipoamka kwa kujivunia kina pakome tu watakuja wajute.
 
Kuelekea Mchezo wa Derby ya Kariakoo iyotegemewa kuchezwa jumapili Movembe 5, 2023

Hebu tuangalie Staili ya kucheza ya makocha hawa Miguel Gamondi wa Young Africans na Roberhno wa Simba

Tukianza na Kocha Gamondi Staili yake ya kucheza inamvutia shabiki yeyote ambaye anataka kutazama soka safi, amekuwa akiitengeneza timu yake kucheza mchezo wa kuvutia kwenye kila mechi, pasi nyingi, kosa kosa nyingi na zaidi mpira wa burudani, Hii ni staili bora ambayo mashabiki wanaipenda na amekuwa na uwezo wa kubadilika kwenye kila mchezo kwenye eneo la ushambuliaji, kiungo na hata mabeki kutokana na kikosi chake kuwa na watu wengi.

Siyo jambo la ajabu kucheza bila mshambuliaji kwenye mechi zake, siyo ajabu kumuona Mzize akianza na siyo ajabu kumuona akiwatumia mabeki watatu badala ya wanne kama ilivyokuwa kwenye mchezo dhidi ya Azam.

Kwa upande wa Kocha wa Simba Robertinho, amekuwa tofauti na Gamondi msimu huu timu yake haijacheza mechi hata moja ikivutia, lakini ni timu ambayo ni ngumu kupoteza mchezo kwenye dakika tisini pamoja na kwamba imekuwa ikiruhusu mabao mengi kwenye timu yake.

Robertinho amekuwa akibadili kikosi chake kila kila kinachopata bao au kinaporuhusu bao kwenye mchezo wowote, ni kocha ambaye analinda alichonacho, huku Gamondi akiendelea kutafuta kitu kipya hata baada ya kupata, akifunga bao moja anatafuta la pili, Robertinho akifunga moja analilinda hilohilo.

Uchambuzi mzuri sana mkuu.
Nikuongezee kitu.

Silaha kubwa kuliko zoye ya kudefence (kujilinda) ni kushambulia.

Silaha kubwa ya pili ni kumiliki mpira.

Hakuna kocha asiyependa kuona timu yake inapiga pasi nyingi sana ianashambulia kwa kasi ,kumiliki mchezo na ku udominate possesion kwa asilimia 80 kwa 20.

Ni wachezaji wenye uwezo mbovu alionao ndio wanamfanya abadili mfumo na kuita Objective football
Wachezaji kama kibu, saido, kanute uwezo wao wa kupiga pass ni mdogo sana wanapoteza mpira kila mala
( Ila workrate yao ni kubwa zaidi uwanjani ndio wachezaji wagumu zsidi uwanjani na wapo kila sehemu.

Nadhani simba watafanya sajili Dirisha Dogo ili kiweza kurudi kwenye ubora wao
Wakipata kiungo kama Lwanga na no 10 wa kuchukua nafasi ya Saido watakuwa na timu nzuri zaidi.

Karibu
 
Yanga wanakaba mtu kwa mtu/man to man na wanapopoteza mipira hawawapi maadui nafasi ya kumiliiki. Kwa upande mwingine Simba wanakaba nafasi na hivyo kuruhusu time pinzani kumiliiki mipra Kwa muda mrefu (sio Ile Mpira biliani tena). Na Hilo limetugharimu mechi nyingi ikiwemo zile na All ahily.
 
gamondi anahaki yakutamba kwasababu anakikosi kipana kile mchezaji anakitu labda wachezaji wachache tuu bado hawajajipata.

Mpira haupo hivyo mkuu.
Gamondi ndie anaiogopa zaidi simba ameenda zaidi ya mala tatu uwanjani kuisoma.

Gamondi ana Deni la kupoteza mchezo Muhimu wa ngao ya jamii uliopita na kumpa simba ubingwa pia amepoteza mchezo wa Ligi na Ihefu.

Robertinho ana Muda mrefu na simba.
Hajawahi kufungwa na Yanga tangu uganda.

Timu yake ina Avantage imecheza michezo mikubwa hapa karibuni ni zoezi zuri kuelekea Dabi
Kutoa sale na Alhly michezo miwili hiyo timu si ya kubeza.

Kiutaalam simba ni Favourate zaidi.
 
Yanga wanakaba mtu kwa mtu/man to man na wanapopoteza mipira hawawapi maadui nafasi ya kumiliiki. Kwa upande mwingine Simba wanakaba nafasi na hivyo kuruhusu time pinzani kumiliiki mipra Kwa muda mrefu (sio Ile Mpira biliani tena). Na Hilo limetugharimu mechi nyingi ikiwemo zile na All ahily.

Simba hawana kiungo mkabaji hivyo hawawezi kukaba man to man.

Viungo wa simba ni Box to box wao ni kishambulia na kurudi kila wakati.

Wanashambulia nafasi na wanarudi kuziba nafasina si mtu.

Kuhusu alhly ile ni timu No 1 Africa usisikitike sana kutolewa na timu No 1
Pili simba haina Golikipa walizingua kwenye usajili.

Hope utakuwa umenielewa.......
 
Mpira haupo hivyo mkuu.
Gamondi ndie anaiogopa zaidi simba ameenda zaidi ya mala tatu uwanjani kuisoma.

Gamondi ana Deni la kupoteza mchezo Muhimu wa ngao ya jamii uliopita na kumpa simba ubingwa pia amepoteza mchezo wa Ligi na Ihefu.

Robertinho ana Muda mrefu na simba.
Hajawahi kufungwa na Yanga tangu uganda.

Timu yake ina Avantage imecheza michezo mikubwa hapa karibuni ni zoezi zuri kuelekea Dabi
Kutoa sale na Alhly michezo miwili hiyo timu si ya kubeza.

Kiutaalam simba ni Favourate zaidi.

dakika 90 sio nyingi tuwe wapole ila nakuambia yanga anashinda.
 
dakika 90 sio nyingi tuwe wapole ila nakuambia yanga anashinda.

Mimi naongea kiufundi siwezi nikasema simba anashinda au yanga anashida.

Mimi naongelea wachezaji na kocha mifumo na mbinu zao

Siwezi kujipa Uungu, unabii ,utabiri,unajimu uchawi nk

Anayejua matokeo ya mwisho yatakuaje ni Mungu tu.
 
Uchambuzi mzuri sana mkuu.
Nikuongezee kitu.

Silaha kubwa kuliko zoye ya kudefence (kujilinda) ni kushambulia.

Silaha kubwa ya pili ni kumiliki mpira.

Hakuna kocha asiyependa kuona timu yake inapiga pasi nyingi sana ianashambulia kwa kasi ,kumiliki mchezo na ku udominate possesion kwa asilimia 80 kwa 20.

Ni wachezaji wenye uwezo mbovu alionao ndio wanamfanya abadili mfumo na kuita Objective football
Wachezaji kama kibu, saido, kanute uwezo wao wa kupiga pass ni mdogo sana wanapoteza mpira kila mala
( Ila workrate yao ni kubwa zaidi uwanjani ndio wachezaji wagumu zsidi uwanjani na wapo kila sehemu.

Nadhani simba watafanya sajili Dirisha Dogo ili kiweza kurudi kwenye ubora wao
Wakipata kiungo kama Lwanga na no 10 wa kuchukua nafasi ya Saido watakuwa na timu nzuri zaidi.

Karibu
Hiv Tadeo yuko wap now???huyu mwamba nmemkumbuka sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuelekea Mchezo wa Derby ya Kariakoo iyotegemewa kuchezwa jumapili Movembe 5, 2023

Hebu tuangalie Staili ya kucheza ya makocha hawa Miguel Gamondi wa Young Africans na Roberhno wa Simba

Tukianza na Kocha Gamondi Staili yake ya kucheza inamvutia shabiki yeyote ambaye anataka kutazama soka safi, amekuwa akiitengeneza timu yake kucheza mchezo wa kuvutia kwenye kila mechi, pasi nyingi, kosa kosa nyingi na zaidi mpira wa burudani, Hii ni staili bora ambayo mashabiki wanaipenda na amekuwa na uwezo wa kubadilika kwenye kila mchezo kwenye eneo la ushambuliaji, kiungo na hata mabeki kutokana na kikosi chake kuwa na watu wengi.

Siyo jambo la ajabu kucheza bila mshambuliaji kwenye mechi zake, siyo ajabu kumuona Mzize akianza na siyo ajabu kumuona akiwatumia mabeki watatu badala ya wanne kama ilivyokuwa kwenye mchezo dhidi ya Azam.

Kwa upande wa Kocha wa Simba Robertinho, amekuwa tofauti na Gamondi msimu huu timu yake haijacheza mechi hata moja ikivutia, lakini ni timu ambayo ni ngumu kupoteza mchezo kwenye dakika tisini pamoja na kwamba imekuwa ikiruhusu mabao mengi kwenye timu yake.

Robertinho amekuwa akibadili kikosi chake kila kila kinachopata bao au kinaporuhusu bao kwenye mchezo wowote, ni kocha ambaye analinda alichonacho, huku Gamondi akiendelea kutafuta kitu kipya hata baada ya kupata, akifunga bao moja anatafuta la pili, Robertinho akifunga moja analilinda hilohilo.
chuki na wivu na inaonyesha wew ni utopolo uliyejificha kwenye kivuli cha kujadili makocha hawa wawili
 
Madunduka msimu huu baada ya kugundua wamebolonga kwenye usajili..nguvu zoote wameelekeza kwenye ushirikina.

Hivyo kinachombeba kocha mburazil ni ushirikina na hawana kubeza timu yoyote wanayokutana nayo, hata wakikutana na timu ya jiji wapo sambamba na mganga wao.

Otopolo wasipoamka kwa kujivunia kina pakome tu watakuja wajute.
Jana tu Mudathir kapigwa faini ya 2m kwa Ushirikina. Sasa sijui Mudathir anachezea wapi?
 
Back
Top Bottom