Siasa mbovu za Uenyekiti wa Halmashauri ya Moshi vijijini, Mbunge anahusika

Eeka Mangi

JF-Expert Member
Jul 27, 2008
3,173
481
Wapendwa Salamu,
Hatimaye nimerejea baada ya matibabu ya muda mrefu! KCMC na Agakhan Hospital. Nilipata FB kwenye koromeo. Usijesema ni Face Book ni Foreign Body! Loh!

Back to issue! Mchakato wa kumpata Mwenyekiti wa Halmashauri ya Moshi unaingia kwenye dosari kubwa baada ya Mbunge Magumashi wa CHADEMA kuingilia mchakato na kutaka shoga aka rafiki yake awe mwenyekiti wa Halmashauri pamoja na kuwa Madiwani Wateule hawamtaki. Ikumbukwe kuwa uteuzi wa Mbunge wa Moshi Vijijini uligubikwa na utata mwingi. Hata baada ya Mteule wa Makao Makuu kupitishwa, madiwani wengi waliokuwa hawamuungi mkono waliamua kukibeba chama ili kisipate aibu. Katika uchaguzi huo madiwani walioshinda ni 15 kati ya 16 kwa maana ya CCM kupata kiti kimoja tu.

Mbunge wa sasa ameamua kumbeba kwa mbeleko kubwa rafiki yake anayesemekana aliwahi kugombea ubunge Kawe na Kinondoni na mara zote alishindwa kwa kuwa hakubaliki. Baadhi ya Madiwani wamepigiwa simu na mbunge huyo na kuwataka wamuunge mkono. Mpango unaosukwa ni kuwa jina la Mwenyekiti litateuliwa na kutolewa UAMUZI NA KAMATI KUU CHADEMA! Hii sio hali ya kawaida maana haijawahi kutokea! Madiwani wengi wanasema wako tayari kufukuzwa chama na sio kuburuzwa Mbunge na team yake ambayo ina tuhuma nyingi! Anayedaiwa kushirikiana naye zaidi ni kiongozi mmoja makao makuu ambaye amediriki kumteua mama yake kuwa Diwani wa Viti maalumu Jimbo la vunjo! Mbunge wa sasa anatuhumiwa kumteua Dada mmoja anayehusishwa naye kimapenzi!

ANGALIZO
Wabunge acheni kujiingiza kwenye michakato hii la sivyo mtaangamiza chama. CHADEMA sio mahali pa mama na wapenzi ni mahali pa kupambana! Ni harakati sio uswahiba! Kaeni chonjo! Mkitaka na majina tutaweka hapa!

Wasalaam
 
ndicho.kilichotokea kyela mbeya hunter mwakifuna kachaguliwa na makenge wengi wa ccm ambalo ni mzigo kwa kyela kutofikia azma ya maendeleo sana
 
Wapendwa Salamu,
Hatimaye nimerejea baada ya matibabu ya muda mrefu! KCMC na Agakhan Hospital. Nilipata FB kwenye koromeo. Usijesema ni Face Book ni Foreign Body! Loh!
Back to issue! Mchakato wa kumpata Mwenyekiti wa Halmashauri ya Moshi unaingia kwenye dosari kubwa baada ya Mbunge Magumashi wa CDM kuingilia mchakato na kutaka shoga aka rafiki yake awe mwenyekiti wa Halmashauri pamoja na kuwa Madiwani Wateule hawamtaki. Ikumbukwe kuwa uteuzi wa Mbunge wa Moshi Vijijini uligubikwa na utata mwingi. Hata baada ya Mteule wa Makao Makuu kupitishwa, madiwani wengi waliokuwa hawamuungi mkono waliamua kukibeba chama ili kisipate aibu. Katika uchaguzi huo madiwani walioshinda ni 15 kati ya 16 kwa maana ya CCM kupata kiti kimoja tu.
Mbunge wa sasa ameamua kumbeba kwa mbeleko kubwa rafiki yake anayesemekana aliwahi kugombea ubunge Kawe na Kinondoni na mara zote alishindwa kwa kuwa hakubaliki. Baadhi ya Madiwani wamepigiwa simu na mbunge huyo na kuwataka wamuunge mkono. Mpango unaosukwa ni kuwa jina la Mwenyekiti litateuliwa na kutolewa UAMUZI NA KAMATI KUU CDM! Hii sio hali ya kawaida maana haijawahi kutokea! Madiwani wengi wanasema wako tayari kufukuzwa chama na sio kuburuzwa Mbunge na team yake ambayo ina tuhuma nyingi! Anayedaiwa kushirikiana naye zaidi ni kiongozi mmoja makao makuu ambaye amediriki kumteua mama yake kuwa Diwani wa Viti maalumu Jimbo la vunjo! Mbunge wa sasa anatuhumiwa kumteua Dada mmoja anayehusishwa naye kimapenzi!
ANGALIZO
Wabunge acheni kujiingiza kwenye michakato hii la sivyo mtaangamiza chama. CDM sio mahali pa mama na wapenzi ni mahali pa kupambana! Ni harakati sio uswahiba! Kaeni chonjo! Mkitaka na majina tutaweka hapa!
Wasalaam
Mbunge Pia ni Diwani,Hata hvyo umeandika umbea mtupu huna hoja,Endelea kuuguza koromeo na Mungu akujalie.
 
ndicho.kilichotokea kyela mbeya hunter mwakifuna kachaguliwa na makenge wengi wa ccm ambalo ni mzigo kwa kyela kutofikia azma ya maendeleo sana

Hivi ccm kyela imerogwa na nani ? Hivi hunter mwakifuna kwanini wanamng'ang'ania wakati hana uwezo ?
 
Chadema kazi yao ni kugombania madaraka. Hawapo kuwatumikia wananchi.
 
hiyo ni sifa kuu ya chadema. nakushangaa unatoa angalizo kwa kitu ambacho ni obvious.

Wapendwa Salamu,
Hatimaye nimerejea baada ya matibabu ya muda mrefu! KCMC na Agakhan Hospital. Nilipata FB kwenye koromeo. Usijesema ni Face Book ni Foreign Body! Loh!
Back to issue! Mchakato wa kumpata Mwenyekiti wa Halmashauri ya Moshi unaingia kwenye dosari kubwa baada ya Mbunge Magumashi wa CDM kuingilia mchakato na kutaka shoga aka rafiki yake awe mwenyekiti wa Halmashauri pamoja na kuwa Madiwani Wateule hawamtaki. Ikumbukwe kuwa uteuzi wa Mbunge wa Moshi Vijijini uligubikwa na utata mwingi. Hata baada ya Mteule wa Makao Makuu kupitishwa, madiwani wengi waliokuwa hawamuungi mkono waliamua kukibeba chama ili kisipate aibu. Katika uchaguzi huo madiwani walioshinda ni 15 kati ya 16 kwa maana ya CCM kupata kiti kimoja tu.
Mbunge wa sasa ameamua kumbeba kwa mbeleko kubwa rafiki yake anayesemekana aliwahi kugombea ubunge Kawe na Kinondoni na mara zote alishindwa kwa kuwa hakubaliki. Baadhi ya Madiwani wamepigiwa simu na mbunge huyo na kuwataka wamuunge mkono. Mpango unaosukwa ni kuwa jina la Mwenyekiti litateuliwa na kutolewa UAMUZI NA KAMATI KUU CDM! Hii sio hali ya kawaida maana haijawahi kutokea! Madiwani wengi wanasema wako tayari kufukuzwa chama na sio kuburuzwa Mbunge na team yake ambayo ina tuhuma nyingi! Anayedaiwa kushirikiana naye zaidi ni kiongozi mmoja makao makuu ambaye amediriki kumteua mama yake kuwa Diwani wa Viti maalumu Jimbo la vunjo! Mbunge wa sasa anatuhumiwa kumteua Dada mmoja anayehusishwa naye kimapenzi!
ANGALIZO
Wabunge acheni kujiingiza kwenye michakato hii la sivyo mtaangamiza chama. CDM sio mahali pa mama na wapenzi ni mahali pa kupambana! Ni harakati sio uswahiba! Kaeni chonjo! Mkitaka na majina tutaweka hapa!
Wasalaam
 
mie nashindwa kuelewa watu si wagombea nafasi ndani ya chama hilo nalo mnataka makao itoe maelekezo kweli hii ni afrika du
 
chadema wasipokuwa makini watazalisha migogoro mingi sana kwenye halmashauri watakazoziongoza na majiji kwa sababu ya kugombania madaraka. walipoteza halmashauri ya jiji la mwanza hivihivi kwa kugombania vyeo. waache demokrasia ichukue mkondo wake....
 
Tatizo sioni hoja inayodhibitisha kuwa wewe ni mkweli, isijekuwa unatumika kuchafuaa watu ambao hawawezi kukujibu humu.

Unaleta hiyo mada unafikiri sisi tutakusaidiajeee??
 
Unachikifanya hapa ni kujaribu tu kuichafua CDM kwa kuwa imefanikiwa kupata raisi ambaye kajiunga kiulaini kwa kutekeleza sera zao zote bila hata kuwa na kadi ya chama.
 
Msiwe mnajibu hovyo tu hapa! Mama yangu sio mwanasiasa ila nakupa hii! Mama yake John Mrema kwenye kura za maoni alipata kura moja lakini kateuliwa na hakufanya chochote kwenye harakati hizi! Elizabeti Temba alipata kura 2 anahusishwa na tuhuma za mapenzi na mbunge! Ukitaka ntakuambia tena!
Tunachotaka Mbunge na viongozi waache Demokrasia ichukue mkondo wake!
Kama CDM inataka isichafuke iache siasa za kizamani!
 
...umeandika yoote bila kum-quote yeyote au kuweka jina lolote, full umbeya na koromeo lako.!
 
Back
Top Bottom