Sizinga
Platinum Member
- Oct 30, 2007
- 9,101
- 6,027
Shirikisho lisilo la serikali la kufanya utetezi wa huduma bora za Afya SIKIKA limeponda mkutano wa Bunge la Bajeti liksema lifupishwe badala ya kumalizika August 30. Vikao kwa miezi 3 havina maana yoyote na ni mojawapo ya matumizi mabaya ya fedha za mlipa kodi kwani kwa mwaka jana bubget la Bajeti lilidumu kwa wiki 5 tu ili kuruhusu maandalizi michakato ya Uchaguzi na hadi hivi sasa hatujasikia madhara yatokayo na kupunguzwa kwa muda ule wa Bunge.
SIKIKA haioni umuhimu wa hii mijadala mirefu baada ya kupitishwa kwa bajeti. Mkutano wa bajeti ni mrefu na sio wamsingi zaidi ya kumaliza fedha za umma. Kwanini wajadili kitu ambacho kimeshapitishwa??Mkurugenzi Irene Kiria alihoji.
Bajeti ilivyowasilishwa,wabunge waliijadili kwa wiki moja na ikapitishwa juni 21 na kwa mujibu wa katiba,kama bajeti isingepitishwa basi Rais angelivunja Bunge. Aliongeza kuwa mijadala ya wizara itakoyokuwa kwa miezi hiyo 3 haina nguvu ya kuipinga/au kufanya mabadiliko yoyote ya maana katika bajeti ambayo tayari ilishapitishwa na wabunge na Mabadiliko yote ilibidi yafanywe wakati kamati za bunge zilipokutana na serikali.
So kwa mantiki hiyo wabunge waende nyumbani na wakome kuendelea kutumbua fedha za walipa kodi kwa miezi yote hiyo 3 kwa mijadala isiyo na Tija.
SIKIKA haioni umuhimu wa hii mijadala mirefu baada ya kupitishwa kwa bajeti. Mkutano wa bajeti ni mrefu na sio wamsingi zaidi ya kumaliza fedha za umma. Kwanini wajadili kitu ambacho kimeshapitishwa??Mkurugenzi Irene Kiria alihoji.
Bajeti ilivyowasilishwa,wabunge waliijadili kwa wiki moja na ikapitishwa juni 21 na kwa mujibu wa katiba,kama bajeti isingepitishwa basi Rais angelivunja Bunge. Aliongeza kuwa mijadala ya wizara itakoyokuwa kwa miezi hiyo 3 haina nguvu ya kuipinga/au kufanya mabadiliko yoyote ya maana katika bajeti ambayo tayari ilishapitishwa na wabunge na Mabadiliko yote ilibidi yafanywe wakati kamati za bunge zilipokutana na serikali.
So kwa mantiki hiyo wabunge waende nyumbani na wakome kuendelea kutumbua fedha za walipa kodi kwa miezi yote hiyo 3 kwa mijadala isiyo na Tija.