chobu
JF-Expert Member
- Nov 5, 2010
- 308
- 26
Naiomba Wizara ya Elimu ifuatilie hizi shule za binafsi; kwa kweli ni unyonyaji mtupu. Hebu fikirieni jamani mtoto wa shule ya msingi unamlipia 2,800,000/= kwa mwaka. Hapo bado kila term ununue vitu vifuatavyo, ambavyo gharama yake ni mbali na school fees navyo ni;
1. NIDO kubwa - 42,000/=
2. OMO kgm 4 - 20,000/=
3. kuonyoa nywele - 10,000/=
pamoja na vyote hivyo bado watoto wadogo wa chekechea kuanzia miaka mitatu hawapati mlo kamili kabisa. Unapochukua watoto wadogo chini ya miaka mitano katika shule zenu za binafsi, mnatakiwa mjipange sawasawa, sio kufikira pesa tu lakini afya za watoto hamzijali. Mimi naona wakati umefika sasa wa hizi shule kuchunguzwa upya tena kwa ukaribu sana. Wanatoza ada kubwa lakini huduma zenyewe ni mbaya. Ni hatari sana kwa afya za watoto chini ya miaka mitano. La msingi kabisa shule hizi hazina hata maji ya kutosha ya kunywa watoto, inabidi wazazi wawanunulie watoto wao maji ya kunywa. Hivi hamuoni umuhimu wa maji safi ya kunywa mashuleni? Mazingira yenyewe si mazuri hakuna uwanja wa michezo, watoto hawapati hewa safi maana eneo lenyewe dogo na lipo kwenye High Density. Ilikuwa ni nyumba ya kuishi ikageuzwa shule. Hii ni hatari kabisa, na viongozi wahusika wanaangalia tu!
Mfano wa shule: ni HAZINA INTERNATIONA SCHOOL iko magomeni.
1. NIDO kubwa - 42,000/=
2. OMO kgm 4 - 20,000/=
3. kuonyoa nywele - 10,000/=
pamoja na vyote hivyo bado watoto wadogo wa chekechea kuanzia miaka mitatu hawapati mlo kamili kabisa. Unapochukua watoto wadogo chini ya miaka mitano katika shule zenu za binafsi, mnatakiwa mjipange sawasawa, sio kufikira pesa tu lakini afya za watoto hamzijali. Mimi naona wakati umefika sasa wa hizi shule kuchunguzwa upya tena kwa ukaribu sana. Wanatoza ada kubwa lakini huduma zenyewe ni mbaya. Ni hatari sana kwa afya za watoto chini ya miaka mitano. La msingi kabisa shule hizi hazina hata maji ya kutosha ya kunywa watoto, inabidi wazazi wawanunulie watoto wao maji ya kunywa. Hivi hamuoni umuhimu wa maji safi ya kunywa mashuleni? Mazingira yenyewe si mazuri hakuna uwanja wa michezo, watoto hawapati hewa safi maana eneo lenyewe dogo na lipo kwenye High Density. Ilikuwa ni nyumba ya kuishi ikageuzwa shule. Hii ni hatari kabisa, na viongozi wahusika wanaangalia tu!
Mfano wa shule: ni HAZINA INTERNATIONA SCHOOL iko magomeni.